Showing posts with label Arusha. Show all posts
Showing posts with label Arusha. Show all posts

Saturday, May 27, 2017

Mkutano Mkuu wa Vijana Kimataifa Kufanyika Arusha

Mkutano Mkuu wa Vijana Kimataifa Kufanyika Arusha kwa Siku 7 [caption id="attachment_79335" align="aligncenter" width="800"] Mratibu wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa kwa Vijana Tanzania, Tajiel Urioh akizungumza na waandishi wa habari leo (hawapo pichani) kuzungumzia Mkutano Mkuu Kivuli wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa unaokutanisha vijana utakaofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 26 mwezi Mei, 2017 mjini Arusha katika Ukumbi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa Tanzania, Arafat B. Lesheoe.[/caption]   AKIZUNGUMZA na waandishi wa habari Mratibu wa Mkutano Mkuu Kivuli wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, Tajiel Urioh alisema mkutano huo ni maigizo ya vitendo ya baraza kuu la Umoja wa Mataifa ambapo vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 30 kutoka sehemu mbalimbali wanapata fursa ya kujifunza Diplomasia, Uongozi na namna Umoja Wa Mataifa unavyofanya kazi. Bw. Tajiel Urioh alisema kuwa, Mkutano huo unaojulikana kama kongamano kubwa kabisa la vijana nchini linalowaleta pamoja vijana wadogo kutoka nchi mbalimbali tangu mwaka 1997. Aidha aliongeza kuwa Mkutano huo Mkuu Kivuli wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa utafanyika mjini Arusha katika Ukumbi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kuanzia tarehe 22 hadi 26 mwezi wa Mei mwaka 2017, ambapo vijana takribani 200 kutoka katika nchi mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria kujadili masuala yanayohusiana na Afya ya Uzazi na Uzazi wa Mpango, Demokrasia na Amani katika nchi zinazoendelea, Kuhama kuelekea kwenye Nishati safi na ya teknolojia mbadala na Elimu kwa Maendeleo Endelevu. Aliongeza kuwa majadiliano ya mwaka huu yatajikita katika mada kuu: “Kuwawezesha Vijana katika Diplomasia na Uongozi”. Mada hii inalenga kuwezesha ushiriki wa vijana na kuwajengea uwezo kwenye masuala ya Diplomasia na Uongozi kwa kuwapa mafunzo ya vitendo katika mada ngumu ambazo zitawaongezea ujuzi wa majadiliano na kufikia muafaka wa masuala mtambuka yanayogusa maslahi ya mataifa. "Tunaishi katika ulimwengu ambao diplomasia yenye ujasiri na uongozi vinahitajika sana hivyo basi kuwakuza vijana katika uwanja huu itachangia kukua kwa mataifa yenye watu wenye uwezo wa kuamua mambo yao. Katika mkutano wa mwaka huu wajumbe watakuja na maazimio mbalimbali ambayo kwa namna moja hama nyingine yatakuwa na manufaa katika maisha yao ya kila siku na watu wanaowazunguka katika jamii zao," alisema Bw. Urioh.   [caption id="attachment_79334" align="aligncenter" width="800"] Mratibu wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa kwa Vijana Tanzania, Tajiel Urioh akizungumza na waandishi wa habari leo (hawapo pichani) kuzungumzia Mkutano Mkuu Kivuli wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa unaokutanisha vijana utakaofanyika kuanzia tarehe 22 hadi 26 mwezi Mei, 2017 mjini Arusha katika Ukumbi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela. Kushoto ni Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akiwa katika mkutano huo pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa Tanzania, Arafat B. Lesheoe.[/caption]   “Ni matarajio yangu makubwa kwamba mtakuwa tayari kujifunza kuendana na mada kuu ya ‛ Kuwawezesha Vijana katika Diplomasia na Uongozi′ lakini pia kubadilishana mawazo na wajumbe wengine na kutengeneza mtandao wa vijana wenye fikra mnazoendana nazo,” aliongeza Tajiel Urioh, Mratibu wa Kitaifa wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2017. Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo alisema kongamano kama hilo la vijana lina umuhimu mkubwa kwa vijana kwani huwajenga vijana kupitia Club za UN. Aliwataja miongoni mwa vijana ambao ni matunda ya Club za UN ni pamoja na Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka, Balozi wa Tanzania nchini Japan, Benedict Kikove, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Salum Hapi, Mbunge wa Kibamba (Chadema), John John Mnyika na wengine wengi.

Tuesday, August 13, 2013

Bilionea Msuya kuzikwa leo, Jeneza lafunguliwa kwa ‘rimoti’

 Marehemu Erasto Msuya, alikuwa bilionea. Mnashangaa nini jeneza lake likifunguliwa kwa remote control? Rest in peace.


*************************************

The late Tanzanian Billionaire Erasto Msuya. He was murdered.


Kutoka Gazeti la MWANANCHI:

Arusha - Mazishi ya kifahari yanaandaliwa na familia ya marehemu Erasto Msuya, huku ikielezwa kuwa jeneza litakalotumika kubeba mwili wake linafunguka kwa kutumia ‘rimoti’.
Msuya aliyeuawa wiki iliyopita, anazikwa leo huku familia ikitangaza kutokulipiza kisasi kwa waliohusika, badala yake wamemwachia Mungu.
Kinachovutia katika msiba huo ni jeneza lililobeba mwili wa mfanyabiashara huyo lililoagizwa Nairobi, la aina yake huku likifunguliwa kwa kutumia ‘rimoti’.
Jeneza hilo lililoagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home, linafunguliwa kwa kubonyeza kifaa maalumu hata mhusika anapokuwa mbali.
Hali hiyo ilionekana kuwaacha na mshangao maelfu ya waombolezaji waliofika kuaga mwili wakati wa ibada iliyofanyika nyumbani kwake, Kwa Iddi, wilayani Arumeru.
Mfanyabiashara huyo aliyeuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20 na watu wasiojulikana, anazikwa leo nyumbani kwao eneo la Kairo Mirerani, Wilaya ya Simanjiro, mkoani Manyara.
Kaka wa marehemu, Israel Msuya, alisema jana kuwa mazishi hayo yatafanyika makaburi ya familia ya mzee Elisaria Msuya ‘Kikaango’, baba wa marehemu Erasto.
Kwa mujibu wa Kamati ya Maandalizi ya mazishi hayo inayoongozwa na kaka mkubwa wa familia ya Msuya, Gady, zaidi ya Sh100 milioni zimepangwa kugharimia shughuli za maombolezo na mazishi.
Jeneza na gari maalumu la kubebea mwili wa marehemu yameagizwa kutoka Kampuni ya Montezuma & Monalisa Funeral Home ya Nairobi, Kenya kwa gharama ya Sh8 milioni.
Chakula, vinywaji, mapambo na magari ya kukodishwa kutoka Arusha kwenda Mirerani na kurudi yanatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh80 milioni.
Katika hatua nyingine, polisi mkoani Arusha imeendelea kuwahoji wafanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani, wilayani Simanjiro, wakidaiwa kuhusika na kifo hicho.
Habari zilizopatikana jana zinadai mfanyabiashara mmoja kijana ambaye aliibuka ghafla kuwa tajiri mkubwa kutokana na biashara ya madini ya Tanzanite, anashikiliwa Arusha kwa mahojiano.


Jana, kwenye viunga vya Mji wa Mirerani watu walitangaziwa kuwa mfanyabiashara huyo, alikuwa anashikiliwa kwa mahojiano kuhusiana na kifo hicho.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, hakupatikana mara moja kuelezea suala hilo kwani simu yake ilipopigwa ilikuwa haipatikani.
Marehemu ameacha mke na watoto wanne, huku akiacha rasilimali nyingi ikiwamo jumba la kifahari lililopo Sakina kwa Idd, hoteli maarufu za SG Resort na Mezza Luna zilizopo Arusha.

Tuesday, May 07, 2013

Rais Kikwete Atembelea Kanisa Lililopigwa Bomu Arusha

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea wakati alipotembelea Mei 7, 2013 katika kanisa la Mtakatifu Joseph kitongoji cha Olasiti jijini Arusha lililoshabuliwa na magaidi Jumapili iliyopta Video kwa hisani ya Kaka Michuzi

Rais Kikwete Akutana na Askofu Mkuu wa Arusha


Rais Kikwete alipoongea na Maaskofu wa madhehebu mbalimbali wa Arusha nyumbani kwa Askofu Mkuu Jimbo la Arusha Muadhama Josephat Lebulu jijini Arusha 
Mei 7, 2013

Video kwa hisani ya Kaka Michuzi

Rais Kikwete Aongea na Waandishi wa Habari - Mlipuko wa Bomu Kanisani Arusha

RAIS KIKWETE ALIPOONGEA NA WANAHABARI BAADA YA KUTOA POLE KWA WAFIWA NA MAJERUHI WA WAATHIRIKA WA MLIPUKO WA BOMU KANISA LA OLASITI, ARUSHA Video kwa hisani ya Kaka Michuzi

Sunday, May 05, 2013

Mlipuko wa Bomu Katika Kanisa Katoliki Arusha


 HABARI KWA KIFUPI:Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.
Anasema ni tukio la kighaidi.

Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu.

Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi.

Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana.

Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano



Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi.
Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.
Tanzania Field Force Unit (FFU) on site of Catholic church bombing
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ibrahim Kilongo.


JESHI la Polisi Mkoani Arusha linamshikilia mtu mmoja ambaye anahusishwa na kutokea kwa mlipuko uliotokea katika kanisa la Katoliki la St Joseph Olasiti Arusha leo asubuhi.

Tukio hilo lilitokea wakati Balozi wa Papa kutoka Vatican akizindua Parokia hiyo mpya ya St Joseph Olasiti ya Jijini Arusha.
Kanisa lililolipuliwa likiwa linaonekana kwa mbali huku wananch wakilitazama kwa mbali kutokana na tishio la kutokea kwa milipuko mingine ...Mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na tukio hilio wakati wengine wanasadikika kukimbia.
Majeruhi wa tukio hilo wakiwa katika hali mbaya..
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMRQWe-3DwwaUndhYh1ip8NOsy0SUDnS9ZaDT4mkleioWUxd9pwcn58XwJEoIty_6JpgECCFiBJrCcsQ3dQoNHKMVOYKG_Ov_IeEUNXNFszp3wwIvmBnDmaMwcziTz4a6MJJKIWA/s1600/IMG_20130505_130432_0.jpg
Waumini pamoja na baadhi ya wanacchi wakiwa katika hali ya taharuki wasiamini nini kilichotokea kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea asubuhi ya leo.






Kanisa Katoliki Lalipuliwa na Bomu Arusha Wakati wa Ibada!

 Hivi Tanzania kuna nini siku hizi? Mapadri wanauawa, kanisa zinachomwa moto na sasa kulipuliwa na mabomu!  Tunalilia nchi yetu!  Shaidi anasema kuwa wakati wa Misa maalum ya kubariki kanisa jipya mwanaume fulani alitokea na kurusha bomu ya petroli.  Baada ya kuirusha alikimbia nje ya kanisa na kuingia ndani ya gari na kuondoka. Misa ilikuwa inafanyika mbele ya kanisa.

KWA KIFUPI:

Mkuu wa Mkoa Mulongo nae yumo kwenye hili sakata. RPC Anatoa hotuba.

Anasema ni tukio la kighaidi.

Anasema alihusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu.

Anasema wanawasaka waliohusika. Anomba mwenye taarifa yo yote aisaide polisi.

Waliojeruhiwa ni 30 majeraha ya kawaida, na 3 wamejeruhiwa sana.

Mtu mmoja anashikiliwa kwa mahojiano

Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DAR ES SALAAM (Reuters) - A suspected bomb blast struck a Catholic church in the northern Tanzanian town of Arusha on Sunday, police said, wounding a number of people.
Sectarian tensions have been simmering in east Africa's second biggest economy after two Christian leaders were killed in the predominantly Muslim islands of Zanzibar earlier this year and there have been attacks on Muslim leaders and mosques.
"Some kind of explosion went off at the church. It is believed to have been a bomb but we don't know what type of bomb it was," Tanzania police spokesperson Advera Senso said.
Senso could not confirm if anyone had been killed in the attack or how many had been wounded.
Tanzania's foreign affairs minister Bernard Membe said in a message on Twitter he was "deeply shocked" by the explosion.
President Jakaya Kikwete has warned about rising religious tensions in several televised addresses.
(Reporting by Fumbuka Ng'wanakilala; Editing by Richard Lough and Mike Collett-White)

********************************************

ARUSHA, Tanzania, May 5 (Xinhua) -- A bomb blast hit a Catholic church on Sunday in Arusha in northern Tanzania, killing one child and injuring more than 30 people, witnesses reported.
The dead was among the church followers who were gathering for Sunday prayers.
The church located in Arusha's Olasiti suburb was bombed just before a mass in the presence of Bishop Josaphat Louis Lebulu of Arusha Diocese, who was accompanied by a representative of Pope of Vatican.
Police in Arusha said one man was arrested in connection with the incident, which caused a lot of panic in the tourist capital of the East African country.
Casualties are yet to be updated. "We are still working on the matter. We'll give more detail after investigating the matter," said Arusha Regional Police Commander Liberatus Sabas.
He said the man was arrested following a tip-off from people at the scene when the explosion occurred.
"We are still interrogating the suspect," he said.
Regional Commissioner Magesa Mulongo described the blast as horrific and unique in Tanzanian history, calling on the public to remain calm.
"So, people should continue with their daily activities, as police and other security organs have normalized the situation," Mulongo said.
A witness said, "I saw more than 30 people, taken by a police vehicle, which took them to the Mount Meru Regional Hospital."
Another witness said the bomb hit the church at around 10:00 a. m. local time when church followers were gathering for the historic Sunday prayer at the new church.
"We were trying to organize ourselves for the mass, when we heard loud sound, the situation that made more people to start rushing out of the church," a witness told Xinhua.
This is the first bomb explosion at the church in the northern safari capital of Arusha. 



One of those injured in Bombing receiving First Aid

Monday, December 03, 2012

Mh. Shy-Rose Bhanji Akutana na Aga Khan



Kiongozi Mtukufu Aga Khan ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) na Kiongozi wa Waislamu wa Ismailia akizungumza mawili matatu ya kimaendeleo na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mh. Shy-Rose Bhanji wakati wa ufunguzi wa Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki mkoni Arusha. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Kidiplomasia ya AKDN Dkt. Shafik Sachedina. ( Picha kwa Hisani ya Ikulu)

Tuesday, November 20, 2012

East Africa Ultimate Frisbee Tournament

East Africa Ultimate Frisbee Tournament

Arusha, Tanzania

November 23-24, 2012

Ausha Ultimate Frisbee Association is pleased to announce the East Africa Ultimate Frisbee Tournament which will be held in Arusha, Tanzania on November 23-24, 2012, Four teams will be participating in game played at Arusha Technical College:-

The teams that will be participating:

1) MOSHI KILL KILLERS -Captain: Frank Mushi

2) MWANZA TOSSERS -Captain: Andrew Bergman

3) ARUSHA ULTIMATE FRISBEE -Captain: Silau Ole Nyasi

4) NAIROBI ULTIMATE -Captain: Aaron Colverson

For any additional information and request, please call one of The Organizers Oli - 0684082908 or 0752216040

Friday, November 16, 2012

Rais Kikwete Afunga Mkutano wa Majaji Mjini Arusha Leo


Waheshimiwa majaji wakimsikilia Rais Jakaya Mrisho Kikwete  wakati wa kufunga mkutano wa siku nne wa Majaji uliofanyika katika hoteli ya Snow Crest jijini Arusha leo Novemba 16, 2012



Rais Jakaya Kikwete akikufunga mkutano wa siku nne wa Majaji uliofanyika katika hoteli ya Snow Crest jijini Arusha leo Novemba 16, 2012.Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Nhe. Magesa Mulongo Jaji Mkuu Mhe. Mohamed Chande Othman, Waziri wa Sheria Mhe Mathias Chikawe, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi Mhe Fakih Jundu

 Picha na Ikulu

Thursday, August 02, 2012

Rais Kikwete Atoa Kifuta Jasho cha Ng'ombe kwa Wananchi wa Monduli

RAIS KIKWETE ATOA KIFUTA JASHO CHA NG'OMBE KWA WANANCHI WA MONDULI

(Picha na Habari Kutoka Ikulu)



 Rais Jakaya Mrisho kikwete akizindua mpango wa kugawa ng'ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jashp cha kupoteza kiasi cha mifugo 800,000 kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009


Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi ng'ombe mmoja wa wakaazi wa Monduli walioathririka na na ukame mwaka 2008/2009 ambapo walipoteza mifugo yao yote. Hafla hii imefanyika leo Monduli. Picha na Ikulu.


SERIKALI itakuwa inagawa ng’ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha karibu mifugo 800,000 iliyopotea kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.

Ahadi hiyo imetolewa leo, Alhamisi, Agosti 2, 2012 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipozindua Mradi wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo kwa waliopotelewa mifugo yote katika Wilaya ya Monduli kwenye sherehe iliyofanyika Makuyuni wilayani humo.

Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi wa Mkoa wa Arusha wakiwemo wakuu wa wilaya na wabunge wa mkoa huo, Rais Kikwete amegawa ng’ombe 500 kwa kundi la kwanza la wananchi ikiwa ni mitamba minne na dume moja la kisasa kwa kaya 16 za mwanzo.

Uzinduzi huo ni wa pili kufanywa na Rais Kikwete chini ya Mradi huo wa kwanza wa aina yake kubuniwa na Serikali katika historia na wenye thamani ya sh. Bilioni 12.9.

Februari 19, mwaka huu, Rais Kikwete alizindua Mradi kama huo katika Wilaya ya Loliondo kwenye sherehe zilizofanyika mjini Loliondo. Kesho Agosti 3, 2012 Rais Kikwete anatarajiwa kuendelea na zoezi hilo katika mji wa Loliondo.

Sunday, December 04, 2011

Tanzia - Alfred Ngotezi (Mwandishi wa Habari)

The Late Alfred Ngotezi
Tumepata taarifa kwamba, Mwanahabari mwenzetu, Alfred Ngotezi amefariki ghafla akiwa mjini Arusha usiku huu. Ngotezi ni Mwandishi wa Habari za siku nyingi na alikuwa kifanya kazi hiyo akitokea mjini Mwanza, lakini baadaye akajiunga na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

NSSF wako mjini Arusha kwa ajili ya uenyeji wa Mkutano wa Kimataifa wa Mashirika ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika (ISSA) ambao utaanza Jumatatu 05.12.2011.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhani Dau ndiye aliyetujulisha kuhusu kifo hicho cha Ngotezi na baadaye Meneja Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume pia kutueleza kile kilichotokea.

Ilikuwaje?
Ni kwamba Ngotezi ameanguka ghafla na walipombeba wakitaka kumpeleka hosipitali, tayari alikwishapoteza maisha. Alikuwa anakula, then akaomba bendi impigie muziki, kisha akacheza vizuri tu. Alipomaliza kuburudika aliwapa mikono wanamuziki kama ishara ya shukrani, halafu alirejea kwenye meza na kuketi. Baada ya dakika chache kupita alinyanyuka kwenda chooni, lakini hakufika kwani alianguka kisha kukutwa na mauti.

Kwa wahariri tuliokwenda Tanga, Kagera na Mwanza, mtamkumbuka bwana huyu (Ngotezi) kwa michapo yake na ucheshi wake pia, kwani tulishirikiana naye sana. Ni miongoni mwa walioshiriki sana kazi ya kuratibu suala la mashamba ya mkonge kule Tanga.

Kifo chake ni pigo kwa tasnia ya habari kwani alituwakilisha vyema NSSF, lakini zaidi mchango wake katika sekta ya habari utakumbukwa daima. Pole nyingi kwa familia ya Marehemu Alfred Ngotezi, pole sana Dk Dau na wafanyakazi wa NSSF kwa ujumla na zaidi ya yote poleni sana wana habari wa Tanzania.

Ngotezi umetangulia, wengine tutafuata kila mmoja kwa zamu yake, RIP Alfred Ngotezi.


Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors' Forum (TEF

Friday, October 07, 2011

Worship Leadership Seminar - Arusha, Tanzania

 WORSHIP LEADERSHIP SEMINAR

Leading People to Experience God’s Presence

Charles Stanley once said that he believed that most Christians in most churches have never worshiped God. We go to church, but we don’t worship. We sing songs, but we don’t worship. We listen to sermons, but we don’t worship. All of these things are elements of worship but they are not worship in and of themselves which means that you can do all of them and yet have failed to truly worship God. We Christians often mistake the means of worship for worship itself.

According to famous researcher, George Barna, “Worship is a non-negotiable obligation and privilege of every Christian…We agree that when it comes to worship, God deserves it, the Bible commands it, and churches try to facilitate it," he stressed. "But we have a problem when it comes to worship. ... True worship is rare.”

The church in our times faces major challenges related to the renewal of worship. I believe one of them, if not the main one is a lack of understanding what a true biblical worship is. What you hear and understand you believe, and what you believe you’ll obviously do. That is life because life is not only in knowing but in doing.

A seminar for Worship Leadership will be held in Arusha that aims in tackling the challenges on Worship.

Date and Time: October 14-15, 2011 9am – 5pm

Venue: TAG Spiritual Power Center, Mbauda ARUSHA

The target audience: Worship Leaders/Pastors, Church Leaders, Musicians/Singers, Audio Technicians/Engineer, Recording Artist and any one related with Worship Ministry.

Seminar program will cover some topics in three areas but not limited to; Introduction to Biblical Worship: Understanding What is Biblical Worship, Applied Worship Ministry: Integrating Leadership and Team Dynamics, and The Role of Music in Worship: Balanced Approach to Music Ministry in Corporate Worship

Bless,

Pastor Nick

+255 788 740296, +255 717 425279

Friday, May 06, 2011

Wataalam Wasema Dawa ya Babu Inafanya Kazi Kiasi

Scientists at work on 'Babu' cure

Kutoka: The Guardian Tanzania



A technical report on retired pastor Ambilikile Masapila’s “miracle cure” has indicated that scientific data supports his claims to its positive effects on a number of ailments.

A report by experts from the National Institute for Medical Research (NIMR) Department of Traditional Medicine Research and Institute of Traditional Medicine, Muhimbili University of Health and Allied Sciences seen by The Guardian, says study findings have revealed that ‘Babu’s miracle cure’ prepared by boiling the roots of Carissa edulis plant is safe and has positive effects on cancer, epilepsy, herpes simplex virus, liver ailments, diabetes, blood pressure and anti-viral activity.

However, the scientists said since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, the government should advance the work of focused pre-clinical studies to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.

“The dose provided by Pastor Masapila which is one cup (about 200 mls) prepared through boiling an estimated 3.0 kg of whole root material in 60 litres of water “falls within safety window and no any overdose or acute poisoning event is expected.”

The results suggested that the plant has anticonvulsant activity which supports the claim of the use of the plant in the management of epilepsy as claimed by Pastor Ambilikile Masapila.

It further indicated that the herb has antidiabetic activity which supports the claim of the use of the plant in the management of diabetes.

The herbal has blood pressure lowering activity which supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of high blood pressure.

Research results show that the pastor’s concoction has hepatoprotective and antioxidant activity which are beneficial in the prevention of liver disorders and cancer.

“This result also reveals that Carissa edulis has potent anti-viral activity against herpes simplex viruses. Taking into consideration that, herpes simplex virus (HSV) infection is a major opportunistic infection in immunosuppressed persons, these findings supports the ethnomedicinal claim of the use of the plant in the management of HIV/Aids as claimed by Pastor Masapila,” said the report.

Drawing general conclusion, scientists said that the plant is safe and the dosage prescribed by Rev. Mwasapila is below the toxic level.

They, however, recommended that since the remedy is being widely used by an exceedingly large number of patients, focused pre-clinical studies need to be conducted to establish pre-clinical efficacy and safety of the remedy.

Scientists also recommended standardisation and formulation of “Babu’s cupful” for human use.

“MoHSW should conduct clinical trial on the prescribed remedy to establish in vivo efficacy and safety in humans and answer questions on optimum dosage, dosing schedule and duration of treatment per ailment,” stated part of the report.

It added “MoHSW should conduct clinical follow up on all patients recorded to have used the remedy for their prognosis.”

Recently, many people have been flocking Samunge village in Loliondo, Arusha, seeking the cure for chronic diseases such as diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/Aids.

According to Rev. Masapila, God instructed him through dreams since 1991 about the medication and that, it will heal people with chronic illnesses namely: diabetes, asthma, epilepsy, cancer and HIV/AIDS. The dream kept recurring to him several times since then and on August 26, 2010 he decided to obey on the instructions and started the healing work.

Earlier this month, HIV/Aids stakeholders blamed the government over its silence on HIV/Aids patients who abandon antiretroviral drugs after taking the herbal concoction being dispensed by Pastor Masapila in Loliondo.

HIV/Aids stakeholders said there was need to give correct messages to the people to avoid negative impacts in future.

SOURCE: THE GUARDIAN

Wednesday, March 30, 2011

Mama Charlotte wa Arusha atakuwa Cambridge, MA Jumamosi



Panther in Africa

with Guest Seaker and Former Black Panther Mama Charlotte

April 2nd, 2011 in Cambridge,Massachuetts


Pete O'Neal, Black Panther in Kansas City , was arrested on October 30, 1969 for transporting a gun across state lines. A year later, O'Neal with his wife, Charlotte Hill ONeal, aka Mama C, fled the United States and eventually settled in Tanzania , where he still lives in exile.


The African Cultural Society of St. Paul AME Church is showing A Panther in Africa on Saturday, April 2, 2011 at 4:00pm in the Christian Life Center , 85 Bishop Allen Drive in Cambridge.


Charlotte Hill ONeal and Pete ONeal are the subjects of the award winning PBS documentary about the lives and activism of the former Black Panthers. Mama Charlotte Hill ONeal will join us and will speak about her experience in the Black Panther Party and as co-founder of the United African American Community Center (UAACC), a non-profit NGO in Arusha, Tanzania with a mission to provide programs and projects for the enrichment of the Arusha community, both urban and rural, and to promote closer cultural ties to communities in America and around the world.


Mama C is an artist, poet, musician, community activist, and co- director of the UAACC. As a member of the Black Panther Party, I was taught the importance of building international solidarity among all people while honoring my Ancestral roots. That philosophy has never changed. Many of my poems and songs reflect this burning desire and mission to spread peace, love and unity through my art, Mama C reflects.


For more information, e-mail sondela@verizon.net or call 617-930-4740.


The Black Panther Party rose to power in the late 60s to uphold self determination and collective vision offering programs such as the Free Breakfast for Children and Free Health Clinics. Pete and Charlotte are proud to have been a part of that historic chapter of American history. Our present day community outreach service continues to be informed by our time as Black Panthers, Pete acknowledges. Our work is truly a continuation of the work we did as members of the Black Panther Party!


The program is sponsored by the African Cultural Society of St. Paul AME Church and the Boston Pan-African Forum with support from Boston University African Studies Center Outreach Program.

Saturday, January 08, 2011

TAMKO LA CUF KUHUSU MAANDAMANO YA CHADEMA ARUSHA

THE CIVIC UNITED FRONT (CUF – Chama Cha Wananchi)

VYOMBO VYA DOLA VINAHATARISHA AMANI YA NCHI.

CUF - Chama Cha Wananchi kimeumizwa sana na kitendo cha kinyama kilichofanywa na jeshi la polisi na serikali ya chama cha mapinduzi kuwapiga na kuwaumiza viongozi, wanachama na wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na wananchi mbalimbali wapenda demokrasia na haki ndani ya nchi yetu waliokuwa wakiandamana kwa amani jijini Arusha jana tarehe 05 Januari 2011. Tunalaani vikali kukamatwa na kwenda kuhojiwa kwa Wabunge wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Taifa Mhe. Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai , Mhe. Godbless Lema Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Joseph Selasini Mbunge wa Rombo na Mhe. Philemon Ndesamburo, Mbunge wa Moshi Mjini.

CUF inaamini kuwa CHADEMA kama chama cha siasa kilichosajiliwa kihalali ndani ya nchi yetu kilikuwa na haki ya kikatiba na kisheria ya kufanya maandamano yao ya amani ambayo mwanzoni tayari jeshi la polisi jijini Arusha kupitia kwa kamanda wa polisi wa mkoa lilishaahidi kutoa ulinzi wa kuyaweka maandamano hayo salama.

Jeshi la Polisi na Serikali ndiyo wanaostahili kulaumiwa kwa uvunjifu wa amani uliotokea Arusha. Ushahidi wa kimazingira unaonyesha wazi kuwa amri ya kusitisha maandamano iliyotolewa na IGP saa chache kabla hayajafanyika ilitokana na shinikizo za kisiasa. Hoja iliyotolewa kuwa taarifa za kiintelijensia zinaonyesha kutakuwa na uvunjifu wa amani na ndiyo maana maandamano yanazuiliwa ni usanii mtupu. Kama kweli polisi wana taarifa za kiintelijensia kuwa kuna watu watavunja amani basi wazitumie taarifa hizo kuwadhibiti watu hao na siyo kuyasitisha maandamano na kuwanyima wananchi uhuru wa kisheria wa kufanya maandamano.

Nchi hii inapaswa kuongozwa na katiba na sheria na Watanzania tusikubali Serikali iliyoko madarakani kutumia vyombo vya dola kuua uhuru na demokrasia ya nchi yetu.

Hivi sasa jeshi la polisi limekuwa mstari wa mbele kuzuia kila aina ya madai yanayotolewa na vyama ili mwisho wa siku jeshi lifanye kazi yake kuu ya kulinda CCM na utawala wao kijeuri na kisanii. Haiwezekani kila watu wakitaka kuandamana jeshi la polisi lianzishe hoja ati “kwa sababu za ki-intelijensia” maandamano hayo yanafutwa. Hizi taarifa za ki-intelijensia ni zipi?

CUF inaamini kuwa polisi na serikali ya CCM wanataka kutumia kitisho cha ugaidi kilichozikumba Kenya na Uganda kama sababu ya kupinga mikusanyiko mikubwa ya kisiasa kwa lengo la kuitetea Serikali. Lazima tujiulize,hivi magaidi wakitaka kulipua Tanzania mbona kuna sehemu nyingi sana ambazo wanaweza kufanya hivyo bila kusubiri maandamano ya CHADEMA au CUF au vyama vingine?

Hivi tujiulize kama kweli pana tishio la ugaidi iweje mechi za mpira ziendelee bila kuzuiwa na polisi? Mikusanyiko yote inafanyika isipokuwa maandamano ya vyama vya siasa tu? Hawa magaidi walio tishio kwa jeshi la polisi wanaotaka kulipua maandamano peke yake wametokea wapi? Kwa nini nchi hii iendeshwe kisanii na kiujanja ujanja namna hii? Kwa nini serikali inaogopa maandamano?

CUF inalaani ukatili waliofanyiwa wakazi wa Arusha katika maandamano ya CHADEMA na kuwa ukatili huo hauvumiliki na unahatarisha amani na utulivu wa kweli wa nchi yetu.

Ukatili huu hauna tofauti na ule tuliofanyiwa CUF – Chama cha Wananchi tarehe 28/12/2010 ambapo maandamano ya amani yaliyokuwa yaongozwe na Kaimu naibu katibu mkuu Julius Mtatiro yalipigwa marufuku ghafla na kisha mamia na mamia ya polisi wakisheheni silaha za kila aina wakaanza kuwapiga na kuwakamata wafuasi wa CUF na wananchi wengine walioshiriki katika maandamano yale. Kitendo kile ambacho polisi walikifanya kimetia doa kubwa sana jeshi la polisi linaloongozwa na kiongozi tunayemheshimu IGP Said Mwema.

Kitendo hiki cha pili kilichofanyika Arusha kinazidi kuharibu kabisa sifa na uaminifu ambao vyama vya siasa vilikuwa nao juu ya IGP Mwema. Ni muhimu sana kwa taifa letu kwa IGP Said Mwema kulinda heshima yake na asikubali kutumiwa kisiasa kukandamiza demokrasia ndani ya nchi.

Chama cha wananchi CUF kinaamini kuwa ustawi wa demokrasia, utawala bora, usawa, maendeleo ya nchi yetu na amani ya nchi havitaletwa kwa mtutu wa bunduki wala mabomu wala kila aina ya nguvu, hata kama CCM wataendelea na mbinu zao za kuwadhibiti wapinzani hatutokaa kimya na wala hatutoacha kutumia fursa za kikatiba kutoa maoni yetu kwa njia ya amani kama walivyofanya CHADEMA tarehe 05/01/2011 na CUF tarehe 28/12/2011.

Tunaamini walichokuwa wakipigania CHADEMA jijini Arusha ni kitu cha msingi sana,walikuwa wakipinga kitendo cha kukiuka demokrasia katika uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha. CHADEMA hawakuwa na budi kutumia njia za kidemokrasia kuonyesha kutokukubali na kutotambua utaratibu huo wa kinyemela ulioendeshwa na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha kwa manufaa ya CCM.

CUF inawapa pole wahanga wote waliopigwa na kuumizwa na mabomu, risasi, maji ya kuwasha n.k katika tukio hilo la kihistoria la kudai haki ya wanyonge jijini Arusha. CUF iko pamoja nao katika kuendelea kupigania haki. CUF inawapa pole viongozi wote wa CHADEMA waliokamatwa katika maandamano ya Arusha na tunawataka waendelee na juhudi za kupigania ukombozi kama inavyofanya CUF.

CUF inamtaka Rais Jakaya kikwete kutumia busara za hali ya juu sana katika kuendesha nchi katika kipindi hiki ambacho anamalizia miaka yake mitano ya mwisho. Rais Kikwete ana fursa ya kujenga misingi imara ya demokrasia ili akitoka madarakani akumbukwe kwa mambo ya heri na siyo kwa mambo ya shari.

Kukaa kimya kwa Rais wakati polisi wanatumia nguvu kubwa kuua demokrasia ndani ya nchi kunaashiria kuwa wanatimiza amri ya Rais.

Pamoja na mambo yote hayo CUF inawataka Watanzania kuendelea kutuunga mkono ili tuweze kuendeleza mapambano ya kudai demokrasia na maendeleo ya kweli ya nchi yetu kama chama mbadala kitakachomkomboa Mtanzania.

Mwisho tunawataka wakazi wote wa Arusha, Dar es salaam na mikoa mingine wazidi kuungana na CUF na wadau wengine wote muhimu katika madai mazito ya kudai katiba mpya.

CUF inaamini suluhisho la sehemu kubwa ya ukatili unaofanywa sasa ni kukosekana kwa katiba mpya itakayotoa mwongozo sahihi wa taifa letu. Tofauti na sasa ambapo jeshi la polisi na vyombo vingine vya dola vinaweza kufanya lolote wanalotaka juu ya maisha ya watanzania huku katiba ikiwalinda au wanaivunja na hakuna mwenye mamlaka ya kuwauliza.

Tanzania inahitaji Katiba Mpya ya Wananchi wenyewe na Tume Huru ya Uchaguzi. Tamko la Rais la kuunda Tume Maalum ya Katiba na ishara nzuri ukilinganisha na matamko ya awali ya Waziri wa Sheria na Katiba. Hata hivyo ni muhimu Rais akawafafanulia Watanzania kuwa lengo la mchakato mzima ni kupata Katiba Mpya yenye misingi imara ya demokrasia itakayotokana na ushiriki wa wadau wote. CUF inawaomba na kuwasisitiza Watanzania watuunge mkono sana ili tuhakikishe kwa pamoja tunapata katiba itakayoandikwa upya na kubeba matumaini ya Watanzania na siyo kuwekwa viraka kwa katiba iliyopo.

Imetolewa na

Prof Ibrahim Haruna Lipumba
Mwenyekiti - CUF.
06 Januari 2011.
Dar es salaam.

Monday, June 14, 2010

Mtoto Nicole wa Arusha

Wadau, hakuna raha kama kuangalia maendeleo ya mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia. Mdau Nicolas wa Arusha amenitumia picha za mwanae wa kwanza Nicole. Nicolas alikuwa hapa Boston na Minnesota kabla ya kurudi Tanzania. Alioa mwaka juzi na Mungu amembariki na mtoto mrembo Nicole.

*******************************************************************



Hi,
I believe God is still faithful to you, as He's been and will always. In brief, we're doing well here in Arusha. Our beloved kid/daughter, Nicole "Shimilimana" is doing well, being now 6 months old, since May 23, 2010.

Blessed,Nico, Nicole and Siima

Monday, December 15, 2008

Funga Mwaka Arusha


MWANAFA, AY NA C4 DJS UNIT KUFUNGA MWAKA ARUSHA

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya (AY) na Hamis Minyijuma (MwanaFA) wanaotesa katika anga ya muziki kwa sasa, wanatarajia kutoa burudani ya aina yake kwenye uzinduzi wa kundi la C4 DJs linaloundwa na wachezeshaji muziki ambalo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika mkesha wa sikukuu ya Krismas ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’ jijini Arusha. Kundi hilo linaundwa na Ma-DJ wenye uzoefu wa siku nyingi wakiwemo DJ Joe, DJ Peter, DJ Gerry na DJ A-Plus. Pia kutakuwa na Madj wengine wakali kusindikiza uzinduzi huu wa aina yake.

Aidha maandalizi kwa ajili ya uzinduzi huo na sherehe za funga mwaka yanaendelea vizuri hivyo mashabiki wakae tayari kupata burudani ya aina yake. Uzinduzi huu ndiyo mwanzo wa mfululizo wa burudani ndani ya Ukumbi wa Club Triple ‘A’ hadi mwaka 2009.

MaDJ hao wa kitanzania waliobobea katika fani hiyo wameamua kuzindua umoja huo ili kuonyesha kwamba wapo pamoja na watatoa kipaumbele kwa wahusika wote katika tasnia hii. Baada ya uzinduzi kutakuwa na program ya burudani kabambe ndani ya Ukumbi wa Triple ‘A’.
Siku ya Krismasi kundi la C4 litaandaa onyesho litakalofahamika kama ‘White Party’ambapo wateja watakaopendeza ndani ya mavazi meupe watapewa zawadi kemkem za papo kwa papo.
Na kwa mara ya kwanza katika historia ya burudani katika Ukumbi wa Triple ‘A’ Arusha kutakuwepo na shindano la kumsaka malkia wa Desemba (Miss Desemba). Shoo hiyo itafanyika usiku wa tarehe 26 Desemba. Shoo hii ya aina yake itawahusisha warembo kumi wenye vipaji mbali mbali.

Burudani ya Funga Mwaka katika jiji la Arusha inatarajia kuleta mageuzi makubwa katika fani ya muziki na burudani nchini Tanzania.

Funga mwaka hii itatoa fursa kwa C4 DJs kupata fursa ya kuonyesha umahiri wao katika kupangilia muziki ikiwa ni moja ya lengo la kuendeleza fani hiyo ya muziki ambao ulishika chati zaidi katika miaka ya 80 na 90 kabla muziki wa dansi haujateka soko na watu kuwapa kisogo maDJ.

Katika kuhitimisha Funga Mwaka Kundi la C4 limeandaa bonge la Bethdei party kwa ajili ya kusherehekea mafanikio ya Club Triple ‘A’ zaidi ya miaka kumi.

JOSEPH NAMALOWE (DJ JOE)
MRATIBU

Monday, November 24, 2008

Mike Sikawa Laid to Rest


REST IN ETERNAL PEACE MIKE.

*********************************************************************

Kutoka Daily News:

Mike Sikawa laid to rest

CHARLES KIZIGHA in Arusha

Daily News; Monday, November 24, 2008

Former Prime Minister Edward Lowassa, accompanied by his wife Regina, yesterday led hundreds of mourners from all walks of life at the burial of veteran journalist Mike Sikawa at Mareu village in Arumeru district, Arusha region.

The well-attended burial service was preceded by paying last respects at the Mareu Rural Cooperative Society grounds, a stone’s throw away from his place of domicile. Mike was laid to rest at the family’s farm where his father and mother were buried.

Prior to paying last respects several speakers, including Mr Lowassa, described Mike as one of the outstanding journalists in the country and Africa at large. The same was echoed by the head of the BBC Kiswahili Service, Solomon Mugera who led a team of four BBC staff to represent the Broadcasting House.

“Although Mike had been sick for a long time, his colleagues did not know because he did not show any sign and continued working normally. This proved that Mike was a hard working journalist and was ready to go out for assignments without showing any hesitation much as he was sick,” said Mr Mogera.

The mourners, who included the clergymen from various churches, government leaders, representatives from AICC, Tanapa and Retired General Mirisho Sarakikya, said the only way to remember Mike is to continue practicing excellent journalism. Mike joined the 'Daily News' and 'Sunday News' in 1975 until 1994 when he joined the BBC. He begun battling with diabetes in 1978 and underwent several treatments inside and outside the country until November 18 when he lost the battle.

**********************************************

Navyokumbuka mimi aliondoka Daily News 1984. Na siyo 1994. Walibandika notice ubaoni newsroom kutujulisha.

Wednesday, November 19, 2008

Mike Sikawa wa BBC Afariki Dunia

(Mike Sikawa 1982 Dar es Salaam, Tanzania - Mike alinitumia hizi picha nikiwa denti Form Five, Tabora Girls. Mbona nilitamba nazo, kwanza zilikuwa za rangi, halafu pili alikuwa mwandishi wa habari maarufu sana hivyo kujuana naye ilikuwa fahari kweli. Miaka yote hii nimekaa nazo.)

*******************************************************************

Nimepokea habari za kusikitisha sana leo. Mwandishi wa Habari wa BBC, Mike Sikawa, amefariki dunia. Aliwahi kufanya kazi Daily News. Alikuwa na kipaji mkubwa wa kuandika habari mpaka Daily News walimpa 'special privileges'.

Nilikutana naye kwa mara ya kwanza nikiwa nasoma 'A' levels Tabora Girls. Nilikuwa likizo Dar na tuliktana kwenye party Chuo Kikuu cha DSM. Wakati huo Mike Sikawa alikuwa maarufu sana. Nilimwambia kuwa nataka kuwa mwandishi wa habari na yeye alisema kuwa huo kazi haufai mwanamke. Nikamwambia kuwa hata hivyo bado nataka kuwa mwandishi wa habari. Nilianza kazi Daily News Agosti 1984, na baada ya muda mfupi yeye alitoka na kwenda Uingereza. Nilikutana naye tena miaka ya 90 na Mike aliniambia kuwa alijua nitakuwa na mafanikio makubwa katika uandishi wa habari.

Nakumbuka huo ugonjwa wa kisukari ulianza kumsumbua wakati huo na ndo ulimaliza.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

****************************************************
Kutoka Lukwangule Blog:

Mike Sikawa wa BBC afariki dunia

MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari.

Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha.

Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni.
Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote.

Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia.
Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti.

Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro.

Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini.

Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi.

Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo.

Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.

Kwa habari zaidi soma:

http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=8536