Saturday, May 27, 2017
Mkutano Mkuu wa Vijana Kimataifa Kufanyika Arusha
Tuesday, August 13, 2013
Bilionea Msuya kuzikwa leo, Jeneza lafunguliwa kwa ‘rimoti’
*************************************
![]() |
| The late Tanzanian Billionaire Erasto Msuya. He was murdered. |
Kutoka Gazeti la MWANANCHI:
Arusha - Mazishi ya kifahari yanaandaliwa na familia ya marehemu Erasto Msuya, huku ikielezwa kuwa jeneza litakalotumika kubeba mwili wake linafunguka kwa kutumia ‘rimoti’.
Tuesday, May 07, 2013
Rais Kikwete Atembelea Kanisa Lililopigwa Bomu Arusha
Rais Kikwete Akutana na Askofu Mkuu wa Arusha
Rais Kikwete Aongea na Waandishi wa Habari - Mlipuko wa Bomu Kanisani Arusha
Sunday, May 05, 2013
Mlipuko wa Bomu Katika Kanisa Katoliki Arusha
HABARI KWA KIFUPI:Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.
Anasema ni tukio la kighaidi. Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu. Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi. Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana. Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano |
| Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi. |
| Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi. |
| Tanzania Field Force Unit (FFU) on site of Catholic church bombing |
| Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ibrahim Kilongo. JESHI la Polisi Mkoani Arusha linamshikilia mtu mmoja ambaye anahusishwa na kutokea kwa mlipuko uliotokea katika kanisa la Katoliki la St Joseph Olasiti Arusha leo asubuhi. Tukio hilo lilitokea wakati Balozi wa Papa kutoka Vatican akizindua Parokia hiyo mpya ya St Joseph Olasiti ya Jijini Arusha. |
![]() |
| Kanisa lililolipuliwa likiwa linaonekana kwa mbali huku wananch wakilitazama kwa mbali kutokana na tishio la kutokea kwa milipuko mingine ...Mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na tukio hilio wakati wengine wanasadikika kukimbia. |
![]() |
| Majeruhi wa tukio hilo wakiwa katika hali mbaya.. |
![]() | |||||||
| Waumini
pamoja na baadhi ya wanacchi wakiwa katika hali ya taharuki wasiamini
nini kilichotokea kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea asubuhi ya leo. |
Kanisa Katoliki Lalipuliwa na Bomu Arusha Wakati wa Ibada!
KWA KIFUPI:
Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.
Anasema ni tukio la kighaidi.
Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu.
Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi.
Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana.
Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano
| Hali ya eneo mlipuko ulipotokea |
********************************************
The dead was among the church followers who were gathering for Sunday prayers.
The church located in Arusha's Olasiti suburb was bombed just before a mass in the presence of Bishop Josaphat Louis Lebulu of Arusha Diocese, who was accompanied by a representative of Pope of Vatican.
Police in Arusha said one man was arrested in connection with the incident, which caused a lot of panic in the tourist capital of the East African country.
Casualties are yet to be updated. "We are still working on the matter. We'll give more detail after investigating the matter," said Arusha Regional Police Commander Liberatus Sabas.
He said the man was arrested following a tip-off from people at the scene when the explosion occurred.
"We are still interrogating the suspect," he said.
Regional Commissioner Magesa Mulongo described the blast as horrific and unique in Tanzanian history, calling on the public to remain calm.
"So, people should continue with their daily activities, as police and other security organs have normalized the situation," Mulongo said.
A witness said, "I saw more than 30 people, taken by a police vehicle, which took them to the Mount Meru Regional Hospital."
Another witness said the bomb hit the church at around 10:00 a. m. local time when church followers were gathering for the historic Sunday prayer at the new church.
"We were trying to organize ourselves for the mass, when we heard loud sound, the situation that made more people to start rushing out of the church," a witness told Xinhua.
This is the first bomb explosion at the church in the northern safari capital of Arusha.
![]() |
| One of those injured in Bombing receiving First Aid |

Monday, December 03, 2012
Mh. Shy-Rose Bhanji Akutana na Aga Khan
Kiongozi Mtukufu Aga Khan ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) na Kiongozi wa Waislamu wa Ismailia akizungumza mawili matatu ya kimaendeleo na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mh. Shy-Rose Bhanji wakati wa ufunguzi wa Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki mkoni Arusha. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Kidiplomasia ya AKDN Dkt. Shafik Sachedina. ( Picha kwa Hisani ya Ikulu)
Tuesday, November 20, 2012
East Africa Ultimate Frisbee Tournament
Ausha Ultimate Frisbee Association is pleased to announce the East Africa Ultimate Frisbee Tournament which will be held in Arusha, Tanzania on November 23-24, 2012, Four teams will be participating in game played at Arusha Technical College:-
The teams that will be participating:
1) MOSHI KILL KILLERS -Captain: Frank Mushi
2) MWANZA TOSSERS -Captain: Andrew Bergman
3) ARUSHA ULTIMATE FRISBEE -Captain: Silau Ole Nyasi
4) NAIROBI ULTIMATE -Captain: Aaron Colverson
For any additional information and request, please call one of The Organizers Oli - 0684082908 or 0752216040
Friday, November 16, 2012
Rais Kikwete Afunga Mkutano wa Majaji Mjini Arusha Leo
![]() |
Waheshimiwa majaji wakimsikilia Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kufunga mkutano wa siku nne wa Majaji uliofanyika katika hoteli ya Snow Crest jijini Arusha leo Novemba 16, 2012
|
Picha na Ikulu
Thursday, August 02, 2012
Rais Kikwete Atoa Kifuta Jasho cha Ng'ombe kwa Wananchi wa Monduli
(Picha na Habari Kutoka Ikulu)
Rais Jakaya Mrisho kikwete akizindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jashp cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009
Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi ng'ombe mmoja wa wakaazi wa Monduli walioathririka na na ukame mwaka 2008/2009 ambapo walipoteza mifugo yao yote. Hafla hii imefanyika leo Monduli. Picha na Ikulu.
SERIKALI itakuwa inagawa ng’ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha karibu mifugo 800,000 iliyopotea kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.
Ahadi hiyo imetolewa leo, Alhamisi, Agosti 2, 2012 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipozindua Mradi wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo kwa waliopotelewa mifugo yote katika Wilaya ya Monduli kwenye sherehe iliyofanyika Makuyuni wilayani humo.
Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi wa Mkoa wa Arusha wakiwemo wakuu wa wilaya na wabunge wa mkoa huo, Rais Kikwete amegawa ng’ombe 500 kwa kundi la kwanza la wananchi ikiwa ni mitamba minne na dume moja la kisasa kwa kaya 16 za mwanzo.
Uzinduzi huo ni wa pili kufanywa na Rais Kikwete chini ya Mradi huo wa kwanza wa aina yake kubuniwa na Serikali katika historia na wenye thamani ya sh. Bilioni 12.9.
Februari 19, mwaka huu, Rais Kikwete alizindua Mradi kama huo katika Wilaya ya Loliondo kwenye sherehe zilizofanyika mjini Loliondo. Kesho Agosti 3, 2012 Rais Kikwete anatarajiwa kuendelea na zoezi hilo katika mji wa Loliondo.
Sunday, December 04, 2011
Tanzia - Alfred Ngotezi (Mwandishi wa Habari)
![]() |
| The Late Alfred Ngotezi |
NSSF wako mjini Arusha kwa ajili ya uenyeji wa Mkutano wa Kimataifa wa Mashirika ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika (ISSA) ambao utaanza Jumatatu 05.12.2011.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhani Dau ndiye aliyetujulisha kuhusu kifo hicho cha Ngotezi na baadaye Meneja Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume pia kutueleza kile kilichotokea.
Ilikuwaje?
Ni kwamba Ngotezi ameanguka ghafla na walipombeba wakitaka kumpeleka hosipitali, tayari alikwishapoteza maisha. Alikuwa anakula, then akaomba bendi impigie muziki, kisha akacheza vizuri tu. Alipomaliza kuburudika aliwapa mikono wanamuziki kama ishara ya shukrani, halafu alirejea kwenye meza na kuketi. Baada ya dakika chache kupita alinyanyuka kwenda chooni, lakini hakufika kwani alianguka kisha kukutwa na mauti.
Kwa wahariri tuliokwenda Tanga, Kagera na Mwanza, mtamkumbuka bwana huyu (Ngotezi) kwa michapo yake na ucheshi wake pia, kwani tulishirikiana naye sana. Ni miongoni mwa walioshiriki sana kazi ya kuratibu suala la mashamba ya mkonge kule Tanga.
Kifo chake ni pigo kwa tasnia ya habari kwani alituwakilisha vyema NSSF, lakini zaidi mchango wake katika sekta ya habari utakumbukwa daima. Pole nyingi kwa familia ya Marehemu Alfred Ngotezi, pole sana Dk Dau na wafanyakazi wa NSSF kwa ujumla na zaidi ya yote poleni sana wana habari wa Tanzania.
Ngotezi umetangulia, wengine tutafuata kila mmoja kwa zamu yake, RIP Alfred Ngotezi.
Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors' Forum (TEF
Friday, October 07, 2011
Worship Leadership Seminar - Arusha, Tanzania
Charles Stanley once said that he believed that most Christians in most churches have never worshiped God. We go to church, but we don’t worship. We sing songs, but we don’t worship. We listen to sermons, but we don’t worship. All of these things are elements of worship but they are not worship in and of themselves which means that you can do all of them and yet have failed to truly worship God. We Christians often mistake the means of worship for worship itself.
According to famous researcher, George Barna, “Worship is a non-negotiable obligation and privilege of every Christian…We agree that when it comes to worship, God deserves it, the Bible commands it, and churches try to facilitate it," he stressed. "But we have a problem when it comes to worship. ... True worship is rare.”
The church in our times faces major challenges related to the renewal of worship. I believe one of them, if not the main one is a lack of understanding what a true biblical worship is. What you hear and understand you believe, and what you believe you’ll obviously do. That is life because life is not only in knowing but in doing.
A seminar for Worship Leadership will be held in Arusha that aims in tackling the challenges on Worship.
The target audience: Worship Leaders/Pastors, Church Leaders, Musicians/Singers, Audio Technicians/Engineer, Recording Artist and any one related with Worship Ministry.
Seminar program will cover some topics in three areas but not limited to; Introduction to Biblical Worship: Understanding What is Biblical Worship, Applied Worship Ministry: Integrating Leadership and Team Dynamics, and The Role of Music in Worship: Balanced Approach to Music Ministry in Corporate Worship
Friday, May 06, 2011
Wataalam Wasema Dawa ya Babu Inafanya Kazi Kiasi
A technical report on retired pastor Ambilikile Masapila’s “miracle cure” has indicated that scientific data supports his claims to its positive effects on a number of ailments.
A report by experts from the National Institute for Medical Research (NIMR) Department of Traditional Medicine Research and Institute of Traditional Medicine, Muhimbili University of Health and Allied Sciences seen by The Guardian, says study findings have revealed that ‘Babu’s miracle cure’ prepared by boiling the roots of Carissa edulis plant is safe and has positive effects on cancer, epilepsy, herpes simplex virus, liver ailments, diabetes, blood pressure and anti-viral activity.
However, the scientists said since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, the government should advance the work of focused pre-clinical studies to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.
“The dose provided by Pastor Masapila which is one cup (about 200 mls) prepared through boiling an estimated 3.0 kg of whole root material in 60 litres of water “falls within safety window and no any overdose or acute poisoning event is expected.”
The results suggested that the plant has anticonvulsant activity which supports the claim of the use of the plant in the management of epilepsy as claimed by Pastor Ambilikile Masapila.
It further indicated that the herb has antidiabetic activity which supports the claim of the use of the plant in the management of diabetes.
The herbal has blood pressure lowering activity which supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of high blood pressure.
Research results show that the pastor’s concoction has hepatoprotective and antioxidant activity which are beneficial in the prevention of liver disorders and cancer.
“This result also reveals that Carissa edulis has potent anti-viral activity against herpes simplex viruses. Taking into consideration that, herpes simplex virus (HSV) infection is a major opportunistic infection in immunosuppressed persons, these findings supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of HIV/Aids as claimed by Pastor Masapila,” said the report.
Drawing general conclusion, scientists said that the plant is safe and the dosage prescribed by Rev. Mwasapila is below the toxic level.
They, however, recommended that since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, focused pre-clinical studies need to be conducted to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.
Scientists also recommended standardisation and formulation of “Babu’s cupful” for human use.
“MoHSW should conduct clinical trial on the prescribed remedy to establish in vivo efficacy and safety in humans and answer questions on optimum dosage, dosing schedule and duration of treatment per ailment,” stated part of the report.
It added “MoHSW should conduct clinical follow up on all patients recorded to have used the remedy for their prognosis.”
Recently, many people have been flocking Samunge village in Loliondo, Arusha, seeking the cure for chronic diseases such as diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/Aids.
According to Rev. Masapila, God instructed him through dreams since 1991 about the medication and that, it will heal people with chronic illnesses namely: diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/AIDS. The dream kept recurring to him several times since then and on August 26, 2010 he decided to obey on the instructions and started the healing work.
Earlier this month, HIV/Aids stakeholders blamed the government over its silence on HIV/Aids patients who abandon antiretroviral drugs after taking the herbal concoction being dispensed by Pastor Masapila in Loliondo.
HIV/Aids stakeholders said there was need to give correct messages to the people to avoid negative impacts in future.
SOURCE: THE GUARDIAN
Wednesday, March 30, 2011
Mama Charlotte wa Arusha atakuwa Cambridge, MA Jumamosi
Saturday, January 08, 2011
TAMKO LA CUF KUHUSU MAANDAMANO YA CHADEMA ARUSHA
VYOMBO VYA DOLA VINAHATARISHA AMANI YA NCHI.
CUF - Chama Cha Wananchi kimeumizwa sana na kitendo cha kinyama kilichofanywa na jeshi la polisi na serikali ya chama cha mapinduzi kuwapiga na kuwaumiza viongozi, wanachama na wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na wananchi mbalimbali wapenda demokrasia na haki ndani ya nchi yetu waliokuwa wakiandamana kwa amani jijini Arusha jana tarehe 05 Januari 2011. Tunalaani vikali kukamatwa na kwenda kuhojiwa kwa Wabunge wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Taifa Mhe. Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai , Mhe. Godbless Lema Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Joseph Selasini Mbunge wa Rombo na Mhe. Philemon Ndesamburo, Mbunge wa Moshi Mjini.
CUF inaamini kuwa CHADEMA kama chama cha siasa kilichosajiliwa kihalali ndani ya nchi yetu kilikuwa na haki ya kikatiba na kisheria ya kufanya maandamano yao ya amani ambayo mwanzoni tayari jeshi la polisi jijini Arusha kupitia kwa kamanda wa polisi wa mkoa lilishaahidi kutoa ulinzi wa kuyaweka maandamano hayo salama.
Jeshi la Polisi na Serikali ndiyo wanaostahili kulaumiwa kwa uvunjifu wa amani uliotokea Arusha. Ushahidi wa kimazingira unaonyesha wazi kuwa amri ya kusitisha maandamano iliyotolewa na IGP saa chache kabla hayajafanyika ilitokana na shinikizo za kisiasa. Hoja iliyotolewa kuwa taarifa za kiintelijensia zinaonyesha kutakuwa na uvunjifu wa amani na ndiyo maana maandamano yanazuiliwa ni usanii mtupu. Kama kweli polisi wana taarifa za kiintelijensia kuwa kuna watu watavunja amani basi wazitumie taarifa hizo kuwadhibiti watu hao na siyo kuyasitisha maandamano na kuwanyima wananchi uhuru wa kisheria wa kufanya maandamano.
Nchi hii inapaswa kuongozwa na katiba na sheria na Watanzania tusikubali Serikali iliyoko madarakani kutumia vyombo vya dola kuua uhuru na demokrasia ya nchi yetu.
Hivi sasa jeshi la polisi limekuwa mstari wa mbele kuzuia kila aina ya madai yanayotolewa na vyama ili mwisho wa siku jeshi lifanye kazi yake kuu ya kulinda CCM na utawala wao kijeuri na kisanii. Haiwezekani kila watu wakitaka kuandamana jeshi la polisi lianzishe hoja ati “kwa sababu za ki-intelijensia” maandamano hayo yanafutwa. Hizi taarifa za ki-intelijensia ni zipi?
CUF inaamini kuwa polisi na serikali ya CCM wanataka kutumia kitisho cha ugaidi kilichozikumba Kenya na Uganda kama sababu ya kupinga mikusanyiko mikubwa ya kisiasa kwa lengo la kuitetea Serikali. Lazima tujiulize,hivi magaidi wakitaka kulipua Tanzania mbona kuna sehemu nyingi sana ambazo wanaweza kufanya hivyo bila kusubiri maandamano ya CHADEMA au CUF au vyama vingine?
Hivi tujiulize kama kweli pana tishio la ugaidi iweje mechi za mpira ziendelee bila kuzuiwa na polisi? Mikusanyiko yote inafanyika isipokuwa maandamano ya vyama vya siasa tu? Hawa magaidi walio tishio kwa jeshi la polisi wanaotaka kulipua maandamano peke yake wametokea wapi? Kwa nini nchi hii iendeshwe kisanii na kiujanja ujanja namna hii? Kwa nini serikali inaogopa maandamano?
CUF inalaani ukatili waliofanyiwa wakazi wa Arusha katika maandamano ya CHADEMA na kuwa ukatili huo hauvumiliki na unahatarisha amani na utulivu wa kweli wa nchi yetu.
Ukatili huu hauna tofauti na ule tuliofanyiwa CUF – Chama cha Wananchi tarehe 28/12/2010 ambapo maandamano ya amani yaliyokuwa yaongozwe na Kaimu naibu katibu mkuu Julius Mtatiro yalipigwa marufuku ghafla na kisha mamia na mamia ya polisi wakisheheni silaha za kila aina wakaanza kuwapiga na kuwakamata wafuasi wa CUF na wananchi wengine walioshiriki katika maandamano yale. Kitendo kile ambacho polisi walikifanya kimetia doa kubwa sana jeshi la polisi linaloongozwa na kiongozi tunayemheshimu IGP Said Mwema.
Kitendo hiki cha pili kilichofanyika Arusha kinazidi kuharibu kabisa sifa na uaminifu ambao vyama vya siasa vilikuwa nao juu ya IGP Mwema. Ni muhimu sana kwa taifa letu kwa IGP Said Mwema kulinda heshima yake na asikubali kutumiwa kisiasa kukandamiza demokrasia ndani ya nchi.
Chama cha wananchi CUF kinaamini kuwa ustawi wa demokrasia, utawala bora, usawa, maendeleo ya nchi yetu na amani ya nchi havitaletwa kwa mtutu wa bunduki wala mabomu wala kila aina ya nguvu, hata kama CCM wataendelea na mbinu zao za kuwadhibiti wapinzani hatutokaa kimya na wala hatutoacha kutumia fursa za kikatiba kutoa maoni yetu kwa njia ya amani kama walivyofanya CHADEMA tarehe 05/01/2011 na CUF tarehe 28/12/2011.
Tunaamini walichokuwa wakipigania CHADEMA jijini Arusha ni kitu cha msingi sana,walikuwa wakipinga kitendo cha kukiuka demokrasia katika uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha. CHADEMA hawakuwa na budi kutumia njia za kidemokrasia kuonyesha kutokukubali na kutotambua utaratibu huo wa kinyemela ulioendeshwa na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha kwa manufaa ya CCM.
CUF inawapa pole wahanga wote waliopigwa na kuumizwa na mabomu, risasi, maji ya kuwasha n.k katika tukio hilo la kihistoria la kudai haki ya wanyonge jijini Arusha. CUF iko pamoja nao katika kuendelea kupigania haki. CUF inawapa pole viongozi wote wa CHADEMA waliokamatwa katika maandamano ya Arusha na tunawataka waendelee na juhudi za kupigania ukombozi kama inavyofanya CUF.
CUF inamtaka Rais Jakaya kikwete kutumia busara za hali ya juu sana katika kuendesha nchi katika kipindi hiki ambacho anamalizia miaka yake mitano ya mwisho. Rais Kikwete ana fursa ya kujenga misingi imara ya demokrasia ili akitoka madarakani akumbukwe kwa mambo ya heri na siyo kwa mambo ya shari.
Kukaa kimya kwa Rais wakati polisi wanatumia nguvu kubwa kuua demokrasia ndani ya nchi kunaashiria kuwa wanatimiza amri ya Rais.
Pamoja na mambo yote hayo CUF inawataka Watanzania kuendelea kutuunga mkono ili tuweze kuendeleza mapambano ya kudai demokrasia na maendeleo ya kweli ya nchi yetu kama chama mbadala kitakachomkomboa Mtanzania.
Mwisho tunawataka wakazi wote wa Arusha, Dar es salaam na mikoa mingine wazidi kuungana na CUF na wadau wengine wote muhimu katika madai mazito ya kudai katiba mpya.
CUF inaamini suluhisho la sehemu kubwa ya ukatili unaofanywa sasa ni kukosekana kwa katiba mpya itakayotoa mwongozo sahihi wa taifa letu. Tofauti na sasa ambapo jeshi la polisi na vyombo vingine vya dola vinaweza kufanya lolote wanalotaka juu ya maisha ya watanzania huku katiba ikiwalinda au wanaivunja na hakuna mwenye mamlaka ya kuwauliza.
Tanzania inahitaji Katiba Mpya ya Wananchi wenyewe na Tume Huru ya Uchaguzi. Tamko la Rais la kuunda Tume Maalum ya Katiba na ishara nzuri ukilinganisha na matamko ya awali ya Waziri wa Sheria na Katiba. Hata hivyo ni muhimu Rais akawafafanulia Watanzania kuwa lengo la mchakato mzima ni kupata Katiba Mpya yenye misingi imara ya demokrasia itakayotokana na ushiriki wa wadau wote. CUF inawaomba na kuwasisitiza Watanzania watuunge mkono sana ili tuhakikishe kwa pamoja tunapata katiba itakayoandikwa upya na kubeba matumaini ya Watanzania na siyo kuwekwa viraka kwa katiba iliyopo.
Prof Ibrahim Haruna Lipumba
Mwenyekiti - CUF.
06 Januari 2011.
Dar es salaam.
Monday, June 14, 2010
Mtoto Nicole wa Arusha
*******************************************************************
Monday, December 15, 2008
Funga Mwaka Arusha

MWANAFA, AY NA C4 DJS UNIT KUFUNGA MWAKA ARUSHA
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya (AY) na Hamis Minyijuma (MwanaFA) wanaotesa katika anga ya muziki kwa sasa, wanatarajia kutoa burudani ya aina yake kwenye uzinduzi wa kundi la C4 DJs linaloundwa na wachezeshaji muziki ambalo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika mkesha wa sikukuu ya Krismas ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’ jijini Arusha. Kundi hilo linaundwa na Ma-DJ wenye uzoefu wa siku nyingi wakiwemo DJ Joe, DJ Peter, DJ Gerry na DJ A-Plus. Pia kutakuwa na Madj wengine wakali kusindikiza uzinduzi huu wa aina yake.
Aidha maandalizi kwa ajili ya uzinduzi huo na sherehe za funga mwaka yanaendelea vizuri hivyo mashabiki wakae tayari kupata burudani ya aina yake. Uzinduzi huu ndiyo mwanzo wa mfululizo wa burudani ndani ya Ukumbi wa Club Triple ‘A’ hadi mwaka 2009.
MaDJ hao wa kitanzania waliobobea katika fani hiyo wameamua kuzindua umoja huo ili kuonyesha kwamba wapo pamoja na watatoa kipaumbele kwa wahusika wote katika tasnia hii. Baada ya uzinduzi kutakuwa na program ya burudani kabambe ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’.
Siku ya Krismasi kundi la C4 litaandaa onyesho litakalofahamika kama ‘White Party’ambapo wateja watakaopendeza ndani ya mavazi meupe watapewa zawadi kemkem za papo kwa papo.
Na kwa mara ya kwanza katika historia ya burudani katika Ukumbi wa Triple ‘A’ Arusha kutakuwepo na shindano la kumsaka malkia wa Desemba (Miss Desemba). Shoo hiyo itafanyika usiku wa tarehe 26 Desemba. Shoo hii ya aina yake itawahusisha warembo kumi wenye vipaji mbali mbali.
Burudani ya Funga Mwaka katika jiji la Arusha inatarajia kuleta mageuzi makubwa katika fani ya muziki na burudani nchini Tanzania.
Funga mwaka hii itatoa fursa kwa C4 DJs kupata fursa ya kuonyesha umahiri wao katika kupangilia muziki ikiwa ni moja ya lengo la kuendeleza fani hiyo ya muziki ambao ulishika chati zaidi katika miaka ya 80 na 90 kabla muziki wa dansi haujateka soko na watu kuwapa kisogo maDJ.
Katika kuhitimisha Funga Mwaka Kundi la C4 limeandaa bonge la Bethdei party kwa ajili ya kusherehekea mafanikio ya Club Triple ‘A’ zaidi ya miaka kumi.
JOSEPH NAMALOWE (DJ JOE)
MRATIBU
Monday, November 24, 2008
Mike Sikawa Laid to Rest

*********************************************************************
Kutoka Daily News:
Mike Sikawa laid to rest
CHARLES KIZIGHA in Arusha
Daily News; Monday, November 24, 2008
Former Prime Minister Edward Lowassa, accompanied by his wife Regina, yesterday led hundreds of mourners from all walks of life at the burial of veteran journalist Mike Sikawa at Mareu village in Arumeru district, Arusha region.
The well-attended burial service was preceded by paying last respects at the Mareu Rural Cooperative Society grounds, a stone’s throw away from his place of domicile. Mike was laid to rest at the family’s farm where his father and mother were buried.
Prior to paying last respects several speakers, including Mr Lowassa, described Mike as one of the outstanding journalists in the country and Africa at large. The same was echoed by the head of the BBC Kiswahili Service, Solomon Mugera who led a team of four BBC staff to represent the Broadcasting House.
“Although Mike had been sick for a long time, his colleagues did not know because he did not show any sign and continued working normally. This proved that Mike was a hard working journalist and was ready to go out for assignments without showing any hesitation much as he was sick,” said Mr Mogera.
The mourners, who included the clergymen from various churches, government leaders, representatives from AICC, Tanapa and Retired General Mirisho Sarakikya, said the only way to remember Mike is to continue practicing excellent journalism. Mike joined the 'Daily News' and 'Sunday News' in 1975 until 1994 when he joined the BBC. He begun battling with diabetes in 1978 and underwent several treatments inside and outside the country until November 18 when he lost the battle.
**********************************************
Navyokumbuka mimi aliondoka Daily News 1984. Na siyo 1994. Walibandika notice ubaoni newsroom kutujulisha.
Wednesday, November 19, 2008
Mike Sikawa wa BBC Afariki Dunia

(Mike Sikawa 1982 Dar es Salaam, Tanzania - Mike alinitumia hizi picha nikiwa denti Form Five, Tabora Girls. Mbona nilitamba nazo, kwanza zilikuwa za rangi, halafu pili alikuwa mwandishi wa habari maarufu sana hivyo kujuana naye ilikuwa fahari kweli. Miaka yote hii nimekaa nazo.)*******************************************************************
Nimepokea habari za kusikitisha sana leo. Mwandishi wa Habari wa BBC, Mike Sikawa, amefariki dunia. Aliwahi kufanya kazi Daily News. Alikuwa na kipaji mkubwa wa kuandika habari mpaka Daily News walimpa 'special privileges'.
Nilikutana naye kwa mara ya kwanza nikiwa nasoma 'A' levels Tabora Girls. Nilikuwa likizo Dar na tuliktana kwenye party Chuo Kikuu cha DSM. Wakati huo Mike Sikawa alikuwa maarufu sana. Nilimwambia kuwa nataka kuwa mwandishi wa habari na yeye alisema kuwa huo kazi haufai mwanamke. Nikamwambia kuwa hata hivyo bado nataka kuwa mwandishi wa habari. Nilianza kazi Daily News Agosti 1984, na baada ya muda mfupi yeye alitoka na kwenda Uingereza. Nilikutana naye tena miaka ya 90 na Mike aliniambia kuwa alijua nitakuwa na mafanikio makubwa katika uandishi wa habari.
Nakumbuka huo ugonjwa wa kisukari ulianza kumsumbua wakati huo na ndo ulimaliza.
Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.
****************************************************
Kutoka Lukwangule Blog:
Mike Sikawa wa BBC afariki dunia
MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari.
Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha.
Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni.
Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote.
Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia.
Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti.
Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro.
Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini.
Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi.
Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo.
Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.
Kwa habari zaidi soma:
http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=8536















