Monday, November 05, 2007

Tangazo kwa wenye magazeti ya Lance Spearman


Kuna mdau anatafuta makala, magazeti/majarida yenye habari za Lance Spearman ambaye alikuwa muhusika wa makala/tamthiliya za picha (photo novel/photo play/photo comic) zilizochapishwa kati ya miaka ya 1960 na 1970 na magazeti ya Afrika Kusini "Drum Publications Ltd".

Mhusika huyu pia alikuwa anajulikana kama "The Spear" au "Spia"Pia kwa Afrika Mashariki kuna magazeti yaliyochapishwa Kenya yanayoitwa "Film" au "African Film" yaliyokuwa na mhusika huyu.

Pia kuna wahusika wengine kama "Fearless Fang", an African "Tarzan" na wengineo pia kama kuna mtu mwenye kumbukumbu zozote hizo pia zinahitajika.

Mdau huyu yuko tayari kununua nakala hizo zilizotumika zitakazopatikana kwa ajili ya kuweka kumbukumbu katika maktaba.

Kulingana na ubora na idadi mdau yuko tayari kulipa Euro 5 mpaka 20 Kwa watu wanaofahamu jarida/gazeti linaloitwa "Film Tanzania" na kama kuna mtu analijua na upatikanaji wake mdau anaomba amfahamishe kupitia vicensiashule@hotmail.com.

1 comment:

Anonymous said...

I am looking for a copy of the book AFTER 4:30.