Saturday, September 24, 2016

Wakuu wa Shule za Sekondari Waagizwa Kuwa na Kiwango cha Ufaulu

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na Wakuu wa Shule za sekondari Wilayani humo

Hifadhi ya Ngorongoro katika Kashfa Mpya!

Hifadhi ya Ngorongoro katika Kashfa Mpya



SEP 22, 2016
by MWANDISHI WETU Raia Mwema

MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeingia katika kashfa kubwa ya kugawa eneo la msitu wa asili wa Olmoti lenye ukubwa wa ekari tano ndani ya hifadhi hiyo kwa kampuni ya Asilia ili kujenga jambi (campsite) kinyume cha sheria za mazingira na uhifadhi.
Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya NCAA na kuthibitishwa na vyanzo vya uhakika zimeeleza kuwa eneo la msitu huo lilimegwa kinyemela na maafisa wa shirika hilo na kulitoa kwa kampuni ya Asilia ambayo inamiliki mtandao wa hoteli kadhaa (lodges) katika hifadhi mbalimbali bila kufuata taratibu zinazotakiwa.
Msitu huo wa asili ambao huheshimiwa na wenyeji wa jamii ya wafugaji wa kimasai upo katika kijiji cha Olchniomelole kata ya Alailelai.
Ugawaji wa sehemu ya msitu huo ni mwendelezo wa menejimenti ya NCAA kugawa kiholela maeneo  ndani ya hifadhi kwa ajili ya ujenzi wa hoteli (lodges) na campsite hatua ambayo inahusishwa na ufisadi uliokithiri miongoni mwa watendaji wa NCAA.
Takwimu zinaonyesha kuwa hadi sasa ndani ya hifadhi hiyo kuna campsite 31 na hoteli tano kubwa zilizojengwa katika kingo za kreta ya Ngorongoro hatua inayolalamikiwa na wadau wa ndani na mashirika ya kimataifa kuwa ni hatari kwa ‘uhai’ wa kreta ya Ngorongoro.
Kutokana na ujenzi wa campsite hiyo ambao umelalamikiwa na wananchi wa kijiji wanaotishia kuichoma moto, Kamati ya Uhifadhi, Utalii, Maendeleo ya Jamii, Ekolojia na Mambo ya Kale ya Bodi ya NCAA inayoongozwa na Lucas  Seleli ilikutana na wananchi wa kijiji hicho Alhamis ya wiki iliyopita.
Mkutano wa hadhara
Akizungumza katika mkutano wa hadhara mbele ya kamati hiyo kusikiliza kero za wananchi hao kuhusu ujenzi wa campsite hiyo, Mwenyekiti wa kijiji hicho Kilembei ole Ngisilo alisema wananchi wanapinga ujenzi huo kwa kuwa hawakushirikishwa  wala kuarifiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Alisema wakati ujenzi huo unafanyika kampuni ya Asilia ilifyeka sehemu kubwa ya miti ya asili kwa malengo ya kusafisha eneo la ujenzi hivyo kuharibu mazingira na mandhari ya msitu huo.
“Pia magari makubwa ya kubeba malighafi za ujenzi yameharibu barabara tuliyojenga kwa nguvu zetu na magari hayo pia yamepita katika maeneo tofauti na kuharibu mazingira yote, wanyama hawapiti, watoto wetu na mifugo pia imeshindwa kupita eneo hilo kutokana na kuwa vumbi nyingi sana,” alidai na kuongeza; “Kama unavyowaona wananchi wana hasira sana walitaka kuichoma campsite hii lakini tumewasihi sana sisi kama viongozi kwa ajili ya kulinda heshima ya serikali yetu.”
Mwananchi mwingine Parmoyat ole Ngaikul ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Kitongoji katika kijiji hicho alisema uharibifu wa mazingira uliofanyika katika eneo hilo hauwezi kuvumilika hata kidogo na kuwataka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kuondoa haraka kambi hiyo.
“Sisi tumeishi ndani ya hifadhi hii kwa zaidi ya miaka 60 sasa, tunauheshimu msitu wa Olomot kwa sababu ni chanzo cha maji katika eneo letu na tumezuia kuingiza mifugo ndani ya msitu tunawashangaa NCAA wamethubutu vipi kugawa eneo la msitu huo kwa mwekezaji?”alihoji ole Ngaikul.
Habari zaidi kutoka NCAA zinafafanua kuwa ujenzi huo ni kinyume cha sheria kutokana na msingi kuwa haukuwa katika mpango wa maendeleo wa hifadhi wa General Management Plan (GMP) ambao hutoa dira ya muda mrefu ya hifadhi.
Akihitimisha mkutano Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Lucas Seleli, alikiri mbele ya wananchi kuwa ujenzi wa kambi hiyo ulikiuka sheria zinazosimamia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kuongeza kuwa waliohusika wanaweza kuwajibishwa.



Seleli Akiri
Akizungumza na Raia Mwema kwa njia ya simu juzi, Lucas Selelii, alikiri kuwapo kwa mvutano huo. “Kamati ilifanya ziara ni kweli kuna malalamiko kuhusu ujenzi wa campsite hiyo kutoka kwa wananchi na tumewahoji watendaji wa NCAA pamoja na uongozi wa Asilia hivyo kamati inaandaa ripoti ambayo itawasilishwa katika kikao cha Bodi mwezi Oktoba mwaka huu,” alisema Selelii.
Selelii ambaye alikuwa Mbunge wa Nzega katika Bunge lililopita, aliongeza kuwa pamoja kuwasilisha taarifa hiyo kamati yake pia itatoa taarifa kwa Bodi kuhusu hali halisi ya uharibifu wa mazingira katika maeneo mbalimbali ndani ya hifadhi hiyo.
“Kwa ujumla ripoti yetu itazingatia jinsi hali ilivyo kwa sasa ndani ya hifadhi hii ambayo ni moja ya maeneo nyeti katika masuala uhifadhi nchini na kimataifa na imebeba taswira ya nchi yetu katika sekta ya utalii kimataifa,” alisema.
Mhifadhi afanya kikao
Habari zaidi kutoka ndani ya NCAA zinabainisha kuwa kutokana na sakata hilo, Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Ngorongoro,  Dk. Fredrick Manongi, alifanya kikao cha siri na baadhi ya viongozi kusafisha hali ya hewa.
Taarifa zinaonyesha kuwa kikao hicho kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Kijiji, Kilembei ole Ngisilo, Diwani wa Kata, Shutuk Kitamwasi; Mjumbe wa Bodi, Edward  Mwaura na Mzee wa kimila (Laigwanan) ambaye hata hivyo jina lake halikupatikana mara moja.
Wengine waliohudhura wametajwa kuwa ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji wilayani wanaoishi ndani ya hifadhi hiyo, Wakuu wa Idara za Utalii na Uhifadhi wa NCAA.
Aidha imedaiwa kuwa katika kikao hicho Dk. Manongi  alijaribu kuwashawishi kuwa waache kufuatilia ujenzi huo na kuahidi kuwa NCAA itatoa fedha kurekebisha kasoro na athari za mazingira zilizotokea wakati wa ujenzi.
“Pia aliwaahidi viongozi hao watakuwa na mamlaka ya kutembelea kambi wakati wowote na kijiji kitapewa mgawo katika mapato yatakayokuwa yanapatikana kutoka kwa wageni watakaolala katika campsite hiyo,” kiliongeza chanzo chetu kutoka ndani ya kikao hicho.
Habari zaidi zimeongeza kuwa hatua hiyo ya Dk. Manongi imelenga kuficha makosa yaliyofanywa na mmoja wa maafisa wake, Asantaeli Melita, Msimamizi wa Idara ya Utalii (Principal  Tourism Officer) ambaye ndiye anayetuhumiwa kujichukulia mamlaka ya kugawa eneo hilo.
“Ni wazi kuwa kwa hatua hii ya kuitisha kikao cha siri Dk. Manongi anajaribu kumteteta Afisa (Melita) aliyehusika na ugawaji wa eneo hilo na pia taarifa za ndani zinadai kuwa ugawaji huo ulifanyika kwa maelekezo ya mhifadhi huyo,” kinadai chanzo chetu cha habari.
Aidha Dk. Manongi pia anatuhumiwa kuunda mtandao wake ndani ya taasisi hiyo huku akiwalinda wakuu wa idara wanaojihusisha na vitendo vya ufisadi ikiwemo matumizi mabaya ya fedha bila kuwachukulia hatua akitegemea zaidi uhusiano wake binafsi na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe.
Akitoa mfano wa tuhuma za matumizi mabaya fedha mtoa habari wetu kutoka ndani ya NCAA alidai kuwa Dk. Manongi hadi sasa anamlinda mtumishi moja wa Idara Fedha (Jina linahifadhiwa) ambaye anatuhumiwa ‘kutumbua’ zaidi dola za Marekani 200,000 (sawa na mlioni 435) kati ya mwaka 2013/2015 bila kuchukuliwa hatua.
Juhudi za kumpata Dk. Manongi kwa ajili ya ufafanuzi kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwake hazikuweza kufanikiwa kutokana na simu yake kuita kwa muda mrefu bila majibu na huku Afisa Uhusiano wa NCAA, Vicent Mbirika, simu yake kutokuwa hewani kwa muda mrefu.
Hata hivyo Afisa anayetuhumiwa kuhusika kugawa eneo hilo Asantaeli Melita akizungumza na Raia Mwema alikanusha vikali akisema campsite hiyo ilikuwepo tangu mwaka 2004 katika eneo hilo.
“Kwanza itambulike kuwa mwenye mamlaka kuhusu ardhi ndani ya hifadhi ni NCAA na si wananchi, eneo hilo liligawiwa tangu mwaka 2004 na wala sikusuhika, hapa kuna kundi la wachochezi wanawapotosha wananchi tu,” alisema Melita na kuongeza; “Kwanza suala hilo limeisha jana (Jumamosi  iliyopita) baada ya kikao cha Mhifadhi na viongozi wa kijiji, Diwani, Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji, Wazee wa Kimila (Laigwanan) na tayari tofauti zilizojitokeza zimemalizika.”
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni hifadhi ya kipekee dunia ambayo hufanya mseto wa maisha kati ya binadamu na wanyama hivyo kuvuta watalii kutoka kila pembe ya dunia na huchukuliwa kama moja ya maajabu ya dunia.
Hata hivyo hifadhi inaelekea kuelemewa na shughuli nyingi za kibinadamu kutokana na kuongezeka kwa ujenzi wa hoteli na campsite hali ambayo inayochangia kuwapo kwa upungufu mkubwa wa maji pamoja na malisho kwa mifugo na wanyama.
Pia inakadiriwa kuwa ndani ya hifadhi hiyo kuna watu zaidi ya 80,000 pamoja na mifugo zaidi ya 120,000 na hali ambayo inahatarisha shughuli za hifadhi kiasi cha shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO mwaka 2008 kutahadharisha kuwa hifadhi inapoteza umaarufu wake kutokana na  uharibifu wa mazingira.
Mwisho
Chanzo Gazeti la Raia Mwema

Saturday, September 17, 2016

Sala ya Kumuaga Marehemu Aisha Rupia Boston Leo

Sala ya kumuaga marehemu Aisha Rupia (39) itakuwa leo jumamosi 9/17/16 saa kumi jioni (4:00pm) huko Hurley Funeral Home, 134 Main St., Randolph, MA 02368.

Baada ya Sala, watu watajumika  kwenye Ukumbi wa VFW, saa kumi na mbili jioni (6:00PM). Anwani mi, Lt. John D. Crawford Veterans Asscociation, 10 Highland Avenue, Randolph, MA 02368.

Mwili wa marehemu Aisha utazikwa Louisiana wiki ijayo.

Madereva wa Malori Watekwa Nyara huko Congo!


   DAR ES SALAAM, Tanzania (AP) - Tanzania's government and a transport group say an armed group operating in eastern Congo has seized six Tanzanian and four Kenyan truck drivers and is seeking ransom.

   Tanzania's foreign ministry said in a statement Thursday that it is working with Congo's government to secure the release of the Tanzanians.

   Angelina Ngalula, who leads the Tanzania Truck Owners Association, says an armed group blocked 12 cargo trucks carrying cement between Tanzania and Congo on Wednesday, setting four trucks ablaze and seizing the drivers. Two of the 12 drivers escaped.

   Ngalula says four of the truckers are from Kenya.

   She says the armed group is demanding $4,000 per driver in ransom.

   Eastern Congo has a number of armed groups active in a vast and mineral-rich region.

  

Mwenge wa Uhuru Wawasili Mkoani Singida na Ishara ya Uhuru wa Tanganyika

MWENGE wa Uhuru baada ya kuwasili mkoani Singida Mwenge huu ni ni kitu mfano wa kikombe chenye mpini mrefu na utambi ambacho aghalabu huwasha na kukimbizwa katika kusheherekea au kutukuza tukio fulani
Askari wa Jeshi la Polisi wakiulinda Mwenge ishara ya kuwasili muda mfupi kabla ya kukabidhi kwa uongozi wa Mkoa wa Singida

Kushoto ni Katibu tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angelina M. Lutambi akimkabidhi Mwenge Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe Geofrey Mwambe tayari kwa ajili ya kumulika Miradi 18 katika Wilaya hiyo

Friday, September 16, 2016

Matokeo ya Tanzania Kukataa EPA


KAMA mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na zile za Umoja wa Ulaya (EU) utaendelea kubaki kama ulivyo sasa, ni wazi kwamba Tanzania itabaki na msimamo wake.

Nimezungumza na baadhi ya mawaziri wa serikali ya Rais John Magufuli na nadhani msimamo huo utabaki ulivyo hata baada ya kupita kwa miezi mitatu kama ambavyo wakuu hao walitangaza wiki iliyopita.

Lakini, hivi kuna nini kibaya kwenye mikataba hiyo ya kiuchumi ambayo inafahamika kwa kifupi cha EPA (Economic Partnership Agreement)?

Kuna mengi lakini nitasema machache tu. Mikataba hiyo inataka Tanzania iondoe ushuru wa bidhaa kutoka nje zisizokuwa za kilimo kwa asilimia 90 na pia ushuru wa asilimia 10 kwa bidhaa za kilimo kutoka kwao. Hapa wanataka bidhaa zao zije kushindana na zetu wakati wao wameendelea zaidi kimtaji na kiteknolojia.

Nchi wanachama wa EAC watabaki kuwa masoko ya bidhaa za Ulaya. Wakati huohuo, kwa utaratibu huo wa bidhaa za kilimo, maana yake ni kuwa nchi hizi za Afrika zitabaki kutoa malighafi tu kwa ajili ya viwanda vya Ulaya kuzalisha bidhaa.

Kwa utaratibu huu wa EPA, Tanzania ya viwanda haitawezekana asilani. Hakuna namna ambayo viwanda vya Afrika vinaweza kushindana na vile vya Ulaya. Kuna kipengele pia katika mkataba huo ambacho kinataka nchi za Ulaya zipewe upendeleo uleule ambao watapewa wabia wengine wa kibiashara wa Afrika kama vile India na China.

Yaani, kwa mfano, kama tukisema India tutawapunguzia ushuru wa bidhaa hii kwa kiwango hiki, basi na Ulaya nao wafaidi kwa kiwango hichohicho. Cha ajabu, mkataba huo hausemi kwamba na wao wazungu wakiingia makubaliano ya namna hiyo na rafiki zao, nasi wa EAC tufaidi vilevile. Hakuna !

Ukiniuliza kwanini Kenya, Rwanda na Uganda wanataka kusaini mikataba hiyo, jibu langu litakuwa sijui. Lakini, ninachojua ni kitu kimoja pekee –kwamba wazungu hawataacha hili lipite hivihivi.

Jijini Dar es Salaam, Rais Yoweri Museveni alizungumza wiki iliyopita mbele ya wageni akiomba watu wa EU wasiiadhibu Kenya kwa kuwa imekubali kusubiri hiyo miezi mitatu.

Museveni anawajua wazungu. Anajua visasi vyao. Inawezekana mara moja au mbili kwenye utawala wake amewahi kukumbana na visanga vyao.

Kwenye kitabu chake Trade is War, Profesa Yash Tandon, ameandika kwamba inawezekana Uganda na Rwanda zimebanwa na wazungu kwamba wakikataa kusaini, wanaweza kukosa misaada mbalimbali mingine ambayo haihusiani na EPA kama vile silaha na vita dhidi ya ugaidi.

Tandon, mmoja wa wasomi mashuhuri barani Afrika, ameandika pia kwamba biashara ya maua; inayofanywa na matajiri wengi wa Kenya wakiwamo wanasiasa, itaathirika endapo viongozi wa EPA wasiposaini. Kwa kuishughulikia biashara hiyo, watu wa EU wanafahamu watakuwa wanafanya jambo ambalo linawaumiza wakubwa moja kwa moja.

Nchi za Ulaya, na mabeberu katika ujumla wao, hawapendi nchi masikini kujiamulia mambo yao. Wanafahamu kwamba Tanzania ikiwa na uchumi wa viwanda, itajikwamua kutoka kwenye makucha yao. Wanafahamu kwamba wao waliendeleza viwanda vyao kwa kuvilinda. Sisi wanataka tusivilinde.

Fidel Castro si kiongozi mbaya. Lakini mabeberu hawakupenda siasa zake za kutotaka kulamba miguu ya wakubwa. Matokeo yake ni kuwa nchi yake leo inachechemea. Hali iko hivyo kwa Venezuela ya Hugo Chavez na hata Chile ya Salvador Allende.

Patrice Lumumba alionyesha dalili mapema kwamba atakuwa mwiba kwa mabeberu, akapotezwa. Hapa kwetu, mtu kama hayati Abdulrahman Babu aliishia kuwekwa rumande na kupewa kazi za kutangatanga tu bila utulivu. Mabeberu wasingekubali apewe nafasi ambayo angeonyesha njia ya kweli ya maendeleo.

Hatua hii ya Magufuli na serikali yake si hatua ya mchezo. Endapo mwishowe atakataa kabisa kusaini mikataba hiyo, afahamu kwamba atatangazwa kuwa adui namba moja wa mabeberu.

Habari zake zote zitakuwa mbaya. Ataandikwa kwa aliyoyafanya na asiyoyafanya. Atapewa majina ya kila namna na uchumi wetu utaanza kufanyiwa hujuma. Na kwa sababu mabeberu ndiyo wameshika uchumi wa dunia, safari ya huko tuendako inaweza isiwe rahisi.

Kama ameamua kwa dhati kufuata njia hii, ni muhimu ajiandae na yanayokuja. Ingekuwa vema pia kama angeweza kushirikisha jamii pana ya Watanzania katika kufahamu kiini na sababu za kuchukua hatua anazochukua. Hii ni sawa na kusema anatakiwa pia kuwaandaa watu wake.

Kama serikali ya Magufuli ina nia ya dhati ya kuhakikisha Tanzania inajenga viwanda vyake na haibaki kuwa soko la malighafi kwa ajili ya viwanda vya mabeberu, ni muhimu ikashikilia msimamo wake wa kukataa kusaini EPA kama ilivyo sasa.

Cha msingi, ni kufahamu kwamba mabeberu hawatakaa kimya wala bwete wakati Tanzania ikichukua uamuzi mkubwa na muhimu kama huo.

Raia Mwema

Usabato na Historia ya Aibu

HISTORIA HALISI YA WASABATO: AIBU TUPU

Imeandikwa na Padri Titus Amigu

Ndugu zanguni nitaendelea na mada yetu ya “viboko hamsa wa ishirini” lakini naomba nikatishe kidogo nipate kujibu swali moja linalojirudia rudia sana. Swali lenyewe naulizwa kwa namna nyingi mno. Mtu wa mwisho ameniuliza akisema hivi: “ Asante sana baba gombera mstaafu, hivi huyu Bi Ellen G. White ni nani katika Kanisa Katoliki? Mbona amekuwa akishambulia sana Kanisa Katoliki au kuna makanisa mengine huanzishwa na misingi yao ni lazima kushambulia Kanisa Katoliki?
Jibu fupi: Bi Ellen G. White ni mmojawapo wa waanzilishi wa kanisa la Wasabato lakini fundi sana wa kulitukana Kanisa Katoliki. Yeye hakuwamo ndani ya Kanisa Katoliki na wala hakujihusisha nalo kwa nia njema isipokuwa aliondokea kuongoza kulitukana.

Wala si siri yapo makanisa ambayo huanzishwa na misingi yao ni lazima kulishambulia Kanisa Katoliki kwa sababu zao mbalimbali. Kanisa mojawapo kati ya hayo ndilo kanisa aliloshiriki Bi. Ellen White kulianzisha yaani kanisa la Sabato. Inasikitisha sana na kukera sana, lakini tutafanyaje. Ndiyo hivyo tena, kisera, kanisa la Sabato limepania kulibomoa Kanisa Katoliki. Sisi hatuwezi kuwachukulia hatua ya kiuhalifu isipokuwa kufahamishana kama ninavyokusudia kufanya ili tukae chonjo nalo tu. Kumbe kwa busara ya maisha, anayekuwinda walau mjue tu kusudi ujue namna ya kumkwepa. Wala si lazima upigane naye.

Sasa kusudi vijana mmwelewe vizuri mtu huyo aheri nikupeni historia nzima ya kuanzishwa kwa kanisa la Wasabato. Katika historia hiyo mtaona aibu ya kushindwa utabiri wa mwisho wa dunia. Cha kushangaza waliposhindwa kutabiri mwisho wa dunia kama walivyojinasibu kuweza, wakageukia kulitukana Kanisa Katoliki ambalo halina kosa lolote na halikuwafanya chochote.

Hivi acheni niitumie fursa ya kujibu swali hili kwa kuwaleteen historia halisi ya Kanisa la Wasabato. Nawaanikieni hadharani aibu yao, aibu inayowatia hasira na hasira yenyewe kuilekeza kwa Kanisa Katoliki ambalo halijawakosea.

Jibu hili nimewahi kuliandika kwenye Gazeti la Kiongozi na vile vile kulirusha hewani kwa njia ya radio. Lakini kwa kuwa bado naendelea kuulizwa, kwa mitindo mbalimbali, kila uchao napenda nilijibu tena sasa kwa kupitia ukurasa wangu wa Facebook. Sina nia ya kuleta uchochezi. Najibu swali kwa kadiri inavyostahili tu.

Jibu refu: Wakatoliki tunatukanwa kwa sababu Wasabato wanajaribu kufunika aibu yao ya kihistoria na wanadhani matusi ndiyo njia ya kuliua Kanisa Katoliki. Hawajui kwamba matusi hayawezi kumharibu mtu isipokuwa kumfedhesha mtukanaji tu. Waungwana hawatukani. Kumbe, aheri tuielewe historia ya dhehebu la Wasabato au S.D.A tupate kuwapuuza wanaotutukana huku wakijiabisha wenyewe. Basi, historia hiyo ya aibu inayofichwa ndiyo hii ifuatayo:
Ni hivi ndugu zanguni, kwa kuiweka bayana historia ya Wasabato, tuambatane katika kuwaelewa watu wanne ambao hutajwa kama watangulizi au waasisi wa dhehebu la Wasabato. Mwishoni nitayapembua waliyofundisha kibiblia na kisaikolojia.

Mtu wa kwanza ni William Miller, wa pili ni Hiram Edson, wa tatu ni Joseph Bates na wa nne na wa mwisho awe Bi Ellen G. White.
Tukianza na Bw. William Miller, yeye alizaliwa mwaka wa 1782 katika mji wa Pittsfield, Massachusetts, huko Marekani.  Ingawa alizaliwa katika familia ya Kikristo, aliuacha Ukristo alipokuwa kijana mbichi.  Kwa kweli hakuiamini Biblia kuwa neno la Mungu.  Basi, akajiunga na jeshi. Baada ya kutumika kama mwanajeshi kwa muda mfupi, akaishi kama mkulima.  Kumbe, mwaka wa 1816, akaongoka na kuurudia Ukristo wake kwa kasi mpya.  Kwa kweli, tangu mwaka huo wa kuongoka kwake, Bw. William Miller alisoma unabii kwa kina na hasa unabii uliohusu kurudi kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. 

Kumbe, kutokana na kujifunza huko, Bw. William Miller akashawishiwa kwamba mwisho wa dunia ungetimia mwaka 1843.  Kifupi, Bw. William Miller alishawishiwa kufundisha jinsi hiyo na unabii wa kitabu cha Danieli 9:24-27, unabii unaohusu majuma sabini yaliyowekwa kwa ajili ya watu wa Mungu, taifa la Israeli.

Zaidi ya hayo, katika Danieli 8:13-14, kuna unabii wa watakatifu wawili wanaoulizana lini patakatifu patatakaswa.  Mintarafu unabii huo, Bw. William Miller alitafsiri kwamba patakatifu patakapotakaswa, ni dunia hii iliyochafuliwa na dhambi za kila sampuli.  Kwa maoni yake, mwaka wa 1843 B.K., ndio mwaka ambao Yesu Kristo angerudi katika dunia iliyonajisiwa kupita kiasi na dhambi na hivyo kuitakasa kabisa kwa kuwapo kwake.
 
Msimamo huu ulimfanya awe maarufu sana katika sehemu nyingi za Marekani, na hatimaye akawa mhubiri mkubwa wa dhehebu la Kibaptisti.  Kwa kuwa mwisho wa dunia ulikuwa unaambatana na kurudi kwa Yesu Kristo, ambako kwa Kiingereza huitwa “Christ’s Advent”, wafuasi wake walianza kujulikana kama “Adventists” au kwa Kiswahili “Waadventisti”, yaani “Watu watarajiao kurudi kwa Kristo”. Ijapokuwa mwanzoni hakutaja tarehe bayana ya kurudi kwa Yesu, punde si punde alisema kurudi kwa Yesu kungekuwa kati ya tarehe 21 Machi, 1843 na 21 Machi, 1844. 

Baada ya mambo kufikia hapo, mfuasi mmoja wa Bw. William Miller aliyeitwa Samwel Snow, akawa jasiri zaidi na kutaja kwamba Kristo angerudi tarehe 22 Oktoba, 1844 saa 6.00 usiku; yaani ndipo parapanda litakapopulizwa, mbingu kukunjwa kama kurasa, na Yesu Kristo kufika  kwa utukufu mwingi.  Lakini mambo hayakutukia hivyo walivyohubiri. Basi, kwa vile Kristo hakurudi kama walivyotarajia, Bw. Miller akakiri kukosea kwake, lakini akawaonya wafuasi wake wasisahau kwamba Kristo atarudi upesi. 

Kwa bahati mbaya, Bw. William Miller alifariki mnamo mwaka 1849 ndoto yake ya kumwona Yesu akirudi upesi ikiwa bado haijatimia.  Hadi hapo, ieleweke kwamba Bw. William Miller, hakuwahi kuwa Msabato.  Hivyo kama Mbaptisti, alikuwa anasali siku ya Bwana, yaani Jumapili au Dominika. Kutokana na kutokutumia kwa utabiri wa Bw. William Miller wafuasi wake wengi wakarejea nyuma.
Basi, tumwachie Bw. William Miller hapo, nasi tusonge mbele tukamwangalie mtu wa pili, yanii Bw. Hiram Edson.  Kwa bahati, bwana huyu alikuwa kati ya Waadventisti wachache waliobaki baada ya kuvunjika moyo kwa wafuasi wengine wa William Miller kutokana na kutorudi kwa Kristo kama ilivyotazamiwa.  Kwa upande wake  kwa kusudi la kuwafariji wenzake kwenye huzuni yao, yeye alidai kwamba Mungu alikuwa ametoa jibu kwa aibu yao kwani alipata mafunuo juu ya kile kilichofanyika siku hiyo ya tarehe 22 Oktoba, 1844. 

Kwa jinsi gani? Sikiliza. Alifundisha kwamba alioneshwa kulikuwa na hekalu mbinguni mfano wa hekalu la duniani. Akadai hekalu hilo lilikuwa na sehemu mbili: patakatifu na patakatifu pa patakatifu, yaani sawa na lilivyokuwa hekalu la Kiyahudi zamani zile.  Kumbe, kilichofanyika siku hiyo ya tarehe 22 Oktoba,  ni kwamba Kristo alitoka patakatifu na kuingia patakatifu pa patakatifu.  Akasema kwisha Yesu kuingia patakatifu pa patakatifu atabaki humo mpaka siku atakapokuja duniani mara ya pili. 
Mintarafu swali, Yesu anafanya nini siku zote hizo? Akasema Yesu anafanya ‘hukumu ya upelelezi’ kwa Kiingereza “investigative judgement”.  Kwa maelezo hayo mapya akadai kwamba kitu alichokuwa amekosea Bw. William Miller kilikuwa tafsiri tu, kwa maana kwamba utakaso uliofanywa tangu siku ile ya tarehe 22 Oktoba haukuwa wa dunia hii, bali wa patakatifu pa patakatifu katika hekalu hilo la mbinguni.

Kwa namna hii, Bw. Hiram Edson akawa Mwadventista wa kwanza, hata kabla hajawa Msabato, kuleta duniani maelezo ya kuwafariji wenzake kwa kutorudi kwa Kristo siku ya tarehe 22 Oktoba 1844.  Hivi basi, mchango wake mkubwa kwa teolojia ya Wakristo ambao baadaye walijiita Wasabato ni suala  hilo la ‘hukumu ya upelelezi’.  Kifupi, kwa maelezo hayo, Wasabato wanafundisha kwamba Yesu Kristo, tangu 22, Oktoba 1844 yuko huko mbinguni, katika patakatifu pa patakatifu akichunguza kwa kina maisha ya Wakristo wote ambao majina yao yapo katika kitabu cha uzima wa milele na kuamua nani anastahili kufutiwa dhambi zake zilizosamehewa wakati alipoamini.  Hivyo, kila mtu anayeonekana kurudi nyuma, naye hakutubu dhambi zake zote, anafutwa jina lake kutoka katika kitabu cha uzima na hivyo huko, mwishoni mwa historia, atakosa nafasi katika ufufuo wa kwanza.  Kinyume chake, kwa upande wao, wote ambao walitubu dhambi zao, majina yao yanabaki kitabuni pasipo kufutwa, nao watafufuliwa katika ufufuo wa kwanza.
Ndugu zangu, hadi hapa umeshagundua mafundisho ya uongo. Mbinguni hakuna hekalu. Huo ndio ukweli wa kibiblia maana mwandishi wa kitabu cha Ufunuo anatuandikia habari za maono yake matakatifu mintarafu Yerusalemu ya mbinguni akisema “Nami sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Bwana  Mungu Mwenyezi na Mwanakondoo, ndio hekalu lake” (Ufu 21:22). Sasa iweje Bw. Hiram Edson amzungumzie Yesu anayetoka patakatifu kuingia patakatifu pa patakatifu? Zaidi ya hayo, mafundisho ya hukumu ya upelelezi ni uzushi kwa sababu ni matokeo dhahiri ya tafsiri potofu ya neno la Mungu. 

Haya tuachane naye, nasi twende tukamwangalie mtu wa tatu, ambaye ni Bw. Joseph Bates.  Kikazi, Bw. Joseph Bates alikuwa baharia.  Bada ya kustaafu kwake alihamia Fair Haven, katika jimboni Massachusetts, huko huko Marekani.  Kwa kweli, Bw. Joseph Bates ni mmoja wa viongozi maarufu  wa Waadventisti.  Yeye aliposoma maandishi ya Thomas Prebble kuhusu Sabato, alishawishiwa kuamini kwamba Sabato ya Wayahudi ilikuwa siku halali kwa watu wote wa Mungu kuabudu.  Basi, akaandika kijitabu chake kilichoitwa, “The Seventh Day Sabbath, a Perpetual Sign””. 
Baada ya kitabu hicho Bw. Joseph Bates aliendelea kuandika vijitabu kuhusu Sabato.  Hivi bwana huyu anakumbukwa sana na Wasabato kwa mchango mkubwa katika kuirudisha Sabato ya Agano la Kale. Kwa kweli, ni yeye aliyekuwa wa kwanza kutafsiri siku ya Jumapili kama siku ya alama ya mnyama; na kwamba siku ya Sabato ndiyo muhuri wa Mungu kwa watu wake walio waaminifu, yaani Waadventisti Wasabato 144,000 (rej. Ufu 7:4). 

Kutokana na ushawishi wake huu, kuabudu siku ya Jumamosi, kukaanza kupata nguvu nyingi, zilizoambatana na vitisho vya hukumu kali kwa wanadamu wote wasioishika Sabato  ya Agano la Kale. Kifupi, miongoni mwa Waadventisti waliomfuata Bw. Joseph Bates kwa karibu, walikuwa ni James na mkewe Ellen White.  Kumbe, Bi Ellen White ndiye aliyeuendeleza usabato, kwa motomoto zaidi kuliko watu wengine wote naye anaheshimiwa na Wasabato kama nabii wao.  Kwa hali hii ya mambo, yafaa tumalizie historia hii fupi kwa kumwangalia mwanamama huyo hata kama ikiwa kwa kifupi sana.

Ndugu zanguni, Bi Ellen G. White, anafahamika pia kwa jina la Bi Ellen Gould Harmon. Ni kwamba kabla hajaolewa alikuwa anaitwa Ellen Gould Harmon na baada ya kuolewa kwake na mpenziwe James White, aliyekuwa mhubiri wa kibaptisti aliyekuwa muadventisti hapo tarehe 30 Agosti, 1846 akajulikana kama Bi Ellen Gould White.

Kwa kufupisha mambo, Bi Ellen Gould Harmon alizaliwa mwaka 1827 huko Goharm, jimboni Maine, maili kumi hivi toka Portland.  Akiwa mtoto mdogo bado, wazazi wake walihamia Portland kwenyewe.  Hapo mwanzoni, yeye pamoja na familia yake walikuwa wafuasi wa dhehebu la Methodisti.  Kumbe, familia ya akina Ellen ilijiunga na uadventisti baada ya Bw. William Miller kuhubiri mjini Portland katika mwaka wa 1840 na 1842.  Lakini kwa kuwa familia hiyo ilisadiki maneno  ya Bw. William Miller, kanisa lao la Methodisti liliitenga familia hiyo. Familia nzima ilitengwa kwa sababu ya kuyapokea mafundisho ya Kiadventisti.  Kwa ujumla, mchango wa Bi Ellen White ulianza kama alivyodai mwenyewe kwamba alipokea maono mengi nyakati mbalimbali, maono ambayo baadaye yalimfanya ajulikane kama nabii wa Waadventisti.  Inasemekana maono yake ya kwanza yalimjia mwezi Desemba, 1844, yaani si muda mrefu sana baada ya watu kukatishwa tamaa na kutokurudi kwa Yesu Kristo. 

Bi Ellen White aliingia ulingoni akidai kuliona kundi la Waadventisti wakisafiri katika njia yenye mwanga wa utukufu, huku wakiongozwa ya Yesu hadi walipoufikia mji wa Mungu.  Bi Ellen akadai kwamba baada ya kuonywa katika maono ya pili asikae kimya juu ya yale aliyooneshwa, alilazimika kutangaza na kuyahubiri maono yake wazi mahali pengi.  Kuanzia hapo, Waadventisti wa Portland na Maine wakaanza kumtambua Bi Ellen White kama nabii wao na kusisitiza kwamba Roho Mtakatifu alikuwa juu yake na kwamba ilikuwa ni lazima unabii wake ufuatwe na Waadventisti wote popote pale walipokuwa. 

Kama jambo hilo halitoshi, mwezi Februari 1845, Bi Ellen White alidai kupata maono yaliyothibitisha maono ya Bw. Hiram Edson mintarafu kitu kilichotokea hapo tarehe 22 Oktoba 1844, yaani kwamba Yesu alikuwa ameingia patakatifu pa patakatifu katika hekalu la mbinguni.  Zaidi ya hapo alidai kwamba miaka miwili baadaye, alipata maono mengine ambapo alidai kwamba alichukuliwa na kupelekwa katika hekalu la mbinguni.  Alisema kwisha kufikishwa mbinguni, kwanza kabisa aliingizwa patakatifu na baadaye patakatifu pa patakatifu ambapo aliona amri kumi zikiwa ndani ya sanduku la agano.

Tukiwa tayari kusonga mbele, tunaweza kujiuliza swali dogo la kuchangamsha bongo zetu. Hebu tujiulize, hivi, humo patakatifu pa patakatifu Bi Ellen White alikumta Yesu akifanya hukumu ya kipelelezi? Tukikijibu  wenyewe,  ndugu yangu, jibu ni kwamba suala hilo haligusiwi ilivyotarajiwa. Basi, acha tuzidi kumfuatilia katika madai ya maono yake. Bi Ellen White anasema alipong’aza macho yake kwenye sanduku la agano la humo hekaluni, aliona amri ya sabato ikiwa imezungukwa na utukufu na hapo eti akang’amua kwamba amri ya kushika Sabato ilikuwa kubwa zaidi.
Ndugu yangu, hadi hapo, tukimpima Bi Ellen White kibiblia, anaongeza uongo mwingine mbaya. Uongo wa kwanza ni ule wa kuliona hekalu mbinguni wakati mbinguni, Maandiko Matakatifu yanasema hakuna hekalu (rejea tena Ufu 21:22). Uongo wa pili ni huu wa kuhesabu amri ya kushika Sabato kama amri kuu kwani amri ya kwanza na kubwa kupita zote, kadiri ya Yesu Kristo mwenyewe, ni ile ya kumpenda Mungu huku ikifuatiwa na ya pili yake, yaani ile ya kumpenda jirani kama tunavyojipenda sisi wenyewe (rej. Mt 22:34-40).
Lakini basi, ndugu zanguni, maono aliyopata Bi Ellen White yakawa, kwake na hatimaye kwa Wasabato wote, kurunzi la kutafsiria  Maandiko Matakatifu yote.  Ndipo, kwa njia ya vitabu vingi alivyoandika, mafundisho ya Kiadventisti yakasambazwa. Hivyo, tangu wakati huo, Waadventisti Wasabato, huitafrisi Biblia kwa vipimo vya maono ya White, na siyo kuyatafsiri maono ya Bi White kwa vipimo vya Biblia.  Je, si ajabu ya mwaka hiyo? Basi, ndugu yangu, fumbuka macho ya roho yako, uyaone na kuyapima mambo haya sawa sawa pasipo kiwi cha macho! Usitoe hoja ya uongo!
Basi, kwa kukata maneno, Bi Ellen White ndiye aliyewapandikiza chuki Wasabato dhidi ya Kanisa Katoliki. Amelifanya hilo kwa kupitia vitabu vyake vingi vyenye chuki ambavyo vinasomwa na kutumiwa na Wasabato karibu kama misahafu.  Kwa taarifa yako, baadhi ya vitabu hivyo ni, kama vile, Vita Kuu, Afya na Raha na Siri ya Ushindaji. Ndani ya vitabu hivi Kanisa Katoliki linatukanwa na kushtakiwa kuhusika na maovu mengi. Kwa mfano, wanashtakiwa kuondoa amri ya kuabudu Sabato. Wanashtakiwa kuabudu sanamu. Wanashtakiwa kumwabudu Bikira Maria. Wanashtakiwa kumwabudu Baba Mtakatifu (Papa) ambaye eti ndiye mnyama anayetajwa katika kitabu cha Ufu 13:1-18. Wanashtakiwa kufundisha mambo ya kidunia badala ya ufalme wa Mungu. Wanashtakiwa kuongeza vitabu kwenye Biblia na mengine mengi ya namna hiyo yanayosikika mitaani na katika mahubiri yao. Mungu utuhurumie!
Ndugu zanguni, kwa ujumla, kanisa la Wasabato likawa muungano wa vikundi vitatu vya Waadventisti: mosi, kikundi cha Bw. Hiram Edson, kilichosisitiza zaidi mafundisho ya huduma ya Yesu patakatifu pa patakatifu mbinguni; pili, kikundi cha Bw. Joseph Bates, kilichosisitiza zaidi kufuata Sabato ya Agano la Kale; na tatu kikundi cha Bi Ellen G. White, kilichomwona Bi Ellen kama nabii ambaye unabii wake ni lazima ufuatwe na Waadventisti wote duniani.
Vikundi hivi vilipoungana Waadventisti Wasabato wakapata kujichipusha duniani. Mwaka 1860, jina la Seventh Day Adventist lilichaguliwa nalo likawa jina rasmi la Waadventisti hao.  Kishapo, mwezi Mei, 1863, katika mkutano mkuu wa kwanza, uliokuwa na wawakilishi kutoka majimbo yote Marekani, isipokuwa jimbo la Vermont, kanisa la Wasabato likazaliwa rasmi duniani.
Basi, tukipiga muhtasari wa historia ya Wasabato, tuseme tu kwamba mwasisi wa Waadventisti Bw. William Miller alikuwa ni Mbaptisti lakini mwanzilishi wa Wasabato yaani Bi Ellen G. White alikuwa ni Mmethodisti. Hata hivyo, kwa kuhitimisha sehemu hii, yafaa sote tukumbuke kwamba makanisa hayo mawili, yaani Wabaptisti na Wamethodisti si chochote isipokuwa matawi ya kanisa la Anglikana, kanisa lililoanzishwa na Mfalme Henry VIII wa Uingereza hapo mwaka 1534 baada ya kukasirika kukataliwa na Kanisa Katoliki kumwacha mkewe aliyeshindwa kumzalia  mtoto wa kiume.

WASABATO MITUME WA MATUSI DHIDI YA KANISA LA KWELI

Msomaji wangu bila shaka umeiona historia ya aibu na ya zigzaga ya Wasabato. Wasabato wenyewe huificha sana historia hiyo, hasa kwa wafuasi wao wanaoingia katika kanisa lao putaputa. Hufichwa ukweli kama paka wanaosafirishwa katika gunia. Kwa nini? Wanafichwa ili wasiujue ukweli walikotokea wasije wakajua kwamba wamekosea njia kiimani.
Kifupi, madai yao kwamba Baba Mtakatifu, Kanisa Katoliki au Mfalme Constantino ndio waliobadili Sabato kwenda Jumapili ni mojawapo ya matusi ya Wasabato. Wenyewe wanahubiri hayo kwa jasho jingi kabisa wakati ni kusepetuka kwa uelewa na fichio la aibu yao katika kushindwa kwao katika utabiri wa tarehe ya mwisho wa dunia, tarehe ambayo Yesu  Kristo, Bwana wetu na Maandiko yanatuambia kwamba haitabiri kabisa.  Kwa maneno mengine, ndiyo matawi ya chuki iliyokosewa mwelekeo na uongo wa binadamu dhidi ya wanadamu wenzake.
Tusisahau, kutokana kushindwa hoja na aibu kubwa waliyoipata mbele ya ukweli unaoshikiliwa na kufundishwa na Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki, Wasabato na makanisa mengine wameamua kutumia mbinu ya kujikosha kwa matusi makali.  Wameamua kujitwika utume wa matusi wakati mwingine hata matusi ya nguoni. Kwa vyovyote, Wakatoliki hawana namna rahisi ya kukabiliana na madai hayo ya kimatusi. Usistaajabu haya kufanyika hivi. Kwa mtindo wa vijijini, ukishindwa hoja kwa mtu fulani unaanza kumtukania wazazi wake, nyumba yao na kadhalika.

KUITUNZA SABATO NI KUSHEREKEA MKESHA WA SIKU YA UHURU
Kuitunza Sabato mbele ya Dominika ingelingana na kusherekea mkesha wa siku ya uhuru badala ya siku ya uhuru yenyewe. Taifa litakalofanya hivyo litachekesha na labda litakuwa la watu punguani. Aidha mtu kupita huko na huko kuwahimiza watu washerehekee mkesha wa uhuru badala ya siku ya uhuru wenyewe ingelikuwa sawa na kucheza Ze Comedy.
Nani amegeuka mkondo wa mambo hata kugeukia tena Sabato wakati Wakristo wa kwanza kwa kumwelewa vyema Yesu Kristo walishaitupilia mbali?  Jibu ni wazi. Ni mmoja wa waanzilishi wa dhehebu la Wasabato, yule mama anayejulikana kama nabii. Kwa taarifa yako waanzilishi wa dhehebu la Wasabato ni akina Hiram Edson, Joseph Bates, E.G. Harmon na Hellen White. Katika hawa aliyekuja na moto wa kurudisha Sabato ni huyo mama ambaye alikuwa mke wa E.G. Harmon. Mwanamke huyo anaheshimiwa na Wasabato kama nabii na vitabu vyake , kama vile Vita Kuu, Afya na Raha na Ushindaji, vinasomwa na Wasabato karibu kama misahafu.

WASABATO WASIMNYANYASE YEYOTE

Maono ya uwongo ya Bi Hellen yasiwe sababu ya kuwanyanyasia Wakristo wasio Wasabato. Wala si siri, makanisa yanayofuata mabadiliko yaliyoletwa na Mungu mwenyewe kutoka Sabato kwenda Dominika yananyanyaswa kweli kweli na kauli za Wasabato wanaomfuasa Bi Hellen White. Lakini, hivi unabii wa mama huyo ni wa kweli hata tutishik
e nao? Hapana, wala si wa kweli. Unabii wa mama huyu lazima tuukatae. Kwa nini tuukatae?

TUHIMIZANE TUMKATAE BI HELLEN NA MAONO YAKE

Ni kwa sababu kuna sababu tatu zinazotuhalalisha tumkatae Bi Hellen White kama nabii. Mosi, kitabu cha Ufunuo kinaonesha kufungwa kwa unabii, yaani kwamba baada ya mambo yaliyoandikwa humo kusingekuwa na ufunuo wowote wa pekee. Ukamilifu wa ufunuo ulitokea katika ujio wa Yesu Kristo. Alichosema yeye ndicho kitu cha kilele. Sasa Bi Hellen anakujaje na mapya kumpikua Yesu Kristo? Tunasoma, “Mungu ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi, amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akavichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu, amefanyika bora kupita malaika kwa kadiri jina alilorithi liliyo tukufu kuliko lao” (Ebr 4:1-4).

Si hivyo tu hata mintarafu ufunuo wa zamani mihuri yake imevunjwa na Yesu Kristo mwenyewe, sasa unabii wa Hellen White unaanzia wapi? Tunasoma, “Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na nyuma, kimetiwa muhuri saba. Nikaona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kuu, Ni nani astahiliye kukifungua kitabu na kuzivunja muhuri zake. Wala hapakuwa na mtu mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. Nami nikalia sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kikifungua hicho kitabu, wala kukitazama. Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba.

Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwanakondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote. Akaja , akakitwaa kile kitabu katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi. Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya Mwanakondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya wakatakatifu, nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaaa hicho kitabu na kizifungua muhuri zake, kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme wa makuhani, kwa Mungu wetu, nao wanamiliki juu ya nchi” (Ufu 5:1-10).

Mintarafu kusasambua ovyo ufunuo wa Mungu, mwandishi wa kitabu cha Ufunuo alishakatazwa, sasa Bi Hellen White anapata wapi nguvu ya kuja na ufunuo mpya? Kuhusu marufuku hiyo tunasoma, “Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike” (Ufu 10:4). Hatimaye, maneno ya ufunuo yaliachwa wazi bila muhuri kwa vile yalivyokuwa njiani kutimia. Juu ya jambo hili, tunasoma hivi: “Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki kwa maana wakati huo umekaribia” (Ufu 22:10). Sasa Bi Hellen White anaongezaje maneno ya ufunuo mpya?

Pili, tuukatae unabii wake kwa vile zile anazoziita njozi, kama elfu mbili hivi, ni batili kwani zinaonesha jinsi alivyojaa chuki kwa Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki nasi tunajua kwamba si kazi ya Mungu Roho Mtakatifu kumjaza mtu chuki kali hivyo dhidi ya mwanadamu mwingine. Kazi hiyo hufanywa na Shetani nayo huonesha kwamba moyo wa mtu umejaa uovu kwani kilichomjaa mtu moyoni ndicho kimtokacho. Tunasoma, “Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. Mtu mwema  katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake”  (rej. Lk 6:43-45). Hakika chuki dhidi ya Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki inatoka katika moyo uliofurika uovu. Na kwa jinsi hii maono yake hayawezi kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Tatu, tuukatae unabii wake kwa sababu mafundisho yake yanaonesha kwamba haijui Biblia. Hoja hii ya tatu nimeshaishuhudia tayari. Nimesema ameota ndoto akaona huko mbinguni kuna hekalu wakati Maandiko yanatakaa jambo kama hilo (rej. tena Ufu 22:22-24). Kisha nimeshashuhudia kwamba kule kusisitiza kwamba Sabato ndiyo amri kuu kunapingana na kile alichotuambia Bwana wetu Yesu Kristo aliyesisitiza kwamba amri kuu ni upendo (rej. tena Mt 22: 34-40).  Naomba itoshe nilivyokuambia nawe uyapuuze maono ya Mrs. Harmon tunayemchambua hapa.

MAJIBU KWA MASHTAKA YA ZIADA

Nikiendelea kidogo, naomba ruksa nijibu mashtaka mawili sambamba wanayotoa Wasabato dhidi ya Wakatoliki: mosi kwamba ndio mnyama yule Shetani aliyejipa jukumu la kubadili majira na pili kwamba Kanisa lenyewe linakiri kufanya hivyo katika Katekisimu zake na katika vitabu vya waandishi fulani fulani wa Kanisa Katoliki.
Mintarafu hoja ya kwanza ni hivi mnyama ni Bi Hellen White aliyethubutu kumpinga Mungu. Mungu aliibadili siku ya Sabato yeye akijipa jukumu la kuirudisha kwa maelezo ya maono yake batili kabisa. Tumeshaonesha jinsi yalivyo batili kwa kadiri ya mizani na darubini ya Maandiko Matakatifu.

Halafu mintarafu hoja ya pili ni hivi Kanisa linajihusisha na mabadiliko hayo si kama ‘mtendaji’ kwani hakuna mkutano mkuu (mtaguso) wowote wa Kanisa Katoliki uliojadili hoja ya Sabato na kuamua kuibadili kwenda Dominika ila kwamba Mungu aliibadilisha Sabato pale alipoanzisha enzi ya Israeli mpya yaani Kanisa.  Natumaini wasomaji wangu hoja hii si ya kitaalamu mno kiasi cha kutonielewa ninachosema. Ninasema hivi Kanisa linajisikia kuhusika na ubadilishaji wa Sabato kwenda Dominika kwa vile Mungu aliufanya kuanzia pale lilipoanza kuwako nalo kwa mamlaka uliyopata kutoka kwa Mungu ikayasimamia na kuyaendeleza mabadiliko hayo.

MALUMBANO SASA YAKOME

Naomba hadi hapa shtaka la kwamba Kanisa Katoliki limebadili majira, yaani kutoka Sabato kwenda Dominika (Jumapili), lififie kabisa. Si unajua kwamba hoja yenyewe hukokotolewa kutoka Dan 7:25 mahali palipoandikwa, “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye Juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye Juu, naye ataazimu kubadili majira na sheria”. 
Kama unavyoisoma sasa, hoja hii haitaji Kanisa Katoliki bali kwa kinyume chake inawataja Wasabato wenyewe. Ndugu zangu Wasabato haliwafahamu jambo hili kwa sababu ndivyo ilivyo, “Jambo usilolifahamu ni sawa na usiku wa giza.” Kwa vipi? Ni hivi, kama Yesu kwa maneno na matendo yake alisema Sabato si lolote na wala si chochote “maana mtu hakuuumbwa kwa ajili ya Sabato”, mtu anayesema Sabato ndiyo yote katika yote ndiye anayeazimu kubadili majira na sheria. Na moja kwa moja mtu huyo anakuwa ndiye mpinga Kristo kwa sababu anapingana na kauli ya Kristo mwenyewe. Hilo ndilo alilofanya nabii Hellen na kuwasadikisha maelfu ya watu kauli yake kengeufu.

Aidha, kama Yesu alisema kwamba amri kuu ni upendo (rej. Mt 22:37) na akataka iwatambulishe wafuasi wake popote watakapokuwa (rej. Yn 13:35), anapokuja nabii Hellen na kusema eti amri kuu ni Sabato ni upinga Kristo wa wazi wazi na kumfuasa mpinga Kristo kama huyo ni kuwa wapinga Kristo wadogo wadogo nyuma ya huyo mkubwa. Ona ushuhuda wa Maandiko Matakatifu. Bila shaka, hata wewe unakumbuka Yesu aliulizwa swali juu ya amri ya kwanza na kuu naye akatoa jibu mwafaka hata wasomi na walimu wa enzi zake wakamvulia kofia.

Tunasoma, “Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. Mmoja wao, mwanasheria, akamwuliza, akimjaribu: Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” na wakati akiwaaga wanafunzi wake jioni iliyotangulia kifo chake alisema na kuagiza, “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi” (Yn 13:35). Sasa Nabii Hellen anathubutuje kusema kinyume cha maneno hayo ya Kristo ambaye tumepewa tumsikilize? Kama huo si upinga Kristo wenyewe ni nini tena? Hukumu mwenyewe; wewe ni mtu mzima. Hivi wewe na mimi na sisi sote hatukumbuki maneno ya Maandiko Matakatifu, “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye” (Mk 9:7)? Na kwa upande wetu, kwa nini, tunamsikiliza binadamu tena? “Tumechanganyikiwa” au “tumerogwa”?

UCHAMBUZI WA KISAIKOLOJIA WA WALIOHUSIKA NA HISTORIA HII YA AIBU

Jina Ugonjwa Tunaoweza Kumtuhumu Upinga Kristo Wake Ulipo
William Miller Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kujaribu kuitaja tarehe ya mwisho wa dunia Kukokotoa tarehe ya mwisho wa dunia kinyume na Mk 13:32.
Samwel Snow Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kujaribu kuitaja tarehe ya mwisho wa dunia Kukokotoa tarehe ya mwisho wa dunia kinyume na Mk 13:32.
Hiram Edson Schizophrenia – kuona hekalu ambalo halipo mbinguni na kudai mwisho wa ulimwengu umeshatokea.  Kuota ndoto ya kuliona hekalu mbinguni ni kinyume cha Ufu 21:22-23.
Joseph Bates Megalomania – kujidai kujua kuliko Yesu Kristo kwa kuunga mkono uongo kwamba mwisho wa ulimwengu umeshatokea. Kuidharau Jumapili, siku aliyoitumia Bwana kufanya mambo yote makubwa.
Hellen White Schizophrenia – kuona hekalu ambalo halipo  Kuota ndoto ya kuliona hekalu mbinguni ni kinyume cha Ufu 21:22-23 na kudai Sabato ndiyo amri kuu kinyume na Mt 22:34-40.

MASWALI NA MASHTAKA 12 MAARUFU YA WASABATO KWA WAKATOLIKI

i. Sabato ndiyo siku ya kuabudu iliyoamriwa. Wakatoliki ndio walioifuta Sabato na kuweka Jumapili.
ii. Wakatoliki wanafuata mapokeo ya binadamu, hawajui na wala hawafuati Maandiko Matakatifu.
iii. Baba Mtakatifu ndiye mnyama yule anayewakilishwa na namba 666. Namba hiyo imeandikwa kwenye kofia na mavazi yake.
iv. Wakatoliki wameifuta amri ya pili ya Mungu. Wamefanya hivyo ili waabudu sanamu.
v. Wakatoliki wanaabudu sanamu. Tazama sanamu makanisani mwao!
vi. Kwa nini Wakatoliki wanakunywa pombe wakati imekatazwa kwenye Biblia?
vii. Wakatoliki wanamwabudu Bikira Maria. Kwa nini wanamfanyia heshima kubwa isivyostahili?
viii. Je, Bikira Maria alikuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu Kristo?
ix. Kanisa Katoliki linafanya makosa kuwatangaza wanadamu kuwa watakatifu. Mwanadamu ana uwezo gani wa kumtangaza mtu mwingine kuwa mtakatifu?
x. Wakatoliki wana sakramenti saba. Wana makosa kwa sababu hazijaandikwa kwenye Biblia.
xi. Kuungama ni kwa Mungu moja kwa moja. Kuna uhalali gani kwenda kuungama kwa mapadri wakati wenyewe wana dhambi?
xii. Wakatoliki wana hatia kubwa kwa sababu hawataki kuokoka. Kwa nini Wakatoliki ni wabishi hivyo?
Ndugu yangu Mkatoliki jaribu kuwa na majibu ya maswali haya, hutahangaishwa na Wasabato wowote katika imani yako na maisha yako yote. Kumbe, usipokuwa nayo siku zote utayumbishwa kama wimbi la baharini wakati ulipaswa kutulia tuli kama maji kwenye mtungi.

HATIMA: TUSIHANGAISHANE TENA JUU YA SABATO KWANI  ILIKUWA KIVULI TU

Kwa sasa Wakatoliki wote tuhitimisha fikra zetu kwa nukuu hii: “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni KIVULI cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo” (Kol 2:16-17).
Ndugu zanguni, kama inavyosomeka katika aya hizi, Sabato ilikuwa kivuli na kivuli hakishonewi suti. Sisi ni watu wazima tuachane na Sabato. Nina hakika tutaadhibiwa na Mungu kwa hatia ya kukipa hadhi kitu kisicho na uzito wa kimani.

Imeandikwa na
Pd. Titus Amigu (2016)

Tuesday, September 13, 2016

Msiba Boston - Mrs. Aisha.Rupia

                                            Aisha Rupia, mume wake Paul Rupia na watoto wao.


Tunasikitika kuwajulisha kuwa Paul Rupia amefiwa na mke wake Aisha Rupia ambaye ametutoka leo alfajiri 9/13/2016.  Mungu amlaze mahali pema peponi, Amin.
Msiba utakuwa nyumbani kwa Paul, 16 Feener Circle, Randolph, MA.
Mipango ya mazishi inaendelea, tutawajulisha zaidi hapo baadaye.
Kwa taarifa zaidi wasiliana na...
Paul Rupia 781-913-9363
John Rupia 857-251-4408
Stella Rupia 617-792-8815
Abela Haley 781-913-2107


It is with great sadness that we announce Aisha Rupia, wife of Paul Rupia has passed away today 9/13/2016. May God Rest her soul in Peace, Amen.  The bereavement will be at their house, 16 Feener Circle, Randolph, MA. Further information will follow after funeral arrangements have been finalized.
For more information, contact...
Paul Rupia 781-913-9363
John Rupia 857-251-4408
Stella Rupia 617-792-8815
Abela Haley 781-913-2107

Saturday, September 10, 2016

Tetemeko la Ardhi Bukoba - Earthquake in Bukoba, Musoma and Mwanza Tanzania

Nimepata ujumbe kupitia Facebook muda huo kuwa kumetokea tetemeka la Ardhi kubwa (Earthquake) Bukoba!!!! Nitawajulisha nikipata habari zaidi!

***********************************
Tetemeko la Ardhi imetokea Mwanza, Bukoba na Musoma.  Magnitude 5.7.



**********************
Earthquake information today.
Magnitude 5.7
Region LAKE VICTORIA REGION, TANZANIA
Date time 2016-09-10 12:27:28.6 UTC
Location 1.06 S ; 31.55 E
Depth 10 km
Macroseismic
Intensity VI Effects: Slightly Damaging
Distances
191 km SW of Kampala, Uganda / pop: 1,354,000 / local time: 15:27:28.6 2016-09-10

42 km NW of Bukoba, Tanzania, United Republic of / pop: 70,700 / local time: 15:27:28.6 2016-09-10
20 km NE of Nsunga, Tanzania, United Republic of / pop: 20,100 / local time: 15:27:28.6 2016-09-10


Picha kwa Hisani ya Innocent Lugumamu.  Picha ni kutoka Bukoba Kijijini.










*****************************************************************
 Picha kutoka Bunda, Tanzania Kwa Hisani ya Mawazo Maduhu





UNESCO Yazindua Ripoti ya Ufuatliaji wa Elimu Duniani (GEM) 2016

 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akimkabidhi mgeni rasmi, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta, sanduku la Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM).
 Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya kisomo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta akigawa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM) kwa baadhi ya wafanyakazi wa wizara yake.


Na Mwandishi wetu
Katika kutambua umuhimu wa kusoma na kuandika Tanzania na mataifa mengine duniani zimeungana kwa pamoja kuadhimisha siku ya Kisomo Duniani ambayo huadhimishwa kila Septemba, 8 ya kila mwaka ambapo pamoja na maadhimisho hayo pia iliambatana na Uzinduzi wa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani (GEM).

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez alisema kuwa dhumuni la UNESCO kuweka siku hii ya Septemba 8 kila mwaka kuwa siku ya kisomo kimataifa ili kuziunganisha jamii zote za kimataifa duniani kuweka na kuendeleza nguvu na juhudi kwa watu kujua kusoma na kuandika ili kuleta maendeleo katika jamii mbalimbali.

“Kauli mbiu hii inatufungulia milango ya uelewa juu ya malengo na mafanikio ya miongo mitano iliyopita ambayo yaliwekwa ya kutaka kila mtu anajua kusoma,” alisema Bi. Rodrieguez na kuongeza.

“Tunataka kujua ni changamoto gani zinazoikabili sekta ya elimu katika kusoma na kuandika na tunataka kufahamu namna ya kukabiliana na changamoto hizo ili kufikia malengo ambayo UNESCO iliyakusudia kufikiwa ya kila mmoja awe anajua kusoma.”

Kwa upande wa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta ambaye alimuwakilisha Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo alisema serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imejizatiti kuondoa tabaka la wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa vijana na watu wazima kwa kujenga uwiano sawa wa utoaji wa elimu kwa watu wote.

“Wizara imejipanga vizuri, na lengo kubwa la wizara ni kuhakikisha tunakuwa na mtanzania aliye elimika na aliye na stadi, maarifa na uwezo wa kutumia elimu aliyoipata,” alifafanua Bureta.

Vile vile Bw. Bureta amesema kwa sasa wizara ipo kwenye mpango wa kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) ambao unaanzia chini kwa wanafunzi wa awali mpaka shule za msingi.

Katika mpango huo walimu wamekuwa wakipata mafunzo mbalimbali ya namna ya kumuwezesha mwanafunzi kujua Kusoma Kuandika na Kuhesabu katika ngazi ya elimu ya awali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, Basilina Levira amesema kwamba kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012, asilimia 78 ya vijana na watu wazima ndio waliokuwa wakijua kusoma na kuandika.

Akaongeza kuwa mwaka 2015 idadi hiyo ya wanaojua kusoma na kuandika ilishuka na kufikia asilimia 77 ambapo ilipelekea wizara hiyo kutoka na mikakati inayokusudia kuondoa kabisa tabaka la watu wasiojua kusoma na kuandika nchini.

Aidha, Basilina amesema kuwa Serikali ilipitisha sheria ya vyumba vya madarasa ya shule zote nchini kutumika kufundishia vijana na watu wazima ambao hawajui kusoma na kuandika muda wa jioni baada ya wanafunzi wa kawaida wanapomaliza masomo yao.

Amefafanua kwa kusema kuwa, wizara imeandaa programu ambayo iko kwenye mfumo wa Televisheni na picha za video (DVD) yenye masomo 65 ya kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu, ambapo kwa kutumia programu hiyo mwanafunzi anaweza kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa muda wa miezi 4 mpaka 6.
Mafunzo hayo kwa njia ya Televisheni na Picha za Video tayari yameanza kutumika kwa wilaya za Ilemela, Dodoma Manispaa, Songea Manispaa, Bagamoyo, Mkuranga, Temeke, Ilala na Kinondoni, ambapo asilimia 65 ya vijana na watu wazima wasiojua kusoma na kuandika wamejitokeza kujiunga na Elimu hiyo huku idadi kubwa ikiwa ni ya wanawake.

Siku ya Kisomo Duniani huadhimishwa Duniani kote kila ifikapo Septemba, 8 ya kila ya mwaka, ambapo mwaka huu 2016 maadhimisho hayo yametimiza miaka 50 tangu yalipoanza kuadhimishwa mwaka 1966.

Kauli mbiu ya siku ya kisomo duniani kwa mwaka huu ni ‘Tunasoma yaliyopita, Tunaandika yajayo, Elimu endelevu’ ambayo kwa lugha ya kiingereza ni ‘Reading the future, Writing the past’.

Mkuu wa Mkoa Mwanza Akabidhi Vyakyula Kwa Niaba ya Rais Magufuli Kwenye Kituo cha Bukumbi

To kmwantepele Dotto Mwaibale Mzee Ahmad Michuzi Cathbert Kajuna and 232 more... Message body
Katika kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj siku ya Jumatatu Septemba 12, 2016, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, ametoa msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi laki saba na elfu themanini (780,000), kwa ajili ya Kituo cha kulelea Wazee na Walemavu wasiojiweza cha Bukumbi Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Akikabidhi msaada huo jana, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, aliuhimiza uongozi wa kituo hicho kusimamia vyema ugawaji wa vyakula hivyo li kuwafikia walengwa, ikizingatiwa kwamba kumekuwa kukiibuka malalamiko kutoka kwa wazee wanaoishi katika kituo hicho kwamba misaada ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali imekuwa haiwafikii yote.

Hata hivyo Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhili mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.

Wazee wanaoishi kituoni hapo waliishukuru serikali kwa msaada huo ambapo walisema wanaendelea kumuombea Rais Magufuli na Serikali yake ili iendelee kuboresha kituo hicho ikiweo kuwekewa uzio ili kuondokana na hofu ya kiusalama waliyonayo kwani wakati mwingine wamekuwa wakiibiwa mali zao ikiwemo kuku ambazo wamekuwa wakizifuga.

Vyakula vilitolewa na Mhe.Rais Magufuli ni, mchele gunia sita (kila gunia kilo 50), mafuta ya kupikia madumu manne (kila dumu lita 20) pamoja na mbuzi wawili.
Baadhi ya wazee wanaoishi kwenye Kituo cha Bukumbi, wakifurahia mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza baada ya Rais Magufuli kuwapatia msaada wa vyakula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Idd El Hajj, itakayofanyika kesho kutwa jumatatu.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (mwenye kofia), akimsikiliza mmoja wa wazee katika Kituo cha Wazee Bukumbi.
Mmoja wa akina mama kwenye Kituo cha Bukumbi akiishukuru Serikali kwa msaada wa chakula ilioutoa kituoni hapo
Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe.Juma Sweda (kulia), akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa chakula uliotolewa na Mhe.Rais Magufuli katika Kituo cha Wazee Bukumbi wilayani humo. Alisema Serikali inawajali Wazee wanaoishi katika kituo hicho na kwamba ina upendo kwao ndiyo maana inaendelea kuwahudumia.
Kaimu Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Georgina Kwesigabo, alitanabaisha kwamba vyakula na misaana ambayo imekuwa ikitolewa na serikali pamoja na wafadhiri mbalimbali kituoni hapo, yote imekuwa ikiwafikia walengwa wote isipokuwa kuna changamoto ya baadhi yao kuuza misaada wanayopatiwa ikiwemo vyakula, jambo ambalo linaulazimu uongozi wa kituo hicho kuandaa utaratibu wa kusimamia misaada hiyo hususani kuwapikia chakula wanaoishi kituoni hapo badala ya kuwagawia chakula ili wajipikie wenyewe.
Vyakula vilivyotolewa na Mhe.Rais Magufuli kwa ajili ya Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Huyu mbuzi, tehe tehe tehe!!
Makao ya Wazee na walemavu wasiojiweza Bukumbi, Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo wa BMG

Wednesday, September 07, 2016

Mama Bishanga na Wadogo Zake Wafiwa na Mama Yao

MAMA BISHANGA NA WADOGO ZAKE WAFIWA NA MAMA YAO

         MWALIMU AGNES NDEMBO HATIA
Watoto wa marehemu mzee Isaya Innocent Hatia tumempoteza mpendwa mama
yetu mpendwa Mwalimu Agnes Ndembo Hatia kilichotokea hospitali ya Regency
 jana jumamamosi mchana. Mama yetu alikuwa nguzo pekee iliobakia nasi baada
ya kufariki baba yetu Mzee Isaya Innocent Hatia mwaka 2011. Tunamshukuru
Mungu sana kwa upendo wake kwa mama yetu aliempa nguvu ya kuishi miaka
tisini na sasa amempenda zaid mama yetu, bibi yetu na amempumzisha usingizi
wa milele na milele Ameni
Mwalimu Agnes Ndembo Hatia amefundisha watu wengi sana darasa la kwanza
tangia miaka ya hamsini hadi alipostaafu Tabora, Uhuru shule yamsingi.
Mama, ametuacha watoto wake Christina wa USA, Geofrey wa Namibia, Mwl
Mark Hatia wa Tambaza shule ya secondary, Bernadetta wa Dar, Isaya wa Finland,
Costancia wa Kibaha, na Oscar mdogo wetu wa mwisho. Ameacha wajukuu, na
vitukuu wengi ambao ni watoto na wajukuu zetu sisi watoto wake pamoja na dada
zetu marehemu Joyce Hatia na Mwalimu Cecilia Hatia. Picha zinaonyesha
mama Hatia mwaka 1966 akiwa na Constacia ambae picha yake pembeni ni Costancia
alivyo sasa, na zingine ni mama na wanae wajukuu na vitukuu
Kwa taarifa za maandalizi na ratiba piga simu zifuatazo. 0653 763 201 Kilian Kamota,
0755 333 948 Dick Hatia, 0788 627 430 Ibra Yunus, na 0763 833 893 Solmon.
 BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA. TUMSIFU YESU KRISTO: AMEN