Wednesday, May 31, 2017

Mama Bishanga Amlilia Ivan X - Mume wa Zari

Pichani ni Mama Bishanga  aka Mrs. Marolen
MAMA BISHANGA AMLILIA IVAN X HUSBAND WA ZARI
Nimesikitishwa sana na kifo cha Ivan, ni mapema sana kwa yeye kuondoka duniani kuacha watoto wadogo sana, wanahitaji sana uwepo wa baba na mama, lakini Mungu ni Mwema amependezwa nae kuwa karibu yake mbinguni.
Zari binti yetu pole sana kwa pigo hili kubwa lisilozibika kwa wepesi, Mungu akutie nguvu. Wewe ni mmoja kati ya mabinti wachache walio na msimamo imara kimaisha, wasioyumba, wanaojitegemea zaidi kimaisha kwa kufanya biashara na shughuli mbalimbali kujipatia kipato, usieyumbishwa na mapito ya maisha ya dunia kirahisi. Naweza kusema nimekufahamu baada ya kuwa na mpenzi wako Diamond, umeonyesha msimamo na uimara wako ambao ni ushahidi mzuri kuwa utawatunza wanao watatu ambao sasa wako mikononi mwako forever. Usikate tamaa wengi tumepitia uliyopitia, kuvunjika kwa ndoa na kufiwa na wenzetu na kubakia na watoto, yalinikuta mimi binafsi hayo sikujua ada, nauli, kusomesha watoto  hadi mwenzangu alipofariki mwaka 1994 nikiwa Idara ya elimu ya juu na mshahara wa ualimu, na watoto kurudi kwangu, hapo ndio niliona jinsi Mungu huongeza baraka zake, na jinsi ukoo wa Kamota ulivyosimama nami kulea watoto. Nawewe daima muweke Mungu mbele mambo yatakuwa mazuri, hasa ukizingatia ulishajiimarisha na baba watoto wako amewaacha vizuri, Mungu atakuongezea na kukutia furaha ya maisha ya familia yako, na bila kusahau kuwa Diamond yuko pemebeni yako, tabasamu lake linatosha kukuongezea amani na nguvu ya maisha na kilo za uzito wa mwili confidence! Diamond amelelewa vizuri sana na mama yake na yuko wazi katika penzi lenu, sasa ni wakati wa kushikamana kikamilfu kupeana raha na amani na kuijenga familia yenu .
Kila la heri Zari, huenda tukaonana JHB maana sehemu ya maisha yangu ni JHB kwa mume wangu Orange Grove na Alexander township!
GOD BLESS YOU AND YOUR FAMILY ZARI
MAMA BISHANGA / MRS MAROLEN
CLEVELAND. OHIO

No comments: