Saturday, June 24, 2006

Ni Summer sasa, usije ukapofuka!

Hivi sasa ni kipindi cha joto hapa Marekani, yaani Summer. Joto linavayozidi na nguo watu wanazovaa zinapungua. Wengine wanatembea nusu uchi au karibu uchi kabisa kwa vile eti joto. Wangeonja ule joto wa Tanzania, sijui wangejionaje. Labda wangetembea uchi kabisa! Wanaume wanatembea bila sharti, na wanawake wanatembea na vikaptura na viblausi kama sidiria.

Cha ajabu basi wanatembea barabarani na vinguo vyao bila aibu. Sawa ni mila ya siku hizi kuvaa nguo viduchu hivyo lakini nimeona vituko na lazima niwasimulie.
Juzi nilikuwa Roxbury, yaani ghetto ya Boston. Basi kapita mama fulani mmarekani mweusi, mtu mzima kwa mtazamo wangu labda miaka 50 na zaidi. Alikuwa amevaa kibukta na kablausi. Halafu kanyoa kipara. Uso wake ulikuwa mchanganyiko wa uso wa yule Mwimbaji Seal na yule mgombea wa Uganda Kizza! Yaani alikuwa na uso mbaya! Halafu mapaja na mikono yake ilikuwa imejaa cellulite, nyama zinacheza ovyo akitembea! DUH, alikuwa kama kinyago. Basi anatembea barabarani na watu unaona kabisa wanaona kinyaa. Hivi alijiona mzuri? Angesikia watu walivyokuwa wanamsema, bora angejifunika.

Haya mtaani kwetu Cambridge niliona mzungu mwanamke, huenda ana miaka 60. Basi naye katia kaptura, na blausi isiyo na mikono. Nguo alizovaa hazikuwa mbaya, lakini mama mwenye alikuwa na kitambi, matiti makubwa na hakuvaa sidiria, kwa hiyo akitembea matiti yana ruka hapa na pale. Hiyo blausi haikuwa na mikono na hakunyoa mavuzi kwapani, hivyo nywele zilikuwa zinaing’ingia karibu zifike kwenye kiuno chake! Alikuwa kama katuni! Naye anatembea bila kujali!

Usifikirie kuwa nasema wazee tu. Kuna ma tineja kibao wanavaa hizo vikaptura na visidiria na kujiona wazuri kabisa. Wengine wanapendeza lakini wengine wanaonekana vituko, hasa hao wasio na shepu na wanavaa nguo saizi ndogo wakati wanahitaji saizi kubwa! Hiyo ni kwa sababu hapa Marekani watu wana ugonjwa wa kutaka kuwa wembamba wakati milli yao haitaki. Pia wakienda dukani wananunua nguo eti saizi 8 wakati wanahitaji saizi 12! Basi sababu hizo nguo ndogo manyama yanaing’inginia! Unakuta visichana vidogo vidogo wana manyama nyama lakini kusudi wawe ‘fashionable’ wanavaa hivi vinguo! Hao ambao unawaona kwenye Rap video ni wazuri na wamechaguliwa kutoka kwenye mamia ya wasichana. Lakini hao wanajaribu kuwaiga na kuvaa kama wao kwa kweli! DUH, wanatisha.

Hivi mila ya summer ni kuwa mradi umefunika nyeti zako basi uko sawa? Nimesikia watu wengi, wazungu na weusi, wakilalamika kuhusu jinsi wasichana wasivyojiheshimu na kutembea nusu uchi. Kumbe watu wanajali!

Swali lingine, mbona sioni wanaume wakivaa vinguo nguo?

Haya tungojee baridi uanze tena watu wajifunika na masweta na makoti!

* Nyongeza - Jana nilimwona mama fulani naye katia fola! Huyo ana miaka 35 hivi, ni Mmarekani mweusi, ngozi yake kama ya chui, kuanzia kichwani, hadi miguuni, sijui ni ugonjwa gani! Ni mwembamba na isingekuwa huo ugonjwa wa ngozi angekuwa mzuri, na ana matako makubwa. Basi gauni kavaa shifti, fupi, ina bana anatembea anajiona mzuri! Nguo ilipanda kwenye matako basi ndo mapaja yanaonekana zaidi nayo yako kama ngozi ya chui. DOH! Anatembea na watu wanamwangalia kwa mshangao! Angekuwa Bongo tungemtupia khanga ajifunike!

Tuesday, June 13, 2006

Usicheze na Wanyama Marekani!

Duniani kuna mambo! Marekani usicheze na wanyama, wakati mwingine wanakuwa na haki kuliko bindamu.

Leo hii jamaa fulani, Christopher Guay (mzungu), kafikishwa mahakamani na kushitakiwa kwa kuua ndege aina ya seagull (wale wa baharini) mjini Boston. Alisema kuwa alimwua kwa vile alikuwa anamsumbua akiwa kazini. Kazi ya Guay ni kuosha madirisha kwenye maghorofa! Lazima mmewaona wanainginia na makamba yao! Kazi hatari hiyo! Na hao seagulls wanakuwa wengi mjini japo bahari ni karibu maana wanatafuta chakula.

Ni hivi kuna mtu kwenye hiyo jengo alimwona na kapiga picha ya tukio. Yule aliyepiga picha kaipeleka kwenye MSPCA (Chama cha Kutetea Haki za Wanyama) nao wakaita polisi. Siku haijaisha Guay kufungwa jela na kufukuzwa kazi. Anaweza kufungwa gerezani miaka mitano!

Cha kushangaza zaidi ni kuwa hiyo habari imeandikwa kwenye kila gazeti, na iko kwenye kila TV stesheni mpaka CNN. Wakati mwingine mtu anaweza kuuawa na habari isiandikwe kwenye gazeti na msione kwenye TV hasa kama marehemu alikuwa ni mweusi.

- Kuna Mfanyakazi mwenzangu mzungu ambaye mbwa wake anaumwa. Jana alitumia nusu siku kwenda kumpeleka hospitali ya wanayama. Leo hakuja kabisa eti anamwuguza. Nisinge jali lakini hapa napofanya kazi kuna mwenzangu MKenya mwenye mtoto mdogo. Mtoto akiugua na inabidi ampeleke hospitalini ni maneno. Mtoto wa mzungu akiumwa wanamwambia atumie muda wowote anaohitaji!

- Nilipokuwa nafanyia zamani mwenzetu alifiwa na paka wake. Wiki mbili nzima anakuja kazini anakaa kwenye deski yake na kulia! Watu walimnunulia makadi, maua na lanchi lakini wapi! Hakufarajika kabisa! Utadhani kafiwa na mtu!

-Kuna MBongo mwenzetu hapa New England alikuwa anafuga mbuzi nyumbani kwake kwa ajili ya kula. Kuna siku majirani zake waliita polisi kwa vile mbuzi moja alitoroka. Polisi waliamua kwenda kufanya ‘search’ nyumbani kwake. Kufika basement wakaona ngozi za mbuzi ambao walichinjwa na kuliwa zamani! Alifungwa jela eti kwa kosa la jinai! Baadaye, baada ya kupata wakili mashitaka yalipunguzwa! Ubaya zaidi walitaka kumnyang’anya watoto wake waliesema eti kama mbuzi anawatesa eti, hao watoto hawako salama!

Hebu mchangie story zenu za wanyama hapa USA!

Sunday, June 11, 2006

Tumefufuka!



Hapa Tumemaliza shoot ya scene yetu kwenye Aftershock! Kwenye scene weusi tuliuawa (massacre)! Tulipakwa madamu feki laini ukiona utadhani ni madamu ya kweli!

Tuliambiwa tulale chini halafu mtu wa make-up alipita na lichupa ya damu! Halafu wakati wa 'take' tuliambiwa "HOLD YOUR BREATH" yaani usipumue! Ilikuwa ni kazi!

Thursday, June 08, 2006

Aftershock - Sinema kuhusu Unyanyasaji wa Weusi















Scene from Aftershock

Habari zenu wapendwa wasomaji? Leo nawajulisha kuhusu sinema inaitwa Aftershock. Film iko sponosred na History Channel na itaonyeshwa kwenye History Channel. Niliwajulisha kuwa nilifanya audition kupata nafasi ya kuigiza kwenye hiyo sinema. Sikupata pati niliyofanyia audition lakini nilipata part nyingine.


Basi juzi nilienda kwenye filming huko Sutton, Massachusetts. Ni kama maili 50 kutoka Boston. Eneo enyewe ni shamba kabisa. Yaani niliposhuka kwenye gari nilifurahi kuona miti mingi, majani, sungura, kuku wanatembea wanavyotaka! Upepo ulikuwa freshi kabisa safi mno! Ama kweli kukaa mjini kunachosha.

Haya kufika kwenye seti ya film, walikuwa wameweka matenti. Moja ya chakula, moja ya make-up, nyingine ya vifaa. Gereji ya nyumba iligeuzwa 'wardobe' (nguo). Nilenda sign-in halafu moja kwa moja nilipelekwa wardrobe kuvalishwa costume. Role yangu ni 'farm hand ' yaani ni 1867 Utumwa umeisha lakini weusi wanaajiriwa kwa hela ndogo sana, na bado kuteswa na kuuliwa ovyo. Walinivalisha sketi nyeusi ndefu, apron, sharti ya dume! Sikuvaa viatu. Baada ya hapo nikaenda make-up. Kwenda huko walinipaka make-up ya uchafu! Kwa kweli ukiona picha zangu kwenye hiyo seti mini na wenzangu ni wachafu kweli kweli! Tulikuwa wachafu mpaka watu walituogopa! Tulikuwa wachafu maana tulikuwa tunalima shamba, na ilikuwa na matope shauri ya mvua! Udongo ulikuwa umejaa wadudu na minyoo wale wakubwa wakubwa (earthworms).

Halafu kulikuwa na farasi mkubwa kweli kweli! Alikuwa anaitwa Barney! Basi alikuwa anapita karibu sana kwangu lakini ali-behave. Tukaanza kuwa marafiki mpaka hapo walipoanza kufyatua marisasi na kaanza kushutuka! Ikabidi wamwondoe kwenye seti. Kaanza kutoka mapovu mdomoni kwa woga!

Niliumwa na mdudu kwenye mguu walimeta EMT (paramedic)! Fikiria walikujwa na huduma ya 911 hapo hapo! EMT’s wawili walikuwa assigned kule kwa shoot yote, pamoja na zimamoto na polisi!

Nitawajulisha zaidi...

Saturday, June 03, 2006

Historia ya weusi Marekani

Hii picha ya watoto haikupigwa Afrika! Ilipigwa Marekani 1867!

Tazama picha ya huyo mzungu (1933)! Fikiria alikuwa na haki ya kubaka mwanamke yeyote mweusi hata mtoto mdogo!

Sisi weusi tunadhani tunashida hapa Marekani. Kwa kweli tunayo lakini miaka ya nyuma ilikuwa balaa! Ubaguzi wa rangi ulikithiri zaidi ya ilivyokuwa Afrika Kusini enzi za apartheid. Nimekuwa nikifanya utafiti na habari nazo soma zinasikitisha na kutia kinyaa kabisa! Weusi waliteswa na waliuliwa ovyo ovyo! Ubaya sheria zilikuwepo za kuwalinda lakini wazungu wengi hawakujali maana walifundishwa kuwa mtu mweusi ni sawa na mnyama! Mapaka walidiriki kusema kuwa watu weusi hawasikii maumivu kama wazungu! Balaa! Basi walikuwa wanapigwa na whips kama ng'ombe na kubakia na makovu ya ajabu mwilini! Wengi wao waliopigwa hivyo walikufa!

Nilijua kuwa weusi walikuwa ni watumwa Marekani na ilitokea vita vya wenyewe kwa wenyewe (Civil War) na Rais Lincoln alisema kuwa watumwa wawe huru. Lakini baada ya hapo wazungu walijitahidi sana kurudisha weusi katika hali sawa na utumwa. Mpaka ikatokea Civil Rights movement miaka ya 1960's ndo weusi kidogo wanaonja usawa Marekani.
Weusi walikuwa na benki yao! Wazungu kuona ina pesa nyingi, walianza kugawa pesa zao kwa mikopo ovyo kwa wazungu. Benki ilikufa na pesa za weusi zilipotea. Shule na makanisa ya wesui zilichomwa moto. Miji ya weusi zilichomwa moto, Florida, Oklahoma, Arkansas na sehemu zingine! Mweusi aliweza kuliwa kwa kumtazama mzungu mwanamke au kumsemesha. Mweusi aliweza kuliwa kama mzungu akimwona anamjibu kijanja (uppity). Mweusi aliweza kuliwa kwa kutokumpisha mzungu kwenye sidewalk! Mweusi aliyejaribu kuunganisha wenzake wachukue hatua dhidi ya mateso anauliwa kwa kudaiwa ni mchochezi (troublemaker)!
Wazungu waliuwa wanawake na watoto na wazee bila kujali! Mwanamke mwenye mimba aliuliwa halafu alipasuliwa mbele za watu na mtoto kutoelewa tumboni! Mwanaume alikatwa uume (nyeti) wake! Wakati mwingine wazungu walikuwa wanafanya pikniki kabisa siku za kuua weusi! Wanamtafuta wa kumyonga hadharani, huko wazungu wanakula chakula chao na kuseherekea! Na hata hiyo kupasua wanawake wenye mimba ilitokea kwenye hizo pikniki!
Baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, wazungu hawakuwa na wafanyakazi wa kulima shmba zao. Basi waliajiri weusi kulima mashamba yao kwa pesa kidogo sana. Siku ya kuja kuchukua malipo walifukuzwa kama wanyama! Basi weusi wengi walikufa kwa njaa shauri ya kutokuwa na pesa za kununua chakula japo walizifanyia kazi!
Kuna vituko vingine vilitokea dhidi ya weusi na hatasijagusia vizuri! Na kumbuka kwa kila mweusi aliyefika akiwa hai kutoka Afrika, Waafrika wanne walikufa! Utumwa ilikuwa maangamizi ya weusi!

Weusi waliteswa. Ubaya ni kuwa unaona vijana weusi Marekani leo, wengi hawajui jinsi mababu zao walivyoteswa. Hawafundishwi shuleni. Wangejua sidhani kama wangekuwa wanaishi kwa ajili ya mabling bling na kutokujali masomo kama wanavyofanya leo!