Friday, March 12, 2010

Kazi New York kama unajua KiMatumbi!

Kutoka Craigslist.

I am making a film that incorporates the story of Kinjikitile "Bokero" Ngwale and the Maji Maji Rebellion in German East Africa during the turn of the century.

I am in need of a male to play the part of Bokero himself (voice only). The text that will need to be be read will be about 2 minutes in length, and will need to be translated from English. No prior acting or voice acting experience is necessary.

Ideally, I am looking for someone who can speak Matumbi, but someone who can speak Swahili or any other East African Bantu language with a Tanzanian or East African accent would work as well.

I am offering $30 compensation and will also provide credit in the film, a copy of the finished film, and a copy of your voice recording.

Recording can be done in person (either Union Square, Manhattan or Clinton Hill, Brooklyn) or over the internet - whichever is preferable for you.

If you are interested, please contact me with a voice sample and I will provide more details about the project.

Unaweza kumjibu kupita Craigslist!

Matumbi, Swahili, or Bantu speaking East African wanted for voice overgigs-zjap7-1640211759@craigslist.org

Thursday, March 11, 2010

Ngono, Afya na Uzee


Haya, mkitaka kufanya ngono kwa muda mrefu maishani mwako, uwe na afya bora! Pia wanaume wanafikiria ngono zaidi ya wanawake! Nini kipya? Soma wataalamu walivyosema kuhusu ngono leo.

***********
(CNN) -- Healthier men, no matter their age, are going to have better sex more frequently and desire it more often than healthier women.
And a healthier sex life could mean a longer life.
That's according to a paper written by University of Chicago researchers that was published Tuesday in the British Medical Journal. While the supposition that men think about sex more than women isn't new, the paper's findings have wider implication for attitudes toward public health and how patients respond to doctors' advice, said Dr. Stacy Tessler Lindau, an associate professor of obstetrics and gynecology and geriatric medicine who spearheaded the research.
"If you are a man diagnosed with diabetes or high blood pressure and I tell you that you need to lose weight and take medication, and I can say the benefit is five extra years of sex life, you might be more inclined to do what I tell you," she explained.
Lindau said that women generally reported wanting less sex or receiving it less often for three reasons: Women outlive men by an average of five to six years and without a partner, women are less likely to engage in sex. Secondly, there's a Western cultural acceptance -- and removal of stigma -- of men who have erectile dysfunction and have turned to relatively recently marketed drugs such as Viagra; women don't have that.
"Also, there's a difference in how we treat women for other diseases that affect their sexual desire," Lindau said. "If a woman is diagnosed with breast cancer and she has, for example, her breasts removed, and we never counsel her about her sexual function, we start to realize how many years of life she's losing. Not doing those things could mean 10 years of lost sexual activity."
There are no FDA approved treatments for female sexual dysfunction other than estrogen to treat pain with intercourse, she said.
Lindau's paper was sponsored by the nonprofit National Institutes of Health.
The paper considers data from two previously published studies that included more than 6,000 men and women, split into two co-ed groups: The first was age 25 to 74. The second group was age 57 to 85. Ninety-eight percent of participants reported having sexual partners only of the opposite sex, she said. Roughly 80 percent of men and 65 percent of women in the study were married or living with a partner.
None of the study's participants was in a nursing home.
Questions were presented that asked them to give their relationship status and rate their health and the quality of their sex life from poor to excellent.
Excellent was defined not by the number of times someone had sex but the emotional and physical satisfaction of the experience. But, the survey described having sex "regularly" as two to three times a month, said Lindau.
Sex was defined to the 57- to 85-year-old group as "any mutually voluntary activity with another person that involves sexual contact, whether or not intercourse or orgasm occurs" in the past year. For the same time frame, those in the 25-74 age group were asked if they had "had sex with anyone."
Participants had the option of assigning a number rating to their sex life, including "0" for "the worst possible situation." That phrase was up to them to interpret, said Lindau.
Women who initiate relationships later in life -- they describe passionate love and sex like the way younger people do.--Stacy Tessler Lindau, study author
The physician concluded that men are more likely to be sexually active, have what they believe is better sex and are consistently more interested in sex than women. This drive for sex among men and the feeling that the sex they get is high quality doesn't diminish with age. Lindau said it was difficult to ascertain exactly how many of these participants might have taken erectile dysfunction drugs.
If men stay in good shape, they can enjoy more years of good sex, the study says. At age 55, men in very good or excellent health on average gained five to seven years of sexually active life compared with their peers in poorer health. Women in very good shape gained 3 to 6 more years of a quality sex life than women who are less healthy.
For women 60 years and older, sex dropped off significantly overall and was even lower among those without partners. For men in that age range, having a partner didn't matter -- they still wanted sex consistently, the study found.
Among 75- to 85-year-old men, four out of 10 were still having sex, compared with two out of 10 women that age. Women whose partners were still alive, however, were having just as much sex as men, said Lindau.
"I don't want to perpetuate the notion that older women don't desire sex," she said. "There's a glass half full here. There's a big hunk of older women still having sex. Women who initiate relationships later in life -- they describe passionate love and sex like the way younger people do."
Lindau said she was frustrated that her sampling was limited to heterosexuals, a typical quandary many experience when testing this topic, she said. She hopes to conduct another study focusing on aging homosexuals, bisexuals or people whose biological sex cannot be classified as either male or female.

Tuesday, March 09, 2010

Mke wa Balozi Daraja Auwawa!

Balozi Andrew Daraja

Hizi ni habari za kusikitisha hasa. Naomba Mungu hao waliomwua wakamatwe! Mungu ailaze roho ya Mama Daraja mahala pema mbinguni. AMEN.

***********************************************************************
Diplomat’s wife killed, houseboy on the run

By ROSE ATHUMAN, 8th March 2010

FORMER Tanzania’s Ambassador to the United States, Andrew Daraja arrived home last Sunday to find his wife, Hanna Daraja (65), stabbed to death by unknown assailants and locked into their garage in Kimara B area in Dar es Salaam.

Ambassador Daraja, who was away in Muheza, Tanga for three weeks, arrived home yesterday to find his wife dead and the houseboy gone.

The former ambassador, who has served in public office in various capacities, told the 'Daily News' today that he last contacted his wife on Saturday afternoon to inform her that he would be travelling back the next day (yesterday).

“When I tried to call again later in the evening, the call could not go through. I tried again later several times and still it didn’t go through,” he explained his eyes welling up with tears.

When he arrived at his home, his driver hooted but there was no response from inside.

“I tried calling again, and got no answer. I was then beside myself with worry, I knew something was definitely wrong. I asked my driver to climb over the fence and open the gate,” he said.

They saw her shoes and bags strewn on the ground close to the gate, propelling ambassador Daraja to rush into the house to check on his wife.

“I looked everywhere in the whole house but I couldn’t find her. My driver and I looked around the compound but did not find her either,” he explained.

Just when he was about to give up, he remembered to look inside his garage and…there she was, laying on the floor with a knife sticking out on her chest.

“We unlocked the garage which was padlocked from outside but she was already dead. We reported the matter to the police and they are investigating,” he whispered, tears streaming down his face.

Ambassador Daraja said the house-help, a young man aged between 19 and 20 years, was not in the house and has never been seen since. He refused to disclose the house-help’s name before the police complete their investigations.

Nothing of value was stolen, but the former ambassador suspects the assailants were looking for cash.

“I think the assailants were looking for cash, because they didn’t take anything of value and the bedroom was in a mess with things strewn all over,” he said.

The deceased was a teacher by profession but left teaching to join her husband when he was first posted to Germany and later to the United States as Ambassador. He explained that burial preparations will take place after the police have completed conducting a postmortem.

Ambassador Daraja began his duties as ambassador to US in July 2002. Prior to that assignment, he served as the ambassador to the Federal Republic of Germany between 1995 to June 2002.

He has also held different position in Public offices including in the State House. The deceased is survived by her husband, four children, three daughters and a son who lives in the United States. Efforts to get comments from the police force were futile as telephone calls went answered.

Source: http://www.dailynews.co.tz/home/?n=8046&cat=home

Tuogope magari ya TOYOTA!!!!

(pichani - gari aina ya Toyota Prius ambayo ilipata ubongo na kuanza kwenda mwendo wa kasi mno, hata breki haikufanya kazi!)

Leo mzee James Sikes (61) karibu auliwe wakati gari yake aina ya Toyota Prius, ilivyoanakwenda mwendo wa kasi ghafla. Bila shaka mmesikia kwenye taarifa ya habari, habari ya magari ya Toyota kuua watu baada ya kuanza kwenda mwendo wa kasi ghafla. Spidi zinakaribia kilomita 100 kwa saa! Watani wanasema eti jini ailingia kwenye injini! Gari inakosa breki...inakuwa balaa. Unaweza kusoma habari zaidi hapa!

http://news.yahoo.com/s/ap/20100309/ap_on_bi_ge/us_runaway_prius

Ruksa kwa Wapenda Jinsia Moja Kufunga Ndoa D.C.!



(Pichani baadhi ya wapenda jinsia moja waliofunga ndoa leo huko Washington D.C.)

Sasa huko mji mkuu wa Marekani, Washington D.C. ni ruksa kwa wapenda jinsia moja (Gay/lesbian) kufunga ndoa. Washington D.C. sasa inakuwa jimbo la sita kuruhusu ndoa za aina hiyo.
Mmmh! Kuna madai kuwa eti ushoga utaongezeka katika nchi za Third World, kwa vile wataona kuwa watapata misaada zaidi wakiwa watu wa aina hiyo.
Kwa habari zaidi someni:

Mzungu Am 'Kanye West' Mweusi kwenye Oscars

Umesikia kituko kilichotokea kwenye Oscars juzi? Huyo Roger Ross Williams alikuwa anapokea tuzo kwa ajili ya sinema ya 'Music by Prudence'. Ghafla katokea bibi wa kizungu, Elinor Burkett, na kuanza kusema, "mwache mwanamke aongee" na maneno mengine ambao watu hawakuelewa.

Sisi watazamaji tulishangaa sana inatokea nini. Kumbe huyo mzungu aliwahi kuwa producer wa hiyo sinema lakini waligombana na Williams. Burkett alimpeleka mahakamni lakini walisuluhisha nje ya mahakama. Burkett aklisem hakupenda jinsi sinema ilivyokuwa inaenda. Ajabu, jinsi ilivyoenda ndo ikashinda Oscar!

Lakini wadau , hii kituko kisingetokea tusingekumbuka habari ya hiyo sinema, Music by Prudence. Pia hao Williams nad Burkett wasingejulikana. Sasa hivi Letterman, Leno na wengine wanamtania huyo Burkett. Bila shaka na Saturday Night Live watamtania!

Pia wanamwita Burkett, Lady Kanye! Kumuka mwaka jana Kanye West alivyoingia hotuba ya Taylor Swift kwenye tuzo za MTV.

Unayanyasaji wa WaBongo Saudi Arabia - II

wanablog na watz wote.
habari za kazi na poleni kwa juhudi zenu za kuwahabarisha watanzania kwa njia ya mtandao. nawatumia link hizi kuonesha hali halisi ya raia wa kigeni wanaokuja kutafuta maisha saudia jinsi wanavyofanyiwa. hatua hii imetokana na mimi mwenyewe kuwa nipo katika matatizo haya lkn mbaya zaidi kuona kuwa walionileta kutoka huko tz wanaendelea kukusanya vijana wengine kama mimi na kuwadanganya kwa kuwaahidi maisha bora wakifika huku saudia.
link hizi ni za vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikiripoti manyanyaso haya sio tu ndani ya saudia bali pia nje ya saudia lakini kwa makusudi serikali ya hapa inafumba macho na kujifanya kuwa inatenda haki. wapo waliouwawa, waliopata ulemavu wa kudumu, nk na daima makosa huwa ni ya wageni. wasaudi hawana kosa hata kama wataua au kumpa mtu ulemavu. nchi nyingine za asia zimeanza kuzuia raia wao kuja kufanya kazi hapa kutokana na hali hiyo.
vyombo vya sheria ndio kabisa kuanzia polisi hata mahakama. kwanza ukifika kulalamika utaambiwa hatujui kiingereza zungumza kiarabu kama hujui ukatafute mwanasheria. sasa mshahara wenyewe riyal 500 hadi 800 (riyal 1 ni tsh 300) utamlipa mwanasheria gani? pili huyo jamaa unayemlalamikia ni bilionea hivyo hata polisi hafiki utasikia unajibiwa huu ni uzushi msaudi hawezi kufanya hivi nenda zako. hapo kesi imeisha.
naomba musambaze taarifa hizi kadri muwezavyo hata kutumia magazeti, redio na tv ili vijana wenzangu watz kama mimi wanaotafuta kazi za udereva, uhouse girl, kuuza maduka, kwenye viwanda na makampuni nk wasidanganywe na kuja kupata mateso kama yaliyonikuta mimi hivi sasa.
tafadhali pokea link hizi.....

Monday, March 08, 2010

Shida Wanaopata WaBongo huko Saudi Arabia

bwana michuzi na wanablog wengine.


kwanza nawashukuru sana kwa kutoa barua yangu niliyowatumia nikiewaeleza hali halisi ya maisha huku saudia kwa sisi madereva na shida ambazo watanzania madereva na raia wa nchi nyengine tunapata. nawashukuru watz kwa kuuona ukweli ijapokuwa wapo wachache ambao kwa sababu zao walikuwa na mashaka.

napenda kueleza zaidi kuwa magenge mawili yanayosafirisha watu huko bongo wa kuwaleta huku moja linaongozwa na jamaa anaitwa bungire (jina lake kamili silijui). huyu jamaa ana wenzake wawili anaoshirikiana nao katika biashara hii. ni mtu mwenye tamaa sana ya pesa. genge hili ndilo lililonileta mimi na wenzangu huku saudia. huyu jamaa anaishi ilala na mambo mengi ya kuandikisha watu hufanya mitaani. sina hakika kama ana leseni au afisi lakini anaonekana ni mtu mwenye ushawishi mkubwa katika afisi za serikali.

wakati anatukusanya huko dar alituambia tusiwe na wasiwasi na pasi za kusafiria au viza. na kweli siku 2 tu tulipata pasi kwa kuwa wengi wetu ni mara ya kwanza kusafiri nje ya bongo. baadae akatuombea viza na tukapata ubalozi wa saudia hapo dsm. ni mtu anayeonekana maarufu au anauhusiano na wakubwa hapo dar.

genge la pili lipo mtaa wa uhuru. hawa jamaa wanaitwa madina (sijui kama ndio jina la kampuni au la mtu). hawa jmaa wamealeta wenzetu pia hapa saudia kwa kutumia njia hizohizo za ulaghai na utapeli. takriban saudia tupo madereva wengi watz tunafika zaidi ya 50 katika makampuni mbalimbali. lkn wote tumeletwa na makundi ya matapeli hao wawili. tunaendesha malori ya saruji, malori ya mafuta na magari ya mizigo mchanganyiko.

baadhi ya watu wanadhani ni chuki dhidi ya waislamu. napenda kuwaanbia kuwa madereva sote tuopo hapa saudia kutoka tz ni waislamu tena swala 5. ijapokuwa tumekusanywa dar lkn wapo wenyeji wa tanga na wengine zanzibar, lkn wengi wetu ni watu wa dar. hatuna nia ya kuwasingizia bali ndio hali halisi ya hapa na ubalozi unajua hilo. hawa jmaa hawafuati uislamu wala nini bali ni makatili na washenzi sana. hayo wanayofanya yote ni kinyume na uislamu lkn hujidai kuvaa kanzu na vilemba kama wachamungu. ni wanafiki tu.

mimi na wenzangu tulishaamua kumshtakia mungu udhalilishaji huu. hao matapeli wa dar na wenzao wasaudi wanaotunyanyasa mungu atatulipia hapa hapa duniani au kesho kiama. kama si kwa wao basi vizazi vyao vitaonja mateso kama haya tunayoyapata sisi muda huu.

lkn nimeguswa na lile tangazo na kuona kuwa kumbe hawa matapeli bado wanakusanya watz wengine na kuwaleta huku. hivyo, nawaomba watz wenzangu wasikubali kuja huku hata siku moja. bora hali ya nyumbani tz mara 100 kuliko mazingira ya huku kwa mgeni.waarabu kwao mgeni ni kama machine tu haichoki, haiumwi, haina njaa wala haipaswi kulalamika.

kwa ujumla mateso na unyanyasaji sio kwa watz tu bali pia kwa raia wengine. michuzi nakuwekea hapa hii link uone mfanyakazi wa nyumbani mkenya alivyofanyiwa hapa saudia na hii imetolewa katika gazeti la kenya. wale wanaoona kuwa saudia hawawezi kufanya mambo kama haya waone wenywe.

link yenyewe ni hii,.....

http://www.nation.co.ke/News/-/1056/840238/-/vp9oc4/-/index.html

ni mimi mtz dereva saudia...

Uvumi Kuhusu Maalim Seif


Muda si mrefu kulipita uvumi kuwa Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad amefariki, lakini ukweli ni kuwa Kiongozi huyo hajafariki lakini amelazwa kwa matibabu katika Hospitali ya Hindi Mandal Dar es Salaama. Na inadaiwa aliugua ghafla akiwa Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.

TEMBELEA MROKI MROKI BLOG KWA HABARI ZAIDI.

BLOG: www.mrokim.blogspot.com

Saturday, March 06, 2010

Ushenzi wa Republicans!


Duh, sasa hao Republicans wametia fola! Wanatumia mbinu za kutishia watu kuwa Rais Obama anataka kugeuza Marekani kuwa nchi ya kijamaa! Wamemtukana pia kiongozi wa Bunge la Marekani Nancy Pelosi na Harry Reid , kiongozi wa Senate wamemfanisha na yule mbwa mkubwa lakini mwoga Scooby Doo!
Makaratasi yalikutwa katika chumba cha hoteli huko Florida. Mnaweza kusoma habari zaidi HAPA:
Baada ya kuisoma utaona jinsi Republicans wanavyodharau watu na kuwaona wana akili finyu!

Mkurugenzi wa TAMWA apata Tuzo Muhimu!

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya akipiga posi na tuzo nje ya ofisi za TAMWA huko Sinza mara baada ya kuwasili kitoka ubalozi wa Marekani

HOTUBA YA MKURUGENZI MTENDAJI WA CHAMA CHA WANAHABARI WANAWAKE NCHINI (TAMWA), ANANILEA NKYA KATIKA MKUTANO WA WANAHABARI, UBALOZI WA MAREKANI KWA AJILI YA KUKABIDHIWA TUZO YA MWANAMKE JASIRI WA TANZANIA KWA MWAKA 2010


Mheshimiwa Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt,
Wafanyakazi wa Ubalozi wa Marekani,
Wanahabari na wanaharakati wenzangu,
Wageni waalikwa,
Mabibi na Mabwana.


Ninashukuru kwa kupata heshima hii kubwa ya kusimama mbele yenu kama mteule wa tuzo ya Mwanamke Jasiri wa Tanzania kwa mwaka 2010.

Kwa heshima na taadhima nianze kwa kushukuru Ubalozi wa Marekani hapa nchini na wananchi wa Marekani kwa ujumla kwa kunichagua mimi kama MWANAMKE JASIRI WA TANZANIA KWA MWAKA 2010 kutokana na juhudi na ubunifu wa kutumia vyombo vya habari katika kuimarisha usawa, fursa na haki za wanawake na watoto wa kike wa Tanzania.

Sina shaka kwamba Ubalozi wa Marekani ulifanya utafiti kikamilifu na tena kwa mapana na kupata majina mengi tu, maana kuwa jasiri maana yake ni kuzungumza kwa sauti kile unachokiamini kuhusu uonevu na uvunjifu wa haki hasa za wanyonge ili hatua ziweze kuchukuliwa kurekebisha hali hiyo. Katika mapambano ya kutetea haki za watu wa hali ya chini hasa wanawake, wasichana na watoto hapa nchini, wako watu wengi wanaofanya harakati hizi kwa juhudi kubwa mijini na vijijini. Hivyo mimi kuchaguliwa miongoni mwao, ni ishara kwamba Marekani imetambua mapambano yetu, ambapo mimi ni mwakilishi wa wapambanaji wengi.

Kwa hiyo, nachukua fursa hii kushukuru na kuipongeza serikali ya Marekani kwa kubuni TUZO YA MWANAMKE JASIRI. Kwa kubuni tuzo hii serikali ya Marekani imedhihirisha kuwa inaunga mkono mapambano mbali mbali ya wanawake katika kupigania haki zao.

Wanawake wanapambana kuweza kushiriki katika masuala ya maendeleo; wanapambana ili waweze kunufaika na rasilimali mbali mbali za taifa, wanapambana kupata haki yao kwenye huduma ya afya, elimu, mirathi, uchumi na uongozi wa nchi yao.

Natambua kuwa tuzo hii ilishatolewa kwa wanawake wawili hapa nchini; Helen-Kijo Bisimba (2008) kwa ujasiri wake mkubwa wa kutetea haki za binadamu akiwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela (Mbunge wa Same Mashariki) kutokana na ujasiri wake katika kupambana na ufisadi.

Nina hakika, baada ya muda, tuzo hii itazaa matunda ya neema hasa kwa wanawake wengi wanaotaabika kwa madhila mbali mbali mijini na vijijini. Wanawake ambao wanapambana ili wapate haki ya kuthaminiwa utu wao. Wanawake wengi hapa nchini hawana amani wala furaha kwa sababu mifumo gandamizi imewapora haki na fursa ya kutoa maamuzi kuhusu mambo yanayohusu maisha yao na familia zao na wameporwa pia fursa ya kushiriki katika vyombo vya kutoa maamuzi kuhusu namna wanavyotaka nchi yao iendeshewe.

Ninaamini kuwa kama taifa letu lingejenga mazingira sahihi ya kuwawezesha wanawake kuwa sehemu ya rasilimali uongozi katika ngazi mbali mbali, hakika wangedhihirishia taifa kuwa wana uwezo mkubwa wa kuongoza, na bila shaka nchi yetu ingenufaika kiuchumi, kisiasa na kijamii kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa. Kwa hali hiyo tungepiga hatua kubwa katika nyanja ya demokrasia na maendeleo na kuweza kufikia ndoto ya ukombozi siyo Tanzania pekee bali pia ukombozi wa Bara la Afrika.

Wanawake na wasichana na hata wanaume na vijana wengi hapa nchini nao wameonyesha uwezo mkubwa wa kuhimili changamoto zinazotokana na sera mbaya za uchumi. Wengi wao wamekuwa wakitegemea kilimo cha jembe la mkono na biashara ndogo ndogo kuweza kujikimu huku wakiwa na jukumu kubwa la kulea yatima ambao wanaongezeka kila siku na kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI ambao hulazimika kurudishwa majumbani kutokana na mfumo duni wa afya.

Wanaume, Wanawake na vijana hawa wa kike na wa kiume wa taifa hili siyo tu wamedhihirisha kuwa ni ni watu jasiri, bali pia ni watu wenye uwezo wa kuibadilisha Tanzania kuwa ni mahali pazuri pa kuishi watu wa wakundi yote wanaume, wanawake, wazee na vijana, wenye ulemavu na wasio na ulemavu. Ndiyo sababu Tanzania inahitaji kuwa na mipango ya maendeleo yenye malengo mahususi na mikakati madhubuti ya utekelezaji wa mipango hiyo. Mipango hiyo ni muhimu itengenezwe kwa kuzingatia sauti, mitizamo, uwezo na mahitaji ya watu wa ngazi za chini na wanaharakati na wanahabari wana wajibu wa kushinikiza bila woga hatua zichukuliwe kutekeleza mipango hiyo kwa ufanisi.

Ukatili wa kijinsia una athari mbaya kwa wanawake na wasichama kwa kuwa unawaathiri kisaikolojia na hivyo kushindwa kutekeleza wajibu wa kuboresha maisha yao na maisha ya wale wanaowategemea. Sheria zilizopitwa na wakati ambazo zinakoleza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa kike zinahitaji taifa kupata viongozi imara na hasa Wabunge wenye ujasiri wa kuisimamia serikali ili iwajibike kubadilishe sheria hizo. Sheria hizo mbaya ni pamoja na ile ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo inaruhusu mtoto wa chini ya miaka 18 kuolewa na hivyo kumkosesha haki yake ya kupata elimu na kuhatarisha maisha yake endapo atapata ujauzito.

Mheshimiwa Balozi,

Mimi ujasiri nilionao kwa kiwango kikubwa umechangiwa na taaluma yangu ya uandishi wa habari na uanaharakati wa masuala ya jinsia, demokrasia, maendeleo na haki za binadamu.

Kunichagua mimi kama mwanamke jasiri mwaka huu 2010, ni motisha kwa wanahabari na wahaharakati; wanawake na wanaume ambao wamekuwa wakijishughulisha kwa namna mbali mbali kuleta mabadiliko katika mila mbaya, mifumo, imani na sera gandamizi ambazo zinabagua na kuwatupa pembezoni wanawake na wasichana.

Kwa hiyo, naipokea tuzo hii kwa niaba ya wanawake wote wa Tanzania na wanaume na wanawake wa umri mbali mbali ambao nimekuwa ninashirikiana nao katika vyombo vya habari, kwenye harakati na Chama cha Wanahabari Wanawake nchini (TAMWA) ambacho tangu kilipoanzishwa miaka 21 iliyopita kimekuwa kikipaza sauti kutetea haki na fursa za wanawake, wasichana na watoto. Tuzo hii niliyoipata leo, sote tuichukulie kama changamoto, mwanzo mpya na kitu cha pekee cha kututia moyo katika kuendeleza jitihada za kutetea usawa, fursa na haki kwa wanawake, wanawake wasichana na watoto wa Tanzania.

Mheshimiwa Balozi,

Kuna msemo wa Kiswahili usemao â€Å“Sema Usiogope Sema”. Naichukulia hii tuzo ya ujasiri niliyopewa leo kama ishara kwamba Marekani inatambua kwamba mapambano katika ngazi ya familia, kitaifa, kikanda na kimataifa kwa ajili ya kuimarisha usawa wa jinsia, haki za binadamu na uhusiano mzuri baina ya mataifa ni muhimili muhimu katika kujenga amani duniani.

Sisi wanaharakati wa Tanzania tunashikamana na wanaharakati wengine duniani kote katika mapambano ya kubadilisha dunia ili iwe mahali pazuri pa kuishi watu wote wanaume na wanawake, maskini na matajiri wa rika zote.

Mhusiano usio sawa katika ngazi ya kimataifa unaguza na kuleta amthari mbaya katika mahusiano ya kikanda, kitaifa na hata ngazi ya familia. Mahusiano kama hayo huchangia moja kwa moja kuwepo na mahusiano yasiyo na uwiano sawa baina ya wanaume na wanawake. Mahusiano yasiyo na usawa huchangia kwa kiasi kikubwa vitendo vya kikatili na ukiukwaji wa haki za binadamu siyo tu dhidi ya wanawake na wasichana, bali pia dhidi ya makundi mengine yaliyoko pembezoni. Hali hii iko dhahiri katika Bara letu la Afrika ambalo limekuwa likishuhudia uporaji wa ardhi ya wanyonye, wimbi la rushwa na ufisadi unaohusisha baadhi ya viongozi na wafanya biasharawakubwa.

Ni imani yangu kuwa tuzo hii ya MWANAMKE JASIRI itaendelea kuimarika na kuwa kichocheo kwa wanaharakati wote ili wasichoke na mapambano, hata yatachukue muda mrefu kiasi gani maana dunia iliyo bora na salama kwa wanawake na watoto ndiyo itatengeneza dunia bora, salama na yenye neema na furaha tele kwa watu wote.

Nawashukuru wote kwa kunisikiliza,

Nakushukuru Mheshimiwa balozi na wananchi wa Marekani kwa wazo hili zuri la kutoa tuzo ya mwanamke jasiri.

Ananilea Nkya

Executive Director (TAMWA)

02/03/2010
*****************************************************
Nami nasema HONGERA Dada Nkya! Kweli umetoka mbali na unfanya kazi nzuri mno TAMWA! - Chemi

Wednesday, March 03, 2010

Jibu - Ilivyokuwa Safari Yangu Mbeya

Na John Mwaipopo

Nimebahatika kutumiwa e-mail ambayo mwandishi wake ameiita ripoti ya safari yake ya kikazi mkoani Mbeya. Ameituma kwa watu wengi ili kueneza uchafu aliouona mkoani humu. Sina uhakika nani alimpa kazi ya kuandika ripoti yake hii maana nijuavyo riporti ina kitu kinaitwa terms of reference yaani waliokutuma na jinsi walivyokutuma kufanya uchunguzi/utafiti. Lakini haidhuru pia inaweza kuwa ripoti binafsi ya muhusika anayejiita mwanahabari, ingawaje ripoti yenyewe inaonyesha alichokiandika sicho alichotumwa kufanya huko mbeya. Waweza isoma hapa
Awali napenda kumpongeza mwanahabari kwa kuonyesha yale ambayo kwa mtazamo wake hayaonwi ama hayajaonwa na watu wasiowahi kufika Mbeya ila nitachukua fursa kidogo kurekebisha yale ambayo yamewasilishwa ndivyo sivyo. Napenda ijulikane mie ni mkaazi wa mbeya kwa karibu miaka 20 mfululizo isipokuwa nikiwa shule ama vyuoni, ambako nako nilitambulika kuwa natoka Mbeya. Hivyo itambulike nina maslahi na uenyeji/ukaazi wangu hapa Mbeya.

Juhudi hii ni kwa ajili ya kuweka sawa kumbukumbu na taarifa kamili. Pili nadhani itamuongezea ufahamu bwana mwanahabari. Tatu juhudi hii itafanya upotoshajia wa makusudi wa mwanahabari pengine kutokana na wembamba wa uwezo wake wa kufikiri, kupembua na kuchanganua mambo, ujulikane.

Nianze na kunukuu mwanzo wa report yake hii. Nanukuu “Duniani kuna mambo mengi sana.” Nukuu hii inaonyesha jinsi gani huyu mwanahabari (lakini mwanahabari aliyetumwa kwenda kutengeneza mashine mbeya. Habari na umakenika wapi na wapi) alivyo maamuma wa kujua mambo hata yaliyo ndani ya nchi yake. Kwake Mbeya tu ni dunia nyingine kabisa! Kwake ilikuwa safari ya kustaabisha eti. Kwa mtu aliyefanikiwa kusafiri kuliko mwanahabari-makenika Mbeya haitofautiani sana kwa raha na mauzauza utakayoyakuta mikoa mingine, pengine mikoa mingine imeizidi hiyo Mbeya. Nitaonyesha kwa kifupi hapa chini.

Kimojawapo ni uwingi wa makanisa na sehemu za kuabudia hapa Mbeya. Eti kutoka kanisa moja mpaka lingine ni hatua 30! Nimekaa Mbeya karibu miaka 20 sijayaona hayo makanisa na viwanja vya kuabudia vilivyopakana hatua 30 kama mwanahabari-makenika anavyotaka kuwadanganya watu ambao hawajafika Mbeya.

Jambo la msingi lililonisukuma sana kujaribu kujibu ripoti hii ni maambukizi ya ukimwi mkoani Mbeya. Ni kweli Mbeya i miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya gonjwa hili hatari lakini haiifuatii Johanesburg kwa maambukizi. Hata hapa Tanzania tu haishiki namba moja. Soma hapa uhakikishe. Labdha atuambie takwimu hizi kazipata wapi.

Ingawaje ripoti hii ina nia ya kutukumbusha kujiepudha na kujilinda na ukimwi lakini imejaa kejeli kama vile Mbeya na Ukimwi ni sawa na samaki na maji. Kwa mfano anasema “wenyeji wa hapa wengi hawaamini kama kuna ukimwi. Wanaamini mtu akifariki basi amefariki kutokana na mungu (sic) kumwita amechoka maisha ya dunia , wengine ndio hizo imani zao akifa mwenzao amelogwa na mambo kama hayo .” Hivi tujiulize ni kweli asilimia kubwa ya watu wa Mbeya hawajui lolote kuhusu ukimwi isipokuwa wachache na pengine wageni wanaokuja kutengeneza mashine? Kumbuka hapa alipofikia kabla hajaenda Tukuyu (alikokuita ‘mkoa’ paragrafu ya 32) na Kyela ni mjini ambako ufahamu wa uwepo wa ukimwi ni mkubwa. Au amesahau Mbeya kuna watu wanaotoka mikoa yote ya Tanzania na si kweli kuwa wote wana imani za kizamaani za washamba wa Mbeya? Kuna wachagga, wahaya, wamasai, wasukuma, wakwere n.k. Na kabila lake ‘walistaarabika’ nao wapo wanaishi hapa, na wengine hawana mpango wa kurudi huko kwa ‘wastaarabu’.

Mwanahabari-makenika anaanika kuwa hapa Mbeya “ukikutana na wasichana 5 basi 3 wanamarafiki wa kiume ambao sio wanafunzi wenzao yaani watu wa nje tu , wamachinga na madereva au watu wa shuguli zingine , hii inaadhiri sana hawa vijana utendaji wao madarasani” (para 24). Nadhani anaongelea wanafunzi lakini hajatuambia takwimu hizi amezitoa wapi ama lini yeye binafsi alifanya utafiti huu. Na pia sidhani mmomonyoko huu wa maadaili miongoni mwa wanafunzi uko Mbeya tu. Pengine kwao hamna huu upuuzi, upuuzi ambao katu siupigii upatu kokote kuwako.

Nina mashaka na tabia binafsi za mwanahabari-makenika hususani katika masuala ya ngono. Nadhani ni muumini mkuu wa kuendekeza ngono. Pengine kafikia ushemasi kabisa. Inakuwaje mtu ambaye si muendekeza ngono ukachombezana kwa simu kimahaba na wanawake asiowajua hata wakapanga siku ya kwenda Mbeya ili wakapene hilo joto (para 11) alafu anaingia mitini dakika ya mwisho. Au sitaki nataka? Pia inakuwaje mtu asiye mzinzi akaongea na msichana asiyemjua kwa masaa mawili na wakatongozana (para 38) kisha unajifanya kuingia mitini. Nashawishika kuwa mwanahabari-makenika alikuwa akina sitaki-nataka. Nilidhani mtu asiye mzinzi, kama mwanahabari-makenika anavyotuaminisha, asingejihusisha na mazungumzo yanayoshadidia ngono. Nadhani angekuwa mkali mara moja! Tena katika hili anadiliki kuwadhalilisha wasichana wa Mbeya (pasi na kuwa na uhakina ni wenyeji wa kuzaliwa hapa) kuwa ni heri atongoze ng’ombe au mbuzi kuliko wao! (para 40 & 41).

Katika mambo yote aliyoyaona Mbeya, mazuri na mabaya, aliona la ngono ndio kuu. Afrika Kusini pamoja na kuongoza kwa maambukizi ya ukimwi bado ilionekana inafaa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia. Safari yote ya Mbeya mwanahabari-makenika ameshindwa kuona mambo chanya kama utekelezaji wa vitendo wa sera ya kilimo kwanza, hakupishana na malori yanayokimbilia Dar es Salaam yakiwa yamesheni vyakula na matunda anuai. Hakushanga hali ya hewa safi tofauti na hali ya Dar es Salaam iliyojaa sumu. Hakuona milima na mabonde yanayohitaji wawekezaji wa aina-aina. Hakuona ukarimu wa watu, wenyeji na wageni. Hakufurahia maji yasiyokatika. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Hitimisho.

Nina wasiwasi na ufahamu na uwezo wa kufikiri wa mwanahabari-makenika. Sidhani kuwa hajaenda shule kwani kusoma na kuelimika sio lazima vikatangamana. Nadhani ni wakati sote tuliolazimishwa kuisoma (ndio katutumia kwa lazima)ripoti hii tukaiangalia kwa jicho la pili. Hata majibu yangu haya pia yanahitaji upembuzi makini. Sio lazima yakawa ya kweli kwani nimeandika kwa kuzingatia maslahi ya kimkoa zaidi. Lakini nachelea mwanahabari alikuwa na nia ya kuupa mkoa wa taswira potofu zaidi ya ile iliyopo. Ni kweli mawazo yake ni baadhi ya changamoto sio tu katika Mbeya bali pia nchi nzima. Wapi hakuna mauzauza kama haya. Huko Dar es Salaam ambako mwanahabari- makenika anatoka/anaishi ndio usiseme!

Mnaweza kumtebelea John Mwaipopo huko Mwaipopo Blog

Tuesday, March 02, 2010

Ilivyokuwa Safari Yangu Mbeya


Imeandikwa na Mwana Habari
Duniani kuna mambo mengi sana , ambayo mengine ni kama vibaya kuhadithia kwa wengine kama labda ni wenyeji wa huko au labda kama wana mahusiano na kitu hicho inakuwa mbaya haswa kwa wale wasiopenda kujua ukweli wa mambo , lakini wote tunakubaliana kitu kimoja bila kusemeana ukweli hakuna mafanikio yanayoweza kufikiwa na binadamu kwa njia yoyote ile hata kwa nini .

Ntakupa mifano michache mfano huku afrika na sehemu zingine za bara asia na amerika ya kusini , viongozi ni waongo , wamewajengea mpaka watoto wao na vizazi vingine uwongo kiasi kwamba mtu akisema ukweli anaonekana muasi mbaguzi au pengine mchonganishi wanabakia kulalia uongo siku zote hawaendelezi vizazi na watoto wao katika secta ya sayansi na elimu ambayo inahitahi ukweli na uwazi kila kitu uwongo na ulaghai

Hata katika mila na desturi , huku afrika mila na desturi za uongo ni fani , angalia hili suala la ushirikina ?? ushirikina ni mali ya mwafrika na huku imejaa sana lakini ushirikina ni uwongo mtupu ni ujanja ambao mwingine akifundishwa ana adapt na unaweza kutumika kwa faida nyingi tu katika maendeleo na makuzi ya watu wengine hii ni sayansi inayohitaji kuwekwa wazi ila ndio hivyo uwongo umetuzidi mpaka tunajichukia .

Mimi huwa napenda kusema kila ninachojisia kinanivutia na nimeshuhudia mwenyewe kwahiyo sio uwongo napenda kuandika kwa njia ya hadithi au makala kwa watu haswa mafariki zangu , juzi nilikuwa mkoani mbeya na hayo niliyoandika ndio hali halisi ya watu wa mkoa ule wanavyoishi wengi wao hata kama wakikataa na kubisha wanakataa lakini wajomba zao , mama zao , wadogo zao na majirani zao wanaangamia .

Haswa katika hili suala tata la ugonjwa wa ukimwi , huu tuuangalie kwa pande 3 kuu yaani mimi , wewe na yule ( wale ) tuna nafasi gani katika kuendeleza jamii zilizobora ambazo hazisumbuliwi na jinamizi la ugonjwa wa ukimwi wala matatizo yoyote wote wakue vizuri waje kuwa taifa bora watoe mchango kwa majirani zao na vizazi vijavyo ?

Usijali bwana ( KILA MTU NA MAISHA YAKE AU SIO )

Ehe vipi mambo hapo ulipo ??

Hapa ni salama sana , maisha ni bam bam naweza kusema , sasa hivi ni mchana wa saa 6 hivi inaelekea saa 7 kamili , ni lunch time kwa wengine ila mimi huwa nakula chakula cha mchana kuanzia saa 9 hivi au saa 10 jioni halafu usiku huwa sili chakula napenda kula samaki na karanga hiyo ndio furaha ya maisha yangu ya kila siku , kila mtu anaamua na kutenda anachoona kinafaa au sio ?

Basi kipindi hichi cha karibuni wiki hizi 2 nilienda mbeya kwa ajili ya kazi katika offisi moja hili ni shirika la uingereza kazi yake ni kusaidia watu wa manispaa na miji katika ukusanyaji wa kodi na mapato na katika kuwafundisha zaidi kuendana na uchumi wa dunia jinsi unavyokuwa kila siku .

Shiriki hili tuna mkataba nalo wa mambo ya ufundi na shuguli zingine zinazohusu data na ukaguzi wa vifaa vyao vya mawasiliano , kutokana na mkataba huu kila baada ya miezi 3 lazima niende mkoani mbeya angalau kwa wiki moja kuangalia hizo mishine zao n akutatua matatizo yao kama yapo na maisha yanaendelea .

Kwahiyo wiki hizi ndio nilienda mimi na walishanizoea , lakini mwaka huu nilijuwana na dada mmoja hivi anafanya kazi pembeni mwa shirika hili yeye ni mama mahesabu , ananipenda sana mimi na wakati mwingine akinipigia simu huwa ananieleza kuhusu ngono jinsi tukikutana atakavyo nikumbatia , mabusu na mahaba mengine mazito mazito yaani amejichambua sana kuhusu maisha yake kule na anavyonizimia mimi .

Huyu dada alipata taarifa kwamba ntaenda kule , lakini huyu dada sijawahi kukutana nae zaidi ya kuchat nae tu na kuongea katika simu , dada wa watu alijiandaa sana kwa ajili ya kunipokea nikalale kwake yaani kitandani kwake na ile baridi anavyonihadithia anapenda kupata joto langu mambo kama hayo .

Nikatoka zangu huku jumatatu asubuhi saa 12 hivi kwa usafari wa Scandinavia , nilikatiwa tiketi mpaka mbeya lakini nilivyofika iringa pale makambako nilishuka katika gari hilo nikapanda basi lingine nilijua tu huyu dada atakuwa ameshaambiwa naenda na basi gani wakanipokee stendi ya mabasi hapo nilishmkwepa kwa kiasi kikubwa .

Muda wa saa 1 hivi usiku basi lilikuwa limeshaingia mbeya mjini mimi sikwenda kule mwanjelwa nikashukia sehemu moja inaitwa fire , hapo pembeni yake wala sikuchukuwa hoteli , nilipeleka vitu vyangu katika nyumba ndogo za wageni kwanza nione hali ya mambo inavyoenda kabla sijaamua mambo mengine .

Saa 3 hivi usiku ikatimia kama nilivyootea yule dada akanipigia kuniuliza kama nimeshafika mbeya , nilimuuliza amejuaje kama naenda mbeya ? akasema ameambiwa na receptionist wa pale kwa mkuu wa mkoa , kwahiyo hali ikawa hivyo sikuwa na jinsi ya kujitetea .

Lakini niliamua kumdangaya tu , nikamwambia safari imeahirishwa bwana , mpaka tutakapowaambia hapo baadaye mwezi huu kwahiyo nitaenda mkoani singida au mtwara kwa kazi kama hizo “ Ohh yona unasema kweli ? nilivyokuwa nakungoja kwa hamu hivyo nikupe mambo ? na majambo ?”

Basi nilienda kidogo katika internet café kwa ajili ya kumwandikia email yule receptionist wa pale kumweleza hali halisi kisha nikampigia simu kumweleza kuhusu niliandisha katika email kwa kifupi alinielewa kwahiyo kazi ikawa kwake asiseme kama nimekuja mbeya na wala nikifika kule asiniite jina langu akinitaka aniite SHY tu mengine sijui .

Asubuhi yake ikafika yaani jumanne , niliamka katika saa 3 hivi asubuhi , hapo nilienda kuweka vitu vyangu katika hoteli moja eneo la meta mjini mbeya karibu na kituo changu cha kazi nikamuuliza tena yule receptionist kama yule dada anayeningoja yuko karibu au la , kweli yule dada alikuwa mbali kidogo .

Nikatoka hapo kuelekea katika kituo cha kazi kufanya ile iliyonipeleka pale , niliifanya kwa masaa 3 hivi ndio nilimaliza kwahiyo nikarudi zangu katika hoteli , huku nilienda tu kujisafi kwa mara ya pili kubadilisha nguo na kuvaa kama mtoto wa kijiweni halafu nianze kutembelea mitaa ya mji wa mbeya kuongea na watu haswa vijana .

Mbeya kuna mambo ya ajabu na wakati mwingine ya kutisha kama hujazoea , maajabu yake ni kwamba “ HUU NDIO MJI WA PILI KWA WINGI WA MAKANISA BARANI AFRIKA “ Ni mji wenye makanisa mengi kuliko yote Afrika Mashariki Na Kati ,huu wingi wa makanisa yaani ukitembelea hatua 30 unakuta kanisa mbele yako au kama sio kanisa unakuta sehemu ya mahubiri mbele yako hata pembeni yako .

Huu wingi wa makanisa sio hoja kwamba watu wa huku wameshiba neno la mungu kiasi kwamba wanaweza kubadili maisha yao na kuwa mazuri zaidi au kuwa bora zaidi la hasha , wamejawa na neno la mungu mpaka limepasuka yaani wamekinai neno la mungu sasa wanaona kuwa na makanisa ni fasheni .

Huu ndio mji unaoongoza kwa kukua kwa maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi katika afrika ukiachilia jberg , huu unafuatia , kutokana na kwanza uko Mpakani , watu wengi wa afrika ya kusini wanapoingia Tanzania kwa njia ya lami hupitia mbeya kuja dsm , wale wa Zambia nao ni mbeya , Botswana na kadhalika ni mji ulio katika majaribu mengi sana .

Unaona makanisa mengi , watu wengi wameokoka na kadhalika lakini watu wanaangamia kwa ugonjwa wa ukimwi kila kukicha na wenyewe wenyeji wa hapa wengi hawaamini kama kuna ukimwi wanaamini mtu akifariki basi amefariki kutokana na mungu kumwita amechoka maisha ya dunia , wengine ndio hizo imani zao akifa mwenzao amelogwa na mambo kama hayo .

Hapa mjini ukikutana na wasichana 5 basi 3 wanamarafiki wa kiume ambao sio wanafunzi wenzao yaani watu wa nje tu , wamachinga na madereva au watu wa shuguli zingine , hii inaadhiri sana hawa vijana utendaji wao madarasani , maishani na katika maamuzi mengine muhimu katika maisha yao kutokana na nguvu za watu wengine wa nje hawa wafanya biashara .

Mimi hoteli niliyofikia ilikuwa karibu na barabara kidogo , nilikutana na wanamuziki wa bendi ya Akudo Sound , hawa wanamuziki wacheza shoo wao wale wasichana wote ni chini ya miaka 22 , basi hapa katika hii hotel unachukuwa chumba halafu wahudumu wanakuuliza kama unapenda kupata dada wa kuishi nae wakati wote uko hapo katika hoteli .

Yaani huyu msichana atakuwa anakufulia nguo zako ulizokuja nazo na kukunyooshea wakati haupo , anakupa huduma ya ngono ( HII NDIO HUDUMA KUU ) , ukipenda atakuwa anakupikia pamoja na mambo mengine kukuogesha , na vitu kama hivyo , sasa unamwangalia huyu msichana mrembo ( WENGI WAO NI WAREMBO HASWA ) ametulia ana miaka chini ya 25 kwanini anakuja kujiuza huku , amekosa nii maishani mpaka amekuja katika hizi hoteli kujiuza .

Ukikataa kuchukuwa msichana inawezekana usiku wanakusumbua kwa kelele kule katika bar au dirishani mwako , wanakuuliza kama unataka huduma au la , kama hutaki wengine wanaaza kukutusi na maneno mengine ambayo siwezi kuyataja kama wewe shoga nini ? Unaliwa kiboga ? yote haya kisa umemkataa .

Ndio unaweza kuamua kumchukuwa , ukimchukuwa tu ujue sio wewe peke yako uliyemchukuwa labda wiki nzima hajalala kwao au kwake yuko pale anatoa huduma kwa wateja mbali mbali , kila siku yuko katika ngono na mambo mengine yasiyo na msingi kwa binadamu wa kawaida kama ameadhirika basi na wewe uko njiani , safari yako inakuja nap engine unaweza kuadhibiwa zaidi .

Saa zingine unaweza kutoka chumbani kwako katika corridor msichana anaweza kukuvulia chupi ? anakuonyesha alivyoumbika , ni kigiza hivi huoni vizuri lakini ukiona msiri wa chupi unalegea na kuteremka chini utasimama uangalie kunani , wengine utakuta wamesimama katika corridor na nguo zinazoonyesha maungo yao kazi ni kwako wewe mtazamaji yaani mimi niangalie nimekubali nichukuwe mzigo ?

Naweza kukubali , kukubali ni rahisi sana kwasababu inasemekana huyu msichana kukaa nae kwa usiku mmoja ni alfu 2 yaani hii alfu mbili hata kondom yaa maana hupati kama unaamua kulala nae na kutumia kinga , kinga zenyewe haziaminiki ya nini kufanya vile wakati najua wako zaidi yake ? na nikwambie siri wanawake wa mbeya wengi ni wanawake asili ya kiafrika yaani wamejazia ndio hapo sasa mate yanakutoka udenda njee , vishawishi na mambo mengine ya usheee .

Kwahiyo ndio hivyo , kesho yake nilitoka katika hoteli hii nikaenda katika hoteli ingine nikawe huru zaidi kwakuwa nilipenda kupiga picha mji ule wakati wa usiku niwatumie baadhi ya rafiki zangu wengine wanaopenda kujua zaidi kuhusu mji wa mbeya na mambo yake , ndio hivyo niliwakimbia hawa wadada mwaaah .

Siku ya pili ni kwenda kuandika report kuhusu ile kazi ya jana na kufanya majaribio kuhusu mashine zingine , kuwauliza maswali kadhaa kama wanamatatizo yoyote yale na kadhalika , kwahiyo hawakuwa na matatizo yoyote kwahiyo niliwaaga kutoka pale nikaanza safari ya kwenda tukuyu sikuwahi kufika tukuyu nilipenda kufika tu kwa kuwa kuna baadhi ya rafiki zangu wanatokea mkoa huu .

Nilifika pale muda wa saa 9 hivi jioni , nikatafuta sehemu ya kupumzika nikapata nikaenda kuhifadhi vitu vyangu , nikabeba kamera yangu , na kitabu changu kidogo kuanza kwenda mitaani , nilibahatika kuona internet café moja jirani pale , nikaingia ndani mule kufanya shuguli zangu .

Basi nilifika katika internet café hii niliwaambia watu kwamba niko mkoani mbeya sehemu inaitwa tukuyu , kuna baadhi ya watu ni wenyeji wa mkoa wa mbeya tulikuwa tunachat pamoja wengine wanatokea tukuyu na kyela , wakanielekeza makwao niwatembelee na wengine walihitaji salamu kutoka kwao .

Ndio hivyo nilipata marafiki wapya wa mkoani mbeya kw anjia ya mtandao , basi pale nilipokuwa jirani kidogo kama kilometa 10 hivi ndio sehemu ya kwanza nilitakiwa kwenda , nilifanikiwa kwenda mpaka kwa hiyo nyumba niliyoelekezwa na rafiki wa internet niliongea nao na kuwapa namba za simu za huyo ndugu yao aliye majuu , kwingine ni kyela lakini kyela mpaka kesho yake safari yangu ya mwisho .

Muda wa saa 3 hivi usiku nilitoka zangu kule mtaani nikarudi zangu katika nyumba niliyofikia , nilienda kuweka vitu vyangu na nikabadilisha mavazi kama ya kijana mtanashati , mwenye aibu sana , niliyekuwa mpweke nahitaji huduma Fulani ??? huduma ya ……?? Nikakaa pale katika bar , nikaagiza nyama choma nikawa nakula na glasi ya juisi .

Dada mmoja hivi ametokea zake huko sijui wapi akaja pale , akakaa mbele yangu nikamkaribisha vizuri sana kwa roho moja tukaanza kuongea , huyu msichana ni mrembo na amejazia kuanzia kigua , miguu na kadhalika hakika huyu ni masha alah kama nilivyokuambia wasichana wengi wa mkoa wa mbeya wamejazia au sio ?

Mrembo wa watu tukaongea kwa masaa 2 hivi mpaka saa 5 usiku , akaniomba namba ya simu nikampa , pia aliniuliza wapi ninapolala usiku huo , kama niko na mke au mtu maalumu usiku huo , nilimjibu sina niko mwenyewe tu na ninapenda kuwa mwenyewe hivyo hivyo inavutia zaidi au sio ?

Dada wa watu aliondoka , nami niliondoka zangu kurudi katika chumba kwa ajili ya mapumziko ya siku ile , basi nilipofika kule kwa hoteli muda kidogo yule dada aliniandikia sms inasema ‘ DEAR , UKO WAPI NIJE ? NINASIKIA BARIDI SANA NAHITAJI JOTO LAKO “ mhh nikakumbuka ni mambo yale yale nilivyokimbia kule mbeya mjini .

Nami nilimjibu “ JAMANI DEAR MBONA NA MIMI NASIKIA BARIDI NIMEJIFUNGIA CHUMBANI FUNGUO SIJUI IKO WAPI USIJE BWANA “ huyu dada akasoma msg yangu nilipokea jibu lake “ WE XXXNGE SANA , KWANINI ULINITONGOZA ? tukaendelea kubishana katika simu “ AHH NIMEKUTONGOZA ? SI BORA NIKATONGOZA NGOMBE AU MBUZI ? “

DADA : YAANI UNANIJIBU HIVYO ?
YONA : NDIO , BORA NITONGOZE NGOMBE

Basi nilizima ile simu yangu ili niwe huru zaidi nilale , kweli nikalala zangu mpaka usiku saa 10 hivi , nikaamka , nikaenda kwa yule mlinzi wa pale kumwambia anifungulie geti nataka kutoka nje akakataa akasema mpaka nimwambie receptionist wa pale naye alikuwa amelala , basi nilijaribu kumgongea hakuamka .

Uvumilivu ulinishinda , nilienda katika begi langu nikachukuwa vifaa nikatengua kitacha cha mlango wake mpaka ndani kwake nilimkuta yuko juu ya msichana Fulani katika fani ahaha , nilitaka kucheka lakini siku cheka , nilimfuata moja kwa moja mpaka pale nikamfunua shuka lile nikamshuka kitandani na kumpiga teke kidogo akajigonga katika kabati la nguo mule chumbani .

Nikimwomba sasa anifungulie mlango nitoke ndani ya ile hoteli kuna sehemu nataka kwenda , alitaka kuvaa nguo nikazichukuwa nguo pamoja na za yule msichana wote nikazitupa nje ya mlango ili anipe funguo nikafungue mwenyewe , alibisha nilivyomwomba basi nikamfuata tena kumtisha .

Ndio alisalimu amri akanipa funguo zile mimi huyo na begi langu nikatoka nje , nilikuta taxi pale karibu na hoteli lilinikimbiza mpaka kituo cha gari kupata basi la kuelekea kyela nikakata tiketi zangu pale na kupakiza vitu vyangu katika gari lile .

Kyela nilifika salama sana , nikafanya na kutekeleza yaliyonipeleka kule mwisho siku hiyo niliyo usiku nilirudi mbeya mjini ili nijiandae kwa safari ya kurudi zangu mjini dare s salaam kama kawaida , nilifika mbeya mjini katika saa 5 hivi za usiku moja kwa moja nilielekea katika nyumba ya wageni kwenda kupumzika .

Kesho yake ya asbuhi ilikuwa ni saa 11 hivi niliamka mapema nikajiandaa kwenda standi ya basi nikapata basin a safari ya kuja dare s salaam ilianza na kunoga kama kawaid nilifika jiji la mzizima nikiwa salama salmin na mwenye afya tele .

Nilifika muda wa saa 10 hivi , nikaja zangu hapa katika office kuleta report za huko kisha nikakimbilia katika mtando usiku huo huo kwa ajili ya kutuma hizi picha kwa watu Fulani marafiki zangu .

Na huo ndio ukawa mwisho wa safari yangu maridadi mkoani mbeya nilienjoy vya kutosha , karibuni nitaenda mkoani Mtwara , Lindi , Dodoma , Morogoro , Singida na Arusha kwa ajili ya kazi hizi hizi tuone itakuaje

Sikiliza tu

Monday, March 01, 2010

Sinema - Ta Kimbia


Kuna sinema mpya iitwayo 'Ta Kimbia' ambayo imetengenewa na dada wa KiKenya, Yasmine Bandali. Itaonyeshwa siku ya jumapili Machi 7, 2010 huko Washington, D.C.

This takes place on March 7, 2010 at 2.30p.m.
Address: 701 Pennsylvania Avenue NW, Naval Heritage Center by the navy archives.

Tickets can be purchased at the door or on line at www.dciff.org (search Ta Kimbia) Please see the trailer: http://www.youtube.com/watch?v=ulESLoc3Ehk


********************************************************
Dada Yasmine Bandali anaaelezea jinsi alivyofanikiwa kutengeneza sinema yake:

After shopping around an award winning script for several years, I decided that the only way to get a movie made (if you had no connections) was to Do-It-Yourself. So in April of 2009 I produced and directed a feature movie in Kenya called TA KIMBIA (I will run).

This film is about a young boy who dreams of running but must contend with family pressure and poverty. The movie was shot over 12 days on a shoestring budget (seriously indie!) Amongst the challenges were: numerous film permits and location fees draining the budget, the intense heat, cultural issues and missing equipment.

But on the good side: the movie DID get made. I got New Balance to donate me shoes and apparel, I got a 2 time gold Olympic medalist Kip Keino to act as the coach in the movie, and I got a real aircraft from Kenya Airways, in the film. And now it is screening at the DC independent film festival.

And also the film website: http://www.takimbia.com/

See you at the screening!

Coming Back Black


THE LORD IS MY SHEPHERD, I SHALL NOT WANT.

Psalms 23:1"Time is like a river, you cannot touch the same water twice because the flow that has passed will never pass again. Enjoy every moment of life."

********************************************

In a round table discussion about whether reincarnation was really possible, a financially struggling single woman said,"I want to come back as a rich white woman's poodle that's pampered and rides around all day in her luxury car."


A tired waitress said, "I want to come back rich and make a lot of money and be a mega-super recording star".
The frustrated computer tech said, "If I can come back, I want to be the President, so I can change a lot of things about this world near and far."
Another woman thought about it and said, "I don't know if it's possible, but if I can... God, please let me come back a BLACK WOMAN. I want to come back with a mind fierce and sharp, with a spiritual faith that never waivers or doubts. With a smile that is warm, and a body divine - with honey, cinnamonOr chocolate skin, draped in purple and gold. And, whether young or old, always have enough money so the words broke, layaway, overdue, or postdated check aren't in MY vocabulary.I want to be a sister to my sister, a woman wise when choosing my mate or a date. I want to be able to cook greens, barbecue chicken, macaroni and cheese, cornbread, a peach cobbler and a lemon pound cake all at the same time.
I want to come back a BLACK WOMAN with self-esteem, worthy of being treated like a QUEEN by my King, a woman with patience, love, and wisdom for children, A BLACK WOMAN with subscriptions to Essence, Jet, Ebony, Black Enterprise, and the Wall Street Journal.I want to come back a BLACK WOMAN with at least one great diamond from the Motherland on my finger.I want to come back with the quiet courage of Rosa Parks, the voice of EllaFitzgerald, the political courage of Ida B. Wells, the determination of Harriet Tubman, spiritual poise of Susan L. Taylor, the business savvy of Oprah Winfrey, the eloquence of Dr. Maya Angelou, and be the author of bestseller books like Iyanla Vanzant.
I want to come back as a BLACK WOMAN, who can stay focused on GOD regardless of the circumstances. I want to be SAVED from the penalty of sin.I want to never let what a person says, or does, change my demeanor. I want to be humble, and to love and be loved unconditionally.I want skin that is flawless and soft, eyes of discernment, and lips that speak ONLY the truth. I want hands of gentleness and feet of prosperity. I want to be a lawyer to enforce the laws which man has broken.If reincarnation is real, please let me come back as a BLACK WOMAN!!!"
BLACK WOMEN ARE WONDERFUL

Saturday, February 27, 2010

Wanajeshi wa Marekani Waugua Malaria Haiti

Leo kuna habari kuwa wanajeshi sita wa kiMarekani walioko Haiti wamepata ugonjwa wa homa (Malaria). Na sasa kuna habari kuwa wanajeshi walioenda Afrika pia wameugua, wengine mpaka karibu wafe. Kwa kweli watu wanaanza kuhaha maana wanadhani malaria ni ugonjwa mbaya mno. Sasa hivi mtasikia watu wanahofu kwenda Haiti au Afrika shauri ya kuhofu kuambukizwa malaria.
Ukiumwa malaria Marekani unafungwa quarantine, utadhani una ugonjwa wa ukoma. Nakumbuka MBongo fulani alienda likizo Bongo, alivyorudi alimwambia mwajiri wake kuwa anaumwa malaria, walifukuza kazi mara moja. Mwingine aliiambiwa asirdui mpaka ana cheti cha daktari kuhakikisha ni mzima.

Mnaweza kusoma habari zaidi hapa:

Friday, February 26, 2010

Swagga Night


INFINITY ENT'S pres, SWAGGA NIGHT. Sat 13th, MAR 2010 at SPICE LOUNGE, 3 Savoy Crecent, Theatre District, MILTON KEYNES. mk9 3pu,DJ DOUBLE T & Dj BILLY will make it happen.BONGO FLAVAS, R&B, RAGGA, OLD SKOOL. Dress Smart to impress. 10Pm till Late, Admission: £5 B4 12.VIP TICKETS AVAILABLE AT THE DOOR. Mishemishe sio mchezoo...

Wednesday, February 24, 2010

Best Poem in the World


BEST POEM IN THE WORLD

I was shocked, confused, bewildered
As I entered Heaven's door,
Not by the beauty of it all,
Nor the lights or its decor.

It was the folks in Heaven
Who made me sputter and gasp--
The thieves, the liars, the sinners,
The alcoholics, and the “trash.”

There stood the kid from seventh grade
Who stole my lunch money twice.
Next to him was my old neighbor
Who never said anything nice.

Herb, who I always thought
Was rotting away in hell,
Was sitting pretty on a cloud,
Looking incredibly well.

I nudged Jesus, 'What's the deal?
I would love to hear Your take.
How'd all these sinners get up here?
God must've made a mistake.

'And why is everyone so quiet,
So somber - give me a clue.'
'Hush, child,' He said, 'they're all in shock.
None thought they'd be seeing you.'

JUDGE NOT!!

Remember...Just going to church doesn't make you a
Christian any more than standing in your garage makes you a car.

And a church is NOT a museum of saints

but a hospital for sinners

Every saint has a PAST...
Every sinner has a FUTURE!

Now it's your turn... Share this poem.

Monday, February 22, 2010

Saturday, February 20, 2010

Mazishi ya Reggie Mhango Leo

Mzee Reginald Mhango amezikwa leo katika makaburi ya Kinondoni. MAY HE REST IN ETERNAL PEACE. AMEN.

Video kwa hisani ya Muhidini Issa Michuzi

Friday, February 19, 2010

Tribute to Reggie Mhango

Chief Secretary katika ofisi ya Rais, Philemon Luhanjo akitia sahihi katika kitabu cha Rambirambi.

Reggie's Enternal Legacy

By Danford Mpumilwa

I am writng this piece from Nairobi. Actually I am in process of soon transiting to Kampala. I have been busy the whole day with some official business with some senior officials from the Ministry of Education here. Under the circumstances, taking into consideration the recent problems facing the top officials of the Ministry, I am happy to say that my 'mission' has been sucessfuly accomplished.

Following a short break in my official engagements I rushed into my hotel's internet room to, among others, catch up with the latest news from Bongoland. I happen to be an ardent follower of Michuzi's blog for the simple reason that it enables me to catch up with the latest info-news from home.But today's updates included the shocking news of Reginald Mhango's passing on.

There is no doubt the likes of me and many otthers who were inducted into the Tanzanian Daily/Sunday newsroom in the mid to late 70s must have received the shocking news with utter helplessness. Me and my colleagues, who include Franklin Mziray and Wence Mushi sauntered into that newsroom in 1977 from the University of Dar es Salaam with the fresh arrogance that we, fresh graduates from the 'Manzese' University, were masters of the journalism profession.

I have to admit that in due course, thanks to Reginald Mhango, fondly called 'Reggie', we were made to swallow our pride and learn the ABCs of the profession in a very conducive and inspirational manner. It is thanks to Reggie who took time, unlike many other senior editors at the paper, to lovingly tutor us in the art of writing simple undertandable language which worships facts.

Many of us have gone into different ways of life but none, and I am sure I speak for most of those who were tutored by Reggie, will forget the important lessons we learnt from his, if I can quote the North Korean-speak ' 'on the spot fatherly guidance' in the profession. By then Reggie was what we called 'kiraka'. He would this day be the News Editor this week and the next one be the Features Editor or Deputyt Editor.

Space does not allow me to say much about him but I can vouch that Reggie played a pivotal role in grooming me and many others into the profession. I and my colleagues will miss him dearly. And we will be left wondering as to who will be the next, Reggie, the comitted and non compromising guide to our nations 'Cub Reporters'.

At times like these it makes all of us roam into our worldly lives' philosophy of the inevitable end. And it is only then that we can serously strive to contribute to a lasting development of a brghter future of humanity for us and our future generations. For only then can our deeds and ideas live in eternity. And that is what Regie has has lovingly left us with.

My the Almighty God Rest His Soul in Peace!

Amen!
Danfod Mpumilwa

Thursday, February 18, 2010

Tanzia - Reginald Mhango (Reggie) Bosi wangu Daily News

Reggie na copy yake ya sinema Bongoland II. Sehemu ya hiyo sinema ilipigwa nyumbani kwa Reggie huko Magomeni Mikumi. Nilipomwomba kupiga sehemu ya sinema hapo allikubali bila kusita na pia alifurahi kuona jinsi wanavyotengeneza sinema. Alifurahi uchapa kazi wa crew waliotoka Marekani.
Mimi, Reggie Jr. (katikati) na Mzee Reggie Mhango. Picha hii tulipiga siku ya October 27, 2009 nyumbani kwa Reggie. Nilisikia kutoka kwa kaka Michuzi kuwa alipata stroke lakini hajambo. Nilimpigia Reggie simu kutoka Marekani mwezi wa saba na kumwaidi kuwa nitafika siku hiyo na nilifika. Alifurahi sana.
************************************
Wadau, nimepokea kwa majonzi habari ya kifo cha bosi wangu mpendwa nilipokuwa Daily News, Reginald Mhango (Reggie). Reggie alikuwa na utu, uvumilivu, na upendo kwa kila mtu. Nakumbuka nilikuwa napata shida nikiwa na mimba mwaka 1989. Tumbo ilianza kuwa kubwa na kutembea ilikuwa shida. Reggie aliniambia nikae nyumbani mpaka nijifungue na kumaliza maternity leave. Si hiyo tu lakini kwa kweli sikumbuki kumwona akiwa na hasira au akigombana na mtu. Alitufundisha sisi waandishi chipukizi uandishi wa habari hasa, na kutusaidia katika kuandika habari safi...to the point! Nje ya kazi, ilikuwa hata kama una shida binafsi alikuwa tayari kusikia na kutoa mawaidha.
Mnakumbuka ile kesi ya Mzee Athumani Ali Maumba. Yule babu wa Magomeni aliyekuwa analawiti watoto wa kike wa primary, Reggie alisaidia hizo habari zichapishwe. Hamwezi kuamini lakini mpaka hiyo kesi ya Maumba ilikuwa kama mwiko kuandika habari hizi. Hata waandishi wa habari wengine walikataa kuripoti. Mimi ndo nilikubali kwenda huko kwenye hiyo shule Kisutu na kuchunguza. Baada ya ripoti kukamilika wakuu walitaka kuzuia, Reggie aliongea. Kesho yake walitoa para mbili tena kwa kificho. Baada ya kuona si mwisho wa dunia, habari za Maumba zikawa front page. Msishangae na kusema najiona,lakini mkumbuke kuwa wakati huo kulikuwa na magazeti machache nchini. Daily News (serikali) Uhuru (Chama) na Mfanyakazi, Kiongozi (Wakatoliki). Redio ilikuwa RTD tu. TV ilikuja baadaye.
REST IN ETERNAL PEACE REGGIE. WE WILL MISS YOU DEARLY BUT YOU IMPARTED GREAT KNOWLEDGE AND WISDOM IN US AND WE WILL PASS IT ON!
Mnaweza kusoma habari zaidi kwa Kaka Michuzi.
Na pia someni Daily News:

Wednesday, February 17, 2010

Wateule wa Oscars 2010 Wala Chakula Pamoja!


Wadau, kila mwaka ni kawaida kwa walioteuliwa kupata tuzo ya Oscars kula chakula cha mchana pamoja. Leo walivigida huko Hollywood. Chakula chenyewe kina kuwa cha fahari kweli. Sherehe ya kujua nani kashinda na kutuza wasanii bora, na watengeneza sinema bora itaka siku ya jumapili, March 7, 2010.

Nangojea kwa hamu kumwona dada Mo'nique akishinda Oscar ya Best Supporting Actress. Mo'nique lazima ashinde maana hiyo kazi aliyofanya kwenye sinema Precious ni kiboko. Pia nina hamu ya kumwona Gabourey Sidibe akitembea kwenye Red Carpet. Akishinda Tuzo ya Mcheza sinema bora wa kike itakuwa maajabu. Nasmea hivyo kwa sababu kwanza ni mweusi, tena kwa hapa Marekani mweusi tii, mnene, na ni mara yake ya kwanza kuigiza katika sinema. Akimshinda Meryl Streep nitasema kweli Hollywood imebadilika.

Sakata la Babu Mweusi Aliyeibiwa Tiketi ya Bahati Nasibu

Wadau, huo Texas kuna babu Mmarekani mweusi aliyeshinda dola milioni moja kwenye tiketi ya bahati nasibu. Kijana wa kihindi (kutoka Nepal) ambaye alikuwa anauza duka kamtapeli huyo babu na kumwambia kuwa eti ina dola $2 tu. Halafu alichukua kaenda kui-cash na kurudi kwao Nepal.

Kwa bahati nzuri polisi na serikali waliingilia na babu yule atarudishiwa kiasi cha hizo pesa. Jamani uchu wa pesa.

Hapa Marekani tumezoea kuona wahindi wanauza maduka ya convenience, na wengi ni wazuri and waaminifu. Huyo kijana wa kihindi kawachafua kweli kweli.

*************************************************************************


Part of Stolen Lottery Jackpot is Returned to Grand Prairie Man

By ALEX BRANCH

Willis Willis will finally get some of his $1 million lottery jackpot.
On Tuesday, state District Judge Bob Perkins signed an order restoring to the Grand Prairie man $395,000 seized from the bank account of a store clerk accused of stealing the winning ticket.
"I feel pretty good, a bit relieved," said Willis, 67, shortly after the hearing in Austin. "I'm glad we finally made it to this point."
Willis said he planned to spend part of the money on medical bills and a daughter's college tuition.
"It's all stuff that has to be paid for," he said. "Things I really needed the money to take care of."
About $365,000 of the cash restored to Willis was seized by Travis County prosecutors from bank accounts opened by the store clerk, Pankaj Joshi. The other $30,000 was recovered from people in Dallas to whom Joshi had given money.
Authorities believe Joshi took the ticket from Willis, told him it was not a winner and cashed the ticket himself. He then returned to his native Nepal.
The Nepalese government has frozen an additional bank account connected to Joshi there, said Patty Robertson, a Travis County assistant district attorney. Sean Breen, Willis' Austin-based attorney, said the account is believed to hold around $300,000.
Prosecutors are working with the U.S. State Department to return to the money to Travis County. However, because a foreign government is involved, the process is complicated, Robertson said.
"I really don't have a timetable on when, or if, that will happen," she said.
About $50,000 of the winnings probably won't be recovered because Joshi withdrew it in cash, Breen said.
Joshi, 25, who was a student at the University of Texas at Arlington, is charged in Travis County with fraud and unlawful flight to avoid prosecution. His bond is set at $10 million.
Authorities have gone to great lengths to locate him. Robertson said. They have contacted his parents and notified the Nepal Embassy in Washington, D.C.
Newspapers in Kathmandu, the Nepalese capital, have reported extensively on the case, she added.
Breen said he will continue to try to force the Texas Lottery Commission to award Willis the rest of the jackpot. Lottery officials have refused, saying they consider Joshi the winner because he signed and redeemed the ticket.
After Tuesday's ruling, Breen said he wondered how the commission could still deny that Willis was the winner.
"The judge looked at the evidence and determined it was obvious Mr. Willis was the winner," he said.
Willis bought the winning ticket May 29 at the Lucky Food Store at 902 Great Southwest Parkway in Grand Prairie, authorities said. He returned there May 31 to have the Mega Millions ticket and others scanned to see whether they were winners.
The Mega Millions ticket was a winner, but Joshi, who scanned it, gave Willis only $2 for a Cash 5 ticket, authorities said.

KUTOKA:
http://www.star-telegram.com/local/story/1973913.html

Tuesday, February 09, 2010

Wasanii Wenzangu - Oscar Micheaux Family Theater

Nimeulizwa maswali mengi kuhusu kikundi chetu cha Oscar Micheaux Family Theater cha hapa Boston. Tunakutana Boston South End, Blackstone Community Center, kila mwaka wanafanya mchezo, The Harlem Renaissance Revisited na michezo mingine lakini hiyoya Harlem ndo kubwa. Mimi nilijiunga na kikundi mwaka jana.

Pichani: Waliosimama kuanzaia kushoto - Charles 'Matumbi' Jackson, Lee Smith, Kushelia Shukhu, Joe Banks Jr. Waliokaa, Bonita Andrade, Chemi, Linda Henderson na Catrina Andrade. Picha ilipigwa mwanzoni mwa January na Tina Bergeron.

Wako wengine wengi zaidi, lakini hawakuwepo wakati tunapiga hii picha.

Saturday, February 06, 2010

The Harlem Renaissance Revisited - Mchezo wa Kuigiza

Mother Africa /Mama Afrika
Linda Henderson akimpaka make-up Joe Banks Jr. (Steve Lucky)

Kushelia, Linda na Catrina walioigiza kama watumwa

Muongozaji (Director) Wetu Lee Smith na Oscar feki tuliyomkabidhi kama shukurani kwa kazi nzuri. Lee aliigiza kama Langston Hughes pia.


Mimi na Ruby Hill tukiwa tumevaa costumes kwa ajili ya Party Scene.


Mimi niligiza kama Mother Africa pia, safari hii. Father Africa alikuwa David Bowden. Kwa mara ya kwanza walikuwa na Mother Africa ambaye anaongea lugha ya Afrika. Khanga na vitenge nilinunua nilivyokuwa Dar mwezi Novemba. Ungo nilinunua Ubungo TANESCO. Nilikuwa na nyingine ambaye nilikuwa nafanya mazeozi nayo, ilibiwa pale tulipokuwa tunafanya mazoezi! LOL!


Costume yangu ya awali kama Ms. Thelma anayetafuta mapenzi na ana ndoto ya kushinda bahati nasibu.


Mimi na Charles Jackson aliyeigiza kama Joe the Bartender. Mwanzo Ms. Thelman anamkataa Joe, lakini baadaye anamkubali na wanafunga ndoa.



Wadau, jana jioni (Ijumaa) niliigiza katika mchezo wa kuigiza, The Harlem Renaissance Revisited with a Gospel Flavor. Mchezo wa Harlem Renaissance umetungwa na Haywood Fennell Sr.

Thursday, February 04, 2010

The Harlem Renaissance Revisited at Northeastern University

Wadau, kesho nitaigiza katika mchezo wa kuigiza The Harlem Renaissance Revisited with a Gospel Flavor. Role yangu ni ile ile ya Ms. Thelma anayependa kucheza bahati nasibu na mabaye anatafuta mwanaume wa kumwoa.

Kiingilio ni bure, tiketi zinapatika Box Office ya Blackman Theater, Northeasternm University, 360 Huntingto Avenue, Boston, MA. Itaanza 7:00pm (saa moja jioni).

Karibuni!

THE HARLEM RENAISSANCE REVISITED

BLACKMAN THEATER

IN ELL HALL, KRENTZMAN QUADRANGLE

NORTHEASTERN UNIVERSITY

360 HUNTINGTON AVE, BOSTON MA.

FRIDAY, FEBRUARY 5, 2010

STARTS AT 7:00PM.

Monday, February 01, 2010

Blogu Mpya - WanaMuziki Tanzania

Imeanzishwa na mwanamuziki John Kitime.

http://www.mwakitime.blogspot.com/

Tukumbuke Waliovyofanya - Greensboro Four


February ni Black History Month yaani mwezi wa kukumbuka historia ya weusi Marekani. Kwa wakati huu ni muhimu sana tukumbushe vijana wetu historia ya weusi Marekani...utumwa, ubaguzi na vitendo vya uonevu na mauaji.

Wadau, hapa Marekani siku hizi tumezoea kwenda madukani na kwenye migahawa na kuhudumiwa bila matitizo. Haikuwa hivyo siku zote. Mpaka miaka ya 1960's kulikuwa na sehemu ambazo weusi walikuwa hawahudumiwi. Walikuwa hawaruhusiwi kula chakula katika migahawa, kulikuwa na mabango 'Whites Only' (Wazungu Tu). Kama walikuwa wanahudumia weusi basi ilibidi waende nyuma ya jengo na kupewa chakula kwenye mfuko, huko si ajabu wazungu waliitemea mate na kuiweka mikojo, mavi na uchafu mwingine.

Greensboro Four walikuwa vijana weusi wanne waliokuwa wanasoma katika Chuo Kikuu cha North Carolina A & T. Siku ya Februari mosi mwaka 1960, waliamua kwenda kukaa katika sehemu ya wazungu kwenye duka la Woolworth's na kudai wahudumiwe. Walisema kwa nini hapo dukani wanauuzia weusi mahitaji, lakini hawawezi kuwaruhusu kukaa kunywa kahawa na kula chakula hapo. Kwanza weusi wenzao waliwaona wajinga na wapuuzi, lakini wengine walijiunga nao na mwisho migomo iliandaliwa katika miji15! Hatimaye ilibidi rais wa wakati huo Rais Dwight D. Eisenhower aiingilie! Hatimaye Woolworth's waliruhusu weusi kula hapo.

Kusoma habari ya Greensboro Four BOFYA HAPA: http://www.cnn.com/2010/US/02/01/greensboro.four.sitins/index.html?hpt=C1