Wednesday, February 24, 2016

Msiba New York - Jessie Chiume

Jumuiya ya Watanzania New York,  New Jersey na Pennsylvania  (NYTC) imepokea habari za msiba ambazo zimethibitishwa na kuruhusiwa kutangazwa na ndugu Michael Chiume kwa niaba ya familia ya Chiume. Dada yetu mpendwa Jessie Chiume hatunaye duniani. Amefariki leo asubuhi kwa kugongwa na gari  huko Mount Vernon,  NY. Mungu ailaze roho ya dada yetu Jessie mahali pema peponi. Ni wakati mgumu sana kwa familia ya Chiume na sisi wote Watanzania ndugu zake. Habari zaidi za mipango  zitatangazwa na jumuiya au familia ya Chiume kadri  zitakavyopatikana.  Mungu ametoa, Mungu ametwaa.  RIP Jessica Chiume. We love you, we will miss you.

1 comment:

Daudi said...

Habari za msiba wa Kitanzania siku hizi mpaka "kuruhusiwa kutangazwa"?

Poleni wafiwa.