Tuesday, December 09, 2008

Ufisadi Marekani - Gavana wa Illinois Akamatwa!

Gavana wa Illinois, Rod Blagojevich

Ni aibu kweli hapa Marekani kusikia kuwa Gavana mzima kakamatwa kwa kuomba rushwa! Yaani ni jambo la aibu sana.

Habari zinasema kuwa Gavana wa Illinois, Rod Blagojevich alikuwa anauza nafasi ya uSenator ambayo iko wazi kwa vile aliyekuwa na kiti hicho, Barack Obama ni rais mteule. Gavana ndiye ana wajibu wa kumteua mtu wa kuchukua nafasi aliyoacha Obama.

Wanasema pia kuwa alikuwa anamtafutia mke wake kazi nono.

Kwingine, haya ni mambo ya kawaida, lakini kwa Marekani haya makosa ni makubwa kweli kweli. Itabidi ajiuzulu kama wa ushahidi kuwa ni kweli kaomba rushwa!

Kwa habari zaidi someni:

No comments: