Friday, February 21, 2014

Ujumbe Kutoka Baraza la Maaskofu wa KiPentecoste


2 comments:

Anonymous said...

Inatakiwa kusema ukweli bila woga. Woga umewagharimu wapetekoste. Elimu ndogo,kujipendekeza kwa serikali na unafiki vimesababisha wapentekoste kutengwa kwenye jambo muhimu kuliko yote katika historian ya nchi yetu.

Maelezo wanayoyatoa hapa yanadhihirisha ukosefu wa elimu naupeo mdogo walionao. Woga unawafanya wajifiche nyuma ya maandiko dhaifu hali wakiwapotezea waumini wa kipentekoste haki yao ya kikatiba.

Haiwezekani wapentekoste wakose uwakilishi wa mawazo yao kwenye katiba mpya


Anonymous said...

Serikali sio baba yetu wapentekoste. Baba yetu ni Mungu aliye mbinguni.

Kwanza Mungu alisema msimwite mtu (taasisi) yeyote kuwa baba.

Jamani hizi tafsiri za maandiko mbona zina kasoro sana?

Masuala ya katiba ni masuala ya kisheria ambayo yanahitaji wataalamu wetu wa sheria wa kipentekoste wangehusishwa kikamilifu. Hapa tunaongelea mustakabali wa wapentekoste kwa miaka mingi ijayo. Katiba hii haitafanyiwa marekebisho hivi karibuni. Mchakato huu ulipaswa kuhusisha watanzania wa tasnia zote na madhehebu yote.