Friday, November 30, 2007

Ofisi ya Hillary Clinton imetekwa nyara New Hampshire

Senator Hillary Clinton
UPDATE: 4:14Pm Eastern - Mateka wote wawili wameachiwa huru
*********************************************************************************

Watu wawili wametekwa katika ofisi ya mgombea rais wa chama ca Democrats wa Marekani, Senator Hillary Clinton. Ofisi enyewe ni ya kampeni yake na iko Rochester, New Hampshire.

Sakata umeanza saa 7 mchana huu na hivyo navyoandika bado inaendelea. Mama moja aliyekuwa ndani ya hiyo ofisi na mtoto wake wa miezi sita aliachiwa huru pamoja na mtoto.

Jamaa aliyeteka nyara ofisi amejifunga mkanda ambayo anasema ina bomu! Ofisi sasa imezungukwa na polisi, SWAT (FFU) na Secret Service. Kama jamaa hajisalimishi msishangae mkisikia kuwa jamaa katunguliwa kwa kupigwa risasi kichwani na FFU.

Pia polisi wameamuru ofisi za wagombea rais wengine maDeomcrats, Barack Obama na John Edwards zifungwe kwa usalama wa raia na wafanyakazi.

Marekani bwana!

http://www.cnn.com/2007/POLITICS/11/30/clinton.office/index.html

No comments: