Showing posts with label American Idol. Show all posts
Showing posts with label American Idol. Show all posts

Saturday, February 09, 2013

MTanzania Agombea American Idol



Sanni alitolewa tarehe 7/2/13 (February 7th), lakini kijana ana kipaji. Atafika mbali.

Tuesday, January 26, 2010

General Lee Platt Apata mkataba wa KuRekodi!

Ukiwa na ndoto siku mja unaweza kufanikiwa. Ona huyo Mzee General Lee Platt (62) alijaribu bahati yake. Kaenda kwenye majaribio (auditions) za American Idol ingawa alikuwa na umri mkubwa. Ingawa hakuchaguliwa kwenda fainali hivi sasa ni staa. Na amepata mkataba, utaona video na CD hivi karibuni!

http://www.gather.com/viewArticle.action?articleId=281474978005721&grpId=3659174697244816

Thursday, June 18, 2009

Fantasia Barrino

Mnamkumbuka Fantasia Barrino, aliyeshinda American Idol Season Three. Hizi picha alipiga hivi karibuni, naona mambo yake yananoga siku hizi!

***************************************************************

Wednesday, June 25, 2008

Ruben Studdard Anaoa!


American Idol wa mwaka 2003, Ruben Studdard (29) (Pichani kulia) anaoa. Habari zinasema kuwa Ruben aka. Velvet Teddy Bear, atamwoa, Bi Surata Zuri McCants (30) jumamosi hii inayokuja!
Kama mtakumbuka alivyoshinda Ruben kulitokea maneno ya kibaguzi. Watu walitaka huyo shoga Clay Aiken ashinde kwa vile ni mzungu. Lakini Ruben na sauti yake tamu kama hayati Luther Vandross alifanikiwa kulewesha watu na ndiye aliyeshinda.
Ruben anatoka Birmingham, Alabama, na Bibi arusi anatoka Atlanta, Georgia. Nawatakia maisha mema ya ndoa.
**************************************************************

BIRMINGHAM, Ala. (AP) — He won the affection of millions of people on "American Idol," but this weekend, Ruben Studdard is giving his heart to one woman.

A representative for the former "Idol" confirmed to The Associated Press on Tuesday that Studdard, 29, plans a Saturday wedding. He and Surata Zuri McCants, 30, took out a marriage license on Monday, according to court records.

The Birmingham native, nicknamed the "Velvet Teddy Bear" on the show for his big frame and sonorous voice, has released three albums since his 2003 win, including the platinum CD "Soulful." He is working on a new album.

Thursday, April 10, 2008

American Idol


Wadau mnamkumbuka huyo jamaa? Alikuwa moja wa contestants wa American Idol. Paula Abdul almwambia aende akanyofoe hizo nywele kwenye kifua. Alitoka alirudi kifua peupe. Hawakumchagua! LOL!

Tuesday, March 04, 2008

American Idol in WANAFIKI!

Antonella Barba (kushoto) Frenchie Davis (Kulia)
David Hernandez
UPDATE 3-5-07 Producers wa American Idol wameruhusu David Hernandez kubaki! Kweli ni wanafiki. Frenchie alionyesha matiti yake, huyo njemba alikuwa uchi wa nyama! Unafiki kabisa! BOFYA HAPA kusoma UPDATE
****************************************************************************

Leo nimechukia sana kusikia kuwa mmoja wa contestants wa American Idol mwaka huu, David Hernandez, aliwahi kuwa stripper! Tena alikuwa anavua ana nguo kabisa na kubakia uchi wa nyama na kucheza ma lap dance! Ustripper huo alikuwa anafanya kwenye bar ya mashoga/wasenge. Hao aliokuwa anawachezea lap dance ni wanaume. Alifanya hiyo kazi kwa muda wa miaka mitatu.

Ukweli nisingejali kusikia habari kama hizi. Maana kwa hapa Marekani kuna watu wengi wanaofanya kazi ya stripper na kucheza hizo lap dance. Tena huyo David anaimba vizuri kweli.

Kinachoniudhi tena sana ni hivi. Kuna dada fulani, mmarekani mweusi, Frenchie Davis, amabaye aliwahi kufukuzwa na producers wa American Idol mwaka 2003. Kisa cha kufukuzwa kwake, alipiga picha akiwa nusu uchi matiti yanaonekana. Frenchie aliwaambia producers mapema kuhusu historia yake na alisema kuwa alikubali kupiga picha hizo kwa vile alihitaji pesa za kulipia ada zake Chuo Kikuu.
Producers hawakumwonyesha huruma hata kidogo Frenchie, alifukuzwa kama mnyama. Je, ni sawa? Kuna watu ambao wanasema kuwa ni wazi kuwa American Idol wana 'double standard'. Pia kuna watu ambao wanataka Hernandez atolewe kwenye mashindano mara moja maana si mfano mzuri kwa vijana na si mtu anayestahili kuitwa 'American Idol'

Mwaka jana kuna binti wa kizungu, Antonella Barba ambaye naye alikuwa na picha kwenye interenet lakini hwakumfukuza.

American Idol wamwombe msamaha Frenchie au wamrudishe apate chensi kama walivyopata hao wazungu waliofanya maovu zaidi yake. Mnasemaje?

Kwa habari zaidi someni:

http://www.mtv.com/news/articles/1582721/20080304/id_0.jhtml

Thursday, May 24, 2007

Mshindi wa American Idol 6 ni Jordin


Natoa pongezi kwa Jordin Sparks aliyeshinda American Idol 6 jana. Ana miaka 17 tu na anasoma darasa la 11 (Form 3). Ni mshindi mwenye umri mdogo kuliko wote waliowahi kushinda.

Baba yake ni mcheza footbal (American style) mweusi, na mama ya ni mzungu. Huyo Jordin ni mrefu na ana mwili. Alifmfanya Ryan Seacrest aonekane kama pygmy kwake.

Kwa uimbaji, sijamfurahia sana. Ila aliimba vizuri kuliko aliyebaki, Blake, kijana wa kizungu aliyependa kutia ma beatbox kwenye nyimbo zake.

Wenye sauti nzuri Melinda na Lakisha walitolewa wiki kadhaa zilizopita. Wanasema watazamaji wa America Idol walipungua kwa vile show mwak huu haikuwa nzuri. Nsiyohaikuwa nzuri, maana walitoa waliojua kuimba mapema. Wengi walikuwa wanaume weusi. Tungojea January 2008, kuona American Idol y itakuaje.

Thursday, May 17, 2007

Kwa Heri Melinda! American Idol IMEOZA!

American Idol imepoteza watazamaji wengi baada ya kutolewa kwa Melinda Doolittle (29) jana.
Waliobaki sasa ni kijana wa kizungu Blake na shombe Jordin. Blake sijapenda staili yake maana anaimba huko anafanya ma beat box, halafu Jordin basi tu ndo wiki hizi za mwaisho ndo kajitahidi sana lakini sijaona kama anasthahili kushinda.

Nimechukia sana kwa sababu hakuna wiki tangu walivyoanza kuonyesha msimu huu kuwa Melinda alikosea wimbo. Ana sauti nzuri ajabu na majaji wote walikubali hivyo. Yeye kati wa wote waliochaguliwa katika Top 24, ndiye alishahili kushinda.

Lakini mshndi anachaguliwa na watazamaji. Na tunajua kuwa bado kuna ubaguzi Marekani. Ukiingia kwenye bodi ya American Idol utaona wanavyotukana waimbaji weusi. Insikitisha kweli kweli.

Haya tuone nani atashinda wiki ijayo, lakini mimi sitazami. Nitaona matokeo kwenye taarifa ya habari. Kwa nini nipoteze muda kuangalia watu wasiostahili kuwa Idol wawe pale? No nitangalia Sopranos reruns! Huenda Tony ataweza kuwawahack hao producers wa show!

Msimu wa sita wa American Idol umeoza kweli kweli.

For the benefit of non Swahili speaking readers, I say that American Idol is rotten and stinks! Is it a talent contest or a popularity contest?

Thursday, May 10, 2007

Kwa Heri Lakisha!


Jana kwenye American Idol, Lakisha Jones alitolewa kwenye mashindano. Kwanza nashukuru kuwa aliweza kufika mpaka kuwa namba 4! Nilikuwa na wasiwasi angetolewa mapema maana wtau walikuwa wanamwita 'Fantasia Part 2' kwa vile ana mtoto. Na kwa kweli sikufurahi kuona Simon Cowell anampiga busu kwenye mdomo wiki iliyopita. Nilijua wazungu watachukia kuona hivyo. Wengi hawajui kuwa mchumba wa Simon Cowell ni mweusi.

Watu wanasema kuwa Show siyo nzuri mwaka huu, kwa vile waimbaji wengi hawana sauti za kuvutia mno kama za mastaa. Nalaumu majaji wa American Idol kwa sababu kulikuwa na waimbaji wzuri lakini hawakuchaguliwa. Kulikuwa na vijana wengi wa kiume wenye sauti za ajabu, lakini hata hatukuwaona kwenye finals! Badala yake walichagua wahuni kama yule malaya Antonella, na Sanjaya asiyeweza kuimba kusudi ratings ziwe juu. Watu wamechukia na ratings zimeshuka! Wameahidi mwaka kesho watakarabati jinsi wanavyochaga waimbaji.
Kwa kweli Lakisha ana suaiti nzuri, anaweza kushindana na Jennifer Hudson. Nina imani kuwa atenda mbali. Tutasikia ana contract hivi karibuni.

Bado wiki mbili za mashindano. Je, mshindi atakuwa Blake, Melinda au Jordin?

Ningependa kuona Melinda akishinda. Kwa kweli ana sauti nzuri mno na hakuna wiki aliimba vibaya.

Thursday, April 19, 2007

Kwaheri Sanjaya!









American Idol Judges Randy Jackson, Simon Cowell, & Paula Abdul

Kwa wapenzi wa American Idol naomba maoni yenu. Huyu kijana Sanjaya aliwezaje kukaa kwenye American Idol kwa muda wote huo? Jana alivyotolewa nilibakia nashabikia kwa furaha maana hakustahili kufika hadi kuwa namba 7 kati ya waimbaji kumi na wawili bora.

Sanjaya ni shombe wa kihindi kutoka Washington State. Ana miaka 17. Mama yake ni mzungu na baba yake ni mhindi. Ana nywele nyingi nyeusi, na sauti yake ni ndogo na ya kike kike kama ya Michael Jackson. Anaweza kuimba nyimbo za stevie wonder vizuri. Akiimba wasichana wadogo wadogo wanaanza kulia shauri ya kuingiliwa na kiwewe fulani. Watu wanasema baba yake kamfanyia dawa za kihindi maana hana sauti ya kuwa American Idol.

Watu kama Howard Stern na wengine wenye chuki walifanya kampeni za kupata watu wa kumpigia kura ili ashinde. Mungu ni mwema na wameshindwa! Sanjaya katoka jana kwa majonzi. Alivyoambiwa ndo siku yake ya mwisho, alibakia analia kama mtoto mdogo.
Kitu kilichowafanya wasichana wadogo wadogo wampende ni, kutabasamu kwake, nywele nyingi (kila wiki alibadilisha staili ya nywele), na eti ana sura nzuri yaani handsome. Lakini kuimba hawezi. Watu waliokuwa wanaimba vizuri kama Stephanie Edwards, Brandon na Gina Glocksen walitolewa kabla yake.

Picha aliyepiga dada yake, Shyamali, akiwa uchi huko anapiga gitaa ilimsaidia pia. Shyamali aliwahi kufanya kazi kwenye restaurant ya Hooters. Alitolewa zamani wakati walivyobakia waimbaji 48.
Bora hakushinda maana kuendelea kuwepo kwake ungehatarisha maisha yake, maana nchi hii kuna vichaa. Angepigwa risasi na mtu mwenye chuki eti kawa nini Sanjaya anaharibu show.

Na leo naamini kuwa producers wa American Idol wanapumua vizuri. Maana Sanjaya angeshinda ingekuwa mwisho wa American Idol maana ushindi wake ungehibitisha kuwa American idol siyo kamchagua anayejua kuimba, bali anayependwa na watu.

Lakini huo si mwisho wa Sanjaya. Kwa vile kapendwa sana lazima tutamwona kwenye matangazo ya TV, au akiigiza kwenye sinema za mateenager.

Thursday, March 08, 2007

Ni Ubaguzi, Uonevu au Upendeleo?

UPDATE: ANTONELLA KATOLEWA ALHAMISI. Alilia kweli. Lakini amepata offers za kupiga picha uchi Playboy magazine na ku-host Girls Gone Wild. Frenchie ata sue American Idol kwa uonevu!
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@



Kwa wapenzi wa American Idol, naomba maoni yenu. Mnakumbuka mwaka 2003, (msimu wa pili aliyoshinda Ruben Studdard) kulikuwa na dada fulani, Frenchie Davis. Huyo dada ni mweusi, mnene na ana zinga la sauti. Yaani anaimba huyo si mchezo, Jennifer Hudson alie kwake.

Kwa bahati mbaya, Frenchie aliwaambia Producers kuwa akiwa mwanafunzi, alipiga picha nusu uchi (topless) kwa ajili ya kupata pesa za kumsaidia kulipia masomo yake Howard University. Producers waliamua kumfukuza kwenye show. Mungu ni mwema na Frenchie sasa ni mwimbaji maarufu kwenye mchezo wa kuigiza, Rent, huko Broadway, New York.

Msimu huu wa American Idol kuna dada fulani, Antonella Barba, ambaye naye ali picha za uchi kwenye internet. Hajafukuzwa na bado yumo. Amepiga picha za uchi kabisa. Kwenye picha zingine anamfurahisha mwanaume kwa kumnyonya ume wake! Zingine kapanua miguu. Loh! Ajabu hajafukuzwa kwenye American Idol.

Sasa imekuwa issue, mpaka Rosie O’Donell anaongelea kwenye show yake The View, yeye anasema kuwa eti ni ubaguzi. Pia wiki hii kulikuwa na maandamano mbele ya Kodak Theater Hollywood kupinga Antonella kuendelea kuwa kwenye show wakati Frenchie alitolewa.
Na Frenchie mwenyewe sasa anataka maelezo kutoka kwa Producers wa American Idol. Anasema kuwa anamtakia huyo Antonella mema lakini ni lazima wamweleze kwa nini alitolewa na kudhalalishwa wakati ule na picha zake siyo mbaya kama za Antonella.

FYI- Producers wanajitetea kwa kusema eti Frenchie alilipwa hela kwa ajili ya zile picha wakati za Antonella zilibandikwa na boyfriend wake.

Mimi navyoona ni ubaguzi. Frenchie ni mweusi na ni mnene. Huyo Antonella ni mwembamba na wanasifia uzuri wake. Lakini jamani uwongo mbaya, Antonella hawezi kuimba.

Mnasemaje wasomaji?

Kwa habari zaidi soma hapa:

http://www.showbuzz.cbsnews.com/stories/2007/03/06/tv_realty_tv/main2540578.shtml?source=RSSattr=Entertainment_2540578

Thursday, May 11, 2006

American Idol Inashangaza Mwaka huu!

kuanzia kushoto (Elliot, Chris, Katharine & Taylor)


Haya wapenzi wa American Idol, pigo lingine! Chris Daughtry, aliyetabiriwa kushinda mwaka huu katolewa jana! Majaji, na watazamaji walibakia kushangaa. Tulisikia watu waliokuwa studi wakilia, "Noooooo!"! Lakini haikufikia mshangao kama siku ile alivyotolewa Dada Mandisa.

Sasa wamebakia Taylor Hicks (mwenye mvi), Eliiot Yamin (MYehudi na anaumwa ugonjwa wa kisukari), na yule dada aliyesoma Boston Conservatory, Katharine MacPhee. Nani atashinda! Inabidi tungojee May 24th kupata jibu.

Lakini ukweli watu wengi wanashangaa maana kwa wanaume waliobakia hakuna ambaye ungeweza kusema atakuwa ni Idol. Kwanza Taylor ana miaka 29 na ana mvi kibao wengine wanamwita, 'The Old Guy' (Mzee). Lakini jamaa ana character, utampenda tu, ni mcheshi sana na lazima akimaliza kuimba utabakia aunatabasamu. Sasa huyo Elliot wengine wamesema ana sura mbaya, halafu wanamchukia kwa vile Myehudi. Ndio Marekani bado kuna chuki dhidi ya waYehudi. Halafu Elliott mara nyingi anaonekana mwoga na kutoka majasho akiimba. Lakini ana sauti nzuri kiasi.

Haya nimchambue huyo Katharine MacPhee. Hao mibaba wa kizungu inasema, "She's Hot!" Yaani mzuri mno! Mara wapambe wa American Idol wamvalishe nguo mbaya mara nini, lakini bado wanasema ni mzuri mno. Ana sauti nzuri kushinda wanawake wa kizungu wote waliokuwepo mwaka huu. Lakini watu wanachoona ni uzuri wake. Na wiki hii Katharine ndo aliimba vibaya kuliko wote. Alisahau na maneno ya wimbo. Lakini kapita shauri ya uzuri.

Wiki iliyopita alitolewa mweusi pekee aliyebaki, Paris Bennett. Huyo alikuwa na sauti nzuri kuliko wote katika mashindano safari hii, lakini nilijua hatafika mbali, maana bibi yake ni mwimbabji mashahuri na anatuzo za Grammy. Watu walikuwa wanalamika kuwa kwa nini Paris awe kwenye show wakati ana ndugu ambao wanaweza kumsaidia kupata mkataba.

Lakini kulikuwa na njama ya kutoa weusi mapema. Mwanaume mwenye sauti bora kuliko wanaume wote, kijana mweusi Gedeon, alitolewa kwenye Top 24. Na watu walisema kuwa si siri kuwa mwaka huu Producers wa show wanataka mwanaume mzungu ashinde. Kwanza walimpampu huyo Ace kuwa sex symbol, mpaka kumfanyia camera angles na ma close up! Lakini hazikusaidia katolewa wiki kadhaaa zilizopita! Jamaa hakuwa na sauti nzuri, na hata huo uzuri wa sura sijaona. Lakini nasikia anatakoa kwenye gazeti la 'Playgirl' kwa hiyo huenda ni kweli ni sex symbol ana uzuri sehemu nyingine.

Haya, tutaona mwaka huu nani atashinda na kuungana na klabu ya American Idols. Washindi wa miaka ya nyuma ni Kelly Clarkson, Ruben Studdard, Fantasia Barrino, na Carrie Underwood.
Ukweli American Idol umekuwa ni nani anapendwa zaidi, na siyo nani ana sauti bora. Mnaonaje?