Tuesday, July 29, 2008

Bagamoyo Beach



Picha kutoka Maggid Mjengwa blog

Nimeona hii picha hii kwa kaka Mjengwa. Aliipiga Bagamoyo beach hivi karibuni. Kweli TV na sinema zinasababisha mabadiliko katika jamii. Miaka ya nyuma usingeweza kukuta wapenzi wakiongea hivyo hadharani. Au siyo? Lakini ni jambo la kawaida kuonyesha mapenzi hadharani katika video na sinema. Watu wameiga. Kwenye giza ni mambo mengine lakini.

Hivi mnakumbuka enzi za censorship Bongo? Enzi za Mwalimu na kabla ya TV kuingia 1993. Yaani kabla ya kuona sinema, Tanzania film company wanafuta busu, na mambo mengine ya mapenzi. Scene ya mapenzi inakatwa! Kweli walikuwa tuchunga kweli. Hata magezeti na vitabu vya mapenzi yalikuwa marufuku. Mmewahi kusoma kitabu cha After 4:30? Labda ganda ilitolewa na kuwekwa brown paper!

Lakini watu walikuwa wanapendana na kufanya mapenzi!

No comments: