Showing posts with label Parliament. Show all posts
Showing posts with label Parliament. Show all posts

Saturday, October 25, 2014

Mh. Shy-Rose Bhanji Ajibu Shutuma Dhidi Yake

Mh. Shy-Rose Bhanji
Mimi Shy-Rose Bhanji, Mbunge wa Afrika Mashariki-Tanzania, ninapinga vikali na kwa nguvu zote shutuma zilizotolewa dhidi yangu kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Shutuma hizi hazina ukweli wowote na zinalenga, si kuniharibia, bali kuchafua sifa yangu na utendaji kazi wangu katika Bunge la Afrika Mashariki.
Lengo kuu la shutuma hizo ni kunivunja nguvu na ari ya kutetea maslahi ya nchi yangu na Watanzania wenzangu kwani daima nimekuwa kikwazo na mwiba kwenye ajenda zinazokiuka maslahi ya Tanzania.
Kwa mfano ardhi ya Tanzania kugawiwa kwa wana Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kinyume na Sera ya Tanzania. Nimekuwa miongoni mwa wabunge wa Tanzania tulio mbele katika kulipinga suala hilo. Sishangai likinijengea uadui.
Isitoshe, kwenye ajenda ya kumuondoa madarakani Spika wa EALA, Dk. Margaret Zziwa, nilisimama kidete kwa kutounga mkono kwa sababu halikuwa na maslahi ya Tanzania na yalikuwa kinyume na malengo ya ushirikiano wa Jumuiya nzima.
Hoja ya kumuondoa Spika ilikuwa ni sehemu ya ‘mchezo mchafu’ ya ajenda ya siri ya kumweka kwenye nafasi hiyo mjumbe mwingine kwa maslahi ya wachache.
Jaribio hili la kumuondoka Spika lilifanywa na kushindikana mara tatu baada ya kukosa sahihi za kutosha kutoka Tanzania, ikiwamo ya kwangu.
Baada ya kampeni ya kumwondoa Spika kushindwa, wabunge kadhaa walikuwa wanasusia vikao vya Bunge wakati wameshachukua posho za vikao. Kwa mfano kikao kilichofanyika hivi karibuni hapa Dar es Salaam.
Malumbano ndio yamekuwa yakitawala na kuinyima Bunge akidi ya kuendelea na ajenda za mtangamano. Huu ni usaliti wa wazi kwa nchi zilizowachagua na kuwatuma katika Bunge la EALA.
Ukijaribu kuwaasa kwamba mwenendo huo si sahihi, unageuka kuwa adui.
Na sasa wameamua kunitukana na kuzusha tuhuma kadhaa kupitia mitandao ya kijamii ambako yote ni utunzi wa kisanii usiokuwa na chembe ya ukweli, uhalali wala ushahidi.
Wahenga walisema ‘akutukanaye hakuchagulii tusi’. Walete ushahidi wa tuhuma zote dhidi yangu.
Kwa mfano, shutuma kwamba nililewa pombe ndani ya ndege, kuvunja chupa, kufanya fujo na kufungwa pingu wakati wa safari ya Ubelgiji si kweli hata kidogo.
Kama hizi tuhuma ni za kweli, kwanini hazikupelekwa polisi, serikalini au vyombo vingine vya sheria baada tu ya tukio?
Ijewe wamesubiri wiki mbili baada ya madai hayo ya tukio la kutunga ndipo wajitokeze wakati wa kikao kinachoendelea mjini Kigali, Rwanda? Kwanini wasubiri kikao cha Kigali ndipo uzushi huu utolewe?
Tuhuma kwamba nimewatukana marais wa nchi tatu hazina mashiko isipokuwa kuhalalisha kampeni ya wale wanaonichafua na kuibua chuki kwa maraisi na raia katika nchi za Kenya, Rwanda na Burundi.
Ninayo heshima kubwa sana kwa marais wa nchi zote tano na raia wa nchi wanachama ambako mara zote nimepokewa na kuishi kwa amani na upendo katika nchi hizo. Naahidi kuedeleza heshima hii.
Hainiingii kichwani ni wapi nilipoteza heshima hii isipokuwa kwa wale wasionitakia mema ambao wamekusudia kufanikisha ajenda zao.
Shutuma zote dhidi yangu zimetengenezwa na watu ambao hatushabihiani katika hoja zetu na sishangai kwa hilo.
Mimi ni Mtanzania na ni Mbunge wa Tanzania. Hivyo nina wajibu wa kulinda na kutetea maslahi ya Watanzania ili kuleta mtangamano wenye uwiano sawa kwa nchi zote wanachama.
Ninaahidi nitaendelea kuwatumikia Watanzania kwa nguvu zangu zote na kutoa ushirikiano kwa wabunge wengine wa EALA kwa manufaa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Nimeyasema haya nikiamini kuwa: “Uongo ukiachwa usemwe mara nyingi unaweza kuaminiwa kuwa ni ukweli.”
Umoja Wetu Ni Nguzo Yetu
Mungu ibariki Afrika Mashariki
Asanteni,
Shy-Rose Bhanji
Mbunge EALA

Tuesday, March 11, 2014

Thursday, January 17, 2013

Wenye Hasira Kenya Wachoma Majeneza 221 - Yawakilisha Wabunge

Duh! Huko Kenya wananchi wenye hasira wamechoma moto majeneza 221 nje ya jengo la Bunge mjini Nairobi! Eti yanawakilisha wabunge 221 wa Bunge la Kenya. Wananchi wana hasira maana wabunge hao walionyesha uroho kwa kutaka mishahara na marupurupu yao yaongezeke marudufu.

Mshahara wa mbunge Kenya ni $170,000 kwa mwaka!  Walitaka wapatiwe bonasi ya $110,000. Huko kipato cha  wastani wa Kenya ni $1,700!   Hebu linganisha na Marekani. Mbunge anapata $150,000 kabla ya kukatwa kodi.  Kipato cha wastani kwa Mwananchi wa Marekani ni $45-50,000/-.   Lazima wakasirike!

********************************************************

Kutoka Yahoo News

NAIROBI, Kenya (AP) — Hundreds of demonstrators angered at the conduct of outgoing Kenyan legislators doused 221 coffins with gasoline and set them on fire Wednesday, causing an inferno outside parliament's main entrance.

Organizers of the protest said the coffins represented the end of an era of parliament's 221 legislators and burning the coffins symbolized the start of a new era away from the dishonorable acts that parliament was known for in the last five years. The legislators' term ended earlier this week. Police looked on as the caskets made of thin wood burned to ashes as protesters shouted and screamed in exhilaration.

"Bye bye parasites," shouted Sheldon Ochieng, 23, a college student studying community development. "MP's do not know their work; they are just stashing money in their pockets. It is time to have new leaders who serve the people."

Kenyans say their legislators are seen as lazy, greedy and self-centered for often improving their welfare lavishly at the cost of tax payers. A Kenya legislator earns about $175,000 a year in a country where the average annual income is $1,700. Last week Kenyan legislators attempted to award themselves a $110,000 bonus, but the president vetoed the legislation.

The package would also provide legislators with an armed guard, a diplomatic passport, and access to the VIP lounge at Kenyan airports and state funerals.

It was the second time the President Mwai Kibaki had refused to sign the bill adding the legislators' bonuses into law. In October members of parliament quietly awarded themselves the bonuses.

However, civil society activists say Kibaki, who is the 222nd legislator, is no different from other parliamentarian's because while he vetoed the hefty raises, he has approved hefty increments to a send-off package for when he retires after two terms in office following the country's March 4 elections.

The organizers of the protests Wednesday said they did not make a coffin for the president because of the veto, and the decision to give himself more money came after the coffins had been ordered.

"It was unsurprising that President Kibaki, while rejecting the MPs' pay deal, retained his own hefty retirement package. Moreover, the failure of his administration to rein in grand corruption remains a blot on what many see as credible efforts to grow the country's economy," said Boniface Mwangi, an official of a lobby group called Kenya Ni Kwetu, or Kenya is Our Home.

Atsango Chesoni, the executive director of the Kenya Human Rights Commission, said Monday that the president had contravened the constitution by approving the law that awards him hefty pension increments.

Chesoni said under the constitution Kenya adopted in 2010, the Salaries and Remuneration Commission is the authority charged with rationalizing and deciding the pay for public servants.

Mwalimu Mati, an anti-corruption activist, said the common argument from legislators is that they deserve pay increases because they have passed more bills. Mati said that argument is without merit. He said that although many laws have been crafted during the current parliamentary term, most of the legislation was passed without scrutiny due to low attendance at parliament.

Mati said the legislators spent a lot of time voting on bills for their own benefit, "like watering down sections of the integrity laws which would have required them to declare wealth." The legislators reduced academic qualifications required for one to be elected that were set out after country adopted the constitution in 2010, Mati said.

Tuesday, September 27, 2011

Tanzia - Mama Wangari Maathai (Mama Miti)

Mama Wangari Maathai (1940-2011)
Mama  Prof. Wangari  Muta Maathai, raia wa Kenya aliyepata Tuzo ya Amani ya Nobel, na Tuzo kibao kwa kazi na jitihada zake za kuhifadhi ardhi na miti amefariki nchini Kenya. Habari zinasema kuwa alifariki mjini Nairobi siku ya jumapili kutokana na ugonjwa wa kansa.  Chama chake cha Green Belt Movement kitendeleza kazi aliyoanza.

Mama Maathai alipigania haki za akina mama na maskini nchini Kenya. Alitunga vitabu kadhaa. Alikuwa mwanamke wa kwanza Afrika Mashariki kupata Ph.D katika sayansi za biolojia. Alipoona jangwa inazidi kukuwa nchini Kenya alianzisha mradi wa kupanda miti ili kuepuka janga hilo na hasa kuanzishwa kwa Green Belt Movement. Aliwahi kuwa Mbunge Kenya na pia alifungwa mara kadhaa kutokana na msimamo wake mkaliw wa kutunza ardhi ambayo mara nyingi ilipingana na serikali ya Kenya.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.     

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:  

Friday, June 24, 2011

Posho Za Wabunge



Nimeona hii FACEBOOK:

BASHE: Ombi Langu kwa Wabunge wa Chama Changukuhusu POSHO

Ombi Langu kwa wabunge wa chama changu, si kila jambo kulipinga swala la Posho (sitting allowance) hakuna sababu ya kulivalia njuga na kulazimisha kulipata,wabunge wanapata Mshahara,posho ya kuwa nje ya kituo ,posho ya ubunge FEDHA HIZI zinawatosha ukiangalia hotuba ya zito tunasema pato la mtanzania ni 770,000 lakini kuna asilimia 20% ambao wanashikilia 42% ya pato la taifa (32trillion) kati ya hizo wakati 20% ya masikini wa chini kabisa wanashikilia only 7% ya pato la Taifa.

Kwa mtazamo wangu ikiwa sitting allowance ambayo kwa ujumla wake ikipunguzwa tuta save 900bn fedha hizi zikiamuliwa kupelekwa katika sekta ya ELIMU kuondoa kero ya waalimu kuishi madarasani kwa kuwajengea nyumba, kwa majirani,ama kuondoa kero ya Mabweni ktk shule za kata,ama kuondoa kero ya MAABARA katika shule za kata,ama kupelekwa katika sekta ya Afya , tutakuwa kama Taifa tutamaliza tatizo kubwa sana tutaipunguzia serekali na walipa kodi mzigo wa fedha ambazo haziendi katika shughuli za maendeleo,Niwaombe wasiitazame hoja imetoka kwa nani wa chama gani waipokee na kuiunga mkono Mtakuwa mmeitendea HAKI nchi yetu,na watanzania ambao mustakabali wa maisha yao katika miaka mitano ijayo upo mikononi mwa serekali ya CCM (cham chetu) hata kama kama mnaipata kwa mujibu wa sheria na kanuni fanyeni cost benefit analysis kwa kuliangalia taifa na si nyinyi peke yenu.kama taifa tutfaidika zaidi fedh hizi msipopokea na kuamua kama bunge zipelekwe katika shughuli za maendeleo.

Wapo wabunge ambao wana jenga Hoja ya kwamba Posho hizo zinawasaidia ktk shughuli za Majimbo, inawezekana inaukweli,lakini kama MFUKO WA MAENDELEO WA JIMBO ,POSHO YA UBUNGE 5M,ALLOWANCE YA KUKAA NJE YA JIMBO 80,000,MSHAHARA 2M vyote hivi vimeshindwa kukusaidia kuhudumia Jimbo basi hata hiyo Posho haita weza,naamini mnatuongoza tutawaona si wabinafsi mkiunga mkono hili kwani mnachpata kwa maisha yenu kinawatosha.

Itendeeni haki Nchii hii katika kipindi hiki ambachi ambacho maisha yanazidi kuwa magumu shilingi inashuka, kuna vijana wenzetu million 11 wanahitaji msaada waliopo mashuleni na vyuoni wanahitaji msaada wenu mtakuwa mmetenda haki sana kwa kusamehe hicho kidogo,nimuombe Mbunge wangu aunge Mkono kusamehe hiyo Posho 70,000 ni Tofali 350 za kuchoma kwa bei ya kule kwetu ,mara siku za vikao ,ni fedha nyingi tutapata mabweni, maabara,ama fedha hiyo utakuwa umesaidia vijana wengi kulipiwa ada ktk shule za Kata. Kwahiyo ni vizuri likaungwa mkono jambo hili ili kuisaida Nchi

SOURCE: Bashe's facebook note