Saturday, November 02, 2019

Leah Mwamoto Awaonya Wazazi wa Kilolo Wanaokatisha Masomo ya Wanafunzi

Mjumbe wa halmashauri Kuu (CCM) Mkoa wa Iringa, Leah Mwamoto akiongea na wazazi wa shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa
 Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wakicheza nyimbo mbele ya mgeni Rasmi

NA FREDY MGUNDA,KILOLO

Mjumbe wa halmashauri Kuu (CCM) Mkoa wa Iringa, Leah Mwamoto amewaonya wazazi wanaokatisha masomo watoto kuwa serikali itawachukulia hatua kali pindi watakapobainika kufanya kosa hilo.

Mwamoto ameongea hayo katika mahafali ya kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika kijiji cha Mlafu wilayani Kilolo alipomuwakilisha mbunge wa jimbo la Kilolo Venance Mwamoto.

Akiwaonya wazazi katika mahafali hayo Mwamoto amewaeleza wazazi juu ya mazingira mabaya wanayoyakuta watoto wanaokwenda kufanya kazi za ndani katika miji mikubwa.

Hata hivyo amewaomba watendaji wa kata kuendelea kuwafutilia watoto ili kuwaepusha kujiingiza katika mazingira hatarishi yatakayoharibu ndoto zao.

Aidha Mwamoto amepongeza uongozi wa shule ya sekondari Mlafu kwa matokeo mazuri pamoja na mbunge wa jimbo la Kilolo, Mhe Venance Mwamoto kuchangia bati 180 na mifuko 100 ya saruji kwa ujenzi wa zahanati kijiji cha Mlafu.

Awali akisoma taarifa fupi ya shule mwalimu mkuu wa shule hiyo Emmanuel Mbangwa ameomba wadau kujitokeza kuboresha mazingira katika shule hiyo hususani kujenga nyumba za walimu na mabweni.

Nae diwani Mlafu Isidory Kiyenge amewataka wazazi wa kata hiyo pamoja na wadau kuwa tayari kuchangia katika sekta ya elimu ili kuongeza mazingira ya ufaulu.

Kayenge amewataka wanafunzi kujiandaa kwa mitihani ya kidato cha nne huku alito ahadi ya kuwaandalia chakula wakati wa mitihani.

No comments: