Showing posts with label Morogoro. Show all posts
Showing posts with label Morogoro. Show all posts

Saturday, August 10, 2019

Uchu wa Mafuta yaua watu zaidi ya 70 Morogoro - Ajali ya Lori la Mafuta

Jamani wadau, mkiona  mafuta yanavuja kutoka kwenye gari kimbia, siyo mnakimbilia kupata mafuta dezo!  Yanawaka kwa kirahisi mno. Umaskini kitu kibaya sana, maana si ajabu wengine waldihani watuuza hayo mafuta wapate hela ya ugali!   Ona sasa watu zaidi ya  sabini wamepoteza maisha baada yakuungunguzwa! 

Wengine waliokufa ni madereva wa bodaboda na mama nitilie!  Walizoa mafuta hata kwenye ndoo! Na wanasema, mafuta yalilipuka baada ya mtu kuchomoa  betri 
ya lori  na mtu mwingine alikuwa anavuta sigara!   Nasikia huyo mvuta sigara aliambiwa asivute karibu na mafuta.  Alijibu mafuta ya kisasa hayawezi kuwaka moto! Nadhani watakuwemo kwenye watu waliokufa!
Mungu alaze roho za waliokufa mahala pema mbinguni. Amen.


Kutoka Associated Press
DAR ES SALAAM, Tanzania (AP) — A damaged tanker truck exploded in eastern Tanzania as people were trying to siphon fuel out of it Saturday, killing at least 62 in one of the worst incidents of its kind in the East African country.
Tanzanian state broadcaster TBC, citing police figures, said at least 70 more people were injured during the explosion in the town of Morogoro, located about 120 miles (200 kilometers) from the economic hub of Dar es Salaam.
Regional police commissioner Steven Kabwe told the local Azam TV that many suffered serious burns.
Witnesses told The Associated Press that a crowd had gathered around the fuel tanker after it was involved in an accident early Saturday and some people were trying to siphon away fuel when the truck burst into flames.
Video footage posted on social media showed people collecting fuel into jerry cans before the fire incident.
In a statement expressing condolences, Tanzanian President John Magufuli said he was dismayed people attacked vehicles involved in accidents instead of offering help.
Residents are routinely killed by explosions while stealing fuel from incapacitated tankers in East Africa. Those who steal the fuel usually hope to be able to sell it cheaply to motorists.
In 2013, at least 29 people were killed on the outskirts of the Ugandan capital, Kampala, as scores swarmed around the scene of an accident.
There is limited awareness about the danger of explosions of damaged fuel tankers, said Henry Bantu, a road safety expert who runs the Tanzania-based Safe Speed Foundation. Local leaders need to do more to educate people on the risks, he said.



Watazamaji kwenye shemu ya mlipuko Morogoro

Friday, July 28, 2017

Tigo Imechangia Kisima kwa wakaazi wa Mji Mpya mkoani Morogoro



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akikata utepe kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Meneja wa huduma za jamii Tigo, Halima Okash, Ofisa Mkuu wa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jérôme Albou,  na  Diwani wa mji mpya Wence Kalogelezi

Mkazi wa Mji mpya akiwa kabeba ndoo ya maji mara baada ya uzinduzi wa kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.




Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akihutubia wakazi wa Mji mpya mara baada ya  kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo akiwa katika picha ya pamoja  na Wakazi wa Mji Mpya Mkoani Morogoro mara baada ya uzinduzi w kisima hicho.

 kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.


·        Uchangiaji huu ni ishara ya shukurani kwa wakaazi hao kwa kuzima moto katika kituo cha data cha Tigo.

Tarehe 27 Julai 2017 – Tigo Tanzania imechangia kisima chenye thamani ya TZS milioni 17 kwa hosipitali ya Mji Mpya na maeneo yanayoizunguka katika mkoa wa Morogoro kama mkono wa shukurani kwa wakaazi kwa kuhatarisha maisha yao wakati wakipambana na moto ambao ulilipuka katika kituo cha data cha kampuni katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Tigo, uchimbaji wa kisima hicho pia ulikuwa sambamba na nia ya kampuni hiyo kusaidia ustawi wa jamii ambako Tigo inaendesha  shughuli zake.
Akizungumza katika sherehe za makabidhiano zilizofanyika katika hospitali ya mji mpya katika manispaa ya mji wa Morogoro Afisa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jerome Albou alielezea matarajio yake kwamba kisima hicho kitawafikisha mbali sana katika kuondoa suala la upungufu wa maji katika hospitali na pia kutoa maji safi na salama ya uhakika kwa jamii inayokizunguka.
“Tunawashukuru sana watu wa Mji Mpya kwa kuonesha kujali na kujitoa wakati wa kupambana na moto ambao karibu uteketeze kabisa kituo cha Data mapema mwaka huu. Kweli Tigo ina deni kwa wanajamii, serikali ya mtaa na viongozi wa ulinzi na usalama wa manispaa kwa kuitika  kwa wakati kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu mkubwa unasababishwa wakati wa moto,” alisema Albou.   
“Kwa hiyo msaada huu, unakuja kutimiza ahadi walioiweka Tigo kwa wakazi wa Mji mwema wa kuwapatia maji safi na salama kama namna ya kutambua juhudi zao katika kulinda mali za kituo hicho cha data.”
Albou alibainisha kwamba uchangiaji huo unakamilisha idadi ya vijiji 20 ambavyo vimenufaika kutokana na jitihada za Tigo za kutoa maji safi na salama nchi nzima, ikiwa inawasaidia zaidi ya watu 187,000.
Mwaka huu, Tigo ina mpango wa kuchimba visima zaidi katika maeneo yanayohitaji ambayo zaidi ya watu 350,000 wanatarajiwa kunufaika katika jitihada zetu za kusaidia juhudi za serikali za kuondoa upungufu wa maji safi na salama nchini.
Makabidhiano yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Stephen Kebwa ambaye aliishukuru Tigo kwa kufikiria kutoa msaada huo. Alisema kwamba kisima hicho kitasaidia utoaji wa huduma bora za kiafya katika hospitali ya Mji Mwema na kusaidia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Aliwaomba wasamaria wema wengine kujitokeza na kuunga mkono juhudi za kuondoa upungufu wa maji katika mkoa huo.
Tunapenda kuishukuru Tigo kwa kutusaidia katika juhudi zetu za kutoa huduma za kiafya za uhakika katika eneo hili kwa kutatua tatizo lililokuwepo la upungufu wa maji. Tunaamini kwamba upatikanaji wa maji safi na salama karibu na wakaazi pia itaongeza uzalishaji wa kiuchumi hasa kwa wasichana na wanawake ambao hawatakuwa wanapoteza muda mwingi wa kutafuta maji safi na salama sehemu zingine. Hii itawapatia wasichana fursa ya kuhudhuria masomo kwa uhuru na kuipa jamii fursa ya kuhudhuria kwa ufanisi katika shughuli zao za maendeleo ya Taifa,  Alisema Dr Kebwe. 

Monday, September 07, 2015

Rais Kikwete Awapa Pole Majeruhi wa Msongamano

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Morogoro Dkt. Ritha Lyamuya alipokwenda kuwapa pole majeruhi walioumia katika msongamano mkubwa uliotokea katika mlango wa kutokea nje baada ya mkutano wa kampeni wa CCM katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro jana Septemba 6, 2015. Watu wawili walipoteza maisha, akiwemo mvulana wa miaka 12 aliyejulikana kwa jina la Ramadhani Abdallah na mwanamama Grace George (42), ambapo jumla ya watu 17 walijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini hapo. Hadi jioni hii majeruhi saba walikuwa wameruhusiwa
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Kaimu Mganga Mku wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro Dkt. Samson Tarimo alipokwenda kuwapa pole majeruhi walioumia katika mlango wa kutokea nje baada ya mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro jana Septemba 6, 2015.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mweka Hazina wa CCM mkoa wa Morogoro Ndg. Hassan BAntu alipokwenda kuwapa pole majeruhi walioumia katika mlango wa kutokea nje baada ya mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro jana Septemba 6, 2015.
 Mmoja wa majeruhi Bw. Kokoliko Ramadhani akiwa kitandani pake hospitalini hapo akiuguza bega la kuume aliloumia kwenye msongamano huo
 Rais Kikwete akimpa pole  mmoja wa majeruhi Bw. Kokoliko Ramadhani akiwa kitandani pake hospitalini hapo akiuguza bega la kuume aliloumia kwenye msongamano huo
 Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimpa pole  mmoja wa majeruhi Bi Flora Maduka akiwa kitandani pake hospitalini hapo baad ya kujeruhiwa katika msongamano huo
 Rais Kikwete akimpa pole  mmoja wa majeruhi Bi. Jalia Mohamed akiwa kitandani pake hospitalini hapo akiuguza bega la kuume aliloumia kwenye msongamano huo
 Rais Kikwete akiendelea kutoa pole kwa majeruhi
 "Pole sana...." Rais Kikwete akimfariji mmoja wa majeruhi

 Rais Kikwete alitumia wasaa huo kuwapa pole wagonjwa wengine waliokuwa wamelazwa wodi moja na majeruhi hao. Hapa anamfariji mtoto aliyeungua kwa moto
  Rais Kikwete alitumia wasaa huo kuwapa pole wagonjwa wengine waliokuwa wamelazwa wodi moja na majeruhi hao. Hapa anamfariji mtoto aliyevunjika mguu wakati akicheza kwenye mti
Rais Kikwete akimpa pole mvulana ambaye aligongwa na gari wakati akielekea kumsikiliza mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dkt John Pombe Magufuli katika mkutano wa kampeni Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro jana 
Rais Kikwete alipata fursa ya kutembelea wodi ya watoto na kuwapa pole kwa kuumwa kwao
Rais Kikwete akiongea na wanafunzi waliokuwepo hospitalini hapo kumtembelea mgonjwa
Rais Kikwete alizongwa na wananchi waliokuwa na hamu ya kuongea naye 
Rais Kikwete akitoa mapendekezo ya kupanua hospitali hiyo ambayo ina eneo kubwa lakini majengo machache ya chini. Alipendekeza uongozi wa hospitali na mkoa ubuni namna ya kuipanua kwa kujenga majengo ya ghorofa ili kuwepo na wodi na sehemu nyingi zaidi za huduma.
Mwishoni Rais Kikwete aliongea na wanahabari wa kutoka vyombo mbalimbali na kueleza masikitiko yake kwa yaliyotokea jana Uwanja wa Jamhuri baada ya mkutano wa kampeni kumalizika.
Rais Jakaya Kikwete akiongea na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Morogoro Dkt. Ritha Lyamuya baada ya kuwajulia hali majeruhi wa msongamano baada ya mkutano wa kampeni uwanja wa Jamhuri Morogoro jana. PICHA NA IKULU

Saturday, July 12, 2014

Mkutano wa Injili Mijini Morogoro Na Pastor Daniel Moses Kulola

Pastor Daniel Moses Kulola anamaliza Mkutano wa Injili, huko Chamwino, Morogoro.



Kutembelea Blogu ya Pastor Daniel Moses Kulola BOFYA HAPA:

Masanja Mkandamizaji in the House

 
Hata waimbaji Kutoka China walishiriki

Saturday, August 10, 2013

Muda Mfupi Kabla ya Sheikh Ponda Kupigwa Risasi


 Kutoka Jukwaa Huru.com

Huku taarifa ambazo zinaendelea kusambaa zikiwa zinadai kuwa Sheikh Ponda amepigwa risasi na Polisi, na huku Jeshi la Polisi likikanusha kuhusika na tukio hili, likieleza kuwa halikuhusika na wala halijui aliko mwanaharakati huyo wa Uislamu, hapa ni picha za kinachoelezwa kuwa kilitokea kabla ya tukio la Ponda kupigwa risasi (kama ni kweli amepigwa risasi) 

Picha hizi ni kutoka blog ya Google Habari, na zimeambatana na maelezo yaliyo chini yake: 




Leo kwenye kongamano la kuita umoja wa waislam katika yanayo wakabili waislam mkoani Morogoro.
Kongamano lillienda vizuri likiwa limepambwa na mashekh wakubwa wakubwa kama vile Riko, Mwaipopo, Kondo pamoja na shekh Ponda.
Shekh ponda alikuwa wa mwisho kutoa mawaidha na aliaga waislam ili aweze kuelekea Msikiti wa Mungu mmoja hivyo waislam walitaka kumsindikiza Shekh Ponda mpaka Mskiti wa mungu mmoja.
Maaskari waliovalia nguo za Field Force wakiwa kwenye defender waliingia na kuanza kuifuata gari kwa nyuma. 
Waislam waliendelea kuizunguka gari ya Shekh Ponda ila maaskari walianza kupiga mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi kisha kuifukuza gari ya sheikh Ponda.
Sikubahatika kushuhudia nini kiliendelea kutokana na mabomu ya machozi yaliyopigwa na maaskari hao lakini dakika chache baadae nilipata taarifa ya kwamba amepigwa risasi ya bega na amepelekwa hospitalini…..endelea kutembelea blog ili ujue nini kinaendelea kwa Shekh Issa Ponda amabae inasemekana yupo Hospitali tayari kupata tiba.

Sheikh Ponda ApIgwa Risasi Na Polisi Morogoro!

Sheikh Ponda Issa Ponda


Mda kama dakika 20 zilizopita  mjini Morogoro shehe Ponda amepigwa risasi na polisi .
Inasemekana pengine umauti umemkuta .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo
akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano
kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye
alikuwa hayupo .

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi za kutosha.

 UPDATE:

Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.


Chanzo: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/502527-sheikh-ponda-ajeruhiwa-vibaya-baada-ya-kupigwa-risasi-kwenye-mhadhara.html#post7045479

*************************************************

 From All Africa.Com

Tanzania: DPP Directs Arrest of Sheikh Ponda for Disobeying Order


Sheikh Ponda was in May, convicted of forcible entry into a plot by the Kisutu Resident Magistrate's Court in Dar es Salaam. He was given a oneyear suspended jail term and directed to refrain from taking part in incitement activities likely to lead to breach of the peace in the country.
Dr Feleshi noted that recent reports have it that the cleric is engaged in organising religious gatherings in Zanzibar, which threatened peace in the Isles. "Such a behaviour is intolerable," the DPP said in an interview with the 'Daily News' on Wednesday.
He added: "We hope the police will exercise their powers wisely to arrest Sheikh Ponda and take him to court for penal actions." Dr Feleshi said what Sheikh Ponda was currently doing was contrary to his sentence. "He was convicted of a similar offence, but was still conducting acts that threaten the public order and concord.
This is not acceptable. We cannot let one disobey court orders and go on unpunished," he said. Counsel for Sheikh Ponda Juma Nassoro was not reached for comment on the matter.
Reports from Zanzibar have it that police are tracing Sheikh Ponda's whereabouts. He is alleged to have called on the citizens to initiate strikes against the government. Zanzibar Commissioner of Police, Mussa Ali Mussa was reported to have said that Ponda's statements breached police directives to religious leaders to avoid giving messages which threaten the country's peace.
The police in the Isles arrested five persons who reportedly gave shelter to the controversial Muslim Sheikh. They were interrogated for hosting Ponda.
Sheikh Ponda, according to the police, had requested the believers to be ready to fight for their rights and stressed that they should soldier on.
Adjourning the Zanzibar House of Reps budget session for 2013/2014, the Second Vice-President, Amb. Seif Ali Iddi announced a ban for Sheikh Ponda to set his foot in the Isles for the purpose of inciting the people. Amb. Iddi warned that the government should not be blamed for serious measures that would take against leaders of such calibre

Friday, May 10, 2013

Polisi Kilosa Wakamatwa na Fuvu la Binadamu - Waliitumia kudai Rushwa


Kutoka Gazeti la Mtanzania!

Mei 10, 2013


JESHI la Polisi mkoani Morogoro limeingia kwenye kashfa nzito baada ya askari wake watatu na raia wanne kukamatwa wakiwa na kichwa cha binadamu. Tukio hilo lilitokea Mei 7 mwaka huu katika eneo la Mgudeni- Dumila wilayani Kilosa.

Inaelezwa kuwa polisi hao kwa kushirikiana na raia hao walikwenda nyumbani kwa mfanyabiashara Samson Mura na kutaka kumbambikizia kesi ya mauaji.

Mbali ya kubambikizia kesi hiyo, polisi hao wanadaiwa kuomba wapewe Sh milioni 25 na mfanyabiashara huyo ili wasimpeleke kituoni.

Wakizungumza na MTANZANIA jana, baadhi ya wananchi walisema wameshangazwa na askari hao ambao wawili ni wa Kituo cha Polisi Dumila na mmoja wa Kituo cha Polisi Mvomero.

Walisema siku ya tukio, polisi hao walifuatana na raia mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kwa ajili ya masuala ya usalama.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mgudeni,Zaituni Kifutu alisema walishangazwa na tukio hilo.

“Tumeshangazwa mno na askari hawa… sijui walichukulia wapi mafunzo yao? Kama walibaini kuwapo tukio hili kwa nini hawakutaka kulifikisha kituoni?

“Inasikitisha mno, eti wao kwa kushirikiana na mfanyabiashara wanakwenda kudai kwa mwanakijiji mwenzetu wapewe Sh milioni 25… haiingi akilini hata kidogo wakamate mhalifu halafu washirikiane kwenda kuomba fedha.

“Tunaona na mazingira ambayo askari na raia huyo ambao walifika kwenye nyumba ya mfanyabiashara huyo, Samson Mura na kumtuhumu kukutwa na kichwa hicho si mazuri ni ya kutaka kumbambikizia kesi tu. Yaani inasikitisha jeshi kujaa uozo kiasi hiki,”alisema Kifutu.

Naye Musa Magisu alisema polisi hao walifika kwenye nyumba ya Mura na kufanya upekuzi ambao hata hivyo hawakuambulia kitu.

“Pamoja na kupekua kwa nguvu kubwa, hawakukuta kitu. Sisi tunamfahamu Mura ana silaha yake ambayo anamiliki kisheria,”alisema.

Alisema baada ya polisi hao kutoka nje ya nyumba walikwenda moja kwa moja kwenye gari lililokuwa limeegeshwa nje ya nyumba.

“Baada ya kufika kwenye gari, yule raia na wale polisi waliona kuna mfuko wa rambo chini na ghafla wakaanza kuuliza eti mfuko huu una nini na walipofungua wakakuta kuna kichwa cha binadamu.

“Yaani baada ya kukuta kichwa kile, walimuamuru mfanyabiashara yule atoe Sh milioni 25 lakini alikataa katakata akidai hajawahi kufanya tukio la aina hiyo,”alisema.

Alisema mpaka sasa hawajui kwa nini polisi ambao ni walinzi wa raia na mali zao, wamegeuka watu wa kumbambikizia kesi wananchi wasio na hatia.

Ofisa Upelelezi Msaidizi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Morogoro, Asifiwe Ulime alikiri kutokea tukio hilo na kusema mpaka sasa polisi hao wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.

Alisema hata yeye mwenyewe, alifika eneo la tukio na kushuhudia fuvu.

“Tunawashikilia polisi watatu na mwananchi mmoja kwa mahojiano ili watoe maelelezo ya kina juu ya tukio hili,”alisema.

Kutokana na hali hiyo, Ulime amewaomba wananchi wa Dumila kuwa watulivu wakati uchunguzi unaendelea.

Thursday, March 14, 2013

Rais Kikwete Afungua Rasmi Jengo la Kitivo Cha Sayansi MUM

HOTUBA YA MHESHIMIWA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA UFUNGUZI RASMI WA JENGO LA KITIVO CHA SAYANSI KATIKA CHUO KIKUU CHA WAISLAMU CHA MOROGORO (MUM),


TAREHE 14 MACHI, 2013, MOROGORO

Mzee Kitwana Suleiman Kondo, Mwenyekiti wa Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu (MDF);
Mheshimiwa Joel Bendera, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro;
Mama Mwantumu Malale, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro;
Profesa Hamza Mustafa Njozi, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro;
Viongozi mbalimbali wa Serikali, vyama vya siasa na Jumuiya mliohudhuria;

Wageni waalikwa;

Mabibi na Mabwana;

Niruhusuni niungane na wenzangu walionitangulia kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kukutana hapa. Nakushukuru sana Mama Mwantumu Malale, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro na viongozi wenzako kwa kunialika kuja kujumuika nanyi katika siku hii adhimu ya ufunguzi wa jengo la Kitivo cha Sayansi katika Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro. Mmenipa heshima kubwa ya kuwa sehemu ya historia ya Chuo hiki. Kwa kweli, nimefarijika sana kuona Chuo chetu kinazidi kupata mafanikio ya kutia moyo hasa ukizingatia ukweli kwamba kina muda mfupi tu tangu kuanzishwa kwake.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Natoa pongezi nyingi kwako, Makamu Mkuu wa Chuo na wale wote walioshiriki kubuni wazo la kuwa na jengo la Kitivo cha Sayansi na kufanikisha ujenzi wake. Juhudi zao na moyo wao wa kupenda maendeleo ndio umetufanya sisi kujumuika hapa leo kushuhudia mafanikio haya. Hakika ni jambo la kujivunia. Pia, nawapongeza sana Wajenzi na Mhandisi Mshauri kwa kazi nzuri waliyofanya ya ujenzi wa jengo hili. Sote tunaliona jengo lilivyojengwa vizuri na kwa namna yake linapendezesha mandhari ya Chuo.

Kwa namna ya pekee napenda kwa niaba yenu nitoe shukrani zangu za moyoni kwa taasisi ya Al-Barakah kwa kufadhili ujenzi wa jengo hili. Asanteni sana kwa ukarimu wenu na upendo mkubwa mliouonesha kwa nchi yetu na watu wake. Naomba taasisi nyingine na watu binafsi waige mfano huu mzuri wa kusaidia miradi mbalimbali inayonufaisha jamii. Tukumbuke ule msemo wa wahenga kuwa “kutoa ni moyo, usambe si utajiri”.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Mabibi na Mabwana;

Kwa miaka mingi madhehebu ya dini na mashirika ya dini yamekuwa washirika muhimu sana wa Serikali katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yetu. Yamekuwa yanajihusisha na kutoa huduma kwa jamii kama vile afya, elimu na nyinginezo. Kwa ajili hiyo watu wengi sana nchini wamenufaika na wanaendelea kunufaika na huduma zinazotolewa na mashirika ya dini.

Kwa miaka mingi mashirika na taasisi za madhehebu ya dini ya Kikristo ndiyo yaliyokuwa yakionekana kutoa huduma hizo. Kwa upande wa Waislamu, ukiacha Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan, mchango umekuwa mdogo sana. Ni jambo la faraja kubwa kuona Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu (MDF) ikionyesha njia. Kwa kumiliki na kuendesha Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kwa ufanisi, MDF inatoa mchango muhimu katika kuendeleza elimu ya juu na maendeleo nchini. Idadi kubwa ya wanafunzi waliofuzu masomo yao na waliopo katika Chuo hiki tangu kilipoanzishwa mwaka 2005 ni ushahidi tosha wa kazi nzuri inayofanywa na MDF. Hongereni sana. Tunawaombea kwa Mola mpate mafanikio makubwa zaidi miaka ya usoni kwa upande wa elimu na huduma nyingine muhimu.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Katika kipindi cha miaka saba sasa, Serikali yetu imeongeza sana uwekezaji katika upanuzi wa elimu tangu ya awali hadi elimu ya juu. Tumeamua kufanya hivyo kwa sababu vijana wengi waliokuwa wanastahili kupata elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi na elimu ya juu walikuwa hawapati. Tanzania ni kubwa kuliko Kenya na Uganda kwa eneo na idadi ya watu lakini ndiyo tuliokuwa na idadi ndogo ya wanafunzi kwa ngazi zote hizo. Kwa mfano, mwaka 2005 idadi ya wanafunzi waliokuwa Chuo Kikuu nchini Kenya ilikuwa 108,407, Uganda 88,360 na kwa baadhi ya nchi za SADC kama vile Afrika Kusini idadi hiyo ilikuwa 717,973. Wakati wenzetu wakiwa na idadi hiyo, sisi tulikuwa na wanafunzi 40,719 tu katika vyuo vikuu nchini. Hali ilikuwa hivyo pia kwa elimu ya sekondari. Kenya ilikuwa na wanafunzi 925,341, Uganda 619,519 na Afrika Kusini 4,186,882 wakati Tanzania ilikuwa na wanafunzi 524,325 tu waliokuwa katika shule za sekondari.

Tuliona hali hii haikubaliki hivyo tukaamua hatuwezi kuiacha iendelee. Tukaamua kudhibiti. Tukachukua hatua tulizochukua za kupanua elimu katika ngazi zote. Matokeo ya uamuzi huo ni kwamba vijana wanaopata fursa ya kupata elimu katika ngazi zote wamekuwa wengi kuliko wakati mwingine wo wote katika historia ya nchi yetu, tumewafikia na kuwapita majirani zetu. Kazi kubwa tunayoendelea nayo sasa ni kuwekeza katika kuimarisha ubora wa elimu waipatayo vijana wetu kwa kuongeza walimu, vifaa vya kufundishia, vitabu na huduma nyinginezo. Inshallah hata kwa dhamira yetu, hii njema Mola atatuwezesha. Mwanzo mgumu lakini hatma itakuwa nzuri.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Kufuatia juhudi hizo, idadi ya wanafunzi waliopo kwenye vyuo vikuu nchini imeongezeka sana, kutoka wanafunzi 40,719 mwaka 2005 hadi wanafunzi 166,484 mwaka 2012. Kwa upande wa sekondari mwaka 2011 tulikuwa na wanafunzi milioni 1.79 na wenzetu wa Kenya walikuwa na wanafunzi milioni 1.77. Haya ni mafanikio makubwa.

Serikali itaendelea kuwekeza kwenye upanuzi wa fursa za elimu na ubora wake. Hata hivyo ushiriki wa wadau wengine kuunga mkono juhudi za serikali ni jambo muhimu sana. Tumeweka mazingira mazuri kwa wadau hao kufanya hivyo na mafanikio yanaonekana wazi. Kama nilivyokwishasema awali, mashirika ya dini yamekuwa wadau wa kutumainiwa na mchango wao uko wazi. Unajieleza wenyewe. Kwa mfano, katika vyuo vikuu 49 vilivyopo nchini, vinavyomilikiwa na umma ni 14 tu. Vyuo vikuu 24 vinamilikiwa na mashirika ya dini na 11 na sekta binafsi.





Ndugu Mkuu wa Chuo;

Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa na muhimu unaotolewa na vyuo vikuu vinavyomilikiwa na mashirika ya dini na sekta binafsi. Ninyi mmekuwa washirika wazuri na wa uhakika katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya elimu katika nchi yetu. Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono na kushirikiana nanyi ili kuwawezesha vijana na Watanzania wengi zaidi waweze kupata elimu. Uamuzi wa kufanya utaratibu wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu uhusishe wanafunzi wa vyuo visivyokuwa vya umma ni moja ya mambo mengi muhimu yanayofanywa na Serikali kuthibitisha usemi wangu huo.

Tulipoingia madarakani mwaka 2005 tulifanya mambo mawili muhimu kuhusu mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Kwanza uamuzi kwamba, mikopo itolewe kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma na vile visivyokuwa vya serikali. Kabla ya hapo ilihusu vyuo vya umma pekee. Pili kwamba, kila mwaka tuongeze fedha zinazotengwa kwa ajili ya Mfuko huo ili idadi ya wanafunzi wanaonufaika iongezeke. Tulikuta Mfuko ukiwa na shillingi billioni 56.1 unanufaisha wanafunzi 16,345 mwaka 2005. Tukaongeza kila mwaka na katika mwaka huu wa fedha (2012/13) tumetenga shillingi bilioni 345 zinazowanufaisha wanafunzi 98,772.

Tutaendelea kuongeza fedha katika Mfuko huo ili wanafunzi wengi zaidi wanufaike na hata ifikie siku moja tuweze kuwakopesha wote bila ya kujali sifa ya uwezo wa wazazi au walezi kulipa ada. Kwa kasi tuliyonayo na kwa jinsi tunavyozidi kufanikiwa katika kukusanya mapato ya serikali, naamini miaka michache ijayo tunaweza kufikia lengo hilo. Nawasihi Bodi ya Mikopo iwekeze katika kuimarisha uwezo wa kuwafuatilia waliokopeshwa kulipa mikopo waliyopewa. Matamanio yangu ni kuwa fedha zilizotolewa zizunguke ili tupunguze kiasi kinachotolewa na bajeti ya serikali kila mwaka.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Mabibi na Mabwana;

Niruhusuni nitumie nafasi hii kukupongeza wewe Mkuu wa Chuo, Makamu Mkuu wa Chuo, Wahadhiri na Jumuiya nzima ya Chuo Kikuu hiki kwa kazi kubwa na nzuri muifanyayo ya kuendeleza na kuboresha Chuo. Tumeshuhudia ujenzi wa jengo nililolifungua leo. Tumeona mafanikio kwa upande wa ongezeko la idadi ya wanafunzi, walimu, wafanyakazi na fani zinazofundishwa katika kipindi hiki kifupi cha uhai wa Chuo hiki.

Nimefurahishwa na kufarijika sana kusikia kuwa ubora wa elimu inayotolewa hapa chuoni ni jambo linalopewa kipaumbele cha kwanza. Jambo hili ni muhimu sana kulisisitiza kwani tunataka wahitimu wa Chuo hiki wafanane na wahitimu wa Chuo chochote kizuri nchini na hata duniani. Ningependa kuona wahitimu wa Chuo hiki wanagombewa katika soko la ajira. Hili ni jambo linalowezekana. Kinachotakiwa ni uamuzi wa Baraza na Seneti kuwa iwe hivyo na kuchukua hatua zipasazo. Sina shaka kuwa mnaweza kufanya hivyo. Hakika mnaweza, na sote kwa umoja wetu tunaweza.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Nimefurahi sana, pia, kusikia kuwa Chuo kinatoa mafunzo ya ualimu. Bila ya shaka mnaelewa kwa nini nafurahi. Tuna uhaba mkubwa wa walimu nchini hivyo Chuo cho chote kinachotoa mafunzo ya ualimu hunifurahisha. Endeleeni kuimarisha mafunzo hayo ili Chuo chenu kitambulike na kukubalika nchini kwa sifa ya kutoa walimu wazuri. Walimu wa kutoka Chuo hiki wawe wale wanaojua vyema masomo wanayofundisha, mahiri kufundisha na waadilifu. Naomba pia mtoe kipaumbele cha juu kwa mafunzo ya ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati. Mkifanya hivyo, mtakuwa mnatoa mchango mkubwa katika jitihada za kupunguza uhaba wa walimu wa masomo hayo nchini. Naamini kitendo cha kuzindua Jengo la Kitivo cha Sayansi, kilichofanyika muda mfupi uliopita kinatoa matumaini ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kuchangia katika jitihada za kupunguza pengo la walimu wa sayansi nchini.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Nimewasikia mkieleza kwa ufasaha changamoto kubwa na ndogo ambazo Chuo inakabiliana nazo. Nawapongeza kwa dhati, wewe na viongozi wenzako kwa ubunifu wenu na hatua mnazochukua kuzikabili changamoto hizo. Nawaahidi msaada na ushirikiano wangu na wa serikali kwa yale yaliyoko kwenye uwezo wangu na wa serikali katika kutafuta ufumbuzi kwa changamoto zinazowakabili.

Nawapongeza kwa uamuzi wenu wa kutafuta vyuo vikuu rafiki vilivyoko katika nchi mbalimbali duniani mnavyoweza kushirikiana navyo. Endeleeni kufanya hivyo kwani vyuo vikuu vingi duniani hufanya hivyo. Hamtakuwa wa kwanza na wala hamtakuwa mnafanya jambo la kustaajabisha. Mnaweza, mkipenda, kuwaomba Mabalozi wetu waliopo katika nchi mbalimbali duniani wawasaidie. Ni wajibu wao kufanya hivyo kwani kusaidia kusukuma maendeleo ya hapa nchini kutoka huko waliko ndilo jukumu lao la msingi. Vile vile, nimefurahishwa na mipango yenu ya baadaye ya kuwa na matawi katika mikoa mbalimbali nchini. Hongereni kwa uamuzi wenu wa busara. Lazima Chuo kitanuke kwa maana ya kuwa kikubwa zaidi, makao makuu na kwa kuwa na vyuo vishiriki na shule au vitivo sehemu mbalimbali nchini.

Ndugu Mkuu wa Chuo;

Kazi iliyo mbele yenu ni kubwa, hivyo ni vyema kuweka mikakati mizuri na mipango thabiti ya utekelezaji na ufuatiliaji wa dhamira yenu hiyo njema. Rai yangu kwenu ni kuwaomba muwe wabunifu zaidi hasa katika kutafuta vyanzo vingine vya mapato vitakavyosaidia Chuo kujiendesha bila kutegemea ada peke yake. Chuo kiangalie uwezekano wa kufanya shughuli zitakazowaingizia mapato kama vile kufanya shughuli za kutoa ushauri. Pia muangalie uwezekano wa kuwekeza wenyewe kwenye miradi ya kiuchumi au kwa kushirikiana na wawekezaji katika baadhi ya maeneo.

Kuhusu nafasi mbili za ufadhili nilizopewa na Chuo kikuu cha Tun Abdul Razak cha Malaysia, nitafuatilia kujua kilichoendelea na kinachoendelea. Je, nafasi hizo bado zipo? Zikiwepo, nitawasiliana na wahusika waangalie uwezekano wa kuwapeni. Kama zimeshagawiwa basi tusubiri safari ijayo. Kwa masuala ya ardhi na maombi mengine nimeyasikia, yaleteni tuangalie namna ya kusaidiana.

Ndugu Makamu Mkuu wa Chuo, na

Wafanyakazi wote wa Chuo cha Waislamu cha Morogoro;

Napenda kuwakumbusha kuwa mnayo dhamana kubwa na wajibu mkubwa na wa kihistoria. Ule ukweli kwamba ni mara ya kwanza kwa Taasisi ya Waislamu wazawa kuwa na Chuo Kikuu inawapeni wajibu maalum wa kuhakikisha Chuo kinafanikiwa. Ni mtihani na changamoto ya aina yake kuthibitisha kuwa Waislamu nao wanaweza kuwa na Chuo kizuri na chenye kutoa elimu ya ubora wa hali ya juu. Kwa sababu hiyo hamna budi kuhakikisha kuwa mna mipango mizuri ya kujenga Chuo cha hadhi na ubora wa hali ya juu. Ihakikishwe kuwa mipango hiyo inatekelezwa kwa ukamilifu.

Aidha jumuiya yote inao wajibu wa kufanya kazi kwa bidii, ubunifu, maarifa na weledi ili dhima hiyo ya Chuo iweze kutimizwa kwa ukamilifu. Timizeni wajibu wenu ipasavyo ili jina la Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro likue haraka. Sifa yake isambae na kuvuma kote nchini. Chuo kifanye vizuri ili wanafunzi waone fahari kuwa wahitimu wa Chuo hiki. Chuo ambacho, wazazi wapende kuleta vijana wao kuja kusoma hapa. Kwa jinsi Mkuu wa Chuo alivyoeleza, mimi nina imani mnaweza, fanyeni kweli.





Ndugu Wanafunzi wa Chuo cha Waislamu cha Morogoro;

Naomba wote muone fahari ya kuwa wanafunzi katika Chuo cha kihistoria hapa nchini. Nawasihi mjitume kwa kadri ya uwezo na vipaji mlivyopewa na Mwenyezi Mungu mfanikishe kile kilichowaleta. Jifunzeni kwa bidii mfaulu vizuri ili mkihitimu muwe kielelezo kizuri cha mafanikio na ubora wa Chuo Kikuu Cha Waislamu cha Morogoro. Muwe Mabalozi na kioo cha ufanisi wa Chuo hiki. Nawasihi mjiepushe na mambo yatakayowapunguzia muda au kuwaondoa katika shughuli ya msingi iliyowaleta hapa ya kujifunza mpate digrii katika fani mliyochagua mwenyewe kuisomea. Vishawishi ni vingi na wapo watu wengi wanaopanga kuwashawishi mtumie muda wenu adhimu kufanya wanayoyataka wao ambayo mkishiriki huwatoa kwenye malengo na kutekeleza yao. Mambo ya dunia ya nje ya Chuo ni mengi huna budi kutambua lipi ufanye na lipi usifanye na kwa wakati gani!

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu ni mtu mzima, si mtoto. Lazima ujue kuwa unawajibika kwa kila unaloamua na kutenda. Amua kuwajibika vizuri. Fikiri kabla ya kutenda, changanua lipi ni lipi kabla ya kufanya uamuzi wa kile unachotaka kufanya. Wakati wote uongozwe na busara na hekima na siyo jazba na ushabiki wa matakwa ya kundi. Kama ni jema fanya na kama si jema usifanye. Kwanza tambua wewe ni nani na uko hapa kwa ajili gani. Lazima ujue kuwa hatma ya yote uko peke yako. Utafaulu au kufeli wewe. Utapata shahada wewe na si mtu mwingine. Hakuna ubia wa kufaulu au kufeli au kiwango cha kufaulu. It will always remain personal. Katika masomo unanufaika wewe. Shirikiana na wengi lakini usisahau kujali maslahi yako. Maslahi ya wengi yasiyojumuisha yako, yahoji vizuri kabla ya kuamua kushiriki au kufanya. Vinginevyo labda kama umeamua kujitoa muhanga, uwe shujaa. Hata kwa hilo, sijui utakuwa shujaa wa nani.

Mabibi na Mabwana;

Kabla ya kumaliza napenda kutambua na kumshukuru Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin Mkapa na viongozi wa MDF kwa juhudi zao za pamoja zilizowezesha Chuo hiki kuwepo. Nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipowashukuru wananchi wanaokizunguka Chuo kwa ujirani mwema na wakazi wa Morogoro kwa ujumla kwa kukipokea vizuri na kuishi na wanajumuiya wa Chuo hiki kwa upendo mkubwa. Naomba muendelee na moyo na ushirikiano huo.

Baada ya kusema hayo, nawashukuru sana kwa kunialika. Nawatakia kila la heri na mafanikio tele.

Asanteni sana kwa kunisikiliza.

Monday, August 27, 2012

Polisi Waua Morogoro Leo!

Marehemu Ally Zona,  alikuwa ni muuza magazeti. Alipigwa risasi kichwani akiwa ameshika magaztei yake!  Hiyo jieraha inaonyesha kuwa marehemu alikuwa anakimbia kutoka kwa polisi. Alipigwa kwa nyuma.


Hapo awali ilielezwa kuwa wakati Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikisitiza kufanya maandamano leo kisha mkutano mkubwa wa hadhara, kuliibuka mvutano baina yake na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, kufuatia Kamanda wake, Faustine Shilogile kupiga marufuku mandamano hayo.

Kamanda Shilogile alieleza sababu za kuzuia maandamano hayo kuwa ni udogo wa barabara za Morogoro na kwamba leo ni siku ya kazi hivyo yanawezesha kusababisha usumbufu kwa wakazi wa mji huo.

Wakati Shilogile akieleza kuzuia maandamano yanayotarajiwa kuanza saa 5 asubuhi, Mkuu wa Operesheni Sangara, Benson Kigaila, alisisitiza kuwa watafanya maandamano kwa kuwa waliskubaliana na Kamanda Shilogile kabla ya kuwageuka.

Kwa mujibu wa Gazeti la Nipashe la 27 August 2012, ilielezwa kuwa Kamanda Shilogile alidai kuruhusu baiskeli na watu kutumia barabara kwa sababu ya mikutano ya Chadema itakuwa ni kuwanyima haki wananchi wengine, na hivyo wataruhusu watu wasiozidi 50 kupita kwa wakati mmoja pasipo kuwa na ishara ya kuonyesha kama wanaelekea katika maandamano.

Pichani ni kijana aliyeelezwa kupigwa risasi kichwani katika tafrani hizo na baadae kupoteza maisha Ametambulishwa kwa jina la Ally Zona, ambae alikuwa ansoma magazeti katika stendi ya Msamvu. Tukio hili lilitokea mapema leo asubuhi kuelekea saa sita mchana wakati Polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi hao wa chadema. Mtoa taarifa anasema Polisi wanadaiwa kutumia risasi za moto pamoja na mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamani hao.

Watu wengine waliojeruhiwa katika tafrani hiyo wameelezwa kuwa ni mwenesha baiskeli Hashim Seif ambae amejeruhiwa kwa risasi mguuni akiwa napita na baiskeli yake na kijana mwingine aliielezwa kuwa ni muuza matunda Frank Valimba ambae amejeruhiwa na risasi tumboni.


KWA HABARI NA PICHA ZAIDI TEMBELEA KIBONGO BONGO BLOG:

********************************
TAMKO KUTOKA TANZANIA JOURNALIST ALLIANCE (TAJOA)


Jumuia ya Waandishi wa Habari Tanzania (Tajoa) inalaani kwa nguvu zote mauaji ya makusudi yaliyofanywa na Jeshi la Polisi leo mjini Morogro. Inashangaza Tanzania sasa inataka kugeuka taifa la polisi wauaji. NI vyema busara, ujuzi na mbinu stahiki zikatumika badala ya kuendelea kuua raia hata wasiokuwa na hatia.

Hebu ona huyu masikini alivyouawa kwa kupigwa risasi kwenye paji lake la uso na kumsab
abishia kifo cha papo hapo. Inaelezwa alikuwa muuza magazeti aliyekuwa kibandani kwake. Sasa tusubiri taaria ya Polisi ambayo huenda ikasema alikuwa amebeba silaha.

Tanzania, tusikubali kuwa taifa la polisi wauaji.

Marafiki wa Tajoa, nini sasa kifanyike kukomesha hali hii ambayo inaonekana kuota mizizi? Toa maoni yako hapa ili nasi tuyapeleke kwa Jeshi la Polisi

— 
Wafuasi wa Chadema wakiwa na maandamao hayo mjini Morogoro


Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya Chadema leo mjini Morogoro

Akina Mama wakikimbia mabomu ya machozi

Thursday, May 31, 2012

Site ya Anayedaiwa Kubakwa Ovyo Queen Butahe Haifunguki!

UPDATE June , 1, 2012  -  I have information regarding Queen's missing brother Walter. He is Queen's half brother. Her mother, the late Sgt. Victoria Kutta, of the Tanzania Police Force was married briefly to his father attorney Banda.  At the the time of her death they were separated. Mr. Banda took his son and left Queen with her maternal family. Mr. Banda is also dead now. Walter is said to be living with an uncle now. As soon as I get his whereabouts I will let you know.

Sgt. Victoria never identified Queen's father. The man listed on Queen's documents as her biological father, Robert Butahe, who is said to be deceased, is actually alive and well and lives in Dar es Salaam, Tanzania.


The justice system in Tanzania can prosecute those who abused Queen. They are waiting for her to say the word to bring her abusers to justice, however all I have spoken with say that they are not aware that any such abuses ever took place. They need Queen to talk to them but she has cut off communication with her Tanzanian family.


Sgt. Kutta/Banda alikuwa anafanya kazi pale kituo cha polisi Msimbazi. 
************************************************************ 
Queen Butahe, Franklin, Massachusetts
Wadau, tangu nimeona ile story ya Queen Butahe, kwenye Fox 25 nilifanya juu chini kujua kama kweli mambo hayo aliodai katokea, yalitokea kweli!  Mimi nilimwumbua yule mbakaji wa watoto Mzee Maumba 1990 na story kama yake ilinigusa sana.  Pia mimi ni mmoja wa waanzilishi wa TAMWA na moja ya kazi yetu ilikuwa kusaidia watoto na wakina mama. Lakini baada ya kusoma website yake, nikajiuliza kama yote ni kweli au chumvi, hamira na pilipili yameongezwa?  Site ya Queen ni Hapa. Ajabu Haifunguki sasa: http://www.queenb.antosca.com/  (Hapo kuna details za waliombaka, kutoa mimba etc.)

Haki ya mungu nilipoona tangazo ya hiyo story kuwa binti kateswa Afrika, nilidhani watasema Congo, nikabaki mdomo wazi waliosema Tanzania!


( Story ilitoka Fox 25 tarehe 10/Mei/2011.  Mnaweza kuona Kideo hapa:


http://www.myfoxboston.com/story/18288735/overcoming-the-odds-and-giving-back )

Kilichonishutua ni kuwa alidai kabakwa na watu wengi sana, ndugu, madereva wa school bus (tena kwa kupokezana), walimu.  Katoa mimba akiwa Primary! Duh, nikasema hivi Tanzania wanaume wetu wamekuaje siku hizi.


Baada ya kuposti taarifa kwenye Blog, Niligundua kuwa huyo binti, alililewa katika familia enye uwezo na waliokuwa wanampenda.
Mjomba wake Queen aliniletea ujumbe na niliongea naye kwa simu. Mjomba alililia kwa hasira na kusema hawezi kukubali Queen achafue jina na familia yake na Tanzania kwa ujumla.

Rev. Gilbert Kutta said...

I am her Family Member Senior Guardian, her Mother's Brother and second to the mother in our Family! Her mother passed away, what a tragedy to our family! She calls herself Queen Butahe? ----- Better the media call her again and get the name of her real Father! You may call me +255766551733! I did contact her when this sad news just came to my notice through the Web! She finally ended up blocking my email to her and said "It is bye bye to you"! She has a mission in mind. I will never allow it to take place the way she has planned by putting to shame my Lovely country TANZANIA and my good family! --- and me in effect! I want her to come out again and say the Truth. I don't brush out all what she said! But we have descent ways to deal with all that took place and not the way it seems her new American Caretaker is using! We do not work on half truth/half false and cooked up stories pitched for gain! I am in contact, and continue to contact all who did that interview to get to know what motivated them to shoot it to the mass! To defame? To what gain? How much did they first make due effort to search for truth? Is it just because a simple girl has come up with a story they see interesting they shoot it to the mass? I have plenty more to say! I have entered this debate because I feel this the only way to seek for cure!

god Bless TANZANIA my mother land! I love you and will protect you!

Please Contact me at rnaioth@yahoo.com. If you can help me clear THIS MESS and help Queen come back to her senses not to defame her Mother, please do!

I need that help!
thank you all-
God bless and keep my daughter safe!
regards to you all-
its me:

Rev. Gilbert Phillip Kutta
rnaioth@yahoo.com
+255766551733
Morogoro, Tanzania!

Mimi nilipeleka habari kwa huyo Mwandishi wa Fox 25,  Maria Stephanos na kumwelezea kuhusu mjomba wake. Maria kimya! Nadhani hatasema kitu, si mnajua jinsi hao waandishi wanvyojaribu kutafuta awards. 
*******************************************

Soma Story ya Queen kwa maneno yake mwenyewe hapa:

http://www.wavuti.com/4/post/2012/2/the-story-of-queen-b.html#axzz1wMvqNbjm

Wadau, ninaendelea kujaribu kuwasiliana na Fox 25 ili watoe story au correction, kuwa nchi yetu si ya watu washenzi kama walivyotupakazia.


Posti yangu wa awali mnaweza kusoma hapa:

Niligundua kuwa huyo binti, alililewa katika familia enye uwezo na waliokuwa wanampenda.


http://swahilitime.blogspot.com/search?q=queen+butahe

Wednesday, May 16, 2012

Travel to Udzungwa Mountain

Visit the Beautiful South of Tanzania. Swim in waterfall plunge pools in the stunning Udzungwa Mountains. We are offering a 10% discount on any safari booked before the end of June 2012  that includes Hondo Hondo Tented Camp in Udzungwa.

see  www.udzungwaforestcamp.com  or mail enquiries@wildthingsafaris.com for more information.

Tuesday, May 01, 2012

Management by Crisis at Mzumbe University: The Failure of Core Values [2]

Mzumbe University Mission Statement


Kuna nini Mzumbe University?

Nimepata kwa E-Mail:

*************************************
Comrades,


Last year in January, I wrote an article on "Management by Crisis at Mzumbe University: The Failure of Core Values". The article was centred on the "University Services Marketing" and depicted the deficiencies in the management of staff and the services so envisaged. Today, the 01st May, 2012 I am sending you an article on the same topic. However, this time mine observations have been derived with respect to the Controller and Auditor General (CAG) Audit Report 2010/2011 dated 28th March, 2012 that was tabled and discussed in House of Assembly (Dodoma, April, 2012). Mzumbe University was in the CAG Audit spotlight and where there are three audit queries and/or anomalies, namely:

1. Ghost workers payments = TZS 194.4 million for just four months;


2. Procurements outside Annual Procurement Plan [APP] = TZS 1.9 billion; and


3. Mis-information on number of staff between two departments of the University.

I therefore, as an internal cusotmer, do hereby convey my discussion, analysis and recommendations for your synthesis and reaction. My fundamental aim is to make the University (Mzumbe) the centre of academic excellence that could provide exemplary execution of the good governance principles. It is therefore our noble task in compliance with the core values - transparency, professionalism, integrity, fairness, ethical behaviour and in line with the requisites of corrupt free Tanzania in public services delivery systems.

I submit,

Bakari M Mohamed, BBA [PLM], CPSP [T], MSc (PSCM), Reg. PSP (AU 0005)

1. Lecturer in Procurement and Supply Chain Management
2. Procurement and Supply Chain Auditor
3. Procurement and Supply Chain Specialist, Consultant, Researcher and Trainer in Procurement Contracts Management
4. Doctor of Alternative Medicines [DAM] & Natural Healing Therapist

Department of Procurement and Logistics Management
Mzumbe University
Box 6
Tel (Office): + 255 23 2604381/3/4
Mobile : + 255 713 593347
MZUMBE, Tanzania.

Thursday, August 26, 2010

Rushwa Kilombero



Kuna mdau ameleta picha hizi. Hebu mlioko huku mtupe habari zaidi za hiyo get ya huko Kilombero.

"Dada Chemi naomba utoe hii waone jinsi rushwa iko njenje gate la mali asili Kilombero River, hasahasa upande wa wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro."
Hiyo ni lory ni usafiri mbadala wa wilaya hiyo,hwa ni wafanyabiashara ambao ulazimika kutoa rushwa ili wasitoe pesa nyingi kwa ajili ya ushuru wa mazao kutoka wilaya hiyo,kwani gunia moja hulipia tshs 20,000/-na hyo alikuwa na gunia 10 za mpunga asingeweza kutoa laki mbili kwa hiyo alihonga 50,000/=na kuruhusiwa kupita nazo!"

Thursday, October 22, 2009

Wanavijiji Wafukuzwa Morogoro

Premier Mizengo Pinda (C), flanked by Morogoro regional commissioner, Colonel (rtd) Issa Machibya (L), Kilombero district commissioner, Evarist Ndikilo and Kilombero Plantations Limited manager, Carter

Huko Zimbabwe, Mugabe anafukuzwa wazungu kusudi wananchi wa kiafrika wapate ardhi ya kulimia. Sisi Tanzania, tunafukuza waafrika kusudi wazungu wapate ardhi ya kulimia. Ukoloni Mamboleo?
**********************************************************

Kutoka ippmedia.com

Prime Minister Mizengo Pinda has ordered villagers who invaded the Mngeta Rice Farm (MRF) in Kilombero district, Morogoro region to leave immediately to make way for massive agricultural investments.

The premier issued the order over the weekend on the second day of his official tour of Morogoro region to inspect agricultural activities including farms and research centres.

Addressing Mngeta villagers, the Prime Minister said about 2,000 residents of Mngeta and Lukolongo villages have illegally taken over 300 hectares out of 5,000 hectares in the potential area for paddy farming.

He directed Morogoro regional authorities to ensure that villagers who have illegally invaded the area are immediately relocated to other areas.

“But this should be done in a proper manner. I would not prefer the use of force during the process of relocation,” the Premier cautioned, stressing that farmers should continue cultivating around the MRF as out-growers and contract farmers.

He said the move would enable the farmers acquire farming skills and access to rice farming infrastructures.

MRF is co-owned by Rufiji Basin Development Authority (RUBADA) and a UK based investor, Agrica.

The two have formed a new company known as Kilombero Plantations Limited (KPL) to help boost modern agriculture in the region.

The farm was established in 1986 under Korea Tanzania Agricultural Company (KOTACO). KPL started to operate the farm in 2008 and succeeded to cultivate more that 2,000 hectares of rice with an investment of 22bn/-.

Pinda arrived in Morogoro last Saturday and started his tour by visiting Kilombero district where he received information on development of the ‘Kilimo Kwanza’ initiative from the District Commissioner, Eng. Evarist Ndikilo. He also visited the Katrin Agricultural Research Centre.

He also visited Chita-Melela valley which is used for rice cultivation.

The Prime Minister also advised farmers to establish a Savings and Credit Cooperative Society (Saccos) that would provide them with funds to improve their agriculture, and promised to give them 10m/- once they manage to contribute among themselves a total of 10m/-.

Pinda yesterday visited Sagamaganga village to see a demonstration farm for livestock keeping where he promised a 3m/- donation as a contribution for purchases of animal feeds and vaccination.

CHANZO: THE GUARDIAN

Friday, September 25, 2009

Soko Kuu la Morogoro 1908

Hii pichani ya soko kuu la Morogoro mjini iliyopigwa enzi za Mjerumani.

Tuesday, August 18, 2009

Morogoro Mjini

Bofya picha kusudi uone vizuri Morogoro Mjini.