Wednesday, April 27, 2016

Kwa Diaspora Wanaotaka Kununua Nyumba Tanzania

National Housing Corporation (NHC) Tanzania Presentation in NYC

The Corinthian, New York, NY

Event Description

Have you thought about purchasing a home in Tanzania while living in the diaspora, but don't know how to get started? Did you miss the 2016 DICOTA Convention, but still want to learn first hand how NHC's programs work?  Well, you don't have to wonder any more.
Ms. Sophia Said Mwema, Senior Sales Manger, National Housing Corporation - Tanzania will be in New York City on May 2nd, to share information on NHC's various housing projects, with Tanzanians living in the metro NY, NJ, CT and PA area.  The discussion will focus on NHC's current housing projects and provide details on how the home buying process works.
This is an event not to be missed.  This even is free, so register now!
Note: Light refreshments will be served!
For more information on NHC, visit http://www.nhc.co.tz/en/
WHEN
WHERE
The Corinthian - 330 East 38th Street 4th Floor, New York, NY 10016

Wednesday, April 20, 2016

Msiba Texas, USA - Andrew Sanga

❗DEATH   ANNOUNCEMENT
   **ANDREW  SANGA***

---With our deep sorrow, we are sad to let you all know that Andrew's heart suddenly stopped.05.45pm Leading to his death.

---We thank you all for all the prayers, and we should please continue praying for his and our peace as family, friend's, employer's, co-workers, Houston community and All his friend's  and family from all over the world are acknowledged as well.

From Andrew's Family

--Daudi  Mayocha
THC President
(Tanzania Houston Community)

*******"***************
Bwana Yesu asifiwe sana wapendwa!
Hii ni siku nyingine ya pili ya wiki Jumatano, siku tuliyopewa na Bwana wetu ni siku yenye baraka. Hii siku tumeichagua maalum kufunga na kuiombea faraja familia ya Andrew Sanga ambaye ametutoka jioni hii.
Karibu sana kwenye maombi yetu yanayoanza sasa. Tafadhali, jiunge pamoja nasi kwa kupiga simu  namba 218-339-8459 ikifuatiwa na Pass code 256445#.
Kwa wale walio nje ya USA anza na '+1'.
Mbarikiwe sana 🙏🙏

Saturday, April 09, 2016

Waziri Ummy Mwalimu Atembelea Hospitali za Mkoa wa Mbeya

Waziri Ummy Mwalimu atembelea Hospitali za Mkoa wa Mbeya
Na Catherine Sungura, Mbeya
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara katika hospitali zilizopo Mbeya na kuzitaka hospitali zinazotumia mfumo wa ukusanyaji mapato wa kieletroniki wasibweteke na mapato wanayoyakusanya kila siku.
Rai hiyo imetolewa na aziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali ya rufaa ya kanda ya mjini Mbeya.
Ummy alisema ukusanyaji wa mapato kwa mfumo huu unasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha huduma za afya nchini ikiwemo ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba pamoja na utoaji wa motisha kwa watumishi.
"Bado tunatambua hali ya uhaba wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kuanzia ngazi zote, tukiweza kusimamia vizuri hili tutafanikiwa," alisema.
Aidha alisema wanatarajia katika serikali ya awamu hii bajeti ya dawa itaongezeka zaidi ya mara tatu kulinganisha na bajeti za nyuma, hivyo wameishauri Bohari Kuu ya Dawa (MSD) wanunue dawa toka kwa wawekezaji wa hapa nchini ambapo itakua na bei nafuu na itaongeza tija na upatikanaji wa dawa kwa haraka.
Waziri Ummy Mwalimu aliutaka Mkoa kufuatilia, kuwafichua na kuwachukulia hatua wale wote watakaojihusisha na wizi wa dawa.
"Tunao watumishi wachache wa afya ambao wanahujumu na kuiba dawa na kuzipeleka kwenye maduka ya dawa binafsi, hao hatutowafumbia macho na kuwapeleka mahakamani"
Kuhusu upungufu wa watumishi wa kada ya afya nchini, Waziri wa afya alisema, nchi ina upungufu wa asilimia 52, hivyo serikali inatarajia kuajiri watumishi takribani elfu kumi hivi karibuni ambao watatawanywa nchi nzima ikiwemo mikoa iliyo pembezoni.
Katika hospitali ya uzazi ya Meta, waziri huyo ameguswa na ufinyu wa wodi za wazazi na kupelekea mama wajawazito na waliojifungua kulala chini na wawili wawili kwenye kitanda kimoja na hivyo kuwataka kufanya haraka ujenzi wa jengo jipya litakaloondoa mrundikano wa mama wajawazito na watoto njiti.
Hospitali ya Kanda ya Rufaa Mbeya inakusanya kwa mwezi kiasi cha shilingi Milioni mia tano na pia inahudumia mikoa saba nchini na kuhudumia zaidi ya watu milioni mbili.
46e02c3a-bc41-4fed-9ff6-a180f42fa264
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akisalimia na watumishi mara alipofika kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mbeya.
afc64d2e-46a1-49a8-be9b-59340b6d8a8a
Waziri Ummy akimsalimia mtoto Jenifer Joel (9) mkazi wa Chunya aliyelazwa hospitalini hapo.
5f7ab771-5109-4c0c-95e6-83931c8ec108
Waziri wa afya akimjulia hali mtoto Baraka Jekonia (1) mkazi wa Chunya aliyelazwa wodi ya watoto, Waziri Ummy ameitaka hospitali hiyo kuwachaji pesa wagonjwa wote wanaofika hospitali ya rufaa moja kwa moja bila kupatiwa rufaa kutoka vituo vya afya vilivyopo jirani na wananchi ili kupunguza msongamano kwenye hospitali za rufaa nchini.
8e796dee-b674-43f7-97f8-3bad1046087d
Katika hospitali ya uzazi ya Meta, Waziri Ummy Mwalimu alimsalimia Binti Kanisia Komba aliyejifungua mtoto wa kike katika hospitali hiyo mama wajawazito wote wanatibiwa kwa kadi ya bima ya afya inayodhaminiwa mpango wa kusaidia akina mama wajawazito wa KFW toka Banki ya Ujerumani.
9518e21d-3e1e-43ad-a96a-c9b85ce91018
Hospitali ya Meta tayari imetekeleza maagizo ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ya kutoa kipaumbele kwa wazee wote nchini wanapofika kwenye vituo vya kutolea huduma.
974627cc-137b-436b-996a-f364952f7580
Waziri Ummy akiwasalimia wazazi waliolazwa kwenye moja ya wodi Hospitali ya Meta kutokana na ufinyu wa wodi inawalazimu akinamama wengine kulala chini hospitali hiyo inatarajia kuanza ujenzi wa jengo jipya ambalo litaondoa msongamano wa wazazi hospitalini hapo.
5b44d003-a727-495c-bde5-dea332ef407f
Waziri wa Afya akiwasalimia wagonjwa waliofika Hospitali ya Uzazi ya Meta kupata matibabu.

Thursday, April 07, 2016