Showing posts with label Forest Hills Cemetery. Show all posts
Showing posts with label Forest Hills Cemetery. Show all posts

Thursday, July 09, 2009

Maiti 300 Zafukuliwa na Kutupwa huko Illinois!

Headstones za wafu zilizoharibiwa.
pichani Jike jenye uchu wa pesa Carolyn Towns (49)

Wadau, kuna habari ya kusikitisha kutoka Illinois. Tena imetokea kwenye makaburi ya weusi huko Alsip, Illinois (nje ya Chicago) kwenye Burr Oak Cemetery. Watu wenye roho ya kikatili wenye uchu wa pesa wamefukua makaburi na kutupa maiti walizokuta na kuzitupa ovyo. Kuna habari pia kuwa maiti zingine zilipondwa pondwa ndani ya makabauri waliozikwa na wengine kuzikwa juu yao! Watu walikuwa wanauziwa plot bila kujua yaliyotokea. Yaani huwezi kuamini.
Aliyekuwa anaongoza huu uharibifu wa makaburi na kutupa maiti ni mwanamke, Carolyn Towns (49) kutoka, Chicago. Waliokuwa wanamsaidia wametajwa kuwa ni: Terrence Nicks (39), Keith Nicks (45) na Maurice S. Dailey (59). Wote wamewekwa ndani ka dhamana kubwa $250,000 kila moja. Wakihukumiwa wanaweza kufungwa miaka sita hadi 30. Naona kila moja atafungwa miaka 30! Huo ni ushenzi wa hali ya juu.
Polisi wanasema wamekuta mifupa ya wafu wakiwemo watoto wadogo kabisa zimezagaa sehemu mbalimbali huko makaburini. Markers/Headstones (misalaba) zimepondwa na kutupwa pia. Wanasema walivyokuwa anafukua makaburi hawakujali kitu, wanachukua bulldoza na kuchimba na kutupa walichopata sehemu yoyote enye nafasi! Rev. Jesse Jackson anasema nafasi zinawangojea hao wanne huko motoni!

Wadau, lazima niseme kuwa nimeona ushenzi kama huo Tanzania! Tabora Mjini! Kuna makaburi fulani kwenye njia ya kwenda Isevya. walikuwa wanafukua maiti na kuzitupa na mtu anajenga nyumba hapo makaburi yalipokuwa. Wewe mpita njia unatukana na mifupa ya binadamu njiani.
Na nina wasiwasi Kinondoni cemetery mchezo huo wa kuzika watu juu ya wengine upo. Hayo makaburi yalijaa zamani lakini bado wanaendelea kuzika watu huko. Na kumbuka miaka ya 70 mwisho walipofungua ule sehemu mpya Kinondoni, na penyewe palishajaa.
Kwa habari zaidi someni:

Mnaweza kuona News Conference hapa:

Friday, July 18, 2008

Tamasha la Taa Boston

Wasichana kutoka China wakijiandaa kucheza densi ya kwao.
Taa zikielea kwenye maji ya Ziwa Hibiscus hapo Forest Hills Cemetery

Wasichana wa China wakicheza densi
Grand Master Kuobta ambaye ni 11th generation Samurai kutoka Japan
Watu wakivizia nafasi ya kuweka taa kwenye ziwa
Kikundi cha Grand Master Kubota (Huyo aliyekaa kushoto mwa Grand master alijaribu kuvunja tofali ya cement kwa mguu, kashindwa) Jamaa mweusi alivunja mbao kwa kichwa!
Baadhi ya taa kwenye ziwa!

Wasichana wa Japan wakicheza ngoma
Baadhi ya watu waliojitokeza kwenye Tamasha la Taa wakiangalia show

Wadau, jana jioni nilenda kwenye makaburi ya Forest Hills hapa Boston kwenye Tamasha la Taa. Ni sherehe ya kukumbuka wafu. Watu wanaandika ujumbe kwenye karatasi maalum kwa wapendwa wao waliofariki na zinawekwa kwenye 'lantern' Ni mbao ambao inaweza kuelea kwenye maji. Katikati ya makaburi hayo kuna ziwa ndogo na 'park' sehemu ya kupumzika na kufanya sherehe.

Tuliburudishwa na wanamuziki wanaoimba nyimbo za injili na wacheza ngoma kutoka China na Japan. Giza ilivyoingia watu waliweka hizo 'lantern' taa kwenye maji ya Ziwa Hibiscus. Ilipendenza sana kuona mataa yanaelea juu ya maji, huko bata wanaogelea kwa mshangao kuna nini leo.
Bahati mbaya giza iliingia na sikuweza kupiga picha nzuri. Zingine zimetoka nyeusi kabisa!
*************************************************
The Lantern Festival
Once a year, Forest Hills hosts the Lantern Festival, an extraordinary community event attended by 3,000 people in 2000. Inspired by Buddhist traditions, this non-denominational ceremony offers a magical way to remember family and friends. After enjoying a program of music and dance, people inscribe the paper shades of simple wooden lanterns with greetings. At dusk, we light the lanterns and watch them float across Lake Hibiscus, bearing their messages to the world of the spirits.

Kwa habari zaidi za Forest Hills Cemetery Bofya hapa: