Wednesday, September 24, 2008

Bongoland itaonyeshwa Dar (Mwenge)


Kutoka Kibira Films:


Haya wadau mlioko Bongo, tunawajulisha kuwa sinema ya Bongoland (Original) stelingi wake ni Mukama (Jimmy Morandi) itaonyeshwa Bongo mwezi ujao hapo mjini Dar katika tamasha la filamu za Ulaya. (European Film Festival 2008) Shoo itakuwa katika ukumbi wa sinema wa New World Cinema katika kitongoji cha Mwenge.

Bongoland itaonyeshwa siku ya Jumamosi Ocktoba 18 saa nane kasoro robo. (14.45). Kwa habari zaidi wasiliana na British Council hapo mjini Dar au piga simu namba 0755-481374

Kama unavyokumbuka sinema hii ni ya hadithi ya kijana Juma Pondamali aliyekuwa anaishi ughaibuni. Baada ya kupatwa na mizengwe mingi na milolongo ya kazi, ubaguzi na shida nyingi tu..akaanza kujiuliza ni kwa nini aendelee kuumia? Je angekuwa Bongo kweli hali ingekuwa hivi? Marafiki zake walimshauri kuvumilia na hadithi hii inamwonesha Juma akikabiliwa na swala la uamuzi ...ataendelea kuumia mpaka lini?

Kwa habari zaidi kuhusu sinema hii BOFYA HAPA

Kwa kuona trela ya sinema hii BOFYA HAPA

Kwa habari zaidi za Kibira Films International BOFYA HAPA


Mipango ya kileta Bongoland II iko mbioni...kwa sasa BONGOLAND II itaonyeshwa Scotland mwezi huu wa Oktoba mwishoni. Habari zaidi BOFYA HAPA

1 comment:

Anonymous said...

Habari zenu?
Kiingilio cha tamasha ni BURE kwa watu wote!
Filamu 40 kutoka Ulaya na 20 kutoka Tanzania zitaonyeshwa.
Mwaka huu tamasha linaandaa na Alliance Française - Dar es Salaam.
Karibuni wote!
Regina