Friday, January 09, 2009

Siku ya Kuapishwa Rais Obama Inakaribia

Wadau, wangapi mmepanga kwenye huko Washington D.C. kwenye Inauguration (Sherehe za Kuapishwa) ya Barack Obama? Nasikia itakuwa balaa huko kwa jinsi watu watakavyojazana. Vyumba vya hoteli hakuna.

Pia watu wa usalama hapa wame weka masharti mengi kwa wanaoenda. Hakuna kwenda na kiti, mwavuli, backpack, na mambo mengi. Simu za mkononi hazitafanya kazi maana signals ziatkuwa jammed.

Pia wana usalama wanasema katika historia hakuna rais aliyetishiwa maisha kama Barack Obama. Na wanasema kuwa hii ni kwa sababu ni mweusi. Wabaguzi nchi hii bado wanachukia kushinda kwa rais Obama.

Wakati huo huo watu wanaanza kushangilia kuondoka kwa Rais Bush! Wanasema jamaa kaharibu nchi na kutesa watu!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.cnn.com/2009/POLITICS/01/08/inauguration.security/index.html?iref=mpstoryview

No comments: