Monday, October 30, 2006

Wacheza sinema wanatafutwa kwa ajili ya Bongoland 2!

Kwa walio na ndoto ya kuigiza katika sinema, hii ni nafasi yako. Samahani lakini sitatafsiri posti na ni kimombo.

Ni hivi Josiah Kibira aliyetengeneza sinema za Bongoland na Tusamehe yuko mbioni kutengeneza sinema nyingine. Sinema hiyo ni Bongoland 2, na itapigwa Tanzania mwakani.

Casting Call ni hii hapa chini
:


SWAHILI SPEAKING ACTOR WANTED

By, Josiah Kibira

Kibira Films International is currently looking actors for its upcoming project to be filmed next year in Tanzania - July 1st - July 31, 2007 This new movie is a sequel to the movie Bongoland which was produced in 2003 by Kibira Films. Bongoland was/is a drama about different challenges that immigrants face once they arrive in the foreign land. It dealt with issues of immigration papers, employment, school and relationships. The main characters asked - "would you rather be a well fed slave or a hungry freeman"? He asked this while contemplating whether to keep chasing the ever elusive American dream or go back to his native land.

The sequel is a continuation of that drama following the main character Juma to see if his dreams for a better life were fulfilled after he decided to go back to his native Bongoland. The working title for the movie is "Bongoland II - There Is No Place Like Home."

Here are the qualifications for the post:

[1.] Be a male actor. [2.] Fluent Swahili speaker.[ 3.] Some film or stage acting - not necessary but would be helpful. [4.] Have seen the movie "Bongoland" [5.] Currently living in the United States [6.] Have legal status to travel in and out of USA. [ 7.] Willing to work on a deferred payment contract. [8.] Ability to get along with people.

Additional Perks for the role:

[1.] Free round trip ticket to Tanzania. [2.] All accommodations provided while in Dar. [3.] Daily stipend while on the set. [4.] Possibility of earning a role in Kibira Films future projects. [5.] Exposure to Film festivals in USA, Europe and Africa. [6.] Screen testing in Minneapolis, MN if selected or being considered. [7.] Possible career move.

For consideration:

[1.] Send a headshot. [2.] Your resume OR. [3.] An essay of why you think you should be considered for the role. [4.] Any tapes, DVD, vocals showing your acting abilities - In actual production i.e. play, movie (if you have it)

[5.] Send to: Kibira Films International 2860 Zanzibar Lane North Plymouth, MN 55447

[6.] Email - info@kibirafilms.com Thanks and Good Luck.

More information about Kibira Films - www.kibirafilms.com

Phone #: Office: (612)-291-2719; Mobile: (763)-229-2495

Saturday, October 28, 2006

Washindi wa 2006 ni Cardinals!


Ukikaa Marekani lazima utasikia habari ya mchezo BASEBALL! Zamani sikuwa na habari na huo mchezo na wala sikuujali lakini siku hizi mimi nimekuwa mshabaki! Kila mji Marekani una timu yake. Miji mikuu ina timu kubwa na wachezaji wanalipwa donge nono. Naona kama watu wana mapenzi na Baseball zaidi ya watu wanavyokuwa na mapenzi ya mpira wa miguu Tanzania.

Jana jioni timu kutoka St. Louis, Missouri iitwayo, Cardinals, walishinda timu kutoka Detroit, Michigan iitwayo, Tigers. Cardinals ni aina ya ndege na Tiger ni aina ya paka kubwa, sasa ungetemea Tigers washinde. Lakini Cardinals walinyakuwa ushindi wa World Series, yaani kuwa timu bora ya baseball ya mwaka 2006. Hongera kwao.

Ukweli nilikuwa nashabikia Tigers. Sijui kwa nini, lakini napenda sana wakicheza kwenye uwanja wao Detroit. Kila wakipata bao (score), na kukanyaga Homeplate basi unasikia mlio wa Tiger halafu macho ya sanamu ya Tiger wao yana waka na kucheza cheza! Kama wangefanikiwa kushinda World series sijui huyo Tiger wao angefanyeje.

Safari ya wacheza baseball ni ndefu kila mwaka. Wanaanza msimu wao April na kucheza na timu mbalimbali na kupunguzwa mpaka wanapata timu bora kwenye mchezo wa World Series. Tofauti na michezo mingine kama Football, wachezaji wa baseball wanacheza karibu kila siku na siku zingine hata game mbili kwa siku! Na kuna washabiki ambao hawakosi hata game moja ya timu wao.

