Monday, May 07, 2007

Sinema ya Simu ya Kifo


(Pic 1) Mwongozaji Hammie Rajab, akipungia Camera.
(Pic 2) Ganda la DVD la Simu ya Kifo
(Pic 3) Baadhi ya walioigiza katika sinema la Simu ya Kifo
All Photos courtesy of Michuzi Blog.



Wikiendi hii sinema mpya ya Bongo iitwayo, Simu ya Kifo, ilizinduliwa. Premiere ilikuwa katika ile kumbi maarufu la wasanii, The Little Theatre, pale Oyster Bay.

Kwa vile siko Bongo, bado sijauona. Lakini nasikia ilikuwa nzuri na watengenezaji wamejitahidi sana kusudi iwe sinema na si video. Hongera sana.

Wengi tunafahamu kile kitabu cha Simu ya Kifo, na hii ndo sinema yake. Nitapenda kuona kama sinema ni nzuri kama kitabu. Mara nyingi inakuwa vigumu kwa sinema kushinda kitabu maana kwenye kitabu wanaelezea kwa undnani zaidi na mambo mengi zaidi.
Mlioiona naomba maoni yenu.
Kama hamfahamu zamani Little Theatre ilikuwa 'Exclusive' kwa ajili ya wazungu. Waafrika walikuwa wafanyakazi tu pale. Hata bei ya tiketi waliweka juu kusudi waafrika washindwe kununua. Kulikuwa na sisters, Erica Khuri na Tony Khuri (wote marehemu) walikuwa wanaandaa michezo mara kwa mara pale. Nafurahi kuona weusi kwenye Stage hiyo.


Saturday, May 05, 2007

Ndege ya Kenya Airways imeanguka huko Cameroon!




Ndugu wa abiria huko Kenyatta Aiport Nairobi.



Kuna habari kuwa ndege ya Kenya Airways enye abiria 115, imeanguka huko Cameroon. Ilikuwa inatoka Ivory Coast (Cote d'Ivoire) kwenda Nairobi lakini ilipitia Cameroon kuchukua abiria wengine. Mungu awalaze marehemu wote mahali pema mbinguni. AMEN/AMIN.

****************************

NAIROBI, Kenya (AP) -- Kenya Airways has lost contact with a commercial airliner carrying more than 100 passengers that took off from Cameroon early Saturday, the airline said.

"The last message was received in Douala after takeoff and thereafter the tower was unable to contact the plane," Kenya Airways CEO Titus Naikuni said Saturday.

The Boeing 737-800 was carrying 106 passengers, eight crew members and a flight engineer, he said. The plane is capable of carrying 189 passengers.

"We have no details about what has happened to the aircraft," Naikuni said.The flight departed Douala at 12:05 a.m. and was to arrive in Nairobi at 6:15 a.m. The flight originated in Ivory Coast but stopped in Cameroon to pick up more passengers, the airline said.

The airline opened a crisis management center near the airport. Relatives of those on the plane were instructed to go to a downtown airport, where they would be provided information as it became available.

The last crash of an international Kenya Airways flight was on Jan. 30, 2000, when Flight 431 was taking off from Abidjian, Ivory Coast, on its way to Nairobi. Investigators blamed a faulty alarm and pilot error for that crash, which killed 169 people.

Thursday, May 03, 2007

Trailer ya Sinema ya Bongoland

Tazameni Trailer ya sinema ya Bongoland original.

Iko YOU TUBE:

http://www.youtube.com/watch?v=g_2XKba__3Y

Barack Obama yuko chini ya ulinzi wa Secret Service


Mgombea wa raisi wa Marekani katika uchaguzi ujao, Senator Barack Obama wa Illinois, amewekwa chini ya ulinzi ya Secret Service. Kazi ya Secret Service ni kulinda watu wazito katika serikali ya Marekani kama Raisi na familia yake na makamu wake, na pia wagombea raisi lakini walioteuliwa na vyama vyao.

Obama bado hajateuliwa, hivyo ina maana kuwa lazima Secret Service wamepata habari kuwa maisha yake iko hatarini. Kama tunavyojua Obama ni mweusi na bado kuna wabaguzi hapa Marekani amabao wasingependa kuona mtu mweusi anashika uraisi. Ametokea kupendwa na watu wa kila rangi na kuna watu ambao hawafurahii kabisa! Tusisahau viongozi weusi waliouliwa na hao wabaguzi kama Martin Luther King Jr., na Medgar Evers.

Mungu amlinde na abariki Barack Obama!


********************************************************************

Thursday, May 03, 2007


(CNN) Democratic presidential hopeful Barack Obama has been placed under secret service detail, according to a statement from the U.S. Secret Service."Secretary Chertoff has, after consultation with the congressional advisory committee, authorized the United States Secret Service, to protect presidential candidate Senate Barack Obama. "As a matter of procedure, we will not release any details of the deliberations or assessments that led to protection being initiated. For security reasons we will not release the timing, scope or details of any protective operations."

Zanzibar International Film Festival - ZIFF






The Zanzibar International Film Festival (Festival of the Dhow Countries) ZIFF will be held June 29th, to July 8th, 2007 in Zanzibar, Tanzania.
ZIFF ni tamasha inayofanyika kila mwaka huko Zanzibar. Wanaonyesha sinema na pia vikundi mbalimbali vya kisanii na muzuki kutoka nchi mbalimbali zinashiriki katika maonyesho kadhaa. Lasiki hasa ni maonyesho ya sinema zinatoka nchi za mwambao ya bahari ya hindi. Huu ni mwaka wake wa kumi. Mwaka huu wataizindua Dar katika hoteli ya Holiday Inn.


Sunday, April 29, 2007

Clip from Bongoland film - Original - Juma and Mukulu

Juma on a date from the original movie Bongoland. See www.kibirafilms.com

Kwa wapenzi wa Bongoland, tazameni scene ya Juma kuonja uchungu wa maisha Marekeni!

Saturday, April 28, 2007

Watalii waharibu Mbuga za Wanyama

(UTANI)

Jamani, jamani, jamani. Inasemekana mtalii kutoka USA alienda kwenye mbuga ya wanyama na backpack mgongoni. Alikuwa kwenye land rover na watalii wengine. Sasa walivyoona simba, waliingiwa na kiwewe na backpack ikaburuzwa kwenye chuma fulani kwenye land rover yao. Kwa bahati mbaya chupa ya shampoo ilianguka mbugani. Shauri ya woga ya kuliwa na hao simba, waliamua kuacha chupa pale pale ilipoanguka.

Watalii waliondoka na gari yao. Sasa simba na utundu wake kaona hiyo chupa, kaanza kulamba lamba maana ilikuwa na ladha ya nazi. Mwisho kaipasua na kulamba shampoo yote. Baada ya wiki moja watalii walirudi na kuona huyo simba wa kiafrika kawa simba wa kizungu (pichani)!

Thursday, April 26, 2007

Muungano

Tanzania Flag (above)
Zanzibar Flag (above)
Tanganyika Flag (above)



Miaka 43 iliyopita, siku ya leo, marehemu Mwalimu Nyerere alichanganya udongo kutoka Tanganyika na udongo kutoka Zanzibar kama ishara ya Muungano wa nchi hizo mbili. Nchi iliyounganishwa ukaitwa Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA (United Republic of Tanzania).

Kama wewe ni Mzanzibar au Mtanganyika wewe ni MTANZANIA! WaTanzania tunajivunia kwani sisi ni mfano mzuri kwa waafrika wenzetu na dunia.

WaTanzania tumepitia mengi lakini bado tuna Muungano wetu.

Mungu alinde Muungano wetu. Tuendelee kukaa kwa amani. Mungu Ibariki Tanzania!


***************************************************************************
Wafungwa wasemehewa!

Ni mila ya marais kusamehe baadhi ya wafungwa siku ya leo. Taarifa zinasema kuwa Rais Jakaya Kikwete amesamehe wafungwa 4,022.

Katika kuadhimisha miaka 43 ya Muungano, Rais Jakaya Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 4,022. Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nchi leo imesema waliofaidika na msamaha huo ni pamoja na wale wanaotumikia kifungo kisichozidi miaka mitano ambao hadi jana walikuwa wameshatumikia robo ya kifungo chao.

Kwa habari zaidi nenda: http://www.ippmedia.com/ipp/alasiri/2007/04/26/89258.html

Wednesday, April 25, 2007

Konyagi


Hata Boston, tunakunywa Konyagi! Ni pombe ya aina ya pekee duniani na waTanzania tunaweza kujivunia kuwa na sisi tuna kikali chetu! Inatengenezwa na Tanzania Distillers.

Jana niliamua kustarehe kidogo na kikali. Huwa napenda wine, au bia baridi! Lakini jana nilipata hamu ya Konyagi! Nilivyoenda Bongo mwaka jana nilirudi na kachupa ya Konyagi. Siku moja moja nikitaka kukumbuka 'home' nakunyawaga. Konyagi ni pombe enye ladha ya pekee. Halafu ni clear kuliko hata maji ya kunywa ya hapa Marekani.

Nashangaa haijanywa kinywaji kikuu ng'ambo kama vodka, najua unaweza kununua Uingereza lakini bado sijauona kwenye maduka ya pombe hapa USA. (Wasomaji mnishahishe kama nimekosea) Je, watengenzaji wamefanya international marketing?

Konyagi inatengenezwa na mabibo. Mnakumbuka tulivyokuwa tunaharibu nguo zetu na juisi ya mabibo. Doh! Pale UDSM, kati ya Hall 3 na Hall 2, kuna orchard kubwa kweli ya mikorosho. Tulikuwa tunashinda huko tuna chuma maikorosho, una kula ile bibo enye juisi kibao na korosho unatupa kwenye mfuko. Mfuko ukijaa unachukua kipande cha bati, halafu unatengeneza moto juu! Tia hizo korosho, na kaa mbali maana moshi huo! Nyie korosho zile za kuchuma na kuchoma wenyewe ni tamu.

Basi niwape story. Mara yangu ya kwanza kunywa Konyagi nilikuwa JKT. CO (Commanding Officer) alikuja Officer's Mess na kunipa offa. Nilmshukuru lakini ilibidi nikatae maana nilikuwa sijaozea kunywa pombe.

OHOOO! Si jamaa kanipa amri sijui adhabu ninywe nusu glass straight mbele yake! Niliinywa kama sumu, baada ya hapo nikaenda bweneni kulala hadi asubuhi huko tumbo na kichwa kinaumwa!

Lakini Konyagi kwa kiasi si mbaya hasa ukichanganywa na soda. Msinywe sana maana inalewesha haraka!

Konyagi JUU!

Tuesday, April 24, 2007

Nani atakuwa Juma?


Wikiendi hii huko Minneapolis walifanya auditions kwa ajili ya kumpata atakayeigiza mhusika mkuu kwenye sinema ya Bongoland 2, Juma. Bongoland 2, ni sinema itakayapigwa Tanzania, mwezi Julai. Ni sehemu ya pili ya sinema ile ya Bongoland.
Pictured Front row: Director Josiah Kibira, na auditioners, Honest, Peter & Deus.
Kwa habari na picha zaidi someni :

Monday, April 23, 2007

Maoni ya Wasomaji kuhusu Mgomo wa wanafunzi UDSM

Expelled UDSM students - pic from Michuzi blog

Nimeamua kubandika maoni machache niliopata kwenye blogu kuhusu mgomo wa wanafunzi wa UDSM. Karibuni mtoe maoni yenu.
Na sasa kuna habari kuwa wanalegeza masharti ya wanafunzi kurejea Chuoni. Kwa habari zaidi someni:
**********************************************************************************

Kithuku said...

Hili suala la kugoma kila mara tena kwa sababu zisizo na mantiki tumechoshwa nalo kabisa. Watu wenye matatizo Tanzania ni wengi tu, sio wanafunzi peke yao. Pesa zinazotolewa za huduma za jamii zinapaswa ziwafaidishe wote, si wanafunzi peke yao. Kwa nini wang'ang'anie 100% sponsorship bila kuwafikiria watanzania wengine wanaohitaji fedha hizohizo? Mbona wagonjwa mahospitalini wanachangia gharama za huduma za afya, wao nani atawasaidia kugoma ili watibiwe bure 100%? Kuna matatizo ya njaa, barabara, nishati, makazi, usalama, n.k, yote yanahitaji fedha. Mbona hawa vijana wanakosa uzalendo? Na hata hivyo serikali ilikwisha waahidi wawe na subira, hatua zinapangwa kuboresha hali iliyopo.

Kwa maoni yangu, vijana hawa wamekosa hekima na tena hawana adabu. Huwezi kumlazimisha anayekukopesha akukopeshe hela yote unayohitaji. Kopa kiasi kwake, nyingine jazia kutoka kwa mkopeshaji mwingine au kutoka vyanzo vyako vingine vya mapato. Na la zaidi, ni ukosefu wa nidhamu uliokithiri kumpa Rais wa Nchi ultimatum, ati atoe majibu ndani ya siku mbili! Wewe ni nani? Rais wetu yuko kushughulikia matatizo ya wanafunzi tu? Au hilo lilikuwa na dharura gani hadi likashindikana kusubiri?

Huu ni ulevi wa madaraka ya kitoto, mtu anachaguliwa kuwa rais wa wanafunzi, nafasi ya mwaka 1 tu, basi anajiona naye ni Rais kama Mh Kikwete, anaweza kumtishia hata Rais wa Nchi! Anampa ultimatum! Uchuro kabisa huu! Rais wa wanafunzi ni mwanafunzi, na urais huo unakoma anapokoma uanafunzi. Waelewe hivyo. Waache kuyumbishana wanafunzi kwa kutumia vyeo feki hivyo na kudanganyana ati "solidarity", hakuna solidarity hapo wakati huna cheti! Subiri upate cheti (degree) ndipo utaweza kumsumbua mwajiri wako kwa masharti kwa sababu atakuwa anahitaji utaalam wako. Sasa hivi huna utaalamu wowote unabwabwaja ati "solidarity"! Utaula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua!

Nashauri UDSM wachambue vizuri wale waliosababisha fracas hii wapewe adhabu ya kukomesha kabisa. Wakomolewe kabisa hao, wala siwatetei ng'o! Uongozi uwe tu makini wasije wakaumiza wale wasio na hatia.

Kuhusu haya masharti mapya mie naona safi sana, kwanza wameyataka wenyewe hao wanafunzi. Nasema University ikaze uzi, masharti ndio hayo, naunga mkono kabisa na naomba serikali isimamie hilo. Hakuna jipya hapo, kwani hata wagonjwa hospitalini wanalipia gharama, sembuse hao wazima kabisa! Walipe hizo hela. Kama kweli yupo asiyeweza kulipa, abaki kwanza nyumbani tuone wangapi wanaweza tuendelee nao kwa kipindi hiki, tena itasaidia kupunguza fujo. Hao watakaoshindwa kabisa watafutiwe mpango wa kuwasaidia (mfano kama kampeni za michango mbalimbali n.k) na fedha zikishapatikana ndipo waitwe chuoni. Hata watoto wanaopelekwa kutibiwa India, ni fedha zinachangwa kwanza zikishatosha ndipo wanapelekwa. Tufanye hivyo kwenye elimu pia. Pesa mbele, hakuna huduma inayoweza kupatikana bila fedha.
Nasema tu poleni sana lakini mmevuna mlichopanda.
4:52 AM

*************************************************************************************
Maricha said...

Da Chemi,

Hakuna mahala ambapo kuna kazi za kumwaga, hata wale walio soma nje wanalijua hilo. Wanasoma by day na kufanya kazi za ajabu ajabu by nite.

Tumefanya kazi za kubeba mabox, kazi za kuosha vibibi, kazi za kuanmgalila taahira, kazi za kuosha vyomba nk ili mradi hela ya rent na shule ipatikane.

Hawa vijana wakiwa creative wanaweza kufanya kazi, hakuna kazi itayoenda kuwatafuta, hakuna! itabidi wao ndio wazitafute kazi. Nitatoa mifano ya kazi wanazoweza kuzifanya.

1) Wanaweza kuanzisha migahwa ya chakula ya kwao wenyewe. Kama watu wanasoma masomo ya biashara ni kwanini wasianze kupractice? Akina mama ntilie wanatengeza hela ya kutosha wao wanawaangalia tu kazi kugoma kila kukicha.

2) pia wanaweza kufanya kazi kama baa tenda. Inasound vibaya mwanafunzi kuw abaa medi lakini kazi ni kazi.

3) wanaweza kufanya kazi za ukarani na utalishi. Makampuni kibao yanahitaji watu wanaoongea inglish sasa wao si ni wasomi bana kwanini wasichukue kazi izo?

TATIZO
Tatizo nilionalo mimi ni Scheduling, jinsi vyuo vya kwetu vinavyopanga ratiba ni vigumu sana kwa mtu kufanya kazi na kusoma. manake utakuta masomo ni kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa 12 jioni.

Ni nini cha kufanya? Mimi naona Chuo kiamriwe na serikali au owner wake ili kiwe na flexible ya scheduling ya ratiba ya madarsa.

La pili ni lazima masomo yapewe credit ili wanafuinzi wachukue lodi wanayoweza na kwa gharama wanayoweza kuimudu.

NaLa tatu ni vyema chuo kikaanzisha Payment plan ya namna fulani ivi. Yaani hata kama unadaiwa laki nane ni vyema wakuruhusu kuendelea na shule huku ukilipa leo shiling elfu kumi kesho laki cha msingi by the end of the semester wanafunzi wawe wamelipa hela yote.
9:34 PM

Saturday, April 21, 2007

Miss America wa mwaka 1944 afanya tendo la kishujaa mwaka 2007!


Waliomsahau mshindi wa mashindano ya urembo Marekani, Miss America, wa 1944, watamkumbuka na wasiomjua, sasa watamjua.
Bi Venus Ramsey ana miaka 82 sasa. Wakati wa ushindi wake ulikuwa wakati wa vita kuu vya dunia ya pili.

Juzi alivamiwa nyumbani kwake kwenye shamba huko Kentucky. Mwizi alijaribu kuwmibia vifaa vyake vya kulimia shamba. Kwa kutumia 'walker' aliweza kusimama imara na kufyatua risasi na kulipua matairi ya gari ya huyo mwizi.
Kwa habari zaidi ya hiyo tukio someni:


Poleni Wanafunzi wa UDSM lakini....

Students trying to Leave UDSM Main Campus
Ofiice Notice about UDSM Closing
Wanafunzi wa Uuniversity of Dar es Salaam (UDSM), waliofukuzwa majuzi wataruhusiwa kurudi Chuoni lakini kwa masharti:

From Michuzi Blog:

" Taarifa za redio mbao zilizonifikia punde ni kwamba wanafunzi wa udsm waliofukuzwa juzi kwa kugoma kuingia darasani wametakiwa waandike barua ya kujieleza ikiwa imeambatanishwa na 100,000/- ya matibabu pamoja na ada asilimia 40 (kama laki nane hivi) kupitia benki na wawe wamezipeleka barua na risiti za malipo hayo ya benki kwa makamu mkuu wa chuo kati ya aprili 23 hadi mei 4 ili kuweza kufikiriwa kurudi chuo. nafanya juhudi kupata waraka kamili wa masharti yote. "


Nimesoma kwenye ippmedia.com, kuwa wanafunzi waliofukuzwa na wasio na familia DSM, wameishia kuuza vitu vyao kama simu na TV ili wapate hela ya chakula na nauli ya kurudi makwao. Wanasema kuwa wasichana 'wanajiuza' ili wapate mahitaji yao. Ama kweli hali inasikitisha.

Nani aliwachochochea wagome? Je, wako wapi? Nikikumbuka miaka ya nyuma na migomo mingine anayeumia ni mtoto wa mkulima, au mtoto aliyetoka kwenye familia enye kipato kidogo. Watoto wanaotoka familia zinazojiweza wanapelekwa 'abroad' kumaliza masomo yao.

Kuhusu eti zamani watu walisoma bure, lazima niseme si kweli. Kumbuka kuwa kulikuwa na JKT, ilikuwa njia moja ya 'kutoa shukurani' kwa serikali kukusomesha. Pia ilikuwa ukianza kazi unatakwa mshahara kwa muda fulani. Kwa kweli ilikuwa si bure. Pia enzi zile wasomi walikuwa wachache. Je wakiamua kurudisha ule utaratibu wa kusomesha mamia kwa mwaka badala ya maelfu hali itakuaje?

Ni mwaka 2007, na siyo miaka ya 1960's au 1970's na hata 1980's. Na wajue maisha ni magumu duniani pote. Hata hapa USA kama huna full scholarship utafanya kazi mbili tatu, huko unasoma ili kuweza kumudu fees. Wenye wazazi wanaoweza kuwalipia 'full' ni wachache sana ukilinganisha na idadi ya wanafunzi. Wanafunzi wengi wanasoma kwa mchanganyo wa mikopo, grants, scholarships na kazi.

Na kumbuka enzi zile wengi walipelekwa Eastern bloc, yaani Urusi, Poland, Bulgaria, East Germany, Yugoslavia etc. kusoma bure lakini hakuna tena. Dunia umebadilika.

REMEMBER LIFE IS NOT EASY.

Thursday, April 19, 2007

Kibira Films bado wanamtafuta 'Juma'!

Bado actor anatafutwa kwa ajili ya kuigiza kama mhusika mkuu wa sinema ya Bongoland 2!

WHERE IN THE WORLD IS JUMA.....

We cannot find him and this is why this weekend on Saturday April 21, 2007 we are conducting a screen test.A screen test of the would be Juma - the lead actor for the movie...Bongoland II. If you are game and think you can act here is the venue...Holy Trinity Lutheran Church in Minneapolis - the address is 27 EAST 31st Street.

The screen test will start at 10:00 AM. Please check our site for the updates on the outcome.


Kwa habari zaidi bonyeza hapa: BONGOLAND 2

Kwaheri Sanjaya!









American Idol Judges Randy Jackson, Simon Cowell, & Paula Abdul

Kwa wapenzi wa American Idol naomba maoni yenu. Huyu kijana Sanjaya aliwezaje kukaa kwenye American Idol kwa muda wote huo? Jana alivyotolewa nilibakia nashabikia kwa furaha maana hakustahili kufika hadi kuwa namba 7 kati ya waimbaji kumi na wawili bora.

Sanjaya ni shombe wa kihindi kutoka Washington State. Ana miaka 17. Mama yake ni mzungu na baba yake ni mhindi. Ana nywele nyingi nyeusi, na sauti yake ni ndogo na ya kike kike kama ya Michael Jackson. Anaweza kuimba nyimbo za stevie wonder vizuri. Akiimba wasichana wadogo wadogo wanaanza kulia shauri ya kuingiliwa na kiwewe fulani. Watu wanasema baba yake kamfanyia dawa za kihindi maana hana sauti ya kuwa American Idol.

Watu kama Howard Stern na wengine wenye chuki walifanya kampeni za kupata watu wa kumpigia kura ili ashinde. Mungu ni mwema na wameshindwa! Sanjaya katoka jana kwa majonzi. Alivyoambiwa ndo siku yake ya mwisho, alibakia analia kama mtoto mdogo.
Kitu kilichowafanya wasichana wadogo wadogo wampende ni, kutabasamu kwake, nywele nyingi (kila wiki alibadilisha staili ya nywele), na eti ana sura nzuri yaani handsome. Lakini kuimba hawezi. Watu waliokuwa wanaimba vizuri kama Stephanie Edwards, Brandon na Gina Glocksen walitolewa kabla yake.

Picha aliyepiga dada yake, Shyamali, akiwa uchi huko anapiga gitaa ilimsaidia pia. Shyamali aliwahi kufanya kazi kwenye restaurant ya Hooters. Alitolewa zamani wakati walivyobakia waimbaji 48.
Bora hakushinda maana kuendelea kuwepo kwake ungehatarisha maisha yake, maana nchi hii kuna vichaa. Angepigwa risasi na mtu mwenye chuki eti kawa nini Sanjaya anaharibu show.

Na leo naamini kuwa producers wa American Idol wanapumua vizuri. Maana Sanjaya angeshinda ingekuwa mwisho wa American Idol maana ushindi wake ungehibitisha kuwa American idol siyo kamchagua anayejua kuimba, bali anayependwa na watu.

Lakini huo si mwisho wa Sanjaya. Kwa vile kapendwa sana lazima tutamwona kwenye matangazo ya TV, au akiigiza kwenye sinema za mateenager.

Wednesday, April 18, 2007

Mauji Chuo Kikuu cha Virginia Tech


Sura ya Muaji Cho Seung-Hui

Poleni waKorea wote. Sasa asante Cho Seung-Hui, itakuwa vigumu wapate visa za kuja kusoma Marekani bila kuchambuliwa kila kitu toka walichofanya toka wazaliwe mpaka wanakunya saa ngapi.

WaMarekani waoga sana na wabaguzi sana na sasa wamepata kisingizio cha kunyanyasa waKorea wote Marekani. Msisahau kabla ya 9/11 jinsi waarabu walivyokuwa wanathaminiwa Marekani shauri ya pesa zao.

Kama hamjasikia, vituko na visa vya kijana, Cho Seung-Hui, mwenye miaka 23, na mwanafunzi aliyekuwa anasoma Chuo Kikuu cha Virginia Tech nitawasimulia kwa ufupi. Siku ya jumatatu akili zilimruka na aliua wanafunzi na walimu wa chuoni hapo. Watu 32, walioamka na kufanya shughuli zao kama kawaida siku hiyo walipoteza maisha yao.

Cha ajabu, watu walijua kuwa huyo jamaa ni mwendawazimu siku nyingi. Hata mwalimu wake alienda polisi kumshitaki kuwa ana wasiwasi naye. Lakini polisi hawakufanya kitu.
Na wote tunajua mweusi angekuwa na vituko kama vyake, angefukuzwa shule zamani. Cho alikuwa anadika michezo ya kuigiza na mashairi zenye plots za kutisha kama kubaka, kuua, na kujiua.

Nani asiyejue kuwa waMarekani wanasema kuwa hao wenye asili ya Asia wana akili sana. Na si ajabu ndo maana huyo Bwana John Markell, alimwuzia bastola bila maswali mengi. Alisema, “he looked like a clean cut College student”, yaani alionekana hana matatizo. Je, kijana mweusi anayesoma Chuo Kikuu angeweza kununua bastola kwenye duka lake kwa urahisi hivyo? Na leo asubuhi nilikuwa nabishana na bosi wangu kuhusu hiyo swala, nikamwambia, huyo Markell asingeniuzia mimi mwanamke mweusi hiyo bastola, lazima angetafuta kisingizio cha kutokuniuzia maana sionekani kama clean cut college student au clean cut period.

Kati ya hao waliouliwa siku ya jumatatu kulikuwa na weusi kadhaa. Mmoja ni Ryan Clark, aliyekuwa na akili sana na kusoma Major tatu (haya nyie wazungu mnaosema kuwa weusi hawana akili). http://www.wrdw.com/news/headlines/7071667.html

Na jambo lingine kinachoniudhi. Wansema kuwa haya ndo mauaji makuu yaliyowahi kutokea nchini Marekani. Wamekosea, au wansema hivyo kwa vile weusi siyo watu kwao. Miaka ya nyuma huko Florida (1923) walikuwa mamia ya weusi, na mauaji ya weusi yalitokea Arkansas (1919) na Oklahoma (1921) pia.

Karibuni mtoe maoni yenu.

Saturday, April 14, 2007

Marudio - Acheni Ushamba

Hii ni kati ya posts zangu za mwanzo:

Tuesday, October 18, 2005

Acheni Ushamba! Jamani, jamani, jamani! Siku hizi nikiona vijana waBongo hapa mitaani Boston nakimbia! Hao vijana siyo wale wa miaka ya nyuma waliokuwa tayari kufanya kazi mbili/tatu ili waweze kuishi vizuri na kupeleka zawadi nyumbani. Hapana vijana wa siku hizi wanataka vya dezo!

Wamekuja Marekani wakidhania maisha USA ni kama vile kwenye video za Rap. Hapana vijana, maisha siyo hivyo kabisa. Hapa USA kama hukuja na hela zako basi uwe tayari kuchapa hizo kazi mbili/tatu, utafanikiwa! Lakini kinacho niudhi hasa ni hao vijana wanaoenda madukani na kuiba, yaani shoplifting! Yaani mtu anaingia dukani anasomba vitu, tia ma-cap kichwani halafu wanatoka nje ya duka. Wanakamatwa halafu unaombwa uwawekee dhamana! Si waliiba wao wacha wakome huko jela! Tena jela za Boston ni nzuri kuliko kupelekwa Keko! Nasema hao vijana ni washamba maana ukiwauliza kwa nini waliiba, watasema, “Oh, sikujua kama wananiona!” Hawakuoni???? Heh!

Mjue mkifika kwenye mall tena parking lot, mnaanza kuchgunguzwa na makamera yaliofichawa kila mahala isipokuwa chooni! Yale mapambo na magololi yanayoing’inia si urembo tu, bali ni masecurity camera. Hivyo huwezi kusema, “Oh sikuiba!” huko store detective anakutolea kanda ya video ambacho wewe ndo star!

Wanaona kwa vile mlango huko wazi hakuna security, au watu wengi basi ni free for all. Kitu kingine hao vijana,utasikia wanaongea, sijui vitu gani, wakidhania English! Wanajaribu kuiga ma-slang wanaosikia kwenye movies. Nyie! Watu hawaongei hivyo!

Ukitaka kazi ya maana ujfinze kuongea English! Yaani inatisha maana huwezi hata kuelewa ansemaje na Slang zake zenye Bongo accent! Na acheni kuvaa kama gangsta! Kwanza ukikosea rangi utapigwa risasi na ma-gang au utasumbuliwa na polisi wakidhania wewe ni gang banga!

Na poleni vijana ambao wanashuka kwenye ndege wakidhania wanaenda kuishi kwenye nyumba inayofanana na ya P. Diddy, lakini wanakuta wanaenda kubanana watu 10 kwenye chumba kimoja.

Na kuna wengine wanafanya uhalifu kama kuingia kwenye biashara haramu ili wapate pesa za haraka. Sijui ni kwa kuwa hawajui au hawajali,lakini wanhatarish maisha yao na za familia na marafiki zao!

Ngoja niishie hapa ...maana!

Bongoland 2


(Photos courtesy of Muhidini Michuzi)

Naona Kibira Films International inasonga mbele na maandalizi ya kupiga picha ya Bongoland 2, Tanzania mwezi Julai. Wasanii nchini Tanzania wanatoka kwa wingi kujaribu kupata nafasi ya kuigiza katika hiyo sinema. Katika picha za juu, ni baadhi ya wasanii waliotokea kwenye Casting Call.
Sinema itakuwa sehemu ya pili kuhusu maisha ya Juma Pondamali, ambaye katika sinema ya Bongoland, alishindwa na maisha ya Marekani. Hatimaye aliamua kurudi zake Tanzania, tena baada ya waBongo wenzake kumchangia nauli ya tiketi. Je, alivyorudi maisha yake yalikuaje?
Kibira Films, inaongozwa na Bwana Josiah Kibira, wa Minneapolis, Minnesota. Kampuni hiyo ilitengenza sinema ya Tusamehe. Mimi naigiza katika sinema hiyo kama Mama Kurusumu.

Wednesday, April 11, 2007

Sinema ya ROOTS




Tangu jumapili TVOne, wamekuwa wakionyesha sinema kabambe ya ROOTS. Hiyo sinema ilionyeshwa kwa mara ya kwanza mwaka 1977 na kuingia katika vitabu vya historia kwa watazamaji wengi. Zaidi ya watu 130 milioni nchini Marekani walitazama.

Nasifia sana hiyo sinema maana inakumbusha watu na hasa waMarekani weusi kuwa wametoka mbali. Inaonyesha kuwa waafrika walikuwa na utamaduni na mzungu alijaribu kuifuta kwa kuzuia watumwa kutoongea lugha zao, kuchukua majina ya kizungu, na walizuiliwa kufanya kitu chochote cha kiaafrika. Katika Roots unamsikia binti Fanta, akisema mimi nimesahau kila kitu cha Afrika, nia yangu niishi. Na utasikia watumwa waliozaliwa Marekani wanavyowakashifu watumwa waliotoka Afrika. Watumwa wanajiona bora kuliko wale waafrika.
Roots ilitungwa na marehemu Alex Haley. Inahusu historia ya familia yake na inaanzia kijiji huko Gambia, na kuzaliwa kwa Kunta Kinte. Kunta anakamtawa na kuletwa Marekani. Ukiona walivyokuwa wanasafirisha weusi utalia. Huko nakumbuka dada moja mmarekani mweusi kaniambia eti kafurahi kuwa mababu zake waliletwa kama watumwa kutoka Marekani maana ana maisha bora na hashindi njaa. Pia inasikitisha ukiona Kunta Kitne kafungwa cheni shingoni na wanam-pat kichwani kama mbwa!
Huko mashuleni Marekani ni lazima vijana watazame sinema ya Schindler's List kusudi waelewe wayehudi walivyouliwa na Hitler wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Sasa kwa nini isiwe lazima watazame ROOTS kusudi waelewe history ya mwafrika Marekani na mateso waliopata.
Ukitazama Roots, pia utaweza kuelewa vizuri zaidi matatizo yanayowakabili wamarekani weusi kwa sasa. Matatizo mengi yanatokana na historia yao ya utumwa. Na kwa maoni yangu wengi bado wana mawazo ya kitumwa.
Leo wataonyesha tena TVone sehemu ya nne. Itatoka kwenye DVD May 22.
Karibuni mtoe maoni yenu.

Tuesday, April 10, 2007

Awatukana eti ni Malaya wenye nywele za kipilipili!

Captain wa Timu ya Rutgers, Essence Carson, akiongea na waandishi wa habari leo 4/10/07.

Mbaguzi Don Imus

Ubaguzi hauishi Marekani. Wiki iliyopita kuna huyo mtangazaji maarufu wa Marekani, Donald Imus, kasema eti wasichana wanaocheza basketball kwenye timu ya Chuo Kikuu cha Rutgers ni nappy headed hos (malaya wenye nywele za kipilipili). Alikuwa anaongea na meneja wake kwenye hicho kipindi na walizidi kusema wamejaa matatoo na pia wamekaa kidumedume. Kisa timu ya Chuo Kikuu cha Tennessee iliwashinda katika mashindano ya Basketball ya wanawake.

Mazungumzo enyewe ni hayo:

Imus started the firestorm after the Rutgers team, which includes eight black women, lost the NCAA women's championship game to Tennessee. He was speaking with producer Bernard McGuirk and said "that's some rough girls from Rutgers. Man, they got tattoos . . ."

"Some hardcore hos," McGuirk said.

"That's some nappy-headed hos there, I'm going to tell you that," Imus said.
Pia walisema kuwa eti hiyo timu ya Rutgers inafanana na timu wa wanaume ya NBA, The Toronto Raptors!"

Jana alikutana na Reverend Al Sharpton kuomba msamaha lakini Sharpton alikasirika baada ya Imus kusema, "You People!" (Nyinyi watu weusi). Na Reverend Jesse Jackson naye amekasirika ana anataka Imus afukuzwe kazi. Jackson kasema hiyo siyo 'Slip of the Lip' (Utelezi wa ulimi).

Lakini kwa hapa Marekani kusema kuwa mtu mweusi ana nywele za kipilipili ni tusi kubwa mno! Hii inatokana na asili ya utumwa Marekani. Pia nywele za kilipili inahusishswa na watu wesui hasa weusi tii. Na kama unataka kuelewa kwe undani zaidi ni kuwa hapa USA, unavyozidi kwa weusi ndo unavyoshushwa kwenye hadhi ya ubinadamu. Insikitisha! Weusi wenyewe wanadharau weusi na hasa weusi tii. Unasikia, "You Too black" yaani wewe ni mweusi mno. Ama kweli Imus, kachokoza watu.

Haya mambo ya nywele ni mjadala mkubwa maana utasikia weusi wanasema, yulekichwa chake kimejaa 'naps' (Kipilipili), na yule ana good hair (nywele nzuri), zimekaa kizunguzungu. Biashara ya ku-perm na ku-relz nywele kusudi zinyoke kama mzungu imeshamiri duniani. Hata Bongo watu hawaridhiki na nywele waliozaliwa nayo, unatukuta watu wanakimbilia saluni kupata 'relaxer'.

Na huyo Captain wa timu leo kaonekana na nywele ambazo zimetiwa Relaxer! Zimenyoka kabisa. Ningemheshimu zaidi kama angetoka na Afro. Ni kama vile wanaona haya kuwa na nywele za kiafrika.

Tangu enzi za utumwa hapa Marekani wanasema kama una hata tone moja ya damu nyeusi basi wewe ni mweusi. Unakuta watu ambao ungedhania ni wazungu lakini la, ni weusi! Na kama umetazama ile sinema ya School Daze ya Spike Lee, utaona mgogoro kati ya wanafunzi weusi. Weupe wanajiona bora kuliko wale ambao ni weusi zaidi.

Haya sasa Imus amesimamishwa kutangaza redioni kwa kipindi cha wiki mbili. Watu wanataka afukuzwe maana wanasema kuwa si mara yake ya kwanza kuongea mambo ya kibaguzi. Siku zijazo tutasikia hii 'issue' inaishia wapi.

Kwa habari zaidi mnaweza kusoma hii tukio:



Tuesday, April 03, 2007

TAMWA

Bila shaka mmesikia majina kama Fatma Alloo, Leila Sheikh, Edda Sanga, Maria Shaba, Pili Mtambalike, Wema Kalokola (marehemu), na Ananilea Nkya. Hao ni kati ya waanzalishi wa chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Tanzania, TAMWA. Na mimi ni mmoja wa waanzalishi wa TAMWA (Tanzania Media Women's Association).

Tulitoka mbali maana mwanzoni tulipata pingamizi nyingi kutoka kwa wanawake na wanaume. Tulitukanwa na kuitwa majina ya ajabu kama, 'frustrated women, na malesbo'. Hivi sasa wanaume wakisikia jina la TAMWA wanatetemeka. TAMWA imefanya mengi kutetea haki za akina mama nchini Tanzania na inaendelea kwa nguvu! Tulianzisha kwa ajili ya kusaidia akina mama waliokuwa waandishi wa habari lakini ilikuwa mpaka kutetetea haki za akina mama Tanzania.

TAMWA Oyee!

Hii picha ilipigwa mwaka 1992. Tulikuwa kwenye safari Zanzibar na wageni wetu kutoka vyama vya akina mama mbalimbali barani Afrika. Mimi niko kushoto kabisa na miwani! Pia wamo Edda Sanga (3rd from left, Maria Shaba 5th from left, Halima Shariff 2nd from right). Wengine ni wageni kutoka nje.
Ndo baada ya hii safari iliyofana ilitokea kasheshe kubwa kutokana na picha fulani aliyopiga Muhidini Michuzi, na kuwekwa kwenye front page ya gazeti ya Daily News mpaka ilibidi viongozi wa TAMWA warudi Zanzibar kuomba radhi. Picha eneyewe ilipigwa kwenye shughuli ya mpendwa somo na kungwi mkuu wa Tanzania, Bi Kidude.
Kwa habari zaidi kuhusu TAMWA someni:

Afungwa Marekani kwa kutokuvaa Mask! Anaumwa Kifua Kikuu!


Jamani, leo nimeshutushwa na habari ya Mrusi kufungwa jela tangu mwezi Julai mwaka jana kwa ajili ya kutokuvaa mask hadharani. Jamaa amefungwa huko Pheonix, Arizona. Anaitwa Robert Daniels, na ana miaka 27. Anaumwa ugonjwa hatari wa kifua kikuu (Tuberculosis au TB). Kisa cha kumfunga ni kuwa anaumwa aina ya TB inaitwa XDR-TB. Wanasema kuwa ni drug resistant na haitibiki.

Mahakama ya huko Phoenix, inasema kuwa ilibidi Daniels afungwe kwe vile akikataa kuvaa mask (kizuio kwenye mdomo na pua), akitoka nje na kuwa na watu wengine. Walisema kuwa ana nia mbaya ya kutaka kuambukiza watu huo ugonjwa wa TB kwa maksudi.

Habari zinasema kuwa haijulikani atafungwa mpaka lini na huenda atafungwa mpaka anafia huko jela. Baada ya kusoma hivyo nikasema ni kweli wana haki ya kumfunga hasa kama hiyo TB haina tiba. Wakubwa wanasema kuwa kama watu wengine watapatikana na huo ugonjwa itabidi nao wafungwe.

Wataalam wa afya wanasema kuwa kama mtu anaumwa HIVAIDS (UKIMWI) na akipata huo ugonjwa atakufa siku 25 tu, baada ya kuambukizwa. DUH!

Na walivyo na woga na huo ugonjwa jamaa haruhusiwi kuoga kwenye shower. Anatumia wipes (vifutio). Hana TV, simu wala redio. Anasema kuwa maisha yake huko jela ni mabaya kuliko ya mtu alifungwa kwa kosa la jinai.

Chumba chake kina ventilation ya peke yake na filters za chumba zinachomwa moto, na watu waliojifunika kama vile astronauts! Ama kweli waMarekani hawataki huo ugonjwa usambae na siwalaumu.

Mnasemaje wapendwa wasomaji?

Kwa habari zaidi ya kufungwa kwa Robert Daniels mnawaeza kusoma:


Wednesday, March 28, 2007

Unawafahamu Cavemen?

Original Cavemen:
And Now the Geico Cavemen!


Kama uko Marekani, lazima mmeona yale matangazo ya Geico insurance yenye Cavemen. Cavemen ni aina ya binadamu walioishi hapo zamani za kale. Yaani wale wa mwanzo kabisa baada ya enzi za dinosaurs.

Sasa kwenye hayo matangazo hao Cavemen ni wa kisasa, na mambo yao ni ya kisasa hasa. Huwa matangazo yao yanafurahisha kweli kweli. Kuna ile ambao wanamhoji Caveman fulani na ana kasirika, anavyokasirika mama moja anasema, "Seems like someone woke up on the wrong side of the rock!"

Kuna habari kuwa wanapata TV show yao mwaka kesho. Kwa kweli watu wamefurahi sana kusika habari hizo na wanangojea kwa hamu.

Kwa sasa unaweza kwenda kuwatembelea nyumbani kwao, sijui Manhattan, sijui ni Los Angeles hapo.


From Variety Magazine:

"Cavemen" will revolve around three neanderthals who must battle prejudice as they attempt to live as normal thirtysomethings in modern Atlanta.

Tuesday, March 27, 2007

Tendo la Ndoa




Nina swali. Ile tendo la kukutana mwanume na mwanamke na kufanya mapenzi ina majina mbalimbali. Wengine wanasema ‘ngono’, wengine’ kut-mbana’, wengine ‘majambo’, wengine ‘kufanya’, ‘vituuz’ na majina mengi. Lakini jina nacho shangaa ni hiyo, ‘tendo la ndoa’. Ndo jina la heshima au sijui ndo kuweza kusema bila aibu. Au ndio wamisionari walituletea hiyo jina.

Lakini watu wanaita ‘tendo la ndoa’ wakati tunajua kuwa watu wengi wanafanya kabla hawajafunga ndoa. Na watu ambao hawajafunga ndoa, wanafanya. Mungu sijui aliumbaje binadamu lakini kuvumulia mpaka kufunga ndoa si rahisi, katika jamii zote za dunia. Wanataka wasichana watunze bikra zao (lakini hiyo ni topiki nyingine). Pia watu wanafanya na watu ambao si wake, waume zao, sasa ndo ni tendo la ndoa?

Au wanaita tendo la ndoa kusudi watu wajisikie vibaya wakifanya bila ndoa? Au wanataka walazimaishe wafunge ndoa? Ndoa ni hatua kubwa katika maisha ya bindamu. Na kwa kweli ukifunga ndoa ndo unafanya mapenzi na mwenzako kwa halali. Lakini wengine wanatembea nje ya ndoa zao.

Je huko gesti au hotelini watu wanaombwa cheti cha ndo kabla ya kupewa chumba? Miili ya watu inacheka, eti hatuwezi kufanya mapenzi mpaka tufunge ndoa. Na nadhani ni vigumu sana wanaume waweze kuvumulia mpaka wafunge ndoa, maana mwili unafika ile peak ya ‘maturity’ kabla hawajafika miaka 19. Hebu someni vitabu vya biologia.

Uwongo mbaya, watu wataendelea kufanya bila ndoa. Ile ume ya mwanaume ikisimama akili anakosa mpaka anapata kitu cha kumpooza! Na kuna wanawake nao kuna kipindi fulani wanashindwa kuvumulia lazima wapate kitu tena hali hiyo inatokea bila kufunga ndoa!

Nafungua mjadala, karibuni mtoe maoni yenu.

Monday, March 26, 2007

Marudio - Miaka Baada ya tukio kaniomba Msamaha!

Naona, kuna 'Anonymous' fulani kagusia hii swala ya yalionipata nikiwa jeshini JKT. Watu wengi wamenitumia e-mail kuulizia details. Nimeamua kuibandika tena. Ni posti ya kutoka April 2006. Lakini mjue enzi za JKT, wasichana wengi walinyanyaswa kijinsia, mimi nilikuwa na bahati maana nafahamu wasichana waliokuwa gang raped. Dada fulani, alimkubali afande, alivyomaliza kaita wenzake kwa kusema, "Njooni, Mboga hii hapa!" Yule dada hakuweza kutembea vizuri kama wmezi baada ya hapo!

*****************************************************************************

Nilipokuwa Jeshi ya Kujenga Taifa (JKT) karibu nibakwe na afande Fulani (jina nahifadhi). Lazima niseme kuwa katika kipindi hicho wanaume wengi waliona makambi ya JKT kama ‘buffet’ ya wasichana. Si maafande wa jeshi tu, bali hata viongozi wa serikali walikuwa wanapitia makambi ya JKT kula tani yao!

Mimi nilikuwa Masange JKT, Tabora. Wakati huo huyo jamaa alikuwa ni Kepiteni wa JKT. Nadhani alidhania kwa vile yeye ni kepiteni basi alikuwa na haki ya kutembea na yeyote aliyemtaka. Kwangu aligonga ukuta! Bila shaka alikuwa hajawahi ‘kunyimwa’ mpaka siku hiyo alipokutana na mimi.

Miaka baada ya tukio nikiwa nafanya kazi Daily News mara nyingi nilikuwa napishana naye Posta Mpya. Basi ananisemesha, na mimi namnunia halafu napita zangu kimya bila kumjibu kwa hasira. Siku moja kanisimamisha kaniambia, "Chemi, naomba msamaha, nisemahe tafadhali, kweli nilikukosea!” Aliongeza kuwa miaka mingi imepita hivyo sina sababu ya kuwa na hasira naye! Na mimi nilimjibu, “Mshenzi sana wewe!” nikaenda zangu.

Ikapita kama mwaka mwiingine. Jamaa anaendelea kunisalimia kila nikimpita njiani na mimi kwa uchungu bado nikashindwa kusema kitu. Basi nikafikiria alichoniambia Posta Mpya. Lakini niliona kama jambo hilo linamsumbua. Na nikasema kama Bwana Yesu aliweza kusamehe watu kwa madhambi yao kwa nini mimi nisimsamehe. Basi baada ya hapo ikiwa nikimwona na akinisalimia naitika na naendelea zangu na nikaona kidogo hata yeye alikuwa na raha.

Lakini bado najiuliza kama kitendo chake kilimsumbua miaka na miaka kama ilivyonisumbua mimi.Unauliza ilikuaje mpaka nikajikuta kwenye situation ya kubakwa. Au mnasema nilitaka mwenyewe. Ngoja niwaelezee ilivyokuwa.

Nilikuwa mhudumu Officer’s Mess, mpishi na msafishaji. Huyo jamaa alikuwa ni mgeni kutoka Makao Makuu ya JKT Dar es Salaam. Kwa kweli sikutaka kufanya kazi pale Mess lakini tulichaguliwa special na Matron, mimi kwa vile niijua kupika vyakula mbalimbali hasa za kizungu. Lakini uzuri wa hiyo kazi ni kuwa uanambulia mabaki ya vyakula (leftovers), na mara nyingine kulikuwa hakuna.

Basi huyo Afande alikaa kambini wiki kadhaa. Katika kumhudumia tukawa tunaongea na mimi nikawa namheshimu kama kaka vile. Wala sikusikia mapenzi yoyote kwake. Basi jioni fulani, kanialika chumbani kwake kunywa soda na biskuti na kwa Maongezi zaidi. Sasa kama ulienda jeshi unajua njaa kali unayokuwa nayo. Nikaenda, kanikaribisha vizuri, nilipewa soda na tukawa tunaongea. Basi nikaona mwenzangu anabadilika ghafla! Mara ananikumbatia kwa nguvu, na kunibusu na mengine. Nikajaribu kuaga lakini jamaa hakuniachia. Baada ya ku-plead naye aniachie, kaniachia. Kaomba msamaha na kaniomba niendelee kukaa nimalize hizo soda alizoninulia.

Kama mjinga nikamwamini, nikakaa nakunywa hizo soda. Tukaendelea na Maongezi, kukaa kidogo huyo kanirukia, najaribu kusimama huyo, kanivuta na kuniangusha kitandani! Mimi saa hizo nikawa naogopa kabisa nia yake!Kaniambia eti, “ukipiga makelele najua nitasema nini! Nyamaza! Huna sababu ya kunikatalia!” LOH! Kanizaba kibao! Nikamwuliza kwa nini anaifanyia hivyo, na mimi nilikuwa namwona kama kaka yangu!Hapo sasa ikaniingia. Nabakwa! Loh!

Nilimpiga mangumi na mateke lakini jamaa alikuwa na nguvu huyo kachana chupi yangu! Baada ya hapo, jamaa kashika miguu yangu huko anafoka kwa sauti kama vile anatoa amri “panua miguu! PANUA MIGUU!” Huko katoa ume wake uliyosimama kwenye suruali! Basi kuona sipanui jamaa kaongeza makofi na kafanikiwa kupanua miguu yangu! Kuona kafanikiwa kupanua huyo kajaribu kupenya. Ilipogusa kwangu nilipiga kelele cha kufa! Nikasema, “Nakuufaaaa!”

Heh! Ghafla jamaa kaniachia kaniambia niende. Alisema, “Nimeigusa na ume wangu, unatosha!” Nenda zako! Na ukimwambia mtu najua nitasema nini!”Loh nilikimbia bwenini na giza lile la Masange huko nalia. Wenzangu wananiuliza vipi, nikashindwa niseme nini! Kwanza niliona haya! Fikiria, niliona haya (shame)!Kesho yake nikaenda dispensary na kujiandikisha mgonjwa. Sikwenda kazini Officer's Mess bali nililala bwenini.

Siku iliyofuatia huyo Afande mshenzi kapita bwenini kwetu kaulizia hali yangu, na mimi huko natetemeka kwa woga nikashindwa niseme nini. Alininunulia Orange squash na biskuti na kuzileta bwenini. Sitasahau alivyonitazama! Ilikuwa kama vile anapanga jinsi gani atanipata. Baada ya hapo alimwopoa msichana mwingine na huyo alimkubali kabisa. Akawa analala kabisa huko Officer’s Mess. Hakuna anayemsumbua wakijua ni bibi wa Afisa. Basi, siku za yule jamaa kukaa kambini zikaisha, na yule binti alienda naye Tabora mjini kwa siku kadhaa. Halafu jamaa karudi zake DSM. Yule binti karudi zake kambini! Kumbe alienda bila pass. Alidhania kwa vile yuko na mkubwa hana haja ya pass. Na yule Afande ndo kaondoka kimoja! Maafande waliobakia wacha wamtese huyo binti alivyorudi kambini! Walimtesa kwa Extra drill na mengine mpaka ikabidi Military Police waombe wakuu wamsamehe la sivyo atakufa. Raha yake iliishia kwa suluba! Sijui yule binti alidhania jamaa atamwoa! Kwa nini alimkubali yule mshenzi.

Anyway, kila mtu na vyake. Alivyotoka kwenye suluba tulimwuguza! Siku haizkupita na mimi nilitolewa kazi Officer’s Mess na kupelekwa kwenye kikosi cha Ujenzi na lazima nisema hapo nilifurahi sana. Basi miaka ilipita. Mimi nilikuwa mwandishi wa habari Daily News, tena nilijenga jina. Sasa nikawa napishana na yule jamaa huko kapandishwa cheo na yuko JWTZ. Jamaa anajaribu kunisalimia na mimi napita zangu kimya, namnunia kabisa.

Nilimwona mshenzi, mnyama, na kila kitu kibaya ndo ilikuwa yeye! Angefanikiwa kuingiza na kunimwagia uchafu wake ningejiona mchafu mpaka leo! Miaka kama 20 imepita sasa na bado nina uchungu naye.Jamani nyie wanaume nawaambia kubaka kinaathari zake kwa wanawake. Unataka raha ya dakika na unamwachia mwenzio na uchungu wa maisha! Wengine mpaka wanakuwa wagonjwa wa akili.

Kwa nini nimeamua kuzungumzia kubakwa kwangu hapa, ni kwa sababu naona wasichana wengi wanabakwa, halafu wanaamua kunyamaza kimya. Kisa wakienda polisi na hospitali wanahofia kuambiwa ni Malaya au walitaka wenyewe! Hata mwamanke mwenzako anaweza kukufokea kuwa ulitaka mwenyewe. Tanzania, wanaume walikuwa na usemi wao kuhusu wanawake na ngono. Walisema eti ukimwomba mwanamke halafu akijibu ndiyo, manake ndiyo atafanya. Akisema labda, manake atafanya, akisema hapana, manake hapana. Lakini jamani tendo si inakuwa tamu kama wote mmekubali? Na kama angefanikiwa kuingiza si angeniumiza sana!

Wengine wanasema ningemshitaki. Je, ningemshitaki ingekuaje? Kwanza jeshini mimi ningepewa Extra Drill mpaka niumie au kufungwa jela ya jeshi iliyojaa maji na mbu kusudi niteswe. Kumbuka ilikuwa Tanzania na yule alikuwa ni Kepiteni wakati huo na mimi nilikuwa Private. Hakuna ambaye angekuwa tayari kunisikia zaidi ya wenzangu maPrivate, na yeye alijua hivyo. SHENZI TAIPU!

Thursday, March 22, 2007

Sinema ya '21'



Wapendwa wasomaji, nimepata bahati ya kuwa katika sinema ya '21'. Wahusika wakuu ni Laurence Fishburne na Kevin Spacey. Kwa habari zaidi mnaweza kusoma hapa:

http://www.imdb.com/title/tt0478087/

Naigiza kama mhudumu wa hoteli ya Planet Hollywood. Nitawapa habari zaidi siku nyingine.

Friday, March 16, 2007

Waziri wa Liberia Ajiuzulu baada ya Skandali kumpata!




AIBU KUBWA JAMANI!

Huyo baba mweupe kwenye picha si mcheza sinema, wala porn star. Ni mtu mwenye wadhifa kubwa Afrika!



Huenda mmesikia mkasa uliyompata Waziri wa Mambo ya Rais (Minister of Presidential Affairs) huko Liberia, Afrika Magharibi. Bwana Willie Knuckles, amejiuzulu baada ya picha ya ajabu ya yeye akiwa uchi wa nyama, tena anafanya tendo la ngono na wanawake wawili, kuwekwa kwenye internet! Yaani tendo enyewe infaaa kuwa kwenye sinema ya pono! Picha enyewe inaonekana kama ilipigwa siku nyingi, na huenda waliyoitoa walikuwa na kisa naye.

Picha nimekata (cropping), lakini kwa kusimulia, kuna wanawake wanafanya tendo la kishoga. Kuna mwanamke kalala chale na kuchezea matiti yake mwenyewe huko mwanamke mwingine ananyonya uke wa huyo aliyelala na kupanua miguu, huko huyo Bwana Knuckles anamwingia kwa nyuma (huyo anayemnyonya mwenzake), mtindo wa chuma mboga au dogi!

Ni aibu kwake na familia yake. Kafunga ndoa na mke wake miaka 37 sasa. Je, mke wake atamvumulia baada ya picha hiyo ya matusi kunonekena karibu dunia nzima? Nasema shauri zake! Mke wake akimwacha ana haki maana yeye asingevumilia kuona picha ya mke wake akiwa kwenye shughuli na mwanaume mwingine.

Nashukuru Bwana Knuckles amejiuzulu. Viongozi wanatakiwa kuwa mifano kwa wananchi. Kwa kweli amejiangusha mwenyewe. Natoa pole kwa Rais wa Liberia, Mama Ellen Johnson-Sirleaf kwa kumpoteza mfanyakazi mzuri, na aibu yaliyopata uongozi wake.

Nalaani tabia mbaya na chafu ya wanaume huko Afrika. Kwanza wanaume waafrika wamezidi kupenda ngono, na tena kutoheshimu ndoa zao. Kutembea nje ya ndoa ni sifa na wanajigamba huko kwa wanaume wenzao…oh nimetafuna yule na yule! Khah! Wanaona sifa kutembea na wanawake wengi, eti inawafanya wanaume! Na wanaume walivyo washenzi badala ya kusutana, wana pongezana! Halafu watu wanashangaa kwa nini magonjwa kama UKIMWI yanasambaa kwa kasi. Si siri kuwa kuna viongozi wetu waliofanya maajabu na wanawake wasio wake zao wakiwa katika uongozi. Wakisafiri, wanasema, oh siwezi kulala mwenyewe! Kisa! Na hiyo misafara ya Mwenge enzi zile ndo usiseme, maana ilitembea kila kona ya nchi, mchana shughuli za Mwenge, jioni ‘ngonofest’!

Kwa kweli yaliyompata Bwana Knuckles iwe fundisho kwa watu. Siku hizi kuna internet na unaweza kudhalalishwa dunia mzima katika dakika chache! Kuna picha za cell phone, na vicamera vidogo vidogo, unaweza kupigwa picha na huna habari. Nafahamu jamaa alipanga chumba kwenye hoteli fulani hapa States, kachukua demu wakafanya mambo yao huko, kumbe kuna mfanyakazi wa hoteli alificha video camera huko chumbani. Hawakuwa na habari. Baada ya miaka miwili yule mfanyakazi alikamatwa na kanda nyingi za watu mbalimbali wakiwa kwenye tendo. Bahati nzuri hakuwa anaaziuza bali anazitazamma mwenyewe. Je angekuwa anaziuza. Fikiria unanunua kanda ya X video au DVD, unaanza kutazama na unatambua watu waliyoomo.. DUH!

Duniani kuna mambo ya ajabu.



Kwa habari zaidi mneweza kusoma:





Saturday, March 10, 2007

Wasio na Makaratasi wakamatwa Massachusetts

Jamani, wiki hii wasio na makaratasi wana haha hapa Massachusetts. Ni hivi, siku ya jumatatu walivamia kampuni fulani huko New Bedford and kukamata wasio na makaratasi karibu 400! Tena wengi wao walisafirishwa kwa ndege na kupelekwa kwenye makambi ya wasio na makaratasi huko Texas. Watarudishwa kwao (Deported)!

Cha kusikitisha ni kuwa wengi ya waliokamatwa walikuwa na watoto wadogo. Wamebaki bila wazazi, bila mama au baba. Kuna watu ambao wanawaonea huruma na wengine wanasema shauri zao, maana walivunja sheria kwa kukaa USA bila makaratasi. Na mbaya zaidi, waligundua kuna duka iliyokuwa inauza vyeti feki (social security card na green card) kwa dola $120! Wanaesema wakuu wa hiyo kampuni walishirikiana na wenye duka kuwapatia hao wafanyakazi makaratasi feki!

Lakini jamani, walikuwa wanafanya kazi kwa hela ndogo, na kufanya kazi ngumu. Wanaofanya kazi pale wanasema hata ruksa ya kwenda chooni ni shida. Ukichelewa kazini dakika tano unakatwa mshahara. Hiyo kampuni ilikuwa inatengeneza vifaa vya jeshi.

Wengi ya waliokamatwa wanatoka Guetemala, na El Salvador. Sijasikia kama mwafrika alikuwemo.

Unaweza kusoma habari zaidi hapa:

http://business.bostonherald.com/businessNews/view.bg?articleid=187373&srvc=biz

http://biz.yahoo.com/ap/070306/ma_immigration_arrests.html?.v=1

Thursday, March 08, 2007

Ni Ubaguzi, Uonevu au Upendeleo?

UPDATE: ANTONELLA KATOLEWA ALHAMISI. Alilia kweli. Lakini amepata offers za kupiga picha uchi Playboy magazine na ku-host Girls Gone Wild. Frenchie ata sue American Idol kwa uonevu!
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@



Kwa wapenzi wa American Idol, naomba maoni yenu. Mnakumbuka mwaka 2003, (msimu wa pili aliyoshinda Ruben Studdard) kulikuwa na dada fulani, Frenchie Davis. Huyo dada ni mweusi, mnene na ana zinga la sauti. Yaani anaimba huyo si mchezo, Jennifer Hudson alie kwake.

Kwa bahati mbaya, Frenchie aliwaambia Producers kuwa akiwa mwanafunzi, alipiga picha nusu uchi (topless) kwa ajili ya kupata pesa za kumsaidia kulipia masomo yake Howard University. Producers waliamua kumfukuza kwenye show. Mungu ni mwema na Frenchie sasa ni mwimbaji maarufu kwenye mchezo wa kuigiza, Rent, huko Broadway, New York.

Msimu huu wa American Idol kuna dada fulani, Antonella Barba, ambaye naye ali picha za uchi kwenye internet. Hajafukuzwa na bado yumo. Amepiga picha za uchi kabisa. Kwenye picha zingine anamfurahisha mwanaume kwa kumnyonya ume wake! Zingine kapanua miguu. Loh! Ajabu hajafukuzwa kwenye American Idol.

Sasa imekuwa issue, mpaka Rosie O’Donell anaongelea kwenye show yake The View, yeye anasema kuwa eti ni ubaguzi. Pia wiki hii kulikuwa na maandamano mbele ya Kodak Theater Hollywood kupinga Antonella kuendelea kuwa kwenye show wakati Frenchie alitolewa.
Na Frenchie mwenyewe sasa anataka maelezo kutoka kwa Producers wa American Idol. Anasema kuwa anamtakia huyo Antonella mema lakini ni lazima wamweleze kwa nini alitolewa na kudhalalishwa wakati ule na picha zake siyo mbaya kama za Antonella.

FYI- Producers wanajitetea kwa kusema eti Frenchie alilipwa hela kwa ajili ya zile picha wakati za Antonella zilibandikwa na boyfriend wake.

Mimi navyoona ni ubaguzi. Frenchie ni mweusi na ni mnene. Huyo Antonella ni mwembamba na wanasifia uzuri wake. Lakini jamani uwongo mbaya, Antonella hawezi kuimba.

Mnasemaje wasomaji?

Kwa habari zaidi soma hapa:

http://www.showbuzz.cbsnews.com/stories/2007/03/06/tv_realty_tv/main2540578.shtml?source=RSSattr=Entertainment_2540578