Sunday, June 21, 2015

Wapiga Picha wa Vyombo Vya Serikali Enzi Hizo!

 Nilifanya kazi nao wapiga picha nikiwa mwandishi wa habari Daily News miaka ya 1980's! Enzi zile tulikuwa wachache na wote tulijuana.  Mzee Makwaia alikuwa Mwalimu wetu TSJ. Alifariki tukiwa mwaka wa kwanza baada ya kugongwa na gari Morogoro Road.

 Kwa hisani ya Kaka Juma Dihule:

WAFAHAMU WAPIGAPICHA WA VYOMBO VYA SERIKALI ENZI HIZO.
Wapigapicha wa wakati huo ambapo vyombo vya habari vilimilikiwa na Serikali pamoja na chama tawala. Waliosimama nyuma toka kushoto marehemu Max Madebe (Mpigapicha Mkuu gazeti la Mfanyakazi, Marehemu Sam Mbando, mpigapicha mwandamizi Shirika la Habari Tanzania (SHIHATA), Marehemu Vincent Urio (Mpigapicha Mkuu magazeti ya Serikali ya Daily News & Sunday News, Marehemu John Makwaia ndiye aliyekuwa mwalimu wetu sisi wote na mpigapicha mkuu wa Serikali katika Idara ya Habari (MAELEZO), akifuatiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye pia ni marehemu, David Saileni ambaye wakati huo akiwa mpigapicha mwandamizi wa Sinema, upande wa Idara ya Habari, (Film Unit), Juma Dihule, Mpigapicha Mkuu SHIHATA, Marehemu Adnani Mihanji, Mpigapicha Mwaandamizi, SHIHATA na Moshy Kiyungi, Mpigapicha mwandamizi ( Idara ya Habari).
Walioketi toka kushoto, Steven Kasange, IKULU, Charles Kagonji , Mkutubi Mkuu wa maktaba ya picha MAELEZO na pia akiwa mpigapicha, Gaspar Msilo, Daily News, Mwanakombo Jumaa, MAELEZO, Hatib Ali Mpichapicha Mkuu (Uhuru na Mzalendo) Raphael Hokoro , ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO).

1 comment:

Mbele said...

Dada Chemi

Umenikumbusha mbali. Miaka ile ya themanini na kurudi nyuma, ninayemkumbuka sana ni Vincent Urio. Kwangu alikuwa kama alivyo Freddy Maro leo au Muhiddin Issa Michuzi. Moto wa kuotea mbali.