![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd9avv1BQg3Z6C5sjMRyXkz-1KaHeRN88dRy66NZsZ8wGqpe5ejCcsfPeXnpRrgBLeOzB_6p4nNCxsDSBHOxBQMH3ZG6QJb92X1wdLu1ibfQC_NiuSJZ2ICCFlHgnX1X5OKf5yUg/s400/plane+crash+turkish.jpg)
Naona ndege zinafululiza kuanguka sasa. Ilianza na ile ya Continental Airlines Flight 1549 iliyoanguka mtoni New York. Watu 50 walikuwa baada ya ndege yao Continental 3407 kuanguka kwenye nyumba huko Buffalo, New York. Na kumekuwa na ajali kadha za ndege ndogo. Hata hapa Massachusetts ndege ndogo ilianguka na kwa bahati mwanamke aliyekuwa anaiendesha alipona na majeraha madogo.
Wadau, yaani wanasema kuwa kusafiri na ndege ni salama kuliko usafiri wa gari. Lakini mimi kila nikipanda kwenye ndege lazima niombe. Na tukitua salama lazima niseme sala ya shukurani.
Mungu alaze roho ya waliopoteza maisha yao katika hiyo ajali mahala pema mbinguni. Amen.
Kwa habari zaidi someni:
http://www.telegraph.co.uk/news/worldnews/europe/netherlands/4805195/Turkish-Airlines-plane-crashes-at-Schiphol-airport-Amsterdam-at-least-nine-dead.html
http://www.google.com/hostednews/ap/article/ALeqM5g_wBSqw0Ju245UxNtpJZ329K0LJgD96IK4780
2 comments:
Kweli ukiingia kwenye ndege ni kuomba! Duh! Hasa hapa kwetu Afrika. Hata mkipona vibaka watawaibia palepale.
kuomba inatakiwa kila mahali ulipo unapoenda lazma uombe ulinzi wa Mungu. iwe majini anagani hata barabarani.
Ms GB
Post a Comment