Monday, May 18, 2009

Picha za Prom

Wadau, hapa Marekani watoto wakimaliza Form 4, wanafanya sherehe kubwa ambayo inaitwa PROM. Wanavyojiandaa kwa mavazi, usafiri wa limo, hoteli, utadhani ni arusi. Nimetumiwa hizi picha za nguo vijana waliovaa kwenye Prom mji fulani hapa USA. Nimetafsiri captions.


Tukae kimya dakika moja tuombee hao ndege.Doh! Mnaweza kuona chupi!
Hivi ilikuwa lazima ageueke? Na huko nyuma ni madudu gani tena?Huyo dada anaenda Prom au Beach?

Njemba kalazimishwa kwenda na huyo dada!
Nywele ya Maiti

Hajawahi kusikia habari ya deo za Invisible Solid?

Hata Mbwa kapakwa rangi!

Hao wamevaa nguo za kulala?

Huyo naye denti?
Yaani huyo bado anasoma Sekondari?

Njemba atahitaji 'counselling'!

7 comments:

Anonymous said...

hiyo picha ya 3 kutokea mwisho ghafla nilifikiri ni wewe chemi baada ya kuitizama kwa makini nikaona ni dada tofauti ila mmefanana!!!

mbona hayo madudu ni wamarekani weusi tu? au ndio vichaa huko states? maana sijaona wale wenye nchi naona si wahamiaji tu ambao kwa kuiga tamaduni za watu huwashinda hao waanzilishi.

Anonymous said...

duh halafu wengi wao chemi unafanana nao sana, kulikoni?

Nautiakasi said...

Ha ha ha Da Chemi acha bias bimkubwa, naona picha ya 3 toka chini hukuitolea maelezo...! Kumbe ukiona "sanamu la micheline" mwenzio unabana eeh??? Si ungaandika tu kama hao wengine ulo washushuwa..na huyu ungeandika hivi " Huyu vipi tena maziwa kama viroba vya mkaa" He he he mmezidi kula, mnakula mpaka vya wenzenu, ngojeni sasa sukari (diabet)na high blood pressure (BP) ziwaandame! Mnakula kama kesho hakuna??? Miumbo hiyo uliza fungus wa sehemu za siri na kwenye mapaja, hawapati kujisafisha vizuri...!

Anonymous said...

dada Chemi mimi mshamba mbona hawa watu ni wazee sana miili mikubwa sana kama mashingingi ya migomigo hapo kwetu mimi najua state watoto wanasoma wakiwa wadogo kumbe ni wakubwa hivi dada washahuri wapunguze milo ahasante ni hayo tu

Anonymous said...

Marekani unakutana na msichana ambaye utadhani ana miaka 30 kumbe ana miaka 16. Sijui ni chakula inawafanya hivyo1

Anonymous said...

Ghetto Prom?

Anonymous said...

Da ungetoa na wliovaa vizuri basi, siamini kama wote kwenye hiyo prom walichemsha.