Showing posts with label Cleveland Ohio. Show all posts
Showing posts with label Cleveland Ohio. Show all posts

Wednesday, May 31, 2017

Mama Bishanga Amlilia Ivan X - Mume wa Zari

Pichani ni Mama Bishanga  aka Mrs. Marolen
MAMA BISHANGA AMLILIA IVAN X HUSBAND WA ZARI
Nimesikitishwa sana na kifo cha Ivan, ni mapema sana kwa yeye kuondoka duniani kuacha watoto wadogo sana, wanahitaji sana uwepo wa baba na mama, lakini Mungu ni Mwema amependezwa nae kuwa karibu yake mbinguni.
Zari binti yetu pole sana kwa pigo hili kubwa lisilozibika kwa wepesi, Mungu akutie nguvu. Wewe ni mmoja kati ya mabinti wachache walio na msimamo imara kimaisha, wasioyumba, wanaojitegemea zaidi kimaisha kwa kufanya biashara na shughuli mbalimbali kujipatia kipato, usieyumbishwa na mapito ya maisha ya dunia kirahisi. Naweza kusema nimekufahamu baada ya kuwa na mpenzi wako Diamond, umeonyesha msimamo na uimara wako ambao ni ushahidi mzuri kuwa utawatunza wanao watatu ambao sasa wako mikononi mwako forever. Usikate tamaa wengi tumepitia uliyopitia, kuvunjika kwa ndoa na kufiwa na wenzetu na kubakia na watoto, yalinikuta mimi binafsi hayo sikujua ada, nauli, kusomesha watoto  hadi mwenzangu alipofariki mwaka 1994 nikiwa Idara ya elimu ya juu na mshahara wa ualimu, na watoto kurudi kwangu, hapo ndio niliona jinsi Mungu huongeza baraka zake, na jinsi ukoo wa Kamota ulivyosimama nami kulea watoto. Nawewe daima muweke Mungu mbele mambo yatakuwa mazuri, hasa ukizingatia ulishajiimarisha na baba watoto wako amewaacha vizuri, Mungu atakuongezea na kukutia furaha ya maisha ya familia yako, na bila kusahau kuwa Diamond yuko pemebeni yako, tabasamu lake linatosha kukuongezea amani na nguvu ya maisha na kilo za uzito wa mwili confidence! Diamond amelelewa vizuri sana na mama yake na yuko wazi katika penzi lenu, sasa ni wakati wa kushikamana kikamilfu kupeana raha na amani na kuijenga familia yenu .
Kila la heri Zari, huenda tukaonana JHB maana sehemu ya maisha yangu ni JHB kwa mume wangu Orange Grove na Alexander township!
GOD BLESS YOU AND YOUR FAMILY ZARI
MAMA BISHANGA / MRS MAROLEN
CLEVELAND. OHIO

Saturday, August 20, 2016

Mama Bishanga Ndani ya White Party ya Birthday ya Rukia Hussein

Kwa Hisani ya Christina Marolen aka Mama Bishanga


            MAMA BISHANGA NDANI YA WHITE PARTY YA BIRTHDAY YA RUKIA HUSSEIN

Rukia mtoto wa marehemu Sheihk Yahya Hussein aliangusha bonge ya white party kusherehekea miaka 50 ya birthday yake kwenye hoteli babu kubwa ya Marrioti, jijini Cleveland Ohio. Mambo yalikuwa mambo haswaaa!

Rumba lilinoga kwa nyimbo za nchi mbali mbali za Africa na hasa za maarufu home TZ za Bado, number one, bora uende, colors of African, na nasema nae taarabu ambao mume wa Rukia ilibidi awekwe kitini na kukatiwa mauno kisawasawa na mkewe na waalikwa akina Mama Bishanga, Prisca Zenda, Michelle Mujuni nk walipotupia mduara wa nguvu! Wapendwa angalieni picha mpate picha ya mambo yalivyokuwa bam bam! 
        
          HAPPY BIRTHDAY RUKIA MUNGU AKUONGEZEE UMRI, MAFANIKIO, NA
                              FURAHA YA MAISHA YAKO NA NDOA NA FAMILIA YAKO!
Birthday Girl Dada Rukia Hussein Awasili

Mama Bishanga (Kulia) na Birthday Girl



Thursday, June 16, 2011

Mshiko Ohio - Uwe 'Extra' Katika Sinema The Avengers!




MARVEL FEATURE FILM ‘THE AVENGERS’ OPEN CASTING CALL

“The Avengers” is now filming in Cleveland and the movie has put out
an open call for background actors and extras.

Seeking Ohio locals for paid jobs as extras – Also seeking crew –
please see bottom

The Avengers has a star studded cast that include Robert Downey Jr.,
Chris Hemsworth, Chris Evans, Jeremy Renner, Mark Ruffalo, Scarlett
Johansson, Clark Gregg, Samuel L. Jackson, Cobie Smulders, Tom
Hiddleston and Stellan SkarsgÄrd. The Avengers is being directed by
Joss Whedon (Toy Story, Buffy The Vampire Slayer, Serenity, Firefly).

The Avengers is shooting this summer and the film is set for release in 2012.


THE AVENGERS is based on the popular Marvel comic book series The
Avengers that came out in the ealy 1960′s.

MARVEL FEATURE FILM ‘THE AVENGERS’ OPEN CASTING CALL

Friday, July 15
Noon – 4 pm
Saturday, July 16
10 am to 4 pm

Holiday Inn – Independence
6001 Rockside Road
Independence, OH 44131

Must be 18 years or older
Parents can submit current pictures of children under 18
Please come well-groomed and wearing your best business executive outfit
Your photo will be taken at no charge
Please bring a pen for application
Know your clothing sizes!

The Avengers is also looking for crew – Crew jobs Cleveland, Ohio

THE AVENGERS is tentatively scheduled to shoot in Cleveland and
surrounding areas starting in early August and will be hiring local
crew in all departments. Crew members who are interested in working on
the show are encouraged to submit their resumes to
cleveland@cupber.com
Subject line: / you role / name/ contact #/
http://twitter.com/teamholdingcorp / 646-240-8133

Monday, April 05, 2010

Ona Mambo ya Wahindi Cleveland, Ohio

Wadau hebu cheki wahindi wanavyokuza utamaduni wao huko Cleveland, Ohio. Wamefungua Bustani - Indian Cultural Garden. Wahindi wana sauti Cleveland, ns sisi waafrika tukiwa na umoja tunaweza kuwa na Sauti hapa Massachusetts. Umoja muhimu! Halafu eti hapa Boston tunasemwa na waafrika wenzetu kwa ajili ya kutaka kukutana na Gavana!


http://www.clevelandseniors.com/family/asian-indians.htm

Friday, May 23, 2008

Mwanamke aliyekufa Afufuka!



Ama kweli maombi yanasaidia. Huko Cleveland, Ohio Bibi Val Thomas (59) alikufa hospitalini. Ubongo wake uliacha kufanya kazi masaa 17, moyo ulisimama mara tatu na mwili ulianza kuganda (rigor mortis) na kubadilika rangi.

Bibi Thomas alikuwa kwenye life support, wakati wanafamilia na madatari wanamua wanfaye nini kuhusu Organ donation, yaani kutoa moyo, mafigo, ini, mapafu nk. kwa ajili ya watu wengine wanayezihitaji.

Walizima mashine, huko watu wanalia. Alishagwa na kusomewa sala za mwisho. Ndipo yule mama alianza kuongea na kufungua macho! DOH! Maombi yalijibiwa. Sasa madaktari wanasema atakuwa mzima tu hatakuwa na aathari zozote mwilini kutokana na kifo.

Bibi Thomas anasema anashukuru kuwa yu hai na kuwa lazimaMungu ana mpango naye, kuna kitu ambacho Mungu anataka afanye.

Kusoma habari zaidi na kuona video BOFYA HAPA: