Wednesday, May 09, 2007

Rest in Peace JWTZ Captain Leticia Oswald


Afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kepiteni Leticia Oswald (pichani), ni mmoja ya abiria waliokufa katika ajali ya ndege ya Kenya Airways, iliyoanguka huko Cameroon, usiku wa kuamkia Jumamosi 5/5/07. Alipandia ndege Abidjan.


Kepiteni Oswald alikuwa Ivory Coast kwenye shughuli za kulinda amani (UN Peacekeeping Force). Alikuwa anakuja Dar es Salaam kwenye likizo.


Mungu amlaze mahali pema mbinguni. Amen.


Pia naomba Mungu ampe nguvu, mume wake, Keptieni John Jumla, katika kipindi hiki kigumu. Habari zinasema kuwa Kepiteni Kumla alienda Uwanja wa Ndege Dar es Salaam kumpokea mke wake. Ndege ya Kenya Airways ilitua salama, lakini mke wake hakuwemo katika abiria walioshuka. Ndipo kwenda kuulizia akambiwa kuwa alikuwa abiria kwenye hiyo ndege iliyoanguka Cameroon.

Habari kutoka kwenye gazeti la Daily News Tanzania, inasema kuwa Kepiteni Jumla amekwenda huko Cameroon, kujaribu kutambua maiti ya marehemu mke wake.
Kwa habari zaidi soma:

2 comments:

Anonymous said...

RIP LETISIA .

Simon Kitururu said...

Familia ya Letisia poleni sana kwa msiba!