Saturday, February 13, 2016

Fahamu Jinsi Radiotherapy Inavyoweza kuokoa Maisha

Dk. Mahadev, mshauri mwandamizi wa radiotherapia kutoka Hospitali za Apollo.


Na Mwandishi wetu,
Matibabu ya kawaida ya saratani huwa yanahusisha upasuaji, radiotherapia na kemotherapia. Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa kwenye tiba kwa njia hizo mbili. Katika hatua za mwanzo, saratani huwa ni ugonjwa unaotibika kwa dozi moja mahususi lakini saratani iliyosambaa au kukomaa inahitaji dozi zaidi ya moja katika kuitibu. Radiotherapia, ni tiba iliyopo katika mfumo maalumu unaoleta matokeo katika mwili mzima.
Dk. Mahadev , mshauri mwandamizi wa tiba ya uvimbe kwa mionzi kutoka hospitali za Apollo anaeleza kwamba radiotherapia inahusisha chembe chembe ndogo za mionzi ya gamma au X-rays katika kutibu saratani na hata matatizo ambayo sio ya saratani pia. Mionzi hii imegawanyika katika ile mionzi ya mbali (external radiotherapy) ambayo chanzo cha mionzi kinakuwa mbali na mwili na ile mionzi ya karibu ambayo mionzi inawekwa karibu ili kuchoma sehemu yenye uvimbe peke yake.

Mionzi ya karibu ni aina nzuri ya kutibu saratani ila kwa uvimbe unaoonekana kirahisi na unaofikika. Hivyo saratani iliyopo mdomoni, saratani ya tezi dume, saratani ya kizazi zote zinaweza kutibiwa kwa mionzi ya karibu peke yake. Faida kubwa ya mionzi ya karibu ukilinganisha na mionzi ya mbali ni kwamba mionzi ya karibu inahusisha uponyaji ndani ya muda mfupi (siku 3-5) wakati mionzi ya mbali inachukua hadi wiki 7 hadi 8. Uvimbe wowote uliokomaa unahitaji mionzi ya mbali.

Lengo kubwa la matumizi ya radiotherapia ni kuchoma sehemu pekee yenye uvimbe na kuepuka kuchoma sehemu nyingine za pembeni katika mwili. Mionzi ya mbali inahistoria ndefu kutoka enzi za cobalt kwenda kwenye hali ya teknolojia ya juu ya kutoa tiba ya mionzi kwa moduli ya hali ya juu (IMRT), mionzi kwa kuongozwa na picha (IGRT), upasuaji kwa njia ya sterio (SRS) na njia ya sterio kwa mionzi mwilini (SBRT). Mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji (Cyberknife robotic radiosurgery ) ni njia bora zaidi katika kufanya SRS na SBRT, aliongeza Dk. Mahadev  kuwa teknolojia hizi zinapatikana katika hospitali za Apollo.

Umuhimu pekee wa kutumia mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji ni kukata milimeta sahihi na uponyaji katika siku chache. Ni tiba ya mgonjwa bila kulazwa na hahihitaji nusu kaputi katika kufanyika. Hivyo saratani ya mapafu na tezi dume inaweza kutibika ndani ya siku 3 hadi 5, wakati muda wake kawaida huchukua wiki 7-8 kwa uangalizi wa karibu. Mashine yenye program maalumu kwa ajili ya upasuaji ni muhimu katika kutibu uvimbe, ambao hauwezekani kufanyiwa operesheni kwa sababu ya eneo ilipo aidha katika ubongo au uti wa mgongo. Inatumika kutibu magonjwa kama meningiomas, uvimbe katika pituitary, mishipa ya ateri iliyodhofika (AVM) na madhara kutokana na saratani katika ubongo, mapafu na ini.

Dk. Mahadev  anaelezea njia bora ya kutumia radiotherapia ni kwa protoni. Faida kubwa ya protoni ukilinganisha na njia ya kawaida ni katika kutoa mionzi kwa umakini zaidi hasa kuchoma sehemu yenye uvimbe peke yake. Hiyo inapelekea matokeo mazuri na madhaifu machache. Kutokana na kutokuwa na dozi zaidi katika kutibu uvimbe, ni vyema kudhibiti uvimbe ukiwa katika hatua za mwanzo ambapo huwa tunaogopaga madhara ya kutumia mionzi. Matumizi ya protoni ni mapinduzi katika tiba ya saratani. Saratani ya kichwa na shingo, mapafu na tezi dume huwa zinatibika kirahisi kabisa kwa mionzi hii ya protoni.

Baadhi ya saratani zinazotibika kwa upasuaji, inaweza kutibika kirahisi kwa radiotherapia tu. Ikiwa hatua ya mwanzo, saratani ya mdomoni, mfumo wa chakula, tezi dume, zaweza tibiwa kwa mionzi peke yake. Faida katika kutibu aina hizi za saratani ni kuwa zipo sehemu zinazofikika. Mgonjwa anaweza kuwa na ogani inayofanya kazi vizuri hivyo kuona ubora wa maisha. Saratani nyingi zilizokomaa huwa zinahitaji kwa pamoja upasuaji, radiotherapia na kemotherapia katika kuitibu ambazo zote zinapatikana katika teknolojia ya juu kutoka hospitali za Apollo.

Tumetoka kwenye enzi za kufanya operesheni kubwa na kuingia kwenye utunzaji wa ogani zetu kwa msaada wa teknolojia ya mionzi bora na dawa mpya na bora za tiba kwa kemotherapia. Kwa mfano saratani ya matiti ndio saratani inayoongoza kwa wanawake duniani. Hapo kabla, titi lote lilikuwa linakatwa. Ila kwa sasa wagonjwa wengi wanabaki na matiti yao salama kwa upasuaji mdogo tu unaofanywa.

Tiba hiyo ndogo katika tiba inawasaidia wanawake kuwa na saikolojia chanya inayowafanya wapone haraka pia. Kichwa na shingo, mfumo wa chakula, saratani ya tezi dume na sehemu nyingine ambazo huwa kutokuondoa ogani ni kitu cha muhimu katika tiba.
Radiotherapia ni mbadaka zuri kuepuka upasuaji au kemotherapia katika kupambana na saratani. Mabadiliko makubwa katika teknolojia na matumizi ya kompyuta yamewezesha utoaji bora wa huduma ya tiba ya mionzi kwa madhara kidogo sana.



Kuhusu Hospitali ya Apollo

Hospitali za Apollo ni za kwanza katika eneo Asia Pacific kutoa huduma za upasuaji kwa kutumia mfumo huu wa Robot, ambayo ni aina ya upasuaji isiyokuwa na madhara. Taasisi ya upasuaji kutumia Robot iliyopo hospitalini hapo wamejitoa kipekee katika kutoa huduma bora kwa wagonjwa.

Taasisi ina wataalamu waliobobea kwenye mafunzo ya upasuaji, upendo katika utoaji wa huduma vifaa vya matibabu vya kisasa vinavyolenga kutoa uzoefu bora kwa mgonjwa. Vifaa hivyo ni pamoja na vifaa Robot ya Da Vinci inayotumika katika upasuaji.

Mfumo huu wa upasuaji hutumika katika teknolojia ya upasuaji wa magonjwa yanayohusiana na mfumo wa mkojo (Urology), magonjwa ya wanawake (Gynaecology), moyo, utumbo, na magonjwa ya watoto na matatizo ya uti wa mgongo.
--

No comments: