Wednesday, March 28, 2007

Unawafahamu Cavemen?

Original Cavemen:
And Now the Geico Cavemen!


Kama uko Marekani, lazima mmeona yale matangazo ya Geico insurance yenye Cavemen. Cavemen ni aina ya binadamu walioishi hapo zamani za kale. Yaani wale wa mwanzo kabisa baada ya enzi za dinosaurs.

Sasa kwenye hayo matangazo hao Cavemen ni wa kisasa, na mambo yao ni ya kisasa hasa. Huwa matangazo yao yanafurahisha kweli kweli. Kuna ile ambao wanamhoji Caveman fulani na ana kasirika, anavyokasirika mama moja anasema, "Seems like someone woke up on the wrong side of the rock!"

Kuna habari kuwa wanapata TV show yao mwaka kesho. Kwa kweli watu wamefurahi sana kusika habari hizo na wanangojea kwa hamu.

Kwa sasa unaweza kwenda kuwatembelea nyumbani kwao, sijui Manhattan, sijui ni Los Angeles hapo.


From Variety Magazine:

"Cavemen" will revolve around three neanderthals who must battle prejudice as they attempt to live as normal thirtysomethings in modern Atlanta.

Tuesday, March 27, 2007

Tendo la Ndoa




Nina swali. Ile tendo la kukutana mwanume na mwanamke na kufanya mapenzi ina majina mbalimbali. Wengine wanasema ‘ngono’, wengine’ kut-mbana’, wengine ‘majambo’, wengine ‘kufanya’, ‘vituuz’ na majina mengi. Lakini jina nacho shangaa ni hiyo, ‘tendo la ndoa’. Ndo jina la heshima au sijui ndo kuweza kusema bila aibu. Au ndio wamisionari walituletea hiyo jina.

Lakini watu wanaita ‘tendo la ndoa’ wakati tunajua kuwa watu wengi wanafanya kabla hawajafunga ndoa. Na watu ambao hawajafunga ndoa, wanafanya. Mungu sijui aliumbaje binadamu lakini kuvumulia mpaka kufunga ndoa si rahisi, katika jamii zote za dunia. Wanataka wasichana watunze bikra zao (lakini hiyo ni topiki nyingine). Pia watu wanafanya na watu ambao si wake, waume zao, sasa ndo ni tendo la ndoa?

Au wanaita tendo la ndoa kusudi watu wajisikie vibaya wakifanya bila ndoa? Au wanataka walazimaishe wafunge ndoa? Ndoa ni hatua kubwa katika maisha ya bindamu. Na kwa kweli ukifunga ndoa ndo unafanya mapenzi na mwenzako kwa halali. Lakini wengine wanatembea nje ya ndoa zao.

Je huko gesti au hotelini watu wanaombwa cheti cha ndo kabla ya kupewa chumba? Miili ya watu inacheka, eti hatuwezi kufanya mapenzi mpaka tufunge ndoa. Na nadhani ni vigumu sana wanaume waweze kuvumulia mpaka wafunge ndoa, maana mwili unafika ile peak ya ‘maturity’ kabla hawajafika miaka 19. Hebu someni vitabu vya biologia.

Uwongo mbaya, watu wataendelea kufanya bila ndoa. Ile ume ya mwanaume ikisimama akili anakosa mpaka anapata kitu cha kumpooza! Na kuna wanawake nao kuna kipindi fulani wanashindwa kuvumulia lazima wapate kitu tena hali hiyo inatokea bila kufunga ndoa!

Nafungua mjadala, karibuni mtoe maoni yenu.

Monday, March 26, 2007

Marudio - Miaka Baada ya tukio kaniomba Msamaha!

Naona, kuna 'Anonymous' fulani kagusia hii swala ya yalionipata nikiwa jeshini JKT. Watu wengi wamenitumia e-mail kuulizia details. Nimeamua kuibandika tena. Ni posti ya kutoka April 2006. Lakini mjue enzi za JKT, wasichana wengi walinyanyaswa kijinsia, mimi nilikuwa na bahati maana nafahamu wasichana waliokuwa gang raped. Dada fulani, alimkubali afande, alivyomaliza kaita wenzake kwa kusema, "Njooni, Mboga hii hapa!" Yule dada hakuweza kutembea vizuri kama wmezi baada ya hapo!

*****************************************************************************

Nilipokuwa Jeshi ya Kujenga Taifa (JKT) karibu nibakwe na afande Fulani (jina nahifadhi). Lazima niseme kuwa katika kipindi hicho wanaume wengi waliona makambi ya JKT kama ‘buffet’ ya wasichana. Si maafande wa jeshi tu, bali hata viongozi wa serikali walikuwa wanapitia makambi ya JKT kula tani yao!

Mimi nilikuwa Masange JKT, Tabora. Wakati huo huyo jamaa alikuwa ni Kepiteni wa JKT. Nadhani alidhania kwa vile yeye ni kepiteni basi alikuwa na haki ya kutembea na yeyote aliyemtaka. Kwangu aligonga ukuta! Bila shaka alikuwa hajawahi ‘kunyimwa’ mpaka siku hiyo alipokutana na mimi.

Miaka baada ya tukio nikiwa nafanya kazi Daily News mara nyingi nilikuwa napishana naye Posta Mpya. Basi ananisemesha, na mimi namnunia halafu napita zangu kimya bila kumjibu kwa hasira. Siku moja kanisimamisha kaniambia, "Chemi, naomba msamaha, nisemahe tafadhali, kweli nilikukosea!” Aliongeza kuwa miaka mingi imepita hivyo sina sababu ya kuwa na hasira naye! Na mimi nilimjibu, “Mshenzi sana wewe!” nikaenda zangu.

Ikapita kama mwaka mwiingine. Jamaa anaendelea kunisalimia kila nikimpita njiani na mimi kwa uchungu bado nikashindwa kusema kitu. Basi nikafikiria alichoniambia Posta Mpya. Lakini niliona kama jambo hilo linamsumbua. Na nikasema kama Bwana Yesu aliweza kusamehe watu kwa madhambi yao kwa nini mimi nisimsamehe. Basi baada ya hapo ikiwa nikimwona na akinisalimia naitika na naendelea zangu na nikaona kidogo hata yeye alikuwa na raha.

Lakini bado najiuliza kama kitendo chake kilimsumbua miaka na miaka kama ilivyonisumbua mimi.Unauliza ilikuaje mpaka nikajikuta kwenye situation ya kubakwa. Au mnasema nilitaka mwenyewe. Ngoja niwaelezee ilivyokuwa.

Nilikuwa mhudumu Officer’s Mess, mpishi na msafishaji. Huyo jamaa alikuwa ni mgeni kutoka Makao Makuu ya JKT Dar es Salaam. Kwa kweli sikutaka kufanya kazi pale Mess lakini tulichaguliwa special na Matron, mimi kwa vile niijua kupika vyakula mbalimbali hasa za kizungu. Lakini uzuri wa hiyo kazi ni kuwa uanambulia mabaki ya vyakula (leftovers), na mara nyingine kulikuwa hakuna.

Basi huyo Afande alikaa kambini wiki kadhaa. Katika kumhudumia tukawa tunaongea na mimi nikawa namheshimu kama kaka vile. Wala sikusikia mapenzi yoyote kwake. Basi jioni fulani, kanialika chumbani kwake kunywa soda na biskuti na kwa Maongezi zaidi. Sasa kama ulienda jeshi unajua njaa kali unayokuwa nayo. Nikaenda, kanikaribisha vizuri, nilipewa soda na tukawa tunaongea. Basi nikaona mwenzangu anabadilika ghafla! Mara ananikumbatia kwa nguvu, na kunibusu na mengine. Nikajaribu kuaga lakini jamaa hakuniachia. Baada ya ku-plead naye aniachie, kaniachia. Kaomba msamaha na kaniomba niendelee kukaa nimalize hizo soda alizoninulia.

Kama mjinga nikamwamini, nikakaa nakunywa hizo soda. Tukaendelea na Maongezi, kukaa kidogo huyo kanirukia, najaribu kusimama huyo, kanivuta na kuniangusha kitandani! Mimi saa hizo nikawa naogopa kabisa nia yake!Kaniambia eti, “ukipiga makelele najua nitasema nini! Nyamaza! Huna sababu ya kunikatalia!” LOH! Kanizaba kibao! Nikamwuliza kwa nini anaifanyia hivyo, na mimi nilikuwa namwona kama kaka yangu!Hapo sasa ikaniingia. Nabakwa! Loh!

Nilimpiga mangumi na mateke lakini jamaa alikuwa na nguvu huyo kachana chupi yangu! Baada ya hapo, jamaa kashika miguu yangu huko anafoka kwa sauti kama vile anatoa amri “panua miguu! PANUA MIGUU!” Huko katoa ume wake uliyosimama kwenye suruali! Basi kuona sipanui jamaa kaongeza makofi na kafanikiwa kupanua miguu yangu! Kuona kafanikiwa kupanua huyo kajaribu kupenya. Ilipogusa kwangu nilipiga kelele cha kufa! Nikasema, “Nakuufaaaa!”

Heh! Ghafla jamaa kaniachia kaniambia niende. Alisema, “Nimeigusa na ume wangu, unatosha!” Nenda zako! Na ukimwambia mtu najua nitasema nini!”Loh nilikimbia bwenini na giza lile la Masange huko nalia. Wenzangu wananiuliza vipi, nikashindwa niseme nini! Kwanza niliona haya! Fikiria, niliona haya (shame)!Kesho yake nikaenda dispensary na kujiandikisha mgonjwa. Sikwenda kazini Officer's Mess bali nililala bwenini.

Siku iliyofuatia huyo Afande mshenzi kapita bwenini kwetu kaulizia hali yangu, na mimi huko natetemeka kwa woga nikashindwa niseme nini. Alininunulia Orange squash na biskuti na kuzileta bwenini. Sitasahau alivyonitazama! Ilikuwa kama vile anapanga jinsi gani atanipata. Baada ya hapo alimwopoa msichana mwingine na huyo alimkubali kabisa. Akawa analala kabisa huko Officer’s Mess. Hakuna anayemsumbua wakijua ni bibi wa Afisa. Basi, siku za yule jamaa kukaa kambini zikaisha, na yule binti alienda naye Tabora mjini kwa siku kadhaa. Halafu jamaa karudi zake DSM. Yule binti karudi zake kambini! Kumbe alienda bila pass. Alidhania kwa vile yuko na mkubwa hana haja ya pass. Na yule Afande ndo kaondoka kimoja! Maafande waliobakia wacha wamtese huyo binti alivyorudi kambini! Walimtesa kwa Extra drill na mengine mpaka ikabidi Military Police waombe wakuu wamsamehe la sivyo atakufa. Raha yake iliishia kwa suluba! Sijui yule binti alidhania jamaa atamwoa! Kwa nini alimkubali yule mshenzi.

Anyway, kila mtu na vyake. Alivyotoka kwenye suluba tulimwuguza! Siku haizkupita na mimi nilitolewa kazi Officer’s Mess na kupelekwa kwenye kikosi cha Ujenzi na lazima nisema hapo nilifurahi sana. Basi miaka ilipita. Mimi nilikuwa mwandishi wa habari Daily News, tena nilijenga jina. Sasa nikawa napishana na yule jamaa huko kapandishwa cheo na yuko JWTZ. Jamaa anajaribu kunisalimia na mimi napita zangu kimya, namnunia kabisa.

Nilimwona mshenzi, mnyama, na kila kitu kibaya ndo ilikuwa yeye! Angefanikiwa kuingiza na kunimwagia uchafu wake ningejiona mchafu mpaka leo! Miaka kama 20 imepita sasa na bado nina uchungu naye.Jamani nyie wanaume nawaambia kubaka kinaathari zake kwa wanawake. Unataka raha ya dakika na unamwachia mwenzio na uchungu wa maisha! Wengine mpaka wanakuwa wagonjwa wa akili.

Kwa nini nimeamua kuzungumzia kubakwa kwangu hapa, ni kwa sababu naona wasichana wengi wanabakwa, halafu wanaamua kunyamaza kimya. Kisa wakienda polisi na hospitali wanahofia kuambiwa ni Malaya au walitaka wenyewe! Hata mwamanke mwenzako anaweza kukufokea kuwa ulitaka mwenyewe. Tanzania, wanaume walikuwa na usemi wao kuhusu wanawake na ngono. Walisema eti ukimwomba mwanamke halafu akijibu ndiyo, manake ndiyo atafanya. Akisema labda, manake atafanya, akisema hapana, manake hapana. Lakini jamani tendo si inakuwa tamu kama wote mmekubali? Na kama angefanikiwa kuingiza si angeniumiza sana!

Wengine wanasema ningemshitaki. Je, ningemshitaki ingekuaje? Kwanza jeshini mimi ningepewa Extra Drill mpaka niumie au kufungwa jela ya jeshi iliyojaa maji na mbu kusudi niteswe. Kumbuka ilikuwa Tanzania na yule alikuwa ni Kepiteni wakati huo na mimi nilikuwa Private. Hakuna ambaye angekuwa tayari kunisikia zaidi ya wenzangu maPrivate, na yeye alijua hivyo. SHENZI TAIPU!

Thursday, March 22, 2007

Sinema ya '21'



Wapendwa wasomaji, nimepata bahati ya kuwa katika sinema ya '21'. Wahusika wakuu ni Laurence Fishburne na Kevin Spacey. Kwa habari zaidi mnaweza kusoma hapa:

http://www.imdb.com/title/tt0478087/

Naigiza kama mhudumu wa hoteli ya Planet Hollywood. Nitawapa habari zaidi siku nyingine.

Friday, March 16, 2007

Waziri wa Liberia Ajiuzulu baada ya Skandali kumpata!




AIBU KUBWA JAMANI!

Huyo baba mweupe kwenye picha si mcheza sinema, wala porn star. Ni mtu mwenye wadhifa kubwa Afrika!



Huenda mmesikia mkasa uliyompata Waziri wa Mambo ya Rais (Minister of Presidential Affairs) huko Liberia, Afrika Magharibi. Bwana Willie Knuckles, amejiuzulu baada ya picha ya ajabu ya yeye akiwa uchi wa nyama, tena anafanya tendo la ngono na wanawake wawili, kuwekwa kwenye internet! Yaani tendo enyewe infaaa kuwa kwenye sinema ya pono! Picha enyewe inaonekana kama ilipigwa siku nyingi, na huenda waliyoitoa walikuwa na kisa naye.

Picha nimekata (cropping), lakini kwa kusimulia, kuna wanawake wanafanya tendo la kishoga. Kuna mwanamke kalala chale na kuchezea matiti yake mwenyewe huko mwanamke mwingine ananyonya uke wa huyo aliyelala na kupanua miguu, huko huyo Bwana Knuckles anamwingia kwa nyuma (huyo anayemnyonya mwenzake), mtindo wa chuma mboga au dogi!

Ni aibu kwake na familia yake. Kafunga ndoa na mke wake miaka 37 sasa. Je, mke wake atamvumulia baada ya picha hiyo ya matusi kunonekena karibu dunia nzima? Nasema shauri zake! Mke wake akimwacha ana haki maana yeye asingevumilia kuona picha ya mke wake akiwa kwenye shughuli na mwanaume mwingine.

Nashukuru Bwana Knuckles amejiuzulu. Viongozi wanatakiwa kuwa mifano kwa wananchi. Kwa kweli amejiangusha mwenyewe. Natoa pole kwa Rais wa Liberia, Mama Ellen Johnson-Sirleaf kwa kumpoteza mfanyakazi mzuri, na aibu yaliyopata uongozi wake.

Nalaani tabia mbaya na chafu ya wanaume huko Afrika. Kwanza wanaume waafrika wamezidi kupenda ngono, na tena kutoheshimu ndoa zao. Kutembea nje ya ndoa ni sifa na wanajigamba huko kwa wanaume wenzao…oh nimetafuna yule na yule! Khah! Wanaona sifa kutembea na wanawake wengi, eti inawafanya wanaume! Na wanaume walivyo washenzi badala ya kusutana, wana pongezana! Halafu watu wanashangaa kwa nini magonjwa kama UKIMWI yanasambaa kwa kasi. Si siri kuwa kuna viongozi wetu waliofanya maajabu na wanawake wasio wake zao wakiwa katika uongozi. Wakisafiri, wanasema, oh siwezi kulala mwenyewe! Kisa! Na hiyo misafara ya Mwenge enzi zile ndo usiseme, maana ilitembea kila kona ya nchi, mchana shughuli za Mwenge, jioni ‘ngonofest’!

Kwa kweli yaliyompata Bwana Knuckles iwe fundisho kwa watu. Siku hizi kuna internet na unaweza kudhalalishwa dunia mzima katika dakika chache! Kuna picha za cell phone, na vicamera vidogo vidogo, unaweza kupigwa picha na huna habari. Nafahamu jamaa alipanga chumba kwenye hoteli fulani hapa States, kachukua demu wakafanya mambo yao huko, kumbe kuna mfanyakazi wa hoteli alificha video camera huko chumbani. Hawakuwa na habari. Baada ya miaka miwili yule mfanyakazi alikamatwa na kanda nyingi za watu mbalimbali wakiwa kwenye tendo. Bahati nzuri hakuwa anaaziuza bali anazitazamma mwenyewe. Je angekuwa anaziuza. Fikiria unanunua kanda ya X video au DVD, unaanza kutazama na unatambua watu waliyoomo.. DUH!

Duniani kuna mambo ya ajabu.



Kwa habari zaidi mneweza kusoma:





Saturday, March 10, 2007

Wasio na Makaratasi wakamatwa Massachusetts

Jamani, wiki hii wasio na makaratasi wana haha hapa Massachusetts. Ni hivi, siku ya jumatatu walivamia kampuni fulani huko New Bedford and kukamata wasio na makaratasi karibu 400! Tena wengi wao walisafirishwa kwa ndege na kupelekwa kwenye makambi ya wasio na makaratasi huko Texas. Watarudishwa kwao (Deported)!

Cha kusikitisha ni kuwa wengi ya waliokamatwa walikuwa na watoto wadogo. Wamebaki bila wazazi, bila mama au baba. Kuna watu ambao wanawaonea huruma na wengine wanasema shauri zao, maana walivunja sheria kwa kukaa USA bila makaratasi. Na mbaya zaidi, waligundua kuna duka iliyokuwa inauza vyeti feki (social security card na green card) kwa dola $120! Wanaesema wakuu wa hiyo kampuni walishirikiana na wenye duka kuwapatia hao wafanyakazi makaratasi feki!

Lakini jamani, walikuwa wanafanya kazi kwa hela ndogo, na kufanya kazi ngumu. Wanaofanya kazi pale wanasema hata ruksa ya kwenda chooni ni shida. Ukichelewa kazini dakika tano unakatwa mshahara. Hiyo kampuni ilikuwa inatengeneza vifaa vya jeshi.

Wengi ya waliokamatwa wanatoka Guetemala, na El Salvador. Sijasikia kama mwafrika alikuwemo.

Unaweza kusoma habari zaidi hapa:

http://business.bostonherald.com/businessNews/view.bg?articleid=187373&srvc=biz

http://biz.yahoo.com/ap/070306/ma_immigration_arrests.html?.v=1

Thursday, March 08, 2007

Ni Ubaguzi, Uonevu au Upendeleo?

UPDATE: ANTONELLA KATOLEWA ALHAMISI. Alilia kweli. Lakini amepata offers za kupiga picha uchi Playboy magazine na ku-host Girls Gone Wild. Frenchie ata sue American Idol kwa uonevu!
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@



Kwa wapenzi wa American Idol, naomba maoni yenu. Mnakumbuka mwaka 2003, (msimu wa pili aliyoshinda Ruben Studdard) kulikuwa na dada fulani, Frenchie Davis. Huyo dada ni mweusi, mnene na ana zinga la sauti. Yaani anaimba huyo si mchezo, Jennifer Hudson alie kwake.

Kwa bahati mbaya, Frenchie aliwaambia Producers kuwa akiwa mwanafunzi, alipiga picha nusu uchi (topless) kwa ajili ya kupata pesa za kumsaidia kulipia masomo yake Howard University. Producers waliamua kumfukuza kwenye show. Mungu ni mwema na Frenchie sasa ni mwimbaji maarufu kwenye mchezo wa kuigiza, Rent, huko Broadway, New York.

Msimu huu wa American Idol kuna dada fulani, Antonella Barba, ambaye naye ali picha za uchi kwenye internet. Hajafukuzwa na bado yumo. Amepiga picha za uchi kabisa. Kwenye picha zingine anamfurahisha mwanaume kwa kumnyonya ume wake! Zingine kapanua miguu. Loh! Ajabu hajafukuzwa kwenye American Idol.

Sasa imekuwa issue, mpaka Rosie O’Donell anaongelea kwenye show yake The View, yeye anasema kuwa eti ni ubaguzi. Pia wiki hii kulikuwa na maandamano mbele ya Kodak Theater Hollywood kupinga Antonella kuendelea kuwa kwenye show wakati Frenchie alitolewa.
Na Frenchie mwenyewe sasa anataka maelezo kutoka kwa Producers wa American Idol. Anasema kuwa anamtakia huyo Antonella mema lakini ni lazima wamweleze kwa nini alitolewa na kudhalalishwa wakati ule na picha zake siyo mbaya kama za Antonella.

FYI- Producers wanajitetea kwa kusema eti Frenchie alilipwa hela kwa ajili ya zile picha wakati za Antonella zilibandikwa na boyfriend wake.

Mimi navyoona ni ubaguzi. Frenchie ni mweusi na ni mnene. Huyo Antonella ni mwembamba na wanasifia uzuri wake. Lakini jamani uwongo mbaya, Antonella hawezi kuimba.

Mnasemaje wasomaji?

Kwa habari zaidi soma hapa:

http://www.showbuzz.cbsnews.com/stories/2007/03/06/tv_realty_tv/main2540578.shtml?source=RSSattr=Entertainment_2540578