Wednesday, February 29, 2012

Mzee George Mbowe Afariki Dunia



Marehemu Mr. George Frederick Mbowe
1935-2012
  Familia ya George Mbowe wa Msasani, Dar es Salaam, wanasikitika kutangaza kifo cha mpenswa wao, Mzee George Frederick Mbowe, kilichotokea usiku wa kuamkia leo jumatano 29/2/12 nyumbani kwake.

Mipango ya mazishi inafanyika nymbani kwa marehemu Plot. No. 94, Msasani, Old Bagamoyo Road karibu na nyumbani kwa Rais Mstaafu , Ali Hassan Mwinyi.

Misa ya kumuage marehemu itafanyika Ijumaa saa nane mchana katika kanisa la Anglican St. Alban.  Heshima za mwisho zitatolewa pia nyumbani siku ya Ijumaa saa 12 jioni.

Mazishi yatafayika Dodoma siku ya jumapili saa kumi jioni.

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA MBINGUNI. AMEN.

***************************

Binafsi, ninatoa pole sana kwa familia ya Mzee Mbowe. Alikuwa rafiki wa familia yetu miaka mingi, alisoma na baba yangu.  Mara nyingi tulienda kwenye shughuli mbalimbali nyumbani kwake na pia alikuja nyumbani kwetu mara nyingi kwenye shughuli.  Mzee Mbowe alikuwa haachi kutabasamu.


Mara la mwisho nilikutana naye kanisani St. Albans mwaka 2009. Alikuwa amepata ugonjwa wa kupooza (stroke) na kuongea ilikuwa shida kwake. Hata hivyo bado aliweza kutabasamu na kuniambia jinsi aliovyofurahi kuniona baada ya ya miaka mingi. 


May Mzee Mbowe Rest in Eternal Peace. Amen.

Saturday, February 25, 2012

Kuna GAS Pwani Ya Tanzania!!!

HOUSTON—Exxon Mobil Corp. and Norway's Statoil ASA said Friday a recent discovery off the coast of Tanzania has proved to hold large quantities of natural gas, further cementing the idea that East Africa could become an exporter of liquefied natural gas to Asian markets. 

Analysis of the Zafarani discovery in Block 2 offshore Tanzania showed it holds up to five trillion cubic feet of natural gas, the companies said in a press release. The gas find was announced a week ago.

The drilling success is good news for several East African countries, where offshore oil and gas exploration is picking up speed and prospecting results have been encouraging. Italy's Eni SpA and Anadarko Petroleum Corp. of the U.S. have made large discoveries in neighboring Mozambique. BG Group PLC last year also made a discovery in Tanzania. 

"This discovery is...an important event for the future development of the Tanzanian gas industry," Tim Dodson, Statoil's executive vice president for exploration, said in prepared remarks. Statoil is the operator of the block with a 65% interest, while Exxon Mobil has the remaining 35%.

The discovery was the second large gas find Exxon Mobil announced in recent days. On Wednesday, Exxon and its partners exploring for hydrocarbons in the Black Sea unveiled a potentially large natural gas discovery. The Domino-1 exploration well, located in the Neptun Block, encountered 70.7 meters of net gas, implying the field can hold between 1.5 trillion and three trillion cubic feet of natural gas. OMV Petrom SA, a subsidiary of the Austrian oil-and-gas company OMV AG, and Exxon Mobil each hold a 50% interest.
The discovery—the first one offshore Romania—is significant as it opens a new frontier. But production is still several years off, according to OMV Petrom. The field lies in an area awarded to Romania in 2009 by the International Court of Justice after a decades-old dispute with Ukraine.

—Katarina Gustafsson contributed to this article. 

Write to Isabel Ordonez at Isabel.ordonez@dowjones.com

Friday, February 24, 2012

Sikummaliza Jumbe – " Maalim Seif"

Maalim Seif Sharif Hamad

 Mh. Aboud Jumbe Mwinyi




















Sikummaliza Jumbe – "Maalim Seif"


22 Februari 2012

Na Seif Sharif Hamad

Mwaka 1984, Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, na Makamo wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Aboud Jumbe Mwinyi, alilazimishwa kujiuzulu katika Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma akishutumiwa kutaka kuvunja Muungano. Kitendo hiki kimekuwa kikichukuliwa na Wazanzibari kama udhalilishaji mkubwa kwa nchi na heshima yao, na msimamo wa serikali tatu, ambao Jumbe anasemekana kuutetea umekuwa ndio msimamo wa Wazanzibari. Kujiuzulu kwa Jumbe kunaunganishwa na tafauti za kimtazamo baina yake na Katibu Mkuu wa sasa wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye hata hivyo anasisitiza katika makala hii kwamba hajawahi kutafautiana na Jumbe kuhusu mtazamo wa Muungano.

Kwanza niweke kumbukumbu sawa. Mwaka 1984 wakati Mzee Aboud Jumbe anajiuzulu nyadhifa zake zote, mimi ni kweli nilikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mkuu wa Idara ya Uchumi na Mipango ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa [NEC] ya CCM, na hivyo kuwa miongoni mwa viongozi wa juu wa Chama cha Mapinduzi. Hata hivyo wakati huo sikuwa miongoni mwa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi. Kwani nilikuwa Waziri wa Elimu wa Zanzibar kuanzia mwaka 1977 hadi mwaka 1980. Nikateuliwa kuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar na Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyeteuliwa kuwa Rais wa Muda wa Zanzibar mara baada ya Mzee Aboud Jumbe kujiuzulu mwaka 1984. Hivyo kuanzia mwishoni mwa 1980 hadi mwanzoni mwa 1984 sikuwa kiongozi katika Serikali ya Mapinduzi.

Pili, tangu Chama cha Wananchi CUF kiasisiwe hapo 1992, sera yake rasmi ni kuwepo kwa Muungano wa serikali tatu: yaani Serikali ya Muungano, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Tanganyika.

Pengine itakumbukwa kuwa hata Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa Chama cha Siasa chochote kile kina haki ya kuwa na sera yake juu ya Muungano. Akasema kuwa kama vile ni haki ya CCM kuwa na sera ya serikali mbili kuelekea serikali moja, CUF wanayo haki hiyo hiyo ya kuwa na sera ya serikali tatu katika Muungano. Mwalimu Nyerere akamalizia kwa kusema kuwa na sera juu Muungano inayotafautiana na sera ya CCM si uhaini. Waachiwe wananchi waamue!

Hivyo basi msimamo wangu tangu kuasisiwa kwa Chama cha Wananchi, CUF haujapata kubadilika. Ni msimamo na sera ya Chama changu cha CUF. Sera ya kuwepo kwa serikali tatu katika Muungano wetu.

Hivyo niseme, kama nilivyokuwa nikisema kila nilipopata nafasi, kuwa bila ya kuubadili muundo wa Muungano wetu kutoka muundo wa sasa wa serikali mbili kwenda kwenye muundo wa serikali tatu, matatizo ya Muungano yataendelea kuutafuna Muungano wetu. Badala ya kuuimarisha tutakuwa tunaendelea kuudhoofisha. Kuimarisha Muungano sio kuongeza orodha ya Mambo ya Muungano katika Katiba. Hili linadhoofisha Muungano. Kwani nguvu za Muungano zitatokana na wananchi wa pande mbili kuukubali kwa dhati Muungano wenyewe. Kuhakikisha kuwa wananchi wa pande zote mbili wanaridhika na muundo wake, mamlaka na madaraka ya kila upande na serikali yake. Na zaidi kuliko yote, wananchi wa pande zote mbili kuridhika kuwa wanatendewa haki katika Muungano.

Vyenginevyo tutakuwa tukibadili misamiati tu: mara tutayaita matatizo ya Muungano; mara tuziite kero za Muungano, pengine tutakuja kuyaita mapungufu ya Muungano, au hata bughdha za Muungano, na kadhalika.

Suala la kutoka serikali mbili kwenda serikali moja hilo halitakubalika. Mimi silikubali. CUF hailikubali, na Mzanzibari mzalendo yeyote halikubali. Siamini kuwa Serikali ya Muungano itakuwa tayari kutumia vifaru, mizinga na madege ya kivita kulazimisha muundo wa serikali moja.

Baada ya kuweka msimamo huo, sasa nigeukie mambo mengine uliyoniuliza.

Kwamba Mzee Aboud Jumbe alituhumiwa kutaka kuwepo kwa muundo wa Muungano wa serikali tatu na akalazimishwa kujiuzulu. Wakati huo mimi nilitetea muundo wa sasa wa serikali mbili.

Ili hili lifahamike vyema na wananchi ni vyema kwanza kuelezea mazingira yaliyomfikisha Mzee Aboud Jumbe kujiuzulu.

Nitangulie kueleza kuwa mimi binafsi na kwa dhati ya nafsi yangu namuheshimu na namthamini sana Mzee Aboud Jumbe. Kwanza ni mwalimu wangu nilipokuwa nasoma katika skuli ambayo wakati huo ikiitwa The King George VI Secondary School (sasa Lumumba College).

Pili, ni Mzee Aboud Jumbe ambaye alisababisha mimi kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya yeye kuwa Rais wa Zanzibar mwaka 1972, baada ya kukaa kwa miaka minane (8) tangu nilipomaliza masomo ya Kidatu cha Sita (Form VI) hapo 1963 na kuzuiwa na Serikali ya Mapinduzi kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu, pamoja na kuwa kila mwaka nilikuwa napata nafasi katika vyuo mbali mbali duniani.

Tatu ni Mzee Aboud Jumbe huyo huyo aliyesababisha mimi kuwa kiongozi katika Serikali ya Mapinduzi na kuwa miongoni mwa viongozi wa juu wa CCM. Hivyo namshukuru na katu siwezi kumsahau kwa mchango wake mkubwa ulionifanya nilivyo.

Sasa nirejee kuelezea mazingira ya wakati huo ambayo yalikuwa kama ifuatavyo:

Nianzie mwaka 1982 ambapo kulikuwa na uchaguzi wa viongozi wa CCM. Katika kipindi kilichotangulia Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM wa 1982 wa kuchagua viongozi wa kitaifa, kulijitokeza makundi mawili miongoni mwa viongozi wa CCM kutoka Zanzibar yaliyokuwa yakikinzana. Kundi la kwanza likijulikana kama Liberators, na la pili likijulikana kama Frontliners. Kundi la Liberators kimsingi lilikuwa na viongozi ambao walikuwa wanapinga mabadiliko ya aina yoyote yale katika uendeshaji wa mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika Zanzibar.

Kwa lugha ya sasa unaweza ukaliita kundi la Wahafidhina. Kundi la Frontliners lilikuwa na vijana, damu mpya iliyoingia katika uongozi wa Chama na SMZ. Kundi hili lilitaka mabadiliko katika uendeshaji wa mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Unaweza ukaliita kundi la Reformers.

Uchaguzi wa viongozi wa kitaifa (Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa) wa 1982 ulishuhudia msuguano mkali kati ya makundi hayo mawili. Nia ya Liberators ilikuwa ni kuhakikisha kuwa Frontliners hawaingii katika Halmashauri Kuu ya Taifa. Nia ya Frontliners ilikuwa ni kuhakikisha damu mpya inaingia katika kikao hicho kikuu cha maamuzi cha Chama ambacho wakati huo kilikuwa ndio kimeshika hatamu zote za uongozi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bahati njema Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM, kwa busara zake, uliwaingiza watu kutoka makundi yote mawili katika NEC na, baadaye, NEC ikawaingiza watu kutoka makundi yote mawili katika Kamati Kuu.. Frontliners walishukuru kuona kuwa miongoni mwao walifanikiwa kuchaguliwa kuingia katika vikao vyote viwili vikuu vya maamuzi vya Chama.

Kwa upande mwengine, Liberators hawakufurahi. Liberators hao walishaweka shinikizo kwa Mzee Aboud Jumbe (ambaye ndiye chanzo cha kuingiza damu mpya katika CCM ya wakati huo) kuwa vijana aliowaingiza watakujamgeukia na kuwaondoa wao, Liberators, na yeye mwenyewe katika uongozi. Inaelekea Mzee Aboud Jumbe alishawishika na shinikizo hilo, na hivyo naye, kwa njia zake (nyuma ya pazia), alitaka kuona kuwa Frontliners hawaingii katika NEC na Kamati Kuu ya Chama ambako pengine wangekuwa na ushawishi katika maamuzi ya sera za Chama. Frontliners walipoingia, ikawalazimu Liberators na Mzee Aboud Jumbe kutafuta njia nyengine ya kuweza kuwazingira ili, ikiwezekana, waweze kuondolewa katika ramani ya uongozi wa Chama na Serikali.

Hivyo basi, mara baada ya kikao cha Mkutano Mkuu wa Taifa kumalizika mwezi Novemba, 1982, Mzee Aboud Jumbe aliwataka Wajumbe wote wa NEC kutoka Unguja akutane nao Unguja, na Wajumbe wote wa NEC kutoka Pemba akutane nao Pemba. Katika mikutano hiyo, hotuba ya mwalimu wangu, Mzee Aboud Jumbe, ilitushtua wengi. Mzee Aboud Jumbe alishtumu kuwa kuna watu wanaoleta uchochezi kutaka kuvigawa visiwa vya Unguja na Pemba; kutaka kuigawa mikoa, yaani mkoa mmoja dhidi ya mwengine katika kila kisiwa; kutaka kuzigawa wilaya, yaani wilaya moja dhidi ya nyengine katika kila mkoa; na kutaka kuvigawa vijiji, yaani kijiji kimoja dhidi ya chengine katika kila wilaya. Akamalizia kwa kusema kuwa watu hao watahukumiwa na kuonja kile alichokiita “Revolutionary Justice”

Hili lilitushtua wengi, hasa sisi vijana wa wakati huo. Tukakumbuka historia ya Zanzibar tangu Mapinduzi ambapo watu walioshukiwa kuwa wapinzani wa serikali, na hasa wasomi, walivyoshughulikiwa kwa kuhakikisha kuwa wanatoweka kabisa. Khofu yetu ikawa jee, hawa wazee si wamekusudia kuturudisha huko huko tulikotoka? Tukasema kama hatukuchukua hatua za kichama kulizuia hili, basi kuna uwezekano wa historia kujirudia na watu wasiokuwa na hatia kupotea kwa kile kinachodaiwa kusimamisha “Revolutionary Justice”

Hivyo baadhi yetu tuliokuwa Wajumbe wa Sekretariati ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, hasa sisi kutoka Zanzibar, tukamfuata Mzee Rashid Kawawa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM na Mwenyekiti wa Sekretarieti na kumueleza khofu yetu hiyo. Mzee Kawawa akatuelewa na akaamua iletwe agenda juu ya suala hilo katika kikao kilichofuata katika Sekretarieti. Agenda ikaletwa. Ikajadiliwa kwa mapana yake, kisha ikawasilishwa katika kikao cha Kamati Kuu. Kamati Kuu ikaamua kuunda timu mbili kwenda kuchunguza madai yaliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Aboud Jumbe. Timu moja ikaagizwa kufanya uchunguzi katika kisiwa cha Unguja, na timu ya pili ikaagizwa kufanya uchunguzi katika kisiwa cha Pemba. Timu moja iliongozwa na Marehemu Moses Nnauye na ya pili iliongozwa na Mheshimiwa Alfred Tandau.

Baada ya uchunguzi, timu zote mbili zikawasilisha taarifa zao katika kikao cha Kamati Kuu. Timu zote mbili ziliona kuwa madai ya Mzee Aboud Jumbe hayakuwa na msingi. Hivyo Kamati Kuu ikamsihi Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar na Makamu wa Mwenyekiti wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Aboud Jumbe, kuzuia kuchukua hatua zozote zile ambazo zingeweza kusababisha ukiukwaji na uvunjaji wa haki za binadamu dhidi ya raia.

Inavyoonekana, hili halikumpendeza mwalimu wangu, Mzee Aboud Jumbe. Alihisi kuwa Chama, na Muungano unamuingilia katika kutekeleza azma yake na ile ya Liberators ya kuisafisha safu ya uongozi wa Chama Zanzibar kwa kuwaondoa kwa njia yo yote ile Frontliners na vijana wenye mawazo mapya .

Kipindi hicho kulikuwa na mjadala ulioanzishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa juu ya mapendekezo ya marekebisho ya Katiba. Mzee Aboud Jumbe na timu yake wakaona kuwa waitumie nafasi hiyo kufanya kampeni kabambe kutaka muundo wa Muungano ubadilishwe. Sisi wa Frontliners tulitafsiri kuwa kampeni hiyo madhumuni yake ni kutaka kubadili muundo wa Muungano ili kundi la Liberators lipate uhuru zaidi, nguvu zaidi, na madaraka zaidi, ambayo, kwa mawazo yetu, yangetumika dhidi ya watu wenye mawazo mapya na ambao walionekana kama ni tishio kwa Liberators. Tulitafsiri kampeni hiyo kuwa na agenda iliyojificha ya kutaka kujiimarisha na kujichimbia katika madaraka kundi la Liberators ili kulinda “status quo.”

Ni kwa msingi huo ndipo mimi na wenzangu wa Frontliners tulimpinga Mzee Aboud Jumbe. Ifahamike kuwa hatukupinga dhana ya serikali tatu! Tulipinga nia iliyojificha ya Mzee Aboud Jumbe na wenzake ya kuibua agenda hiyo. Tulipinga njia zilizotumika katika kuisimamia na kuiendesha agenda hiyo. Ndio maana mara baada ya Chama cha Wananchi, CUF, kuundwa, tukabuni sera ya muundo wa Muungano wa serikali tatu. Ikumbukwe kuwa wengi wa waasisi wa CUF walitokana na kundi la Frontliners.

Ingalikuwa kulikuwa na nia njema, Mzee Aboud Jumbe angetuita, walau baadhi yetu na kutaka mawazo yetu. Nina hakika wengi tungekubaliana naye na tungezungumzia mkakati wa kulikabili suala hilo. Mimi nina hakika tungekwenda Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu kama uongozi wa Zanzibar ulioungana, wenzetu wa Bara wasingeweza kutupuuza. Na hapa niseme, tena kwa masikitiko makubwa, kwamba hili ndio limekuwa tatizo letu Wazanzibari. Wazanzibari tuna madai ya msingi katika Muungano. Lakini tunashindwa kuyasimamia madai yetu hayo hadi kupatikana mafanikio kwa kuwa tumekubali kugawiwa na tumegawika. Kugawika huko hakuyanufaishi maslahi ya Zanzibar.

Nitoe wito, kupitia gazeti lenu, kwamba wakati umefika kwa Wazanzibari bila kujali tafauti zetu za kiitikadi, kuungana ili kusimamia, kutetea na kuendeleza masilahi ya Zanzibar na watu wake katika Muungano.

Kwa kumalizia basi, kwa maoni yangu, Zanzibar ni nchi. Zanzibar ni taifa. Zanzibar ni dola.

Zanzibar ni nchi kwa sababu ni eneo lenye mipaka inayotambulikana na Katiba ya Zanzibar na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia ina watu wanaotambulika.

Zanzibar ni taifa kwa vile Wazanzibari kwa ujumla wao wanatambulikana kuwa na mila na utamaduni wao. Wazanzibari wanaweza kutafautishwa na watu wa sehemu yoyote nyengine duniani. Taifa la Wazanzibari lina uhai na ni taifa endelevu.

Zanzibar ni dola kwa vile kuna mamlaka iliyowekwa na Katiba zote mbili, yaani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar [SMZ] yenye madaraka yasiyoweza kuingiliwa na chombo chochote chengine katika mambo yasiyo kuwa ya Muungano katika nchi ya Zanzibar. Ni kweli kuwa Zanzibar haina jeshi lake wala polisi yake. Lakini ni kweli pia kuwa Zanzibar ina vyombo vyake vyengine vya maguvu vilivyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Katiba inayotambuliwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano na sheria za Zanzibar. Hivyo ni vyombo vya maguvu vilivyo halali kwa mujibu wa sheria za nchi.

Ni kweli kuwa suala la Mambo ya Nje ni jambo lililomo katika orodha ya Mambo ya Muungano. Lakini ni kweli pia kuwa suala la mahusiano ya kimataifa halijawahi kuingizwa katika orodha ya Mambo ya Muungano. Hivyo Zanzibar ina uwezo kamili wa kushirikiana na mataifa na mashirika ya kimataifa katika kuwaletea maendeleo Wazanzibari. Ni bahati mbaya kuwa Serikali ya Muungano imejaribu na inaendelea kuiminya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusimamia ushirikiano wa kimataifa. Mambo kama haya ndio yanaoudhoofisha Muungano wetu.

Kama kuna watu wanasema kuwa Zanzibar sio nchi, basi wasiishie hapo. Waeleze jee Zanzibar ni Mkoa, au ni Wilaya, au ni kijiji au ni kitongoji?
--

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Uwepo wa Dawa Bandia Kutiba Malaria

TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE
 
TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE (Quinine Sulphate 300mg USP)

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ni wakala wa Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti ubora, ufanisi na usalama wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya ya jamii.

TFDA inapenda kuutaarifu umma kuwa imebaini kuwepo kwa dawa bandia ya kutibu ugonjwa wa Malaria katika soko. Dawa hiyo inaitwa Eloquine (Quinine Sulphate 300mg U.S.P) na ipo katika makopo ya vidonge 1000 (elfu moja) kila moja. Maelezo yaliyopo katika lebo yanaonesha kuwa dawa hiyo imetengenezwa na kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd cha nchini Kenya.

Hata hivyo, TFDA imebaini kuwa kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd hakitengenezi dawa yenye jina la biashara la ‘ELOQUINE’. Kiwanda hicho kimesajili Tanzania Quinine Sulphate 300mg B.P isiyo na jina la kibiashara. Aidha, kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd kimebainisha tofauti mbalimbali zilizopo katika lebo ya dawa bandia ikilinganishwa na dawa halisi inayotengenezwa na kiwanda hicho iliyosajiliwa na TFDA na hivyo kuthibitisha kuwa kiwanda hicho hakitengenezi dawa hiyo.

Katika kudhibiti usambazaji wa dawa hiyo hapa nchini, hadi sasa TFDA imekamata jumla ya makopo 155 ya dawa hiyo bandia ya Eloquine jijini Dar Es Salaam yaliyokuwa yakisubiri kusambazwa. Aidha, kopo moja lenye vidonge 115 limekamatwa Moshi, Kilimanjaro. Tayari mtuhumiwa mmoja amekwishafikishwa mahakamani na upelelezi wa chanzo na wasambazaji wa dawa hii unaendelea kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Uchunguzi wa dawa bandia katika maabara umebaini kuwa vidonge hivyo havina kiambato hai (active ingredient) cha Quinine Sulphate kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Malaria na hivyo matumizi yake ni hatari kwa afya ya binadamu.

Maelezo ya kina yanayotofautisha dawa halisi iliyosajiliwa na dawa bandia ni kama yalivyoainishwa katika jedwali hapa chini.

Dawa halisi iliyosajiliwa
Maelezo ya dawa bandia

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg B.P

· Jina la biashara: Haina jina la biashara

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterprise Road, P.O Box 40411, 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi ya Lebo: Nyeupe na kahawia (Brown)

· Namba ya toleo: Huanzia na namba na siyo herufi. Kwa mfano: 2167E

· Muda wa matumizi (Shelf life): Miaka 4

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg U.S.P

· Jina la biashara: ELOQUINE

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterpises Road, P.O Box 4011 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi la Lebo: Njano na Nyekundu

· Namba ya toleo: GE410

· Tarehe ya kutengenezwa: 04/2009

· Tarehe ya mwisho wa matumizi: 4/2014 (Miaka 5)

Wafanyabiashara wote wa dawa na wananchi wanatahadharishwa kutozitumia dawa hizi na wale wote waliouziwa dawa hizi wanaelekezwa kuzirudisha dawa hizo katika ofisi za TFDA, vituo vya afya vya Serikali au vituo vya polisi vilivyo jirani nao.

TFDA inapenda pia kuwakumbusha wafanyabiashara wa dawa, wasafirishaji wa vifurushi na wananchi kutoa taarifa haraka iwezekanavyo pale wanapohisi kuuziwa dawa duni, bandia au zilizoisha muda wa matumizi. Taarifa zitolewe ofisi za TFDA makao makuu zilizopo Barabara ya Mandela, EPI Mabibo External, Dar es Salaam na Ofisi za Kanda zilizopo mtaa wa Nkurumah, Mwanza, Mtaa wa Sakina – Arusha, Hosptali ya mkoa ya Dodoma na Jengo la Ofisi ya Mifugo Mkoa wa Mbeya.

Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:-

MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
EPI MABIBO EXTERNAL,
S.L.P 77150, DAR ES SALAAM
Simu: + 255 222 450512/450751/452108
Nukushi: + 255 222 450793
Barua pepe: info@tfda.or.tz
Tovuti: www.tfda.or.tz

Thursday, February 23, 2012

Bibi Arusi Ana Miaka 100, Bwana Arusi Ana Miaka 87! Kweli Kabisa!

Duh! Naona Cougar wa miaka 100 kaolewa leo na kijana  mwenye miaka 87 huko Kentucky.  Wanaarusi wanaishi katika nyumba ya wazee na walikutana huko.   Ni kweli mapenzi yakinoga unajisikia kijana.  Bibi Dana Jackson (100) anasema kuwa anajiona kama ana miaka 50 tu! Nawatakia maisha mema ya ndoa! 

Congratulations Mr. & Mrs. Strauss!

***************************************************

(Dana Jackson & Bill Strauss)
Woman Weds on Her 100th Birthday


By Bridal Guide

On February 6th, Dana Jackson celebrated a century of life with about 100 of her nearest and dearest at the Rosewood Health Care Center in Kentucky. An ice cream cake in her honor was frosted with the special message, "Congratulations, you are never too old." But this wasn't your average birthday party, not even for a centenarian: Jackson decided to mark the momentous occasion by marrying boyfriend Bill Stauss, 87.

Stauss never imagined that he would ever wed again, since his previous marriage lasted 55 years. However, Jackson was the exception: "I found one that's just as nice as can be. Treats me good. Like a human being should be treated. It's rare to find a girl like that."

"I feel 50," Jackson told BG Daily News. "I don't feel 100."

This was Jackson's third trip down the aisle, but the first time she wore an engagement ring and traditional gown. Her first wedding took place when she was only 15 years old. She marveled at how much has changed since then: "Gettin' married wasn't a big thing back when I was young. It wasn't no big thing...it was just simple, you know? Just simple...we wore clothes and maybe a bouquet cut out of the yard. It's not what you got, it's what you make out of a marriage," she said.

Jackson's message is timeless, and in the AARP video below, her happiness is infectious, just as with any other bride. But marrying at 100 does have its challenges: The couple sipped grape juice in lieu of cocktails and Stauss had trouble seeing his wife walk down the aisle. The moment didn't disappoint-the husband thought his wife looked "beautiful" when he finally got a closer look.

Kuona Video ya Arusi BOFYA HAPA:

Producer wa Amazing Race Afariki Uganda

Wadau, kama mtakumbuka kama miaka mitatu iliyopita TV Show Amazing Race, walipitia Tanzania.  Katika Amzaing race timu zinasafiri katika nchi kadhaa za dunia, timu ya kwanza kufika katika sehemu mjia kadhaa inashinda siku hiyo.  Zanzibar ilipata umaarufu walipopitia hapo.

Leo kuna habri kuwa moja wa maproducer, Jeff Rice, amefariki dunia mjini Kampala.  Alikuwa anafuatilia habari tofauati lakini.  Polisi wa Uganda wanasema kuwa kafa kwa cocaine overdose.  Jamani,  kama kweli kafa kwa cocaine overdose itakuwa si mara ya kwanza mzungu/mtalii kufa kwa overdose barani Afrika.  Wakati nafanya kazi Daily News kuna mwarabu kutoka Royal Family alikufa kwa overdose Embassy Hotel lakini tulizuiliwa kuchapisha hiyo habari.

Kuna watalii ambao kazi yao ni kwenda nchi zingine kutumia madawa ya kulevya na kufanya ngono ya ajabu kwa vile wakifanya hapa Marekani sifa zao zinaharibika na wanaweza kufungwa.

Lakini familia ya marehemu, Jeff Rice, wanadai kuwa huenda alipewa sumu kwa vile alikuwa anafanya uchunguzi sijui kuhusu nini.  Ukweli utajulikana.

REST IN PEACE JEFF RICE.


***************************



Production facilitator Jeff Rice, who worked for reality shows including the current season of 'The Amazing Race,' was found dead after a suspected poisoning.
'Amazing Race' Producer's Death: Police Await Assistant's Recovery to Gain More Info


By BAZI KANANI and KEVIN DOLAK
Good Morning America –

....Investigators and family of the former "Amazing Race" producer Jeff Rice, who was found dead in a Uganda hotel room last Friday, are waiting to learn more about what might have killed him -- a cocaine overdose or suspected poisoning -- from his assistant, who remains in critical condition in a Kampala hospital.

Rice's body was found at the luxury Serena hotel in the capital city of Kampala. His assistant, Katheryne Fuller, was found unconscious.

"Ms. Fuller is slowly recovering, and when she is recovered enough we will be able to talk to her and find out more about what happened," Uganda Police Force spokesman Asuman Mugenyi said. "She is not able to speak. Although she is responding to the treatment, she is not yet available to explain what transpired."

Police say hotel staff noticed a man hanging on a balcony last Friday, and when they went to the room they found the 39-year-old's body on the balcony and Fuller unconscious in the room. Staff called police and rushed the two to a hospital, where Rice was declared dead, police said.

Investigators initially believed Rice and Fuller may have been sickened by some type of food poisoning. Later Mugenyi denied reports that Rice had been poisoned after he rebuffed a shakedown attempt from local "thugs," although friends remain skeptical.

"I was shocked. Jeff was someone who was terrific at his job," Josh Gates, a friend of Rice's told ABC News. "I don't know exactly what to think about what happened to Jeff. I hear conflicting reports coming out of the region."

Ugandan police said they have now ruled out poisoning and said further testing found high-levels of cocaine in Rice's system. Sources said Rice and Fuller were working on an investigative documentary, and many fear they might have been targeted by locals.

"For him to pass away so young so suddenly is alarming, obviously, but also is surprising because he was someone who was really able to take care of himself in the field. He was excellent at what he did," Gates added.

Rice was a veteran producer who worked on the latest season of the hit reality series "The Amazing Race" and the Emmy-nominated Animal Planet series "Whale Wars." In addition to raising two young kids, Rice and his wife, Sally Blackman, operated a television and film production company called SB Productions in Durban, South Africa.

Katheryne Fuller's father Stuart Fuller confirmed Rice were shooting a documentary, and other crew members who were with them should know more about what sickened them. Stuart Fuller said he is now with his daughter at the hospital in Kampala.

"She is OK. We are trying to get her back to South Africa. She needs medical attention that they can't do here," he said.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Wednesday, February 22, 2012

Nafasi za Kazi Kongwa Beef

NATIONAL RANCHING COMPANY LIMITED
(KAMPUNI YA RANCHI ZA TAIFA LIMITED)
NAFASI ZA KAZI ZA WAKALA MAUZO “SALES AGENTS”

“Kongwa Beef” ni Nyama yenye Ubora wa Kimataifa inayozalishwa na NARCO,
Kampuni ya Ranchi za Taifa Limited ambayo hivi sasa inafanya maboresho ya namna
ya kuwafikia wateja wake wa nyama ya “Kongwa Beef”. Ili kuhakikisha tunawapatia
wateja wetu huduma zinazozidi matarajio yao, tumeamua kutoa nafasi 200 za
Wakala Mauzo “Sales Agents” kwa vijana wa kike na wa kiume wa miaka 18-30. Hii
ni fursa muhimu sana kwa vijana wote wenye uzoefu au wanaopenda kujenga
uzoefu na kufanya kazi katika upande wa Masoko na Ujasiriamali.
Kama unashauku ya kupata nafasi ya kutafuta oda za “Kongwa Beef” kutoka kwa
wateja, basi hii ni nafasi yako.

MAJUKUMU YA WAKALA MAUZO WA “KONGWA BEEF”
 Kutangaza Ubora wa Kongwa Beef na kutafuta oda kutoka kwa wateja kwenye
maofisi, mahoteli, na taasisi mbalimbali.
 Kugawa vipeperushi na kushawishi wateja kununua “Kongwa Beef”.
 Kukusanya na kutunza kumbukumbu za wateja na mauzo
 Kuelimisha wateja wajue Ubora wa Kongwa Beef

MALIPO NA FAIDA UTAKAZOPATA
 Utalipwa kwa kila kilo moja ya nyama utayoleta oda na kuhakikisha imemfikia
mteja kupitia wasambazaji wetu.
 Kadiri utakavyoleta oda nyingi zaidi na kuhudumia wateja vizuri zaidi ndivyo
utakavyopata kipato ki-kubwa zaidi.
 Utakutana na mazingira mazuri ya kufanyia kazi na kupata changamoto za
kujiendeleza kitaaluma na kimapato.
 Utapata mafunzo ya masoko, biashara na ujasiriamali ili kukuwezesha kufanya
kazi kwa ufanisi zaidi.
 Vyeti vya heshima na vya mafunzo vitatolewa
 Utapata fursa ya kuendeleza ujuzi na taaluma yako katika fani za
biashara,ujasiriamali na masoko.

TAALUMA NA UZOEFU UNAOHITAJIKA
Mwombaji:-
 Awe na uwezo mkubwa wa kutoa huduma inayozidi matarajio ya wateja.
NATIONAL RANCHING COMPANY LIMITED
(KAMPUNI YA RANCHI ZA TAIFA LIMITED)
 Awe na uwezo wa kujieleza vizuri kwa Kiswahili.
 Uwezo wa kuongea Kiingereza kwa ufasaha itakua ni sifa ya nyongeza
 Awe mwenye shauku ya kuuza sana.
 Uwe na uwezo wa kuandaa na kutunza kumbukumbu za wateja na taarifa za
Mauzo na Masoko.
 Awe Mbunifu na Anayependa Kujiendeleza

NAMNA YA KUTUMA MAOMBI
 Andika barua kwa mkono bila kuchapisha na uambatanishe “CV” yako pamoja
na barua kutoka kwa wadhamini watatu (3) mmoja kati yao awe mzazi au
mlezi wako. Barua ziwe na namba za simu za wadhamini
 Ambatanisha namba za simu na anuani ya barua pepe kama unayo.
 Ambatanisha barua kutoka kwa Serikali za Mitaa iliyogongwa Muhuri na yenye
picha yako.

Maombi yote yatumwe kwa:
Meneja Mkuu,
Kampuni ya Ranchi za Taifa Ltd (NARCO),
Mavuno House, Azikiwe Street,
S.L.P 9113,
Dar es Salaam.
Simu : +255 22 211 0393/211 1956
Barua Pepe: info@narco.co.tz
Tovuti: www.narco.co.tz
Tuma maombi yako kwa kuleta mwenyewe ofisini au kwa Posta. Kila tutakapopokea
maombi tutayafanyia kazi mara moja.

*********Wahi Wateja Wanatusubiri Tuwahudumie**********

Monday, February 20, 2012

Bi Kizee Amuenzi Whitney Houston Kwa Ngoma!


.
Hebu cheki huyo bibi wa kizungu mwenye miaka 90 anayocheza ngoma. Hii kacheza kuonyesho upendo wake kwa marehemu Whitney Houston. Anasema amefariki dunia mdogo mno. Huyo bibi anasema alikuwa kipenzi cha muziki wa Whitney.

REST IN PEACE WHITNEY HOUSTON.

Lakini jamani hii iwe fundisho kwa sisi waafrika. Tunamwona bibi mwenye umri mkubwa ni wa kuanika juani tu!. Kumbe bado wamo!

Mtoto wa Gaddafi Aomba Msaada!

Hao matapeli wanazidi kuchekesha!

**********************************************************
How is everything over there?

I know this letter will definitely come to you as a huge surprise, but I implore you to take the time to go through it carefully as the decision you make will go a very long way to determine my future and continued existence.

My name is Saadi Gaddafi, I am the son of the late Muammar al-Gaddafi and the National Security Adviser of Libya. I am at the moment very depressed as I write to you. I got your mail from search engine and I really think you can be of help to me. At the moment I have been banned from traveling and some of my assets have been frozen already and that of my late father (Muammar al-Gaddafi ) and families.

Due to the situation at hand, I do not possess the right to move about as I will be arrested and prosecuted in an international court of justice. In my possession right now is my internet connection, it is the only means I am able to make contact with the outside world. Also as another measure that has been taken by the international community, our asset i.e the assets of Muammar al-Gaddafi and family worldwide have been frozen due to the actions of my late father.

The above mentioned reasons are what have compelled me to write you this mail as I seek to partner with a trustworthy person who can assist me in transferring some of my monetary assets worth about 5,000,000 GBP (FIVE MILLION GREAT BRITISH POUNDS). This funds has been lodged in a bank account in the United Kingdom and as things are shaping now this money is likely to be discovered soon, all the legal documentation concerning the deposit are with me, I will only authorize the power of attorney and next of kin certificate making you the new beneficiary of the deposit so that the bank will transfer the funds into your account immediately, so I seek your assistance in helping me transfer this money into your account so that it is not discovered. I am ready to offer as much as 30% of this money to you if you render to assist in transferring this money and the money is transferred successfully,
Please i want this to be a confidential deal between both us and if you are not interested in this deal, kindly delete this message from your email box  without keeping any content of this message and never act like if you received any mail from me, because i will not be pleased to lose this money in any way.
This is my personal email saadi_gaddafi101@yahoo.com i created this email today just to have a confidential communication with you, if you know you can assist me out from my present pain and stress, you are free to contact me.

Please be honest and truthful because some of my assets have been frozen already, and i don't want to lose this money.

PLEASE LET ACT FAST AS A MATTER OF URGENT.

Thanks,
Saadi Gaddafi.

Taarifa ya CHADEMA Kuhusu Ombi la CCM kw Dr. Slaa

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KURUGENZI ya Habari na Uenezi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) inapenda kutoa taarifa kuhusu habari zilizoripotiwa kupitia
njia mbalimbali za upashanaji habari, juu ya maombi ambayo Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kimesema kinafanya usiku na mchana ili eti Katibu Mkuu
wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, agombee ubunge, kwenye uchaguzi mdogo
unaotarajiwa kufanyika Jimbo la Arumeru Mashariki, Aprili 1, 2012.

Ingawa haijajulikana maombi hayo yanafanyika msikiti upi au kanisa
lipi au sehemu ipi yoyote ile nyingine ya kufanyia maombi, Kurugenzi
imeshangazwa sana na mantiki ya kuwepo kwa maombi hayo ya CCM
yakionesha upendo wa kutiliwa mashaka kuwa chama hicho kimefikia
mahali kinaweza kufanyia maombi vyama vingine ili vipate wagombea
makini wa kukibwaga vibaya sana katika uchaguzi.

Kurugenzi inapenda kusema yafuatayo juu ya maombi hayo ya CCM, ambayo
kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye,
kama ilivyoripotiwa katika njia mbalimbali za upashanaji habari,
imedhihirika dhahiri kuwa ni maombi yanayoongozwa zaidi na hila,
husuda kwa CHADEMA na Katibu Mkuu wake, Dkt. Slaa;

Tunapenda CCM wajue kuwa CHADEMA na viongozi wake makini, akiwemo
Katibu Mkuu, Dkt. Slaa, si watu wa kurudi nyuma. Chama hiki daima muda
wote kinapanga mikakati na mipango ya kusonga mbele, kikionesha
utawala mbadala, kikijiandaa kushika dola na kutekeleza malengo ya
Watanzania!

Kwa mantiki hiyo, chama hiki hakiwezi kurudi nyuma, hakiwezi
kumrudisha nyuma Katibu Mkuu wake, Dkt. Slaa kuwania ubunge. Kiongozi
huyu makini, ambaye umma wa Watanzania una imani kubwa naye,
ameshavuka viwango vya ubunge, si mtu wa kuwania nafasi ya ubunge
tena, (is not parliamentary material).

Kwa nafasi yake ndani ya CHADEMA, anao wajibu mkubwa kujenga chama.
Kwa kutimiza wajibu huo, Dkt. Slaa anafanya kazi ya kutengeneza na
kuivisha watu wengine makini zaidi, kuweza kuwa viongozi ndani ya
chama, nafasi za udiwani na ubunge, ili kuendeleza umakini na uimara
wa chama hiki ambacho dhahiri ni tumaini jipya la Watanzania katika
kutoa uongozi mbadala wa nchi.

Kwa umakini wa CHADEMA, uwezo wa Dkt. Slaa na matumaini makubwa ya
Watanzania, ambayo wameendelea kuyaonesha kwa chama hiki tangu mwaka
2007, kilipoanzisha rasmi mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi,
kisha kudhihirika wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, nafasi pekee
inayomstahili Dkt. Slaa ni urais kwa maana ya kuwa ni ‘presidential
material’, si ubunge.

Lakini pia, tunatambua kuwa CCM, wameweza kutoa kauli hiyo ya
kukurupuka baada ya Dkt. Slaa kuwa tayari ametamka wazi tangu awali na
kurudia kauli yake thabiti mara kadhaa kuwa hana nia wala mpango wa
kuwania ubunge mahali popote pale nchini. Hawezi kufanya hivyo kwani
hata ubunge wa Karatu hakushindwa bali aliacha mwenyewe kwa hiari
yake, ili kutekeleza mahitaji ya umma wa Watanzania.

Kurugenzi ya Habari na Uenezi inatumia nafasi hii kuwaambia CCM kuwa
watambue CHADEMA ni chama makini. Kimedhihirisha hivyo mara kadhaa
katika masuala makubwa kwa maslahi ya Watanzania. Kitaendelea
kudhihirisha hivyo pia katika uchaguzi wa Arumeru kwani kina utaratibu
wa kuwapata wagombea wake, kutokana na maamuzi ya wanachama wake.

Tunatambua kuwa kauli hiyo ya CCM pia ni sehemu ya mkakati wa makusudi
kuwakatisha tamaa baadhi ya watu wanaotaka kugombea jimbo hilo kupitia
CHADEMA. Kurugenzi ya Habari na Uenezi inapenda kusisitiza taarifa ya
awali, kuwataka wanachama wetu wajitokeze kwa wingi kuwania uteuzi wa
kugombea ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki.

Tunataka CCM wajue kuwa suala la kuteua mgombea wa CHADEMA ni la
CHADEMA yenyewe, kwa kutumia utaratibu wake, ikiongozwa na katiba,
kanuni na mahitaji ya umma, wala hatuhitaji ushauri wa chama ambacho
kadri siku zinavyokwenda, kinadhihirisha kila dalili ya kuchoka
kujisimamia chenyewe, kusimamia wanachama wake, kusimamia serikali na
maendeleo ya watu, hivyo kupoteza kabisa ushawishi kwa wananchi. Wala
hatujawahi kuomba ushauri kutoka kwao hata siku moja.

Lakini maombi hayo ya CCM, kama ambavyo Nape amenukuliwa katika vyombo
vya habari akisema, yamedhihirisha namna ambavyo chama hicho bado
kinaandamwa na mzimu wa CHADEMA na Dkt. Slaa tangu baada ya uchaguzi
mkuu, kwa kuiba kura na kuvuruga matokeo ya uchaguzi huo.

Kauli ya Nape kuwa iwapo maombi yao yatafanikiwa na Dkt. Slaa akawania
ubunge, CCM watakuwa wamemaliza kazi katika uchaguzi mkuu wa mwaka
2015, inathibitisha tuhuma hizo na namna ambavyo CCM hakikushinda kwa
haki uchaguzi huo.

Kurugenzi ya Habari na Uenezi ya pia inataka CCM waelewe kuwa umaarufu
wa CHADEMA hautokani na umaarufu wa mtu mmoja mmoja wala hausubiri
matukio pekee, bali unatokana na uongozi makini, kuanzia ngazi ya
taifa hadi ya msingi, kikijikita katika kusimamia masuala yenye
maslahi kwa Watanzania na nchi yao muda wote!

Imetolewa leo Februari 18, 2012, Dar es Salaam na

Tumaini Makene
Afisa Habari wa CHADEMA

Sunday, February 19, 2012

Skeleton za Wavaa 'Gawa Kundu'

Kumbe milli ya wavaa mtindo 'Gawa Kundu' (sagging) iko hivyo!

Saturday, February 18, 2012

Dk. Mwakyembe Amjibu DCI Manumba!


Dr. Harrison Mwakyembe (picha kutoka JamiiForums.com)

           Dk. Harrison G. Mwakyembe (Mb), NW-UJ
Dar es Salaam
18/02/12
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nimelazimika leo Jumamosi, tarehe 18 Februari, 2012 kutoa taarifa hii kwa vyombo vya habari kufuatia mkutano wa DCI Robert Manumba na waandishi wa habari jana (17/02/12) kuongelea, pamoja na mambo mengine, hali yangu ya afya na kuhitimisha, kienyejienyeji tu kuwa “sikunyweshwa sumu” ila naumwa tu ugonjwa wa ngozi bila kufafanua ugonjwa huo wa ngozi umesababishwa na nini!
Napenda nisisitize mapema kabisa kuwa msimamo huo wa Jeshi la Polisi umenikera sana katika hali niliyonayo ya ugonjwa, kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake unaoendelea hospitali ya Apollo nchini India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu; pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa “sikunyweshwa sumu” wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu; na tatu kwa Jeshi la Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.
Itakumbukwa kuwa tarehe 9 Februari, 2011 nilimwandikia barua IGP Said Mwema kumtaarifu kuhusu njama za kuondoa maisha yangu na ya viongozi wengine. Kwa kutambua kuwa Jeshi la Polisi la Tanzania daima husisitiza kuletewa ushahidi kwanza ndipo lifanyekazi, nilihakikisha nimeainisha katika barua  hiyo kila ushahidi nilioupata au kupewa. (Utaratibu huu wa Jeshi la Polisi kusubiri kuletewa ushahidi mezani, kama ambavyo mahakimu wanavyosubiri ushahidi mahakamani, haupo popote pale duniani (ila Tanzania tu) kwani kazi ya msingi ya Polisi si kuletewa, ni kutafuta ushahidi. Polisi wanachohitaji duniani kote ni kupata clue au tetesi tu. Hiyo inatosha kufukua ushahidi wote unaohitajika). Pamoja na kujitahidi kuanika kila aina ya ushahidi niliokuwa nao, mambo manne yalijitokeza ambayo yalionyesha wazi kuwa Polisi hawakuwa na dhamira ya dhati ya kupeleleza suala hilo:
(i)                Siku chache baada ya kumkabidhi IGP barua hiyo, nilitumiwa timu ya “wapelelezi” ofisini kwangu kuja kuchukua maelezo yangu ya ziada. Timu hiyo ilikuwa inaongozwa na ACP Mkumbo, afisa wa polisi ambaye wiki chache zilizokuwa zimepita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wa Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi, suala ambalo mpaka leo hii uongozi wa Polisi umeshindwa kulitolea maelezo ya kuridhisha. Kwa msingi huo, nilikuwa nimeletewa mtuhumiwa wa rushwa/ ujambazi kuendesha uchunguzi wa watuhumiwa wengine wa ujambazi! Nikatambua mara moja kuwa zoezi zima lilikuwa la mzaha, tena mzaha mkubwa!
(ii)              Wiki chache baada ya barua yangu kuwasilishwa kwa IGP na timu ya ACP Mkumbo “kuanza kazi”, Jeshi la Polisi likachukua hatua ya kuwapongeza na kuwazawadia askari niliowatuhumu kushirikiana na majambazi! Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwa ujumbe tosha wa kunipuuza.
(iii)            Hivi karibuni tuhuma za askari polisi kujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto na kuwagusa askari “wale wale” niliowatuhumu kwenye barua yangu, IGP alichukua hatua ya kuwahamishia mikoa mingine!
(iv)           ili kunikatisha tamaa kabisa, barua yangu ya “siri” kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kama habari ambayo ilikebehi na kukanusha taarifa nzima niliyotoa, sijui kwa faida ya nani! Lakini huu ni mchezo wa kawaida kwa polisi kwani hivi karibuni Mhe. Waziri Samuel Sitta alipohojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi ofisini kwake, wakiwa wawili tu, taarifa ya kikao hicho ikawa kwenye moja ya magazeti ya mafisadi ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta! The integrity of the police force leadership is on the line.
Nimeelezea vizuri katika barua yangu kwa IGP kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kuniua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima Polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wenyewe.  Sasa huu msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama nilipewa sumu au la na kukurupuka kutoa tamko hata kabla ya kunichunguza nilivyo, kunihoji mimi na wasaidizi wangu ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaonifanyia uchunguzi, umetokea wapi?  Si ni polisi hawahawa ambao, badala ya kushukuru,  wamekuwa wakikerwa na tahadhari ambazo Waziri Sitta amekuwa akitoa ili suala hili lichunguzwe kwa kina?
Aidha napata taabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matatibabu yangu au walisoma taarifa “nyingine”, na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au “walisomewa”! Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa wandishi wa habari hakifanani kabisa na picha iliyo kwenye taarifa halisi ya Apollo ambayo inatamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua, kukidhibiti /kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu: “hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu”!
Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Mlimani na DCI Manumba. Baadaye IGP Mwema alikuwa mwanafunzi wangu wa sheria Mlimani. Vigogo hawa wawili wa usalama wa raia nchini hawajanitendea haki, nao wanajua. Wanajua vilevile kuwa sitakaa kimya au kumung’unya maneno come what may pale ambapo haki inakanyagwa.
Tuendelee kuombeana afya na uhai ili tutendeane haki na vilevile tuitendee nchi yetu haki kwa kuvimalizia viporo vinavyokera vya Dowans, EPA, Kagoda n.k. kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
 
Mungu Ibariki Tanzania .

Mpinzani Ralph Kasambara Alazwa Hospitalini Malawi

 BLANTYRE, Malawi (AP) - The lawyer for an outspoken opponent of Malawi's president says his client has been moved from jail to a hospital, where he is being treated under police guard for a heart ailment.

Ralph Kasambara's lawyer Wapona Kita said he went with him to a hospital early Saturday. Kita says doctors say Kasambara "has developed a serious cardiac condition."

 Kasambara was arrested Monday, accused of kidnapping and torturing three men he told reporters had confessed they had been sent by the government to firebomb his office. The government denies Kasambara's accusations. Kasambara denies the charges against him.

 Kasambara's arrest came days after weekly newspapers quoted him saying President Bingu wa Mutharika "wants to be a dictator" and should be impeached.

Thursday, February 16, 2012

Matatizo ya Kijiji cha Nanja Wilaya ya Monduli

Nafanya kazi katika Asasi inayotoa elimu ya UKIMWI na Afya ya Uzazi kwa jamii iliyopo Arusha. Mwishoni mwa mwezi huu tulifanya survey ya UKIMWI katika vijiji vya Nanja na Makuyuni vilivyopo wilaya ya Monduli kwa ajili ya mradi tunaotaka kuanza hivi karibuni.

Kilichonisukuma kuandika katika jukwaa hili ni matatizo tuliyoyakuta katika kijiji cha Nanja

HAWANA MAJI

Yaani hakuna kisima wala bomba la maji hivyo hutegemea maji ya mvua ambayo watu wachache ndio wanamatenki ya kuvunia maji hayo. Katika kipindi ambacho si cha mvua hununua maji ndoo ya lita kumi kwa tsh 300 hadi 500.

HAWANA KITUO CHA AFYA

Hakuna kituo cha afya/Zahanati wala clinic ya kutibu wanakijiji. Ikitokea kuna mgonjwa mpaka wampeleke Monduli,Makuyuni au Mto wa mbu ili waweze kupata matibabu. Kwa upande wa kinamama wajawazito wengi wao huzalishwa na wakunga wa jadii hivyo kuna uwezekano mkubwa wa vifo vya mama a mtoto.

Ombi langu kwa wanabidii kama kuna mtu aliyewahi kufanya utafiti au ana uzoefu wa maeneo haya ya Nanja aieleze jamii kuhusu sehemu hii kwakua watanzania wenzetu wanateseka.

Nawakilisha

Malima P. Macha
PM - CHAWAKUA

Chupi Bomber Afungwa Maisha

Umar Farouk Abulmutallab baada ya kukamatwa na FBI
Yule kijana MNigeria, aliyejaribu kulipua ndege na bomu alivaa ndani ya chupi yake siku ya Krismasi mwaka 2009 amepata kifungo cha maisha.  Umar Farouk Abdulmutallab, alikuwa na miaka 25 alivyojaribu kulipua hiyo bomu ya chupi. Haikulipuka kama alivyotarajia na badala yake kaunguza nyeti zake, bolo na mapumbu!  Hivi ni mwanaume gani wa kiafrika asiyethamini nyeti zake?! Alikuwa tayari kujiua na kuua watu wengine eti kwa ajili ya dini! Atakuwa punguani huyo, wala si dini. Mwache akae huko gerezani maisha atakuwa mke wa Big Bob.***********************************


DETROIT (AP) — A Nigerian man on a suicide mission for al-Qaida was sentenced Thursday to life in prison for attempting to blow up an international flight with a bomb in his underwear as the plane approached Detroit on Christmas 2009.

The mandatory punishment for Umar Farouk Abdulmutallab, the well-educated son of a wealthy banker, was never in doubt after he surprised the courtroom and pleaded guilty to all charges on the second day of trial last fall.

Abdulmutallab sat with his hands folded under his chin, leaning back in his chair as the sentence was announced.

In October, Abdulmutallab said the bomb in his underwear was a "blessed weapon" to avenge poorly treated Muslims around the world. It failed to fully detonate aboard an Amsterdam-to-Detroit flight but caused a brief fire that badly burned his groin. Passengers pounced on Abdulmutallab and forced him to the front of Northwest Airlines Flight 253 where he was held until the plane landed minutes later.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI!

Tuesday, February 14, 2012

Ni Katerero au Katelelo? - WAKUBWA TU!


Leo ni Valentine's Day! Mfurahishe mpenzi wako! 

***********************************************************
Dada Dina anatutoa ushamba hapa!  Asante sana Dada Dina kwa somo nzuri sana.

Kutoka Dinahicious Blog:

Katelelo


"Dada Dinah habari ya kazi. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kazi unayoifanya ya kuelimisha jamii kuhusu ngono na mambo ya mapenzi kwa ujuma.

Leo katika pita pita mtaani nimekutana neno linaloitwa KATELELO. Nasikia ni jina la style ya kufanya sex maarufu huko Bukoba. Nimemwuliza rafiki yangu wa huko Bukoba anielezee, amebakia tu kucheka, kacheka kweli, amekataa kunieleza inafanywaje.

Basically nasikia ni Cli-toris Stimulation technique ambayo nasikia mwanamke akifanyiwa hata kama tangu azaliwe hajawahi pata orgasm atapata tu. Tena zaida ya yote nasikia mwanamke anaweza mwaga maji hadi LITA 3 au hata 4.

Jamani hiki kitu kipo kweli? Sasa kama kipo jamani mke wako au mpenzi wako akitombwa na hao jamaa wa katelelo si ndio atakukimbia tena kibaya zaidi awe hapati orgasm akisex na wewe.

Please dada Dinah pamoja na wadau wote kama hiki kitu ni kweli na kuna mtu anajua basi naomba na mimi animegee huo utalaam.

Asante, Mdau kutoka A-TOWN"

Jawabu: Asante, Katelelo ipo na nina uhakika wengi huwa wanaifanya ila majina ndio hutofautiana au hawaipi jina zaidi ya "nilimsugua kisimi", "nilichapwa kisimini" "nilinyonywa/lambwa kisimi".

Swala la lita tatu za maji sina uhakika linasababishwa na "katelelo" bali ni maumbile zaidi kwamba wapo wanawake wanamwaga maji na wengine wanatoa ute mwingi lakini sio kisai cha kuleowesha godoro.

Sasa ni hivi, Kitendo cha kucheza na kisimi kwa utaalamu na mirindimo tofauti mpaka mwanamke anamaliza ndio kinaitwa "katelelo", kitendo hiki hakina tofauti sana na "kumshukia" mwanamke yaani kucheza na kisimi kwa kutumia ulimi japokuwa ulimi ni mtamu zaidi kwa vile ni laini kutokana na mate kinywani vilevile unanyonya kila baada ya "vibrashi" vichache, bila kusahau kuna "speed" amabyo huongezwa na kupunguzwa.

Kitendo hiki hufanywa kwa kufuata mikao fulani kama ilivyo kwenye "kumshukia Chumvini" na mikao hiyo ni kama vile "Doggy" Inaweza kuwa ya kupiga magoti au ya kuinama, kulala chali na kupanua miguu, kukaa kochini au kitini na kupanua miguu.....kama hakionekani basi mwana mama itamlazimu kutumia mikono yake ili kupanua maeneo yake nyeti ili uweze kufanyia kazi "kiharage".

Kuna namna ya ukamataji wa uume ili kufikia lengo, kuna wale wanaoushikilia karibu zaidi na kichwa hali inayoongeza ukubwa wa "kichwa" na ugumu hali inayo ongeza utamu alafu ndio wanasugua (hii kama inauma vile eeh), wacha niseme ku-brashi Kisimi, ku-brashi huko hutofautiana (nitakuambia jisni ninavyoendelea)

Pia kuna wanaume wengine hushikilia uume kama vile wanavyo kojoa (sio manii bali mkojo maji) au wanavyouingiza ukeni lakini sasa wanaishia kisimini tu na kufanya ile-brashi. Sasa wakati unaendelea na ku-brashi unatakiwa kuongeza manjonjo na "spidi" ili kumpa mpenzi wako utamu makini.

Unaweza kuwa unachovyesha kichwa pale ukeni (unapoingia uume) pale mwanzo wa uke kuna utamu wake ambao ni tofauti au niseme ni zaidi ya ule wa kisimi japokuwa huwezi kufikia kilele.......wakati "unamkaTelelo" Kisaikolojia atakuwa anasikilizia Utamu wa ajabu bila kujua tofauti, yeye atakuwa akijua unacheza na sehemu ya juu ya uke wake ambayo ni Kisimi.

Ikiwa mwanamke unaefanyanae ni mmoja kati ya wale wenye kutoa maji mengi (nasikia baadhi ya Wahaya,Wachaga, Wanyakyusa (kwa Tz), Waganda, Warundi na Wanyarwanda) hii ni kwa ajili ya kula ndizi nini hehehehehe......basi wakati anakaribia utaanza kuona maji yakiongezeka na akifika kabisa basi ndio vile......usisahau kuanika Godoro.

Wanawake wengi wa Kiafrika wanapenda sana mtindo huu wa ufanyaji ngono kwa vile ni rahisi kufika kileleni kuliko aina nyingine ya ufanyaji hasa ukizingatia kuwa asalimia kubwa ya wanawake hawana uwezo wa kusikilizia/kupata utamu wa ngono kwenye maeneo mengine (mwanzo wa uke, Kipele G, Kuta za uke na eneo linaolitwa AFE).

Kisimi ni eneo pekee la linaloweza kumfanya mwanamke kupata uzoefu wa utamu wa ngono kwa haraka kuliko sehemu nyingine za uke wake hata kama kajaaliwa kusikilizia utamu ikiwa maeneo mengine manne yakifanyiwa kazi vema.

Natumai maelezo yangu na yawachangiaji wengine yatakuwa yamekusaidia kwa kiasi fulani....

Kila la kheri!

Happy Valentine's Day!

Nawatakia wadau wote siku njema na enye furaha tele na yule umpendaye leo hii siku ya Valentine's Day! 

Msisahau kufanya mapenzi kwa usalama!

Saturday, February 11, 2012

Whitney Houston Afariki Duna!!!!

(Pichani Marehemu Whitney Houston nwaka 2004)

Whitney Houston, superstar of records, films, dies



LOS ANGELES (AP) — Whitney Houston, who ruled as pop music's queen until her majestic voice and regal image were ravaged by drug use, erratic behavior and a tumultuous marriage to singer Bobby Brown, has died. She was 48.

Houston's publicist, Kristen Foster, said Saturday that the singer had died, but the cause and the location of her death were unknown.

News of Houston's death came on the eve of music's biggest night — the Grammy Awards. It's a showcase where she once reigned, and her death was sure to cast a heavy pall on Sunday's ceremony. Houston's longtime mentor Clive Davis was to hold his annual concert and dinner Saturday; it was unclear if it was going to go forward.

At her peak, Houston the golden girl of the music industry. From the middle 1980s to the late 1990s, she was one of the world's best-selling artists. She wowed audiences with effortless, powerful and peerless vocals that were rooted in the black church but made palatable to the masses with a pop sheen.

Her success carried her beyond music to movies, where she starred in hits like "The Bodyguard" and "Waiting to Exhale."

She had the perfect voice and the perfect image: a gorgeous singer who had sex appeal but was never overtly sexual, who maintained perfect poise.

She influenced a generation of younger singers, from Christina Aguilera to Mariah Carey, who when she first came out sounded so much like Houston that many thought it was Houston.

But by the end of her career, Houston became a stunning cautionary tale of the toll of drug use. Her album sales plummeted and the hits stopped coming; her once serene image was shattered by a wild demeanor and bizarre public appearances. She confessed to abusing cocaine, marijuana and pills, and her once pristine voice became raspy and hoarse, unable to hit the high notes as she had during her prime.

"The biggest devil is me. I'm either my best friend or my worst enemy," Houston told ABC's Diane Sawyer in an infamous 2002 interview with then-husband Brown by her side.

 http://music.yahoo.com/news/whitney-houston-superstar-records-films-dies-005927033.html

Zilipendwa - How Will I Know



Rest in Peace Whitney Houston (1963-2012)

Friday, February 10, 2012

Warsha ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu - UDSM

WARSHA YA UANDISHI WA MISWAADA YA FILAMU/SCREENPLAY WORKSHOP
(Level 1)


Je? Unajua kuwa hadithi za Filamu zozote hujengwa kwa wahusika, wahusika ndiyo wabeba lengo zima la filamu?  Je, wajua jinsi ya kuwa jenga wahusika wako ili waweze kubeba lengo la hadithi ya Filamu kiufasaha? Je,unajua kuwa ukikosea kumjenga mhusika mkuu katika hadithi ya Filamu yako ni vigumu hadithi ya Filamu bora?

Basi ukitaka kuyajua yote haya karibu katika warsha ya uandishi wa miswada ya filamu pale IDARA YA SANAA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM Kuanzia tarehe 13-15 Februari 2012. Kuta kuwa na Warsha ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu/Screenplay Workshop (Level 1) Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kila siku kuanzia saa 3 asubuhi hadis aa 8 mchana , Cheti cha Ushiriki kitatolew amwishoni mwa mafunzo.

Warsha itakuwa kwa Kiswahili (na Kiingereza ikibidi)na mshiriki anaweza kuwa mtu yoyote anayependa kuandika miswada ya filamu (amateur scriptwriter) au mwandishi anayechipukia (upcoming scriptwriter)

Hima wadau wote wa Tasnia ya Filamu ,Sanaa, Sanaa za Maonyesho na Uandishi wa ubunifu msikose nafasi hii muhimu ya warsha mafunzo daraja la kwanza ilikujijengea misingi mizuri ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu.

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na warsha hii tafadhali wasiliana na IDARA YA SANAA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM , Ndg. John Mwakilama SimuN amba0714 13 22 49, na barua pepe: mwakilamajohn@yahoo.com

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Maazimio ya Kikao Kati ya Waziri Mkuu na Madaktati Leo CPL

Asante Da Subi kwa Kuleta Taarifa Hii:


Tamko la Kamati: MAAZIMIO YA KIKAO CHA WAZIRI MKUU; MADAKTARI

09/02/20120 Comments Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa Madaktari, Dkt. Stephen Ulimboka baada ya kuzungumza na madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam, Februari 9, 2012. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)
TAARIFA KWA UMMA NA MADAKTARI WOTE NCHINI JUU YA MAAMUZI YALIYOFIKIWA LEO FEBRUARY 9, 2012 KUFUATIA MKUTANO KATI YETU NA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA KATIKA UKUMBI WA CPL, HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari nchini inapenda kuwajulisha madaktari wote pamoja na kada nyingine zote za afya nchini juu ya kile ambacho kimejiri katika siku ya leo ya tarehe 09.02.2012 ikiwa ni matokeo ya kikao wanataaluma wa kada za afya na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na baadaye kufuatiwa na kikao kati ya madaktari na kada nyingine za afya.

Ifahamike kuwa kama Kamati tulipata mwaliko wa kushiriki katika Mkutano huo ambapo ilitarajiwa kuwa Mhe, Waziri mkuu atafika kwa nia ya kutoa mrejesho wa madai ya madaktari yaliyowasilishwa mezani kwake mnamo tarehe 23.01.2012. Madai yetu yalikuwa manane na Mh Wazizri mkuu aliweza kutoa maelezo ya dai moja baada ya lingine.

Miongoni mwa madai ambayo mpaka sasa yamepatiwa majibu ya kuridhisha ni pamoja na;

Kuwawajibisha watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wakiwemo Katibu Mkuu Mama Blandina Nyoni , na Mganga Mkuu wa Serikali Dr. Deo Mtasiwa. Aidha Mh waziri mkuu alisema kuwa ameshalifikisha kwa Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania suala zima la kuwawajibisha watendaji wa wakuu wa kisiasa wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambao ni Waziri Mh Hadji Mponda na Naibu Waziri Mhe. Lucy Nkya.

Kama sehemu ya maridhiano, Mh Waziri Mkuu pia aliahidi mbele ya mkutano kuwa hakutawepo na unyanyasaji au vitisho vya aina yoyote ile kwa wale wote walioshiriki katika kushinikiza Serikali kutatua kero hizo. Aidha kama sehemu ya maridhiano, Mh waziri Mkuu pia alifuta zuio la madaktari kutokufanya mikutano. Lakini pia, Mh waziri Mkuu alisema kuwa Serikali haina kusudio la kumfukuza kazi mtumishi yeyote wa afya yule kazi aliyeshiriki katika mchakato huu wa kuishikiniza Serikali kutafuta ufumbuzi madai ya madaktari nchini.

Aidha, Mh waziri Mkuu amesema “Interns” wote waliokuwa wamehamishwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamesharudishwa bila masharti katika hospitali hiyo ili kuendelea na program kama kawaida. Hili pia linaambatana na kulipwa na kupewa stahiki zao zote.

Pia suala la madaktari na familia zao kuwa na Kadi ya Bima ya Afya ya kijani( Green Card) limekubaliwa na kwa sasa tusubiri utekelezaji.

Pia ilikubaliwa kuwa madaktari watapata fursa ya kukopeshwa magari kama watumishi wengine wa umma.

Mbali na madai hayo, pia Mh. Waziri Mkuu alitoa ufafanuzi juu ya madai yanayuhusu maslahi ya watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na Mishahara na Posho na stahiki mbalimbali. Lakini hata, Mh waziri Mkuu hakutoa majibu ya moja kwa moja ya kiwango gani kitakachoweza kulipwa na Serikali kama mishahara, posho na stahiki mbalimbali kwa minajili kwamba bado zinafanyiwa kazi na kamati ya wataalamu aliyoiunda ili waweze kumshauri. Aidha, Mh waziri Mkuu alisema kuwa kwa wakati huu inaweza kupandisha “on call allowances” za kada mbalimbali za afya kutoka shilingi 3,000 – 10,000/= na kufikia kati ya shilingi 5,000 hadi 25,000. Madaktari bado wanaona ongezeko hili halilingani na ukubwa wa kazi ifanywayo pindi mtumishi wa afya anapokuwa “on call” na hivyo basi kuendelea kupendekeza kuwa “on call” allowance iwe ni 10% ya mshahara wa mtumishi husika.

Pia Mhe, Waziri Mkuu hakuweza kueleza kinagaubaga mkakati kazi wa uboreshaji wa huduma za afya wapatayo wananchi wa Tanzania.

Baada ya tamko hilo la Serikali kumalizika, Mh Waziri Mkuu na ujumbe wake waliondoka, na Mkutano huo ukaendelea kwa Kamati kufanya Mkutano na madaktari wote, lengo ikiwa kujadili tamko hilo na kutoa maazimio.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, madaktari walikubaliana kwamba; kwa kuwa Serikali imeanza kuonyesha nia ya kutatua tatizo hili kwa kutekeleza baadhi ya maazimio yetu, wajumbe kwa niaba ya madaktari wote nchi nzima tulikubaliana na kuazimia yafuatayo;

Kurudi kazini mara moja kuanzia kesho tarehe 10.02.2012 bila masharti yeyote.

Kamati ya jumuiya ya madaktari kama sehemu ya MAT kuendelea kukaa mezani ya majadiliano na Serikali ili kuanza kupitia madai hasa yale yanayohusu maslahi.

Kukutana tena tarehe 03.03.2012 ili kupata mrejesho wa kiwango cha utekelezaji wa madai hayo kwa mujibu wa vikao vya majadiliano na makubaliano na hatimae kuchukua hatua zaidi.

Kujadili utekelezaji juu ya Kuwawajibisha Waziri na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi na Jamii.

Mwisho kabisa Madaktari wote kwa ujumla wake walilaani na kukemea kitendo cha Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwahoji wanaharakati wa haki za kibinaadamu na mashirika ya kijamii wakiwemo Dr. Hellen Kijo-Bisimba na Mama Ananilea Nkya na wanaharakati wengine wote waliokumbwa na kamata kamata hiyo na hivyo basi tunalitaka jeshi hilo kuwaachilia huru mara moja bila masharti yeyoye.

Pamoja Tunaweza

Imetolewa na Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari Tanzania

Dr, Ulimboka Stephen
Mwenyekiti.

Monday, February 06, 2012

Bibi Yake Rais Obama Apata Ajali ya Gari Kenya!

Wadau, Bibi yake Rais Barack Obama, amaepata ajali ya gari Kenya. Bibi Obama ana miaka 91.
Mungu yu mwema na hakuumia sana.  Kweli alikuwa na malaika alivypata ajali.

********************************

A man looks inside the car that President Barack Obama's grandmother Sarah was in when it rolled in Kisumu, Kenya, Feb. 4, 2012. (Courtesy Nation Media)
 President Obama's Grandmother in Car Accident

By Bazi Kanani

NAIROBI - President Obama's grandmother, Sarah Obama, is home recovering at her home in western Kenya after an accident that, judging by the condition of the vehicle, could have been much worse.

"God is with me, because if you could have seen the wreckage that we came out of safe, one would wonder," Sarah Obama said Monday.

Police in the town of Kisumu say the 91-year-old was traveling to her home in the village of Kogelo Saturday night when the driver lost control, and the vehicle rolled into a ditch.

All five people in the car, including her two bodyguards, were taken to a hospital for treatment. All were released with minor injuries.

A hospital spokesperson says Sarah Obama was bruised and in shock when she arrived at the hospital. She was released about two hours later.

"You can see I was not injured save for this small scar on my right hand and I am not even using a walking stick," Obama said.

She said friends from as far away as the United States and the Middle East have been calling to check on her, but she assures them, "Hakuna tabu!" That means 'no problem' in Swahili.

Sarah Obama is the step-mother of President Obama's Kenyan father. She has been to the U.S. a few times, and the President has been to the village to visit with her and other relatives three times. In his memoir, "Dream from my Father," Obama called her "Granny."

Mimba na Siri ya Precious

Imeletwa na Mdau YM:

Mimba na Siri ya Precious

MIMBA
Mimba ilitungwa baada ya baba kutoa hongo kwa kimada

Ili kuthibitisha kama ni mimba kweli kimada akatoa rushwa kwa daktari ili apimwe harakaharaka kwa kuwa kulikuwa na msongamano wa wagonjwa

Kila alipoenda kliniki wakati wote wa Ujauzito alitoa 'chai' ili ahudumiwe vizuri na wauguzi na madaktari

Hata wakati wa kujifungua akatoa 'chai' kwa manesi apate huduma safi

BAADA YA KUJIFUNGUA
Baada ya kujifungua aliendelea kutoa hongo awe wa kwanza kuhudumiwa, mwanae awe wa kwanza kuchomwa sindano za Chanjo n.k.

Mwanae akaitwa 'Precious'

ELIMU KWA PRECIOUS
Kuandikishwa chekechekea akatoa hongo ili Precious apate nafasi katika shule nzuri kwa kuwa nafasi zilikuwa chache, Precious anaangalia

Kuandikishwa shule ya msingi mchezo uleule, Precious anaangalia

Tena sekondari akatoa 'Chai' kwa mwalimu wa Hisabati ili Precious apate alama nzuri

Chuo kikuu Precious hali ikawa ngumu, akagawa uroda kwa mkufunzi ili apate alama nzuri

KAZI
Precious akagawa uroda ili apate kazi, akapata

Precious akatishiwa mara kwa mara kufukuzwa kazi kutokana na utendaji mbovu kinga ikawa ni kugawa uroda

Akatumia nafasi yake kwa manufaa yake binafsi

Kwa tamaa ya vitu vya thamani kuliko mshahara wake akaendelea kupokea rushwa

NDOA
Kwa kuwa wazazi wake (baba yake) hakuwa mwaminifu katika ndoa yake (Precious ni mtoto wa kimada), naye Precious hakuona sababu ya kuwa mwaminifu ktk ndoa

Watoto wake wote walifuata mlolongo kama wa kuzaliwa kwake

KIFO

Hata alipougua ghafla , hongo ikatumika apate huduma bora lakini Mungu alimpenda zaidi

Walipoenda kuchonga jeneza, wakakuta kuna order nyingi ikabidi watoe 'Cha Juu' ili kuchukua jeneza lilokuwepo tayari

Wakati wa mazishi Kwaya iliyotakiwa kuimba wakati wa Maombolezo ilikuwa na safari , ikapewa 'cha juu' ili kuahirisha safari

MWISHO

Kwaya ikaimba na Kumsifia Precious alivyokuwa 'mtumishi mwema wa Mungu', tena wakamwomba Mungu ampokee kwa mikono miwili , amuepushe na Moto wa milele.

Risala ikasomwa, na kusifia utumishi wake uliotukuka, tena kaacha pengo lisilozibika.


TAKE HOME MESSAGE
Wazazi 'huwapakaza' watoto wao matope ya dhambi toka pale mimba inapotungwa hata baada ya kuzaliwa

Watoto wote huakisi tabia walizojifunza toka kwetu, kama wazazi (Observational Learning)

Kama hatuwezi kuwa wawazi hasa pale kaburini hata kwa mtu aliyekufa na sifa mbaya akasifiwa basi tunahalalisha matendo mabaya aliyoyafanya marehemu.

Ili Kupambana na Rushwa twahitaji kuanzia wakati wa Ujauzito, mtoto azaliwe bila rushwa, akue bila rushwa n.k

KWA LEO NI HAYO TU!!!

Aolewa na Wanaume Wawili huko Katavi!

Sijui ilitoka kwenye gazeti gani. Lakini kwa kweli nimependa ushujaa wa huyo Mama Kaela!

********************************************************
MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME WAWILI


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani hapa, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zililifikia gazeti hili na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Ndugu wa Arcado wao wanalaani kitendo cha ndugu yao kuolewa na mama huyo, wakidai kuwa walishamshauri na kumuahidi kuwa endapo ataachana na mama huyo watamwozesha mwanamke mwingine, lakini yeye Arcado, amedai kuwa yuko tayari kufa, lakini si kuachana na mama huyo, kwani ndiye ubavu wake wa maisha.

“Sasa tumebaki tunamwangalia tu huyu ndugu yetu Arcado, tumemshauri, lakini mkaidi, hatusikilizi. Basi nasi hatuna la kufanya zaidi ya kumwangalia,“ alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Arcado. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Florence Katobasho, alikiri kuwa mwanamke huyo anaishi kinyumba na wanaume wawili na wanaishi kwa amani kwani hajawahi kufikishiwa malalamiko yoyote kuhusu wanandoa hao.

“Ni ukweli usiopingika, kwamba Mama Kaela anaishi na wanaume hao wawili … lakini kwa kuwa sijafikishiwa malalamiko yoyote kuhusu maisha ya wanandoa hao, mimi kama kiongozi hapa sina la kufanya na siwezi kuwafukuza, kwa kweli wanaishi kwa amani, mengine ni yao,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji

SOMA   ZAIDI http://www.fotobaraza.me/profiles/blogs/mwanamke-aolewa-na-wanaume#ixzz1lVfLAlP4