Friday, November 21, 2008

Walimu Wachachamaa Tena!

Walimu wakitafuta majina yao


OFISI za maDC na Maded wa Temeke na Kinondoni leo zilipata matatizo kidogo wakati walimu walipovamia kutaka kujua kulikoni baada ya majina yao kutokuonekana katika karatasi za malipo kwenye mbao.Pichani ni walimu wakiangalia majina yao.Imeelezwa kuwa wilaya ya Kinondoni zaidi ya walimu 200 walijiandikisha kuuliza kulikoni kwingine wakafanya maandamano.

OniSomething is wrong somewhere kwanini taarifa sahihi zisitolewe kuhusu nini kinafanyika mbona watu wanafanya vitu vionekane kama matusi? Na nilipowatafuta jamaa kujazia stori kila mtu akawa anaruka kimanga. Kuna shida kwelikweli na ofisi hizi za umma, utafiti vile wanalinda magunia ya bangi. - Lukwangule
********************************************************
Nami nauliza hivi Tanzania walimu wetu wanadhauruliwa kiasi hicho? Hao walimu wanakazi nzito ya kuelimisha watoto wetu. Kazi wataweza kufanya vizuri kweli kama wanakuwa na wasiwasi wa kulipwa mshahara, tena ambao wamekwishaifanyia kazi? Hii ni aibu sana. Zamani shule za serikali zilikuwa za hakika lakini siku hizi mmmmh!- Chemi

No comments: