Monday, August 04, 2008

Vigogo Wahaha! - Kifo cha Wangwe

Naona hata mwandishi wa hii stori kahofia maisha yake, wameandika 'mwandishi wetu' . Sasa kilichobaki ni kuita Scotland Yard wachunguze.

*******************************************************

Kutoka ippmedia.com

Kifo cha Wangwe: Vigogo BP juu!

2008-08-04

Na Mwandishi Wetu, Jijini

Mazingira tata ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, Mhe. Chacha Wangwe (CHADEMA), yamewafanya baadhi ya vigogo kuingiwa na hofu kubwa ya maisha yao na sasa wengine wamedai kuwa wana data ambazo hata kuzianika hadharani wanaogopa kwa sababu za kiusalama.

``Uchunguzi umethibitisha wazi kuwa Wangwe hakuuawa kwa risasi... lakini pamoja na ukweli huo, bado baadhi ya vigogo katika siasa, hasa wale wa upinzani, wamekuwa na hofu kutokana na mazingira tata ya ajali yenyewe na kile kilichomtokea (Wangwe) hadi kufa,`` kimesema chanzo chetu kimoja kilicho jirani na vigogo maarufu wa upinzani nchini.

``Hivi sasa kuna data nyingi zilizopatikana na kuibua maswali mengi kuhusiana na kile kilichotokea. Kijana aliyekuwa na Wangwe wakati wa ajali ndiye anayeelekezewa kidole zaidi kutokana na maelezo yake kila alipohojiwa... hili limeongeza hofu zaidi kwa vigogo hao, wakiamini kuwa wao wako hatarini na taifa pia liko hatarini,`` kimeongeza chanzo hicho.

Taarifa hizo za kuwepo kwa hofu miongoni mwa baadhi ya vigogo zimetiwa nguvu na yale yaliyosemwa jana Wenyeviti wa Umoja wa Vyama vinne vya upinzani nchini jana na kunukuliwa na vyombo vya habari leo asubuhi, kuhusiana na shaka iliyopo katika ajali iliyomuua Mheshimiwa Wangwe.

Wakizungumza hiyo jana, wenyeviti wa vyama hivyo vya CUF, CHADEMA, TLP na NCCR, wamesema wanazo taarifa zinazoibua maswali mengi kuhusiana na kifo cha Wangwe, hasa juu ya kijana anayedaiwa kuwa naye ndani ya gari, Bw. Deus Mallya.

Wakasema maelezo ya kijana huyo juu ya tukio hilo, namna Wangwe alivyopata majeraha yaliyomuua na ziada ya taarifa walizopata toka kwa watu wanaomfahamu kijana huyo (Mallya), ni baadhi ya mambo yanayowafanya wawe na hofu kuwa kuna ujasusi umefanyika.

Wakasema viongozi hao ambao ni Prof. Ibrahim Lipumba wa CUF, Augustino Mrema (TLP) na James Mbatia (CHADEMA), kuwa kwa taarifa walizo nazo, wanaamini vilevile kuwa upo mtandao hatari unaotishia usalama wa taifa.

Akizungumzia hofu hiyo, Prof. Lipumba akasema waliyemuona Mallya kabla ya tukio, wanasema alikuwa ni mtaalam wa kompyuta, alikuwa na vitambulisho vingi na vingine vimeandikwa kiarabu na pia, wanahisi kuwa amepata mafunzo ya kijasusi nchini Libya.

``Imekuwaje akawa karibu na marehemu kwa muda mfupi?`` Akahoji Profesa Lipumba wakati wakizungumza na waandishi wa habari. Akautaja utata mmojawapo juu ya kifo cha Wangwe kuwa ni kuonekana kuwa kichwa cha marehemu kimepondeka na hakuna maelezo dhahiri ya suala hilo. ``...mle ndani ya gari hakuna hakukuwa na vyuma wala mabati yaliyopondeka.

Kweli hakufa kwa kupigwa risasi... lakini ile ajali ilitokeaje mpaka lochwa kikapondeka?`` akasema Prof. Lipumba. Aidha, Mbatia naye akasema.

Aidha, Mbatia naye akasema kutokana na utata mwingi juu ya kifo hicho ikiwa ni pamoja na maelezo ya kujikanyaga ya kijana Mallya, wao wameamua kumuona IGP Said Mwema ili wampe taarifa za siri kuhusiana na ukweli wa kifo hicho, kwa maslahi ya taifa.

``Inaonekana kuna mtandao unaohatarisha usalama wa nchi.... kijana huyo (Mallya) ana mafunzo ya Kimafia,`` akasema Mbatia.

SOURCE: Alasiri

2 comments:

Anonymous said...

Na Bado! Kifo cha Wangwe ndo mwanzo!

Anonymous said...

Da Chemi,

Morgan Freeman, imekuwaje tena hebu tupe habari.