Monday, May 07, 2007

Sinema ya Simu ya Kifo


(Pic 1) Mwongozaji Hammie Rajab, akipungia Camera.
(Pic 2) Ganda la DVD la Simu ya Kifo
(Pic 3) Baadhi ya walioigiza katika sinema la Simu ya Kifo
All Photos courtesy of Michuzi Blog.



Wikiendi hii sinema mpya ya Bongo iitwayo, Simu ya Kifo, ilizinduliwa. Premiere ilikuwa katika ile kumbi maarufu la wasanii, The Little Theatre, pale Oyster Bay.

Kwa vile siko Bongo, bado sijauona. Lakini nasikia ilikuwa nzuri na watengenezaji wamejitahidi sana kusudi iwe sinema na si video. Hongera sana.

Wengi tunafahamu kile kitabu cha Simu ya Kifo, na hii ndo sinema yake. Nitapenda kuona kama sinema ni nzuri kama kitabu. Mara nyingi inakuwa vigumu kwa sinema kushinda kitabu maana kwenye kitabu wanaelezea kwa undnani zaidi na mambo mengi zaidi.
Mlioiona naomba maoni yenu.
Kama hamfahamu zamani Little Theatre ilikuwa 'Exclusive' kwa ajili ya wazungu. Waafrika walikuwa wafanyakazi tu pale. Hata bei ya tiketi waliweka juu kusudi waafrika washindwe kununua. Kulikuwa na sisters, Erica Khuri na Tony Khuri (wote marehemu) walikuwa wanaandaa michezo mara kwa mara pale. Nafurahi kuona weusi kwenye Stage hiyo.


1 comment:

Anonymous said...

nimeona sinema lakini siyo nzuri kama kitabu, imeigizwa kizamani sana, nina DVD yake