Friday, November 23, 2007

Sofia Productions wataandaa Fimbo ya Mnyonge Awards


Kampuni ya Sofia Productions, inayoshugulika na mambo ya filamu na muziki Tanzania imechaguliwa kuandaa tuzo za filamu Tanzania zitakazoitwa 'Fimbo ya Mnyonge Film Awards 'kutoka Baraza la Sanaa la Taifa. Naona ndo zitakuwa Oscars zetu Tanzania!

Habari hizo zimethibitishwa na meneja mkuu wa Sofia Productions, Bwana Musa Kissoky.

Tuzo hizo wanatarajia kuzifanya mapema mwakani kati ya mwezi March na April.

Kwa kweli fani ya sinema inashamiri siku hizi Tanzania, tunangojea kwa hamu kuona washindi wa Awards!

No comments: