Showing posts with label Electricity. Show all posts
Showing posts with label Electricity. Show all posts

Saturday, December 02, 2017

TANESCO: HITILAFU KWENYE GRIDI YA TAIFA IJUMAA

MAJIRA ya saa 7:20 leo hii Alhamisi Novemba 30, imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha umeme kukatika takriban kwenye mikoa yote iliyounganishwa kwenye Gridi hiyo.


Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, mafundi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO wameanza kufuatilia kujua chanzo chake hasa ni nini na taarifa Zaidi zitatolewa kila baada ya muda ili kuufahamisha umma na watuamiaji wa umeme.

Monday, July 01, 2013

Elumelu's Heirs Holdings Commits USD2.5 Billion to Obama’s Power Africa Initiative

PRESS RELEASE
Elumelu's Heirs Holdings Commits USD2.5 Billion to Obama’s Power Africa Initiative
African investment group is the single largest investor to US-led pan-African power initiative
DAR ES SALAAM, Tanzania, July 1, 2013/ -- As part of his commitment to deliver affordable and accessible power to the continent, African business leader Tony O. Elumelu is committing US$2.5 billion to the power sector in Africa. The investment is being made through his pan-African proprietary investment company Heirs Holdings (http://www.heirsholdings.com) – the single largest investor included in the White House statement announcing the Power Africa initiative.
Power Africa is a multi-stakeholder partnership between the United States, the governments of Ghana, Tanzania, Kenya, Liberia, Nigeria and Ethiopia, and the African private sector, with the shared objective of accelerating investment in Africa's power sector over the next five years. The initiative was launched in South Africa during Obama's town hall at the University of Cape Town.
Earlier this year, Elumelu’s holding company, through its investee company, Transnational Corporation of Nigeria (Transcorp), purchased the Ughelli power plant, one of Nigeria’s largest power assets, which it plans to restore to its full generating capacity of 1000 megawatts.
"The investment we are making demonstrates our intent to become a significant player in the power sector. It also shows in a clear and meaningful way that African capital can and should be part of the solution to Africa’s challenges. We need more African companies to step up and get involved in Africa’s development.”
Elumelu, who is Chairman of Heirs Holdings, went on to say, “Heirs Holdings’ investment in Power Africa is not just about creating value for shareholders. We want to conduct business in this strategic sector for the long term, in a way that links economic return to social benefits – a key component of what I call Africapitalism. Access to affordable, uninterrupted power will have an immeasurable impact on the economic ecosystem. The cost of doing business will come down, entrepreneurs will expand and innovate, and jobs will be created as a result. That is a very tangible example of what Africapitalism is about: the private sector creating economic prosperity and social wealth.”
Distributed by the African Press Organization on behalf of Heirs Holdings.
Read the White House Power Fact Sheet and Press Release: http://www.whitehouse.gov/the-press-office/2013/06/30/fact-sheet-power-africa
For more information:
Moky Makura
Director, Marketing and Corporate Communications
Heirs Holdings

Sunday, July 31, 2011

Serikali Iombe Wananchi Msamaha - Mgao wa Umeme

Nimepata hii kwenye email.

*******************************************************************

Imeripotiwa kuwa Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ameitaka serikali iwaombe radhi wananchi kwa mgao wa umeme unaoendelea. Kauli hiyo ya Sitta imewafanya maadui wake ndani ya serikali, CCM na baadhi ya vyombo vya habari vinavyotumiwa kuibuka na kumuita waziri huyo kuwa ni msaliti na lazima afukuzwe kazi.Lazima tukubali kuwa tuna tatizo kubwa sana la uwajibikaji katika nchi hii. Ni wajibu wa serikali kuhakikisha kuwa Watanzania wanapata umeme kwa ajili ya kuhakikisha ukuaji wa uchumi, upatikanaji wa huduma za jamii na maisha ya kila siku ya wananchi.

Leo hii, wastani wa asilimia 15 tu ya Watanzania milioni 44 wanapata umeme. Na serikali imeshindwa kuhakikisha kuwa asilimia hiyo ndogo ya wanaopata umeme wanapata huduma ya uhakika. Hapa ndipo dhana ya uwajibikaji inapokuja.

Kitendo cha serikali yenyewe kulazimika kuitoa bajeti ya wizara ya nishati na madini Bungeni ili
wakajipange upya ni ishara nyingine kuwa serikali haiko makini kwenye kutatua mgao wa umeme. Ni baada tu ya kuona kuwa Wabunge wamekuja juu na huenda hawatapitisha bajeti hiyo ndiyo serikali ikashituka usingizini na kusema wanahitaji muda wa kujipanga zaidi.

