
Taylor Hicks, mwenye mvi na kakitambi kashinda American Idol 2006! Katharine MacPhee aliyefika mbali kwa ajili ya uzuri wake kawa wa pili. Kwa kweli Katharine sikumwona kama ana cha zaidi ila nilimwona kama 'clone' wa waimbaji waimbaji wengine. Taylor ni Taylor, mtu wa aina yake.
Safari ya Taylor mpaka kuwa mshindi ni ndefu. Kwanza Jaji Simon Cowell, hakumtaka. Waliompitisha kwenda Hollywood kwenye mashindano ni majaji Paula Abdul na Randy Jackson.
Kwenye audition Simon alimdhalisha kwa kumwambia unaonekana Mzee, unataka nini hapa.
Lakini lazima niseme kuwa siku zote Taylor alikuwa na heshima kwa wote. Pia hakuficha kuwa ni mpenzi wa muziki wa weusi hasa Ray Charles na Stevie Wonder. Wapenzi wake wanajiita Soul Patrol, na kila akiimba lazima awataje. Utasikia, Soul Patrol, Soul Patrol. Lakini nilijua kuwa anpendwa hasa nilipoona watoto wadogo wanavaa mawigi enye mvi kumwiga na kuona wanamwiga kwenye show ya vichekesho, Saturday Night Live.
Kama mliangalia show jana lazima mlifurahia. Mandisa na Paris walikuwepo pamoja na wenzao waliokuwa katika waimbaji kumi bora mwaka huu. Sijawahi kuona show ya kumaaliza season kama show ya jana. Paris alimba na Al Jarreau, Taylor alimba na Toni Braxton, Elliott alimba na Mary J. Blige, wote kumi bora waliimba na Dionne Warwick! Halafu kwa kumalizia Prince kaimba!
Namtakia mafanikio mema katika uimbaji na pia huu mwaka anayokaa kama American Idol. Kama hakujua utajiri, ataujua sasa.
Nangojea kwa hamu kuona nani atashinda American Idol 2007.