
Hivi, hao walimu walishikwa na 'mob mentality' nini? Kwanza lazima nisema kuwa naogopa sana maana hao ndio wanaofundisha watoto wetu! Na kwa nini walitaka kumwua kiongozi wao? Waseme tu ni wavivu na wanatafuta kisingizio cha kutokwenda kazini!
Walivyofanya ni vibaya na washukuru kuwa si enzi za Mwalimu Nyerere. Wangesombwa wote hao na kupelekwa Gezaulole kulima kwa muda!
****************************************************************
Walimu wataka kumuua Rais wao
2008-10-15
Na Richard Makore
Rais wa Chama cha Walimu Nchini (CWT), Gratian Mkoba, jana alinusurika kuuawa na walimu wenzake baada ya kuwatangazia uamuzi wa kuahirisha mgomo wao uliopangwa kuanza leo, hali iliyowalazimu polisi kuingilia kati na kumtoa katika Ukumbi wa Diamond Jubilee kupitia mlango wa nyuma.
Kabla ya polisi kumuokoa, viongozi wenzake waliokuwa meza kuu, walimkinga dhidi ya silaha zilizokuwa zikirushwa, zikiwamo viti na chupa za maji.
Walimu hao wakiwa wanawaka hasira walivamia meza kuu na kuzonga huku wakimlaani kuwa amewasaliti kwa kukaa upande wa serikali, hivyo kupoteza heshima na imani aliyojijengea kwao.
Umati wa walimu kutoka manispaa tatu za Jiji la Dar es Salaam, walikutana katika ukumbi huo pamoja na mambo mengine ili kujua hatma ya mgomo huo na madai yao kwa serikali kama ulivyotangazwa na CWT kwa muda mrefu.
Baada ya Mkoba kutangaza kusitishwa mgomo huo, baadhi ya walimu, walianguka kwa mshtuko huku wengine wakiangua vilio, hali iliyosababisha ukumbi kugeuka eneo lililojaa huzuni kubwa na kutawaliwa na kelele za vilio.
Mkoba aliwaambia walimu hao kuwa, mgomo wao umefutwa kwa amri ya Mahakama na kuwataka leo wasigome kama walivyopanga kwa kuwa watakuwa wamekiuka amri hiyo halali.
Kabla ya kumalizia neno `` hakutakuwepo mgomo kesho``, ukumbi huo uligeuka kuwa kama uwanja wa vita kutokana na baadhi ya walimu kumrushia Rais huyo chupa za maji, viti, kuvunja meza kuu, alikokuwa amekaa hali iliyosababisha viongozi wote wa chama hicho waliokuwa wamekaa naye kukimbia.
Hata hivyo, jitihada za baadhi ya viongozi hao, waliojipanga kuwakabili walimu waliokuwa wameanzisha vurugu hizo kwa lengo la kumdhuru Rais huyo zilishindikana hadi walipofika askari wa Jeshi la Polisi kumuokoa kwa kumuondoa ukumbini hapo kwa kupitia mlango wa nyumba.
Wakati hayo yakijiri, walimu wasikika walikisema kuwa: `` Hatukutaki, umenunuliwa na serikali, acha gari letu na ngoja tukufundishe adabu kwani naona hutujui.``
Baada ya walimu kushtuka kwamba mlengwa wao ameondolewa ukumbini hapo kwa kupitishiwa nyuma, walitoka nje na kulizingira gari la polisi kwa lengo la kulizuia kuondoka na Rais huyo wakiwa wamebeba mawe.
Polisi walilazimika kufyatua risasi za moto hewani na kuwatanya walimu hao kisha kuondoa gari lao kwa mwendo wa kasi.
Kufuatia kiongozi huo wa CWT kuokolewa na polisi, baadhi ya walimu walirudi na kumalizia hasira zao kwa kutoa upepo kwenye magurudumu ya gari lake lililokuwa limesimama nje ya ukumbi huo na kutaka kulipasua vioo.
Dalili za kuzuka kwa vurungu hizo, zilianza kuonekana ukumbini hapo baada ya viongozi wa chini wa CWT kugusia habari za kusitishwa mgomo huo ambapo walimu walikuwa wakiguna kuashiria kutokuunga mkono uamuzi huo.
Kabla ya kutokea kwa vurugu hizo wakisubiri mkutano wao uanze, walimu hao waliimba nyimbo za kumsifia Mkoba wakati anaingia ukumbini na wakisema wana imani naye.
Baadhi ya nyimbo hizo ni ``tuna imani na Mkoba oyaa! oyaa!`` na nyingine nyingi, lakini hali ilivyogeuka walimuona kama mtu mbaya na mhalifu wa siku nyingi.
Wakizungumza na Nipashe ukumbini hapo, walimu hao walisisitiza kuwa mgomo wao uko pale pale na kwamba Mkoba hawezi kuwazuia kwani wao ndiyo watendaji.
Walidai mazingira yanaonyesha kwamba Rais wao amenunuliwa na serikali na hivyo amepoteza sifa za kushika wadhifa huo, hivyo ajiuzulu.
Wakati Mkoba akiwa amebana kwenye kona ya ukumbi huo huku akitetemeka, walimu walisikika wakimwambia kuwa kuanzia jana awaachie gari lao ambalo ni la CWT na atafute usafiri mwingine au aondoke kwa miguu.
Rehema Kimweri Mwalimu wa Shule ya msingi Mivinjeni wilayani Temeke alisema, ana miaka 25 kazini, lakini hajawahi kupewa fedha za likizo pamoja na kushindwa kumrekebishia mshahara.
Lyidia Mhina kutoka Shule ya Msingi Mtoni aliangua kilio na kushindwa kuzungumza zaidi ya kutamka jina lake na shule anayofundisha.
Atanas Mwinyi wa shule ya msingi Kimara B, alisema kuwa serikali na CWT ni kitu kimoja kwani anaamini kwamba Mkoba alikwenda ukumbini hapo kuwahadaa.
Alisema anaidai serikali zaidi ya Sh. 600,000, deni ambalo alidai amejibiwa hadi leo linafanyiwa uhakiki.
Rais huyo alipotakiwa kutoa maoni yake juu ya vurugu zilizoibuka ukumbini hapo aligeuka bubu huku akiwaangalia waandishi wa habari.
Mahakama ya Kuu kitengo cha Kazi, juzi ilizuia kufanyika kwa mgomo huo, uamuzi ambao walimu hao wameupinga na kudai kuwa hawataingia madarasani, isipokuwa watakwenda kazini.
Walimu wameazimia kugoma kwa madai kuwa serikali imeshindwa kuwalipa madai yao licha ya kuipa siku 60 tangu Agosti mwaka huu.
Siku hizo zilimazika jana na leo ilikuwa ni siku iliyopangwa na walimu hao kugoma baada ya kupata baraka za CWT.
SOURCE: Nipashe
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/10/15/124522.html
Walivyofanya ni vibaya na washukuru kuwa si enzi za Mwalimu Nyerere. Wangesombwa wote hao na kupelekwa Gezaulole kulima kwa muda!
****************************************************************
Walimu wataka kumuua Rais wao
2008-10-15
Na Richard Makore
Rais wa Chama cha Walimu Nchini (CWT), Gratian Mkoba, jana alinusurika kuuawa na walimu wenzake baada ya kuwatangazia uamuzi wa kuahirisha mgomo wao uliopangwa kuanza leo, hali iliyowalazimu polisi kuingilia kati na kumtoa katika Ukumbi wa Diamond Jubilee kupitia mlango wa nyuma.
Kabla ya polisi kumuokoa, viongozi wenzake waliokuwa meza kuu, walimkinga dhidi ya silaha zilizokuwa zikirushwa, zikiwamo viti na chupa za maji.
Walimu hao wakiwa wanawaka hasira walivamia meza kuu na kuzonga huku wakimlaani kuwa amewasaliti kwa kukaa upande wa serikali, hivyo kupoteza heshima na imani aliyojijengea kwao.
Umati wa walimu kutoka manispaa tatu za Jiji la Dar es Salaam, walikutana katika ukumbi huo pamoja na mambo mengine ili kujua hatma ya mgomo huo na madai yao kwa serikali kama ulivyotangazwa na CWT kwa muda mrefu.
Baada ya Mkoba kutangaza kusitishwa mgomo huo, baadhi ya walimu, walianguka kwa mshtuko huku wengine wakiangua vilio, hali iliyosababisha ukumbi kugeuka eneo lililojaa huzuni kubwa na kutawaliwa na kelele za vilio.
Mkoba aliwaambia walimu hao kuwa, mgomo wao umefutwa kwa amri ya Mahakama na kuwataka leo wasigome kama walivyopanga kwa kuwa watakuwa wamekiuka amri hiyo halali.
Kabla ya kumalizia neno `` hakutakuwepo mgomo kesho``, ukumbi huo uligeuka kuwa kama uwanja wa vita kutokana na baadhi ya walimu kumrushia Rais huyo chupa za maji, viti, kuvunja meza kuu, alikokuwa amekaa hali iliyosababisha viongozi wote wa chama hicho waliokuwa wamekaa naye kukimbia.
Hata hivyo, jitihada za baadhi ya viongozi hao, waliojipanga kuwakabili walimu waliokuwa wameanzisha vurugu hizo kwa lengo la kumdhuru Rais huyo zilishindikana hadi walipofika askari wa Jeshi la Polisi kumuokoa kwa kumuondoa ukumbini hapo kwa kupitia mlango wa nyumba.
Wakati hayo yakijiri, walimu wasikika walikisema kuwa: `` Hatukutaki, umenunuliwa na serikali, acha gari letu na ngoja tukufundishe adabu kwani naona hutujui.``
Baada ya walimu kushtuka kwamba mlengwa wao ameondolewa ukumbini hapo kwa kupitishiwa nyuma, walitoka nje na kulizingira gari la polisi kwa lengo la kulizuia kuondoka na Rais huyo wakiwa wamebeba mawe.
Polisi walilazimika kufyatua risasi za moto hewani na kuwatanya walimu hao kisha kuondoa gari lao kwa mwendo wa kasi.
Kufuatia kiongozi huo wa CWT kuokolewa na polisi, baadhi ya walimu walirudi na kumalizia hasira zao kwa kutoa upepo kwenye magurudumu ya gari lake lililokuwa limesimama nje ya ukumbi huo na kutaka kulipasua vioo.
Dalili za kuzuka kwa vurungu hizo, zilianza kuonekana ukumbini hapo baada ya viongozi wa chini wa CWT kugusia habari za kusitishwa mgomo huo ambapo walimu walikuwa wakiguna kuashiria kutokuunga mkono uamuzi huo.
Kabla ya kutokea kwa vurugu hizo wakisubiri mkutano wao uanze, walimu hao waliimba nyimbo za kumsifia Mkoba wakati anaingia ukumbini na wakisema wana imani naye.
Baadhi ya nyimbo hizo ni ``tuna imani na Mkoba oyaa! oyaa!`` na nyingine nyingi, lakini hali ilivyogeuka walimuona kama mtu mbaya na mhalifu wa siku nyingi.
Wakizungumza na Nipashe ukumbini hapo, walimu hao walisisitiza kuwa mgomo wao uko pale pale na kwamba Mkoba hawezi kuwazuia kwani wao ndiyo watendaji.
Walidai mazingira yanaonyesha kwamba Rais wao amenunuliwa na serikali na hivyo amepoteza sifa za kushika wadhifa huo, hivyo ajiuzulu.
Wakati Mkoba akiwa amebana kwenye kona ya ukumbi huo huku akitetemeka, walimu walisikika wakimwambia kuwa kuanzia jana awaachie gari lao ambalo ni la CWT na atafute usafiri mwingine au aondoke kwa miguu.
Rehema Kimweri Mwalimu wa Shule ya msingi Mivinjeni wilayani Temeke alisema, ana miaka 25 kazini, lakini hajawahi kupewa fedha za likizo pamoja na kushindwa kumrekebishia mshahara.
Lyidia Mhina kutoka Shule ya Msingi Mtoni aliangua kilio na kushindwa kuzungumza zaidi ya kutamka jina lake na shule anayofundisha.
Atanas Mwinyi wa shule ya msingi Kimara B, alisema kuwa serikali na CWT ni kitu kimoja kwani anaamini kwamba Mkoba alikwenda ukumbini hapo kuwahadaa.
Alisema anaidai serikali zaidi ya Sh. 600,000, deni ambalo alidai amejibiwa hadi leo linafanyiwa uhakiki.
Rais huyo alipotakiwa kutoa maoni yake juu ya vurugu zilizoibuka ukumbini hapo aligeuka bubu huku akiwaangalia waandishi wa habari.
Mahakama ya Kuu kitengo cha Kazi, juzi ilizuia kufanyika kwa mgomo huo, uamuzi ambao walimu hao wameupinga na kudai kuwa hawataingia madarasani, isipokuwa watakwenda kazini.
Walimu wameazimia kugoma kwa madai kuwa serikali imeshindwa kuwalipa madai yao licha ya kuipa siku 60 tangu Agosti mwaka huu.
Siku hizo zilimazika jana na leo ilikuwa ni siku iliyopangwa na walimu hao kugoma baada ya kupata baraka za CWT.
SOURCE: Nipashe
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/10/15/124522.html