Friday, February 29, 2008

Jina la 'Tanganyika'

Wanawake enzi za Tanganyika

Nimeona historia ya jina la Tanganyika hapa: Je, hayo maelezo ya kupatikana kwa jina, Tanganyika ni kweli. Mimi nilikuwa nadhania 'nyika' ni msitu. Au?




It is said that the mainland portion of what is now Tanzania was named by a British civil servant in 1920, from the Swahili words tanga (sail) and nyika (bright arid plain). Thus what was known formerly as German East Africa became Tanganyika Territory. In 1964, Tanganyika was joined with Zanzibar, an offshore archipelago of islands, to form the present United Republic of Tanzania.

Maiti ya SuperModel kutoka Guinea yakutwa mtoni Ufaransa



Habari kutoka Ufaransa zinasema kuwa maiti ya supermodel, Katoucha Niane, (47) umepatikana katika mto Seine. Mrembo Katoucha alikuwa hajaonekana tangua mweza January na jitihada zilifanywa za hali ya juu kumtafuta.

Katoucha ni kati ya wanawake wa kwanza kutoka Afrika kutamba katika dunia ya u-model. Alizaliwa Guinea.
Katoucha aliwahi kutamba na madesigner wakubwa kama Yves Sain Laurent, Christian Lacroix, Paco Rabanne na Thierry Mugler.
Katoucha alikuwa pia ni mpigania haki za wanawake. Alilaani vikali kitendo cha kuketa wasichana huko kwao. Yeye mwenyewe alikeketwa akiwa na miaka 9. Alikimbia kwao akiwa na miaka 17 na alienda Ufaransa. Alisema kuwa hawezi kusahau maumivu makali ambayo alisikia kutokana kutokana na kitendo hicho.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.
Kwa habari zaidi someni:

Casting Call ya ajabu yasababisha serikali iingilie!

Hillbillies

Hapa Marekani kuna jimbo inaitwa West Virginia. Hiyo jimbo inajulikana kwa watu washamba sana (hillibiilies). Wanavyosema kwenye milima ya kule ni jambo la kawaida mtu kufunga ndoa na ndugu yake, hatimaye watoto wanakuwa na nyuso za ajabu na hawana akili sana.

Sasa kuna sinema ambayo inaanza kutengenezwa mwezi ujao, inaitwa Shelter. Stelingi wake ni Julianne Moore. Sasa katika kutafuta extras, mtu aliyekabidhiwa hiyo kazi alitangaza casting call ya ajabu.

Donna Belajac Casting iliyoko Pennsylvania ilitangaza kuwa inatafuta, watu warefu mno, watu wafupi, watu wenye shepu za ajabu na uso za ajabu. Walisema pia kuwa wanatafuta watu wenye kasoro kwenye miili yao hasa macho. Pia walikuwa wanatafuta viwete wasiohitaja msaada maalum.

Haya hiyo siyo mbaya, lakini aliharibu aliposema anatafuta watu ambao wanafanana na 'inbred' yaani waliozaliana wenyewe kwa wenyewe. Tena waliongeza watu wanafanana na 'holler people' ni kabila fulani ya ya wazungu wanaokaa kwenye milima ya West Virginia.

Hapo huyo Donna Belajac kawasha moto! Viongozi wa West Virginia walichachamaa maana walisema kuwa ni stereotype kuamini kuwa watu wa West Virginia ni inbreds na washamba! Gavana Joe Manchin wa West Virginia alilaani hiyo sinema na hiyo casting call vikali! Pia viongozi wengine waliingilia.


Mwisho watengeneza sinema ya Shelter, waliomba msamaha kwa watu wa West Virginia na pia walifukuza kazi kwenye hiyo sinema, hiyo kampuni ya Donna Belajac! Duh!

Kwa habari zaidi za mkasa huo someni:




Thursday, February 28, 2008

Zanzibar International Film Festival 2008





Zanzibar, February 2008 –The Zanzibar International Film Festival has released its programme for the 11th Edition of ZIFF the Festival of the Dhow Countries, to take place between 11th to 20th July this year.


ZIFF will this year welcome top names to the festival proving the status that the festival enjoys in world festival circles., as director Newton Aduaka from Nigeria winner of Etalon Yenenga at FESPACO 2007 confirmed his attendance. Efforts are underway to bring multiple award winner Danny Glover and Charles Burnett with their film Namibia: Struggle for Liberation which is expected to open the festival.

Tanzanian acting circles have applauded plans to bring Ramsey Nouah, the king of Nollywood melodramatic film production who will also conduct acting workshops and show his films at ZIFF! “ZIFF will not have enough space to hold the crowds, should he confirm coming to Zanzibar!”, said a film enthusiast, “Many women have vowed to travel to Zanzibar should the suave actor confirm coming to ZIFF in July”

This year shall carry the theme Cultural Crossroad though which Zanzibar becomes again the crucible of cultural intersections and mutual respect.“Preparations are underway to deliver to our patrons a sumptuous program of films and other cultural offerings befitting the long wait for ZIFF”, said the ZIFF CEO, Dr. Martin Mhando.

Amongst the standout events for the year is the return of the Zanzibar Fensi! This veritable Zanzibari cultural activity has not taken place for over 8 years and this year will see the return of Fensi in its carnival form!

Dr Mhando also announced that Nollywood, the third world largest film feature production industry, will be fĂȘted in Zanzibar during the festival. The impact that Nollywood has had on Africa cinema will also be debated under the Soko Filam program.60 films will be in competitions judged by four International Juries, and currently 4 world Premieres Films have been confirmed.

Amongst the premieres is Tanzanian Josiah Kibira’s Bongoland II which will have its African premiere at the festival.

The ZIFF management again reminded filmmakers that the deadline for entering films into ZIFF 2008 is 31st March.

Entry forms for films and musical groups are available on the ZIFF website http://www.ziff.or.tz/

Mtindo wa 'Lishuka' mpaka Liberia!

Mammy Dresses Scarlett in Gone With the Wind
President Bush with Liberian President Ellen Johnson-Sirleaf during his recent trip to Liberia (photo courtesy of Michuzi Blog)

Aisei, kumbe watu wanausudu fesheni zetu za Bongo! Mtindo wa kutundika kitambaa begani umefika mpaka Liberia! Cheki gauni ya Rais wa Liberia Mama Ellen Johnson-Sirleaf.

TAMWA waliwahi kufanya mashindano ya National Dress ya Tanzania, miaka ya 80. Mtindo uliyoshinda ni huo wa kitambaa begani. Nadhani walisema ni fesheni ya tangu enzi za Tanganyika.

Sasa nikichambua vazi la Mama Johnson-Sirleaf, zaidi naona Kilemba chake kinaelekea kwenye asili ya mababu zao yaani watumwa waliotoka Marekani. Nimeweka picha ya Mammy hapo kuonyesha watumwa walivyokuwa wanafunga kitambaa kichwani. Mnaonaje?
Liberia ulianzishwa na watumwa walioachiwa huru Marekani na kurudishwa Afrika.

Kwa habari zaidi za kuanzishwa taifa la Liberia someni:

http://www.bbc.co.uk/worldservice/africa/features/storyofafrica/9chapter9.shtml

http://www.loc.gov/exhibits/african/afam002.html

Tuesday, February 26, 2008

Kampeni ya Hillary wazua Mambo - Eti Obama ni Msomali!

Laura Bush dons Muslim robes and head scarf
President Bush dons foreign attire
This is what Hillary's campaign is using for fear mongering. They claim that Obama really is a Muslim in hiding! By the way, Obama is not a Somali! That is Somali attire he is dressed in!
President Bill Clinton dons African attire
Woops! Hillary and her daughter Chelsea wear Muslim headscarves!
Hillary dons a Head Scarf!
Now we know that Hillary must be affiliated with terrorists!


Hii kampeni ya uchaguzi Marekani safari hii imezidi kuwa chafu mpaka inatia kichefuchefu! Mara kuna 'plants' za kuharibu ofisi za kampeni, mara kuna wengine ambao kazi yao ni ku-twist ukweli.

Leo nimesikitika sana, tena mno, kusikia baadhi ya wazungu wakisema kuwa kumbe ni kweli Obama ni mwislamu. Oh kumbe yuko Al-Qaeda! Oh, kumbe kaelekea zaidi kwenye Uislamu. Kwenye WCVB TV Channel 5 hapa Boston, mtangazaji alisema kuwa kwenye hiyo picha Obama kavaa nguo za Middle East!

Kisa, kampeni ya Hillary wanazungusha picha kwenye neti ya Obama akiwa amevaa nguo za wazee wa kiSomali. Picha ilipigwa alipotembea huko Kenya mwaka 2006. Hivi Obama si MJaLuo?
Hillary anatafuta kura kwa nguzu sasa huko Texas na Ohio. Alishindwa kwenye uchaguzi wa awali kule ndo mwisho wake katika kugombea. Lakini watu wanasema hii tactic ya kutoa picha itamwangusha Hillary haitamsaidia. Wanasema kuwa kumbea huyo mama ni bytch na yuko tayari kufanya kitu chochote ili ashinde!

Nimebandika picha za waheshimwa wakiwemo Hillary wakiwa wamevaa hijab na nguo zinge zi kiutamduni.

Kwa waongea kimombo:

Hey you ignoramuses out there, Mr. Obama's father is from the Luo tribe ofKenya! He is not a Somali. He was just visiting a group of people who live in Kenya and they showed him their respect!

Plus it is a sign of disrespect no to don the attire of the people you are visiting in some foreign lands. Take a look at the photos above!

Kwa habari zaidi someni:

http://youdecide08.foxnews.com/2008/02/25/photo-showing-obama-in-somali-garb-circulated-by-clinton-campaign-source/

http://www.news.com.au/couriermail/story/0,20797,23277403-952,00.html?from=public_rss

http://www.bayoubuzz.com/News/US/Politics/President_Race_2008/Hillary_Clinton_Over_Hill_With_Obama_Somali_Photo__5883.asp

http://bigheaddc.com/2008/02/25/drudge-falsely-accuses-clinton-of-obama-photo-ties/

Binti Daria Adamu Juma


Hii habari inatoka kwa mdau aliyeona hii picha ya 'Mzungu na mke wake 1905' . Bado hatujajua ni akina nani hao katika picha hii. Lakini Bwana Komba Muhili ameniletea habari za mzaa babu yake aliyelazimishwa kuolewa na mjerumani wakati huo huko Songea.
********************************************************************************

Binti Daria Adamu Juma


Imeandikwa na Komba Muhili

Hii picha inanikumbusha marehemu Mama mkubwa yaani Bibi yake Baba. Alikuwa anaitwa daria Binti Adamu alifariki mwaka 1981. Tulikuwa tunahisi alifariki akiwa na miaka 107. Alikuwa akitusimulia Habari za wajerumani wakati akisimulia alikuwa analia sana mpaka tunamwambia asilie kwani atatupa majonzi sana.

Yeye na familia yake waliishi katika Kijiji kimoja kiitwacho Rumecha, Songea wakati wa vita ya Maji maji alikuwa na miaka kama kumi na sita alikuwa amewekwa ndani si kama amefungwa amewekwa ili achezwe unyago pune vita ikaanza na wajerumani wakvamia kijiji chao.

Klichotokea ni cha kusikitisha baadhi walitekwa na wengine walikimbia cha kusikitisha zaidi yeye alikuwa mwali ndani akuweza kukumbia pamoja na familia yake ilibidi wakamatwe kilichotokea wazazi wake na nduguzake wote walipigwa Risasi na kufa papo hapo. Huku akiwaona wazazi wake wakiuliwa na wajerumani.

Kilichotokea yeye alichukuliwa na kamanda mmoja wakijerumani akawa mke wake bila ridhaa yake mwenyewe. Alikuwa aklia sana akikumbuka wazazi wake na nduguze alikaa na yule mjerumani zaidi ya miaka kumi na tano kama mke na mume kwani akuweza kufanya kitu chochote. Kilichotokea vita ilivyoisha tu yule mzungu akaenda nae Ujerumani na wakaishi huko na kubahatika kupata watoto wawili wakiwa na asili ya kizungu.

Baada ya kuzaa mtoto wa pili alilia sana na akaanza kususa hata kula akiulizwa shida nini akasema nakumbuka sana nyumbani hasa ndugu zangu. Basi yule mjerumani alichofanya alikuja nae mpaka Tanganyika akamuacha Bandari salama mwaka 1918 wakati vita ya kwanza ya Dunia ilivyokwisha.

Alivyofika hapa nyumbani alibusu ardhi ya Tanganyika huku akilia sana kwa uchungu alikuwa anafikilia watoto wake aliowaacha Ujerumani. Basi alifanikiwa kufika kijiji kwao kule Rumecha,Songea lakini akumfahamu mtu yeyote kilichotokea pale alipokewa na kukaribishwa kwa furaha.

Sasa kuna Mtu mmoja alitokea kumpenda sana Daria kilicho tokea pale alikubali kuolewa na yule mzee alikuwa anaitwa muhili komba na hatimae wakabahatika kupata watoto watano. Kati ya hao mmoja wapo ndio babu yangu mzaa baba na bahati nzuri niliishi nae. Mama mkubwa takribani miaka mitatu nikiwa na akili chakushangaza alikuwa mzee sana lakini meno yake yote yaliku meupe na hajang`oa hata moja.
Kwa kusema ukweli alikuwa mzuri sana nafikiri hata yule Mjurumani alimpenda kwa uzuri wake .Nimeona niwape kisa hiki ili nanji muone huko tilikotoka.

Monday, February 25, 2008

Auliwa kwa ajili ya Bling Bling zake!



Charles Ross (29) ameuliwa na jambazi aliyemwibia bling bling zake mjini New York. Bling bling zenyewe zilikuwa na thamani ya zaidi ya dola $10,000 zikiwemo na pete zenye almasi.
Ross alikuwa ametoka kazini shifti ya usiku anatembea kwa mguu kwenda nyumbani ndipo jamabazi alimvaa kwa nyuma na kumwibia hizo bling bling. Kuiba haikumtosha huyo jambazi, aliamua kutoa roho Ross!
Huko New York mambo yalikuwa posa kidogo lakini siku hizi mmmh!
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Mama Pinda na Mama Maria Nyerere

Kutoka Food for Thought Blog

Mke wa Waziri Mkuu, Tunu Pinda(kushoto) akiwa na Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam hivi karibuni Mke wa waziri mkuu Tunu Pinda pamoja na waziri Mkuu Mizengo Pinda walikwenda kumjulia hali Mama Maria Nyerere.

Rest in Peace Sembene Ousmane - 1923 -2007



Bila shaka wadau wengi mmesoma vitabu vya African Writers Series. Hivyo jina la Sembene Ousmane si ngeni kwenu. Alikuwa ni MSenegal. Alitunga vitabu vingi vikiwemo, God's Bits of Wood, na Xala.

Zaidi ya kuandika vitabu, marehemu Sembene alikuwa ni muongoza sinema maarufu barani Afrika. Alikuwa anaitwa, " The Father of African Cinema" yaani baba wa sinema Afrika. Hiyo ni kwa sababu alikuwa ni mwafrika wa kwanza kujulikana katika viwanjavya sinema vya kimataifa kama Hollywood. Huenda mmeona sinema zake za Xala, Faat Kine, Black Girl na Moolaade. Aliongoza kama sinema kumi na tano. Huko Afrika Magharibi hasa nchi zilizotawaliwa na Mfaransa (francophone) zimeendelea sana katika sinema kuliko nchi zilizotawaliwa na Mwingereza. Sinema zao huwa zina ubora zaidi kuliko za Anglophone.

Kwa kweli sijui kama alifariki mpaka jana nilipokuwa naangalia sherehe za Academy Awards (Oscars). Katika kumbukumbu ya waliofariki mwaka uliyopita alikuwemo. Mbona nilishutuka.

Sembene Ousamane alifariki nyumbani kwake Dakar, Senegal, mwezi Juni mwaka jana. Alikuwa na miaka 84.

REPOSE EN PAIX - REST IN PEACE

Jambo Forums Is back online!

Kuna habari njema. Jambo Forums imerudi hewani. Ilikuwa imefungwa kwa muda na baadhi ya posters wake walihojiwa na polisi nchini Tanzania.

http://www.jamboforums.com/

Nafasi za Kazi Tanzania - Wizara ya Mambo ya Nje



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFATANGAZO LA NAFASI ZA KAZI


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa anapenda kuwatangazia Watanzania wenye sifa kutoka Bara na Visiwani, kuomba kazi zilizotangazwa hapa chini. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inazingatia usawa wa kijinsia katika kutoa ajira. Hivyo Wanawake wenye sifa wanahimizwa kuomba.Nafasi zinazotangazwa ni kama ifuatavyo:-


1. AFISA MAMBO YA NJE MKUU DARAJA LA I,TGS H(NAFASI 2)


KAZI ZA KUFANYA:


i) Kusimamia utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje kwa kutilia maanani masuala yaliyopewa kipaumbele katika kukuza na kuimarisha uchumi wa Taifa.ii) Kufanya tathmini za utekelezaji wa Sera mbalimbali za kiuchumi na kutoa ushauri na mapendekezo ya utekelezaji wake.iii) Kuratibu Wizara na Taasisi mbalimbali kutekeleza majukumu/makubaliano yaliyokubalika Kikanda na Kitaifa (Regional and International Cooperation) kwa wakati uliokubalika.

SIFA ZA MWOMBAJI:


i. Awe na shahada ya Uzamili (Masters) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapoya fani zifuatazo:a. Uhusiano wa Kimataifa;b. Public Policy;c. Uchumi;d. Biashara ya Kimataifa; nae. Sheria ya Kimataifa.ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta pamoja na uzoefuwa kazi kwa muda usiopungua miaka kumi na mbili

(12).SIFA ZA ZIADA:Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kamavile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani,Kihispania na Kiarabu.


2. AFISA MAMBO YA NJE MWANDAMIZO, TGS F(NAFASI 1)

KAZI ZA KUFANYA:1. Kuhudhuria mikutano ya Kimataifa.2. Kutafiti na kuchambua taarifa mbalimbali.3. Kuratibu njia za wageni toka nje zinazopitia Anga zaNchi yetu au kutua nchini.4. Kuratibu mabaraza ya pamoja ya ushirikiano baina yanchi yetu na Mataifa ya nje.5. Usaili katika ngazi za Kiwaziri na Kibalozi.SIFA ZA MWOMBAJI:i. Awe na shahada ya Uzamili (Masters) kutoka VyuoVikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapoya fani zifuatazo:a. Uhusiano wa Kimataifa;b. Public Policy;c. Uchumi;d. Biashara ya Kimataifa; nae. Sheria ya Kimataifa.ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta pamoja na uzoefu wa kazi kwa muda usiopungua miaka saba (7).

SIFA ZA ZIADA:Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani,Kihispania na Kiarabu.


3. AFISA MAMBO YA NJE DARAJA LA II, TGS D(NAFASI 8)

KAZI ZA KUFANYA:i. Kuandaa Muhtasari, nakala na taarifa zinazohusu masuala ya mahusiano ya Kimataifa.ii. Kuhudhuria mikutano mbalimbali.iii. Kuandaa mahojiano.iv. Kufuatilia masuala mbalimbali ya kimataifa.v. Kufanya utafiti juu ya masuala mbalimbaliyanayohusu uchumi, siasa na jamii.vi. Kutunza kumbukumbu za matukio mbalimbali.

SIFA ZA MWOMBAJI:i. Awe na shahada ya Sanaa (B.A.) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serkali, na ambaye amejiimarisha (major) katika mojawapo ya fanizifuatazo:a. Uhusiano wa Kimataifa;b. Uchumi; nac. Sheriaii. Awe amefanya na kufaulu mtihani unaotolewa na Chuo cha Diplomasia, Dar es Salaam.iii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.SIFA ZA ZIADA:i) Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani, Kihispania na Kiarabu.ii) Mwenye Shahada/Stashahada ya Uzamili (Masters/Postgraduate Diploma) kutoka VyuoVikuu vinavyotambuliwa na Serikali katikamojawapo ya fani zifuatazo:i. Uhusiano wa Kimataifa;ii. Public Policy;iii. Uchumi;iv. Biashara ya Kimataifa; nav. Sheria ya Kimataifa


4. AFISA TAWALA MWANDAMIZI, TGS F (NAFASI 7)

KAZI ZA KUFANYA:i. Kuandaa bajeti ya matumizi ya Wizara.ii. Kuratibu na kuhifadhi kumbukumbu za matukio muhimu katika Wizara.iii. Kufanya kazi za uhusiano na itifaki Serikalini.iv. Kushughulikia masuala ya nidhamu na ufanisi wa kazi kwa watumishi wa Wizara.v. Kusimamia utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo kulingana na mahali alipo.vi. Kuandaa taarifa za utendaji na matukio mbalimbali kila mwezi.vii. Kutekeleza utaratibu wa uundwaji na utendaji wa Mabaraza ya Wafanyakazi kwa mujibu wa kanuni na taratibu.

SIFA ZA MWOMBAJI:
i. Awe mwenye Shahada/Stashahada ya Uzamili (Masters au Postgraduate Diploma) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika fanizifuatazo:-a. Utawala;b. Elimu ya Jamii;c. Sheria (baada ya internship);d. Menejiment Umma; nae. Uchumiii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta pamoja na uzoefu wa kazi kwa muda usiopungua miaka saba (7). Aidha, maafisa tawala wakaoajiriwa katika cheo hiki watatakiwa kufanya au kufaulu mtihani wa maafisa tawala katika kipindi cha miaka miwili tangu waajiriwe.

SIFA ZA ZIADA:Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani,Kihispania na Kiarabu.


4. KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III, TGS B (NAFASI 2)

KAZI ZA KUFANYA:i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida.ii. Kupokea wageni na kuwasaidia shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapowezakushughulikiwa.iii. Kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi, na kumuarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitajika.iv. Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kaziWizarani.v. Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.vi. Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio katika sehemu alipo, na kukusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.

SIFA ZA MWOMBAJI:i. Awe amehitimu Kidato cha Nne (IV) na kuhudhuria Mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa Hatua ya Tatu.ii. Awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na awe amepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika programu za windows, Microsoft Office, Internet, E-mail na Publisher.

SIFA ZA ZIADA:Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani,Kihispania na Kiarabu.MASHARTI YA WAOMBAJI WOTE:1. Maombi yaandikwe kwa mkono na kuambatanishwa nakala za vyeti vya Shule, Vyuo, Vyuo Vikuu (Certificat and transcript) na kozi ulizohudhuria.2. Wasifu binafsi wa mwombaji (CV) pamoja na picha moja ya pasipoti ya siku za karibuni.3. Kwa wale wote walioajiriwa maombi yao ya kazi ni lazima yapitishwe kwa waajiri wao.4.


Waombaji wawe na umri kati ya miaka 18 na 45.5. Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi yote ni Februari 29, 2008.Maombi yote yatumwe kwa anuani ifuatayo:

Katibu Mkuu,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
S.L.P. 9000
DAR ES SALAAM.

Friday, February 22, 2008

Uzinduzi Rasmi - Bongoland II





Moja kwa moja kutoka mjini Dar-Es-Salaam, tunafurahi kutangaza siku ya uzinduzi maalumu wa sinema ya Bongoland II. Tarehe ya uzinduzi ni mwezi April 5, 2008 hapa mjini Minnepolis, Minnesota katika ukumbi wa sinema wa Oakstreet Cinema.

Sinema hii ilitengenezwa mwaka jana July pale mjini Dar. Vitongoji maarufu vya mji huo kama Manzese na Magomeni vilitumika katika utengenezaji wa sinema hii. Kusema kweli, hii itakuwa ni hadhi kubwa ya wasanii wa ki-Tanzania maana sinema hii itaonyeshwa katika tamasha mbali mbali za sinema za kimataifa.
Sinema hii ni inamhusu Juma Pondamali ambaye baada ya maisha na malengo yake kutofanikiwa nchini Marekani, aliamua kurudi nyumbani. Lakini visakato alivyovikuta nyumbani vilimshangaza sana na hakuna kitu chochote hapa ulimwenguni ambacho kingemtayarisha kupambana na visakato hivyo.ANGALIA TRELA MPYA

Jitayarishe kuwaona wacheza sinema wakongwe wa Tanzania kama Mzee Kipara, Bi Chuma Selemani Mzee na Bi Thecla Mjatta. Vile vile pia kuwaona wachezaji chipukizi kutoka mjini Dar-es-salaam.
Msanii mhusika mkuu ni Peter Omari ambaye anacheza kama Juma. Peter, ambaye kwa sasa anishi Mwanza, aliwahi kucheza katika sinema yetu iliyopita iliyoitwa TUSAMEHE.

Thursday, February 21, 2008

Trailer Mpya - Bongoland II




Premiere ya sinema, Bongoland II, itakuwa Minneapolis, Minnesota.

April 5th, 2008 2:00PM & 5:00PM at the Oak Street Sinema, 308 Oak Street.

Haya Chapeni Kazi sasa!

Now that President Bush has left Tanzania the new government Ministers must get back to work!

Mke wangu Mpendwa!

Mzungu na mke wake (1905)

Hii picha pia iko kwenye collection ya Northwestern University, lakini hawajui ni akina nani. Imepigwa Tanganyika enzi za Mjerumani.

Machifu Wetu walivyonyongwa!

Wangoni Chiefs
Walivyonyongwa!
Hii picha ya machifu wetu kunyongwa iko kwenye maktaba ya Northwestern University hapa Marekani! Mjerumani alikuwa MSHENZI!

Update - Jambo Forums


JAMBO FORUMS


Jioni ya leo (February 20, 2008) kwenye kipindi cha BBC mara baada ya Mwanakijiji kuhojiwa, alifuatia Msemaji wa Jeshi la Polisi ambaye alijaribu kuelezea ni kwa nini vijana wawili wanashikiliwa na Polisi kwa sababu ya kuhusika na mtandao wa Jambo Forums. Katika madai ya jeshi hilo ni kuwa mtandao huo siyo tu ni wa uchochezi bali pia unamawazo ya kigaidi au uvunjaji mwingine wa sheria.

Tafadhali ingia kwenye "Pics and Docs" kwenye "Press Releases" na kujisomea tamko hilo pamoja na makala iliyowatambulisha watu wengi kwenye Jambo Forums iliyotolewa karibu mwaka mmoja uliopita na kuwekwa hapa bila ya kufanyiwa uhariri wowote au mabadiliko.
Wakati huo huo tunaitisha michango ya wana JF katika kuwasaidia ndugu zetu. Wengine tumetoa muda wetu, watu wawili tu wamechangia fedha kidogo na wengine wanaendelea kutoa michango ya "maneno ya kizalendo" na mshikamano.

Tunahitaji michango ya kuhakikisha siyo tu JF inarudi bali inarudi ikiwa na nguvu zaidi lakini pia kusaidia juhudi za ndugu zetu nyumbani. Endapo vijana hawa watafunguliwa mashtaka tunahitaji kuwa na "Legal Defence Fund".

Michango inaweza kuingizwa kupitia tovuti hii au kwa kuwasilina na klhnews@klhnews.com This e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it .
Mwisho tunaomba kuwahakikishia kuwa Jambo Forums iko salama kabisa na kila kitu kilichokuwapo bado kipo na muda si mrefu itarudi hewani.

Ndugu yetu "Invisible" anaendelea kufanya vitu vyake bila kubughudhiwa na matukio yanayoendelea.

First Ladies

American First Lady Laura Bush walks down the red carpet with her Tanzanian Counterpart First Lady, Salma Kikwete during the recent visit of President Bush to Tanzania. (Photo courtesy of Mpoki Bukuku).

Sasa jamani, hiyo khanga ilivyokunjwa. Picha ya Bush imefichwa lakini maneno WE CHERISH DEMOCRACY ni prominent. Hivi aliamua kuikunja hivyo kusudi picha ya Bushi isionenekane? Hapa Marekani watu walikuwa wanacheka kweli hizo khanga wanasema picha ya Bush iko kwenye butts (matako) na bosoms (vifua) vya wanawake wa kiafrika. Hawaelewi utamduni wetu wa khanga.

Wednesday, February 20, 2008

President Bush in Arusha, Tanzania



Mwone President Bush akijaribu kucheza ngoma ya waMasai!!

Uwe Mwangalifu ukipanda Teksi Dar

Nimepokea hii kwa e-mail:

*****************************
Dear,
Here comes another safety alert for everybody.

I think the message is clear and what me and you are supposed to do is
to share to as many people as possible.

Remember:
* Take the reg. number once you board a taxi,
* Inform your colleague/relative of the taxi particulars and the route,
* Let the driver understand that you have informed somebody else about
the route.
The story start-

A close friend of mine has told me of what happened to his wife on
Tuesday 12th February 2008!

She drew from Bank House ATM Tshs. 300,000/= and she was heading to
Regency Hospital. She went for a taxi at Old Post Office, during the
course of bargaining for price with the first Taxi driver, another Taxi
pulled around and the driver asked where this woman was heading to. He
was told and agreed to take her after dropping the other passenger as
they were heading the same route.

She was surprised when she saw the taxi going along Ally Hassan Mwinyi
road even After they passed Salender Bridge, on asking she was told that
they were going to drop the other passenger at Oyster bay and thus they
took Kenyatta Drive. As the drive way was clear this taxi was traveling
at a reasonably high speed when they asked her for the Phones and the
money she withdrew from the ATM of which she gave them.

When they were approaching Masaki the Taxi slowed down due to the number
of vehicle in the drive way. She took this chance to scream for help;
the guys were not amused, they opened the car and pushed her out and
sped off.

The good Samaritans and the onlookers went for the rescue; she was safe
then and they told her she was luck to be dropped un hurt as the average
number of such victims, most of them injured is about 10 to 12 per day;
all of them claiming to have hired taxis from Posta or city centre.

"Please let it be known to others and be careful with Taxis in town! Let
you friends know, let members know so are your neighbors"

Regards-

Mwigizaji wa Bongo - Emmanuel Myamba

(kutoka kushoto, Emmuel Myamba, Mimi, Steven Kanumba)

Hii picha nilipiaga mwezi wa saba mwaka jana Bongo. Tulikuwa Magomeni, Dar es Salaam kwenye shoot ya filamu Bongoland II siku ya kwanza. Bongo Superstars Steven Kanumba na Emmanuel Myamba walikuja kututembelea kwenye seti. Sikujua kuwa huyo Emmanuel naye ni actor alielekea mpole kweli.

Nimebahatika kuona sinema ya Fake Pastors. Mle Emmanuel anaigiza kama Evangelist wa kanisa. Kwa kweli ana kipaji cha kuigiza yaani kama kuna tuzo ya Best Supporting Actor Bongo, anastahili yeye. Anaigiza vizuri mno mpaka wewe mtazamaji unasema unataka kumwona zaidi na zaidi. Unaamini kabisa kuwa huyo ni Evangelist anayependa kanisa lake, dini yake na waumini wake. Haonekani kama anaigiza hata kidogo. Natabiri ataenda mbali sana katika fani ya uigizaji na si Bongo tu hata nje ya nchi. Sinema ya Fake Pastors ina kasoro zake lakini huyo jamaa ni nyota!

Jifunza Kuongea Ki-Boston!


Nimepata kwenye e-mail:


Welcome to Bawstin (Boston )


For those of you who have never been to "Bawstin", this is a good guideline. I hope you will consider coming to "Beantown" in the near future. For those who call New England home, this is just plain great!

Information on Boston and the surrounding area:

There's no school on School Street , no court on Court Street, no dock on Dock Square , no water on Water Street . Back Bay streets are in alphabetical "oddah": Arlington , Berkeley ,Clarendon, Dartmouth , etc. So are South Boston streets: A, B, C, D, etc. If the streets are named after trees (e.g. Walnut, Chestnut, Cedar), you're on Beacon Hill . If they're named after poets, you're in Wellesley .
Massachusetts Avenue is Mass Ave ; Commonwealth Avenue is Comm Ave ;
South Boston is Southie. The South End is the South End.
East Boston is Eastie. The North End is east of the former West End . The West End and Scollay Square are no more; a guy named Rappaport got rid of them one night. Roxbury is The Burry, Jamaica Plain is J.P.
Definitions:
Frappes have ice cream, milkshakes don't.
If it is fizzy and flavored, it's tonic.
Soda is CLUB SODA.
"Pop" is DAD.
When we want Tonic WATER, we will ask for TONIC WATER.
The smallest beer is a pint.
Scrod is whatever they tell you it is, usually fish. If you paid more than $7/pound, you got scrod.
It's not a water fountain; it's a bubblah.
It's not a trashcan; it's a barrel.

It's not a shopping cart; it's a carriage.
It's not a purse; it's a pock-a-book.
They're not franks; they're haht dahgs; Franks are money in Switzahland.

Police don't drive patrol units or black and whites they drive a "crooza". If you take the bus, your on the "looza crooza". It's not a r ubber band, it's an elastic. It's not a traffic circle, it's a rotary. "Going to the islands" means Martha's Vineyard & Nantucket.

The Sox = The Red Sox
The C's = The Celtics
The B's = The Bruins
The Pat's =The Patriots

How to say these Massachusetts city names correctly:
**Say it wrong, be shunned**
Worcester: Wuhsta (or Wistah)
Gloucester : Glawsta
Leicester: Lesta
Woburn : Wooban
Dedham : Dead-um
Revere : Re-vee-ah
Quincy : Quinzee
Tewksbury : Tooks berry
Leominster : Lemin-sta
Peabody : Pee-ba-dee
Waltham : Walth-ham
Chatham : Chaddum
Samoset: Sam-oh-set or Sum-aw-set but nevah Summerset!


Things not to do:

Don't pahk your cah in Hahvid Yahd .. they'll tow it to Meffa ( Medford ) or Summahville (Somerville).
Don't sleep on the Common. (Boston Common)
Don't wear Orange in Southie on St. Patrick's Day.

Things you should know:
There are two State Houses, two City Halls, two courthouses, two Hancock buildings
(one old, one new for each).

The colored lights on top the old Hancock tell the weatha':
"Solid blue, clear view...."
"Flashing blue, clouds due...."
"Solid red, rain ahead...."
"Flashing red, snow instead...." - except in summer;
flashing red means the Red Sox game was rained out!
Most people live here all their life and still don't know what the hell is going on with this one.
Route 128 is I-95 south. It's also I-93 north.
The underground train is not a subway. It's the "T", and it doesn't run all night (this ain't Noo Yawk).
Order the "cold tea" in China Town after 2:00 am you'll get a kettle full of beer.

Bostonians... think that it's their God-given right to cut off someone in traffic.
Bostonians...think that there are only 25 letters in the alphabet (no R's) except in "idea".
Bostonians...think that three straight days of 90+ temperatures is a heat wave.
Bostonians...refer to six inches of snow as a "dusting."
Bostonians...always "bang a left" as soon as the light turns green, and oncoming traffic always expects it.
Bostonians...believe that using your turn signal is a sign of weakness.
Bostonians...think that 63-degree ocean water is warm.
Bostonians...think Rhode Island accents are annoying.

Send this to your friends who don't live in Boston (and the ones who do)

Tuesday, February 19, 2008

Kipanya Anasema....

Translation-

Kipanya (rat character) is standing outside a building on Mawaziri St. (Ministers' St.)

Kipanya - Hey, Hey have you heard? He (President Bush) said that he isn't giving money to theives! Do you understand? Don't get mad at me, I am just the messenger! Hello you greedy people! Helloooo!

Voice from the building - You would think he was sent here! That creature is really annoying me!

Jambo Forums - Vipi Tena?????



Walioshikiliwa waachiwa

Written by Mwanakijiji
Tuesday, 19 February 2008

Jeshi la Polisi Mkoani Dar-es-Salaam limewaachilia vijana Mike Mushi na Mac DeMello ambao ilikuwa inawashikilia kwa zaidi ya masaa 24 yaliyopita. Vijana hao walikuwa wanashikiliwa kwa madai ambayo hadi hivi sasa hayajaeleweka lakini inadaiwa kuhusiana na mtandao maarufu wa Jambo Forums. Muda mfupi uliopita email kutoka kwa mtu anayejiita Melo imetuma ujumbe kwa klhnews ikisema kuwa

" Kaka unayafanya maisha yangu kuwa hatarini SANA. Sina simu ningekupigia. Tafadhali SANA futa haraka habari hiyo inayotuhusu kwakuwa itaharibu kila kitu na kunifanya nitoweke kwenye uso wa dunia. Mapambano niliyaona yenye haja lakini sasa hali NI MBAYA SANA. Wasiliana na mwenzio....... akwambie nini kimempata. NAKUOMBA SANA leave us for this moment, unawarahishia upelelezi wenzio!
Bora kuendeleza mijadala mingine kuliko hivi, kaka balaa kwangu!"

Hata hivyo haieleweki ni kwanini kama kweli email hii ni ya vijana hao wanakuwa na wasiwasi hata wa "kutoweka duniani" wakiwa chini ya vyombo vya usalama. Msimamo wa KLH News ni kuwa jambo lolote likiwatokea vijana hao hata kujikwaa au kuvunjika ukucha wakiwa mikononi mwa Polisi watakaowajibika mbele za wananchi ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Tanzania na Inspekta Jenerali wa Polisi kwa kushindwa kulinda usalama na uhaki wa vijana hao.

Tunaendelea kutoa wito kwa vyombo husika kwenda kutafuta majambazi na wezi wa fedha zetu za umma kama kina Balali ambao wanatanua ughaibuni badala ya kuwatafuta na kuwabambikizia kesi zisizo na msingi vijana ambao wanatumia vipaji vyao kuinua uhuru wa habari nchini.

Taarifa za vijana hawa kuwekwa kizuizini zinaanza kuendelewa kuandikiwa ripoti ya kuonesha ni jinsi gani Taifa lililosifiwa kuwa ni "mfano" katika Bara la Afrika limeshindwa kujizuia kuvumilia maoni huru siku chache baada ya kumpokea kwa shangwe Rais wa Marekani Bw. George Bush nchi ambayo hakuna kitu kinaenziwa sana kama uhuru wa maoni na mawazo.
*****************************************************************

Naona mambo mazito!!!

Kusoma na maoni ya watu Bofya hapa:

Rais Castro wa Cuba Ajiuzulu!

Cuban President Fidel Castro with his host Tanzanian President Julius Nyerere in Tanzania in 1978. I was there!


Rais Fidel Castro, wa Cuba amejiuzulu urais. Castro aliongoza nchi hiyo kwa miaka hamsini! Alipindiua serikali ya kibepari ya Batista siku ya mwaka mpya mwaka 1958! Castro alikuwa mgonjwa muda mrefu, hajaonekana hadharani kwa miaka miwili sasa. Kulikuwa na uzushi kuwa amefariki dunia, lakini habari hizo si kweli.

Alikuwa adui mkubwa wa Marekani shauri ya siasa zake za Communism. Mdogo wake, Raoul Castro atakuwa rais sasa.

Nakumbuka mwaka 1978, nilimwona laivu. Alikuja Dar es Salaam kumsalimia Mwalimu Nyerere. Wakati huo nasoma Zanaki secondary Form II. Tuliambiwa tukajipange pale Ikulu kumpokea. Alikuwa bado fiti wakati huo. Sasa ni mzee kabisa. Nakumbuka watu walisema eti, Castro alijialika kutembea Tanzania. Sijui walikuwa na maana gani. Tulitolewa haraka darasani na kuambiwa tuwahi Ikulu.

***********************************

Kwa habari zaidi soma:

http://www.cbsnews.com/stories/2008/02/19/world/main3843492.shtml?source=mostpop_story

http://ap.google.com/article/ALeqM5jo_74bCqDvop0iQubmaRzy42RadwD8UTE7E00

http://blogs.guardian.co.uk/politics/2008/02/so_fidel_castro_has_finally.html

Monday, February 18, 2008

Tanzanian Cartoonist Kipanya on Pres. Bush's Visit



Translation-

Patient- You've taken me from the ground and put me in a bed! What is the meaning of these niceties? Or am I about to die?!

Nurse- How are you feeling this morning?

Nurse - Would you like your eggs made into an omlette or spanish style?

Doctor - How do you feel?

Kipanya (rat character) - No you are not dying! President Bush is coming!

***********************************************************************************

Amana Hospital is known for poor treatment of patients and poor conditions overall. When President Bush visited suddenly the place was cleaned up, the staff were doing their jobs and the patients got good food to eat! Can the President visit all of the public hospitals Please!!!!

Kwa kweli Kipanya kajitahidi sana leo!

President Bush makes waves in Tanzania


President Bush is leaving a lasting impression on multitudes of Tanzanians. He has not put on airs and has even evaded his security to meet, shake hands and hug common people! It sounds like he is enjoying his trip to Tanzania immensely!

*********************************************

From ippmedia.com

Rais Bush apagawisha

2008-02-18
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Licha ya kutoka katika taifa lenye nguvu kubwa zaidi za kiuchumi duniani, Rais George W. Bush wa Marekani ameweza kujichanganya na Wabongo Jijini na kuwapagawisha maelfu ya waliofika kumpokea.

Bush, aliyewasili Jijini tangia Jumamosi jioni kwa ajili ya ziara ya kitaifa ya siku nne nchini, amefanya jambo hilo lisilokuwa la kawaida kwa marais wa taifa hilo walio madarakani na kuwashangaza hata maafisa wake wa Kikosi cha FBI.

Kwa ujumla, mambo yenyewe aliyoyafanya Rais Bush mara tu baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuwapagawisha watu ni kama haya:

Ajitosa uswazi:
Awali ya yote, alipotua pale kwenye `terminal one`, Bush alitoa mpya wakati alipositisha ghafla zoezi lake la kupungia mkono watu waliokuja kumpokea na kisha kujichanganya nao kwa muda.

Ilianza kama masihara vile, Bush alichomoka ghafla toka kwenye kapeti kali jekundu alilokuwa akipitishwa na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Jakaya Kikwete.

Kisha kwa mastaajabu ya wengi, akamuendea mama mmoja aliyekuwa miongoni mwa watu tele waliokuwa wakimpungia na kukumbatiana naye. Jambo hilo liliamsha hisia kali za furaha na nderemo.

Jana, Bush akaendelea kujichanganya `uswazi`, kunako mitaa ya Buguruni na Ilala ambako, ingawa alikuwa akilindwa vikali, aliweza kutimiza ratiba yake ya kuzindua majengo mapya katika Hospitali ya Amana, yaliyofadhiliwa na Serikali yake.
Atema Kiswahili.

Wakati alipopewa fursa ya kuzungumza pale katika viwanja vya Ikulu, ambako yeye na mwenyeji wake walikutana na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, Rais Bush alibonga Kiswahili kwa namna isiyotarajiwa.

Alikamata mic, kisha akasalimia kwa kusema `Mambo viipiii!``
``Alinishangaza. Kamwe sikujua kama Rais Bush anaweza kutusalimia kwa Kiswahili,`` amesema Bw. John Jacob, mkazi wa Manzese Jijini.

Amwaga Mapesa
Pamoja na kuwapagawisha Wabongo kwa staili ya ujio wake na mivifaa ya kisasa ya kumlinda ikiwa ni pamoja na midege na migari myeusi ya bei mbaya, Rais Bush amewaletea neema Wabongo.

Yeye na mwenyeji wake, Rais Kikwete, wamesaini mkataba utakaoiwezesha Tanzania kupata msaada wa dola za Kimarekani Milioni 698 sawa na pesa za Kitanzania bilioni 800. Haijapata kutokea!

Pesa hizo zitatumika kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na kujengea miundombinu ya barabara.

Aidha, mke wa Rais Bush, Bi. Laura Bush, amemwaga msaada wa dola za Kimarekani Milioni 43 kwa mradi unaokwenda kwa jina la `Pamoja Inawezekana`, ulio chini ya Mama Salma Kikwete, kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima nchini.

  • SOURCE: Alasiri

Sunday, February 17, 2008

President Bush Visit to Tanzania in Pics III

President Bush at Amana Hospital in Ilala District,Dar es Salaam.


President Bush waves to well wishers in Dar es Salaam

President Bush greets a patient at Amana Hospital in Ilala Districti, Dar es Salaam

President Bush is entertained by traditional dancers. This time his photo is on their chests.


President Bush waves to a crowd of wellwishers at the Tanzanian State House

President Bush speaks outside the historical Tanzanian State House

Kuna Slideshow Bofya Hapa:

*****************************************************

We Tanzanians can be proud that our country is trustworthy when it comes to donated dollars. President Bush praised Tanzania for putting the money donated to battle AIDS to work in the country and save lives.



It's the largest deal under a Bush program that offers economic aid to countries that treat their people fairly, rule justly and root out corruption.


"I'll just put it bluntly, America doesn't want to spend money on people who steal the money from the people," Bush said. "We like dealing with honest people, and compassionate people. We want our money to go to help human condition and to lift human lives as well as fighting corruption in marketplace economies."

President Bush Visit to Tanzania in Pictures II

Americans were amused to see people wearing clothes with President's Bush's picture on it. Hon. Margareth Sitta gets complemented by the President for outfit. Kitenge/Khanga for special occasions are part of Tanzanian culture.
President Bush admires the warm welcome he received the Tanzania. His host is Tanzanian President Jakaya Kikwete.
President Bush and his wife Laura greet Tanzanian officials. Behind President Bush if Tanzanian first Lady, Salma Kikwete.
USA Secretary of State Condoleeza Rice greets Honourable Sofia Simba.

The Tanzanian News media reps getting checked over by the Secret Service.


All Photos from Michuzi Blog and were taken by famous Tanzanian photojournalist, Muhidini Issa Michuzi:

President Bush Visit to Tanzania in Pictures

A Special Sniffer dog, checks out the grounds on the Julius Kambaraga Nyerere Airport in Dar es Salaam, Tanzania, East Africa.
Air Force One carrying President Bush approaches the runway of the Dar es Salaam airport.
A grand welcome awaits President Bush and his wife, Laura.
President Bush and his wife disembark from Air Force One.
President Bush and his host, Tanzanian President Jakaya Kikwete walk on the official Tanzaniana red carpet.

All Photos from Michuzi Blog and were taken by famous Tanzanian photojournalist, Muhidini Issa Michuzi: