Wednesday, July 31, 2013

Mimi Katika Sinema American Hustle

Wadau, mnaweza kuniona nyuma ya mcheza sinema maarufu, Amy Adams katika trela ya sinema mpya American Hustle.  Inatoka mwezi Desemba.  Niliigiza mwezi wa pili mwaka huu. Waliomba wacheza sinema wasio na miili ya stars kujitokeza kwa ajili ya hii scene ya party.  Nilituma picha nimevaa nguo ya kuogelea na wakanichagua. Awali ilikuwa nivae bikini lakini kutokana na urithi wa bibi (matiti makubwa) walishindwa kunipatia nguo iliyofaa.  Sehemu ya chini  ilikaa viuri lakini juu ziilikuwa ndogo hadi matiti yanamwagika!  Basi, wakanipatia hiyo one piece nyeusi na ndo nilivaa.  Ajabu siku tulivopiga sinema nilidhani kuwa sitaonekana hata kidogo.  Pia ilikuwa winter na kulikuwa na theluji na barufu nje!  Leo asubuhi, nilishangaa watu walipoanza kunipigia simu na kunitumia text kuwa wameniona.  Kumbe hiyo sehemu imeongelewa na kuonyeshwa sana kwa vile Amy Adams kavaa nguo ya kuogelea ilitengenezwa kwa mkono kwa mtindo wa macrame.  Katika sinema hiyo naonekana katika scene hii moja tu kwenye bwawa ya kuogelea kwenye nyumba ya tajiri fulani hapa Boston.  Waigizaji wote tulizuiliwa kusema kitu, yaani tumefanya nini na tumeona nini.  Tulisaini agreement za usiri.  Sasa tunaweza kusema. 



Afisa Uhamiaji Asimamishwa Kazi Kwa Kukaa Vibaya Kazini!

  http://www.arabnews.com/news/458770

JEDDAH: Saudi authorities arrested a local airport officer after social networks published a picture of the man showing him in a “rude sitting position” while checking the passports of passengers, a newspaper reported on Sunday.


The picture, which was captured by a Saudi passenger at the airport in Jeddah, showed the uniformed officer giving his back to the passengers as he sat on the desk and his legs rested on a chair.

Newspapers had earlier said the unnamed officer was suspended this week after the photograph triggered online criticism by hundreds of viewers.

“The passport officer was ordered arrested after his suspension this week ... the director of the passports department ordered his arrest for questioning about his behavior and uncivilized way of sitting,” the Arabic language daily Arar said.

.

The Saudi Immigration Sitting in a Rude Position


Monday, July 29, 2013

Lipa Dola $650 Upate Dola Milioni 10 - Utapeli

Wadau, kuna mtu  TZ kaniforwardia hii email.  Kaomba nimkopeshe dola $650, halafu tutagawana hizo $10,000,000. Pia kaomba atumie akaunti yangu ya benki hapa USA.  Jamani, kwanza mjue huna haja ya kulipa hela ili upate hela. Kwa kawaida kama wanakudai watakata kutoka hela ambayo wanakulipa! Hao matapeli wamezidi lakini wanaendelea kutapeli watu kwa vile wanajua wengi wana uchu ya kupata hela haraka!  Pia kama benki kwa nini utumie Western Union au Money Gram. Yule jamaa hataki kunisikia kasema atamtafuta mtu mwingine amsaidie! Duh! FYI - Nimekwishafanya kazi Bank of America. Hakua kitu kama wanavyodai hapo chini.

***********************************************

Bank of America Corporate Office Headquarters.

Bank of America Corporate Office Headquarters100 N.Tryon St Charlotte,NC 28255. Our Ref:BOA/IRU/SFE/15.5/WD/011United States of America. Monday-Friday 8 a.m.-9 p.m. Eastern Daylight Time (EDT) Saturday and Sunday 8 a.m.-4 p.m. Eastern Daylight Time (EDT) Tel + 1 9406041808.Dear esteemed customer,

The Management of the Bank of America Corporate Office Headquarters here In 100 N.Tryon St Charlotte, NC 28255 wishes to inform you that after a Brief meeting held by the Bank executives on, the 11th Day of June, 2013 at Precisely 8 a.m. Eastern Daylight Time (EDT), we deem it appropriate to Intimate you that your funds will be transferred into the United States Treasury Account with the JP Morgan Chase Headquarters at 270 Park Avenue In New York according to the record we got from Africa due to your Inability to complete the transaction and your failure to meet up with a Minor payment obligation.Investigations revealed that you have spent a lot on your personal earned money just to conclude the successful transfer of your funds to your nominated bank account by obtaining transfer documents as requested by the imposters, costing you a lot of money but all to no avail.

The actual transfer of your funds ($10,700,000.00) Into the government account comes up next week. This is in line with the instructions of the USA Treasurer, Mrs.Rosa Gumataotao Rios that all unclaimed funds be paid into the United States Government Treasury Account as unserviceable funds in compliance to Section 3 subsection 1(a) of the United States Financial Law enacted in 2001 after an attack on our dear country on September 11, 2001. Find below the profile of the banking institution where your funds will be Transferred into following the government directive: Name of Bank: JP Morgan Chase Headquarters at 270 Park Aveanue in New York. JP Morgan Chase Official Bankers for the United States Treasury Department AC NO: 68302345093 Routing NO: 021109593 Account Name: United States Treasury Department, USA Note that if you still wish to receive your funds do get back to us Immediately so that we will remove your funds transfer from the list of Those transactions to be seized by the United States Government.

Also be Informed that we need only a DIPLOMATIC IMMUNITY SEAL OF TRANSFER (DIST) to complete the wire transfer. The fee to obtain the SEAL was reduced From $3600 to $650 and no other fee is involved. You are required to send The fee of $650 by WESTERN UNION or MONEY GRAM to the issuing officer at The bank where your transaction originated as stated below: INFORMATION
Receivers Name:......ZUMA KABORE
Country ...Burkina Faso
City ....Ougadougou
Test Question.... Be Rest
Answer ...Assure
AMOUNT to send... $650
Sender's name...
MTCN Number....... 

If we receive the MTCN today, we will transfer your funds ($10,700,000.00) Before we close office and the funds will reflect into your bank account whithin 3 hours after the Transfer. We will send you all the transfer documents to enable you start making cash withdrawals from your account same day the funds are Transferred. We have waited for so long and we cannot Continue to wait. Thank you for giving us the opportunity to serve your banking needs.However, we are happy to inform you that based on our recommendation/Instructions; your complete funds have been credited in your favor through banking system. You are therefore advice to contact: Mrs. Patricia ADAM of Central Bank of Burkina Faso with the DIPLOMATIC IMMUNITY SEAL OF TRANSFER (DIST) fee of $650 via e-mail: stadaon@rediffmail.com

As soon as you establish a contact with him, he will process and effect the release/ transfer your fund into your account. After receiving series of other reports similar to yours as you are not the only person awaiting the legal transfer of funds from Africa.So if you wish to receive your funds through this means you're advised to contact ( Mrs. Patricia ADAM ) and provide her the following information as required below: 1. Your Full Names: 2. Physical Address 3. Your Age: 4. Occupation: 5. Telephone Numbers: 6. Country:.............
Do not hesitate to contact me with any questions at: (Tel + 1 9406041808) if you are still interested
in claming your fund.Please stop your dealing with those impostors because they are not capable of handling your approved payment fund.

Yours faithfully,
Mr.Anwarul Quaium (CEO)
Bank of America®Corporate Office Headquarters, Charlotte, N.C.
Bank of America, N.A. Member FDIC© 2011 Bank of America Corporation. All rights reserved.AR72768/DD6A66
When
Mon Jul 29, 2013 2:30am – 3:30am Eastern Time
Calendar
anw.qu1@gmail.com
Who
(Guest list has been hidden at organizer's request)
Going?   Yes - Maybe - No    more options »
****************************************

Na huyo ana dola Bilioni 9$


My Dearest,

Greetings to you my dear beloved, I am Mrs. Christy Walton a great citizen of
United States of America.

I bring to you a proposal worth $ 9,000,000,000.00(Nine Billion United State
Dollars) which i intend to use for CHARITY.

Please reply me back if you are interested, so i can provide you with further
details. Email:waltonc87@yahoo.ca


God Bless You.
Mrs. Christy Walton.

Sunday, July 28, 2013

WaTanzania 200 Wafungwa Hong Kong!

 Kutoka: http://www.v2catholic.com/johnw/2013/2013-07-21drug-mules.htm

 TANZANIAN DRUG MULES

Below is one drug mule story, the story of mules from Tanzania entering Hong Kong. Because of its location on the East coast of Africa, Tanzania is the favorite launching place for drug lords to mission their mules. The drugs they carry are mainly from Pakistan and Afghanistan....taken by boat to Tanzania ....meeting small boats along Tanzania's long coastline

In Hong Kong there are currently about 200 inmates from Tanzania. About 130 convicted and about 70 on remand (...unofficial figures..). In May-June 2013, some 50 Tanzanians were arrested in Hong Kong and China

Those convicted serve a minimum time of about 9 years if they plead guilty. They serve 21 years if they don't plead guilty (but drugs are found in their possession)

The story of these Tanzanian mules entering Hong Kong is typical of what happens around the world. Hopefully this story will be seen by many people in Africa, especially in Tanzania, and will discourage others from becoming mules. If this article stops even one person from being a mule, it is worthwhile

Here is the story, written in Swahili by a Hong Kong Tanzanian inmate, translated into English by another inmate. The story names and shames some very important people in Tanzania, including:

Iddi Azan, a leading politician who has his own blogspot, a Facebook account, and many other items when you put "iddi azzan" into www.google.com

Story ya Wazee Kusubiri Kufa

 Na Nape Nnauye

Nimestushwasana na stori ya gazeti la Mtanzania inayodai kuninukuu kuwa nimesema wazee waliopendekeza serikali tatu wanasubiri kufa!

Kwa kweli nimesikitishwa sana hata na jinsi maneno ndani yalivyopangiliwa kiasi kwamba inanipa tabu kuamini kama mhariri aliipitia hii stori ukiachilia mbali kama aliyetumwa kuja kuandika stori alikua ni "too junior".

Nawaheshimu sana wazee wangu hawa hata kama nikipishana nao kimawazo siwezi kufikia kutamka maneno makali kiasi hicho.

Nilichosema ni kuwa ukilinganisha vijana na wazee, vijana wanawajibu mkubwa wa kuamua kesho yao badala ya kudhani kuna mtu atawaamulia. Hivyo wanawajibu mkubwa kwani takwimu zinaonyesha asilimia 60% ya idadi ya watu nchini ni vijana! Sasa sijui kama kwa mwandishi na mhariri wake tafsiri ndio hiyo?!!!
Imenisikitishasana!

Nape Moses Nnauye
The CCM Secretary for Ideology & Publicity

Mh. Nape Nnauye

Friday, July 26, 2013

Wanaume wa KiTanzania Wakamatwa na Unga Hong Kong!

Jamani, WaTanzania kwa kutafuta pesa za haraka! Sasa hao midume miwili inaweza kunfungwa maisha huko Hong Kong shauri ya kukamtwa na Unga! Mnachafua jina la Taifa yetu na kusabisha wasafiri wenzio kupata shida zisizo na maana safirini!

*************************
Asante sana Dada Subi kwa Taarifa hii:
Picture
Hong Kong Customs yesterday (July 25) detected three drug trafficking cases, with seizures totally valued at $4.78 million, in the department's escalated anti-narcotics efforts to combat drugs.

Customs officers at the Hong Kong International Airport (HKIA) intercepted a 26-year-old incoming male passenger arriving from Tanzania for clearance yesterday afternoon and seized 1.6 kilogrammes of heroin concealed in two false compartments of his hand carry briefcase. The drugs would fetch a value of about $1.28 million.

Later in the evening, Customs officers at the HKIA intercepted another 45-year-old man from Tanzania for clearance. On suspicion of concealment of drugs inside his body, the suspect was escorted to hospital where he discharged 204 grammes of heroin after staying for one day. The value of the drugs was about $0.16 million. The suspect is still in the hospital.

In the same evening, Customs officers intercepted a 28-year-old man at a carpark in Tai Kok Tsui. Approximately 2.03 kg of cocaine camouflaged as snacks were found inside a plastic bag carried by him.

Customs officers later escorted the suspect to a domestic flat nearby for a search and seized 1 kg of cocaine and 290 grammes of crack cocaine there. The total value of the seizure was about $3.34 million.

A Customs spokesperson said today (July 26) that all three suspects in the three cases were arrested for drug trafficking. The cases are still under investigation.

Under the Dangerous Drugs Ordinance, drug trafficking is a serious offence. The maximum penalty is life imprisonment and a fine of $5 million.

Ends/Friday, July 26, 2013
Issued at HKT 23:43



KUTOKA: http://www.wavuti.com/4/post/2013/07/mwingine-tena-male-passenger-from-tanzania-detained-in-hong-kong-with-heroin.html#ixzz2aBYuEnAK


Onyo Kwa Wanapoenda Kusuka Mwenge

Nimetoa hii onyo Facebook. Sijui kama kuna ukweli ndani yake lakini miaka ya 1980's kitu kama kii ilitokea Manzese.


Thursday, July 25, 2013

Vazi la Nusu Uchi Lazuia Ndoa Kufungwa Kanisani St. Peter Dar!

Binafsi sioni shida ya kuvaa nguo ya harusi ya mabega wazi, ndo fesheni sehemu nyingi. Mbona, tunavaa khanga na vitenge na tunakuwa mabega wazi? Lakini kama umeambiwa mapema kuwa nguo hiyo haifai kanisani basi msikilize Padri au tafuta Kanisa lingine!

***************************************
KUTOKA  GAZETI LA HABARI LEO

VAZI LA NUSU UCHI LAZUIA NDOA KUFUNGWA JIJINI DAR....PADRI AGEUKA MBOGO NA KUWATIMUA WAPAMBE


KIVAZI cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa  Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri.

*“Ninatoa dakika 10 kwa aliyeingia na mavazi ambayo hayatakiwi kanisani humu kutoka mara moja akavae vizuri, la sivyo ndoa yao haitafungwa,”* alisema Padri Haule wa Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

Awali vurugu hizo zilizotokea Jumamosi iliyopita, zilianzia nje, wakati Katekista wa Parokia hiyo, Yohane Maboko, alipotangazia wanandoa na ndugu zao waliokuwa mabega wazi au kuvaa nguo fupi, kutafuta nguo za kujifunika au wasiingie kabisa kanisani.

Maharusi walikubali kutekeleza ombi hilo, wakavishwa vitambaa mabegani vya rangi tofauti na gauni jeupe la harusi, wakaruhusiwa kuingia kanisani, tayari kufunga pingu zao za maisha.


Aliyegoma kutoka na nguo yake ya nusu uchi

Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa maharusi hao ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alipotaka kulazimisha kuingia na kivazi chake cha mabega wazi, alizuiwa na Katekista Maboko. Katekista huyo alimfuata mwanamke huyo ili kumrudisha akavae vizuri, lakini aliibua zogo na kulazimisha kuingia na
vazi hilo.

Zogo hilo lilipoendelea, wanandugu waliingilia kati, wakitetea vazi hilo ambapo mmoja wa wanandugu, alimvua miwani Katekista Maboko na kuipiga chini ikavunjika huku yeye na wenzake wakimtolea maneno makali ya kumtaka asimzuie ndugu yao kuingia kanisani.

Wakati ndugu hao wakimdhibiti Katekista Maboko, mwanamke huyo alitumia mwanya huo na kupenya hadi ndani ya Kanisa, ambamo Padri Haule, alikuwa akijiandaa kuanza ibada.

*Baada ya Padri Haule kupata taarifa, alitangaza kuwa ndoa ya maharusi wa msichana huyo, haitafungwa hadi awe ametoka. *

Licha ya Paroko kutangaza hivyo, bado ukaidi uliendelea jambo lililomfanya Katekista Maboko kumfuata tena dada huyo na kumwamuru atoke nje, ambapo aliendelea kupinga na baadaye akatekeleza amri hiyo ya Paroko.

Baada ya hapo shughuli za kufungisha ndoa ziliendelea kwa amani na utulivu hadi mwisho maharusi wakatoka kwenda kuendelea na mambo mengine.

Akizungumza na mwandishi wetu, Katekista Maboko alisema waumini hao walikiuka maadili ambayo Kanisa lina wajibu wa kulinda na kuyasimamia ili  waumini wake wayafuate.

Alisema miwani yake iliyovunjwa ilikuwa na thamani ya Sh 90,000 na baada ya  ibada hiyo, aliyetenda kosa hilo alimwendea na kumwomba radhi na kulipa Sh 50,000 na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki wakati wowote.

Maboko alisema uvaaji wa mavazi yasiyotakiwa kanisani hapo, umekuwa ukipigiwa kelele mara kwa mara, na hata katika mafundisho ya ndoa huambiwa lakini ukaidi unaendelea.

*“Maharusi wakati wa mafundisho ya ndoa tunawaambia kuhusu mavazi yao na hata ya ndugu zao watakaowasindikiza kanisani, kuwa wavae kistaarabu lakini  hawasikii,”* alisema Katekista Maboko.

Makanisa mengi siku hizi yamekuwa yakipiga marufuku uvaaji wa nguo fupi na  zinazoacha mabega wazi kwa wasichana na wanawake, wakati wa ibada za kawaida na za ndoa.

Habari Leo

Hii fesheni inapendwa na vijana wengi

Wednesday, July 24, 2013

Rais Kikwete Awasili Bukoba Kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Sita

RAIS KIKWETE AWASILI BUKOBA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU SITA
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. Fabia Massawe baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita mkoani humo
 Rais Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman ambaye pia yuko mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi
 Rais Kikwete akisalimiana na Mstahiki Meya wa Bukoba Mhe Anatory Amani
 Vijana wa Skauti wa Bukoba wakimlaki Rais Kikwete uwanjani hapo
 Wanahabari toka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini
 Kijana wa Skauti akipiga saluti kuomba kumvisha skafu Rais Kikwete
 Rais Kikwete akivishwa skafu
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli. Kushoto ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi na wananchi waliofika uwanjani kumlaki
 Rais Kikwete akisalimiana na Mkuu wa JKT
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi wa dini mbalimbali waliokuwepo uwanjani
 Rais Kikwete akiangalia ngoma za utamaduni
 Ngoma ya Kihaya ikimlaki Rais Kikwete Bukoba
 Karibu Bukoba mheshimiwa Rais....
 Sehemu ya viongozi waliohudhuria sherehe ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 Viongozi wa dini wakiwa bega kwa bega kwenye sherehe hizo
 Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akimkaribisha Rais Kikwete kuongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 Rais Kikwete akiongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akipata maelezo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya kuweka  jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe na Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe Peter Serukamba wakishangilia wakati Rais Kikwete akiweka jiwe la msingi
 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau baada ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Rais Kikwete akisalimiana na Mhashamu Methodius Kilaini, Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba
 Sehemu ya uwanja wa ndege wa Bukoba unaokarabatiwa na kupanuliwa
 Rais Kikwete akiwasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akisalimiana na wanachama wa KCU alipowasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akisalimiana na wananchi waliofurika kushuhudia ufunguzi wa  jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akiendelea kusalimia wananchi
Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu  akimkaribisha Rais Kikwete Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Sehemu ya umati wa wananchi kwenye ufunguzi wa jengo hilo
 Jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akipokea risala toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu 
 Rais Kikwete akipokea zawadi ya kahawa toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu 
 Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya Kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akikata utepe Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akihutubia wananchi baada ya Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Wananchi wakimsikiliza Rais Kikwete
 Rais Kikwete akihutubia
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wa KCU baada ya kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
---------------------------------------------------------------
Ndugu Wananchi, kama ambavyo nimewahi kuwajulisha mara nyingi kupitia vyombo vyetu vya habari juu ya Mkoa wetu wa Kagera kupewa heshima kubwa ya kuandaa maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kitaifa mwaka 2013, leo napenda kuwajulisha juu ya maandalizi ya maadhimisho hayo ambayo yataadhimishwa tarehe 25/07/2013 hapa mkoani kwetu katika Wilaya ya Muleba katika Kambi ya Jeshi la Wananchi Kaboya. Pia nawajulisha kuwa maadhimisho hayo yataambatana na ziara ya kikazi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkoa wa Kagera.

MAADHIMISHO YA MASHUJAA MWAKA 2013
Ndugu Wananchi, Maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kumbumbu ya Mashujaa mkoani Kagera yanaendelea vizuri kamati mbalimbali za maandalizi zinatekeleza majukumu yake ya mwisho ili kufanikisha maadhimisho siku ya Alhamisi ya wiki hii tarehe 25 Julai, 2013. Kamati zinazoandaa maadhimisho hayo ni Kamati ya Mapokezi, Usafiri na Malazi; Kamati ya Ujenzi Uwanja na Mapambo; Kamati ya Chakula na Afya; Kamati ya Ulinzi na Usalama; na Kamati ya Burudani, Habari na Uhamasishaji.

Ndugu wananchi, Kwa kiwango kikubwa maandalizi yote yamekamilika na tunatarajia kuanzia leo kupokea wageni kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya mkoa, pia nje ya nchi watakaohudhuria maadhimisho hayo.
Mkoa wetu umejipanga vizuri kuwapokea wageni wote watakofika mkoani hapa kwa ukarimu na bashasha kubwa.

Wajibu wa Wananchi
Ndugu wananchi, Napenda kutumia fursa hii kuwaomba kuwa wakarimu kwa wageni wetu wote tunaowatarajia kuanzia leo kwa kutekeleza majukumu yenu kama Wanakagera kama ifuatavyo;
Ø Kila mwananchi kuhakikisha maeneo yake na mazingira yanayomzunguka yanaendelea kuwa katika hali ya usafi kama utamaduni wetu. Pia kumwajibisha mtu yeyote atakaeonekana anachafua mazingira yetu. Hili ni jukumu la kila mwananchi.
Ø Kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha Siku yenyewe ya Kumbukumbu ya Mashujaa tarehe 25 Julai, 2013 huko Kaboya Wilayani Muleba. Kwani hatuna budi kuwakumbuka Mashujaa wetu kwa sababu ya historia ya mkoa wetu kushiriki katika vita ya kumwondoa adui aliyekuwa amevamia nchi yetu kupitia ardhi ya mkoa huu mwaka 1978 hadi 1979.
Ø Kila mwananchi kuhakikisha anaitunza amani na utulivu kama destuli ya mkoa wetu kwa wakati wote wageni wetu watakapokuwepo hapa mkoani na baada ya maadhimisho ya Mashujaa. Aidha, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha amani na utulivu vinatawala wakati wote. Kwa mwananchi yeyote atakayeona viashiria vya uvunjifu wa amani atoe taarifa mara moja ili taarifa hizo zifanyiwe kazi mara moja.

Wajibu wa Vyombo vya Habari
Ndugu Wananchi, Vyombo vyetu vya habari vina wajibu wa kuhakikisha vinaendelea kutoa taarifa mbalimbali kwa wananchi kuhusu Maadhimisho ya Mashujaa kama ambavyo vimekuwa vikifanya kuanzia mwezi Mei, 2013.

Aidha, nawaombeni Waandishi, Wahariri na Wamiliki wa vyombo vya habari kutumia fursa hii kuutangaza mkoa wetu wa Kagera katika sekta mbalimbali za uwekezaji na fursa mbalimbali zinazopatikana katika mkoa wetu.
Vilevile nawaombeni Wamiliki wa vyombo vya habari hasa redio zetu za jamii kutoa muda wa kutosha katika vituo vyenu vya redio kurusha habari na matukio ya Kumbukumbu za Mashujaa papo kwa papo (live coverage) siku ya maadhimisho ili wananchi ambao hawatapata muda wa kufika Kaboya wazipate habari hizo kupitia redio zetu za Jamii.

ZIARA YA MHE. RAIS MKOANI KAGERA
Ndugu Wananchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye atakayekuwa mgeni Rasmi Katika Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa tarehe 25 Julai, 2013. Pia Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kufanya ziara ya kikazi katika mkoa wetu wa Kagera.
Ndugu Wananchi, Katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais Kikwete anatarajia kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa wetu kama ifuatavyo:
§ Kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
§ Kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Kagoma - Rusahunga
§ Kuweka jiwe la msingi barabara ya kiwango cha lami Kyaka hadi Bugene
§ Kufungua Jengo la Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba.
§ Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
§ Kuzindua mradi wa maji Muleba
§ Kuzindua kivuko kipya Rusumo (Ngara)
§ Kuzindua mradi wa usambazaji umeme vijijini Nyaishozi (Karagwe)
§ Kuzindua Wilaya Mpya ya Kyerwa
Ndugu Wananchi, Vilevile Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ataongea na wananchi kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara katika Wilaya zetu ndani ya mkoa.
Ndugu Wananchi, nawaombeni kujitokeza kuanzia tarehe 24/07/2013 uwanja wa ndege wa Bukoba ili kumpokea Mheshimiwa Rais, pia atakapokuwa anafanya ziara katika Wilaya zetu tujitokeze kwa wingi kumsikiliza. 
Mwisho; Nawatakia ushiriki mzuri katika kuadhimisha Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa na mapokezi mazuri ya wageni wetu hasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Kagera: Amani na Maendeleo. 
Amani na Maendeleo; Kagera.

Imetolewa na: Kanali Mstaafu Fabian I. Massawe
Mkuu wa Mkoa
KAGERA