Showing posts with label Uchawi. Show all posts
Showing posts with label Uchawi. Show all posts

Saturday, April 13, 2019

Wehu Wavunja Kaburi ya Marehemu na Kubaka Maiti!

Imani ya Ushirikina (Uchawi) umezidi Tanzania!  Watu wanafukua maiti halafu wanaibaka!  Wana uchu ya pesa na mengine kuweza kufanya hivyo au ni wagonjwa wa akili?  Upumbavu! Mary Mkwaya Malamo alikuwa miaka 35. Alifariki mwanzoni mwa wiki.

*********************************************************************
The Late Mary Mkwaya Malamo

Mwili wa aliyekuwa Afisa wa Wizara ya Nishati Mery Mkwaya Maramo aliyefariki mwanzoni mwa wiki hii na kuzikwa jana katika Makaburi ya Pugu Mwakanga jijini Dar es Salaam, Usiku wa kuamkia leo (Ijumaa) watu wasiojulikana wameufukua na kuutoa nje ya jeneza kisha kuuvua nguo .
Kaka wa Marehemu Mary, Deogratius Maramo amesema inasemekana mwili wa marehemu uliingiliwa kimwili lakini bado wanasubiri ripoti ya Polisi ili wajue kilichomtokea ndugu yao.

Kaka huyo wa marehemu amesema kuwa hakuna kitu chochote kilichoibiwa kaburini humo.!


Kaburi la Marehemu Mary Mkwaya Malamo baada ya kuvunjwa na wachawi


Mnaweza kuangalia Video HAPA:

Maelezo ya Fundi aliyegundua Kaburi Imevunjwa. HAPA

Saturday, October 22, 2016

Pikipiki Mzimu Jijini Dar Yazua Hofu!

 Mwananchi akipita kwa kuikwepa pikipiki yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika Kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Dar es Salaam.
 Mwonekano wa pikipiki hiyo kwa nyuma.
Pikipiki hiyo ikiwa katika kijiwe hicho cha  Veterinary Maganga Temeke jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

PIKIPIKI yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Temeke jijini Dar es Salaam inazua hofu kwa wananchi na hata kwa askari polisi ambao wameshindwa kuipeleka kituoni.

Imeelezwa kwamba pikipiki hiyo iliegeshwa katika eneo hilo na mtu mmoja ambaye alifika nayo akiwa akiiendesha mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza jana na mtandao wa www. habari za jamii.com mmoja wa waendesha bodaboda wa kituo hicho ambaye hakupenda kujitambulisha jina lake alisema pikipiki hiyo inawapa hofu wananchi wa eneo hilo na hata waendesha bodaboda.

"Hata sisi wenyewe tuna hofu na pikipiki hii ndio maana tunaegesha mbalimbali na pikipiki zetu na ndio maana sitaki kutaja jina langu" alisema mwendesha bodaboda huyo.

Aliongeza kuwa awali baada ya pikipiki hiyo kutelekezwa katika kituo hicho mtu yeyote alipokuwa akiisogelea au kuigusa ilikuwa ikijiwasha yenyewe lakini baada ya kupita mwezi mmoja iliacha kujiwasha jambo ambalo limeongeza hofu kwa wananchi.

Mkazi mwingine wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Ismail alisema hata walipotoa taarifa kituo cha polisi cha Maganga walishindwa kuichukua pikipiki hiyo kutokana na tabia ya kujiwasha.

Alisema aaskari wa kituo hicho ambacho kipo mita 10 na eneo ambalo ipo pikipiki hiyo walitoa taarifa kwa wenzao wa kituo cha Chang'ombe ambao nao wameshindwa kuichukua na kwenda nayo kituoni kwa ajili ya kumtambua mmiliki wa pikipiki hiyo kupitia namba zake za usajili.

Ismail alisema inawezekana pikipiki hiyo ilifungwa kifaa maalumu cha utambuzi iwapo kama imeibiwa na ndio maana ilipokuwa ikiguswa au kusogelewa inajiwasha yenyewe licha ya baadhi ya watu wanahusisha kujiwasha kwake na imani za ushirikina.

Imeelezwa kuwa pikipiki hiyo wakati inatelekezwa ilikuwa katika hali ya upya lakini hivi sasa imeanza kupoteza upya wake kwa kukosa huduma ya matunzo.

Jitihada za mtandao huu kumpata Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa huo wa Maganga ili kuzungumzia suala hilo zimeshindika baada ya kuelekezwa alikuwa Manispaa ya Temeke kwenye mkutano.


Saturday, October 31, 2015

Siku ya Maruhani - Halloween

Na Swahilivilla blog. Washington D.C
Jana ililkuwa ni "Siku ya Maruhani" nchini Marekani. Siku hii ijulikanayo kama "Halloween" husherehekewa kila tarehe 31 Oktoba, na ina historia ndefu.
Siku ya Maruhani ilianzia huko barani Ulaya kiasi miaka 2,000 iliyopita ikifungamana na imani za kishirikina. Wazung walipoyavamia mabara ya Amerika walihamia pia na utamaduni mila, desturi, dini, na silka zao - na sema upendavyo. Miongoni mwa hayo ilikuwa ndiyo hii siku ya Maruhani ambayo jina lake la asili ni "Samhein".
Sherehe za Maruhani  Photograph by treasuredragon/iStock.
Tuyaachie ya historia kwa wanahistoria, lakini kwa ufupi hii iliaminika kuwa ni siku ambayo pepo, majini, maruhani, mazimwi na mizimu au mizuka ya watu waliokufa hurejea hapa duniani katika maeneo yao ya asili na kujichanganya na watu waliohai.
Maudhui kuu ya siku hii ni kutisha, kuadhibu na mauti, ingawaje katika enzi zetu za leo imekuwa ni siku kuu ya watoto zaidi kuliko watu wazima. Sherehe zake hufanyika kuanzia familia, mitaa, makazini na hadi kufikia Ikulu yenyewe. Rejea kwenye toleo la jana la Swahilivilla uone Ikulu ya Marekani ilivyoadhimisha siku hii akiwepo rais Obama na familia yake.
 Wana maruhani wakiwa katika kwaride. (Photo Jefferson Siegel/New York daily news)
Kama ambavyo kila siku kuu au sherehe huwa zinaaambatana na ada maalum ambazo zikikosekana basi siku hiyo huwa kana kwamba haijatimia, Siku ya Maruhani nayo pia ina ada na desturi zake. Na kama zilivyo sherehe nyingi hapa Marekani siku hii pia nayo imekuwa fursa ya wafanyabiashara kujipatia rizki zao.
Mapambo: Shamra shamra za Siku ya Maruhani huanza mapema, pengine tangu mwezi wa Septemba kwa kuweka mapambo kwenye majumba, mabarabara na hata sehemu za kazi na biashara. 
Na kama tulivyotangulia kusema, mapambo yote huwa yanalenga kwenye hali ya kutisha, kuadhibu na mauti. Miongoni mwa mapambo hayo ni buibui na nyumba zao, popo wakining'inia, mifupa na mabufuru ya vichwa vikiashiria watu waliokufa, panga, paka weusi, masanamu ya mizuka au mazombi na vimbwanga vyengine. Almradi kuonesha kuwa nyumba zimesibiwa na maruhani (haunted house). Si hasha ukapita vichochoroni ukakutana na kitu ukashtuka. Kwa ufupi ni kama vile tunavyoona kwenye picha za kutisha (scary movies).

Wednesday, September 04, 2013

Dawa ya Kuzuia Busha

Hawatokwenda kunywa dawa za kuzuia upofu, ngirimaji-busha na watagoma kupasuliwa busha kwa imani potufu lisha ya mabango haya vijijini na mijini. NGO hadi za nchi ya nje zipo kutuelimisha na kutugharimia lakini matokeo madogo lawama tu.

Saturday, June 15, 2013

Unyama Wanofanyikwa Zeruzeru Tanzania Katika Taarifa Ya Habari USA

By JACQUELYN MARTIN
Associated Press

   KABANGA, Tanzania (AP) - As an infant in rural Tanzania, Angel Salvatory was unusual. Snow white skin, blond hair, and blue eyes set her apart from others in her village. Those unique looks have also made her a target.

   "Her father thought she was a gift from God," says Salvatory's mother, Bestida Simon. "One that he could use to get riches."

   Since surviving an attack led by her father, Salvatory has spent the past four years living in the Kabanga Protectorate Center, a government safe house for people living with albinism.

   "Angel's father led a group to attack her. He had wanted to attack her since she was 3 months old. He thought if they'd take Angel to a witch doctor as a sacrifice that they could get rich," Simon said.

   Burning in the daylight and hunted in the shadows, having albinism is often a death sentence in East Africa. In Tanzania, one out of every 1,400 people has albinism, a genetic condition characterized by a lack of pigment in the body. That compares to a global average of one in 20,000 people according to Under the Same Sun, a Canada-based albinism advocacy group.

   The group says that more than 100 people with albinism have been physically attacked in Tanzania since 2006, including 71 who died. Albinos are widely seen as a source of magic in Tanzania's traditional communities.

   Long in danger and neglected in their own country, albinos in Tanzania now have a bit of hope for increased government assistance.

   In April members of Parliament heard emotional testimony that moved some to suggest making sun screen tax free, and Parliament voted to donate part of their salary to the cause.

   Severin Edward, a program officer with the Tanzania Albino Society, noted that parliament promised to set aside funds for the special needs of people with albinism and that the country's prime minister said the government has agreed to grant special priority to court cases involving albinos, to bring about justice faster.

   "This is the good point to start," Edward said by email last month.

   A government census done in 2012 could reveal the exact numbers of albinos in Tanzania. The portion of the census regarding people with disabilities, including albinos, is expected to be released in 2014.

   In Tanzania, albinos are often referred to as ghosts, or zero zero, which in Swahili signifies someone who is less than human. Legends here suggest that that even when an albinos is killed, he or she never really dies.