Baseball ni mchezo uliyoanza marekani. Zamani weusi walibaguliwa na hawakurusiwa kucheza japo kwenye timu za weusi tupu. Miaka ya 1950's walianza kuruhusu weusi kucheza. Siku hizi kuna wachezaji wengi kutoka nchi za Amerika ya Kusini kama Dominican Republic, Cuba na Colombia. Na pia waJapani na waChina wapo. Wacehzaji wa kizungu katika Major Leagues wamekuwa wachache lakini bado watu wanashabikia.

Watoto wadogo wanacheza kwenye timu za Little League. Uwongo mbaya game zingine ni kama vile game za wakubwa Major Leagues. Watoto na wazazi wa wachezaji wanakuwa tayari kushikana masharti. Mwaka huu kocha wa timu fulani ya Little League alifungwa jela baada ya kumlipa mtoto wa miaka minane kumpiga na kumjeruhi mtoto mwingine kwenye timu yake na mpira kwa vile aliona kama yule mtoto atafanya washindwe.

Navyoona mchezo ni mgumu na lazima uwe na roho kuucheza maana ukipigwa na kale kampira (baseball) utaumia! Mchezaji anajitahidi kuupiga mpira unaoenda spidi kali mno na kamti (bat). Kusudi watu wasivunje mikono wakiudaka wanavaa gloves maalum. Batter ambaye ni zamu yake kujaribu kuupiga anavaa kofia kubwa na ngumu kichwani maana ukipgwa nayo unaweza kufa. Hapa Boston kwenye timu yetu, Red Sox, kuna jamaa, Matt Clement ambaye ni fundi wa kutupa mpira (pitcher) kapigwa kichwani na mpira mwaka jana na hajawa mzima tokea hapo!

Hapa Boston, timu yetu ni Red Sox na walishinda World Series, mwaka 2004. Japo ni timu ya mji wetu mimi siwapendi sana. Ni ghali mno kwenda kwenye game zao halafu tiketi zinauzwa magendo mpaka dola $3,000! Kukaa bleacher ni dola $70 na huoni kitu bila kuwa na binoculaurs!Waachie wenyewe tutazama kwenye TV! Au nitaenda Baltimore na New York kuangalia game huko maana tiketi ni dola $40 tu.

Haya nawaachia nafasi mtoe stori zenu za baseball.

Thursday, October 26, 2006

David Banda Madonna



Huyo mtoto mweusi ni mtoto wa miezi kumi na tatu, David Banda ambaye baada ya miezi kumi na nane atakuwa mtoto wa mwimbaji maarufu Madonna na mume wake, Guy Ritchie. David yuko Uingereza sasa na familia yake mpya.

Juu, ni picha ya Madonna na watoto wake wote, chini ni picha ya David na baba yake mpya Guy Ritchie. Yaani wiki mbili tu, mtoto kanawiri na kuonekana mwenye furaha!

Madonna alimpata David kutoka kwenye nyumba ya watoto yatima huko Malawi. Mama yake alikufa katika uzazi na pia wakubwa zake walifariki shauri ya malaria. Baba yake mzazi Yohane Banda, alishindwa kumtunza mwanae na kumpeleka huko kwa watoto yatima. Baba yake anasema ni bora amchukuea maana angebakia Malawi angekufa.

Huyo mtoto atalelewa katika nyumba ya fahari na atakuwa na mahitaji yake yote na atasoma digrii zote anazotaka kusoma. Pia mama yake Madonna lazima atamwachia mamilioni ya dola za kurithi. Si uwongo kulelewa katika familia ni tofauti na kulelewa kwenye nyumba ya yatima.

David Banda kazaliwa katika umaskini, lakini leo anaishi katika utajiri. Na lazima kuna watu wanamwonea wivu!

Monday, October 09, 2006

Leo ni Sikukuu ya Columbus Marekani

Leo ni sikukuu ya Columbus hapa Marekani. Ni siku ya kusherekea aliyegundua Marekani, Bwana Christopher Columbus. Columbus alitua Marekani na meli zake tatu mwaka 1492. Kuna nyimbo kadhaa za kumsifia na utasikia watoto wanaimba, "Columbus sailed the Ocean blue in 1492!"

Columbus alikuwa ni mwitalia aliyepewa pesa na malkia na mfalme wa Spain kugundua nchi kadhaa duniani. Kwanza enzi hizo wazungu walidhani kuwa dunia iko fleti na ukienda mbali utaanguka na kuishia motoni. Columbus alisema dunia ni mviringo. Alivyochukua meli zake na wakawa wanaenda, wanaenda, wafanyakazi wake kwenye meli waliokuwa na hofu kubwa kuwa meli yao itafika mwisho wa dunia, wataanguka na kufa wote. Walipanga hata kumpindua Columbus na hata kumwua na kurudi huko Spain. Lakini Columbua alifanikiwa kuwatuliza na hatimaye walifika Marekani. Ukweli alligundua Marekani kwa bahati tu, maana nia yake ilikuwa afike India. Alivyofika alishangaa kuwa hauko kama alivyofikiria na ndo kajua kagundua sehemu nyingine ndo kapaita West Indies. Ukweli Columbus hakufika Marekani tunayojua leo, bali alifika visiwa vya Bahamas. Lakini alifungua mlango kwa ajili ya wazungu kuja kwa wingi huko walivyojua kuna ardhi huko upande wa pile wa bahari!

Ajabu, utadhania kuwa kulikuwa hakuna watu Marekani kabla ya Columbus kufika. Watu walikuwepo. Hao wenyeji waliteswa na kunyanyaswa na hao wazungu. Waliuliwa na kuibiwa mali zao na kufanywa watumwa. Hao wazungu waliwaletea magonjwa, kama surua, na mafua na kaswende na wenyeji walikufa kwa wingi.

Watu unaowaona Marekani leo ni mchanganyiko wa watu kutoka kila pande ya dunia. Wako wa kila rangi, kila, kabila na kila dini. Uzuri Marekani wanasema kuwa kuna 'melting pot' yaani watu wanayeyushwa na kuwa moja. Na huko serikali ya Marekani inataka kufunga milango wahamiaji waache kuja. Wanasahau kuwa hii ardhi ilinyang'anywa kutoka kwa wenyeji waliokuwepo. Maangamizi ya wenyeji wa Marekani ilikuwa ni ya hali ya juu.

Kwa kweli kuna mengi ya kusema, lakini kwangu mimi sioni kama huyo Coulumbus ni shujaa.

Wednesday, October 04, 2006

Ngoma ya 'Tap'



Najifunza kucheza ngoma ya Tap Dance. Hii picha nilipiga baada ya Show niliyofanya na Studio yetu hivi karibuni.

Tap Dance ni ngoma inayochezwa ukiwa umevaa viatu maalum vyenye vyuma chini. Kuna kuwa na chuma mbele na nyingine nyuma kwenye kisigino. Unacheza heel-toe, heel-toe na kila kikigonga chini kinaitwa tap. Na hivyo viatu vinatoa sauti kama muziki ukiweza kuvimudu.

Tap Dance ulianzishwa na waMarekani weusi na baadaye kudakwa na wazungu. Miaka ya nyuma watu wengi sana Marekani walijua kucheza lakini siku hizi 'interest' nayo inafifia. Watoto walikuwa wanacheza tangia wadogo. Marehemu Gregory Hines alijitahidi sana kufufua. Bila shaka mmeona watu wanacheza kwenye sinema kadhaa hasa zile sinema za zamani na musicals.

Kwa kweli inahitaji kazi na mazoezi na moyo. Ukiona wakina Savion Glover wanacheza ujue wamejifunza miaka na miaka. Ajabu ni mchezo wa mahesabu, maana lazima uwe na taps kadhaa katika sehemu ndogo ya muziki na zifuate muundo maalum. Huwa inategemea na muziki unayaotumia. Kwa sasa vijana wengi wanapenda Jazz Tap na Hoofing. Hizo staili kidogo una uhuru wa kwenda nje ya muundo wa ku-tap kwa mahesabu.

Kuna mama fulani marehemu sasa alikuwa anaitwa Ann Miller, alikuwa anaweza kupiga tap zaidi ya 500 kwa dakika moja. Ndo mwenye rekodi ya kutap haraka. Wandugu sitafika huko! Sitini kwa dakika moja ni kazi.

Si ajabu unauliza sababu iliyonifanya nianze kujifunza. Ni hivi, nilienda kwenye audition ya show fulani na kuulizwa na nina dance experience. Nikasema najua kucheza ngoma za East Africa. Wao walisema wanataka watu wanaojua ngoma za hapa USA kama ballet na tap. Basi ikabidi ninunue viatu na nitafute darasa! Mwanzo ulikuwa mgumu lakini sasa sioni kitu cha ajabu sana. Na naona raha kuwa naweza kucheza wimbo mpaka mwisho bila kukosea. Na next time nafanya audition wakisema wanataka nicheze dance niko tayari kuwa 'tapia'!

Kama uko Marekani au Ulaya bila shaka kuna studio karibu na wewe inayofundisha tap dance.