
Showing posts with label Carolla Kinasha. Show all posts
Showing posts with label Carolla Kinasha. Show all posts
Friday, June 17, 2011
Carola Kinasha Atakuwa Sweet Eazy Leo!
Mwimbaji maarufu wa Tanzania, Carola Kinasha atakuwa Sweet Eazy leo jioni huko Dar. Carola alikuwa classmate wangu Zanaki. Alikuwa anapenda kuimba wakati ule na anazidi kuendeleza kipaji chake na mapenzi yake ya muziki.


Labels:
Carolla Kinasha,
Muziki,
Sweet Eazy Restaurant
Tuesday, October 19, 2010
Maisha Lounge - Ijumaa
Wednesday, August 22, 2007
Mjue Mwimbaji Maarufu wa Bongo Carolla Kinasha


Huyu ni Dada Carolla Kinasha. Ni mwanamuziki mkongwe wa Bongo. Aliwahi kualikwa kuimba na bendi ya Dr. Remmy na wanamuziki wengine maaraufu.
Carolla namfahamu miaka mingi. Nilisoma naye Zanaki Girls Secondary School. Alikuwa anapenda sana kuimba wakati huo. Alikuwa anajua nyimbo zote za Boney M na ABBA, tena alikuwa anaziimba vizuri mpaka walimu walichukia na kusema kuimba kizungu ni kasumba!
Namsifu sana maana alifuata mapenzi yake ya kuimba japo alisomea sheria. Ana bendi kali sana huko Bongo.
Kwa habari za Dada Carolla nendeni kwenye tovuti yake:
http://www.carolakinasha.com/index.html
Subscribe to:
Posts (Atom)