Showing posts with label Kahama. Show all posts
Showing posts with label Kahama. Show all posts

Saturday, July 27, 2019

TANZIA - Agnes Kabigi

Wadau, Agnes Kabigi alikuwa rafiki yangu pamoja na mwandishi wa habari mwenzangu.   kweli nina huzuni leo.  Mungu ailiaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

HABARI KUTOKA https://www.habarimtaa.com/2019/07/picha-mwili-wa-agnes-kabigi-waagwa.html
Mwili wa Meneja Mawasiliano wa asasi inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI), Bi. Agnes Kabigi umeagwa leo Jumamosi Mjini Kahama na kusafirishwa kwenda jijini Dar es salaam kwa ajili ya mazishi.

Agnes Kabigi alifariki dunia aliyefariki dunia jana mchana Ijumaa Julai 26,2019 baada kuanguka ghafla wakati akitekeleza majukumu yake akiwa katika Hospitali ya wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Agnes Kabigi ni mwandishi Mwandamizi aliyewahi kufanya kazi katika Magazeti ya Uhuru,Mzalendo na Nipashe na mpaka umauti unamkuta alikuwa anafanya kazi katika shirika la AGPAHI linalojihusisha na mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambalo linafanya kazi zake katika mikoa ya Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Mara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa shirika la AGPAHI,wakati wa kuaga mwili wa marehemu,Mfanyakazi wa AGPAHI mkoa wa Shinyanga,Kasablankhahr Herman amesema mwili wa Agnes utasafirishwa kwa ndege majira ya saa 10 leo jioni kutoka Mwanza hadi Jijini Dar es salaam kwa ajili ya mazishi.

Agnes alizaliwa tarehe Julai 13,1967.
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Agnes Kabigi . Amina

Sunday, November 01, 2015

Harufu ya Urais Ilianzia Kahama

Harufu ya Urais ilianzia Kahama

HADI saa nne za asubuhi ya Oktoba 26 mwaka huu, mgombea wa ya urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, alikuwa anatumia ?mifumo na muundo wa kiprotokali? ya chama hicho tawala.

Lakini mfumo huo wa kiprotokali ulibadilika ghafla wakati msafara wake ulipowasili mjini Kahama, mkoani Shinyanga, ukitokea wilayani Chato ambako mgombea huyo alikwenda kupiga kura yake Oktoba 25, Jumapili iliyopita.

Kwa kawaida wakati wa kampeni Dk. Magufuli alitumia gari la CCM na wakati wote alikaa kiti cha mbele na kuhudumiwa kiulinzi na maofisa wa CCM wakisadiwa pia na maofisa protokali wa chama hicho.

Dk. Magufuli na timu yake ya kampeni waliamua kutumia usafiri wa barabara kurudi jijini Dar es Salaam akitokea Chato badala ya usafiri wa ndege uliozoeleka kwa viongozi wengi wa Tanzania.

Msafara huo uliwasili Kahama majira ya nne asubuhi na kusimama katika hoteli moja iliyoko pembezoni mwa barabara kuu ya Kahama-Shinyanga, kwa lengo la ?kuchimba? dawa.

Baada ya mapumziko hayo mafupi yaliyochukua dakika 10 hivi Raia Mwema lilishuhudia maofisa wa CCM na wale wa Idara ya Usalama wakijadiliana na kabla msafara kuendelea, Dk. Magufuli alibadilishiwa gari na ?kukalishwa? kiti cha nyuma, hali iliyoashiria kuwa kuna mabadiliko katika mfumo wa kiprotokali.

Aidha mfumo wa kuendesha magari ulibadilika, kwa tahadhari huku gari la mgombea huyo likiwekwa kati na kuhakikisha kuwa hakuna gari au kitu chochote kitakachohatarisha usalama wake na ule wa msafara mzima.

Wakati viongozi wa mikoa husika ambako msafara ulipita kuanzia Geita, Shinyanga, Tabora na Singida, walitokeza kumpokea wakiongozwa na makamanda wa polisi wa mikoa hiyo.

Moja wa maofisa wa juu wa CCM aliliambia Raia Mwema kuwa wamefikia uamuzi wa kubadilisha mfumo huo na kumkabidhi Dk. Magufuli kwa timu maalumu ya maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa, baada ya kupokea maelekezo kutoka ngazi juu.

Tumepokea maelekezo kutoka juu tubadilishe utaratibu na sisi ni wajibu kutekeleza amri,alieleza ofisa huyo bila ya kufafanua zaidi.

Kuna kila dalili kuwa kwa taarifa za matokeo ya awali, ushindi kwa CCM unanukia na tumeongoza katika baadhi ya mikoa na majimbo hivyo jukumu la ulinzi sasa tunaliacha kwa timu maalumu ya watu wa Idara,? alieleza ofisa mwingine.

Msafara wa Dk. Magufuli ulipumzika juzi, Jumatatu, mjini Dodoma na uliendelea na safari ya kurudi Dar es Salaam kwa njia hiyo hiyo ya barabara, kusubiri matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo wa kihistoria nchini.


CHANZO - RAIA MWEMA

Tuesday, July 09, 2013

Ofisi ya Ardhi Kahama Kuna Nini?

Nimepokea kwa Email: OFISI YA ARDHI KAHAMA KUNA NINI? Ndugu zangu,ninaomba mnisaidie kupata majibu sahihi kwa wanaohusika na suala hili. Mimi ni mwanchi wa Wilaya ya Kahama mtaka mabadiliko na maendeleo binafsi pamoja na Taifa zima.Mwezi wa tisa mwaka jana nilipeleka maombi yangu ya kuomba Hati milki ya kiwanja changu katika ofisi ya wilaya ya kahama.Wahusika wa ofisi hiyo walishughulikia suala hilo hadi kufikia mwisho wa upatikanaji wa Hati Milki.Baada tu ya kufikia mwisho wa hatua hiyo,kikajitokeza kizingiti cha mtu mmoja kuhitajika kuweka sahihi ya nyaraka hiyo ili baada ya hapo ipelekwe kwa Kamishna wa Kanda ili asaini na kuwa tayari Kabla haijasainiwa na Kamishna wa Kanda kuna mtu mmoja anaitwa Afisa Ardhi Mteule.Afisa mteule wilayani Kahama alishasimamishwa toka mwaka jana kwa matatizo yake yeye na waajiri wake na sikumbuki ni mwezi gani.Lakini cha Kusikitisha toka mwaka jana ofisi hiyo iko wazi hakuna mtu aliyewekwa hapo ili aweze kusaini nyaraka za wananchi wa Kahama.Kwa masikitiko makubwa ofisi hiyo haina hata kibali cha kuweka kaimu wa kukaimu kiti chake.Na kwa masikitiko zaidi mtu huyo mdogo hawezi kuteuliwa na mtu yeyote isipokuwa ngazi za juu sana. Huku chin yuko mwananchi ambaye alishafanya hatua zote za nyaraka zake pamoja na malipo ambayo tayari serikali ilishapokea na hata kutumia hela hizo kwa shughuli za serikali mimi mwananchi na mvuja jasho nyaraka zangu bado zimo ofisini kwa kisa cha kwamba Afisa Mteule hajateuliwa na wakubwa.Yanapofanyika haya,wapo tu watu mhimu kama vile Afisa Ardhi wilaya,Mkurugenzi,Mkuu wa Wilaya na hata kamishna wa Kanda kwa nini wasiteue mtu wa kuhudumia wananchi?Mimi ninajua yuko hapo kwa kusudi moja tu ni kuhudumia wananchi. Ukipata nafasi ya kuuliza jibu ni moja tu kuwa mtu huyo hajateuliwa,Je leo ni mwaka,atateuliwa lini ili huyo mwananchi naye apate nafasi ya kufanya maendeleo yake?jibu utapata kuwa hatujui,tunasubiri.Wakati huohuo serikali inahimiza maendeleo,bado serikali hiyo hiyo inazuia watu wasifanye maendeleo kwa kitendo cha dakika 10 tu mtu anakaa kwenye ofisi hiyo na anasaini kila kitu kwa siku moja lakini cha ajabu sahihi moja kwenye nyaraka unaingoja mwaka.Ndugu zangu wanamabadiliko hii ni kweli na sahihi kweli?Kwa picha hii inaonyesha wakubwa wana maslahi yao binafsi katika suala hili,maana kusingekuwa na maslahi,wakubwa wasingenyamaza katika suala hili kwa mwaka mzima huku mwananchi anaendelea kuumizwa.Au katika suala hili serikali iko wapi hapa?Kwa nini serikali inyamaze wakati mwananchi ametoa hela yake?Je sisi wananchi wa chini tukamuulize nani? Je nini kifanyike ili huyyo Afisa Ardhi Mteule Kahama ateuliwe ili wananchi waeze kupewa haki zao?Kama mimi nimmoja je wangapi wananchi wanaolia nyaraka zao hazijasainiwa kwa mwaka mzima? Je wakubwa hawalijui hili?na kama wanalijua kwa nini wako kimya kama kweli hawana maslahi katika hili? Ninaomba nipelekewe malalamiko na nipatiwe majibu toka kwa watu wafuatao; Mbunge wa Kahama mjini Waziri wa Ardhi na makazi. Naibu waziri wa Ardhi Kamishna wa Ardhi makao makuu Dar. Niwakilisha.

Saturday, December 10, 2011

Barrick Gold Mines Wakwepa Kulipa Kodi!


IMEBAINIKA kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama imepoteza mapato zaidi ya sh milioni 300 kutokana na kampuni 30 zinazofanya kazi migodi ya Kampuni ya African Barrick Gold Mines LTD kukwepa kulipa
ushuru wa huduma za jamii.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Biashara wa Wilaya ya Kahama, Boniphace Bulali, alipokuwa akitoa
ufafanuzi juu ya msako mkali wa kuzisaka kampuni hizo katika migodi hiyo unaofanywa
na wakala wa kukusanya madeni ya halmashauri hiyo, Mustered Seed International LTD.

Bulali alisema kampuni hizo zimekwepa kulipa ushuru unaopaswa kulipwa wa huduma za jamii kwa kipindi cha miaka mitatu, hali ambayo imezorotesha mapato ya halmashauri na kushindwa kufikia baadhi ya malengo yake katika kuleta maendeleo stahiki kwa wakati wilayani humo.

Alisema katika msako huo tayari baadhi ya kampuni zimekiri kushindwa kulipa fedha hizo kwa madai
jukumu hilo hufanywa na makao makuu ya ofisi zao zilizopo Dar es Salaam kinyume cha utaratibu
wa sheria ndogo za halmashauri zinazoeleza kulipa ushuru huo kwenye eneo wanalofanyia kazi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mustered Seed International LTD ambayo ni wakala wa kukusanya madeni hayo, Zacharia Soko, alisema kuna kampuni 15 zinazofanya kazi katika mgodi wa
Buzwagi pekee ambazo hazijapata kulipa ushuru huo kwenye halmashauri hiyo tangu zianze
kuwajibika katika mgodi huo.

Soko alisema pia kuna kampuni 15 katika Mgodi wa Bulyanhulu ulio kilometa 74 kutoka Kahama
mjini ambazo nazo zimebainika hazijalipa ushuru huo na tayari katika msako huo baadhi ya mali zake
zikiwamo magari yanashikiliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kahama.

Chanzo: Tanzaniadaima

Wednesday, December 29, 2010

Mwandishi wa Habari Apigwa Kahama

Natoa pole kwa Kaka Ali Lityawi. Hao polisi wanastahili kuadhibiwa. Kutokana na maelezo sioni kama Ali alifanya kosa. Hao polisi wangefurahi kuwa wanapigwa picha wakiwa wanafanya kazi yao kama ilivyotakiwa.

******************************************************

Kahama Police Beat Up Journalist, Seize His Camera
By The guardian reporter
29th December 2010

A group of police officers whose identities and force numbers could not be immediately established last weekend beat up Tanzania Daima newspaper journalist Ali Lityawi, and seized his camera allegedly for taking pictures without permission.

The police said the newsman was 'punished' for taking pictures of a police officer on duty while chasing a prisoner, who had apparently escaped from custody.

The incident took place on Sunday at Lumelezi near Magai hospital, where the journalist, who was on the beat looking for news, found a police officer running after a prisoner.

According to Lityawi, the police officers saw him taking pictures of his colleague, whereupon they attacked him before seizing his camera.

Later, he was taken to the central police station where he was remanded in custody by Kahama Officer Commanding District George Simba on allegation of taking photographs of a police officer and a suspect without a permit.

“The district police chief ordered that the photos in my camera be deleted and ordered his assistants to remove from the camera the smartcard used to store pictures,” he said.

When reached for comment about the incident, Shinyanga regional police commander Diwani Athumani condemned the action by the police officers and ordered repair of the camera, which the journalist claimed was damaged in the fracas.

“It is a police force’s policy to collaborate with journalists to educate the public on public safety and security. If they (police officers) thought the pictures were not good enough, they should have advised the reporter not to use them instead of beating him up and deleting them,” he said.