Wakati serikali imeongeza bajeti ya miundombinu kwa asilimia 85 na kufikia shilingi trilioni 2.78 ($1.73 billion), ilitenga shilingi bilioni 402.4 ($250m) tu kwa wizara ya nishati na madini katika kipindi hiki ambacho taifa liko kwenye janga kubwa la umeme. Ni kweli tunahitaji barabara, bandari, reli na airport, lakini ni lazima tuweke vipaumbele sawa. Kama pesa hazitoshi kufanya vyote kwa wakati mmoja, serikali makini ingetatua tatizo la umeme kwanza ndipo ijenge barabara.

Narudia tena, tatizo la umeme nchini si ukame. Ni matokeo ya serikali kutotoa kipaumbele kwa suala hili tangu ilipoingia madarakani. Ndiyo maana serikali imekiri yenyewe kuwa katika kipindi chake cha kwanza cha miaka mitano, imeongeza megawati 145 tu kwenye gridi ya taifa. Lazima kuwe na hatua za dharura, muda mfupi na muda mrefu (immediate, medium-term na long-term) za kukabiliana na tatizo hili. Serikali inabidi isimamishe safari za nje, posho, semina, manunuzi ya Landruiser VX, na matumizi mengine ya anasa ili pesa zote ziende kwenye umeme. Na ikibidi hata ikope pesa nje ili kuwekeza kwenye umeme. Kwenye global financial crisis, serikali ilitoa 1.7 trillion shillings (over $1 billion) na kugawa pesa hizi kwa kampuni zenye utata. Leo hii serikali inasemaje haina pesa za kuzalisha umeme na kutoa $250m tu? Athari za mgao wa umeme ni kubwa mara dufu kuliko zile za global financial crisis.

Serikali inabidi ifanye budget re-allocation kubwa na kutoa pesa kwenye wizara na mufungu mengine na kuzipeleka kwenye umeme.

Huko Afrika Kusini mwaka 2008 wakati nchi hiyo ilipokutwa na tatizo la umeme, aliyekuwa Rais wa wakati huo, Thabo Mbeki, alikuwa na uungwana wa kwenda mbele ya Bunge la nchi hiyo na kuwaomba radhi wananchi kwa mgao wa umeme. Sijaona mkuu wa nchi yetu akichukua hatua kama hii.

Thabo Mbeki alisema kuwa Eskom (TANESCO ya Afrika Kusini) ilikuwa inaomba pesa serikalini kila siku iwekeze kwenye umeme serikali ikakataa na kuwambia wasubiri mpaka baadae. Mbeki akakiri kuwa Eskom ilikuwa sahihi na serikali ilikosea. Na akaomba radhi. Wataalamu wa TANESCO waliikataa Richmond, vigogo serikalini wakalazimisha wapewe mkataba na matokeo yake tumeyaona. Hakuna aliyeomba radhi, na mhusika kuu akabaki kusema hajutii maamuzi yake na kujisifu kuwa yeye ni hodari wa kufanya maamuzi magumu. TANESCO kila siku imekuwa ikiomba pesa za miradi mikubwa ya umeme lakini serikali imekuwa ikiwaambia waendelee kusubiri tu. Hakuna aliyekiri kosa, kuomba radhi wala
kuwajibika.

Angalia:
http://www.news24.com/SouthAfrica/Politics/Mbeki-apologises-for-power-cuts-20080208-2
http://www.iol.co.za/news/politics/mbeki-apologises-for-sa-power-cuts-1.382421
http://www.southafrica.info/about/government/stateofnation2008-electricity.htm

Idara ya hali ya hewa iko pale kufanya utabiri wa hali ya hewa. Hivyo basi, tangu mwaka 2005 walitabiri kuwa 2010/11 kutakuwa na upungufu wa mvua. Hata hii leo wanaweza kutoa utabiri wa hali ya hewa ya mwaka 2015/16 itakuwaje. Serikali ilikuwa na taarifa tangu miaka mitano au hata kumi iliyopita kuwa mwaka huu kutakuwa na mvua chache na hii itaathiri uzalishaji wa umeme, upatikanaji wa chakula, mfumuko wa bei, nk. Serikali iache kusingizia ukame. Iombe radhi kwa taifa kuwa mgao huu wa umeme unatokana na serikali yenyewe kutotoa kipaumbele kwa tatizo hili na kutojipanga kukabiliana nalo. Na iseme ukweli chanzo cha mgao ni nini, umeleta athari gani kwa taifa, serikali inafanya nini na tatizo hili litaisha lini. Serikali sikivu ingewaomba radhi wananchi wake. Na wananchi makini na wazalendo wangedai uwajibikaji kutoka serikalini, si visingizio vya ukame!

Mdau