Thursday, September 29, 2005

Barack Obama

Hii ni jambo la kujivinia sisi wana Afrika Mashariki kuwa huenda rais wa kwanza wa Marekani Mweusi huenda akawa Barack Obama ambaye ni Senator huko Illinois. Senator Obama ni hafukasti, mama yake ni Mzungu na baba yake ni Mkenya. Ajabu zaidi ni kuwa mama yake ni mtukuu wa Jefferson Davis ambaye alikuwa Kiongozi wa Confederates. Yaani enzi za utumwa Marekani, Davis alikuwa ni rais wa maConfederates waliochukia weusi na kutaka wabakie katika utumwa na kusababisha Civil War, vita vya wenyewe kwa wenyewe (1860’s). Watu wa Kaskazini hawakutaka utumwa na watu wa Kusini walitaka utumwa udumu. Huyo Jefferson Davis bila shaka anajigueza huko kaburini kwake.

Mwaka jana, Obama alipewa nafasi kuwa keynote speaker katika Democratic National Convention, wana Demokrat walivyomchagua bwana John Kerry kuwa mgombea wa rais katika uchaguzi uliyopita. Na nilishangaa jinsi alivyoweza kuongea na watu kumsikiliza kwa makini kama vile wanamsikiliza Martin Luther King au Mahatma Gandhi. Kila mtu alimpenda na wazungu ndo kabisa sikusikia neno baya juu yake isipokuwa kutoka kwa mpumbavu Alan Keyes (MRepublican) aliyekubaliwa kuwa toi.

Na hivi karibuni alitoa shutuma kali dhidi ya serikali ya Marekani kuhusu Jinsi walivyowasaidia walioathirika na Hurricane Katrina. Bila haya, alisema kuwa serikali ilikuwa legelege na response yao kwa vile walioathirika wengi walikuwa ni weusi na maskini. Katika siku zijazo tufuatilie kawa makini matendo na maneno ya Senator Barack Obama.

Wednesday, September 28, 2005

Any time is Swahili Time

Baada ya kuongo waBongo wenzangu wakiblogu wa Kiswahili na mimi nimeamua nianzishe blogu ya kutoa maoni kwa Kiswahili. Hii ni posti ya kwanza.