Saturday, December 31, 2005

Heri ya Mwaka Mpya!

Wapenzi wasomaji, nawatakia heri ya mwaka mpya. Naomba mwaka 2006 iwe wa amani na upendo na majalio tele kwa wote.

HERI YA MWAKA MPYA!

Wednesday, December 21, 2005

OmbaOmba

OmbaOmba


Hapa Boston kuna ombaomba kibao! Tena wengi ni wazungu. Hao ombaomba wengi wao ni walevi na watumia madawa y kulevya na wenye ugonjwa wa akili. Miaka nenda, miaka rudi, ombaomba ni hao hao!

Unapita njiani, unasikia “Spare Change”! Utaona mtu kasimama na kikombe chake anakitikisa. Kuna wengine usipowapa kitu wanakutukana matusi ya nguoni. Halafu kuna wale wakali wanakufuata mpaka ndani ya ATM. Basi watu kwa uoga wanatoa walichonacho na kuwapa kwa kuhofiwa kupigwa au kuibiwa.

Haya, lakini ni lazima niongelee kitu ambacho nimeona, na labda wengine hapa USA mmeona. Kuna ubaguzi katika kile watu wanachotoa kwa ombaomba. Tuseme mtoaji ni mzungu, na ombaomba ni mweusi, basi kama atampa kitu anampa vichenji. Huyo huyo mzungu atatoa noti kwa ombaomba mzungu. Nimeshuhudia mara nyingi tu. Nimeona ombaomba wa kizungu wakipewa noti za $1, $5, $10 na hata $20! Lakini mweusi atapewa vichenji, kwa nini? Je, ni kwa vile mzungu anajisikia vibaya kuona mzungu mwenzake katika hali hiyo, hivyo ni jitihada ya kumwinua? Je, ni kwa vile anaona kuwa mweusi ni hali ya kawaida kuwa maskini? Sijui kama tutaelewa sababu.

Halafu utaona weusi wako tayari kutoa kwa yeyote. Atampa mzungu, atampa mweusi lakini mara nyingi nimeona weusi wakisaidia weusi wenzao kuliko mzungu. Kisa, anajua kuwa yule mzungu anaweza kuishi maisha mazuri akitaka maana Marekani maana bado kuna ubaguzi Marekani.

Lakini nisiseme kuwa wazungu wote ni wabaguzi, maana mwaka juzi kuna ombaomba Cambridge, anaitwa Ramsey, alikuwa amesimima pale Memorial Drive. Basi Mzungu jike tajiri kapita ndani ya gari yake ya fahari na kampa noti ya $100. Ndiyo kampa dola mia moja! Halafu mzungu kamwambia Merry Christmas, maana ilikuwa Christmas Eve. Lakini jambo kama hiyo kutokea ni bahati nasibu.

Utaona wazungu wana jaribu kusaidia wazungu wenzao kupata public housing na huduma zingine. Lakini mweusi anaweza kupitwa. Kuna magari ya kuwasaidia zinapita mitaani, lakini hebu cheki, hao ‘volunteers’ wataenda kwa wazungu kwanza halafu mweusi ataambulia kilichobaki.

Ajabu na si kitu cha kushangaza sana ni kuwa hao ombaomba wa kizungu wakienda kuoga, ku-shave, kuchana nywele na kuvaa vizuri, anaweza kupata kazi kabla ya wewe mweusi na digrii zako!

Na kama hamniamini ukipita barbarani tazama mwenyewe. Ngoja niishie kwa leo, na kwa maksudi sijaongelea habari ya welfare, na shelters maana hii blogu ingekuwa ndefu mno!

Monday, December 12, 2005

Asante Civil Rights Movement!

Bibi Rosa Parks amefariki dunia jana 10/24/05 akiwa na umri wa miaka 92. Kwa kweli aliishi mpaka uzeeni kabisa, lakini alifanya mengi na alibarikiwa kuona matunda ya matendo yake.

Siku ya Desemba mosi, 1955, Bi Parks akiwa kwenye basi akielekea kurudi nyumbani alikataa kusimama kumpisha baba wa kizungu. Alikuwa amechoka baada ya kazi ngumu. Kwa nini ampishe mzungu tena mwanaume? Kumbuka, enzi hizo weusi Marekani hawakuwa na haki sawa na wazungu. Weusi Marekani walikuwa watumwa, na baada ya kupata uhuru wao 1864 walikuwa bado wanaishi katika nchi ya kibaguzi!

Kabla ya Civil Rights movement kafanikiwa, weusi walisoma shule duni, na kuishi sehemu zilizotengwa na wazungu. Ulikuwa huwezi kukaa na wazungu hata kama ulikuwa na pesa. Kazi walizokuwa wanafanya zilikuwa za kuhudumia wazungu, yaani maklina, mesenja, kubeba mizigo, kuzoa takataka. Walikuwa hawawezi kupata kazi ya maana shauri ya ubaguzi, hata kama angekuwa amesoma kiasi gani! Kulikuwa na mabomba ya maji ya kunywa, mzungu alikuwa na bomba safi na mweusi labda alikuwa na kabomba na maji yanatoka ovyo ovyo na iko sehemu chafu! Au unaenda restaurant kula lakini unawekewa meza jikoni au karibu na choo! Au unaambiwa uchukue chakula mlango wa nyuma! Vyoo (restrooms) vilitengwa kwa ajili ya wazungu na weusi. Weusi waliokuwa hawezi kuingilia mlango wa mbele ya majumba, ilikuwa lazima wapitie mlango wa nyuma. Walikuwa hawawezi kukaa hoteli za wazungu. Na mara nyingi ilikuwa kama wewe mweusi unasafiri unalala ndani ya gari au nyumbani kwa mweusi mwenzio. Enzi hizo weusi walikuwa wanasaidiana sana shauri ya huo ubaguzi.

Fikiria unaenda Airport halafu unaambiwa kwa vile mweusi ukalie sehemu duni. Yaani sehemu enyewe ina viti vya mbao, baridi na mavumbi, halafu unaona sehemu ya ‘White Only’ wamewekewa masofa mazuri kabisa, halafu pamepambwa vizuri. Au unasafiri, halafu wazungu wanaenda kwenye vyoo vya kisasa vya ku-flush, weusi mnaambiwa muende kutumia choo cha shimo! Ndivyo hali ilivyokuwa. Shule za weusi zilikuwa duni pia. Walikosa vitabu vya kutosha halafu majengo mabovu! Yaani! Na ilikuwa ukisema kitu, basi unaweza kuuwawa!

Unaweza kusema hali ya weusi Marekani ilikuwa ni sawa na apartheid ya Afrika Kusini. Lakini ilikuwa ni tofauti maana katiba ya Marekani inasema kuwa watu wote ni sawa. Eti “All Men Are Created Equal” Walikuwa sawa kwenye karatasi tu! Fikiria, ukienda kwenye historic archives, unakuta weusi waliorodhewa kama mali, sawa na wanyama, na! Wazungu hawakutuona sisi weusi kama binadamu, na eti ukimpiga mweusi hasikii maumivu! Loh!

Kweli WaMarekani weusi wametoka mbali toka enzi za Utumwa na Civil Rights. Waliopigania Civil Rights ni wengi, tusisahau akina Dr. Martin Luther King, Jr., Malcolm X, Frederick Douglas, W.B. DuBois, Medgar Evers, yaani watu wengi tu! Na watu walikufa wengi pia majina yao hatuyajui, na wamesahaulika.

Lakini ni lazima tushukuru, hao waliotangulia na kufanya weusi leo wawe na haki Marekani. Kutokana na juhudi zao na damu iliyomwagwa, si weusi tu, bali watu kutoka nchi mbalimbali na rangi mbalimbali wanaweza kuishi vizuri Marekani na kula matunda ya Civil Rights movement. Marekani sasa kweli wanaweza kusema, “All Men Are Created Equal”.

Saturday, December 03, 2005

Wapenzi wa Matako Makubwa

Wapenzi wasomaji, leo nimeamua kuzungumzia suala ya matako makubwa. Tafadhali msione kama ni matusi lakini hapa USA ni issue kubwa, maana watu wanayachukia! Nimeona nizungumzie suala ya matako makubwa kwa vile jana kazini, mzungu aliyekondeana mno kasema ni mnene na akila keki eti yote itaenda matakoni. Nilishangaa na kusikitika sana.

Uzuri kwa wazungu ni kuwa na matako fleti kama vile yamepigwa pasi. Sijui kwa nini. Mtu anashepu ya mbao, mwanamke hana hips kakaa kama dume vile eti ndo uzuri. Kumbe ni kwa sababu hao models na wacheza sinema wako hivyo! Basi wasichana ana akina mama wanajinyima chakula kusudi wakonde na eti wapendeze. Ndo maana magonjwa kama Bulimia na Anorexia zimeshamiri hapa. Lakini ukitazama sinema za miaka ya nyuma kama za 1930's na 1940's, wanawake walikuwa na shepu na walikuwa wamejaa na hata wanaume wa kizungu walikuwa wanasifia. Mpaka 1950's kulikuwa na mcheza sinema Marilyn Monroe, alikuwa na zinga la figure 8, na wanaume wote walikuwa wanampapatikia. Ama kweli mambo yanabadilika. Hivi sasa wanasema eti walikuwa ni obese yaani wanene!

Mbona mimi naona matako fleti kama chapati ni mabaya na hayapendezi? Au ni kwa sababu nimekulia Africa? Brothas (waMarekani Weusi) wanapenda mwanamke awe na matako ya maana! Akipita mwanamke mwenye mbarikio utasikia brothas wakisifia, "umm, umm umm!" Kuna siku nilisikia wanaume wa kizungu wakijadili sababu ya wanaume weusi kupenda matako makubwa, walisema ni "cultural thing". Kwa kweli ni culture yaani utamaduni! Kama umekulia katika mazingara ya kupenda kitu utakipenda. Na ndo maana kuna weusi USA wanataka kuwa na shepu iliyokondeana kama mzungu kumbe haiko katika 'genes' zake. Wajitahidi kupunguza mzigo lakini wapi, iko pale pale.

Sisi wanawake wenye asili ya Afrika tumebarikiwa huko nyuma. Yaani boxi, siha, wowowo, booty, na nasikia waGhana wanaita yokohama, matako makubwa yana majina mengi. Waafrika tunaona kama ni urembo, lakini wazungu na waliokulia uzunguni wanaona kinyaa. Wanasema eti ni dalili ya ulafi na uvivu! Lakini kama ni dalili ya ulafi mbona hata mwanamke mwembamba mwafrika anaweza kuwa na kamzigo huko nyuma? Ubaya mwenye matako makubwa anaweza kubaguliwa kwa vile bosi anaweza kuona kuwa ni 'ugly' na mwenye nacho anachafua mazingira ya ofisi. Kweli kabisa!

Hayo matako makubwa ni 'genes' za sisi waafrika. Lakini ajabu kuna siku nilisikia wazungu wakisema eti waafrika tuna matako makubwa kwa sababu ya utumwa. Eti mabibi zetu walinyimwa chakula hivyo matako ndo ilikuwa godown ya mafuta ya akiba. Nadhani ni uzushi kama ile ya ngamia kuweka maji kwenye nundu zake!

Mimi mara nyingi nimeambiwa nina matako makubwa, niyapunguze kwa kwenda gym kufanya mazoezi. Hayo mazoezi haisadii kitu ni makubwa vile vile! Lakini msione kama naona haya, wala! Mtu akiniambia nina matako makubwa namwambia mbona kama ni madogo, na ningependa yawe makubwa zaidi! Wanabakia kushangaa hasa nikiwaambia kuwa Afrika, matako makubwa ni uzuri.

Na amini usiamini kuna opresheni ya kuyapunguza inaitwa Liposuction. Wanawake wengi weusi na wazungu wamefanya hiyo liposuction ya matako, akiwemo mwimbaji Janet Jackson. Ubaya, ni kuwa ukishafanya hiyo liposuction, mafuta yataenda kwingine mwilini, hivyo utakuwa na shepu ya ajabu!

Sisi waafrika tunapenda kuringia huo mbarikio wa matako makubwa. Nilipokuwa nacheza ngoma shuleni na jeshini, tulikuwa tunatia nguo ndani ya bukta kusudi tuonekana na matako makubwa kweli kweli! Lakini, mara nyingi mitaani hapa USA, nimesikia akina dada wakifokewa, "You got a big a-s!" Kuna siku nilikuwa kwenye kituo cha Subway hapa Boston, kapita mama fualni Mganda, aisei alikuwa amejaliwa kweli huko nyuma, mpaka nikaona wivu. Basi ungeona wazungu walivyokuwa wanamtazama kwa mshangao ungecheka. Ila nilishuhudia baba fulani Mmarekani Mweusi akimtazama kwa furaha na kawa kama vile anamezea mate.

Nampenda sana mecheza sinema, Whoopi Goldberg. Nilikuwa nasoma jinsi akienda kwenye audition au akiwa kwenye movie shoot, wazungu wanamwambia kuwa ana matako makubwa au avae nguo ya kuzificha. Yeye alichoka, na mwishowe kusema, " Mimi ni mwanamke mweusi, nina matako makubwa niache kama nilivyo!" Wanawake wote tungedai heshima kama Whoopi nashani wazungu wangeheshimu matako yetu makubwa.

Tatizo linigine la kuwa na matako makubwa USA ni kupata nguo. Ukienda kununua sketi au gauni uanweza kukuta mbele refu nyuma umepanda. Au unavaa hiyo nguo lakini kwenye hips na matako haipiti! Hii ni kwa sababu nguo imeshonwa kwa ajili ya wazungu wenye matako fleti. Na kupata Jeans inayofiti ni vigumu. Mtu ambaye atatengeneza nguo 'molded for the black woman' atapata wateja kweli kweli, maana tunalilia nguo kama hizo.

Pamoja na yote haya sasa wazungu wameibuka na staili ya kuwa ka ka-butt. Yaani jeans inakuwa na pedi ndani kusudi mtu aonekana ana matako. Loh! Watu hawaridhiki! Sijui tuseme asante J-Lo (mwimbaji Jennfier Lopez) au nini. Kwanza walikuwa wanamcheka J-Lo na matako yake makubwa lakini naona watu wanaanza kuyapenda. Mpaka kuna opresheni sasa ya kuongeza matako. Wacha wafanye haitapendeza kama matako natural tulytozaliwa nayo waafrika.

Matako Makubwa Oyee!