Monday, December 01, 2008

Philips


Wadau mnakumbuka hii tangazo?

" Philips ndio enyewe....Sauti safi sauti kubwa!"

Enzi hizo wewe mtu kama una redio kama hii, short wave, universal etc.! LOL!

4 comments:

Anonymous said...

Hahaha da chemi umenikumbusha mbali sana sisi kwetu usukumani zilikuwa zinabebwa mgongoni halafu mtu anaendesha baiskeli yake huku yeye anaimba kisukuma, na redio nayo imefunguliwa mpaka mwisho zilikuwa zinaitwa asante mkulima mtu akiuza pamba tu lazima atanunua redio na baiskeli, kweli tumetoka mbali.

Anonymous said...

Enzi hizo ni redio tu hakuna cha TV wala DVD wala kideo. Redio ilikuwa mali kweli si mchezo. Na huo wimbo ya Philips kila mtu aliijua. Mtu akisema Philips watu wanaitika Sauti safi sauti kubwa!

John Mwaipopo said...

Nafurahi kupata simulizi hizi. Sie akina pre-dot.com era zinatufurahisha sana story hizi za wakati wa azimio la arusha, hasa tunaopenda kujua nini kilikuwako huko.

Anonymous said...

heheh dada hapo umenikumbusha mbali nakumbuka mtangazaji wa phillips redio club alikuwa julius nyaisanga kipindi fulani alikuepo mwnamke nimesahau jina lake na kilikuwa kila siku ya jumatano saa mbili na nusu usiku basi bana baba anasema we kalale mie nataka kusikiliza ngoma za kuruka na majoka hapo nilikuwa hatuelewani we acha tu enzi hizo saa mbili. usiku mkubwa sana kwa mwnafunzi enzi zile tulifaidi