Saturday, June 03, 2006

Historia ya weusi Marekani

Hii picha ya watoto haikupigwa Afrika! Ilipigwa Marekani 1867!

Tazama picha ya huyo mzungu (1933)! Fikiria alikuwa na haki ya kubaka mwanamke yeyote mweusi hata mtoto mdogo!

Sisi weusi tunadhani tunashida hapa Marekani. Kwa kweli tunayo lakini miaka ya nyuma ilikuwa balaa! Ubaguzi wa rangi ulikithiri zaidi ya ilivyokuwa Afrika Kusini enzi za apartheid. Nimekuwa nikifanya utafiti na habari nazo soma zinasikitisha na kutia kinyaa kabisa! Weusi waliteswa na waliuliwa ovyo ovyo! Ubaya sheria zilikuwepo za kuwalinda lakini wazungu wengi hawakujali maana walifundishwa kuwa mtu mweusi ni sawa na mnyama! Mapaka walidiriki kusema kuwa watu weusi hawasikii maumivu kama wazungu! Balaa! Basi walikuwa wanapigwa na whips kama ng'ombe na kubakia na makovu ya ajabu mwilini! Wengi wao waliopigwa hivyo walikufa!

Nilijua kuwa weusi walikuwa ni watumwa Marekani na ilitokea vita vya wenyewe kwa wenyewe (Civil War) na Rais Lincoln alisema kuwa watumwa wawe huru. Lakini baada ya hapo wazungu walijitahidi sana kurudisha weusi katika hali sawa na utumwa. Mpaka ikatokea Civil Rights movement miaka ya 1960's ndo weusi kidogo wanaonja usawa Marekani.
Weusi walikuwa na benki yao! Wazungu kuona ina pesa nyingi, walianza kugawa pesa zao kwa mikopo ovyo kwa wazungu. Benki ilikufa na pesa za weusi zilipotea. Shule na makanisa ya wesui zilichomwa moto. Miji ya weusi zilichomwa moto, Florida, Oklahoma, Arkansas na sehemu zingine! Mweusi aliweza kuliwa kwa kumtazama mzungu mwanamke au kumsemesha. Mweusi aliweza kuliwa kama mzungu akimwona anamjibu kijanja (uppity). Mweusi aliweza kuliwa kwa kutokumpisha mzungu kwenye sidewalk! Mweusi aliyejaribu kuunganisha wenzake wachukue hatua dhidi ya mateso anauliwa kwa kudaiwa ni mchochezi (troublemaker)!
Wazungu waliuwa wanawake na watoto na wazee bila kujali! Mwanamke mwenye mimba aliuliwa halafu alipasuliwa mbele za watu na mtoto kutoelewa tumboni! Mwanaume alikatwa uume (nyeti) wake! Wakati mwingine wazungu walikuwa wanafanya pikniki kabisa siku za kuua weusi! Wanamtafuta wa kumyonga hadharani, huko wazungu wanakula chakula chao na kuseherekea! Na hata hiyo kupasua wanawake wenye mimba ilitokea kwenye hizo pikniki!
Baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, wazungu hawakuwa na wafanyakazi wa kulima shmba zao. Basi waliajiri weusi kulima mashamba yao kwa pesa kidogo sana. Siku ya kuja kuchukua malipo walifukuzwa kama wanyama! Basi weusi wengi walikufa kwa njaa shauri ya kutokuwa na pesa za kununua chakula japo walizifanyia kazi!
Kuna vituko vingine vilitokea dhidi ya weusi na hatasijagusia vizuri! Na kumbuka kwa kila mweusi aliyefika akiwa hai kutoka Afrika, Waafrika wanne walikufa! Utumwa ilikuwa maangamizi ya weusi!

Weusi waliteswa. Ubaya ni kuwa unaona vijana weusi Marekani leo, wengi hawajui jinsi mababu zao walivyoteswa. Hawafundishwi shuleni. Wangejua sidhani kama wangekuwa wanaishi kwa ajili ya mabling bling na kutokujali masomo kama wanavyofanya leo!

1 comment:

Anonymous said...

kweli ni tabu sana.Bush akimaliza anasema tunaandamwa na magaidi kwa sababu ya ustaarabu wetu.Isije kuwa naye hiyo historia hakusoma.
Ila nisichoelewa na hili la kuwa wanatupenda mpaka wanatupatia misaada sijui likoje nalo?