   Brutal attacks against albinos are often led by witch doctors who use albino body parts in potions they claim bring riches. In response, the government began placing children and adults with albinism into safe houses. Although they may be physically protected in the centers, many there feel imprisoned.

   In 2008 the government of Tanzania suffered a rash of negative stories by Western journalists about the killings of albinos, said Peter Ash, founder of Under The Same Sun.

   "These centers came in response to the killings. It's how the government has chosen to respond. The government has basically abandoned these kids," he said. "There is no long-term plan."

   Holding her 2-month-old baby Jessica on her back in a traditional kanga cloth, Helen Sekalima, 40, sorts dry beans. The dark-skinned mother came to live at the Kabanga Protectorate Center after her newborn infant was threatened.

   "The people in the village said that the children are not normal people, that they are like devils," Sekalima said.

   Her husband, Anderson Naimoni, doesn't agree with the idea of centers where, "our people are being turned into refugees," he says.

   Ash said his group discovered that in some centers emotional and even sexual abuse "was rampant." His group has informed the government "but they'll probably do nothing about it," Ash said.




   Experts say staving off attacks from witch doctors is just one of many issues that Tanzania's albino population must address. Low vision problems complicate schooling, and with little cultural precedent for skin protection rates of skin cancer are high. More than 80 percent will die by age 40 due to skin cancer, Ash said.

   In rural northwest Tanzania dried corn stalks sway gently in a field sheltering a concrete slab that protects the grave of 3-year-old Naimana Daudi from grave-robbers. The albino toddler was kidnapped at night and found in pieces in the morning.

   A tear slips down the dark cheek of her mother, 30-year-old Angelista Ngarama. After her daughter was killed, Ngarama took her youngest child, Ferister, to the Kabanga Protectorate Center. No one knows when it will be safe enough for the 2-year-old to return home.


Friday, June 29, 2012

Ogopa Magari enye Madirisha Tinted!

Nimepata kwa email, lakini hii kali!  Mambo ya ushirikina yataisha lini!!!!


*************************************************************

Dear Friends:

Leo nimeona ni vyema nika-share nanyi kisa hiki cha kutekwa mfanyakazi mwenzetu ambaye ni cashier siku ya jumatano jioni wiki iliyopita. Ni kama movie lakini ni ukweli, cashier wetu aliomba ruhusa siku hiyo ya tukio aende kwenye mkutano wa wasabato uliokuwa uliendelea viwanja vya biafra.

Yeye pia ni msabato aliyeishika dini ya Sabato haswa, kwa hiyo aliondoka saa kumi kamili badala ya saa kumi na moja. Baada ya dakika 40 tulianza kupokea sms zinazosema mwenye namba xxx amepata ajali na kufa papo hapo na kwa taarifa zaidi twende muhimbili hospital. Baada ya kutazama hiyo namba xxx ilikuwa ni ya cashier wetu. Tulijaribu kuipiga iliita tu bila kupokelewa, na pia tulipiga namba iliyotutumia sms iliita bila majibu. Ilipofika saa kumi na moja tuliamua kuelekea muhimbili, ma baada ya kufika pale emergence tukaambiwa tuelekee chumba cha kuhifadhia maiti. Tulioneshwa mwili wa mtu aliyepata ajali lakini haukuwa wa cashier wetu, tukawatuma wenzetu waende hospitali zote lakini hapakuwa na taarifa zake.

Baada ya kuzunguka bila mafanikio tulitoa taarifa makao makuu ya usalama barabarani na baada ya dk kumi wakatwambia kuwa hakuna taarifa za ajali mbaya iliyotokea jioni hiyo. Hatua iliyofuata ilikuwa ni kutoa taarifa polisi juu ya tulio hilo na ndipo waliposema kwa kuwa ni mtu mzima tusubiri hadi siku inayofuata.

Wakati huo huo ndugu zake pamoja na wafanyakazi wenzetu walikuwa pamoja wakiendelea na jitihada za kumtafuta hadi saa sita usiku.

Kilichokuwa kinatia wasiwasi zaidi ile namba iliendelea kutumia sms namba takribani zote zilizokuwa kwenye phonebook yake na ndugu zake hawakuwahi kuona ndugu yao akichelewa kiasi hicho.

Ilipotimu mida kama ya saa sita na nusu walisikia mtu akigonga mlango, alikuwa kaumizwa na amejaa matope, hakuwa na uwezo wa kuzungumza sana, ilibidi wampeleke kituo cha polisi na baada ya muda hospitali ya mwananyamala. Alipopata nguvu alianza kuwasimulia nduguze kilichotokea. Alipotoka ofisini alikwenda moja kwa moja kwenye kituo cha daladala cha karakana, pale kituoni walikuwa abiria wawili
yaani yeye na mama mmoja. Baada ya dk chache ilikuja coaster iliyoandikwa mbele Kawe na ilikuwa na tinted nyeusi, yule mama hakupanda sababu alikuwa anaelekea posta ila yeye alipanda. Ndani ya gari kulikuwa na watu watatu pamoja na dereva, wawili wakiwa wamekaa nyuma na mmoja akiwa amekaa karibu na driver. Gari hiyo hiyo ilikuwa ni mpya, mmoja wa abiria alimumba simu cashier apige simu
moja kwa jamaa yake maana alidai kuwa simu yake illiishiwa charge na walikuwa wametoka mtwara kupeleka maiti, alimuuliza cashier umri wake na kama ameoa na anafanya kazi wapi, cashier akamjibu hajaoa na hana kazi pia ana miaka 32.

Walipofika Tazara hawakutaka kupakia abiria yoyote na walikuwa wote wamevaa miwani myeusi, na ndipo akaanza kuingiwa na mashaka akaomba ashuke, wao wakamwambia watapita biafra na hawana mpango wa kusanya kwa kuwa hata yeye walimpa lifti tu.

Gari ilipokaribia taa za buguruni akainuka ili ashuke, jamaa wale wa nyuma wakamkalisha chini kwa nguvu, na sio kwenye viti yaani chini kabisa. Mmoja wao akafunga kitambaa cheusi kwenye macho na mikono ikafungwa kwa nyuma na mipira, baada ya muda akasikia kama wamempulizia perfume. Akihisi fahamu kumtoka polepole na neno lamwisho analokumbuka alisikia kuwa waelekee misitu ya Kibaha wakamalize kazi. Kilichomwamsha ni kofi zito alilopigwa na kusukumwa hadi nje ya gari. Alianza kulia na kuwasihi wasimdhuru, wakaanza kumrusha kichurachura huku wakimkanyaga.

Walikuwa wameshamfungua kitambaa machoni na waliacha gari umbali kama wa dk kumi na lilikuwa ni pori zito na giza, wao walivaa vitu usoni na walikuwa wamevaa gloves.

Wakamwekea simu yake mfukoni wakiwa wametoa simcard, walichomwambia wanachohitaji ni sehemu zake za siri na sio kitu kingine. Mmoja wao akaambiwa alete kisu kikali wanachokitumia, na walipompigia boss wao akawasisitiza nyeti zinazotakiwa lazma ziwe za mtu wa miaka 40 na kuendelea.

Mwenzao mmoja akasema cashier alisema alikuwa na miaka 32, baada ya kumkagua wakakuta card yake inaonyesha kazaliwa mwaka 1979. Kulingana na yeye asemavyo ndicho kilichomwokoa ila waliendelea kumkung'uta kwa hasira. Wakamrudisha kwenye gari na baada ya mwendo wakampakia kwenye gari nyingine ndogo iliyokuwa na watu wawili ambao walimchukua na kumtelekeza maeneo ya sayansi.

Hawakuchukua kitu hata kimoja wala kumwambia lolote, siku iliyofuata alipelekwa agakhan kwa uchunguzi zaidi na kwa sasa anaendelea vizurr. Kwa ufupi ni hayo, ukweli mwenyezi Mungu atulinde na tumwombe pia
abadilishe mioyo ya watu ambayo imekuwa migumu mno kwa ajili ya kupata vyeo na utajiri wa haraka.

Friday, March 13, 2009

Uchawi Kenya

Jamani, wachawi bado wapo Afrika. Hebu cheki huyo Bi Kizee, na inaeleka yeye kweli ni mchawi hakisingizwa!
Bi Kizee Karutu Chai wa Kilifi, Kenya akisindizwa na polisi kwenda kuondoa uchawi aliyomfanyia mtoto wa miaka 10 huko kijijini kwao!

Sunday, January 25, 2009

Mwizi Ageuka Mbuzi Nigeria


Wadau, huko Nigeria mbuzi kashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuiba gari. Watu walioshuhudia tukio wanasema kuwa eti mwizi alitumia uchawi kusudi ageuke mbuzi wakati anakimbia kutoka kwenye eneo la tukio.

Nilidhani kuwa Tanzania tuna imani kubwa na uchawi kumbe hata huko Afrika Magahribi wamo!

Ujumbe kwa polisi huko. Na nasema hebu lete huyo mbuzi tumgeuze nyama choma! LOL!

*******************************************************

Goat Detained over Armed Robbery

LAGOS (Reuters) – Police in Nigeria are holding a goat on suspicion of attempted armed robbery.

Vigilantes took the black and white beast to the police saying it was an armed robber who had used black magic to transform himself into a goat to escape arrest after trying to steal a Mazda 323.

"The group of vigilante men came to report that while they were on patrol they saw some hoodlums attempting to rob a car. They pursued them. However one of them escaped while the other turned into a goat," Kwara state police spokesman Tunde Mohammed told Reuters by telephone.

"We cannot confirm the story, but the goat is in our custody. We cannot base our information on something mystical. It is something that has to be proved scientifically, that a human being turned into a goat," he said.

Belief in witchcraft is widespread in parts of Nigeria, Africa's most populous nation. Residents came to the police station to see the goat, photographed in one national newspaper on its knees next to a pile of straw .

Friday, July 11, 2008

Hakuna Sumu! - Skandali ya 'Uchawi' Bungeni


Sijiui kama wabunge watakaa wakiamini kuwa wako salama sasa. Mkemia mkuu wa serikali anasema kuwa ule unga uliyomwagwa bungeni haukuwa na sumu. Lakini kwa wanaojua uchawi, huo sumu hauwezi kuonekana kabisa kwa binadamu wa kawaida. Kwa hiyo bado tutasikia mbunge fulani atakaa sehemu fulani huko Bungeni na baada ya muda kidogo atasema kuwa anajiskia kachoka kichwa kinamwuma nk.. Hii siyo mwisho wa skandali ya uchawi/juju Bungeni.


***************************************************************************


Unga uliomwagwa Bungeni hauna lolote-Mkemia

2008-07-11

Na Jackson Kalindimya, Dodoma

Hakuna ushahidi wowote uliopatikana wa mtu kuona au picha za mitambo ya kamera maalum-CCTV unaothibitisha kumwagwa sumu ndani ya ukumbi wa Bunge kama ilivyodaiwa.

Taarifa iliyotolewa jana mjini hapa na Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Naibu Kamishia wa Polisi, Bw. Omari Mganga, ilisema kuwa baada ya sampuli kukusanywa na kutumwa kwa Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali ambaye baada ya uchunguzi wake hakuweza kuona sumu yoyote ile inayotambulika.

``Kwa maana hiyo basi hakuna ushahidi wowote ule, uliopatiakana wa ama mtu kuona au poicha za mitambo ya CCTV au wa kisayansi unaothibitisha kufanyika vitendo kama hivyo`` ilisema taarifa hiyo.

Wakati wa kikao cha Mkutano wa kumi na mbili cha Bunge la Tanzania lilipoanza mkoani Dodoma, kulitokea minong\'ono au uvumi kuwa kuna Mbunge mmoja na Afisa Mmoja walionekana ndani ya Ukumbi wa Bunge wakizunguka kwenye viti vya waheshimiwa Wabunge huku wakinyunyizia vitu/unga uliohisiwa ulikuwa kwa ajili ya kudhuru binadamu au imani za kishirikina.

Kamanda Mganga alisema, katika taarifa yake kuwa, baada ya kuenea kwa uvumi hadi kwenye vyombo vya habari, uchunguzi ulifanyika kwa kukusanya ushahidi mbalimbali. ``Watu mbalimbali walihojiwa na hakuna hata mmoja aliyeweza kuthibitisha kuwa aliona watu wa aina hiyo wakifanya hayo yaliyokuwa yakiongelewa,`` ilifafanuliwa.

Alisema, uchunguzi pia ulifanywa na wataalamu wa kampuni ya SSTL GROUP wakisaidia na Maafisa wa Usalama wa Taifa na Polisi kwa kupitia picha zinazochukuliwa na mitambo ya CCTV ndani ya ukumbi wa Bunge, milango ya kuingilia na kuzunguka eneo lote la Bunge waliona kuwa hakuna kamera zilizozimwa tangu mwaka 2006 na katika kumbukumbu hizo za picha hakuna iliyuoonyesha mtu/watu wakifanya vitendo vilivyokuwa vinavumishwa.

Alisema pia sampuli mbalimbali zilichukuliwa kutoka katika ukumbi wa Bunge pamoja na vumbi lililopatikana kutoka ndani ya mashine ya kusafishia ndani ya ukumbi wa Bunge (hoover) ambao kama kungekuwa na kitu kilichokuwa kimenyunyuziwa ndani ya ukumbi huo tangu tarehe 9/6/2008 na kuendelea ingesaidia kwa kiwango kikubwa.

Tuesday, June 17, 2008

Wazee Waja Juu! - Kuugua kwa Dr. Harrison Mwakyembe


Huko kwetu kusini, kuna imani kubwa sana na mambo ya uchawi, si uongo. Wadau, sasa naona hii story ya Dr. Mwakyembe, itakuwa sinema kiboko hapo baadaye. Alivyowaumbua mafisadi na baada ya hapo kuugua ghafla na wazee wa kijijini kutokea kumsaidia.

***************************************************************

Kutoka ippmedia.com

Kuugua Dk. Mwakyembe: Wazee waja juu...!

2008-06-17

Siku chache tu baada ya Mbunge wa Jimbo la Kyela, Mhe. Dk. Harrison Mwakyembe kuugua ghafla wakati akiwa bungeni na kukimbiziwa kwenye zahanati ya ukumbi huo mjini Dodoma, limeibuka jopo la wazee mbalimbali maarufu mjini Kyela lililokuja juu na kudai kuwa kuumwa kwa mbunge wao huyo si bure na kwamba sasa wanajipanga katika kuhakikisha kuwa hadhuriwi na mambo ya kiuchawi.

Na kwa kuanzia, wazee hao wamesema tayari wameshaunda kamati ya wenzao kumi, ambao wamepiga kambi katika Kijiji cha Nduka kilichopo wilayani Kyela kwa ajili ya kupeana mbinu kali za kiulinzi kabla ya kufunga safari ya kuelekea Dodoma, ili hatimaye wakaonanane na mbunge wao huyo kipenzi na kumueleza kusudio lao la kumpa ulinzi kijadi.

Wakizungumza na PST mjini Kyela, wazee hao waliokataa kuandikwa majina yao gazetini kwa sababu walizodai kuwa ni za \'kiufundi\', wamesema kamati yao hiyo ya wazee kumi mahiri wa mambo ya kijadi, itaanza kwa kufuatilia kiundani ili kujihakikishia kile wanachoamini kuwa kweli, kuugua ghafla kwa mbunge wao huyo ndani ya Ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumetokana na kulogwa.

``Baada ya hapo, kama itabainika kuwa ugonjwa uliompata (Dk. Mwakyembe) umetokana na mikono ya watu wanaokwazika na kazi yake ya kututetea sisi na Watanzania wengine, kitakachofuata ni kumganga na kisha kumtengenezea ulinzi imara ili asidhuriwe tena,`` akasema mmoja wa wazee hao.

Wakasema wamepata wasiwasi mkubwa juu ya kuugua ghafla kwa mbunge wao huyo, hasa baada ya kusikia habari za kuwepo kwa hofu ya vitendo vya kishirikina kufanyika ndani ya Jengo la Bunge.

``Tunajua kuwa siku zote Serikali haiamini mambo haya... na hata mheshimiwa si mfuasi wa mambo haya. Lakini yeye ni mtu wetu muhimu sana. Tukigundua kuwa alichezewa, sisi tutamlinda kwa namna tunayoijua hata kama mwenyewe akikataa,`` mzee mwingine akaongeza.

Alasiri ilipojaribu kuwasiliana na Dk. Mwakyembe ili kupata maoni yake kuhusiana na kikosi cha wazee hao kinachodai kutaka kumpa ulinzi maalum, hakuweza kupatikana kwenye simu yake ya mkononi. Hata hivyo, kuna taarifa kuwa sasa Dk. Mwakyembe yuko buheri wa afya na jana alirejea tena Bungeni kwa ajili ya kuungana na wenzie katika kuijadili bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha wa 2008/09.

Dk. Mwakyembe amejijengea heshima kubwa baada ya Kamati yake iliyotumwa na Bunge kufuatilia mkataba tata baina ya Serikali na Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Richmond kuibua udhaifu mwingi, ambao mwishowe ulimfanya Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wengine watatu kujiuzulu.

Aidha, umahiri wake ulimfanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bwana Jakaya Kikwete amteue kuwa mmoja wa wajumbe waliounda Tume ya Jaji Bomani iliyopitia mikataba ya Madini na kuwasilisha mapendekezo yake (kwa Rais) hivi karibuni.

SOURCE: Alasiri

Monday, June 16, 2008

WaBunge Waogopa Kukalia Viti Vyao! Vina uchawi!


Ilibidi nicheke baada ya kusoma hii habari hasa nikifikiria wabunge kwenye ukumbi wa bunge wakichunguza viti vyao. Hivi kweli unaweza kufuta uchawi/juju hivi hivi?

*******************************************************************

Ndumba Bungeni: Wabunge wahofia viti vyao
2008-06-16
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Ikiwa leo ni siku ya kwanza kwa wabunge kuingia tena ndani ya ukumbi wa Bunge baada ya kuwapo kwa uvumi wa kunyunyizwa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni vya kichawi kwenye viti vyao, baadhi ya wabunge wameonekana leo asubuhi wakiwa bado wanahofia siti zao na hivyo kulazimika kuangalia na wengine kuvipangusa na leso zaidi ya mara moja kabla ya kuketi.
Tukio hilo la wabunge kudaiwa kuwekewa vitu vya kichawi kwenye siti zao, limedaiwa kutokea katikati ya wiki iliyopita na kuzua hofu kubwa, hivyo kuilazimu ofisi ya Bunge, kupitia kwa Kaimu Katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashilillah kutoa taarifa kuwa ukumbi uko shwari na hakuna tishio lolote la usalama kwa waheshimiwa wabunge.
Hata hivyo, licha ya kuhakikishiwa kuwa hakuna hofu yoyote bungeni humo, bado baadhi ya wabunge walionekana wakiwa na hofu na kuchunguza sana viti vyao kabla ya kukaa.
Hata hivyo, hofu ya wabunge hao waliokuwa bado wamejawa na hisia kuwa pengine wamefanyiwa kitu mbaya kwa kuwekewa vitu vya kudhuru, iliondolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Samwel Sitta, ambaye alitoa ufafanuzi wa kina kuhusiana na sakata lenyewe kabla ya kuwataka wasiwe na hofu na badala yake waendelee na majukumu yao bungeni humo kama kawaida kwani ukumbi ni salama.
Akizungumza wakati wa kikao cha asubuhi ya leo, Spika Sitta amesema vyombo vya usalama, ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, vimefanya uchunguzi ukumbini humo na kumhakikishia kuwa hauna hatari yoyote.
Akizungumzia sakata lenyewe, Spika Sitta akasema lilianza kwa kuonekana watu wawili wakitangatanga bungeni humo siku ya Jumanne iliyopita, mishale ya saa 2:00 usiku. Akasema taarifa za kuwapo kwa tukio hilo, alizipata siku ya Alhamisi baada ya kuambiwa na Katibu wa Bunge kuwa kamera za usalama ndani ya ukumbi wa Bunge, zimenasa watu wawili wakitangatanga Bungeni.
Akasema picha hizo zikamuonyesha mtu mmoja kati yao akiwa na vitu mkononi ambavyo alikuwa akivinyunyiza sehemu mbalimbali.
Spika Sitta akasema siku hiyo baada ya kupewa taarifa wakati kikao cha Bunge kikiendelea, akatumiwa kimemo na Mbunge Victor Mwambalaswa, akimjulisha kuwa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe alikuwa ameugua ghafla ndani ya ukumbi huo.
Akasema alipohusianisha matukio hayo, alihisi huwenda vitu vilivyoonekaka vikirushwa na mtu aliyenaswa na kamera za usalama ilikuwa ni sumu ya kisasa. Akasema hapo ndipo akachukua hatua ya kulikabidhi suala hilo kwa Polisi na Usalama wa Taifa ili kulifanyia uchunguzi wa kina.
Akasema Jumamosi ya juzi, Polisi na maofisa wa Usalama wa Taifa walimpatia ripoti ya uchunguzi, wakimhakikishia kuwa ukumbi huo ni salama. Akasema hata hivyo, suala la kuwabaini watu walionaswa na kamera wakitangatanga ndani ya ukumbi wa bunge, bado linaendelea kuchunguzwa na kuwa litachukua muda mrefu kidogo.
Akasema kuwa suala hilo linahitaji muda kwa vile uchunguzi wake unahitaji kurejea kwenye matukio ya nyuma kwa zaidi ya saa 72 ili kujua kilichotokea siku hiyo. Baada ya ufafanuzi huo, Bunge liliendelea na kikao chake kama kawaida, ambapo mjadala kuhusu bajeti ulianza na hadi tukienda mitamboni, wabunge 56 walishajiorodhesha kwa ajili ya kuchangia mjadala huo.

Saturday, April 26, 2008

Update - Mtoto Kichaa akutwa na kichwa cha mtoto


UPDATE - April 29, 2008

Mama mzazi wa mtoto salome yohana aliyechinjwa majuzi akilia kwa uchungu wakati akisaidiwa kuweka udongo kwenye kaburi la binti yake wakati wa mazishi tabata segerea jioni hii.

Picha kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com

**********************************************************


KUTOKA MICHUZI BLOG:

Katika kufuatilia tukio la huyu kijana pichani kukutwa na kichwa cha msichana leo asubuhi kule muhimbili, globu yenu imethibitishiwa kwamba jana usiku msichana mdogo alipotea nyumbani kwao tabata.

Inasemekana leo asubuhi ndugu wa marehemu walikuta kiwiliwili kitupu cha msichana huyo karibu na nyumbani kwao na wakaita polisi ambao wakaupeleka hospitali ya taifa ya muhimbili kwa uchunguzi. huko ndiko kichwa kinachosadikiwa kuwa cha kwake kikakutwa na huyu kijana kwenye geti la chuo kikuu cha tiba cha muhimbili ambapo mlinzi alimkamata.

Afande charles mkumbo, mkuu wa upelelezi kanda ya ilala, amethibitisha yote hayo usiku huu na kwamba kichwa hicho ni cha mtoto salome yohana mwenye umri wa miaka kati ya miaka 3 na 4 na kijana huyu ametambulwa kama ramadhani mussa na anashikiliwa na polisi yeye na mama yake kwa kutuma za kukutwa na kichwa cha mtu kwa kile kilichosemwa kuwa ni mambo ya kishirikina.

Kijana mussa mwenye umri wa miaka 12 inasemekana pia amewahi kukumbwa na mikasa mingine, ikiwa ni pamoja na kuanguka toka paa la kanisa la assemblie of God la msasaani analoongoza mh. getrude rwakatare. inasemekana baada ya mkasa huo ambapo alikuwa na mwenzie wa umri kama yeye walipelekekwa kupimwa akili muhimbili na kuachiwa baada ya kuonekana wana akili timamu.

Mtoto Kichaa Muhimbili - Onyo Picha Zinatisha!





Nimepokea haabri hii ya kusikitisha. Inaelekea ni habari ya kweli. Naomba mlioko Dar mthinitishe kama ni kweli. Je, huyo mtoto kichaa anaitwa nani? Huyo mtoto marehemu ni nani?

Kama ni kweli ni lazima wakubwa walihusika! Wakamatwe wahusika wote na wapewe adhabu ya kifo!
******************************************

On 4/26/08, Dr. M Wrote

Dakika chache zilizopita kumetokea tukio la kusikitisha hapa MPL Muhimbili. Askari mmoja alimsimamisha mtoto wa miaka kama 9 hadi 11 akiwa amebeba kichwa cha mtoto mzuri kama wa miaka mitatu. Kijana yule akatoa kichwa mfukoni na kuanza kula live. Nikifika home nitawatumia picha. Ajabu sana



Kijana mla kichwa cha mtoto alisema kuwa anapeleka zawadi kwa shangazi yake yuko IPPM (siyo psychiatry). Ni kweli tukio hili la kusikitisha sana limetokea.Kichwa ni cha mtoto wa kike mzuri (binadamu), it seemed to be fresh.


Alidai anapeleka zawadi hiyo kwa shangazi yake yuko psychiatry!Mara baada ya kukamatwa, alianza kula kile kichwa live !!! !!! Hata hivyo baadhi ya mashuhuda wanasema aliyekamatwa aliwahi kulazwa psychatry unit.Kwa kuaangalia umbo lake, naye ni mtoto pia; hivyo nina walakini kuwa ni psychiatric patient (unless ana childhood neuropsychiatric/ neurodevelopmental disorders).



Mbona amekuja Muhimbili na si kwingineko. Mfano, angekamatwa maeneo ya Ubungo ama kwingineko; akataja Muhimbili psychiatry tungesikuwa na maswali mengi sana. Kwa upande mwingine, kula kichwa LIVE mbele ya kada mnasi inatia walakini kwa binadamu wa kawaida mwenye akili timamu.



Wazazi/ walezi wa watoto hao (aliyetafunwa na aliyetafuna) wako wapi?Wana maelezo yapi?Pamoja na hayo, kiwiliwili kiko wapi? Kikipatikana chote (kuanzia shingoni hadi miguuni) kitatoa baadhi ya majibu.Polisi wa kutosha (magari mawili) wameondoka na kijana huyo uchunguzi (forensic investigation) unaendelea.



AMINI USIAMINI, NI KWELI YAMETOKEA.

Thursday, April 03, 2008

Ufisadi na Uchawi

Imeandikwa na mdau SUBI.

The Land of Kilimanjaro, Olduvai, Serengeti, Tanganyika, Zanzibar, Ufisadi and Uchawi!.... of course there are exceptions! Na ndiyo ukweli wenyewe kwa baadhi ya WaTz.Wametusema sawasawa.Nchi ya wachawi? Na ndiyo maana bado tunabishana kuhusu nani ameficha kiatu cha kukimbilia, wakati wenzetu wameshajipanga kwenye mstari.

Na tukishakipata kiatu cha pili tunacholitafuta, kiatu cha kwanza watakuwa wajinga fulani fulani wanaojiona werevu sana wamekificha ama wamekitoboa. Yaani ali munradi tuna visingizio gunia tele.Kazi tumekalia kusema na kuamini uchawi, uvivu, kusemana, kutafutana visa, kuomba omba na kuamini miujiza tuuuuuu badala ya kufanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa.

Yaani mtu anaamini kabisa kuwa atapataga mautajiri ya fasta fasta kwa ulozi. Hata anayejitahidi kufanya kazi anaogopa kutishwa kulogwa. Yaani ni aibu mfanowe hakuna.Dawa? Elimu inayoendana na wakati na mazingira. We mtu anafundishwa nadharia tu shuleni, vipindi vya vitendo, maabara hamna vifaa ya kutosha ama hakuna kabisa vifaa, anaishia kukariri tu, sasa huyu mtu akihitimu atatarajiwa vipi afanye kazi kwa ufanisi?

Ndiyo usanii tena unakuja bila kutaka. Maneno meeengi, kuagiza kwiiingi, lakini mwambie akuonyeshe kwa mfano kwa vitendo..... utasikia, 'fanya tuu', 'yaani hujui', 'hiyo rahisi', Ningejua ningeuliza? Shule ndiyo zimeshakuwa sehemu za kukulia tu sasa na kujifunza ujamaa! Maanake walimu wanasema utajifunza utapoanza kazi!Wengine wenu mtanichukia tu lakini ndiyo hivyo tena, nimeshayasema mawazo yangu, kwani nimekulazimisha ukubali? Hatufanani!

Subi (usibofye jina langu)'

Witchdoctor killings condemned

NAIROBI (Reuters) - Tanzania's President Jakaya Kikwete has condemned witchdoctors who kill albinos and harvest their body parts in the hope it will bring prosperity.

He said 19 albinos had been murdered since March 2007, and another two were missing presumed dead in the east African country.

"Sometimes, word spreads around that body parts of people with certain physical attributes like bald people or albinos contribute greatly to attaining quick prosperity," Kikwete said in a monthly state of the nation speech late on Wednesday.

"These killings are shameful and distressing to our society," he added.
Albinos are often accused in Tanzania of being witches themselves.

There are an estimated 270,000 people who suffer from the condition which stops them producing pigment in their skin, hair and eyes in the country of 39 million.

Kikwete blamed charlatan witchdoctors, many masquerading as traditional healers, for extracting body parts such as genitals, tongues and breasts.

"Many of the witchcraft killings happen because of a false belief that by using other peoples' body parts they can succeed in business or in activities like mining or fishing," Kikwete said.
Most killings took place in the Victoria region and were committed by gangs for hire, he said.
(Reporting by George Obulutsa; Editing by Giles Elgood)