Monday, August 31, 2009

Katika Hifadhi ya Wanyama Mikumi

Ramadhani Njema Kutoka Jamii Forums


JamiiForums.com The Home of Great Thinkers inapotimiza miaka 3 tangu kuanzishwa kwake, inapenda kuwatakia watanzania wote pamoja na wadau wote mitandaoni mfungo mwema na kuwatakia kila lililo jema katika mwezi huu.

"Enyi Mlioamini! Funga ya Ramadhani imefaradhishwa kwenu kama ilivyokafaradhishwa kwa wale waliokuwa kabla yenu ili mpate TAQWA"(QURAAN Surah Al-Baqarah 2:183)Unakaribishwa kwa mijadala huru ili ushiriki na wazalendo wenzako. Tembelea www.JamiiForums.com
JF Management

Introducing Elite Model Tanzania


Compass Communications Company Limited introduces the largest and most prestigious modeling international competition in the world - Elite Model Look.

Compass Communications Company Ltd is an independent TV production company that produces various TV programs and also is the organizer of Miss Universe Tanzania and other beauty pageant titles like Miss Earth, Miss International and Miss Tourism Queen International in Tanzania.

The company has now branched out into a more specialized part of the industry namely professional modeling. Elite Model Look contest was created in 1983 under the name Look of the Year. Elite Model Look competition is the largest model contest of its kind. This contest has become one of the most prestigious springboards for talents into the modeling industry.

Up to now Elite Model Management is present in 5 continents and it represents more than 2,000 (Two Thousand) models internationally. Each year, the Elite Model Look competition sees over 350,000 contestants attend regional and national castings that take place in more than 55 different countries, with at least one contestant of each country participating in the main event - the World Final..

The competition is made of several steps. Thus, through an intensive and rigorous selection process, which drives them from regional castings to national finals, at least one local contestant of each country gets a chance to participate in the World Final.

Here in Tanzania Compass Communications will hold local auditions in Dar-Es-Salaam : where all applying contestants will be narrowed down to 10 to 15 semifinalists. No final event will be held this year in Tanzania and the 10 - 15 semifinalists will then be judged by a panel of judges including a representative from Elite Model Look headquarters in Paris, France, in order to find the Tanzanian model who will represent Tanzania in the World Finals in October in Sanya, China.

All girls are invited to make their dreams come true by participating in auditions of Elite Model Look Tanzania. The auditions are open to strictly girls aged 14 to 20 years, with the minimum height of 172 cm.

The winner will be selected to meet the fast changing trends and needs of the fashion industry. She will be chosen based on photogenic quality, personality and natural beauty. From the approximately 70 finalists at the World Finals, 15 are chosen by an international panel of judges and they all sign an exclusive contract with Elite Model management.

And out of the 15 luck ones, 3 are voted as winners. The top 3 winners will share a guaranteed remuneration of 325,000 USD in total as modeling contract.

This is the first time for Tanzania to hold the license and to select a finalist for Elite Model Look although in 1999 Miriam Odemba was selected and participated successfully in the Elite Model Look World Final in Nice, Paris through MNet Face of Africa.

For more information kindly contact

Maria Sarungi Tsehai
OR
Mwanakombo Salim,

Compass Communications,
Tel: (022) 2182405, 2182596
Mob: 0784 305122

Sunday, August 30, 2009

Maonyesho ya Filamu Hadharani Marufuku-Mkuchika

Naona wanapunguza milo ya watu! Yaani leo ndo wanarudisha Bodi ya Ukaguzi wa Filamu! Video na DVD zilivyozagaa nchini Bongo mbona watakuwa na kazi ngumu!

**********************************************************
Kutoka ippmedia.com

Na Mwandishi wetu

Serikali imepiga marufuku maonyesho yote ya filamu kwenye hadhara ya watu, majumba yasiyo rasmi, hoteli na maeneo ya baa bila kufuata masharti kwa mujibu wa Sheria.

Agizo hilo limetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika, wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu nchini ambayo itakuwa na jukumu la kukagua na kusimamia maonyesho na shughuli za filamu nchini.

Alisema sehemu nyingi zinazotumiwa kuonyesha filamu hazina leseni halali za kuonyeshea na kuongeza kuwa sio salama kwa mali na afya za watu. “Nachukua fursa hii kutoa onyo kwa mtu yeyote atakayeonyesha filamu kwenye hadhara ya watu katika majumba yasiyo rasmi, vibanda, kumbi ndogondogo, hotelini, baa na katika vyombo vya usafiri waache mara moja,” alisisitiza.
Alifafanua kuwa sehemu nyingi zinazotumika kuonyeshea filamu sasa hazikidhi matakwa ya ujenzi wa kumbi za kuonyeshea filamu na ni kinyume cha sheria kwani nyingi zimekuwa chanzo cha maficho ya wahalifu, majambazi, biashara ya dawa za kulevya na kuchochea vitendo vya ngono kwa vijana.

Alisema athari nyingi tayari zimeshajitokeza katika jamii yetu na kuongeza kuwa filamu nyingi zimechangia kubomoa na kudunisha Utamaduni wa taifa letu na hata kuchangia kwa kiasi kikubwa kubomoa misingi ya amani , Upendo , Uadilifu, heshima, uaminifu na utu ambao ni utambulisho wa mtanzania jinsi ulivyokuwa umejijenga na kuenea katika jamii yetu.
Aidha alisema serikali iko makini kuhimiza na kusisitiza matumizi ya sanaa katika masuala mbalimbali ya maendeleo na kuvitambua , kuvikuza na kuviendeleza vipaji vya wasanii katika kukuza taaluma na fani ya filamu nchini.

Awali akizungumza kuhusu majukumu ya Bodi hiyo, alisema kuwa Bodi itakuwa na jukumu la kuweka misingi ya kuimarisha utaratibu wa usimamizi wa utengenezaji wa filamu na pia kutoa vibali vya kutengeneza filamu hapa nchini.

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Rose Sayore ameihakikishia serikali kuwa Bodi yake itafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kuhakikisha kuwa kanuni, sheria , maadili na taratibu za uonyeshaji na utengenezaji wa filamu zinazingatiwa kwa maslahi ya watanzania na vizazi vijavyo.

Saturday, August 29, 2009

Mazishi ya Senator Kennedy


Leo mji wetu wa Boston umejaa viongozi karibu wote wa Marekani. Ma Senator wote wapo hapa, Rais Obama, Bush II, Carter wapo, pia kuna maGavana kadhaa! Kisa, wako kwenye mazishi ya Senator Edward Kennedy. Misa ya kumwombea inafanyika kwenye kanisa kuu la kikatoliki (Our Lady of Perpetual Help) ya ghetto letu, Mission Hill! Ghetto imekuwa ikisafishwa tangu juzi, yaani naangalia kwenye TV nasema kweli ndo Tremont St. hiyo! Lakini sisi makamchape hatuwezi kusogea karibu na hapo! Ulinzi mkali mno! Tunaangalia kwenye TV!

Thursday, August 27, 2009

Wimbi la Kutoa Mimba Dar!

Navyoona wasichana was shule na wanawake wafundishwe uzazi wa majira. Pia wakazanie hao wanaume wao watumie kondomu. Pia wanaume na nyege zao waache kudanganya wanawake, "Oh usiponipa ina maana hunipendi!" au wanasema, "Usiponipa nitampata atakayenipa!"

LOH! Nyie, nakumbuka kuona wanafunzi wenzangu wakifa kwa septic abortion.
Nimeona wakiteseka kwa maumivu na kuoza na kufa! Kisa walienda kwa watu wasiojua wanafanya nini kuzitoa. Napenda kuwe na sehemu ambayo mtu anaweza kuwa na sehemu ya kutoa mimba kwa usalama. Lakini pia sipendi wazo la kutoa mimba. Lakini kwa vile bado kuna sheria za ajabu, eti msichana akipata mimba afukuzwe shule, wengine wanalazimishwa kutoa ili waendelee na masomo.

********************************************************
Kutoka ippmedia.com

ABORTION BUSINESS BOOMING IN DAR

Most private and some public dispensaries, health centres and hospitals camouflaged as family health planning units are centres for performing abortions, ‘The Guardian’ can report today.

A survey carried out over the last two weeks has revealed shocking statistics on health facilities engaged in abortions. A clinic in the city (name withheld) performs as much as 40 abortions per month, raising questions on safety and the health risks posed to their clients.

The Executive Director of Muhimbili National Hospital Prof Leonard Lema said that the institution does not perform abortions, but is forced to save the lives of the victims who are rushed to the hospital in critical state after bleeding seriously from unsafe abortion.

“Some victims are brought to us in a serious condition, bleeding so we help them in cleaning the blood clots so as to save their lives,” he said

Another gynaecologist from Muhimbili who preferred not to be named said that the government was ‘quiet’ about abortion and yet the practice is going on in many private hospitals and clinics.

“Professionally it can only be performed after clearance of two specialists when there is an adequate risk to the mother’s life if the foetus is retained,” he said.

He also noted that while abortion is going on, the rate of crude abortions is on the decline especially since the doctors who do it have adopted the use of the MVA (Manual Vacuum Aspiration) kits to carry out the illegal surgery.

Almost every private hospital checked during the investigation that covered more than 10 of them in Dar es Salaam, the story was the same, “You want to have an abortion? You will get it, just pay for it.”

The cost of the services is high. Some of the clinics have resorted to abortions as the quickest and most reliable way of generating income.

“Yes the majority of women coming here for gynaecological services want to abort…you cannot stop them, so we just help them do it in the safest way without subjecting their lives to danger,” said a gynaecologist at one of the clinics.

He said charges vary depending on how old the pregnancy is. For example it would cost 70,000/- to terminate a six-month pregnancy, while anything below that would cost 50,000/-.

The clients include students, unmarried and married women, according to our investigation. Another gynaecologist said it was difficult to turn away pregnant mothers who visited the clinics crying for help.

Two months ago a mother of a family residing at Mbezi Beach in Dar es Salaam, lost her only daughter, a 15 – year old, who took tablets prescribed by a quack doctor to induce an abortion.

The daughter had obtained a week’s leave from school in Arusha after complaining that she was not feeling well.

“When at home in Dar she seemed to lose her appetite and ate very little. I didn’t know what was going on because her condition got worse by the day, yet when I wanted to take her to hospital; she refused, telling me she had already taken malaria tablets. However her condition became worse,” the mother narrated.

She rushed her to hospital and after the usual medical tests, a drip was administered on the girl, but after 30 minutes, she passed away

“We were shocked to learn that she had been bleeding intensively. One doctor told me that she couldn’t make it because she had taken some tablets to abort,” the mother said, tears streaming down her face.

She said that she was shocked by the news and couldn’t believe that her daughter had been pregnant, opted for an abortion and never told her. She learnt from the doctor that the tablets which her daughter took worsened her condition, rupturing the foetus which was also rotting inside her, resulting into more complications which caused her death.

The woman talking to a friend later learnt that women who opt for abortion in most of these clinics in the neighbourhood are given an option of using either the tablets or a vacuum machine. Her daughter had probably been afraid to use the vacuum and went for the pills.

“She was the only daughter I had because her siblings are boys. It is like a nightmare to me up to now. It is important for these girls to be told and taught about pregnancy, abortions and their effects,” she said.

In a separate interview, Jangwani school teacher Grace Michael said that abortions happen frequently in secondary schools and can only be controlled if the students are made aware of the negative effects.

“Some of them who are day students have an abortion and we never know about it because one can decide to stay home for sometime after the operation to recover before resuming school. Sometimes, it is hard to identify such students,” said Michael.

She added that in some schools students are taken to hospital every month for pregnancy test and those found positive end up dropping out of school.

“I think there is still a lot to be done to protect students from getting pregnant and having abortions because the rate has really gone up,” she added.

A Makongo Secondary School student, Amina Abdul, said that as long as the students get pregnant and are still in school, abortions are likely to happen because they want to finish school.

“There is a lot to be done to create awareness among the students because abortion is performed as if it’s a simple issue. If you have money it can be performed, but it is dangerous when someone uses tablets. It is better to have the vacuum system. I haven’t experienced this, but I have heard other students talk about it,” she said

Another student, Anna Msekwa said that the rate of abortions has gone up especially for those girls who are staying in hostels.

“The rate has really gone up especially in boarding schools and hostels. This worsens during the cold months… and if it happens you have to do something before your parents become aware,” she said.

Residents in various parts of Dar es Salaam said that many institutions operating as family life health clinics were actually havens for performing abortions. Almost every member of the public who was interviewed concurred that the crime was rampant in the city.

“It is an open secret that hospitals in Dar es Salaam do perform abortions. A woman walks into a clinic and no one bothers to ask who made her pregnant. Most hospitals here are not there to treat patients but to perform abortions,” said Ali Omar a resident of Mbagala

Joyce Michael a resident of Mbezi in Dar es Salaam said some clinics were so careless that after inducing abortions they didn’t clean the tools they had used.

“So many women have been infected with diseases after undergoing abortions in some of the so–called private hospitals in Dar es Salaam. They know that women who are going for abortions in secret are desperate so they take advantage of them,” she said.

The deputy minister for Health and Social Welfare Aisha Kigoda said that most private hospitals perform abortions secretly because it is illegal, but warned that if such hospitals are exposed and evidence provided, they will be prosecuted.

“Private hospitals are performing abortions in secret because they know it’s illegal, but I am warning them that if they are caught with evidence, then legal action will be taken against them, including withdrawing their licenses,” said Kigoda.

She said that the government is planning to formulate a set of laws to allow for safe abortion so as to reduce mortality rate in the country.

“The government is still thinking over the proposals. We have to look at the advantages and disadvantages of such a move,” said Kigoda, refusing to be drawn into stating when the laws on safe abortion will be in place.

SOURCE: THE GUARDIAN

Mrembo Auwawa Dar!

Sijui na sikuwepo lakini baada ya kusoma hii habari niliona kama hao waliomwua mrembo, Tina Athumani (25), walitumwa kufanya hivyo! Mnaonaje wadau?

**************************************************************
Kutoka ippmedia.com

27th August 2009

Mrembo mmoja anayefahamika kwa jina la Tina Athumani, 25, mkazi wa Jijini, ameuawa kikatili na watu wasiojulikana baada ya kuvamiwa usiku na kucharangwa mapanga na kisha mwili wake kuachwa mbele ya nyumba anayoishi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Mark Kalunguyeye, ameiambia Alasiri leo asubuhi kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo, majira ya saa 7:00, pale katika eneo la Kunduchi Salasala ambako ni nje kidogo ya Jiji.

Kamanda Kalunguyeye amesema kuwa mwanadada huyo, amekutwa na umauti baada ya kukubali wito wa kutoka nje ambako alikuwa amesikia mayowe na hivyo kutaka ajue kinachoendelea.

Akasema, mara baada mwanadada huyo kutoka nje, ndipo alipokumbana na watu watatu ambao walimvuta pembeni ya nyumba na kuanza kumcharanga mapanga, pasi na sababu za kufanya hivyo kufahamika.

Hata hivyo, watu hao ambao dhamira yao haikufahamika, waliuvuta mwili wa marehemu huyo pembezoni mwa nyumba yake na kuutelekeza hapo na kisha kutokomea kusikojulikana.

Kamanda Kalunguyeye amesema hadi sasa, Polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi ili kuweza kuwapata wauaji na hatimaye kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Wasichana 12 Wafa Baada ya Bweni Kuungua Moto!

Kuna ajali ya moto iliyotokea huko Iringa juzi katika bweni la wasichana wa shule ya sekondari Idodi. Jamani eti hao mabinti walifungwa bwenini usiku kusudi wasitoroke! Kama watataka kutoroka watatoroka tu hata wawafungeje! Sasa hao mabinti wamekufa katika moto na maiti zao hazikuweza kutambulika. Mbona inasikitisha! Hivi kwenye hiyo shule hakuna walinzi?

*********************************************************************

Tanzania buries school fire dead

Hundreds of mourners have attended the mass burial in Tanzania for 12 girls who died in a dormitory fire.

The BBC's Josephat Mwanzi said the bodies, which were burned beyond recognition, were put in separate graves with numbered markers.

Their names will be added to the graves in school in Idodi, 460km (285 miles) west of Dar es Salaam, when the results of DNA tests are known.

The fire is thought to have been caused by a student reading by candlelight.

Police say it probably set light to a mosquito net and the flames spread through the dormitory at Idodi Secondary School on Saturday night.
shul
Our reporter says parents and pupils gathered around the graves to see the coffins being lowered.

He said it was heartbreaking to watch and many of the mourners were in tears.

Afterwards, some of the pupils said the girls' dormitories at the school were often locked at night to stop them going out.

Fourteen girls who were seriously injured in the fire are being treated at a hospital in nearby Iringa town.

Nine others are being looked after in Idodi village - and at least two of them attended the funeral.

After the funeral, the pupils were sent home for three weeks so a new dormitory can be built.

Officials had earlier said the dead would be buried in a mass grave because their bodies had been burnt beyond recognition.

Scores of schoolchildren have died in similar incidents in neighbouring Kenya and Uganda in recent years

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/8219940.stm

Wednesday, August 26, 2009

President Obama's Message on the Death of Ted Kennedy

Michelle and I were heartbroken to learn this morning of the death of our dear friend, Senator Ted Kennedy.

For nearly five decades, virtually every major piece of legislation to advance the civil rights, health and economic well-being of the American people bore his name and resulted from his efforts.

His ideas and ideals are stamped on scores of laws and reflected in millions of lives -- in seniors who know new dignity; in families that know new opportunity; in children who know education's promise; and in all who can pursue their dream in an America that is more equal and more just, including me.

In the United States Senate, I can think of no one who engendered greater respect or affection from members of both sides of the aisle. His seriousness of purpose was perpetually matched by humility, warmth and good cheer. He battled passionately on the Senate floor for the causes that he held dear, and yet still maintained warm friendships across party lines. And that's one reason he became not only one of the greatest senators of our time, but one of the most accomplished Americans ever to serve our democracy.

I personally valued his wise counsel in the Senate, where, regardless of the swirl of events, he always had time for a new colleague. I cherished his confidence and momentous support in my race for the Presidency. And even as he waged a valiant struggle with a mortal illness, I've benefited as President from his encouragement and wisdom.

His fight gave us the opportunity we were denied when his brothers John and Robert were taken from us: the blessing of time to say thank you and goodbye. The outpouring of love, gratitude and fond memories to which we've all borne witness is a testament to the way this singular figure in American history touched so many lives.

For America, he was a defender of a dream. For his family, he was a guardian. Our hearts and prayers go out to them today -- to his wonderful wife, Vicki, his children Ted Jr., Patrick and Kara, his grandchildren and his extended family.

Today, our country mourns. We say goodbye to a friend and a true leader who challenged us all to live out our noblest values. And we give thanks for his memory, which inspires us still.

Sincerely,

President Barack Obama

Rest in Peace Senator Edward Kennedy


1932-2009

Senator wetu mpendwa, Edward M. Kennedy, amefariki dunia leo asubuhi huko nyumbani kwake Hyannisport, Massachusetts. Alikuwa anaumwa ugonjwa wa kansa ya ubongo. Senator Kennedy alikuwa mdogo wake rais John F. Kennedy aliyeuawa mwaka 1963. Senator Kennedy alipendwa sana kwa kuteteta haki za wanyononge Marekani na hapa Massachusetts. Asante ssenator Kennedy, maskini hapa Massachusetts wana unafuu wa maisha kuliko sehemu zingine. Kama mtu alikuwa na shida za uhamiaji na matatizo mengine waliweza kumwendea kumomba msaada. Alisaidia maelfu ya watu.

Kwa sasa watu wa Massachusetts tuna majonzi. Atakumbukwa daima.

REST IN ETERNAL PEACE SENATOR KENNEDY!

Monday, August 24, 2009

Ajali ya Basi Tanzania



Nimekuta hii You Tube. Ilitokea Februari 18, 2008. Ila haisemi barabara gani.

Kifo cha Michael Jackson Sasa ni Kesi ya Mauaji!!!


Duh! Kumbe Michael Jackson aliuawa na daktari wake! Makubwa!

***************************************************************
Coroner rules Jackson's death homicide

LOS ANGELES - The Los Angeles County coroner has ruled Michael Jackson's death a homicide, a law enforcement official told The Associated Press, a finding that makes it more likely criminal charges will be filed against the doctor who was with the pop star when he died.

The coroner determined a fatal combination of drugs was given to Jackson hours before he died June 25 in his rented Los Angeles mansion, according to the official who spoke on condition of anonymity because the findings have not been publicly released. Forensic tests found the powerful anesthetic propofol acted together with at least two sedatives to cause Jackson's death, the official said.

Dr. Conrad Murray, a Las Vegas cardiologist who became Jackson's personal physician weeks before his death, is the target of a manslaughter investigation by the Los Angeles Police Department. According to a search warrant affidavit unsealed Monday in Houston, Murray told investigators he administered a 25 mg dose of propofol around 10:40 a.m. after spending the night injecting Jackson with two sedatives in an unsuccessful attempt to get him to sleep.
The warrant, dated July 23, states that lethal levels of propofol were found in Jackson's system. Besides the propofol and two sedatives, the coroner's toxicology report found other substances in Jackson's system but they were not believed to have been a factor in the singer's death, the official said.

Murray has spoken to police and last week released a video saying he "told the truth and I have faith the truth will prevail." His attorney, Edward Chernoff, had no immediate comment but has previously said Murray never administered anything that "should have" killed Jackson.
A call to the coroner's office was not returned Monday.

Murray did not say anything about the drugs he gave to Jackson

Sunday, August 23, 2009

Hashim Awaponda Wanaotaka Kumgeuza Ngazi!

Na Mpoki Bukuku

NYOTA wa mchezo wa kikapu wa Tanzania, anayecheza katika ligi ya NBA ya Marekani Hasheem Thabeet amesema viongozi wa mchezo huo nchini wasimtumie kama ngazi kwani mafanikio aliyoyapata ni juhudi zake binafsi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi usiku katika hafla iliyoandaliwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Larry Andre, Hashim alisema ameshangazwa na viongozi wengi kumtumia yeye kama daraja kwa kujidai kuwa ndio waliomsaidia hadi hapo alipofikia wakati si kweli.

''Nadhani kuna watu wanataka kujinufaisha kwa kusema wamenisaidia kwa ajili ya uchaguzi wa chama chao, lakini si kweli. Nashangaa baadae wengine wamenifuata hadi Marekani na kudai kuwa wametumwa kunipongeza alisema."

Hashim alikuwa akimaanisha baadhi ya viongozi waliomfuata huko kwa madai wametumwa na Rais Kikwete kwa kuwa amekuwa akimtembelea mara nyingi na kumpa moyo.

Akizungumzia kuhusu mchezo huo nchini, Hashim alisema mpira wa kikapu utachukua miaka mingi kufikia mafanikio kwa kuwa viongozi hawana nia ya kusaidia wachezaji.

''Watu wanaohusika ndio wanafanya mchezo huu ushindwe kuendelea kwani tangu niondoke nchini hadi sasa, hali ni ileile hakuna maendeleo, hata viwanja viko katika hali ileile,'' alisema.

Alitahadharisha kuwa kutokana na hali hiyo itakuwa vigumu kwa Mtanzania mwingine kupata nafasi kama yake kwa hapa nchini bila ya kujipeleka mwenyewe kwa juhudi zake, ìlabda mmoja katika milioni moja sijui kama itatokea.''

Chanzo: Gazeti la Mwananchi 08-18-2009

Tanzia - Dr. Abdulhashim Masudi

Wadau, nimepokea habari za kusikitisha ya kifo cha Dr. Masudi leo hii. Alifariki mwezi uliopita 27/7/09. Poleni sana wafiwa na hasa mjane wake Da Flora.

Mola Ailaze Roho Yake Mahala Pema Peponi. AMIN.

*************************************************************
Waungwana,

Dr. Abdulhashim Masudi aliyekuwa Mhadhiri Mwandamizi, na Mkuu wa Skuli ya Elimu, Chuo Kikuu cha Dodoma amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya mkoa wa Dodoma. Maziko yanatariwa kufanyika kesho kijiji kwao Usangi. Kabla ya kifo chake, Dr. Masudi aliwahi kutumikia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Elimu kuanzia mwaka 1985 hadi 2007 alipojiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma.

Inna Lilahi wa Inna Illaihi Raj'uun

Subira

Saturday, August 22, 2009

Ramadhani Karim!

Ninawatakia wadau WaIslamu wote Mfungo Mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Rais Obama Atuma Salamu za Ramadhani



Mwezi Mtukufu wa Ramadhani umefika. Rais wa Marekani, Barack Obama amewatumia waislamu wote salamu. Nadhani ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kutuma salamu za Ramadhani kwa waislamu nchini Marekani na duniani pote. Nampongeza Rais Obama kwa ushujaa wake wa kutoogopa maneno ya wazungu wasioelewa kuwa dunia imebadilika.

Friday, August 21, 2009

Update - Hali ya Peter Owino

NDUGU JAMAA NA MARAFIKI,

FAMILIA YA OWINO INATANGULIZA SHUKRANI TELE KWENU NYOTE MLIOTOA HUDUMA YA AWALI/HARAKA KWA KAKA YETU PETER MARA ALIPOFIKISHWA HOSPITALI YA BUGANDO KWA MATIBABU MARA BAADA YA KUVAMIWA NA MAJAMBAZI AKIWA SAFARINI KWENDA SHIRATI KUPITIA BARABARA KUU YA KATI.

KHERI PIA KWA MADAKTARI WOTE WA BUGANDO KWA TIBA NZURI NA MAKINI.

SHUKRANI PIA KWA MARAFIKI NA WATANZANIA WOTE WALIOPATA FURSA KUMJULIA KHALI NA KUTUMA SALAAM ZA TIBA NJEMA NA MAOMBI YA UNAFUU WA HARAKA. MUNGU AWABARIKI.

AIDHA TUNAWASHUKURU MLIOHUZUNIKA ZAIDI NA KUTAKA KUANDAA MICHANGO YA ZIADA ILI KUSAIDIA KTK HUDUMA YA TIBA KWA PETER. NAOMBA NIWAHAKIKISHIE KUWA TUNATHAMINI ARI YA UPENDO HUO LAKINI FAMILIA IMEWEZA NA INAENDELEA KUMUDU HUDUMA ZOTE ZA TIBA VIZURI KWA SASA. PETER AMETOKA HOSPITALI NA ANAPONA HARAKA NYUMBANI.

FAMILIA HAIJAANDAA UTARATIBU WOWOTE WA MICHANGO NA TAFADHALI MASHAURI KAMA HAYA LAZIMA YAWE NA IDHINI YA FAMILIA.

KWA UPENDO NAWASHUKURU NYOTE, MUNGU AWABARIKI.
Maina Ang'iela Owino

k.n.y FAMILA YA OWINO

Thursday, August 20, 2009

Mzungu Auwawa Zanzibar

Mazishi yalifanyika huko Ireland juzi , ya Robert De Courcey Stringer (26). Alikutwa kwenye ufukwe wa Zanzibar tarehe 8/8/09 akiwa amepigwa kichwani na kuibiwa mali yake. Alikuwa Zanzibar akifanya kazi na mradi wa 'Camara' ambayo ina gawa computer zilizotumika (second hand) na teknolojia zingine kwa watu. Hivi huko Zanzibar siku hizi kuna nini? Zamani ulikuwa husikii habari ya wizi.

Mwaka jana wageni wa Cristal Resort walivamiwa na kuibiwa mali yao zaidi ya mara moja.

Na majuzi kuna wazungu waliibiwa mali yao kwenye beach Zanzibar.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.irishtimes.com/newspaper/breaking/2009/0818/breaking31.htm

http://www.rte.ie/news/2009/0808/stringerr.html

http://www.google.com/hostednews/ukpress/article/ALeqM5h8grmvaZDlHjMTifiw2jc1QFF7Gg

Je, Semenya ni Mwanamke au Mwanaume?


Wadau, kuna huyo binti kutoka Afrika Kusini, Caster Semenya (18). Ni mwanariadha na ameshinda katika kukimbia mita 800 katika World Athletic Championships (wanawake). Tena aliwaacha wenzake nyuma kabisa!
Sijui, nikimtazama naona kama anashepu ya kiume, lakini uso mzuri wa kike. Halafu ana sauti besi kama dume! Lakini wanariadha wengi wa kike wana shepu za kidume, matiti na hips hakuna. Kama ni mwanamke nampongeza nadhani tutasikia mengi kutoka kwake. Hivi sasa wataalam wanampima na tutajua matokea baada ya wiki tatu.
Ila najua Afrika kuna watu wanazaliwa na nyeti zote mbili, na wanalelewa kama mtoto wa kike au kiume kwa chaguo la wazazi.
Mnaonaje?
Kwa habari zaidi someni:

Kaza Mkanda!


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Bwana William Lukuvi na kamanda wa polisi, Bwana Sule Kova, wakimshauri dereva wa teksi wa Temeke, Saidi. Walimshauri kuhusu lishe bora. Walimwambia apungunze kula vyakula vyenye starches kama ugali na aongeze kule vyakula vya maboga. Kamanda Kova alimwambia kuwa polisi watakuwa makini naye kusudi asizidishe uzito hivyo gari lake itenda kwa shida.

Michelle Obama Avaa Kaptura na Kuzua Zozo!


Jamani, hizi siku za karibuni kumekuwa na joto kweli hapa Marekani. Sehemu zingine joto ni kupita 100Degrees Farenheit! Rais na familia yake wako likizo. Kesho nadhani watafika hapa Massachusetts. Watakuwa Martha's Vineyard. Mke wa Rais amezua zozo, eti hatakiwi kuvaa kaptura. Mimi nasema kwa nini asivae? Si wako likizo, siyo kwenye ziara rasmi. Hapa watu wanatembea karibu uchi, na kuvaa vinyuzi wakisema eti nguo! Hebu wamwache mama wa watu afaidi likizo yake! Au wanamwonea wivu miguu yake mizuri?
Mnaweza kusoma habari zaidi:

Tuesday, August 18, 2009

Libeneke la Kulizwa Airport Dar

Mdau amenitumia maoni yake:

Kuhusu libeneke la kulizwa airport na ufisadi unaoendelea Tanzania kwa ujuma; Mtazamo wangu nini kifanyike!

Kwanza nawashukuru kwa pongezi mlionipa katika ile makala ya libeneke la tathmini ya bei za nyumba nilipost kwa kaka Michuzi, nimepata moyo kuwa nimeandika kitu ambacho kitawasaidia wengine. Asanteni sana kwa maoni mazuri. Sasa nikija kwenye kadhia ya airport na ufisadi tanzania. Nakubaliana na baadhi ya maoni yoliyosema na wadau mbali mbali kuhusu huyo mtasha aliekutwa na mkasa airport. Binafsi, nadhani huyo mzungu alitia chumvi katika hizo allegations zake, kwa mfano polisi kumuomba dola 500, polisi wetu kwanza wanaogopa sana wazungu na wageni wengine matokeo yake wanaishia kutuumiza wenyeji! sijui ni tatizo la lugha ama vipi ila huo ni ukweli, istoshe wanapoa kwa kitu kidogo hata ukiwatoa kwa buku tano tu wanafurahi! Nawapa pole waliobiwa, ila nina shaka na baadhi ya hizo complaints, wanaosema wameibiwa laptop kwa posta ni sawa inakubalika ila airport, jamani laptop ilikuwa inafanya nini kwenye checked luggage, tusidanganyane hapa! Natoa tahadhari, hii makala kidogo iko inclined kwenye kuonesha the negative side of our society, ni kutokana na nature ya mada yenyewe sikusudii kukashifu au kuashiria hakuna jema huko kwetu naomba mniwe radhi kama nitaudhi ieleweke sio lengo langu, makala nimekusudia iwe constructive analysis ya jamii yetu na sio kuonesha udhaifu wetu. Siku hizi watu wamekuwa sensitive sana ndio maana najihami na ninachokiandika sio kwa woga bali sitaki kuudhi kundi lolote.

Mimi naamini chimbuko la matatizo haya na mengine ya aina hii ni hali mbaya ya uchumi huko nyumbani, ajira chache, mishahara midogo sana na dukani wafanyabiashara wanapanga bei wanavyopenda wenyewe. Hali ya kiuchumi na kipato kidogo kinachangia moja kwa moja kwenye migogoro mingi ya kijamii kuanzia kuibiwa simu mtaa wakongo, kuchomolewa wallet kwenye daladala hadi wizi kama ule wa NMB, ila hili la wizi kama huu wa airport, vifurushi vya posta, na kadhalika linaendekezwa na usimamizi mbovu katika hizo idara husika. Haya mambo yaashiria serikali yetu inabeza majukumu yake sana, sio kama inashindwa kutatua matatizo makubwa tu bali hata kero ndogo ndogo. Huo wizi wa mizigo kama wahusika wangekuwa makini kidogo tu usingekuwepo, ila ndio hivo kubwa ni changa la macho wanaweka CCTV halafu hata ikitokea wizi hakuna kumbukumbu yeyote inayoweza kupatikana! Halafu mwisho wa siku mkurugenzi ana kuja kujikosha tuandikie utueleze uliwasili siku gani na ndege gani, sasa nauliza, nikishatuma hiyo barua na ukanijibu mikanda ya hizo CCTVs ambazo nyingi huwa ni dummies haioneshi tukio la uhalifu itakuwaje? Si ndio mwanzo wa kusutana tu mimi nasema nimeibiwa na wewe kumbukumbu zako hazioneshi! Jambo la muhimu hapo kama mkuu wa idara unaskia malalamiko kama haya unaweka mikakati kuhakikisha hayo malalamiko na kasoro zinashughulikiwa, usikae sana ofisini unakula kiyoyozi jaribu kupita pita bila kutoa taarifa ujionee mwenyewe watendaji wako wanafanya nini (Hiyo itakusaidia hata kupunguza hicho kitambi). Any way, hii mada si juu ya unene, muhumu ujitahidi kufanya kazi yako vizuri, naamini juhudui zako hazitakuwa in vain, waswahili wanasema wema hauozi. Hapa nazungumzia kinadharia wala sikusudii kukashifu mtu yeyote, ila mara nyengine utakuta baadhi ya hao wasomba mizigo bosi anawaonea aibu kuwajibisha kwa vile ni watoto wa dada yake aliwasaidia kupata hicho kibarua au mbaya zaidi ni ndugu zake mkewe.

Ukiachana na udhaifu wa hizo mamlaka husika, jengine nadhani inatokana na jinsi tunavolitizama hili swala la maisha bora kwa kila mtanzania, yani lazima tuelewe jamani jamii yeyote haitafikia kuwa utopian, na Tanzania ndio tuko mbali zaidi, sasa basi watu inabidi tukubali katika jamii kutakuwa na watu wenye uwezo na wasio kuwa, iliobaki tuzungumze na roho zetu ukishapata ya lazima basi tupunguzeni tamaa. Hii tamaa ndio inatufikisha pabaya, ndio maana viongozi, wafanyabiashara na wengi wetu bado tu wanaendelea na ufasadi kila kukicha yani hawatosheki, sijui ni kutokana na ushandani au nini. Wengi tunaangalia alie juu yetu ana nini na mimi nile dili wapi nikipate, badala kuangalia wa chini ukashkuru, hii ndo hatima yake inapelekea mauwaji ya maalibino. Cha ajabu kuna baadhi yetu hata hawakubahatika kupata watoto, lakini bado unakuta mtu huyo huyo ana majumba zaidi ya moja na bado tu anaendelea kukomba ulaji, sijui anategemea kumuachia nani manake wengi wetu tunajustify our struggle kwa ajili ya watoto wetu. Yani tumekuwa consumed na ulafi enough is not enough! Wenzetu mtu wanapigania apate uongozi ili waache legacy, sisi zaidi tuko materialistic kwenye kila kitu, kuanzia mahusiano, ndoa na kadhaika, achievements za mtu tunaziangalia kwa nyumba na gari analoendesha. Mitazamo kama hii ndio inayobreed mafisadi na wahalifu kwenye jamii zetu, sasa kama kipimo cha mafanikio kwenye jamii ni utajiri matokeo yake ni nini, na njia za halali za kupata utajiri huko nyumbani ni finyu na chace. Yani mtu kamaliza chuo mwaka huu kabahatika ajira anakwera na nyumba ya kupanga, anataka awe amejenga baada ya miaka miwili wakati mshahara wenyewe haueleweki, hube niambie atafanyaje kama hajahujumu.

Kwa kuongezea juu ya kubadilisha tabia na mitizamo, inabidi tupunguze tabia tegemezi kutoka kwa ndugu zetu hasa hawa wenye nyadhifa serikalini, pia akina mama nyumbani wawe na huruma kwa baba sio kila kukicha anadai vitu vipya baada ya kumuona navyo mke wa jirani. Jengine tupunguzeni wivu, kule kwetu zanzibar tuna msemo bahari hailindwi(unfortunately ndio wa mwanzo kuwazuia wake zetu wasitoke nje wakati hatuwezi kuwatimizia mahitaji yao) akina mama ambao hawana watoto wadogo tusiwaache nyumbani wakawa "goal keepers", nao watoke wakatafute rizki mradi iwe ya halali tukiwaacha nyumbani hawa tunapunguza labour force kwa kiwango kikubwa sana katika jamii na kuzidisha uzito wa mzigo. Nahimiza kubadili tabia kwani lazima tukumbuke sio wafanyakazi wote maofisini na katika sector nyengine nyeti wanaingia kwenye corruption kwa kupenda, yani wengine wanakuwa ni victims of circumstances, kama mlibahatika kusoma kitabu cha mwandishi wa kinaijeria Chinua Achebe kinaitwa "No Longer at Ease" mtaelewa zaidi naongelea nini hapa.(nilipokuwa secondary ilikuwa lazima usome hiyo novel). Muhusika mkuu Bwana Obi, alisoma ulaya na aliporudi kwao initially he was determined to fight corruption, but to his dismay mwisho wa mambo akatumbukia humo humo nae akawa fisadi kutokana na ugumu wa mazingira alikuwa nayo na high expactions za jamii yake, tena ikumbukwe hiyo ni settings ya 1960s sembuse leo.

Hebu fikiria wewe ni afisa wa kawaida tu, nyumbani kuna mahitaji ya kawaida ya lazima, mama ana ng'ang'ania hili na nile unaogopa usipompatia haraka atakukimbia, watoto wanaenda shule wanahitaji kulipiwa ada, umefanya kosa la kuwapeleka shule mjini na wewe unakaa tegeta kama vile huko hakuna secondary, sasa inabidi uwape nauli ya kutosha wasinyanyaswe na makonda kwenye mabasi, pia pocket money ya kula chips mayai wakati wa mapumziko, unahofia usipofanya hivo binti yako wa miaka 16 ataharibika, mtoto mdogo yupo nyumbani mgonjwa anahitaji hela ya matibabu, kuna ndugu na jamaa zako na ndugu zake mkeo wametoka kijijini wapo nyumbani wote wanakutegemea, huwezi kulisha wote unaamua waondoke, huruma inakujia huwezi kuwatimua mikono mitupu, unasubiri kimshahara kije uwape nauli warudi mkoa, ulitaka kujirahisishia usafiri (au sijui kushindana na class mate ulisoma nae mlimani), ukajiroga na kununua kicorolla cha mwaka 91 ambacho baada ya kusota sana kama taxi ndio uliuziwa wewe kwa milioni tatu baada ya kumshinda huyo mmiliki wa mwanzo, hicho nacho hakikuonei huruma, kila jumamosi lazima ukipeleke garage na huko kuna kigongo chake mara inatakiwa hili mara lile! kuna mchango wa harusi ya rafiki yako mara sijui mwengine kapata maafa na majambazi na wewe alikusaidia sana, kumetembezwa bakuli kwenye mtandao unahisi unawajibika kuchangia, mshahara wenyewe mkia wa mbuzi! Sasa hebu niambie bosi wako corrupt anafanya mambo yake kupitia idara yako, kweli hutakula nae ukizingatia hali yako ya kimaisha? besides huwezi hata kumripoti ukizingatia yeye ana udugu na waziri wenu ukileta longo longo unapigwa transfer kigoma, bye bye dari salama, the only logical thing ni kula nae sahani moja tu. Na kwenye hili wadau wala tusianze kujiona tofauti, ndio maana wengi wetu hasa wanasiasa, wanapiga kelele sana wakati wakiomba kura na kuahidi watasimamia hayo maswala, na inawezekana kipindi hicho walikuwa na nia hiyo safi ya kufanya mema, ila siku akiingia na kujionea mambo yanavyokwenda mwenyewe wananywea, manake ni aidha ushirikiane nao kufisidi au ukubali kupigwa vita. Kule kwetu Zanzibar, wafanya kazi serikalini wamebuni kirefu chao cha CCM, yani wanasema Chukua Chako Mapema na hiyo ndio hali halisi hata bara.(huu ni mfano tu, naomba nisieleweke vibaya sipigii kampeni chama chochote sina uhusiano wala uwanachama na chama cha siasa, na wala sikusudii kuponda au kukashifu CCM kama chama nazungumiza jamii, Infact sijawahi hata kupiga kura na nina miaka 27 ila hiyo ni mada nyengine). Hapa sio kama najaribu kujustify hiyo tabia ila lazima tuelewe hili tatizo linachangiwa na jamii yetu wenyewe.

Niliwahi kuandika paper ya economics of crime kwenye darasa langu la ECON243 nilichukuwa kama elective, humo nilijaribu kuonesha uhusiano wa kiuchumi na tabia ya uhalifu, nilitumia refferences kutoka makala mbali mbali na moja wapo ni maarufu kutoka kwa mchumi mmarekani alieshinda tunzo ya nobel, Gary Becker juu ya Crime and punishment. Hadithi inasema aliandika hiyo paper baada ya siku mmoja kuwa katika haraka, akapima faida na hasara ya kuegesha gari lake katika sehemu inayoruhusiwa ila ingebidi atembee masafa hivo angechelewa zaidi, au aegeshe karibu pasiporuhusiwa ili awahi! Baada ya kupima na kuona uwezekano wa kukamatwa kuwa mdogo na pia hata angekamatwa angetozwa fine ndogo basi akaamua kuvunja sheria na kuegesha sehemu isiyoruhusiwa. Cha kuzingatia hapo ni kwamba, kinadharia, mhalifu sio mtu wa aina ya peke yake sana kwenye jamii, yani hakuna anaezaliwa mhalifu. Katika kutenda uhalifu mara nyingi kanuni za uchumi zinafanya kazi katika kupelekea uamuzi wa kutenda kosa au ku refrain. Mtu wa kawaida mwenye kazi nzuri inayomuwezesha kupata mahitaji yake ya lazima ni vigumu kwenda kuvunja nyumba na kuiba baada ya kutathmini "Opportunity cost" ukizingatia kuiba kunaweza kupelekea kukamatwa na kufungwa au hata kuchomwa moto na raia wema, ila sasa kwa kijana asie na kazi au mwenye kazi ya kipato cha chini sana ni rahisi kwake kutenda kosa kama hilo manake what else is there for him? Ndio maana huko nyumbani karibu nyumba zote kasoro ikulu madirishani zimewekewa vyuma na huku ughaibuni hawaweki vyuma ukizingatia ni wachache sana wanaweza ku opt kuvunja na kuiba. Hapa naamini Bw. John Mashaka anaweza kutuandikia akatuelewesha zaidi huo uhusiano na nini kina hitajika kufanyika huko kwetu, tafadhali bwana mashaka! (Again, sina affiliation yeyote na Mashaka au mtu mwengine anaetoa makala humu, personally I dont know him na wala yeye hanijui, hapa najihami na wapinzani wa Mashaka kama akina US Blogger).

Kwa kutumia kanuni hizo hizo za uchumi tunaona ni jinsi gani hawa vibaka, wizi wa airport na kadhika tunavowalea wenyewe, wengi wao wakichukua hivi vitu wanategemea kwenda kuuza mtaani au kwa pawnshop, sasa hapa kuna tatizo jengine sisi wa mtaani tunaonunua hivi vitu ndio tunapromote hii tabia kuendelea, manake kusingekuwa na hiyo demand ya hizo bidhaa za wizi au magendo wizi na uhalifu ungepungua. Hapa nimekumbuka, huko nyumbani sasa kumekuwa na fesheni ya kuwa na laptops simu sio dili tena, rafiki yangu aliibiwa laptop april mwaka huu, kwenye bus akitokea Morogoro na ilikuwa na kazi zake muhimu sana! Hizi ndio zinaibiwa sana zinaenda kuuzwa laki 4 na watu tunanunua, jamani kuna ulazima gani wa kuwa na laptop kama hatumiliki milioni mmoja ya laptop kwanini mtu usinunue desktop na unapata nzuri tu kwa huyo laki 4, istoshe hakuna ulazima wakuwa na computer kama humiliki tujifunze kujikuna tunapojipata, kuna njia mbadala kama kwenda internet cafe tena huko nyumbani zimejaa kama uyoga! besides wanaojua mambo computer wala hawabodhi na laptop, mi binafsi hapa nilishaachana na laptop na siwezi kabisa kutrade desktop yangu kwa laptop uchwara!

Kwa uolewo wangu mdogo, nadhani ili kupambana na uhalifu na ufisadi kwa ujumla inabidi tuwe makini na kuwashughulikia wakorofi wote ipasavyo, tuwajengee hofu au hata nidhamu ya woga ili kabla mtu hajafanya hiyo hujuma afikirie mara mbili madhara yatakayomkuta akishikwa, pia tuongeze msako wa watu hao wakiona uwezekano wa kushikwa mkubwa watasita. Naamini sheria za adhabu tanzania ni kali za kutosha ila tatizo hazitumiki! Haitoshi kwa mfano akishikwa huyo mwizi wa airport baada ya kurudisha alichoiba kusamehewa, na wale wa EPA waliopewa sharti warudishe hela au watakamatwa, au kiongozi kufanya urichmond na kumwambia ajiuzulu kwisha habari, kwa utamaduni huo bado wataendelea na ufasaidi. Nahisi kuna haja sehemu nyeti kuweka maasifa wa kipelelezi, au kutoka PCB, ofcoz baada ya kufanya housekeeping huko manake nako kumeoza kinyama, hii itaongeza hofu na woga wa kukamatwa hivo makosa yatapungua. Hapo airport si waweke angalau wawili au ndio na wawao watakula pamoja! noma kweli. Jengine muhimu zaidi, serikali na sekta binafsi tujitahidi kuongeza ajirai, vijana wengi tunamaliza kusoma, na wengine wana vipaji vingi sana vya ufundi ila wanakosa vibarua, hapa sina hakika sana kama kubuni mashindano ya urembo ya msindi wa mwanzo anajinyakulia laki 5 kunastahili much praise, mwisho wa mambo wengine wanazirai jukwani na kwa ukatili au sijui kuogopa kukosa taji wenzake wanampita kama mzoga, hatari! Serikali yetu pia ijikite kuimarisha kilimo ili kupunguza ongezeko la vijana mijini. Wito kwa viongozi wetu wazee nadhani muda wa kung'atuka umewadiwa hata kama ni brain kiasi gani you have played your cards baki pembeni bado ungali na heshima toa nafasi kwa damu mpya ivuruge! naamini bado mtaweza kutoa mchango wa taifa na kusikilizwa sio lazima muwe serikalini au ndio tumekuwa nzi hadi tufie kwenye kidonda? Nashauri jamii tuzingatie uzazi wa mpango ili tupunguze ukali wa maisha, tukubali mambo yanakuwa magumu zaidi ukiwa na watoto 6 wa rika moja badala ya 3. Jengine, mwisho wa mwezi, siku tukipata mishahara jamani tusijisahau, huto tuhela ni tudogo mno na nyumbani ndio mwezi mzima walikuwa wanasubiria baba yao upokee, kwa hiyo tusikimbilie kwenye kiti moto na bia, au nyumba ndogoz. Nadhan kama utajitahidi kumtunza vizuri mamaa na mtanzaa kwa mpango, basi haja ya nyumba ndogoz naamini haitakuwepo. Hapa najaribu kujenga hoja tuwe makini na matumizi ili hicho kidogo tunachopata kitutosheleze na hivo tuweze kushinda vishawishi vya kufanya ufisadi na uhalifu kwa ujumla. Nimekumbuka ile hutuba ya baba wa taifa katika mchakato wa kumpata raisi wa awamu ya 3, alitoa hadithi ya yule mgiriki aliyejitapa serikali yake iko mfukoni, mwalimu akasema enzi zake ukithibitika umekula rushwa viboko 12 siku unaenda ndani na 12 siku ukitoka ukamuoneshe mkeo!, sijui hiyo sheria ilishafutwa, nahisi yafaa irudishwe hiyo na hao wa airport na wengine aina hiyo au hata wale wakubwa wanaojitapa shs. bilioni moja vijisenti kamateni japo mmoja mtembeze fimbo japo nusu ya hizo 12 angalau muoneshe mfano.

Hapa najaribu ku tackle morals zetu in general, hii ni hadithi ya kweli kabisa imenitokea mimi binafsi, mwaka 2003 mimi na rafiki yangu wa kike tuliokota simu ya mkononi maeneo ya posta karibu na british council, enzi hizo simu za coloured screen ilikuwa ndio zinaingia, bado ilikuwa on sikuizima niliitia mfukoni na baadae ilipigwa nikaipokea nikamuelekeza mwenyewe nilipo akaja kuifata, alikuwa ni mama mmoja balozi wa tanzania kama sijasahau alisema india. Alitueleza sijui alitoka foreign akaidondosha! akatuombea dua ya mafanikio na alishangaa sana Tanzania bado kuna vijana kama sisi, akaomba contacts zetu mimi nikasita kumpa nikamwabia haina haja, ila ng'ang'ania nikampa namba ya mwezangu akatuahidi atatutafuta atushukuru zaidi ukweli sikumskia tena ila yawezekana alitutafuta hakutupata. Honestly, sikukusudia kuichukua hiyo simu ila awali nilikuwa naomba mwenyewe asitokee, tulipokuwa wadogo tulikuwa na msemo cha kuokota si cha kuiba. Rafiki yangu ni kutoka bara yeye alisema hii ni simu ghali sana aliomba tu mwenyewe atokee, huwezi jua ningekuwa peke yake yangu pengine nisingeirudisha kutokana na madhila nilifanyiwa. Nilisomea A level dar katika kipindi cha miaka 2, niliibiwa simu mbili shuleni na ya tatu nilitupa kwenye daladala mpya kabisa nimechaji mara mmoja, nikaja kupiga siku mbili baadae ikapokewa na dada mmoja, akanieleza aliokota hiyo simu card tu na sio simu, nikamsihi tukutane anipatie hiyo chip angalau nipate contacts zangu akakubali, maskini kijana nilikuwa so naive, nikajitoa kwenda posta mpya kumsubiri nikaishia kuachwa solemba! Ila kuna siku mimi binafsi pia nilishangazwa, nilikuwa naelekea Zanzibar mwaka 2002, tulipelekwa bandarini kwa taxi na dereva nisie mfahamu, nilikaa nae mbele tukawa tunaongea kawaida tu na nilikuwa nimeshikilia discman (ilikuwa ya sony nilinunua mwaka 2000 kwa pound 100 na tanzania enzi hizo bado ilikuwa ni kitu tunu hasa kwa vijana) tulishuka kwenye taxi na nikaidondosha bila kujua, huwezi kuaamini tulikaribia kuingia kwenye geti la kuelekea kupanda boat yule dereva alitukimbilia huku anashout, bila kujua ataka nini nilishangaa, kumuona ameshika ile discman sikuamini kabisa kama dar ningeona dereva wa taxi wa aina ile, sasa kwa kuogopa kuibiwa sikurudi nayo tena badala yake nikamuomba dada yangu aniazime walkman yake zile za kuweka tape Mungu wangu shahidi nayo nilienda kuiponza ikaibiwa. Hizi hadithi zote ni za ukweli sijatia chumvi inawezekana na mimi mwenyewe nilizidi uzembe ndio wakaniibia. (Natoa tahadhari hapa nisije nikaeleweka vibaya nawaaccuse wabara wezi kwa vile niliibiwa, hata zanzibar kuna wizi vile vile ila nashkuru kule sijawahi kuibiwa simu, ila niliibiwa mountain bike mwaka 1999 na nyumbani kwetu tushalizwa mara kadhaa). In fact hata huku ughaibuni wizi upo, kama mchangiaji mmoja aliesema Heathrow nako kunasifika inawezekana ni kweli ila sina ushahidi nishapita hapo mara 3 na sikuibiwa! binafsi huku shuleni kwetu niliibiwa flash drive ya 2 Gb mwaka 2007, yani niliisahau computer lab kama nusu saa tu, kurudi wapi, nilipita lost n found mwezi mzima manake kulikuwa na kazi zangu za shule humo sikuipata hadi leo hii.

Samahanini sana kwa kuwachosha na makala ndefu, sina skills za uandishi najaribu tu kutoa mchango wangu, hii ni makala ya kwanza kutuma hapa swahili time. Ukiangalia kwa makini unaweza kuona sehemu nyingi nimeandika kama naaddress wanaume tu, hapana ni mfumo dume tu katika makala yangu, ila sijakusudia kubagua wala kudhalilisha wanawake au kuashiria wanaume tu ndio mafisadi! Naombeni msome na mtoe maoni yenu, tafadhali nieleweke kwa nilichoandika sitatufi uongozi, bara wala Zanzibar kwanza nasoma science na haina uhusiano na uongozi in fact I'm too timid hadi nashindwa kuweka jina langu hapa! Labda kwa kumalizia nitoe ushauri wa bure, tukiona post kama hizi kwenye blog au kwengineko tujaribu kusoma na ku dig zuri lolote ambalo muandishi kaandika na tusiwe tunaangalia wapi kumekosewa grammar ya kiswahili au kiengereza bila hivo hatutofika. Kwa mfano kumuandama mdau kama US Blogger na Phd yake ya Oxford, alikosea aliandika "hungry"badala ya "hunger" nadhani is being shallow, sijui huko Oxford ila huku Canada, shuleni kwetu kuna professors wageni kutoka poland, india na asia, english inawapiga chenga balaa, matumizi ya tense wabovu kabisa na mwalimu ana lack vocabularies inafika hadi anauliza class kitu gani kinaitwaje, yet akifundisha unamskiliza kwa makini uelewe anachofundisha na wala wanafunzi hawacheki! Hiyo ni kasumba mbovu, kweli duniani leo english ni lugha muhimu sana, personally I admire hao akina Mashaka na wenzake kwa elimu zao na umahiri wa kujieleza ila sijioni nikifanya bidii yeyote ya kuwa kama wao, naomba hii isiwe chanzo cha kudharau mtu. Kwanza sisi watanzania tuna advantage tunaweza angalau kuomba maji kwa kizungu na wengine wanaongea lugha za makabila yao in addition to kiswahili. Huku Canada, wanatumia english na french kuna jimbo la Quebec wanaongea french zaidi, hawa wengine wengi tu hawawezi hata kuomba maji kwa kifaransa sembuse lugha nyengine kama kispanish. Natoa wito kwa akina Mashaka, US Blogger na wengine jamani bora tutumie kiswahili kwenye haya makala, besides nyote mkofluent kwenye kimombo manake akina mimi angalau naweza kusema wacha niandike in english ili ni practice ila nyinyi mko super na naamin audience yenu kubwa wanapendelea na wataelewa vizuri kwa kiswahili, kutumia english mwisho wake ndio huo mshindwa kueleweka watu wanaishia kukosoa grammar badala ya kuzingatia mlichoandika, mnajua tena siku zote kazi ya critic nyepesi, ngoja ni nyamaze na mimi nisije kuoneka critic!

Nawasilisha

Morogoro Mjini

Bofya picha kusudi uone vizuri Morogoro Mjini.

Monday, August 17, 2009

Zombe na Wenzake Waachiwa Huru!

SIWEZI KUSEMA ZAIDI YA DUUUHH!!!!

Kwa habari zaidi mtemblee Kaka Michuzi!

Saturday, August 15, 2009

Revival Meeting , Dallas Texas


Saluya 44 Blog

Blogu mpya ya Saluya 44:

http://www.saluya44.blogspot.com/

DHARURA Dallas, Texas - Prisca Mushi

UPDATE - Prisca Mushi Amefariki


Familia ya Bw. George na Bi. Judith Muro wa Dallas TX USA, wanayo huzuni kutangaza kuondokewa kwa mama yao mpenzi, Prisca Mushi, kilichotokea jana August 16, 2009 nyumbani kwao Dallas Texas.
Utaratibu mzima wa mazishi na safari ya kuelekea Tanzania utatolewa baadaye, ila kwa wote watakaoweza, mnakaribishwa nyumbani kwa wafiwakatika anuani hii:1652 Crown Point Dr
Frisco TX 75034
Kwa maelezo zaidi tafadhali
piga simu kwenye namba hii
940 465 5195.
*************************************************************************
Tangazo la dharura Dallas

Ndugu Watanzania,

Kwa niaba ya Jumuiya ya Watanzania waishio Dallas na familia ya ndugu George na Judith Muro ya Frisco, Texas tunapenda kuchukua fursa hii kuwataarifu kuwa mama yetu Prisca Mushi ambaye amelazwa katika hospitali ya UTSouthwestern@Zale, atasafirishwa kurudi nyumbani Tanzania haraka iwezekanavyo. Uamuzi huu umeafikiwa kati ya madaktari, mgonjwa na familia ya ndugu Muro. Taarifa hii ni ya muda mfupi, lakini tunategemea Watanzania wote mliopo popote pale, mtaelewa kuwa hii ni dharura hivyo tunaomba msaada wenu wa hali na mali. Kutokana na hali ya mgonjwa, itabidi aambatane na nesi, ndugu wa karibu na machela (stretcher). Gharama ya kuwasafirisha watu wote watatu kutoka Dallas mpaka Kilimanjaro-Tanzania ni $8000. Hii imetokana na masharti ya waganga pamoja na shirika la ndege. Msaada wako utafanikisha safari hii ambayo tunatarajia iwe jumapili au jumatatu.
Tafadhali wakilisha mchango wako kwenye:

Benki: Wells Fargo
Jina la akaunti: George Muro
Namba ya akaunti: xxxxxxx8424
Anwani ya mwenye akaunti: 1652 Crownpoint Dr, Frisco TX 75034

Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na Ndugu Muro simu: 940-465-5195

Tunatanguliza shukrani na Mungu akubariki kwa msaada wako.

Simon Nkanda na Abdul Amiri
(Mwenyekiti na katibu wa muda)

Friday, August 14, 2009

Mchango wa Kumsaidia - Peter Owino

MCHANGO WA KUMSAIDIA MWENZETU

PETER OWINO


Reading uingereza tunapenda kutoa Taharifa kwamba, Daftarin la kumchangia Peter Owino Aliyevamiwa na majambazi mwanza juzi tarehe, 11/07/09 limefunguliwa Bongo Flavour Reading.

Yeye mwenyewe Bado anaendelea na matibabu katika hospitali ya Rufaa ya bugando (mwanza) na mipango ya kunsafirisha kwenda Hospitali ya taifa muhimbili inafanyika.

Yeyote anakaribiswa kutoa chochote kwa kwenda bongo falaour au kulipia kwa njia ya benki.

Kwa taharifa zaidi Piga simu

01189585878

07900040288

07760200372

07806792348

Kutoa ni moyo usambe ni utajiri

Thursday, August 13, 2009

Divorce Cakes - Keki za Kuachana

Wadau, mapenzi ni matamu lakini wakati mwingine yanakwisha. Waliokuwa wanapendana wanajikuta wanachukiana. Kama walikuwa wamefunga ndoa basi wanaachana (divorce). Sasa imeanza biashara ya kufanya party za kusherekea kuachana. Hebu mcheki hizi dizaini za keki!

******************************************







Memorial Service - Andrew Mang'enya

MEMORIAL SERVICE OF

ANDREW SYLVESTER KITENGE MANG'ENYA


Saturday August 15th 2009 at 4:00pm
Point of Grace Church, 500 Commons Drive Birmingham Al 35209.

The leadership of Association of Tanzanians in Birmingham Alabama (JUTABI), together with the families of Mang’enya and Lubala would like to announce a sudden death and invite you to the memorial service of their beloved

ANDREW SYLVESTER KITENGE MANG’ENYA.

Andrew passed away suddenly on Frida y August 7th 2009. Arrangements are being made to transport his body to Tanzania . As a community of Tanzanians living in Birmingham and the family we will kindly appreciate your support of any kind.

You may forward your financial support to the following account

Wachovia Bank
Account name JUTABI
Account number 2000045629839
Routing number 062000080
For wire transfer domestic ABA # (with in USA ) 111025013
For wire transfer International (swift Code) PNBPUSBB

You may also contact us:
Email: jutabi@jutabi.com
Web: www.jutabi.com
James Kopwe 615-738-0145
Jonas Mwakajumba 205- 566-5729
Tony Igata 205-913-4665
Leonard Lubala 205-966-5384
Fidelis Irengo 205-643-3400

Thank you so much for your cooperation.

Shkurani Kutoka New England Umoja

Ndugu wanajumuia.....
Kwa niaba yangu Binafsi,Na hasa kwa niaba ya wanakamati wenzangu Napenda kutowa shukurani zangu za dhati

Kwenu nyonte Mliochangia,Mlioshughulikia,Na hasa kuhudhuria Kwenu Na Kufanikisha Tena Shughuli yetu ya mwaka huu
Kwani Imefunja record kwa idadi ya watu
Bila ya upendo wa moyo wenu wa kujitolea,Shughuli hii isingefanikiwa na Haitafanikiwa...
Baada ya Uchofu wa Tangu Jumapili kuanza Kupunguwa,nimeona ni muhimu kama ada yetu Ahsanteni sana
Kwa yote Mazuri Yaliyotendeka
Tunatowa Shukurani kwa wale wote waliochoma nyama, na wale wote waliojitolea kupika Mahanjumati
Vilevile tunawashukuru wale wote Walioandaa Fashion Show,ilikuwa Babu Kubwa
Tunatowa Shukurani vilevile kwa Ndungu Zetu wa New Hamsher kwa Mara yao ya kwanza kwa kujitokeza kwa wingi

Bila ya kusahau kwa mara nyengine tena Boston wameibuka kuwa washidi,Hawakamatiki
Tutakuwa na kikao cha mwisho cha kufunga Kutathmini shuhuli yetu
kwa Ujumla kitachofanyika Jumapili 2:00PM
August16,2009 kwa Mwanakamati Mwezetu Ahmad Mkambavange 96 Warregan St Chicopee MA 01013
(Tunashukuru Familia Ya Ahmad kwa Kutukubalia kufanya Mkutano huo)Ambao utafatiliwa Na nyama choma

Baada ya kikao tutawatumieni Email kuwajuulisha yote tuliyoyazungumza
Katibu
N.E.Umoja faundation

Wednesday, August 12, 2009

Blogger Summit Bongo

Je wewe ni mwanablogu (Blogger) au mdau wa habari na mawasiliano kwa umma kwa kutumia mtandao? Kama jibu ni ndio, tafadhali unaombwa kujiorodhesha kwa ajili ya maandalizi ya Kongamano Maalumu la Kitaifa kwa ajili Wanablogu (Bloggers) na wadau wa habari na mawasiliano wa Tanzania (Tanzanians Bloggers Summit) linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu jijini Dar-es-salaam,Tanzania.

Dhumuni la kongamano hili ni Kuelimishana, Kufahamiana, Kuamsha Utambuzi Rasmi Kuhusu Tekinolojia ya Blogu na Mawasiliano ya Umma kwa Kutumia Mitandao, Kusaidia Utambuzi Rasmi juu ya mchango wa blogu nchini Tanzania kama chombo muhimu cha habari na mawasiliano, Kuelimishana jinsi gani blogu zinaweza kutumika katika kuleta maendeleo katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, kuburudisha, kukuza utamaduni nk.

Wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wataalikwa kutoa mada na mafunzo mbalimbali kuhusiana na tekinolojia ya kublogu, zana nyinginezo za mawasiliano mtandaoni kama vile mitandao jamii(social networking), online forums nk.Kutakuwa na vipindi vya maswali na majibu.

Ili kufanikisha maandalizi ya Kongamano hili la kihistoria, kujiorodhesha kwako ni muhimu sana. Muda wa kujiodhoresha ni kuanzia tarehe 12/8/2009 (Jumatano) mpaka 12/9/2009 (Jumamosi) tu.

Kinachohitajika ili kujiandikisha ni :

Jina Lako, Anuani yako ya barua pepe (E-mail), Mahali Ulipo au unapoishi (Nchi,mji nk),Namba ya Simu (sio lazima) na Anuani au URL(Universal Resource Locator) ya blogu yako (mfano www.kongamano.blogspot.com/wordpress.com/.com/typepad nk). Vyeti vya Ushiriki vitatolewa kulingana na habari utakazoziorodhesha hapa.

Unaweza kujiorodhesha kwa kutuma ombi lako kwa barua pepe kwenda; summit@bongocelebrity.com.

Zingatia tarehe za kujiandikisha.

Ni mwezi mmoja tu! Asante kwa ushirikiano.

UMOJA NI NGUVU!

Peter Owino na Familia Wavamiwa na Majambazi Nzega

Kutoka Michuzi Blog:

HABARI ZA HUZUNI ZINAWAKILISHA KUWA NDUGU YETU PETER ANG'IELA OWINO ALIYEKUWA ANASAFIRI BARABARA KUU YA KATI AMEVAMIWA NA MAJAMBAZI MAENEO YA NZEGA AKIWA NA MKE NA WATOTO WAWILI WA MIAKA MIWILI NA MWINGINE MIEZI TISA NA WOTE KUKATWA NA MAPANGA VIBAYA NA YEYE YUKO MAHTUTI HOSPITALI YA BUGANDO, MWANZA.

NDUGU OWINO ANAISHI UINGEREZA NA AMEWASILI JUZI AKIWA LIKIZO FUPI KUELEKEA NYUMBANI SHIRATI, RORYA.

MAJAMBAZI HAO WAMEWANYANG'ANYA KILA KITU WALICHOKUA NACHO HADI LISHE ZA WATOTO HAO WADOGO WALIOJERUHIWA PIA. POLISI NZEGA WAMETHIBITISHA KUTOKEA KWA TUKIO HILO LA HUZUNI, NA HABARI ZAIDI ZINAFUATA.

PETER OWINO NI MMOJA WA WATU WALIOTOA MAPOKEZI NA HIFADHI KWA WATANZANIA WENGI WALIOKWENDA KUSOMA UINGEREZA TOKA MIAKA YA 1990
TUMWOMBEE NAFUU YA HARAKA.

Tuesday, August 11, 2009

Semina Kubwa Dallas, Texas


Kwa mara nyingine kupitia mtandao huu tuupendao,ninapenda kuwakaribisha watu wote kutoka Afrika katika mkutano wa kihistoria ambao unaandaliwa na makanisa kutoka nchi mbali mbali za Afrika.Nchi hizi ni Uganda,Ghana,Kenya, Nigeria,Sudan na wenyeji Tanzania. Mkutano huu unawafanya APOSTLE VERNON na Mke wake PASTOR ANN, ambao ni wamiliki wa kituo cha Television cha Agape cha nyumbani Tanzania kuwa miongoni mwa wahubiri wachache kutoka Afrika kuandaliwa mkutano na nchi zaidi ya moja hapa Marekani.

Baadhi ya watumishi kutoka Afrika ambao huwa wanaandaliwa mikutano ya namna hii ni Robert Kayanja kutoka Uganda, Theresia Wairumi kutoka Kenya,Bishop Bismak kutoka Zimbabwe, Bishop Duncan William kutoka Ghana na wengine wachache ambao sijawataja.Kwa ujumla huu ni ukurasa mpya kabisa katika historia ya nchi yetu na kanisa kwa ujumla.Kuanzia wiki ijayo gazeti kubwa la hapa lijulikanalo kama DALLAS MORNING NEWS pamoja na redio station ya KLTY 94:9 FM,Zitaanza kurusha matangazo ya mkutano huu.Tunategemea pia Television ya DAY STAR itamrusha hewani huyu mtumishi wa Mungu pamoja na mke wake siku moja kabla ya mkutano.Ili kuhakikisha tunapeperusha bendera ya nchi yetu vema naomba tuweke uzalendo mbele.Ndugu zangu, naomba mnisaidie kufanya yafuatayo;

-Kwa watanzania ambao watasoma ujumbe huu na wanandugu,jamaa au rafiki katika jiji hili la Texas naomba muwajulishe juu ya mkutano kwa kuwaandikia email au kuwapigia simu kwani huenda wasisome tangazo hili.
-Kama wewe ni member katika FACEBOOK naomba uwakaribishe watu kupitia njia hiyo ya mawasiliano hata kama upo nje ya Marekani.
-Kama una watu maalumu ambao ungependa niwakaribishe na wako huku Marekani naomba unijulishe kwa kuniandikia email.
-Kama utapenda kuhudumu katika mkutano huu kwa njia moja au nyingine pia nijulishe.
-Kama utapenda kuchangia pesa ili kufanikisha maandalizi haya naomba uwasiliane nasi kupitia

JESCA KATARAIYA -972 506 7780 au 972 387 7104(kataraia@hotmail.com)
Kwa mawasiliano zaidi, nipigie au niandikie:

PASTOR ABSALOM NASUWA
UMOJA INT'L CHURCH
12727 DALLAS TEXAS,75230
CELL:214 554 7381, 972 780 2668
FAX:972 991 9460

Da Flora Aongelea Suala la Mahausegeli

Wadau, hii suala la mahausegeli kugeuza nyumba danguro lipo siku nyingi. Pia mahausgeli kupata mimba za baba mwenye nyumba au vijana wa kiume kwenye nyumba ni jambo la kawaida. Tufanye nini ili kutokomeza hiyo tabia chafu?

***********************************************************************
Na Flora Wingia
9th August 2009

Mpenzi msomaji, lipo jambo moja nimesimuliwa nikaona ni vema nawe nikumegee pengine huna habari kama hata hayo yanatendeka nyumbani kwako bila kujua.

Ndani ya familia zetu nyingi, hazikosi mtumishi wa nyumbani awe ni hausigeli au shambaboi. Katika nyumba hizi, zipo zenye watoto wadogo au zingine zina wazee ambao wanatunzwa na mahausigeli hao.

Pia zipo ambazo hazina wazee wala watoto bali ni mahausigeli pekee ambao hubakia nyumbani baada ya matajiri zao kwenda kazini. Hizi ndizo nitakazozungumzia leo, nikigusia kidogo zile zenye watoto wadogo.

Ipo familia moja jirani na kwa rafiki yangu pale Makonde, Mbezi Beach inafanyiwa shere na hausigeli wao lakini hawajui kwa kuwa wote ni wafanyakazi.

Rafiki huyu akanisimulia kwamba binti huyo ambaye anaishi na familia moja yenye watoto ambao wote wanasoma shule za bweni, amekuwa akialika rafiki zake wa kiume pale nyumbani bila woga.

Majirani zake wamekuwa wakimtizama kwa jicho moja na hata walipomtaarifu mama mwenye nyumba kuhusu tabia hiyo, yeye alipinga kwa maelezo kuwa huenda wanamuonea gere kwa kumpata hausigeli mzuri na mchapakazi. Kumbe anasahau msemo kuwa ‘kikulacho kiko nguoni mwako’

Msichana huyu toka moja ya mikoa ya Kusini mwa nchi, anachofanya ni kuamka alfajiri na kuhakikisha kuwa anawaandalia matajiri zake kila kitu wanachohitaji ili wanapoondoka tu majira ya saa 12 asubuhi aweze kurudi kulala kwa saa kadhaa.

Hiyo ndiyo imekuwa ratiba ya bibie huyo kila siku isipokuwa Jumamosi na Jumapili ambapo wenye nyumba wanakuwa nyumbani. Lakini katika siku zingine yeye ndiyo hujipangia ratiba ya kujirusha na yule ampendaye.

Jirani huyu anasema kuwa yupo baba mmoja wa makamo ambaye amekuwa akionekana karibu kila siku nyumbani kwa familia hiyo kuanzia majira ya saa moja asubuhi hadi baada ya mlo wa mchana.

Swali ni je, baba huyu anayedhihirisha kuwa ameoa na anao watoto, haoni aibu kuzoea nyumba hiyo yenye wenyewe? Isitoshe, umri wa binti anayemmendea ni mdogo ikilinganishwa na ule alionao. Na wenyewe wakiibuka ghafla atajitetea vipi? Au ndio amekolewa na ule msemo kuwa inzi kufia kidondani ni halali yake’?

Hicho ni moja ya vimbwanga vya mahausigeli. Tena wengine, huthubutu hata kuleta wanaume zao ndani ya nyumba kama huyo niliyemzungumzia na kudiriki kujirusha juu ya kitanda cha bosi wake.

Eti naye aone raha kama ile aipatayo bosi akiwa na mamsapu wake. Na ukiona hivyo, binti wa aina hiyo huenda analala chumba cha ovyo ovyo, hivyo kujiongezea thamani anaamua kujiliwaza katika mandhari wanayofurahia matajiri zake.

Mahausigeli wengine bila aibu, hujipitishapitisha mbele za mabosi wao wa kiume ili waweze kunasa kwenye ulimbo. Ushawishi huu ni ushetani usiokubalika lakini unazitesa sana baadhi ya familia zetu. Ukweli ndio huo.

Matokeo yake, wanawavuruga vichwa baadhi ya kinababa na hivyo kutamani bila kupenda. Ndio hao unaosikia kuwa mama kamfumania mumewe na hausigeli.

Au mama anamtilia shaka hausigeli kuwa ana mahusiano na mumewe hivyo anamtimua. Wapo kina mama waliowafukuza mahausigeli kibao, kisa macho hayatulii wanapokuwa nyumbani na hasa akiwepo baba mwenye nyumba. Maisha Ndivyo Yalivyo! Au siyo? Kwamba purkushani za aina hii hazikosekani.

Mahausigeli wengine wanapoibukia kwenye nyumba zenye mashambaboi au wengine huwaita mahausiboi, inakuwa kama wamefungishwa ndoa za mikeka. Mabosi wakiondoka kwenda kazini wao ndiyo huanzisha nyumba zao za muda. Wapo waliobebeshana mimba kwa mtindo huo.

Bila kusahau wale wanaotoroka usiku kwenda kujirusha na washikaji wao na kisha kurejea alfajiri bila matajiri wao kung’amua. Hii ni hatari kwani wanaweza kutoa mwanya kwa wezi na kuiba.

Naam. Mpenzi msomaji, hapa nilitaka kuonyesha kuwa pamoja na umuhimu wa watumishi hawa katika kuhudumia familia zetu, lakini wengi wana madhaifu yao kama binadamu. Yapo yanayovumilika lakini mengine hakika hayakubaliki.

Kwa mfano kwa zile familia zenye watoto, wapo baadhi ya mahausigeli wameharibu watoto. Kwa mfano atamleta mshikaji wake nyumbani halafu kwa raha zao wanapigana mabusu huku watoto wakishuhudia. Haya sio malezi mazuri kwani badala ya kuwajengea watoto nidhamu nzuri anawaharibu kwani wataiga matendo yake

Mpenzi msomaji, kwa kifupi nilitaka kuwatahadharisha wazazi wenzangu kuhusu hawa wafanyakazi wetu wa majumbani. Pamoja na umhimu wao, lakini wanahitaji uangalizi wa karibu ili mabosi wanapokuwa makazini, na nyumbani nako kuwe na heshima yake badala ya kugeuzwa nyumba za wageni au sehemu za kufanyia maasi ya kimya kimya.

Tusiwape uhuru wa moja kwa moja. Ikiwezekana katika nyakati fulani mmoja wao, awe baba au mama afanye ziara ya kushtukiza. Yapo mambo mengi yanayoweza kubainishwa na ikiwezekana kuzimwa mapema badala ya kuachwa na hatimaye yakatokea madhara.

Wanapogundua kuwa zipo ziara za kushtukiza, sidhani kama wale waliozoea kuleta washikaji mara tu mabosi wanapoondoka watathubutu kufanya hivyo tena. Pia taarifa za majirani zisipuuzwe kwani wao ndio walioko karibu na wanaona mengi yanayotendeka wakati wenye nyumba hawapo. Au siyo? Huo ni ushauri wa bure, waweza kukubalika au kukataliwa lakini ukweli unabakia pale pale kwamba, lisemwalo lipo na kama halipo linakuja.

Msomaji wangu, kama unayo maoni au mchango wowote nikandamizie kupitia

flora.wingia@guardian.co.tz

Sunday, August 09, 2009

Msiba Alabama - Andrew Kitenge Mang'enya

The Late Andrew Kitenge Mang'enya

The leadership of Association of Tanzanians in Birmingham, Alabama (JUTABI), together with the families of Mang’enya and Lubala would like to announce a sudden death of their beloved ANDREW KITENGE MANG’ENYA.

Andrew passed away suddenly on Friday August 7th 2009. Arrangements are being made to transport his body to Tanzania. As a community of Tanzanians living in Birmingham and the family we will kindly appreciate your support of any kind.

We will be having a fundraising event on Tuesday August 11, 2009 at 6:00pm

Homewood Public Library

1721 Oxmoor Rd. Homewood, AL 35209.

You may also forward your financial support to the following account

Wachovia Bank

Account name JUTABI
Account number 2000045629839
Routing number 062000080


For wire transfer domestic ABA# (with in USA) 111025013
For wire transfer International (swift Code) PNBPUSBB
There will be a memorial service on Saturday August 15th 2009 in Birmingham, Alabama.

more details will follow.

You may also contact us:

Email: jutabi@jutabi.com

Web: www.jutabi.comJ

Ames Kopwe 615-738-0145
Jonas Mwakajumba 205- 566-5729
Tony Igata 205-913-4665
Leonard Lubala 205-966-5384
Fidelis Irengo 205-643-3400

Thank you so much for your cooperation

Ajali ya Treni Morogoro - Central Line

Picha Kutoka Michuzi Blog

Wadau, inasemekana hii ajali ya treni ilisababishwa na 'sabotage' yaani kuna watu walienda na kuondoa misumari kwenye njia ya reli kwa maksudi! Treni ilipata ajali kati ya Mkata na Mazimbu. Nchi yetu inakwenda wapi?!

Ninaomba waliosababisha ajali hiyo wachukuliwa hatua kali za kisheria na hata wapew adhabu ya kifo! Wapepelezi wafanya kazi hao washenzi wakamatwe!

Ni mwaka 2009, kwa nini Central Line bado ina reli moja tu, badala ya mbili zinazopishana? Reli ni ile ile tuliyoachiwa na wakoloni! Ninakumbuka kusafiri sana na Central Line kwenda Tabora Girls na kuona familia enzi hizo.

********************************************************
70 Injured as Train Derails

Na Robert Ochieng

9th August 2009
One of the injured passenger get treatment at Morogoro Regional Hospital yestarday.
About 70 commuters were injured, scores of them critically, when their Kigoma/Mwanza-bound passenger train from Dar es Salaam derailed in Kilosa district in Morogoro region, Railway Police Commander Ruth Makelemo has said.

Makelemo said the accident occurred at around 3 a.m., when the locomotive’s engine including its six trailing coaches overturned between Mkata and Mazimbu villages.

She said the accident victims were taken to Morogoro Regional Hospital, where some were treated and discharged while others, who sustained serious injuries, were admitted for thorough treatment.

With investigations to establish the cause of the accident underway, she said, Tanzania Railways Limited (TRL) had provided another locomotive for the unhurt passengers of the ill-fated train to continue with their journey.

Railway officials opine sabotage after they discovered a spanner, which they suspect was used to unscrew two bolts from the rails, but said they were waiting for the outcome of their joint investigation with the police.

Morogoro Police Commander Tobias Andengenye said that a team of police investigators had been dispatched to the accident scene.

“Right now, it is too early to give any conclusive remarks since we do not have all the facts yet. However, as soon as we have a final report in place, we’ll let you know the cause of the incident and our next line of action,” RPC Andengenye said over the phone.

Morogoro Regional Commissioner Issa Machibya, who visited the accident scene, however, cited foul play after unknown people pulled out the rails.

As recently as last week, rail workers downed their tools demanding better pay and improved working conditions, but TRL manager Hundj-Lalshaudhary quickly dismissed links between the protests and the accident.

The workers resumed their duties after a deal was struck between them and the management, with the latter agreeing to look into the grievances of the former, which have constantly put the two sides at loggerheads since the organisation was privatised.

Nzega MP Lucas Selelii (CCM) last month described controversy-riddled TRL as bearing the hallmarks of the infamous Richmond corruption scandal.

Selelii, a member of the parliamentary select committee chaired by Dr Harrison Mwakyembe that investigated the Richmond power generation scandal, said in an interview with a local daily that reports of a contract for the leasing of locomotive engines and coaches from India were “scandalous.’’

He said the Government, through TRL, had been forced to pay much-inflated rental fees and capacity charges for the hired equipment - in a similar manner to how the state-run Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO) was financially crippled by the Richmond deal.

According to the MP, the second-hand locomotives and coaches were being leased from India at a staggering cost of $31m (approx. 41bn/-).

Going by the provisions of the lease agreement, this means TRL would eventually be forced to pay a whopping 4.555bn/- in capacity charges for 25 locomotive engines and 23 coaches.

In addition to these capacity charges, the financially-troubled railway firm has already had to folk out a total of 1.181bn/- for the shipment of the engines from India to the port of Dar es Salaam.

Last week when contributing to the debate on the 2009/10 budget proposals of the Ministry of Infrastructure Development in Parliament, the Nzega legislator was one of several MPs who launched strong arguments for the TRL contract to be terminated forthwith.

The contract itself sees the Indian investor company RITES Limited owning 51 per cent of shares in the company while the Tanzanian Government maintains a minority 49 per cent stake.

Selelii said that the privatisation of TRL amounted to “daylight robbery’’ and blasted the Government for entertaining such a poor deal.

He asserted that the investor firm leased worn-out engines and coaches to TRL, which is now paying through its nose for the dilapidated equipment imported from India.

The Government has said a special task force appointed to review the TRL privatisation contract with a view of amending some of the key provisions therein, has already completed its task.

Saturday, August 08, 2009

Kili Nyepesi Blog

Amani Masue, anatuletea Blogu mpya kutoka Moshi, Tanzania.

http://kilinyepesi.blogspot.com/

Ili Mambo Yanoge....."WAKUBWA TU!"

Wadau, najua kuna watu watachukia lakini niliamua kubandika kwa sababu naona vijana wetu wanapotoshwa na DVD na video za ngono XXX. Mnakumbuka hapo zamani za kale, hizo sinema za ngono zilikuwa marufuku Bongo? Hata magazeti yalikuwa yanchujwa. Sisi tulikuwa tunasoma vitabu kama'After 4:30' yaani ndo somo! Mambo ya mapenzi ya kweli hayako hivyo.

************************************

JINSI YAKUJIANDAA NA SEX



KUTOKA BUSATI LA MALAVEDAVE BLOG

Wapenzi na wanandoa wengi hivi leo wanapoingia kitandani tayari kwa kuianza safari ya kupeana haki zao za msingi hushindwa kufurahia tendo na hasa hali hii hujitokezwa kwa wanawake kwani mwanaume huwa na haraka iliyopitiliza!

Mwanaume atamkumbatia na kumbusu mwanamke kwa muda mfupi na kabla hata hamasa ya mapenzi ya mwanamke ahaijashika hatama, atamwingilia na ndani ya dakika sekunde ama dakika zisizozidi 3, mwanamme hufika mshindo.

Katika hali ya kusikitisha baada ya mwanaume kujitosheleza hujongea pembeni bila kujali mwenza wake hajafika mwisho wa safari hali inayosababisha mwanamke kupoteza hamu ya tendo endapo endapo tabia hiyo ya mwanaume itaendelea.

Kunahatua nne muhimu ambazo wapendanao wakizishika na kuzitekeleza ipasavyo basi watafanikiwa kujitosheleza kila wanapokutana na kwa hakika watakuwa miongoni mwa watu wachache wanaofurahia faragha kila wakutanapo!

Hatua ya kwanza ni kusameheana:
Wanandoa wengi hushindwa kupata raha ya mlo wa usiku kutokana na kushindwa kumaliza tofauti zao kabla ya giza halijaingia, mgogoro wowote baina ya wapendanao ni lazima umalizwe kabla ya kukutana kwa ajili ya mlo wa usiku. Hii husaidia kuondoa kinyongo miongoni mwao na kuwafanya mioyo yao igubikwe na upendo ambao humfanya ahamasike kunako majambo!

Hivyo basi endapo unataka kufurahia mambo fulani hakikisha unamaliza tofauti, ombaneni msamaha na samehaneni kwa dhati kwani kwa kufanya hivyo kutawasaidia muwapo faragha kufurahia kile mnachokifanya kwa kuwa mtakuwa mmemalzia tofauti zenu.

Hatua ya pili ni mchezo ya mahaba:
Mashamsham hunoga na kupamba moto kiasi cha kumfanya yoyote aliye kwenye uwanya wa raha kusahau kwa muda shida na matatizo yanayomuandama pale anapokutana an mtu anayeweza kumpagawisha kwa michezo ya mahaba kabla ya kuianza safari yenyewe!
Michezo hii husaidia kuamzsha hamasa na muhemko baina ya wapendanao, hivyo ili wapendanao waweze kufika mwisho wa safari pamoja na kila mmoja alidhike na udereva wa mwenzake uliowafikisha safari yao lazima watumiye muda wakutosha katika michozo yakimahaba!

Hata hivyo kila mmoja wenu anapaswa kuujua mwili wa mwenza wake. Mwili wa mwanaume ni rahisi kuuelewa kwani una sehemu moja kuu ambayo ni kama kiini cha muhemko na msisimko wa mapenzi. Sehemu hiyo ni uume. Hivyo endapo mwanamke yoyote atatumia muda wakutosha kuhangaika na sehemu hiyo basi mambo huwa safi kwa upande wa mwanaume.

Mwili wa mwanamke una shughuli pevu kubaini sehemu zenye ambazo huamsha hisia za mapenzi na ndiyo maana wanaume wengi hushindwa kuwafikisha mwisho wa safari wapenzi wao. Kiini cha hisia za mapenzi kwa mwanamke ziko kwenye kipegere G (namaanisha critoris wadu, haya ni mambo ya infenizimu tu). Kipegere G kipo nje ya uke ambapo wataalamu hudai kuwa kipo sentimita 4 kutioka ukeni.

Wanaume wengi wanaelewa hili lakini walio wengi wamegubikwa na imani potofu kuwa, kwa kuingiza kidole ukeni watafanikiwa kuinua hamasa ya za wenza wao kutaka kuanzisha safari jambo ambalo si kweli, kwani wanawake wengi hujisikia vibaya kuingizwa vidole ukeni kutokana na ukweli kwamba kucha zinabeba uchafu na bakteria wengi ambao huwasababishia kupata fangasi!

Hivyo basi, endapo wewe ni miongoni mwa wanaume waliokuwa wakiaminin dhana hii nataka nikujulishe kuwa, ukitaka kumpa msisimko uliotukuka mwenza wako usiangaike kuingiza kidole chote ukeni badala yake hakikisha unatumia kidole chako (hakikisha si kikavu) kucheza na sehemu ya nje ya uke ambapo utakutana na kipegere G na lips za ndani. Hata hivyo usisahamu kuhangaika na uke pia lakini hasa shughulika na sehemu za nje!

MUHIMU KUJUA: Mwanaume huahamasika kwa sekunde kadhaa lakini mwanamke humchukua takriban dakika 20 kuweza kuamsha hisia zake na kumfanya awe tayari kwa kuianza safari! Hivyo, mwanaume mwenye busara yaani asiye mbinafsi huakikisha anatumia muda wakutosha kumuuanda mwenza wake kabla ya kuanza safari! Hivyo mwanaume anapaswa kunza michezo ya mahaba kwa kuzingatia hatua tatu muhimu ambazo ni:-
Sehemu ya juu:

Wanume wengi kutokana ana haraka zao hukimbilia sehemu ya chini ya mwili wa mwanamke na kuacha s............... itaendelea

****************************************************

ASANTE KAKA MWAKILAGA, MAWAIDHA MAZURI SANA KWA WAPENZI!