Saturday, January 30, 2016

WaTanzania Wengi Wanakosa Fursa za Maendeleo Kutokana na Kutokujua Lugha

Charles Mombeki (Kulia) ambae ni Mkurugenzi wa International Language Training Centre akizungumza na George Binagi kuhusiana na Umhimu wa Watanzania kujifunza lugha za Kimataifa hususani Kiingereza kwa ajili ya kuendana na muingiliano wa Kimataifa uliopo katika shughuli mbalimbali ikiwemo biashara.
"Watanzania wengi wanakosa fursa mbalimbali zilizopo. Wengine wanakosa fursa za kibiashara pamoja na kazi kutoka katika Mashirika na Makampuni mbalimbali duniani kutokana na kushindwa kufahamu lugha za Kimataifa hususani kiingereza, Kijerumani, Kifarasa, Kichina na hata lugha nyingine. Hivyo niwasihi waamue kujifunza lugha, kwa kuwa lugha inafungua milango ya mafanikio maishani". Anasema Mombeki.

Anasema, Watanzania wawaandae watoto wao katika lugha ya Kiingereza katika kupata elimu, akiunga mkono shule za watu ama Mashirika binafsi kutumia lugha ya Kiingereza kufundishia, tofauti na ilivyo kwa shule za Serikali kutumia lugha ya Kiswahili katika kufundishia katika shule za msingi akitanabaisha kwamba bado kiswahili hakijawa na nafasi kubwa kutumika kimataifa kama ilivyo kiingereza ambayo ni lugha inayowaunganisha watu wote Kimataifa. 

Mombeki anadokeza kuwa wanafunzi waliofundishwa kwa misingi ya kiingereza tangu wakiwa wadogo wana nafasi kubwa ya kufikia malengo yao ikilinganishwa na wale walioanza elimu yao ya  awali na msingi kwa lugha ya kiswahili.

Anabainisha kuwa kuna wanafunzi wengi kutoka Mataifa ya Afrika, Amerika na Ulaya wanapenda kufika katika Centre hiyo ambayo ilianza kutoa elimu ya lugha mbalimbali tangu mwaka 1998. Pia inafundisha lugha ya Kiswahili pamoja na lugha za asili ikiwemo Kisukuma pamoja na Mila na Desturi za Tanzania.
Imeandaliwa na George Binagi

Shamba la Waziri Mkuu Mstaafu Sumaye Mabwepande Imevamiwa!

 Nimepata kwa E-Mail:

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mhe. Fredrick Sumaye,ameiangukia serikali na kuomba msaada baada ya wananchi kuchukua sheria mkononi na kuvamia eneo lake la ekari 33 lililopo Mabwepande katika Manispaa ya Kinondoni nje kidogo ya jiji la Dar es salaam. Serikali imemuahikikishia Mhe. Sumaye kuwa haina mpango wa kumkandamiza mtu mnyonge wala tajiri hivyo itahakikiha inatoa haki kwa kila mmoja baada ya wiki mbili kwa kua imesikiliza pande zote mbili katika mgogoro huo.

Akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya wananchi wa kitongoji cha Kimondo mtaa wa mji mpya Kata ya Mabwepande na Mhe.Sumaye Dar es Salaam leo asubuhi, Mkuu waWilaya ya Kinondoni Paul Makonda alisema ili kumaliza mgogoro huo ambao Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye ameiomba serikali kuingilia kati ni lazima busara kutumika. Alizitaka pande hizo mbili kuiachia serikali kwa wiki mbili ili kutafuta njia bora ya kumaliza tatizo hilo huku wananchi wakitakiwa kuache kuendelea na ujenzi na kugaiana maeneo katika shamba hilo.

“Serikali ya Rais Magufuli ni sikivu na ndio maana ilikuwa tayari kumsikiliza Waziri Mkuu wetu Mstaafu Sumaye na kusikiliza wananchi ili kutenda haki tunatambua migogoro ya ardhi ilivyokuwa na athari kwa jamii hatuna mpango wa kumkandamiza tajiri wala mnyonge,”alisema. Alisema katika eneo hilo anajua jinsi wananchi walivyotumia nguvu katika kuwekeza ujenzi na rasilimali zao lakini kwa sasa wasitishe shughuli hizo na kuendelea kugawana maeneo na Sumaye pia kuacha uwekezaji ili kutafuta suluhu.

Zipo njia nyingi tutazitumia kumaliza mgogoro huu ikiwemo kufuata sheria kwa kuangalia iwapo mzee wetu alikiuka taratibu kweli za kumiliki ardhi kama ilivyodaiwa na wananchi hatua gani serikali tuchukue,”alisema. Alisema pia wanaweza kukaa na Sumaye na kuzungumza naye ili kukubali hasara kwa kutoa eneo kidogo na kuwapatia wananchi hao ambao hawana makazi au Manispaa kutafuta eneo mbadala na kuwauzia kwa bei nafuu.

Alizitaka pande hizo mbili kutambua umuhimu wa kulinda amani katika mgogoro huo kwa changamoto zilizopo kutatuliwa bila kutumia nguvu.Makonda pia aliagiza serikali ya kijiji kufanya utambuzi wa wananchi hao wenye makazi katika shamba la Sumaye. Awali katika mkutano huo Mhe. Sumaye alimueleza Mhe. Makonda jinsi serikali ilivyo na kazi ngumu ya kushughulikia migogoro ya ardhi na kuomba kutumia busara zake kumpatia eneo hilo analomiliki kihalali.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kama nilivyokueleza awali serikali yetu inakazi ngumu sana hasa kutokana na viongozi wa chini kutokuwa wasikivu na wakweli eneo hili namiliki kihalali nina nyaraka zote na ninalipia kila mwaka na nilikuwa katika mpango wa kutafuta wafadhili ili kuliendeleza kwa kujenga Chuo Kikuu,”alisema. Alisema yeye na familia yake waliuziwa eneo hilo toka mwaka 1997 na anaamini serikali itatenda haki.

Diwani wa kata hiyo Suzan Masawe alisema anauthibitisho kuwa eneo hilo lilikuwa pori na Sumaye alilitelekeza kwa muda mrefu na kusababisha uhalifu ikiwemo wanawake kubakwa,mali za wizi kufichwa na uhalifu mbalimbali. Alisema kutokana na hatua hiyo walimtafuta Sumaye lakini hakuwa na ushirikiano kwakuwa hata alipofanya uwekezaji kwa kuchimba kisima cha maji alikataa kuwapa wananchi .

Suzan alisema kutokana na hasira za wananchi hao kwa kukosa huduma za kijamii kwa muda mrefu ikiwemo eneo hilo kutokuwa na shule,Zahanati wala kituo cha polisi waliamua kuvamia na kujigaia maeneo. Mmoja wa wananchi hao Athuman Mnubi alikiri kweli hawana umiliki halali wa eneo hilo na katika hatua ya kutafuta makazi walivamia msitu huo uliotelekezwa na Sumaye.

Alisema wanaamini kutokana na ahadi ya serikali ya Rais Magufuli katika kupora maeneo yaliyotelekezwa na wawekezaji watasaidiwa. WAKATI huo huo Makonda alisimamisha na kukamata baadhi ya malori ya kokoto na mchanga, wafanyakazi na Mwekezaji wa kigeni kutoka India Sules Waljan wanaochimba mchanga,kokoto na kifusi katika eneo la Mabwepande. Hatua hiyo imekuja baada ya kuona uharibifu mkubwa wa mazingira na alipowahoji wafanyakazi na Mwekezaji huyo kama wanavibali walisema hawana.
Makonda amewafikisha watuhumiwa hao kituo cha polisi cha Wazo Hill ili kutoa maelezo ya kina na kusema kuwa serikali inatumia gharama kubwa kwa uhalibifu huo wa mazingira ambao pia unafanywa katika vyanzo vya maji na matengenezo ya madaraja yanayoharibiwa ni makubwa.

Murder in Burundi

By ELOGE WILLY KANEZA and RODNEY MUHUMUZA
Associated Press

   BUJUMBURA, Burundi (AP) - Satellite images, video footage and witness accounts show that dozens of people allegedly killed by Burundian security forces in December were later buried in mass graves, Amnesty International reported Friday.

   The report came as unrest in Burundi escalated with the arrest of 17 people in a security sweep, including two foreign journalists who were released later Friday.

   The rights group reported five possible mass graves in the Buringa area on the outskirts of the capital, Bujumbura, which has been wracked by violence as the security forces go into neighborhoods seen as opposition strongholds. Two journalists on assignment for the French newspaper Le Monde were among 17 people swept up in a military operation Thursday, said Moise Nkurunziza, a deputy spokesman for Burundian police.

   Journalists Jean-Philippe Remy of France and British photographer Philip Edward Moore were released on Friday afternoon, Le Monde said.

   Witnesses described how police and local officials scoured Nyakabiga and other neighborhoods in Bujumbura to retrieve the bodies of those who were killed late last year and took them to undisclosed locations, according to Amnesty International.

   "The imagery, dating from late December and early January, shows disturbed earth consistent with witness accounts. Witnesses told Amnesty International that the graves were dug on the afternoon of Dec. 11, in the immediate aftermath of the bloodiest day of Burundi's escalating crisis," the group said.

   Earlier this month, U.N. human rights chief Zeid Raad al-Hussein also called for an urgent investigation into the alleged existence of mass graves following the violence in December. Zeid said the "increasing number of enforced disappearances, coupled with allegations of secret detention facilities and mass graves is extremely alarming."

   Burundi's government has dismissed those allegations, saying they were based on false information supplied by the regime's opponents.

   In coordinated attacks, gunmen stormed three military installations in Burundi on Dec. 11. The next day, 28 people were found shot dead in three Bujumbura neighborhoods. An witness told The Associated Press that some of the dead had their hands tied behind their backs. Another witness blamed government security forces, saying they went after the victims in door-to-door searches.

   President Pierre Nkurunziza's decision to seek re-election to a third term last April touched off street protests that led to a failed coup in May and a rebellion that has left the central African country on the brink of civil war.

   The Burundian government has rejected the proposed deployment of African Union peacekeepers in Burundi, saying they will be treated as an invading force.

   ---

Saturday, January 23, 2016

Utawala wa Rais Magufuli


Rais Mstasfu Jakaya Kikwete Atunukiwa Shahada ya Udakatari ya Uhusiano ya Kimataifa

 Mkuu wa Chuo Kikuu  Huria cha Tanzania  (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika ana, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi  ya Kinondoni, Dar es Salaam. (Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog)
 Mkuu wa Chuo Kikuu  Huria cha Tanzania  (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari  ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi  ya Kinondoni, Dar es Salaam.
  Mkuu wa Chuo Kikuu  Huria cha Tanzania  (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari  ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi  ya Kinondoni, Dar es Salaam.
 Mkuu wa Chuo Kikuu  Huria cha Tanzania  (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimpongeza baada ya kumhudhurisha Shahada ya heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi  ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Wednesday, January 20, 2016

Dkt Kingwangalla Aunda Kikosi Kazi Kuboresha Suduma za Afya ya Jamii

IMG_0652

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla.

Na Rabi Hume, Modewjiblog

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameanzisha kikosi kazi cha watu 24 ambacho kitakuwa na kazi ya kutengeneza mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Katika taarifa ambayo imetolewa na Dkt. Kigwangala imeeleza kuwa kazi ya kuanzisha kikosi kazi hicho ni agizo kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ambaye alimtaka aanzishe kikosi hicho ili washirikiane kuanzisha mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii.

“Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu alinipa kazi ya kuunda kikosi kazi maalum na kushirikiana nacho kutengeneza mpango mkakati wa kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF),” alisema Dkt. Kigwangalla.

Dkt. Kigwangalla amewataja wajumbe wa kikosi kazi hicho kuwa ni Prof. Angwara Kiwara, Prof. Phares Mujinja, Dkt. Francis Frederick, Dkt. Heri Marwa, Dkt. Deogratius Pisa, Dkt. Amos Kahwa, Irenei Kiria, Semkae Kilonzo, Gemini Mtei, Dkt. Jehovaness Aikaeli na Obey Assey.

Wengine ni Mathias Kabunduguru, Dkt. Dereck Chitama, Prof. Flora Kessy, Florence Mwanri, Athuman Rehani, Maximillian Mapunda, Bedason Shallanda, Daniel Ngowi, Beng' Issa, Edwin Mikongoti, Hussein Sengu, Dkt. Beatus Leon na Dkt. Pastory Sekule.

Aidha Dkt. Kigwangalla amewashukuru wajumbe hao kwa kukubali kufanya kazi na wizara ya afya kupitia mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii bila malipo yoyote.

Hata hivyo mara baada ya kuwachagua wajumbe wa kikosi kazi hicho tayari kimependekeza mapendekezo yao jinsi ya kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii ambayo ni kuipa nguvu kadi ya CHF ili itumike kwenye mfumo wa Afya mpaka ngazi ya Hospitali za Rufaa za Mikoa na vituo vya Jirani na kupandisha kiwango cha kuchangia CHF mpaka 30,000.

Mapendekezo mengine ni kuweka bei za kukatisha tamaa watumiaji wa huduma za Afya bila kadi ya Bima ya Afya ama ya CHF na kuwahamasisha waamue kujiunga kuliko kulipa gharama za kila huduma watakayotumia, kuhamisha Mfuko wa fedha za CHF kutoka Halmashauri na kuupeleka NHIF ngazi ya mkoa lengo likiwa kumtenganisha mtoa huduma na mteja na kuweka 10,000 kuwa kiwango cha chini kwa bei za huduma za afya sehemu yoyote nchini kwa mtu asiye na kadi.

Aidha mapendekezo yao yatatumika kama serikali itayaridhia na wao wametoa mapendekezo hayo kutokana na kutambua kuwa Watanzania wapo tayari kulipia huduma za afya kwa bima ilimradi wawe wanapatiwa huduma bora ambazo zitawaridhisha.

No MiniSkirt Ban in Tanzania



PRESS RELEASE
NO BAN ON MINISKIRTS BY PRESIDENT MAGUFULI
The Ministry of Foreign Affairs, East African, Regional and International Cooperation of the United Republic of Tanzania has noticed, with serious concern and disapproval, a grossly distorted report in the KenyanStandard newspaper, purporting that H.E. President John Pombe Magufuli has banned the wearing of miniskirts in Tanzania.
Unfortunately, the false report, appearing in the daily newspaper's 'MondayBlues' gossip page on 18th January 2016, was taken for factual and circulated widely by other outlets and the social media in Kenya and beyond.
The ministry deplores the casual manner in which the Standard handled the hearsay report and the reckless, totally unwarranted attribution of the imaginary 'ban' to the Tanzania Head of State.
While it appreciates the enthusiastic, positive reviews of H.E. President Magufuli's performance in the Kenyan and international media, the Ministry of Foreign Affairs takes strong exception at irresponsible distortions and misreporting, such as the one on miniskirts.
There is no doubt that H.E. President Magufuli and his government are strong proponents of decent dressing, but the ministry wishes to put the record straight that the President has not issued any ban on miniskirts for any reason.
The ministry understands that as a mainstream newspaper, the Standard is obliged to observe the highest standards of journalism, central of which is respect for facts and accurate reporting.
The ministry trusts that the distortion in question was inadvertent, not a malicious attempt to undermine the new administration in Tanzania, and that the Standard will show good faith by at least retracting the wrong information fed to its readers.
Ends

Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs, East African,
Regional and International Cooperation.
Dar es salaam.
January 20, 2016


Saturday, January 16, 2016

Ndoto ya Dr. Martin Luther King Jr


Marehemu Dr. Martin Luther King Jr. alipigania haki za watu weusi Marekani. Aliota kuwa siku moja wazungu hawatabagua weusi na kutuheshimu. Aliuawa na Mbaguzi mwaka 1968 akiwa na miaka 39.

Kwa Habari zaidi za Dr. King BOFYA HAPA:

Friday, January 15, 2016

Taswira Mbovu ya Barabara ya Market Street Mjini Mwanza

Hii ni barabara inayotegemewa na daladala za Bwiru-Kisesa, Airtport- Kishiri pamoja na Ilemela-Kishiri hii ikiwa ni kwa upande wa daladala. Lakini pia ikitegemewa na watumiaji wengine wa vyombo vya moto vya binafsi.
Ni barabara iliyotumika pia na wakazi wengi wa Jiji la Mwanza wakiwa wanatoka katika mizunguko yako ikiwemo kutoka Soko Kuu la Jiji la Mwanza. Kama inavyoonekana katika picha inahitaji msaada maana wakati huu wa mvua imeharibika sana.

"Hii barabara inaharibika mara kwa mara kutokana na mitaro iliyopo hapa kuziba mara kwa mara kutokana na wafanyabiashara katika maeneo haya kuwa na tabia ya kutupa makopo mitaroni na hivyo kusababisha mitaro kuziba na hivyo mvua ikinyesha maji yanajaa katika barabara hii na hatimae kusababisha hali hii unayoiona". Binagi Media Group imeeleezwa na baadhi ya wafanyabiashara waliopo jirani na barabara hiyo.

Watumiaji wa barabara hiyo wameiomba halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kushughulikia ukarabati wa barabara hiyo pamoja na kusimamia suala la usafi ili kuzuia uchafu kutupwa katika mitaro iliyo katika barabara hiyo ili kuzuia kuziba na hatimae kusababisha uharibifu katika barabara hiyo.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @BMG

Thursday, January 14, 2016

Maombi ya Kumombea Rais Magufuli na Serikali Yaka Mjini Mwanza

Viongozi mbalimbali wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo (wa pili kushoto walioshikilia bendera), katika Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo @Binagi Media Group (BMG)
Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza kwa kushirikiana na Umoja wa Maaskofu kutoka Jijini Dar es salaam jana January 13,2015 ulifanya Mamombu Maalumu ya Kumuombea Rais wa wa awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli pamoja na Wasaidizi wake.

Maombi hayo yalifanyika katika Uwanja wa Furahisha Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali na Dini huku pia wananchi wakijumuika pamoja na waumini wa dini mbalimbali katika maombi hayo.

Mgeni Rasmi katika maombi hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo ambae katika hotuba yake, aliwasihi Watanzania wote kuendelea kuliombea Taifa ili kuondokana na vikwazo mbalimbali ambapo alidokeza kuwa kupitia maombi kama yaliyofanyika jana, migogoro mbalimbali ikiwemo ya kisiasa kama iliyopo Zanzibar itamalizika.

Viongozi mbalimbali wakiwemo Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Askofu Charles Sekelwa, Makamu wake Zenobius Issaya pamoja na Kiongozi wa Kundi la Maaskofu kutoka Jijini Dar es salaam la Good News For all Ministry Askofu Dr.Charles Gadi pamoja na viongozi wengine wa dini kutoka mikoa mbalimbali nchini waliliombea Taifa na kuhimiza utuliza nchini.

Wasaidizi wa wa Rais Maguguli ambao ni pamoja na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu, Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu Mhe.Othman Chande, Spika wa Bunge Mhe.Job Ndugai, Mawaziri pamoja na viongozi wengine wa Serikali wa awamu ya tano waliombewa ili kuliongoza vema taifa kwa kuendana na kasi ya Rais Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, ia maombi hayo yalijumuisha toba kwa taifa, kumuomba Mungu kukomesha mauaji ya Vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kuombea taifa mvua zisizo na madhara. 
Viongozi mbalimbali wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo (Wa tatu kushoto) katika Maombi ya Kumuombea Rais Magufuli na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Viongozi mbalimbali wa dini
Maombi ya kuliombea Taifa yaliyofanyika Jijini Mwanza jana
Viongozi mbalimbali wa dini wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Kulia ni Mwenyekiti Msaidizi wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Zenobius Isaya akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Mwenyekiti Msaidizi wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Zenobius Isaya akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Mmoja wa Viongozi wa dini akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Jijini Mwanza Askofu Charles Sekelwa  akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Kiongozi wa Kundi la Maaskofu kutoka Jijini Dar es salaam Askofu Dr.Charles Gadi akiwa katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Viongozi wa dini
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo akizungumza katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo akizungumza katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Kwaya ya EAGT Mabatini Jijini Mwanza ikitumbuiza katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Wanahabari katika kunasa habari kwenye Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.
Meneja wa HHC Alive Fm Radio ya Jijini Mwanza (Kulia) akiwa pamoja na GB Pazzo (Kushoto) katika Maombi ya kumuombea Rais Magufuli, wasaidizi wake pamoja na Taifa yaliyofanyika jana Jijini Mwanza.

Saturday, January 09, 2016

Unaweza Kutajrika na Powerball Sasa Jackpit ni Dola $900 Milioni!!!


POWERBALL JACKPOT INCREASED TO $900 MILLION
Top prize in Saturday night’s drawing is largest jackpot in U.S. lottery history
BRAINTREE, MA (SATURDAY, JANUARY 9, 2016) The Powerball jackpot for tonight’s drawing has been increased for the third time in as many days and now stands at an estimated $900 million. The cash option on the prize is now an estimated $558 million.
Last hit on November 4, 2015, this jackpot has been growing for 18 consecutive drawings without a top prize winner.  The $900 million jackpot eclipses the previous U.S. lottery record of $656 million that was split by three winners in the Mega Millions drawing on March 30, 2012.  Powerball’s highest-ever jackpot had been $590.5 million, won on May 18, 2013.
Powerball tickets are $2 each and can be played in 44 states, Washington D.C., Puerto Rico and the U.S. Virgin Islands. Tickets for tonight’s drawing can be purchased until 9:45 p.m. this evening at any Massachusetts Lottery retailer in the state. Drawings are held every Wednesday and Saturday at 10:59 p.m. EST in Tallahassee, Florida.
Powerball drawings are available locally via the Lottery’s website – masslottery.com, and can also be viewed on the Lottery’s official Facebook, Twitter and YouTube accounts.

Picha Rasmi ya Rais John Pombe Magufuli

Picha Rasmi ya Rais Magufuli (Official Portrait)



Picha rasmi ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli imetoka leo (Januari 8, 2016) katika Ofisi ya Idara ya Habari (Maelezo) Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Zamaradi Kawawa, amesema kuwa Picha hiyo ya Rais Magufuri kwa kila moja itauzwa kwa shilingi 15,000 ya Kitanzania (bila fremu), huku picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ikiuzwa kwa sh. 5,000/=.

Chanzo cha habari: http://www.channelten.co.tz/rasmi-picha-ya-rais-magufuli-itakayotumika-katika-ofisi-za-serikali/

Saturday, January 02, 2016

Sababu ya Mwimbaji Ommy Dimpoz Kufungwa Jela Marekani

Mwimbaji maarufu wa Bongo Flava, Ommy Dimpoz (28) alifungwa jela Marekani katika ziara yake ya hivi karibuni.  Alifungwa jela huko Minnesota. 

Si kweli kuwa alikutwa na madawa ya kulevya kama wengine walivyodai.  Tatizo, Ommy hakuwa na Visa ya kumruhusu kufanya kazi Marekani. Alitakiwa kuwa na O-1 Visa ambayo wanapewa wasanii.  Wale wafadhili wake walifanya makosa katika kumwombea Visa hasa kama walijua atafanya show kubwa kinachotangazwa sehemu nyingi na kiingilio kikubwa. Uncle Sam (Serikali ya USA) anataka hela yake (kodi).  Inaelekea alivyochelewa ndege ilifanya maswali mengi kuulizwa.

Mimi kama Msanii ninaelewa process ya kuomba Visa ya Usanii.  Zinatolewa kiasi fulani kila mwaka na nyingi zinaenda kwa wasanii kutoka Canada, Ulaya, na  nchi za Marekani ya Kusini (South America). Chache sana zinaenda kwa wasanii kutoka Afrika.  Navyoona kulikuwa na njama za kumwonea Ommy hapa USA. Nani aliwaambia hao polisi kuwa hana Visa ya Usanii na wamhoji huko uwanja wa ndege.

Pole sana Ommy  Dimpoz.


Msanii wa Bongo Flava Ommy Dimpoz


Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:


Pia unaweza kusoma maelezo ya Dimpoz  HAPA: