Saturday, December 01, 2007

Ajisalimisha


Kichaa aliyeteka ofisi ya kampeni ya Senator Hillary Clinton huko Rochester, New Hampshire, Leeland Eisenberg, alijisalimisha jana jioni. Aliachia mateka wote huru kabla ya kujisalimisha kwa polisi.

Eisenberg alisema alifanya hivyo kwa sababu anahitaji matibabu ya ugonjwa wa akili na hana pesa za kulipia. Alisema watu wenye ugonjwa wa akili wanateseka Marekani hasa kama hawana bima au hela za kulipia matibabu.
Senator Clinton anasema kuwa anaelewa kuwa Eisenberg aliteka ofisi yake kwa ajili ya kutoa mwanga kwenye hiyo swala. Alisema pia kuwa anashukuru hakuna mtu aliyeumia au kufa katika tukio hilo.
Kwa habari zaidi someni:

No comments: