Showing posts with label Gillian Gibbons. Show all posts
Showing posts with label Gillian Gibbons. Show all posts

Tuesday, December 04, 2007

Mwalimu Gibbons arejea Uingereza!


Mwalimu Gibbons na watoto wake


Mwalimu Gillian Gibbons (54), yuko Uingereza na familia yake. Alirejea leo asubuhi na ndege ya Emirates.
Mwalimu Gibbons, alisifia waSudani na alisema yaliyompata yasiwakatishe moyo wengine kwenda huko. Anasema hakujua nini inatokea duniani na jinsi kesi yake ilivyogusa wengi maana alifungwa peke yake (Solitary). Baadaye kuna mtu alimdokeza kuwa kesi imekuwa kubwa.

Kwa sasa anataka kupumzika na kushrekea Christmas na familia yake. Halafu atatafuta kazi.

Imegundulika kuwa chanzo cha matatizo yake ni visa vya dada moja aliyekuwa anafanya kazi kwenye shule hiyo, Unity High School. Sarah Khawad, alikuwa karani kwenye hiyo shule. Alifukuzwa kazi Novemba na aliahidi kuifunga hiyo shule ili kulipiza kisasi!
Mweza Septemba Khawad aliwaomba wazazi wa watoto wa darasa la Mwalimu Gibbons (darasa la pil) kwenda polisi kumshitaki. Walikataa.

Khawad ndo aliwaambia polisi kuhusu darasa la Mwalimu Gibbons kuita mdoli, Mohamed na kusababisha matatizo yote. Unity High School imefungwa kwa muda.

Kwa habari zaidi someni:



Monday, December 03, 2007

Rais wa Sudan amsamehe Mwalimu Gibbons!



UPDATE 1:29PM Eastern - Mwalimu Gibbons ameondoka Sudan, kurejea Uingereza.
****************************************************************************
Rais wa Sudan, Omar Al-Bashir, amemsamehe mwalimu mwingereza Gillian Gibbons (54)! Mwalimu Gibbons alifungwa Sudan wiki iliyopita baada ya kuruhusu darasa lake la wanafunzi wa darasa la pili kuita mdoli wa darasa, Mohamed.

Wasudan walisema kuwa ilikuwa kashfa kwa waislamu. Wengine walidai auliwe. Baada ya mwalimu huyo kufungwa wabunge wawili waislamu kutoka Uingereza walienda Sudan kuongea na rais Al-Bashir. Msamaha huo umetolewa leo asubuhi.

Mwalimu Gibbons naye ameomba msamaha kwa watu wa Sudan na kusema kuwa hakuwa na nia ya kuwakashifu. Hivi sasa yuko chini ya ulinzi ya waingereza ubalozini mwao kwa usalama wake. Ataondoka kwenda Uingereza hivi karibuni.

Wakati huo huo, Serikali ya Sudan bado inaendelea kuua waDinka (waafrika) huko Darfur.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.cnn.com/2007/WORLD/africa/12/03/sudan.teacher/index.html

http://www.thestar.com/comment/article/281848

http://www.news.com.au/heraldsun/story/0,21985,22865462-663,00.html

Thursday, November 29, 2007

Mwalimu Mwingereza afungwa Sudan!

Mwalimu Gillian Gibbons


Macho ya waiingereza yamekuwa Sudan tangu jumapili kwa sababu ya mwalimu kutoka Uiingereza anayefundisha katika shule ya International huko. Mwalimu Gillian Gibbons ana miaka 54. Wanafunzi wake wana miaka saba na lazima bado wako kwenye umri wa kupenda toys (vitu vya kuchezea). Walikuwa na mdoli wa darasa. Aliwapa zoezi la darasa kumpa jina. Wengi walichagua jina Mohamed. Kwa kidemokrasia wengi wanashinda. Hao watoto wa miaka 7 ndo waliochagua jina la Mohamed. Majina mengine yaliyopendekezwa ni Hassan na Abdullah.

Huyo mwalimu namhurumiwa sana. Lazima hakuelewa uiislamu vizuri. Hakuna picha ya mtume Mohamed na wala hakuna sanamu yake. Hivyo kumwita huyo mdoli Mohamed ilikuwa tusi kubwa kwa waislamu. Pia kaanza kufundisha Sudani juzi juzi tu. Kwa wazungu kutoa jina kwa midoli ni kawaida. Sasa anashitakiwa kwa kosa la kutukana uislamu.

Sasa nauliza hivi, hao waSudani hawakuweza kumwelezea kuwa kafanya kosa na kumwelimisha. Baadala yake walitishia kumchapa viboko 40 na kufungwa jela.

Leo mahakama huko wameamuru afungwe siku 15 na awe deported akitoka. Tayari waSudani wanaonekana wabaya duniani kwa kuua raia wao wanye asili ya Afrika hasa kabila la Dinka huko Darfur.

Nawauliza wasomaji waislamu, je, walivyofanya waSudani ni sawa au walizidisha kipimo na hii tukio?

Na hao watoto je, waadhibiwe kwa kuchagua hiyo jina au waelimishwe sheria za uisilamu? Lazima wataathirika maishani mwao wakikumbuka mwalimu wao mpendwa alivyonyanyaswa kwa kosa hiyo.

Hii kesi inasisitiza umuhimu wa watu wanaoenda nchi zingine kuelewa mila na desturi na dini za huko!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.cnn.com/2007/WORLD/africa/11/29/sudan.bears/index.html

http://www.abcnews.go.com/International/story?id=3931681&page=1

http://www.cfnews13.com/News/International/2007/11/29/briton_convicted_in_sudan_blasphemy_case.html