Sunday, February 17, 2008

President Bush Visit to Tanzania in Pictures

A Special Sniffer dog, checks out the grounds on the Julius Kambaraga Nyerere Airport in Dar es Salaam, Tanzania, East Africa.
Air Force One carrying President Bush approaches the runway of the Dar es Salaam airport.
A grand welcome awaits President Bush and his wife, Laura.
President Bush and his wife disembark from Air Force One.
President Bush and his host, Tanzanian President Jakaya Kikwete walk on the official Tanzaniana red carpet.

All Photos from Michuzi Blog and were taken by famous Tanzanian photojournalist, Muhidini Issa Michuzi:

President Bush in Tanzania

From Michuzi Blog

2-17-08

American President George Bush arrived in Tanzania last evening to a rousing welcome at the airport and by Dar es Salaam residents, who had lined up the streets for more than five hours to catch just a glimpse of his motorcade.

His visibly thrilled host, President Jakaya Kikwete, and First Lady Salma Kikwete, received President Bush and his entourage at Julius Nyerere International Airport, where normal activity came to a standstill during the welcoming ceremony that took about an hour.

The entire Cabinet, including Vice-President Mohammed Shein, was at the airport as Mr Bush began his four-day State visit. Air Force One touched down at exactly 6.30pm.

Mr Bush was accompanied by First lady Laura Bush and Secretary of State Condoleeza Rice.
He was given a 21-gun salute and the National Anthems of the two countries played by members of the TPDF.

Later, President Bush, who was dressed in a navy blue suit, white shirt and red tie just like his host, inspected a guard of honour.

He also sampled Tanzanian culture as a variety of cultural troupes entertained him at the airport. The US President danced and hugged two dancers as he made his way to the motorcade, comprising specially airlifted Cadillac limousines that drove him to the city.

He arrived from Benin and will leave on Tuesday for Rwanda.

It was a show of might at the airport from the time the two-plane entourage arrived up to when the two-kilometre long motorcade sped to the city centre.

US and Tanzanian security personnel kept everything at the airport under check.

City residents who had gathered along the route from the airport were forced to trek long distances as daladalas were in short supply due to the closure of some roads as part of the security arrangements for the visiting American leader..

Saturday, February 16, 2008

WaKenya wataka Amani



Waimbaji maarufu wa Kenya wameungana na kutoa wimbo huo wa kuomba Amani nchini mwao.

Asante mdau Subi, kwa kunidokeza kuhusu hii video.

Jifunze Lugha mpya!

Kama unataka kujifunza lugha mbalimbali za dunia kuna website mpya ambayo inaweza kukusaidia.

http://www.italki.com

Wanatafuta watu ambao wanaongea Kiswahili kuwasaidia.

Friday, February 15, 2008

Mjue Msanii wa Bongo - Shafii Abdul

Shaffii Abdul in a scene from Bongoland II

Shaffii Abdul (26) ni mwigizaji maarufu nchini Tanzania. Katika sinema ya Bongoland II anacheza kama Hamisi, mdogo wake Juma ambaye ni mhusika mkuu wa sinema. Shaffii amecheza vizuri sana kama mtu mwenye hasira za karibu.

Kusoma habari zake tembelea:

http://bongoland2.blogspot.com/

Gauni ya Arusi zilizotengenzwa na Toilet Paper






Kama mnavyofahamu kununua gauni ya arusi ni ghali. Kumbe si lazima ununue gauni kwa bei ya juu wakati unaweza kutengeneza na kitu ambacho bei ni rahisi kidogo tena ukitumia coupon ni bei rahisi zaidi.

Hapa Marekani ukienda dukani kununua toilet paper kuna kila aina. Kuna Charmin, kuna double ply, kuna quilted, zenye michoro na ngumu na laini. Mwaka jana kulikuwa na mashindano ya kutengeneza gauni ya arusi na Toilet paper baadala ya kitambaa. Ila nauliza hivi, ukitoka majasho hiyo gauni haitayeyeyuka huko umeivaa. Maana Toilet paper inaanza kuharibika (disintergrate) mara mkitia maji!

Hizi ni baadhi ya picha zilizoshinda. Kuona design zingine bofya hapa:

Raisi Bush matakoni Mwetu!

Picha na Caption kutoka Food For Thought Blog

Maandalizi ya ujio wa rais George Bush wa marekani yamepamba moto kwa njia mbalimbali kama kanga hii yenye maneno ya kumkaribisha rais huyo nchini ambayo imetolewa rasmi kwa ajili ya mapokezi yake. Picha na Mpoki Bukuku

****************************************************************************

Wapendwa wadau, nawauliza hivi, "WHO IS KISSING WHO'S ARSE HERE?"
Duh, Rais Bush atablow kuona picha yake kwenye matako makubwa ya wanawake wa kiafrika! Wazungu wanavyochukia matako makubwa halafu sasa picha ya rais Bush hiyo! Nadhani TMZ na stesheni zingine, akina Leno na Letterman watafanya utani kweli hapo! Utasikia utani kuhusu, 'sit on it'.
Khanga siyo mbaya ila mmh kuna watu hawapendi kuona uso ya huyo Bush kutokana na vitu alivyofanya kama kuanzisha vita isiyo na maana huko Iraq! Lakini watasema iko where it deserves to be, on an arse!

Thursday, February 14, 2008

Leo ni Siku ya Wapendanao - Valentines Day!



Mkumbuke mpenzi wako siku ya leo!


HAPPY VALENTINES DAY!

Kiswahili Kigumu


Hii nimepata kwenye e-mail:

A famous American preaching couple (Mr & Mrs Stumbles) resorted to using a Mr. Hamisi for translation once they failed to get a proper bi-lingual local in Lamu.....the preaching had the following translation.

STUMBLE: Everything comes from above.!!
HAMISI: Vitu vyote huja juu juu,

STUMBLE: So you see my brothers and sisters
HAMISI:.......Basi ndugu zangu waangalieni akina dada,

STUMBLE: know perfectly well,
HAMISI:.....Na muwajue vizuri sana,

STUMBLE: That all world affairs,
HAMISI:.........Kwamba mapenzi yote duniani,

STUMBLE: are successfull only if held from above,
HAMISI.............Hufanikiwa tu ikiwa mmeshikana juu juu.

STUMBLE: Remember, faith is your pillar,
HAMISI:...Kumbuka kuuamini mlingoti wako,

STUMBLE: Keep it first and above,
HAMISI:..............uuweke kwanza juu juu.

STUMBLE: Let it run very deep and stong,
HAMISI:...............Ndo kisha uukimbize ndani kabisa tena kwa nguvu,

STUMBLE:Should anybody want to test you,
HAMISI:..............Mtu yeyote akitaka kukuonja,

STUMBLE:......will feel its work,
HAMISI:...............Ataisikia kazi yake

STUMBLE: Then from deep inside you'll feel peace pouring out,
HAMISI:........ndo kisha baadaye utasikia kutoka ndani sehemu moja ikimwagika nje,

STUMBLE: That peace will flow and enter even those you are with,
HAMISI:.......Sehemu hiyo ita tiririka na kumwingia uliye naye,

STUMBLE: and that peace will remain.
HAMISI:..............Na sehemu hiyo itabakia.

STUMBLE: Amen.
HAMISI:............Huyo ni mwanamme.

Wednesday, February 13, 2008

Kipanya Anasema...


Duh! Nimeblow na hii! Yaani anamwita PM 'Beast'? Kweli kuna uhuru wa vyombo vya habari Bongo siku hizi maana Mwalimu asingevumilia. Wadau mnasemaje?

Ukatili wa Polisi Florida!

Deputy Charlette Marshall-Jones (mugshot)








Huko Tampa Florida, polisi wa kike, deputy Charlette Marshall-Jones, 44, alimwaga chini mwanaume aisyejiweza na anayetumia wheelchair.

Huyo Marshall-Jones alimwambia Brian Sterner (32), asimame ingawa alimwona yuko kwenye wheelchair. Sterner alimwambia kuwa hawawezi kusimama ndipo huyo katili Charelette Marshall-Jones, alimwaga chini! Alitenda maovu yaka January 28, 2008 lakini jana ndo waandishi wa habari walizipata na kusambaza habari. Wakuu wa polisi eti hawakuwa na jabari mpaka walipoambiwa na waandishi wa habari!

Sterner ni Quadraplegic. Alipata ajali miaka 14 iliyopita akiwa anacheza wrestling na kuumia shingo. Hawezi kutumia viungo vyake chini ya kifua ndo maana anatumia wheelchair. Hatua ya kishenzi ya huyo mama zingeweza kumwua mgonjwa kama huyo. WaBongo waliopitia home health aide wanajua jinsi ya kuwageuza na kushugilia wagonjwa kama huyo. Ajabu ukiona hiyo video polisi wengine wanacheka!

Kisa cha Sterner kupelekwa Polisi - alikuwa anatuma gari maalum kwa ajili ya maquaraplegic, ilmgomea barabarani. Alikuwa anashitakiwa kwa kuzuia magari kupita.

Kwa sasa watu wanaoiona hiyo video wamechukia mno! Wanataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya huyo polisi mshenzi, msimamizi wake na polisi wengine waliokuwepo huyo mama alivyofanya ushenzi wake! Habari zinasema polisi wanne wamesimamishwa kazi kuhusiana na tukio huo. Huyo mama anastahili afukuzwe kazi na afunguliwe mashitaka!

Yaani nchi hii inaoza mpaka watu wanakosa huruma!

Kuna Video ya tukio bofya hapa:

Kwa habari kamili ya tukio soma:





Tuesday, February 12, 2008

Flaviana Matata


Picha Asante Michuzi Blog

Miss Universe Tanzania, 2007, Flaviana Matata (20), alienda Budapest, Hungary hivi karibuni kwenye sherehe ya Budapest Opera Ball. Ni sherehe inayofanyika kila mwaka na ni tafrija yenye hadhi kubwa nchini Hungary. Wanasiasa, wakuu wa nchi, mabalozi na watu mashuhuri kutoka nchi hiyo na jirani barani Ulaya huhudhuria. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mrembo kutoka Afrika kuhudhuria hafla hiyo.

Sasa kuhusu ombi la Michuzi kwa msaada kwa Flaviana kuendelea na Modelling. Namshauri apeleke habari zake, Trump Model Management. Sasa hivi wanae MSudani Artong Arjok.

Hiyo kazi ya modelling ni know-who na namshauri pia afanye networking kali akiwa safarini. Hao warembo wenzake wanaweza kumsaidia pia.

Namshauri pia ajifunze lugha mbalimbali pia kama Kifaransa, Kispanish, Kijereumani. Sijui ana kipaji gani cha Kiingereza, maana kwenye Miss Universe waliweka Sub-titles alivyokuwa anaongea.
***********************************************************************************
OMBI LA KAKA MICHUZI
Mrembo wetu hivi majuzi alialikwa hungary kuhudhuria hafla maalumu ambapo warembo wa dunia nzima walialikwa kushiriki. hizi ni baadhi ya picha za safari hiyo inayoonesha kwamba bado flaviana anatambulika kama mmoja wa warembo bomba duniani baada ya kushika nafasi za juu miss universe mwaka jana. tatizo hadi leo anasota waya bongo wakati wenzie wote wamepata nafasi za kufanya kazi na kampuni kubwa za mitindo. mdau mwenye uwezo ajitokeze amsaidie kuendeleza kipaji chake. unaweza kuwasiliana nami kupitia issamichuzi@gmail.com nitafikisha ujumbe. hima wadau na tumsaidie mrembo wetu huyu aliyelera sifa kwa nchi hii. asije akaishia hapo alipo kwani umri wake bado wa miaka 20 unadai kabisa kufanya maajabu zaidi kwenye ulimbwende.

Baraza Jipya la Mawaziri!

Kutoka ippmedia.com

BREAKING NEWS: Baraza jipya la Maziri latangazwa

2008-02-12

Na Mwandishi Wetu

Rais JK ametangaza Baraza jipya la mawaziri, baada ya kuvunja baraza la mawaziri ya kufuatia Edward Lowasasa kujiuzulu baada ya kukumbwa na kashfa ya Richmond. Akizungumza katika ukumbi wa Tamisemi mjini Dodoma amesema baraza hilo limepunguzwa na kubakia na Mawazirii 26 badala ya 29 wa awali na Manaibu 21 badala ya 31.

(Menejimenti utumishi wa umma) Hawa Ghasia.

(Ofisi ya Rais muungano) Seif Mohamed Khatib.

(Mazingira) Batilda Burian.

(Ofisi ya waziri mkuu utaratibu wa bunge) Philipo Marmo.

(Tamisemi Tawala za mikoa na serikali za mitaa) Stephen Wasira, naibu Serena Kombani.

(Wizara ya mipango na Fedha) Mustafa Mkulo, manaibu Jeremia Sumari, Omari Yusuph Mzee.

(Afya na ustawi wa jamii) Prof Mwakyusa, Naibu Asha Kigoda.

(Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi) John Chiligati.

(Elimu na mafunzo ya ufundi) Prof Jumanne Maghembe, Manaibu Gaudensia Kabaka , na Mwantum Mahiza.

(Mawasiliano na Sayansi na Technologia) Shukuru Kawambwa Naibu Maua Daftari.

(Miundo mbinu) Andrew Chenge, Naibu Milton Mahanga.

(Habari Utamaduni na Michezo) George Huruma Mkuchika, Naibu Joel Bendera.

(Kazi Ajira na maendeleo ya Vijana) Prof Juma Kapuya, Naibu Ezekiel Chibulunje.

(Maji na Umwagiliaji) Mark Mwandosya, Naibu wake ni Engineer Christopher Chiza.

(Kilimo Chakula na Ushirika) Peter Msola, Naibu Mathayo David Mathayo.

(Maendeleo ya jamii Jinsia na Watoto) Magreth Sitta naibu Lucy Nkya.

(Maendeleo ya mifugo na uvuvi) Johhn Pombe Magufuli, Naibu DR. James Wanyancha.

(Maliasili na utalii) Shamsa Mwangunga, Naibu Ezekiel Maige.

(Mambo ya Ndani) Lawrence Masha, naibu Hamis Kagasheki.

(Wizara ya Sheria) Mhe. Matthew Chikawe.

(Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa) Bernard Membe, naibu Seif Ally Idi.

(Wizara ya madini) Wiliam Ngereje, Naibu ni Adam Malima.

(Wizara ya Ulinzi) Hussein Ally Mwinyi, Naibu Emmanuel Nchimbi.

(Wizara Ya Afrika Mashariki) Dr. E Kamala.

(Viwanda na Masoko) Mary Nagu, Naibu Cyril Chami.

Awali kabla ya kutangaza baraza hilo Rais Kikwete alisema kuna mawaziri walioomba kupumzika baada ya kutumikia serikali kwa muda mrefu na watabaki katika kushauri tu. ambao ni Mzee Kingunge Ngombare Mwiru, na Joseph Mungai.

SOURCE: Alasiri

Monday, February 11, 2008

Vituko Vya Michael Jackson

Michael Jackson kabla hajajiharibu kwa plastic surgery na vidonge vya kubadilisha rangi ya ngozi na dawa za kuogea za kubadilisha rangi.
Michael Jackson na mkwe wake wa wahakti huo, Debbie Rowe. Rowe alikuwa ni nesi wake na alimzalia watototo watatu. (Hao watoto ni wa Jackson kweli?)
Michael Jackson na watoto wake Prince na Paris wakiwa wamejifunika ushungi.
Watoto wa Jackson, Paris and Prince Michael walivyo leo.

Mke wa zamani wa mwimbaji maarufu Michael Jackson ambaye pia ni mama watoto wake, Debbie Rowe (49) amekasirika mno! Kisa, watoto aliyozaa na Jackson, wamepigwa picha bila kufunikwa ushungi.

Anasema kuwa walivyokuwa wadogo watu walitiisha kuwateka hao watoto. Sasa wanajua walivyo itakuwa rahisi wao kutekewa.

Baada ya kuwaona watu wanauliza kama hao kweli ni watoto wa Michael Jackson. Au ni kweli huyo Debbie Rowe alifanyiwa Artificial Insemination (kuchomwa sindano zenye shahawa/mbegu) ukeni. Si siri kuwa Jackson hakupenda weusi wake, pua kubwa, nywele za kipilipili, rangi yake. Ndo maana kajiegeuza kuwa kinyago.

Si ajabu Jackson alimchagua baba watoto wake na alinunua hiyo shahawa! Watu waliozoea kuona watu mixed wanajua kuwa lazima hao watoto watakuwa na rangi kiasi na curly hair. Hao nywele zao zimenyoka kizungu! Hebu cheki mifano ya watu mixed, kama Halle Berry, Shemar Moore, Barack Obama, na Derek Jeter. Wataalamu wa DNA wanasemaje hapo?

Kwa habari zaidi someni:

http://www.foxnews.com/story/0,2933,330232,00.html

http://breakingnews.iol.ie/entertainment/story.asp?j=245984520&p=z45985zz6

Mh. Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda

Mh. Rais Jakaya Kikwete na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda
Mh. Rais Kikwete akisalimiana na baba mzazi wa Mh. Pinda, Mzee Xavery Kayanza Pinda, na mama mzazi, Bi Albetina Kasanga.Mke wa Waziri Mkuu, Mh. Pinda, (kushoto) Tunu Rehani Pinda akiongea na mbunge wa Viti Maalum Martha Mlata mara baada ya sherehe za kumwapisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda zilizofanyika ikulu ndogo ya Chamwino Dodoma.

(picha asante Michuzi blog)

Sijui ni furaha gani wazazi wa Mh. Pinda walionayo kumwaona mwanao anakuwa Waziri Mkuu. Mungu awabariki.

Na nasema hivi, jumatatu ya wiki iliyopita, Mh. Pinda alijua atakuwa Waziri Mkuu? Kweli huwezi kujua mipango ya Mungu.

Na wameumbua skandali ya Richmond, je wataumbua skandali ya machimbo ya madini?

Saturday, February 09, 2008

Marudio - Tupende Urembo Asili




Baada ya kuandika kuhusu matako makubwa, na kusoma feedback yenu, nimeona niongee kuhusu mashindano ya urembo. Asante kaka Ndesanjo kwa kunichokoza!

Hivi karibuni Miss Tanzania 2005, Bi Nancy Sumary alienda kwenye mashindano ya Miss World na kafanikiwa kutwaa taji la Miss Africa. Kwa kweli lazima nimpongeze maana toka mashindano ya Miss Tanzania ifufuliwe miaka ya 90, hakuna Mtanzania aliyefanikiwa kuingia katika raundi za fainali na hata kutwaa taji lolote.

Kwa kweli Tanzania imepata sifa kubwa katika dunia ya mashindano ya U-Miss. Pia Tanzania imepata sifa kuwa ina wanawake wazuri, lakini nauliza ni uzuri wa aina gani? Maana sioni kama ni uzuri unayafuata maadili ya kiafrika bali ni uzuri wa kizungu!Nikitazama picha na kanda za video za Miss Ilala, Miss Kinondoni, Miss Utalii, na mashindano mbalimbali za u-Miss huko Tanzania nashangaa nachoona. Kwa kweli naona wasichana weusi wakijaribu kuiga wazungu!

Wengine wanapaka make-ups usoni ambazo zimetengezwa kwa ajili ya wazungu wakati make-up za weusi zipo. Yaani ni vichekesho mpaka wengine wanaonekana vituko. Najua hapo niatambiwa nawaonea wivu lakini si kweli na naomba mnisikilize kabla ya kunipa hukumu.

Kwanza tutazame hao wanaopelekwa na nchi zao katika mashindano hayo. Ukiangalia walio kwenye Miss World na Miss Universe, washindi wote wana hulka (characteristics) za kizungu. Tutazame waafrika wanaoenda, cheki nywele zao, zinafanana na wazungu, yaani zimenyoka kabisa. Na kama tunavyojua, sisi wenye asili ya Afrika nywele zetu ni za kipilipili. Hawa wanaweka dawa au weave! Wanaficha nywele zao za asili, sijui wanazionea haya.

Je, wanaona haya kusuka nywele zao au kuonyesha mtindo wa nywele enye asili ya Afrika?Haya, tutazame shepu zao, wote ni wembamba, hakuna mnene, hata hips za maana hawana. Na kama ana matako ni kiasi, sio ile boxi, wowowo, yokohama inayopendwa Africa. Yaani wanafanya mazeoezi eti kusudi wapunguze matako yao.

Na hao weusi kutoka Marekani na Ulaya wanafanya liposuction na surgery kupunguza matako yao asili, eti iwe ya kizungu fleti. Huko Afrika tunasema mtu mwembamba ana shida, hana raha, mgonjwa, lakini mzungu anasema ni uzuri. Na sisi tunaiga! Basi unakuta akina dada hata Tanzania, “Oh nafanya diet!” Kheh! Kisa anataka kufanana na mtu amliyemwona kwenye gazeti.

Hawajui kuwa hizo picha zinafanyiwa editing na air brushing. Kwa hiyo dada zetu wanashinda njaa kusudi wawe wembamba! Hawajui kuwa hao wanaofanikiwa kwenda kwenye u-Miss, wanajitapisha, na kujinyima chakula kusudi wasinenepe, na ukweli hawana raha.

Haya tuangalie wanavyotembea na kuongea…wanaongea na kutembea kizungu! Jamani na hata macho hawasahau, maana wanatia contact lenses zenye rangi ya bluu na kijani kusudi wawe na macho ya kizungu! Doh! Matokeo ni kuwa hao siyo watu tena bali na madoli.

Na kuhusu rangi ya ngozi, ni lazima niulize, je, umewahi kuona mshindi mweusi tii? Hao weusi wanaofanikiwa wengi ni weupe. Basi hao dada zetu wanajichibua na madawa ya ajabu. Ubaya ni kuwa usoni wanaonekana weupe lakini miili yao bado rangi yao ya asili. Mwisho wanakuwa na rangi mbili. Halafu wengine baadaye wanajikuta wana kansa ya ngozi shauri ya dawa hizo za kujichibua.Ubaya ni kuwa kama nchi ya kiafrika inataka kushinda mashindano kama Miss World, Miss Universe ni lazima mtu wao awe Mdoli wa kizungu.

Mfano, miaka mingi Nigeria walikuwa wanapeleka mrembo wao ambaye alikuwa mrembo Nigeria lakini mbaya kwa wazungu. Mwaka 2001, waliamua kumpeleka Mdoli wa kizungu, yaani dada fulani, mwembamba, futi sita na kashinda. Na tazama kesi ya aliyeshinda Miss Universe 1996, Miss Venezuela, Bi Alicia Machado…baada ya kashinda, alinenepa kweli! Yaani aliongezeka kama kilo 20! Basi majaji wakasema watamvua taji lake kama hatapungua! Dada wa watu alilia na kusema kachoka kashinda njaa!

Na tuanganlie hatima ya hao wanaoabudu hiyo standard ya kizungu na kuwa wembamba. Wanapambana na magonjwa kama Osteoperosis, yaani ugonjwa wa mifupa kuvunjika kwa urahisi, utapialmlo, na magonjwa wa akili. Ndiyo, mtu ambaye kila saa anawaza kujikondesha na kuwa hatapendwa kama si mwembamba ana ugonjwa wa akili.

Je, madaktari huko Tanzania wako tayari kutibu hayo magonjwa wa kisasa?Mashindano ya U-Miss yataendelea kuwepo, na dada zetu wataendelea kutaka kushindana na kufanana na madoli wa kizungu. Bahati mbaya ndo dunia ya leo. Lakini napendekeza tuwe na mashindano ya Miss Bantu, Miss Tanzania asili pia. Mashindano hayo yawe na nia ya kusifia uzuri asili wa mwanamke wa kiafrika. Tusisahau tulikotoka. Na hao wazungu wakiona tunajipenda basi wao wataanza kuheshimu maadili zetu.

UPDATE - Flaviana Matata aliwakilisha Tanzania kwenye Mashindano ya Miss Universe 2007 na kufika kwenye Top 10. Bado wanamzunguzia.

Thoughts for 2008

Asante Mdau Subi.:

Number 10
Life is sexually transmitted.

Number 9
Good health is merely the slowest possible rate at which one can die.

Number 8
Men have two emotions: Hungry and Horny. If you see him without an erection, make him a sandwich.

Number 7
Give a person a fish and you feed them for a day, teach a person to use the internet and they won't bother you for weeks.

Number 6
Some people are like a Slinky .. Not really good for anything, but you still can't help but smile when you shove them down the stairs.

Number 5
Health nuts are going to feel stupid someday, lying in hospitals dying of nothing.

Number 4
All of us could take a lesson from the weather. It pays no attention to criticism.

Number 3
Why does a slight tax increase cost you $200.00 and a substantial tax cut saves you $30.00?

Number 2
In the 60's, people took acid to make the world weird. Now the world is weird and people take Prozac to make it normal.

And The Number 1 Thought For 2008:

We know exactly where one cow with Mad-cow-disease is located among millions and millions of cows in America but we haven't got a clue as to where millions of illegal immigrants and terrorists are located. May be we should put the Department of Agriculture in charge of Immigration.

Friday, February 08, 2008

Waziri Mkuu Mpya ni Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda!


Maelezo mafupi ya Mh. Pinda Bungeni leo:


WAZIRI MKUU MTEULE MH. PINDA AMESEMA YEYE NI MTOTO WA KWANZA KWENYE FAMILIA YAO NA ANA SHAHADA YA SHERIA YA CHUO KIKUU NA KWAMBA AMEFANYA KAZI KAMA MSAIDIZI WA RAIS IKULU TOKA ENZI ZA MWALIMU KWA MIAKA 7, KWA ALHAJI MWINYI MIAKA 10 YOTE NA MIAKA KAMA MITANO KWA MH. MKAPA KABLA YA KWENDA JIMBONI KWAKE MPANDA KUOMBA KURA KUWA MBNGE MWAKA 2005.

Kipanya anasema....


Nani atakuwa Waziri Mkuu sasa?

Mara Mh. Lowassa alipotangaza kujiuzulu kwake, wananchi walianza kuulizana na kutabiri nai atakuwa Waziri Mkuu mpya.

Je, ingefaa arudishwe mtu mwenye uzoefu na hiyo kazi nzito. Wapo Mzee Malecela , Mzee Sumaye na Mzee Warioba. Je, Mzee Salim Ahmed Salim?

Je, Rais Kikwete atamchagua mtu mgeni kabisa? Je atamchagua mwanamke?

Kuna maswali mengi na kuna watu ambao watashikwa na homa wakiwaza mrithi wa Lowassa.

Nacho weza kusema ni kuwa wananchi na TZ Diaspora watamweka chini ya darubini (microscope).

Mungu ambariki na kumpa nguvu atakayeteuliwa kuwa Waziri Mkuu mpya.

Mungu Ibariki Tanzania na Watu Wake.

****************************************************************************

Kutoka ippmedia.com

Wananchi wanong`ona wanaofaa kumrithi Lowassa '

2008-02-08

Na Mwandishi Wetu

Kufuatia Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa, kutangaza kujiuzulu, wananchi wamekuwa na shauku kubwa ya kujua nani atakayemrithi endapo Rais Kikwete atamkubalia. Hata hivyo, kumekuwa na majina ya mawaziri kadhaa wa kuchaguliwa yaliyokuwa yakizungumzwa zungumzwa kwamba wanafaa kumrithi Bw. Lowassa.

Miongoni mwa majina hayo ni pamoja na la Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. Bernard Membe, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. John Magufuli na Waziri wa TAMISEMI Bw. Mizengo Pinda.

Mwingine aliyetajwa ni mbunge wa Sumbawanga, Bw. Paul Kimiti.

Aidha wananchi wengi walizungumzia kuwepo haja ya kuteuliwa Waziri Mkuu mwanamke. Wanawake waliotajwa ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, Getrude Mongela na Anne Kilango Malecela.

SOURCE: Nipashe
Kumbe Lowassa hakupendwa! Nasikia watu walifanya parties za kusherekea kuondoka kwake. Tutajua huko mbele mambo yatakavyokuwa, lakini wazungu wanasema, "Be Careful What you Wish For".

Tuone kama pesa zilizopotea/kuibiwa zitapatikana na kurudishwa serikalini. Je, Serikali wata-sue hiyo kampuni ya Richmond Printerrs?



*************************************************************************
Kutoka Ippmedia.com

Dar yazizima kwa furaha Lowassa kujiuzulu

2008-02-08

Na Waandishi Wetu

Jiji la Dar es Salaam, jana lilizizima kwa mayowe na vifijo vya furaha huku madereva hasa wa teksi, wakipiga honi baada ya kusikia Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake.

Miongoni mwa maeneo yaliyozizima kwa furaha ni ya benki ambako televisheni zilifunguliwa huku kipindi cha Bunge kikiwa kinaendelea wakati wa asubuhi. Maeneo mengine ni ya vituo vya mabasi ambako kuna migahawa iliyo na televisheni, watu walijazana kuangalia wabunge wanavyochangia sakata la Richmond huku hamu ya wengi ikiwa ni kusikia kauli zinazotolewa na wabunge baada ya Kamati Teule ya Bunge, kumtangaza Waziri Mkuu kuwa miongoni mwa watuhumiwa wakubwa wa mkataba bomu wa Richmond.

Wananchi wengi walijazana kwenye magari yenye redio kusikiliza kauli hiyo ya Waziri Mkuu. Katika Benki ya CRDB makao makuu, wafanyakazi wa benki hiyo pamoja na wateja waliokuwemo ndani kupata huduma, walilipuka kwa shangwe baada ya kumsikia Bw. Lowassa akitangaza azma yake ya kuachia ngazi.

Ilibidi hata huduma za benki hiyo zisimame kwa takriban dakika tatu kutokana na wafanyakazi wake kuziacha kompyuta na kuanza kuruka ruka wakionyesha hisia zao kutokana na uamuzi huo mzito wa Bw. Lowassa.

Kelele hizo ziliwashtua hata watu wengine ambao hawakuwa wakifuatilia mjadala huo wakidhani kuwa kuna jambo lisilo la kawaida limetokea. Hali kadhalika, wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), nao walisitisha masomo na kuanza kupiga kelele za furaha baada ya kusikia Bw. Lowassa ametangaza kumwandikia barua ya kujiuzulu Rais Jakaya Kikwete.

Vile vile, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaaam, walikuwa wamekusanyika makundi kwa makundi wakijadili kwa furaha, tangazo la Bw. Lowassa la kumwandikia barua ya kujiuzulu Rais Kikwete. Katika kujadili kwao, wanafunzi hao walitaka vigogo wengine waliotajwa kuhusika katika kashfa hiyo, kujiuzulu pia na sheria ichukue mkondo wake.

Katika eneo la Feri, nako hali ilikuwa hivyo hivyo kwani wachuuzi wa samaki walikusanyika huku wakishangilia kwa mbwembwe. Bw. Omar Abdallah aliishauri serikali kuwa, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu isiwe ni danganya toto, kwani haitoshi, lazima sheria ichukue mkondo wake ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zake.

``Serikali iwawajibishe mawaziri wote waliohusika na ufisadi huu. Ameanza Lowassa anayefuatia awe Karamagi ili wananchi waendelee kuwa na imani na serikali yao,`` alisema Bw. Said Hussein. Naye

Bw. Athuman Bakari alisema kujiuzulu siyo sababu ya kukwepa kujibu tuhuma zinazomkabili. ``Aisee, unaweza kudhani ni Simba kamfunga Yanga au Yanga kamfunga Simba. Hii ni dalili kuwa wananchi wamechukizwa na ufisadi uliofanywa na kampuni hiyo ya Richmond kwani matokeo yake ni maumivu kwa wananchi kupandishiwa bei ya umeme.

``Tunashindwa hata kutumia vifaa vyetu kama majiko ya umeme kutokana na bei ya umeme kuwa kubwa,`` alisema Bw. Bakar Awadhi. Aidha kwenye daladala gumzo kubwa lilikuwa ni kauli ya Waziri Mkuu kuchukuwa uamuzi huo. Wengi walionekana kufurahia uamuzi huo, ingawa baadhi walimpongeza kwa maamuzi yake, ambayo ni nadra sana kufikiwa na viongozi wakubwa hasa wa Kiafrika.

SOURCE: Nipashe



Thursday, February 07, 2008

Hotuba ya Mwisho ya Mh. Lowassa Bungeni


IFUATAYO ni hotuba fupi aliyoitoa Waziri Mkuu Edward Lowassa katika Bunge mjini Dodoma leo (Alhamisi Feb. 7, 2008) asubuhi, wakati wa mjadala wa Taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi "Richmond Development Company LLC" ya Huston, Texas, Marekani mwaka 2006:

"Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii.


Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison Mkwakyembe, Mwenyekiti wa kamati Teule kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli.


Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa. Mheshimiwa Dk. Mwakyembe ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni "Natural Justice".
Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.
Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu hata kama wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.

Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini kwamba wanaweza wakafanya oversite kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga wamesema Waziri Mkuu ilikuwa hivi. Kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza Waziri Mkuu wanasema uliotoa dokezo hili ni sawa sawa kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa Westminster kuthibitisha hapo unaposema mwenye Richmond ni fulani uka-lay on the table records na ushahidi kuwa ni fulani.

Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe. Kama katika chombo hiki haki haitaonekana kutendeka nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia. Kwa nhiyo nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba naona si sahihi, nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana, nimeonewa sana katika hili.
Maana zimechukuliwa tuhuma zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijauliza. Kulikuwa na shida gani kuniuliza, kwa nini muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo yangu. Sisi wote hapa ni wanasiasa tukianza kuamini minong'ono ya mitaani niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi, Tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini hata pale uliponinong'oneza ukaniambia una ushahidi wowote? Nilikupa ushahidi huo wa maandishi. Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka Waziri Mkuu. Kile kitabu cha majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na magazeti mpaka ya Udaku lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika, naamini ingekuwa ni heshima wangeiweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii, hiyo ndiyo imejengwa hoja. Lakini kujenga hoja na kuja hapa Bungeni tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu wa chini itakuwaje?

Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi kulikoni mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo kulikoni? Mimi nadhani there is a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe.

Mheshimiwa Spika, nimetafakari kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi. Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini kutokubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya Bunge wa kumsingizia mtu.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais kwa heshima aliyonipa ya kutumikia nchi hii kwa Uwaziri Mkuu kwa miaka miwili.
Namshukuru sana Mheshimiwa Rais.

Nakushukuru wewe, nawashukuru Mawaziri na Manaibu Waziri, nawshukuru Waheshimiwa Wabunge na wanachama wa CCM tuliyosimamia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nashukuru".

Hotuba ya Rais Jakaya Kikwete - Februari 7, 2008 -SAMAHANI

Wapendwa wadau, naomba mnisamehe hapo.

Ilikuwa usiku na siku verify kama Mh. Rais alisoma speech kweli. Nimegundua ni usanii unaozunguka kwenye internet.

Baraza la Mawaziri Lavunjwa!!!!


Rais Jakaya Kikwete, kaonyesha waTanzania kuwa hana mchezo. Amevunja Baraza la Mawaziri!

Pia amekubali ombi la kujiuzulu uwaziri mkuu, Mheshimiwa Edward Lowassa.

Kuona Baraza la Mawaziri lilliyovunjwa bofya HAPA:

Cheche zimetembea Bungeni tangu ripoti ya Mheshimiwa Dr. Harrison Mwakyembe kusomwa Bungeni jana. Ripoti ilihusu sakata la umeme na kampuni tapeli la Richmond.

Kusoma Ripoti hiyo bofya HAPA:

Mwalimu Nyerere aliwahi kuvunja Baraza lake la Mawaziri.

Kampuni ya Richmond - Utapeli Mtupu!

Jamani, lazima niwakumbushe kuwa tangu hiyo deal ya Richmond itangazwe, wanablogu hasa kwa Michuzi walikuwa wanasema kuwa hiyo kampuni ni feki. Kuna wanablogu waliofanya uchunguzi wao kabisa. Lakini dili iliendelea! Wanablogu walichambua mpaka bei ya vifaa. Serikali ingewasikiliza tusingekuwa hapa leo tunaongelea hii habari ya kusikitisha.

Leo mambo ndo yameharibika kwa wahusika. Sijui kwa kimombo tuseme mambo yame 'explode' ame 'implode.'

Habari za Lowassa na Richmond imekuwa habari za kimataifa.


***************************************************************************

Kutoka http://abdallahmrisho.blogspot.com/

HAKUNA hapa nchini wala Marekani, kampuni iliyosajiliwa kwa jina la Richmond Development Company LLC. Bunge lilielezwa jana.

Mwenyekiti wa kamati Teule ya Bunge ya kuchunguza mchakato wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura ulioipa ushindi kampuni hiyo, Dk, Harrison Mwakyembe alibainisha hayo bungeni mjini Dodoma jana.

Akiwasilisha muhtasari wa taarifa ya kamati hiyo, Dk. Mwakyembe alisema uchunguzi umeonyesha hakuna kampuni yenye jina hilo iliyosajiliwa katika jimbo la Texas nchini Marekani wakati wa kusaini mkataba huo.

“Kamati teule imejiridhisha kuwa hakuna kampuni yenye jina la Richmond Development Company LLC iliyokuwa imesajiliwa JImbo la Texas wakati wa kusaini mkataba huo hadi tunapowasilisha ripoti hii…” alisema.

Alisema hitimisho lilifikiwa na kamati hiyo, linashabihiana kwa vigezo na ushauri wa kitaalamu uliotolewa na kampuni mashuhuri ya mawakili wa Virginia, Marekani inayoitwa Hunton & Williams LLP kwa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO, Oktoba mwaka juzi “katika ripoti yake yenye kurasa 10, kampuni hiyo ya mawakili imetamka bayana kuwa hakuna kampuni yenye jina la Richmond Development.

Company LLC kwenye masijala ya katibu wa Jimbo la Texas ambaye moja ya majukumu yake ni sawa na ya Msajili wa kampuni Tanzania.

Dk. Mwakyembe alisema, Humton & Williams LLP wameituhumu Richmond Development Company LLC kwa upotoshaji wa hadhi yake kikampuni na kutoa tamko lisilo sahihi kuhusu hadhi yake chini ya sheria za Texas.

Alisema ukaguzi wa kumbukumbu za katibu wa jimbo la Texas uliofanywa na kampuni hiyo Oktoba 2006 ulionyesha hakuna kampuni yenye jina la Richmond Development Company LLC iliyokuwa imeanzishwa na kuendesha shughuli zake jimboni humo.

Dk. Mwakyembe alisema wajumbe wa kamati hiyo, waliokwenda Marekani Desemba 10 hadi 16 mwaka jana, waliambiwa na Mohamed Gire, kuwa Richmond Development Company LLC ni jina mbadala la biashara la kampuni yake iitwayo RDEVCO LLC.

“Bwana Gire ambaye aliamua mkutano wake na wajumbe wa kamati Teule ufanyike ofisini kwa wanasheria wake, Duane Morris LLP waliopo 3200 Southwest Freeway, suite 3150, jijini Houston, alisisitiza kuwa sheria na Texas zinawaruhusu wafanyabiashara na kampuni kutumia majina mbadala au tofauti na yale yaliyopo kisheria kwa sababu za kibiashara alisema Dk. Mwakyembe.

Alisema kamati yake iliyazingatia maelezo ya Gire kwa ajili ya kuyafanyia kazi, kwa sababu kuna, majimbo mengi Marekani, likiwemo la Texas yanaruhusu matumizi ya majina mbadala katika biashara au huduma.

Lakini, Dk. Mwakyembe alisema, sheria zinaweka taratibu za kuzingatia ili kuepusha vitendo vya kitapeli katika matumizi ya majina mbadala ya kibiashara.

“Katika jimbo la Texas ambako Gire anaishi ni kosa la jinai kutumia jina mbadala bila kulisajili. Usajili wa jina mbadala unadumu kwa miaka mitano ambapo mtumiaji lazima asajili jina hilo upya kati ya januari mosi na Desemba 31 ya mwaka wa tano,” alifafanua Dk. Mwakyembe ambaye pia ni mbunge wa Kyela.

Alisema, Gire aliwakabidhi wajumbe wa Kamati hiyo hati ya uthibitisho ya Harris County, Texas ambayo kwa maoni yake, ilikuwa inathibitisha kuwa Richmond Devilopment Company LLC ni jina mbadala la biashara.

“Kamati Teule imeikagua hati hiyo kwa kina na kuona kuwa badala ya kumsaidia Gire, inazidi kuthibitisha kuwa si mfanyabiashara mwadilifu ila tapeli kwa sababu kuu mbili:
Mosi, mbali na kwamba hati hiyo ya Gire ni kivuli tu au nakala ya “hati” halisi (kama ipo), nakala ambayo haina uthibitisho wowote wa uhalali na uhalisia wake, ilikuwa ina saini ya ofisa mmoja mbadala ya wawili walioainishwa katika hati hiyo pili, badala ya hati hiyo kutamka kuwa RDEVOCO LLC imesajili jina la Richmond Development Company LLC kama Gire alivyotaka Kamati Teule ielewe, hadithi mpya kabisa inaanzishwa kuwa Richmond Development Company ni jina mbadala lililosajiliwa na Richmond Development Company LLC!

La kushangaza ni kuwa katika baadhi ya barua zake alizoiandikia TANESCO na wizara ya Nishati na Madini, Gire anatamka kuwa Richmond Development Company ni jina mbadala la biashara la RDEVCO LLC.
“Mtu anaweza akadanganyika akifikiri kuwa kiwango hiki cha ubabaishaji hakithibitishi utapeli pekee, bali vilevile elimu duni ya mmiliki wa kampuni hizo, Gire, inayomfanya asione hatari kubwa anayojitwalia ya hata kumfikisha jela kwa udanganyifu,” alisema Mwakyembe, Kwa mfanyabisahara mzoefu aliyejizungushia mawakili wa kumtetea mambo yakimwendea mrama, anajua analolifanya, hivyo Richmond Development Company LLC ni kampuni ya kimakusudi ya kimkakati ambayo haikamatiki, haishitakiki, haipigiki faini na haiadhibiki kwa lolote lile itakalolifanya kwani haina uhai wa kikampuni,” alisema.

Dk. Mwakyembe alisema, Richmond Development Company LLC, kwa maneno mengine, si kampuni ya mchana bali ya usiku, kampuni ya mfukoni ambayo shirika la umma TANESCO liliingia nalo mkataba wa mabilioni ya fedha ya walipa kodi wa Tanzania.

Rushwa, Vistisho, Uchongoanishi....




Kamati ya Dr. Mwakyembe ilifanya kazi pamoja na kwa walitishiwa na kufanyiwa mambo mengine mabaya!


SEMA, USIOGOPE, SEMA!

Nasema mkono wa Mungu umetembea, maana kuna majina mazito yametajwa mle! DUH!

*********************************************************************

" Mheshimiwa Spika, leo tunapowasilisha taarifa hii mbele ya Bunge lako tukufu, tunajisikia kuutua mzigo mzito sana ulioanza kutuelemea kutokana na kuzongwa kila kukicha na kila aina ya uzushi, uchochezi, uchonganishi na hata vitisho. Tumezushiwa kuhongwa magari ya kifahari na fedha taslimu; tumetuhumiwa kuendesha vita dhidi ya Waislamu na mara nyingine tuhuma hiyo ikageuka kuwa vita dhidi ya Wakristo ndani ya Serikali; tumesingiziwa kuibadilisha taarifa yetu mara mbili, baadhi wakisema kwa ushawishi wa fedha, wengine wakidai kwa shinikizo la Mhe. Spika na wengine kwa shinikizo la Waziri Mkuu; tumeshuhudia pilikapilika za usiku na mchana za kujipanga na kuwashawishi baadhi ya Mawaziri na Wabunge kuikana taarifa hii na mapendekezo yake kiasi cha wengine wetu kujiuliza: kulikoni mtu asiye na hatia kuweweseka?

Mheshimiwa Spika, naomba kwa niaba ya wajumbe wenzangu wa Kamati Teule, kukuhakikishia wewe binafsi na Bunge lako tukufu kuwa tumekamilisha kazi tuliyopewa kwa uaminifu na ujasiri mkubwa, dhamira safi, moyo wa uzalendo na kwa kumtanguliza mbele Mwenyezi Mungu katika kila tulilolifanya. "

KUSOMA RIPOTI NZIMA BOFYA HAPA:

Lowassa Ajiuzulu Uwaziri Mkuu!!!!


DAH! Yaani wadau kwa kweli mnisamehe, maana hii habari ya Mhesimiwa Lowassa nimesikia saa hizi, 9:56Am (EST). Nilikuwa busy na mambo ya audition ya sinema fulani.

Kwa kweli nimeshutuka sana na nimesikitika mno hasa chanzo cha kujizulu kwake. Ila nimefurahi kuona kuwa Tanzania kuna haki ya kusema siku hizi, FREEDOM OF SPEECH. Na safari hii uchunguzi ulifanyika na haikutiwa maji!

Dr. Harrison Mwakyembe, NAKUSIFU! Bado unaujasiri wa enzi zile! Ila uko salama kweli sasa?


Haya tuone nani atateuliwa kuwa Waziri Mkuu sasa. Any suggestions/predictions?



*******************************************************************************


HABARI TOKA DODOMA SASA HIVI ZINASEMA KUWA SPIKA WA BUNGE MH. SAMWEL SITTA AMETANGAZA KWAMBA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA AMEAMUA KUJIUZULU UWAZIRI MKUU.

MH. SPIKA BAADA YA KUTANGAZA HILO AMESEMA MJADALA WA RIPOTI YA RICHMOND, NA SIO MJADALA WA LOWASSA, NDIO UENDELEE. NA NDICHO KINACHOFANYIKA HIVI SASA HUKO BUNGENI.

HABARI ZAIDI ZINASEMA KWAMBA MH. LOWASSA AMESEMA KWAMBA INGAWA HAJAMTAARIFU JK UAMUZI WAKE HUO, AMEAMUA KUJIWEKA KANDO!

*************************************************************

KARAMAGI NAYE AOMBA KUJIZULU!

KARAMAGI NAYE AOMBA KUACHIA NGAZI

MH. NAZIR KARAMAGI AMEMALIZA KUJIELEZA NA AMELIAMBIA BUNGE KWAMBA NA YEYE LEO ASUBUHI AMEPELEKA BARUA KWA JK KUOMBA KUJIUZURU WADHIFA WAKE WA UWAZIRI WA NISHATI NA MADINI.

YEYE PIA AMEJITETEA KWAMBA HANA HATIA KATIKA SAKATA HILI!
******************************************************************

MSABAHA NAYE AJIUZULU!
MSABAHA NAYE AMWAGA MANYANGA

WAZIRI WA AFRIKA MASHARIKI AMBAYE AWALI ALIKUWA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI DK MSABAHA NAYE KAMPELEKEA BARUA JK KUOMBA KUJIUZURU KWA MUJIBU WA MAELEZO YAKE ALIYOTOA DAKIKA HII BUNGENI

WHAT A SAD DAY IN TANZANIA POLITICS!

WAPI Zanzibar


Wednesday, February 06, 2008

Fesheni Mpya Bongo!



Hii Fesheni ya suruali nimeona kwa Maggid Mjengwa. Mnaionaje? Karibu ifanane na sketi. Sijui wametumia mita ngapi kuishona. Halafu tai karibu inafika kwenye magoti!

Issac Mizrahi atasemaje hapo, tutaiona kwenye runway Paris?




Premiere ya Bongoland II itakuwa Minneapolis, Minnesota


Taarifa leo kutoka Kibira Films International zinasema kuwa onyesho la kwanza la sinema mpya, Bongoland II, itakuwa Minneapolis, Minnesota. Tarehe bado haijapangwa.

Pia kuna updates kwenye website ya sinema:




Uchaguzi wa wagombea Rais Marekani - Hakuna mshindi kamili

Mamilioni ya waMarekani walipiga kura zao jana kupata mgombea rais wa upande wa Democrats na Republicans. Hakuna mshindi kamili kwa pande zote.

Hivi kwa Dems, bado tunaye Obama na Clinton. Kwa Republicans bado wapo Huckabee, Romney na McCain.

Kwa habari zaidi soma:

http://www.cnn.com/2008/POLITICS/02/06/super.main/index.html

Tuesday, February 05, 2008

Leo ni Super Tuesday! - Nani atagombea Uraisi wa Marekani!








Leo mamilioni ya waMarekani wanajitokeza kupiga kura. Wanaiita siku ya leo, Super Tuesday. Kura wanaopiga leo zitasaidia kuchagua nani atakuwa mgombea rais kwa upande wa Democrats na upande wa Republican.

Kwa upande wa Republicans waliobaki kugombania nafasi ni Mike Huckabee, John McCain, na huyo mshenzi/mnafiki alikuwa Gavana wetu hapa Massachusetts, Mitt Romney.

Kwa upande wa wa Democrats waliobakia ni Hillary Clinton, na Barack Obama. Kuna mashindano makali sana kati ya hawa wawili. Wote wana wafuasi wengi. Huenda leo hatutajua nani kapita upande wa Democrats na itabidi tusibiri hadi siku ya Convention (mkutano mkuu wao), itakayofanyika mwezi wa nane huko Colorado.
Nadhani kuna chensi kubwa kuwa Democrats watanyakua White House safari hii. Watu wamechoka utawala wa Bush. Wanasema ameharibu nchi na hadi yake, pia kaanzisha vita isiyo na maana huko Iraq. Pia hali ya maisha kwa Marekani umekuwa mbaya, watu wanfukuzwa katika majumba yao, bei ya mafuta umepanda, hata bei ya chakula umepanda mno!
Bush aliwaahidi waMarekani kuwa kama atakuwa Rais bei ya mafuta utashuka. Wakati huyo ni kama $1.80 a gallon. Leo ni $3.10! Wajinga ni nani! Hao waliompigia kura Bush kwa hasira wanaweza kupiga kura zao kwa Democrats! Warudishe hadi ya nchi ilivyokuwa enzi za Rais Clinton!

May the Best Man/Woman win!

Sunday, February 03, 2008

Patriots walia! Kumbe siyo PERFECT!

Tom Brady na wanawake wake (Bridget(shoto), Tom (Katikati), Gisele(Kulia)


Doh! Yaani jioni hii nimeona watu wanalia kwa masikitiko utadhani wamefiwa! Wanalia, wanatapika, wanasema miii yao imekufa ganzi! Yaani! Kisa cha masikitiko....Patriots wameshindwa katika SuperBowl. New York Giants wamewashinda 17-14 tena katika sekunde za mwisho wa mchezo!

Kama Patriots wangeshinda ingekuwa historia maana msimu wote hawakuwahi kushindwa.

Mimi nasema kushindwa kwao ni laana ya Bridget Monahan! Kwa wasiojua Quarterback wa timu ya New England Patriots, Tom Brady, alimtupa mpenzi wake mwenye mimba, mcheza sinema maarufu, Bridget Moynahan kwa ajili ya Supermodel Gisele Bundchen.

Moynahan alijifungua mtoto wa kiume na kwa hasira kamnyima mtoto jina la baba yake.

Na walivyoanza kucheza SuperBowl walionyesha huyo Gisele yuko pale stadium kumshabikia mpenzi wake! Haya, watu bado wanfutamachozi lakini naamini siku zijazo tutasikia watu wanavyomlaani huyo Gisele na Bridget kwa kushindwa kwa Patriots kuwa timu bora katika historia ya American football!

Na sasa wanamlaumu kocha wao Bill Belichick kwa kuvaa sweata nyekundu.

Leo wanacheza Superbowl aka The Stupid Bowl!


Leo timu yetu maarufu ya Football, The New England Patriots watacheza katika SuperBowl. Wapinzani wao ni timu ya New York Giants. Wanacheza huko Glendale, Arizona.

Timu yetu haijashindwa katika mchezo hata moja msimu huu. Wakishinda Superbowl watukuwa wamevunja rekodi katika mchezo huu.

Mchezo wa football siipendi. Si ule mpira wa miguu wanaocheza Tanzania, Soccer, hii inafanana zaidi na rugby, kazi kuumizana! Wanaume wanakuwa vichaa kipindi hiki. Leo kuna Superbowl party nyingi tu.

Huwezi kupata tiketi kwenda kuona Superbowl laivu kwa chini ya dola $2,000! Na watu wako tayari kulipa hizo pesa kwa jinisi walivyo washabiki! Wako tayari kuingia katika madeni ili waende.

Katika msimu wa football kuna kuwa na 'football widows', yaani wajane wa Football. Kwa maana hiyo wanaume wao walivyo na ushabiki na mchezo hawajali wake zao.

Akina dada wanaotaka wachumba wanashauriwa wajifunze lugha ya football, Touchdown, field goal penalty. Halafu wajidai kuwa wanapenda huo mchezo. Hapo utampata mwanaume!

Haya tutaona nani atashinda hiyo SuperBowl. Wengi waniita The Stupid Bowl kwa jinis watu wanavuoingiliwa na kiwewe! LOH!

Kwa habari zaidi za SuperBowl soma:

http://www.nfl.com/superbowl

Saturday, February 02, 2008

Serikali ya Chad yapinduliwa!


Inaelekea magaidi wanajaribu au wamekwisha pindua seriakali ya Chad. Wazungu wanashauriwa kukimbia nchi! Nilidhani huo mchezo wa Coup d'Etat Afrika umepitwa na wakati...kumbe!


Wamegundua mafuta huko Chad. Tutaona nani anawafadhili hao wagaidi.

***********************************************************


NAIROBI, Kenya (AP) -- Hundreds of rebels penetrated the capital of Chad on Saturday, clashing with government troops and moving on the presidential palace after a three-day advance through the oil-producing central African nation, officials and witnesses said.

Col. Thierry Burkhard, a French military spokesman, said groups of rebels gathered outside the capital, N'Djamena, overnight before 1,000 to 1,500 fighters entered early Saturday and spread through the city.

A leader of Chad's main opposition alliance, which is unarmed and not associated with the rebels, said shooting erupted after rebels entered the city around 8 a.m. but appeared to die down about two hours later. Ibni Oumar Mahamat Saleh said about 12:45 p.m. that there were no soldiers in his neighborhood and state radio had gone off the air.

"At the moment we are not hearing any firing ... The rebels are in the city. Civilians are in the streets. They are watching what is happening," said Saleh.

Chad, a French colony until 1960, has been convulsed by civil wars and invasions since independence, and the recent discovery of oil has only increased the intensity of the struggle for power in the largely desert country.

The rebel force is believed to be a coalition of three groups, including the biggest led by former diplomat Mahamat Nouri, who defected 16 months ago, and a nephew of Deby's, Timan Erdimi. They long have been fighting to overthrow Deby, whom they accuse of corruption.

The rebels also have said they were unhappy with the president not providing enough support to rebels in Sudan's Darfur region, some of whom are from Deby's own tribe, the Zaghawa, who are found both Chad and Sudan.

The renewed fighting has led the European Union to delay its peacekeeping mission in both Chad and neighboring Central African Republic, which was due to be up and running early next month, said Commandant Dan Harvey, speaking at the EU military headquarters in Paris on Friday. The deployment of the advance force could be postponed for days, he said.

The force already has met repeated delays. It is aimed at protecting refugees from Darfur, which borders Chad, as well as protecting Chadians and Central Africans displaced by turmoil in their own countries.

The news that rebels reached Chad's capital broke just as African leaders were listening to the closing speeches of a three-day summit in Addis Ababa, the Ethiopian capital. Representatives from the Chad delegation refused to comment to The Associated Press.

The new head of the African Union said that the bloc would not recognize Chadian rebels should they seize power.

"If the rebellion succeeds, certainly we will excommunicate them from the African Union until normalcy and democratic institutions are restored in that country, if it has to happen that way at all," Tanzania's President Jakaya Kikwete told a news conference.

The United Nations decided to temporarily evacuate all its staff from Chad's capital because of the fighting, said William Spindler, spokesman for the U.N. High Commissioner for Refugees. The U.S. Embassy said in a bulletin on its Web site that any American citizens seeking evacuation should immediately move to the embassy. State Department spokesman Karl Duckworth said the embassy had authorized the departure of nonessential personnel and family members.

"At this time the U.S. is monitoring the security situation closely," Duckworth said in a statement. "The serious violence that has occurred has not been directed at any U.S. personnel or facilities. We are taking all appropriate precautions to ensure the security of U.S. mission personnel and all American citizens in Chad."

France's embassy in Chad sent messages over Radio France Internationale telling citizens to head to the Lycee Francais high school and two other locations in N'Djamena, a French diplomatic official said on condition of anonymity because government policy barred him from providing his name.

A hotel operator at the Hotel le Meridien, about a mile from the headquarters of President Idriss Deby, said gunfire and explosions had been resounding through the capital since 7 a.m.
The man, who would not give his name, said he had not seen any rebels. The line went dead before a reporter could get more details. Other phone lines also were dead and the information could not immediately be confirmed.

Rebels in more than a dozen vehicles drove past the Libya Hotel, which overlooks the parliament building, said a man who answered the telephone at that hotel.

"I saw more than 15 vehicles and they (the rebels) were firing into the air," said the man, who also would not give his name. He said he also watched looters go into a police station opposite the hotel, stealing chairs and throwing papers on the ground.

Rebel forces have been advancing on the capital for three days in about 250 pickup trucks from the direction of the border with Sudan, about 500 miles to the east of N'Djamena.

Deby himself came to power at the head of a rebellion in 1990; he has won elections since, but none of the votes were deemed free or fair. He brought a semblance of peace after three decades of civil war and an invasion by Libya, but became increasingly isolated.

The most recent series of rebellions began in 2005 in the country's east, occurring at the same time as the conflict in Darfur saw a rise in violence. One Chadian rebel group launched a failed assault on N'Djamena, in April 2006.

The governments of Chad and Sudan repeatedly exchange accusations the one is backing the other's rebel groups.

U.N. officials estimate that around 3 million people have been uprooted by conflicts in the region, including the fighting in western Sudan's Darfur region and rebellions in Central African Republic.

France sent more troops late Thursday to boost a longtime military presence in Chad. About 1,500 French citizens live in Chad, most in N'Djamena.

It appeared that Chad's government might be getting less help from France than during previous rebel attempts to take the capital, said Henri Boshoff, a military analyst at the Institute for Security Studies in Pretoria, South Africa.

Previously, "the French gave them intelligence using aerial reconnaissance and that allowed the Chad government to act," Boshoff told The Associated Press. "But it looks like this time it's too late, the rebels got too close to the city."

The difference could be that former President Jacques Chirac was leading France during the previous coup attempts, a leader who made every effort to project France as a friendly protector on the African continent. France's new president, Nicolas Sarkozy, has called for a "healthier relationship," saying it will not be business as usual with France's old corrupt allies on the continent.
Kwa habari zaidi soma:

Hollywood in Bostwana!



Tanzania tujifunze kutoka Botswana. Serikali ya Botswana imetoa baraka zote kwa ajili ya kutengeneza hii sinema huko. Hata mawaziri na viongozi wa dini wana acti kwenye hii filamu!

Kwa habari zaidi za hii sinema bonyeza hapa:

The No. 1 Ladies Detective Agency

Onyo kwa wapenzi wa 'Chumvini'


Jamani, leo naongelea mambo nyeti. Kwa hiyo nyie watoto wadogo...ONDOKENI!

Kuna huo mchezo katika ngono wa kumfurahisha mpenzi kwa kunyonya huko sehemu za siri. Sasa wataalamu wanasema kuwa mwanaume anaweza kuambukizwa HPV, yaani virusi vinavyosababisha ugonjwa wa kansa ya kizazi.

Mungu atunusuru, kwanza tunaambiwa kuwa wanaume wanaweza kuambukiza wanawake hiyo HPV na kusababisha kansa ya kizazi. Sasa wanaume nao wanaweza kuambukizwa na kupata kansa ya koo na mdomo! Duh!

Licha ya HPV kuna HIV unaosababisha ugonjwa wa UKIMWI. Nadhani mwisho watu wataishia kujifurahisha wenyewe maana magonjwa yamezidi! Kila siku kuna kipya!

Nawashauri kila mwaka mfanye physical check-up. Kwa wanawake in maana mfanye Pap Smear, hapo watajua kama una HPV au la. Daktari anakata kipande cha mlango wa kizazi (cerivx) na kuipima. Uzuri unatibika ukikamatwa mapema.
**************************************************************************


ATLANTA (AP) -- The sexually transmitted virus that causes cervical cancer in women is poised to become one of the leading causes of oral cancer in men, according to a new study.
The HPV virus now causes as many cancers of the upper throat as tobacco and alcohol, probably due both to an increase in oral sex and the decline in smoking, researchers say.

The only available vaccine against HPV, made by Merck & Co. Inc., is currently given only to girls and young women. But Merck plans this year to ask government permission to offer the shot to boys.

Experts say a primary reason for male vaccinations would be to prevent men from spreading the virus and help reduce the nearly 12,000 cases of cervical cancer diagnosed in U.S. women each year. But the new study should add to the argument that there may be a direct benefit for men, too.

"We need to start having a discussion about those cancers other than cervical cancer that may be affected in a positive way by the vaccine," said study co-author Dr. Maura Gillison of Johns Hopkins University.

The study was published Friday in the Journal of Clinical Oncology.

Human papillomavirus, or HPV, is the leading cause of cervical cancer in women. It also can cause genital warts, penile and anal cancer -- risks for males that generally don't get the same attention as cervical cancer.

Previous research by Gillison and others established HPV as a primary cause of the estimated 5,600 cancers that occur each year in the tonsils, lower tongue and upper throat. It's also been known that the virus' role in such cancers has been rising.

The new study looked at more than 30 years of National Cancer Institute data on oral cancers. Researchers categorized about 46,000 cases, using a formula to divide them into those caused by HPV and those not connected to the virus.

They concluded the incidence rates for HPV-related oral cancers rose steadily in men from 1973 to 2004, becoming about as common as those from tobacco and alcohol.

The good news is that survival rates for the cancer are also increasing. That's because tumors caused by HPV respond better to chemotherapy and radiation, Gillison said.

"If current trends continue, within the next 10 years there may be more oral cancers in the United States caused by HPV than tobacco or alcohol," Gillison said.

Studies suggest oral sex is associated with HPV-related oral cancers, but a cause-effect relationship has not been proved. Other researchers have suggested that even unwashed hands can spread it to the mouth as well.

Gillison pointed toward sex as an explanation for the increase in male upper throat cancers. However, HPV-related upper throat cancers declined significantly in women from 1973 to 2004.
Merck's vaccine, approved for girls in 2006, is a three-dose series priced at about $360. It is designed to protect against four types of HPV, including one associated with oral cancer.

Merck has been testing the vaccine in an international study, but it is focused on anal and penile cancer and genital warts, not oral cancers, said Kelley Dougherty, a Merck spokeswoman.
"We are continuing to consider additional areas of study that focus on both female and male HPV diseases and cancers," Dougherty said.

Merck officials praised Gillison's research, saying it will elevate the importance of HPV-related oral cancers.

Government officials and the American Cancer Society say they don't know yet whether Merck's vaccine will be successful at preventing disease in men. No data from the company's study are available yet.

Indeed, it's not clear yet that the vaccine even prevents the HPV infection in males, let alone cancer or any other illness, said Debbie Saslow of the American Cancer Society.
Merck plans to seek U.S. Food and Drug Administration approval for the vaccine in men later this year, meaning a government decision would be likely in 2009

Friday, February 01, 2008